Maswali ya Wazanzibari kwa CCM

MrFroasty

JF-Expert Member
Jun 23, 2009
1,195
592
Ni vyema wawaambie Wazanzibari wameshindwa nini kuiletea Zanzibar maendeleo tokea 1977 wakati Chama chao kilipoanzishwa hadi leo? Cha muhimu zaidi, wawajibu Wazanzibari angalau Masuala 7 yafuatayo kati ya masuala zaidi ya 700 ambayo Wazanzibari wanayo:

- Kwa nini walitumia Jeshi mwaka 2015 kupindua matokeo ya Uchaguzi wa Zanzibar? Na kimewashinda nini kuleta maendeleo ya Zanzibar baada ya Mapinduzi hayo wakati Serikali zote mbili wanazitawala wao?

- Kwa nini waliamua kuwasafirisha Masheikh wa Uamsho na kuwafungulia mashtaka Tanzania Bara kwa tuhuma za makosa yaliyofanyika Zanzibar? Kwa nini walifanya hivyo, wakati walijua na walikiri katika vikao kuwa jambo hili ni kinyume na Katiba na Sheria za Zanzibar na hata zile za Tanzania Bara? Na ni kinyume pia na maamuzi na maelekezo ya wazi ya Mahkama Kuu ya Zanzibar na Mahkama ya Rufaa ya Tanzania yaliyotolewa katika maamuzi kadhaa. Utaileteaje Zanzibar maendeleo wakati unaidharau na hutambui hata mamlaka yake ya kikatiba?

- Kwa nini walitunga Katiba Inayopendekezwa mwaka 2014, ambayo kwa wazi na dhahiri ilikusudia kuiangamiza Zanzibar, kinyume kabisa na mapendekezo ya Rasimu ya Tume ya Warioba? Na kwa nini walikataa katakata kuingiza mapendekezo ya Zanzibar yaliyokusudia kuinusuru Zanzibar hata katika mfumo wa Serikali Mbili uliopendekezwa na rasimu yao? Miongoni mwa mapendekezo yaliyokataliwa na akina Polepole, na ambayo yalipendekezwa na Kamati ya Mawaziri wa CCM Zanzibar iliyoongozwa na Balozi Seif Ali Idi, ni pamoja na kuondoa kipengele cha kumpa Rais wa Muungano uwezo wa kuigawa Zanzibar katika mikoa, wilaya na sehemu na pia lile la kuifanya ardhi kuwa jambo la Muungano.

- Kwa nini akina Polepole wameshindwa kuiwezesha Zanzibar kupata mkopo wa dola 200 milioni za Kimarekani kwa ajili ya mradi wa bandari ambazo Dkt. Ali Shein alienda kuziomba mwenyewe kwa Rais wa China na kukubaliwa? Mradi wa bandari ulikuwa miongoni mwa vipaumbele vya Ilani yao. Kilichokwamisha kupatikana fedha za mradi huu ni barua tu kutoka kwao akina Polepole. Benki ya Exim ya China ilishakubali kutoa fedha hizo. Zanzibar walipokoseshwa fedha hizo, Wachina hao ndio waliosikitika na sio akina Polepole.

Walichokifanya akina Polepole ni kuiambia Zanzibar ifanye upembuzi yakinifu mwengine [feasibility study] kwa vile gharama za ujenzi ni kubwa sana. Kufikia hatua ya Zanzibar kupewa barua hiyo ya kuagizwa kufanya upembuzi yakinifu ilichukuwa zaidi ya miaka mitatu. Suala la nyongeza hapa ni kuwa utafanyaje upembuzi yakinifu, wakati Zanzibar ilishaingia mkataba na Kampuni ya CHEC na kilichobaki ni kutimiza masharti ya awali [conditions precedent]?. Moja ya masharti hayo ni kuandaa maelezo yakinifu ya masharti na gharama za mradi [employer’s requirement], ambayo ndio njia sahihi ya kupunguza gharama.

