Mkuu
Macos , kwanza hakuna nchi inayoitwa Tanganyika, wala Zanzibar, nchi inaitwa Tanganyika na nchi ya Jamhuri ya Watu wa Zanzibar, zote mbili zilikufa siku ile ya muungano kwa kuungana kuwa kitu kimoja, tukaunda nchi moja ya JMT, hivyo sasa Tanzania ni nchi moja tuu ya JMT, Zanzibar sio nchi bali ni sehemu ya JMT.
Kwenye hili la upanuzi wa bandari ya Zanzibar, kama nilivyo jibu kwenye jibu langu la msingi, kinachelewesha ni taratibu tuu, tena kwa taarifa yako, sio tuu kupanua bandari ya Zanzibar bali in future, kuifanya Zanzibar kuwa a free port kama Japan, Singapore na Dubai, makampuni makubwa ya kuuza magari kama Be Forward waweke yard zao Zanzibar, the rest of Africa badala ya kuagiza magari kutoka Japan na Dubai, waagize kutoka Zanzibar !.
Kwavile Zanzibar ni sehemu ya Tanzania, Tanzania ndio baba na Zanzibar ni mtoto, baba ni baba na mtoto ni mtoto, kama ilivyo kwa masikio hayawezi kuzidi kichwa!.
Hili la kuitana ukoloni mara utumwa ni maneno maneno tuu ya vitimbakwiri, Zanzibar inapokea asilimia 4.5% ya misaada yote ya Tanzania inayopokea kutoka nje.
Hivyo kwenye kuleta maendeleo sometimes JMT lazima iidhibiti Zanzibar, ili kuleta even development, mfano kwenye issue ya sukari, Zanzibar ina kiwanda cha sukari ambacho kinazalisha sukari ya kutosha ku suppliers soko la Zanzibar. Huko Zanzibar kilo ya sukari ni TZS 1,500 tuu. SMZ inaruhusu Wafanyabiashara wa Zanzibar import sukuri kutoka nje, matokeo yake sukari inayozalishwa kiwanda cha Zanzibar inadodea kiwandani!.
Wenye kiwanda cha sukari Zanzibar wanataka kuleta sukari hiyo huku bara kwasababu huku bei ni kuanzia TZS 2,500. Serikali ya JMT imewagomea!. Maadam Zanzibar inajitosheleza kwa sukari, tumieni sukari yenu mnayozalisha, na sio mzalishe sukari msiitumie, mtake kutuletea huku bara, huku mkitumia cheap imported sugar, hatuwakubalii!. Lengo la hatua hii muhimu ni kuwalazimisha Zanzibar mjitegemee. Hii ndio kazi ya Baba responsible!.
On top of mgao wa asilimia 4.5% ya pato la taifa, bado Zanzibar tunakupeni umeme bure!, hamlipi!. Tanesco ilitaka kuwazimia umeme, msivyo na shukrani mkasema zimeni tuu, nyie mtawasha vibatari!. Tunawapeni elimu ya juu bure, ajira, mnamiliki ardhi huku, mnafanya biashara huku, maduka makubwa karibu yote huku bara ni ya Wapemba!. Badala ya kutushukuru, ama kweli shukrani ya punda mateke!.
Siku zote tumekuambieni acheni kelele!, maadam mnayo sheria ya kura ya maoni, amueni moja...
Wanzanzibar amueni moja, ama acheni kelele za muungano!, ama pigeni Kura ya Maoni, muamue moja!.
P.