- Kwa nini akina Polepole wamekataa katakata kuyatoa mafuta katika mambo ya Muungano ili kuiwezesha Zanzibar kuendeleza rasilimali hiyo kwa viwango na taratibu zinazokubalika kimataifa na kibiashara? Kwa nini, badala yake, wamefanya lile walilozowea la ghilba, kwa eti kuipa Zanzibar ruhusa ya kusimamia sekta ya mafuta na gesi asilia, huku wakitunga sheria ya Bunge kusema kuwa utajiri wote wa mafuta ni mali ya Serikali ya Muungano?

Wazanzibari wanaifahamu vyema Serikali ya Muungano hata ikivaa nikabu na juba. Wanaifahamu hata ikihema tu, sikwambii ikitembea au ikiongea. Wanaifahamu kwamba ni Serikali ya Tanganyika. Ndio maana hawajawahi kumsikia Rais wa Serikali hiyo akiitaja Zanzibar na nini wameifanyia katika hotuba yoyote ya kufunga Bunge tokea ya Rais Benjamin Mkapa, Jakaya Kikwete na ya hivi juzi ya Rais Magufuli. Kama huamini zitafute. Wazanzibari wamezisoma zote na hawajawahi kuona kitu cha namna hiyo.

- Kwa nini akina Polepole wameuwa biashara na kudamirisha uchumi wa Zanzibar kwa kuiwekea vikwazo vya kikodi, vya kibiashara, mfumo wa fedha na kuinyima haki zake ndani ya Muungano? Wakitaka ushahidi wa jambo hili, nawaomba wakodi hata Uwanja wa Amani, Wazanzibari wawaletee mashahidi wa jinsi ya dhulma ya kiuchumi wanavyoifanya.

Wazanzibari wanahitaji majibu ya masuali haya kabla akina Polepole hawajaja kuwauzia ghilba nyengine. Kimebadilika nini mwaka huu ambacho hakikuwepo miaka iliyopita? Mgombea? Sifa, uwezo au aila yake?

Sababu ya kumpa pole Polepole ni kuwa amesahau ile busara ya wazee: “Sikiliza kwa makini yale yasiyosemwa!”

TANBIHI: Mwandishi wa makala hii, Bwana Othman Masoud Othman, ni mwanasheria mkuu wa zamani wa Zanzibar, ambaye kwa sasa anaendelea kufanya shughuli zake binafsi kwenye taaluma yake ya sheria.
 
Wazanzibari wanahitaji majibu ya masuali haya kabla akina Polepole hawajaja kuwauzia ghilba nyengine. Kimebadilika nini mwaka huu ambacho hakikuwepo miaka iliyopita? Mgombea? Sifa, uwezo au aila yake?

Sababu ya kumpa pole Polepole ni kuwa amesahau ile busara ya wazee: “Sikiliza kwa makini yale yasiyosemwa!”
 
Wazanzibari wanahitaji majibu ya masuali haya kabla akina Polepole hawajaja kuwauzia ghilba nyengine. Kimebadilika nini mwaka huu ambacho hakikuwepo miaka iliyopita? Mgombea? Sifa, uwezo au aila yake?

Sababu ya kumpa pole Polepole ni kuwa amesahau ile busara ya wazee: “Sikiliza kwa makini yale yasiyosemwa!”
Swali la nyongeza

Pamoja na Baraza la wawakilishi kuwa na wabunge )wawakilishi wa CCM peke yao kwa miaka mitano,
Je Zanzibar imebadilika na kuwa kama ulaya?
Je kelo,shida na matatizo ya wazanzibar zimeisha?
 
Swali la nyongeza

Pamoja na Baraza la wawakilishi kuwa na wabunge )wawakilishi wa CCM peke yao kwa miaka mitano,
Je Zanzibar imebadilika na kuwa kama ulaya?
Je kelo,shida na matatizo ya wazanzibar zimeisha?
Juj wa majuj kasema imekuwa dubai baada ya kuzindua mall :D
 
Mkuu MrFroasty, kwanza it's wrong kumtaja Polepole kwenye issues za kiserikali, hizi issues ulizoibua hapa sio issues za kichama, CCM, ni issues za kiserikali, URT.

Mimi nitajibia mambo mawili, la mkopo wa dola milioni 200 za Exim bank ya China kupanua bandari ya Zanzibar na issue ya mafuta.

1. Mkopo.
Mikopo ya kimataifa ni issue ya muungano, kimataifa Zanzibar sio nchi, Zanzibar ni sehemu ya JMT, nchi ni Tanzania, hivyo Zanzibar haiwezi kukopa as Zanzibar, bali ina uhuru wa kutafuta mikopo na misaada ya kimaendeleo.

Lakini anaye idhinisha hiyo mikopo ni JMT, hivyo Zanzibar ilipotafuta mkopo huo wa $ 200 milioni, na kukubaliwa na Exim Bank ya China, nani aliyefanya feasibility study to establish that cost?.

Ili kukopeshwa mkopo wa kimataifa wa kiserikali ni lazima serikali ya muungano ndio itoe government guarantee. Serikali yetu inaweza kutoa government guarantee kwa kitu ambacho hawakijui!.

Kwa faida ya wasiojua kuhusu government guarantee, serikali inapotoa government guarantee, inamaanisha Zanzibar, ikishindwa kulipa, Tanzania ndio tunalipa, hatuwezi kuji commit kulipa kitu tusichokijua, hivyo serikali yetu iliamua kwa nia njema kabisa process ianze upya, starting with a new feasibility study tuje na realist costs, tuwasainie hiyo government guarantee mpatiwe huo mkopo mpanue hiyo bandari.

Na kwa wasio fahamu hii issue wasitake kuifanya kisiasa ikaonekana ni kero ya muungano, serikali yetu yenyewe imeishawahi kugomea mkopo wa Exim Bank upanuzi bandari ya Dar es Salaam na pia kugomea ujenzi wa bandari ya Bagamoyo kutokana na mazonge mazonge.

WaChina they are very good kwenye lobbying, baadhi ya miradi hawafuatia international good practice procedures.
Kinachofanyika kwenye baadhi ya miradi ni hiki
  1. Wao ndio wanatoa suggestions ya kufanya mradi fulani, ukikubali
  2. Wao ndio wanafanya feasibility study and establish the cost
  3. Wao ndio wanatafuta funding kuufund mradi huo na ni lazima ujengwe na Chinese companies
  4. Hapo ndipo Exim Bank ya China huingia na masharti yao ya ajabu ajabu wanakuwa tayari kutoa fedha zote za mradi ikiwemo a 20 year grace period!. Bomba la Gesi Mtwara:A "20 -Year Grace Period" ya Mkopo wa Exim Bank-China ni "Changa la Macho?!".
  5. Ili fedha zitoke, wanahitaji government guarantee ili mkishindwa kulipa, serikali ndio iwepa bure huo mradi
  6. Wao ndio wajenzi kwa mtindo wa Built and operates hadi mkopo utakapolipwa.
  7. Mkishindwa kulipa, wanataifisha mradi unakuwa mali yao.
  8. Gharama usually ni highly inflated ili kutoa kickbacks za maana kwa waliofanikisha.
  9. Mambo kama haya tuliyakataa hapa Omari Nundu: Sioni sababu ya kujiuzulu
  10. Pia tuliyakataa katika bandari ya Bagamoyo
Mafuta,
Japo Mafuta ni issue ya muungano, sheria ya mafuta ni sheria ya muungano, ila sheria imetoa mamlaka kwa Zanzibar kutunga sheria yake ya mafuta bila hitaji la kubadili katiba na kuyatoa mafuta kwenye mambo ya muungano.

P
 
Mkuu MrFroasty, kwanza it's wrong kumtaja Polepole kwenye issues za kiserikali, hizi issues ulizoibua hapa sio issues za kichama, CCM, ni issues za kiserikali, URT...
Tanganyika ikikopa nani ndio guarantee wake?

Mradi huu ulibuniwa muda mrefu na ni mradi kimkakati kwa Zanzibar. Akiulizwa suala hili bungeni Waziri Wa Fedha Mpango alisema hawawezi kuidhisha kwa utaiua bandari ya Dar!

Wakati Tanganyika wanakopa kujenga SGR na Steigler hukopa kwa jina la Tanzania na Zanzibar hawaulizwi kama sawa kwa deni la Taifa llikiongezeka ni Tanzania ndio itakua haikopesheki.

Kwa ufupi kabisa Huu muungano ni wa bwana na mtumwa. Zanzibar ni mtumwa hawana haki mpaka bwana akubali. Ni ukoloni kwa jina la muungano. Na Zanzibar haiwezi kupiga hatua za kweli za maendeleo kama huwezi kukopa wala kusaidiwa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mmesomeka. 27 na 28 October 2020 maamuzi ya mwisho tutegemee yako mikononi mwenu.
 
P.Mayalla hata aibu huna licha ya kuwa na wajukuu,unaijibia Serikali kwani wewe ni msemaji wake? Uteuzi haiji kwa kuuokota . acha kijidhalilisha wewe ni mtu mza kwa sasa,jalibu kuficha njaa yako
 
Tanganyika ikikopa nani ndio guarantee wake?

Mradi huu ulibuniwa muda mrefu na ni mradi kimkakati kwa Zanzibar. Akiulizwa suala hili bungeni Waziri Wa Fedha Mpango alisema hawawezi kuidhisha kwa utaiua bandari ya Dar!

Wakati Tanganyika wanakopa kujenga SGR na Steigler hukopa kwa jina la Tanzania na Zanzibar hawaulizwi kama sawa kwa deni la Taifa llikiongezeka ni Tanzania ndio itakua haikopesheki.

Kwa ufupi kabisa Huu muungano ni wa bwana na mtumwa. Zanzibar ni mtumwa hawana haki mpaka bwana akubali. Ni ukoloni kwa jina la muungano. Na Zanzibar haiwezi kupiga hatua za kweli za maendeleo kama huwezi kukopa wala kusaidiwa.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu Macos , kwanza hakuna nchi inayoitwa Tanganyika, wala Zanzibar, nchi inaitwa Tanganyika na nchi ya Jamhuri ya Watu wa Zanzibar, zote mbili zilikufa siku ile ya muungano kwa kuungana kuwa kitu kimoja, tukaunda nchi moja ya JMT, hivyo sasa Tanzania ni nchi moja tuu ya JMT, Zanzibar sio nchi bali ni sehemu ya JMT.

Kwenye hili la upanuzi wa bandari ya Zanzibar, kama nilivyo jibu kwenye jibu langu la msingi, kinachelewesha ni taratibu tuu, tena kwa taarifa yako, sio tuu kupanua bandari ya Zanzibar bali in future, kuifanya Zanzibar kuwa a free port kama Japan, Singapore na Dubai, makampuni makubwa ya kuuza magari kama Be Forward waweke yard zao Zanzibar, the rest of Africa badala ya kuagiza magari kutoka Japan na Dubai, waagize kutoka Zanzibar !.

Kwavile Zanzibar ni sehemu ya Tanzania, Tanzania ndio baba na Zanzibar ni mtoto, baba ni baba na mtoto ni mtoto, kama ilivyo kwa masikio hayawezi kuzidi kichwa!.

Hili la kuitana ukoloni mara utumwa ni maneno maneno tuu ya vitimbakwiri, Zanzibar inapokea asilimia 4.5% ya misaada yote ya Tanzania inayopokea kutoka nje.

Hivyo kwenye kuleta maendeleo sometimes JMT lazima iidhibiti Zanzibar, ili kuleta even development, mfano kwenye issue ya sukari, Zanzibar ina kiwanda cha sukari ambacho kinazalisha sukari ya kutosha ku suppliers soko la Zanzibar. Huko Zanzibar kilo ya sukari ni TZS 1,500 tuu. SMZ inaruhusu Wafanyabiashara wa Zanzibar import sukuri kutoka nje, matokeo yake sukari inayozalishwa kiwanda cha Zanzibar inadodea kiwandani!.

Wenye kiwanda cha sukari Zanzibar wanataka kuleta sukari hiyo huku bara kwasababu huku bei ni kuanzia TZS 2,500. Serikali ya JMT imewagomea!. Maadam Zanzibar inajitosheleza kwa sukari, tumieni sukari yenu mnayozalisha, na sio mzalishe sukari msiitumie, mtake kutuletea huku bara, huku mkitumia cheap imported sugar, hatuwakubalii!. Lengo la hatua hii muhimu ni kuwalazimisha Zanzibar mjitegemee. Hii ndio kazi ya Baba responsible!.

On top of mgao wa asilimia 4.5% ya pato la taifa, bado Zanzibar tunakupeni umeme bure!, hamlipi!. Tanesco ilitaka kuwazimia umeme, msivyo na shukrani mkasema zimeni tuu, nyie mtawasha vibatari!. Tunawapeni elimu ya juu bure, ajira, mnamiliki ardhi huku, mnafanya biashara huku, maduka makubwa karibu yote huku bara ni ya Wapemba!. Badala ya kutushukuru, ama kweli shukrani ya punda mateke!.

Siku zote tumekuambieni acheni kelele!, maadam mnayo sheria ya kura ya maoni, amueni moja...
Wanzanzibar amueni moja, ama acheni kelele za muungano!, ama pigeni Kura ya Maoni, muamue moja!.

P.
 
P.Mayalla hata aibu huna licha ya kuwa na wajukuu,unaijibia Serikali kwani wewe ni msemaji wake? Uteuzi haiji kwa kuuokota . acha kijidhalilisha wewe ni mtu mza kwa sasa,jalibu kuficha njaa yako
Mkuu mdudu , acha tabia za vidudu humu, unauliza kitu kuhusu serikali humu jf, kwani humu ndio serikalini?. Kuna Msemaji wa serikali humu kukujibia?. Ukiuliza lolote humu jukwaani kuhusu jambo lolote, yoyote mwenye jibu, atakujibu!. Kama ni maswali kwa serikali tuu, mpe Mbunge wako akakuulizie Bungeni usubirie majibu ya serikali, ukileta humu, utajibiwa na sisi Watanzania wazalendo wa taifa hili, tupo!.
P
 
Halafu malaya inatia kichefuchefu ujue, huwezi kupita kinya kimya kwenye mambo ya zanzibar. Umeandika mafindofindo yako nimeshindwa kuyapuuza kabisa
 
Mkuu Macos , kwanza hakuna nchi inayoitwa Tanganyika, wala Zanzibar, nchi inaitwa Tanganyika na nchi ya Jamhuri ya Watu wa Zanzibar, zote mbili zilikufa siku ile ya muungano kwa kuungana kuwa kitu kimoja, tukaunda nchi moja ya JMT, hivyo sasa Tanzania ni nchi moja tuu ya JMT, Zanzibar sio nchi bali ni sehemu ya JMT.

Kwenye hili la upanuzi wa bandari ya Zanzibar, kama nilivyo jibu kwenye jibu langu la msingi, kinachelewesha ni taratibu tuu, tena kwa taarifa yako, sio tuu kupanua bandari ya Zanzibar bali in future, kuifanya Zanzibar kuwa a free port kama Japan, Singapore na Dubai, makampuni makubwa ya kuuza magari kama Be Forward waweke yard zao Zanzibar, the rest of Africa badala ya kuagiza magari kutoka Japan na Dubai, waagize kutoka Zanzibar !.

Kwavile Zanzibar ni sehemu ya Tanzania, Tanzania ndio baba na Zanzibar ni mtoto, baba ni baba na mtoto ni mtoto, kama ilivyo kwa masikio hayawezi kuzidi kichwa!.

Hili la kuitana ukoloni mara utumwa ni maneno maneno tuu ya vitimbakwiri, Zanzibar inapokea asilimia 4.5% ya misaada yote ya Tanzania inayopokea kutoka nje.

Hivyo kwenye kuleta maendeleo sometimes JMT lazima iidhibiti Zanzibar, ili kuleta even development, mfano kwenye issue ya sukari, Zanzibar ina kiwanda cha sukari ambacho kinazalisha sukari ya kutosha ku suppliers soko la Zanzibar. Huko Zanzibar kilo ya sukari ni TZS 1,500 tuu. SMZ inaruhusu Wafanyabiashara wa Zanzibar import sukuri kutoka nje, matokeo yake sukari inayozalishwa kiwanda cha Zanzibar inadodea kiwandani!.

Wenye kiwanda cha sukari Zanzibar wanataka kuleta sukari hiyo huku bara kwasababu huku bei ni kuanzia TZS 2,500. Serikali ya JMT imewagomea!. Maadam Zanzibar inajitosheleza kwa sukari, tumieni sukari yenu mnayozalisha, na sio mzalishe sukari msiitumie, mtake kutuletea huku bara, huku mkitumia cheap imported sugar, hatuwakubalii!. Lengo la hatua hii muhimu ni kuwalazimisha Zanzibar mjitegemee. Hii ndio kazi ya Baba responsible!.

On top of mgao wa asilimia 4.5% ya pato la taifa, bado Zanzibar tunakupeni umeme bure!, hamlipi!. Tanesco ilitaka kuwazimia umeme, msivyo na shukrani mkasema zimeni tuu, nyie mtawasha vibatari!. Tunawapeni elimu ya juu bure, ajira, mnamiliki ardhi huku, mnafanya biashara huku, maduka makubwa karibu yote huku bara ni ya Wapemba!. Badala ya kutushukuru, ama kweli shukrani ya punda mateke!.

Siku zote tumekuambieni acheni kelele!, maadam mnayo sheria ya kura ya maoni, amueni moja...
Wanzanzibar amueni moja, ama acheni kelele za muungano!, ama pigeni Kura ya Maoni, muamue moja!.

P.
Naona unajicontradict mwenyewe, umesema nchi mbili zilikufa zikawa moja. Halafu unatoa mfano wa baba na mtoto ? Kwanini mfano wako usiwe wa binadamu mmoja ambae hafanyi ubaguzi bali kila mmoja anafanya jukumu lake tuu.

Kwa vile ni nchi moja, sioni sababu ya kusema sehemu moja kuanza kuidhibiti nyengine. Hiki ni kiashiria cha ubaguzi, na jibu lake linatokana na fact kuwa si nchi moja bali mbili nyengine ikimtawala mwenzake kwa kisingizio cha kuungana.

Sababu haswa ya Tanganyika kutaka kuidhibiti na kuwa king'ang'anizi wa visiwa vile ilielezwa wazi na Lukuvi siku moja kwenye kanisa ().

Mfano wa sukari ni mmoja tuu, kwa ufupi kama maada inavyosema sukari, zantel, drop n.k. ni miongoni mwa adhabu na madhila ya muungano yasio na idadi ni mingi. Labda nikujibu kwanini Zanzibari haijaweka kura ya maoni kutoa maamuzi ya muungano. Nadhani kichwa chako hakifanyi kazi vizuri, ikiwa viongozi wanaoweza kuleta suluhu ya muungano kwa mitutu ya masheshi maamuzi ya wazanzibari yanapinduliwa na kuekwa watu kama akina Sheni, Mwinyi n.k. Ulitarajia uongozi gani haswa kule Zanzibari ufanye maamuzi kama haya ya kura ya maoni ???

Naona pengine muda umefika kwa mtazamo wako muungano una kelele nyingi, sasa huyo anaejiita baba aseme muda umefika wa kumtimuwa uyo mtoto aende akaishi anavyotaka mwenyewe. How about that ?
 
Poleni.. Kero za muungano bado hazijaisha.. Baada ya kuliona hilo, Rais wetu mpendwa alimkabidhi mama Samia jukumu la kuhakikisha anatatua kero zote zilizobakia kwa kuzitafutia suluhu za kudumu.. Naamini katika ngwe hii ya pili atakamilisha kazi hiyo.
 
Poleni.. Kero za muungano bado hazijaisha.. Baada ya kuliona hilo, Rais wetu mpendwa alimkabidhi mama Samia jukumu la kuhakikisha anatatua kero zote zilizobakia kwa kuzitafutia suluhu za kudumu.. Naamini katika ngwe hii ya pili atakamilisha kazi hiyo.
Sidhani kama CCM ina uwezo wa kuleta suluhisho ya masuala ya muungano. Umeona wapi tatizo likajitafutia suluhisho ? CCM yenyewe ni sehemu ya kero, ASP na TANU viliunganishwa wakati masuala ya siasa si ya sehemu ya mkataba au mambo ya muungano.

Hebu tupe orodha ya kero zilizopatiwa ufumbuzi tuone ivo vichekesho. Kwa mfano wa hili li akaunti ya pamoja tokea napata fahamu zangu linapigwa danedane tuu! Au ni lipi katika mambo 7 hapo juu Samia ameleta ufumbuzi ?

Allah(SW) amewapa laana mara hii na kuwafumba macho wakati wa kutafuta mgombea. Mwinyi ndio waziri wa ulinzi, na yeye ndio anahusika moja kwa moja na masheikh wa Uamsho kuwa ndani bila ya hatia na kinyume na sheria.
 
Sidhani kama CCM ina uwezo wa kuleta suluhisho ya masuala ya muungano. Umeona wapi tatizo likajitafutia suluhisho ? CCM yenyewe ni sehemu ya kero, ASP na TANU viliunganishwa wakati masuala ya siasa si ya sehemu ya mkataba au mambo ya muungano.

Hebu tupe orodha ya kero zilizopatiwa ufumbuzi tuone ivo vichekesho. Kwa mfano wa hili li akaunti ya pamoja tokea napata fahamu zangu linapigwa danedane tuu! Au ni lipi katika mambo 7 hapo juu Samia ameleta ufumbuzi ?

Allah(SW) amewapa laana mara hii na kuwafumba macho wakati wa kutafuta mgombea. Mwinyi ndio waziri wa ulinzi, na yeye ndio anahusika moja kwa moja na masheikh wa Uamsho kuwa ndani bila ya hatia na kinyume na sheria.
Pole sana iwapo CCM ilikukwaza kwa namna moja ama nyingine.. Ipe nafasi ya pili kwa kumchagua Mwinyi aweze kushughulika na haya yote.. Naamini Dr Mwinyi kwa jinsi anavyoaminika na kuheshimiwa na mh Rais, akiwaombea msamaha hao mashehe wa uamsho, basi hapana shaka Rais wetu mpendwa atayaridhia maombi yake na mh Mwinyi ataweza kurejea nao Zbar kwenye ndege moja.
 
Pole sana iwapo CCM ilikukwaza kwa namna moja ama nyingine.. Ipe nafasi ya pili kwa kumchagua Mwinyi aweze kushughulika na haya yote.. Naamini Dr Mwinyi kwa jinsi anavyoaminika na kuheshimiwa na mh Rais, akiwaombea msamaha hao mashehe wa uamsho, basi hapana shaka Rais wetu mpendwa atayaridhia maombi yake na mh Mwinyi ataweza kurejea nao Zbar kwenye ndege moja.
Tukimpa Mwinyi hadi akaombe ruhusa kwa bwana wake, Maalim katuahidi ataenda mwenyewe kuwatoa! You see we have a better choice!
 
Mkuu Macos , kwanza hakuna nchi inayoitwa Tanganyika, wala Zanzibar, nchi inaitwa Tanganyika na nchi ya Jamhuri ya Watu wa Zanzibar, zote mbili zilikufa siku ile ya muungano kwa kuungana kuwa kitu kimoja, tukaunda nchi moja ya JMT, hivyo sasa Tanzania ni nchi moja tuu ya JMT, Zanzibar sio nchi bali ni sehemu ya JMT.

Kwenye hili la upanuzi wa bandari ya Zanzibar, kama nilivyo jibu kwenye jibu langu la msingi, kinachelewesha ni taratibu tuu, tena kwa taarifa yako, sio tuu kupanua bandari ya Zanzibar bali in future, kuifanya Zanzibar kuwa a free port kama Japan, Singapore na Dubai, makampuni makubwa ya kuuza magari kama Be Forward waweke yard zao Zanzibar, the rest of Africa badala ya kuagiza magari kutoka Japan na Dubai, waagize kutoka Zanzibar !.

Kwavile Zanzibar ni sehemu ya Tanzania, Tanzania ndio baba na Zanzibar ni mtoto, baba ni baba na mtoto ni mtoto, kama ilivyo kwa masikio hayawezi kuzidi kichwa!.

Hili la kuitana ukoloni mara utumwa ni maneno maneno tuu ya vitimbakwiri, Zanzibar inapokea asilimia 4.5% ya misaada yote ya Tanzania inayopokea kutoka nje.

Hivyo kwenye kuleta maendeleo sometimes JMT lazima iidhibiti Zanzibar, ili kuleta even development, mfano kwenye issue ya sukari, Zanzibar ina kiwanda cha sukari ambacho kinazalisha sukari ya kutosha ku suppliers soko la Zanzibar. Huko Zanzibar kilo ya sukari ni TZS 1,500 tuu. SMZ inaruhusu Wafanyabiashara wa Zanzibar import sukuri kutoka nje, matokeo yake sukari inayozalishwa kiwanda cha Zanzibar inadodea kiwandani!.

Wenye kiwanda cha sukari Zanzibar wanataka kuleta sukari hiyo huku bara kwasababu huku bei ni kuanzia TZS 2,500. Serikali ya JMT imewagomea!. Maadam Zanzibar inajitosheleza kwa sukari, tumieni sukari yenu mnayozalisha, na sio mzalishe sukari msiitumie, mtake kutuletea huku bara, huku mkitumia cheap imported sugar, hatuwakubalii!. Lengo la hatua hii muhimu ni kuwalazimisha Zanzibar mjitegemee. Hii ndio kazi ya Baba responsible!.

On top of mgao wa asilimia 4.5% ya pato la taifa, bado Zanzibar tunakupeni umeme bure!, hamlipi!. Tanesco ilitaka kuwazimia umeme, msivyo na shukrani mkasema zimeni tuu, nyie mtawasha vibatari!. Tunawapeni elimu ya juu bure, ajira, mnamiliki ardhi huku, mnafanya biashara huku, maduka makubwa karibu yote huku bara ni ya Wapemba!. Badala ya kutushukuru, ama kweli shukrani ya punda mateke!.

Siku zote tumekuambieni acheni kelele!, maadam mnayo sheria ya kura ya maoni, amueni moja...
Wanzanzibar amueni moja, ama acheni kelele za muungano!, ama pigeni Kura ya Maoni, muamue moja!.

P.
Sijui unesema haya kwa akili yako au umehadithiwa hebu jaribu kufuatilia zanzibar kila mwisho wa mwezi inalipa tsh ngapi kwa tanesco halifu wanawauzia umeme ghali sana ulizia tu bara unity shilingi ngapi na zenji ngapi,kuhusu suala la sukari ni dhana ile ile iliyoachwa na hayati kama ni nchi moja vipi sukari ishindwe kuingia bara hii ni biashara huru huwezi kuzui kuingiza sukari zanzibar kisa kiwanda wakati bara kuna uhitaji mkubwa wa sukari
 
Back
Top Bottom