Maswali kuhusu Bandari mpya ya Bagamoyo

Maswali kuhusu Bandari mpya ya Bagamoyo

Bandari ya Dar es Salaam ni badnari ya kawaida. Transshipment ports ni zile zinazofaulisha mizigo kwenda bandari ndogo za karibu.mfano bandari ya singapore inafanya kazi hii. kwa nini transhipment?kuleta meli 20 africa sio economical kama kuleta meli moja kubwa yenye kubeba mizigo yenye ujazo sawa na meli ndogo 20. halafu vimeli vidogo vinachukulia hapo kwenye bandari kupeleka vibandari vyengine. ofcourse itafanya pia mambo mengine mengi.

Huo uhusiano uko sahihihi.

Hii ni bandari muhimu kuliko zote Africa inayojengwa miaka ya hivi karibuni, hizi ni one in a generation investments kama vile Suez Canal. The government did well to secure this investment. I think this is a BOT type of scheme. Wakirudisha fedha zao after 40 years bandari inakuwa ya kwetu 100%. wanaobeza wanasahau Suez Canal kwa mfano haijajengwa leo wala jana. Investment za aina hii hakuna anayeweza kuzirudisha in 5-10 years,kwa hivi vinchi vyetu maskini.

Ukimkopesha mwalimu wa msingi bilioni moja, jiandae kumdai yeye na wajukuu zake, ndio kilichotokea, hapa TZ ni kama mwalimu wa shule ya msingi, kinyume na hapo jua ni utapeli.

Bandari ya dar ina kazi za kutosha, kama kupokea mafuta,na bidhaa nyengine zinazoelekezwa kwa nchi kama Zambia n.k, infact ingekuwa vema kama Bandari ya dar ika-focus kwenye aina flani ya cargo ili kuongeza ufanisi. Bandari ya bagamoyo itakuwa kama Jalala, hakuna itakachoshindwa kupokea/kutuma.

Sina taarifa nyingi kuhusu financing structure.Ila nina uhakika wahusika wapo na wanafahamu zaidi.

Mkuu Kimweri heshima kwako. Wewe ni mmoja wa wanaJF ambao wana michango iliyonyoka kwelikweli. Hebu tunyoshee na hili;

Uwekezaji kama huu wa kampuni ya kichina utakao fanywa hapo bagamoyo port, share holders ni hao wachina peke yao au kuna wengine? Kama kuna wengine ni serikali ya Tanzania au kina nani hawa?
 
JokaKuu,
Umeleta mada mahimu sana na ni matumaini yangu tutapata majibu! Binafsi, kuna wakati nilimtembelea mwana-TPA mmoja na moja ya malengo yangu ilikuwa nikamdodose kuhusu huu mradi... huyu ni mtu wa jikoni na kutokana na wadhifa wake am certain atakuwa anafahamu mengi lakini kwa bahati mbaya hatukuongea kutokana na mazingira niliyoyakuta!

Jambo la msingi kwangu, keeping other issues constant, huu mradi ni muhimu sana kinyume na watu wanavyosema ni kwanini hayo matrilioni yasitumike kupanua bandari ya Dar! Kwa anayeifahamu bandari ya Dar, pale ni kama imefika mwisho na kama tunataka kupata competitive port for the next 100 years basi hatuna budi kutafuta eneo lingine! Kwa huu upanuaji wa kawaida tu, tayari Kurasini inakaribia kuisha (kubomolewa) na sasa inaanza kutafunwa Mivinjeni kwa ajili ya maghala! Katika miaka 10 ijayo, kijiji cha kwanza ukitoka bandarini am sure kitakuwa Mtoni baada ya maeneo ya jirani yote kwisha. Kwahiyo tunahitaji eneo kubwa zaidi unless kama tunataka ku-opt kuendelea kuivunja Temeke!

That's one but concern yangu nyingine ni ule mlango wa bahari kwenye bandari ya Dar es salaam! I doubt ikiwa ule mlango una sifa za kuwa a gateway to a competitive 21st century port where we anticipate the growth of intercontinental business! Ni kama naiona mimeli mikubwa maradufu ya hii tuliyonayo hivi sasa ikija in the next 20 years, mimeli ambayo, kwa mtazamo, si tu kwamba pale bandarini hakuna pa kuya-accomodate bali pia hata ule mlango wenyewe unaweza kuwa changamoto kwa mimeli ya aina hiyo kuingia!

Kwamba hao Wachina wataendesha bandari kwa miaka 40, ktk nchi hii hakuna kinachoshindikana! Ikiwa TICTS walikuta kila kitu kipo kwenye order na bado wakapewa mkataba wa miaka 25, sioni ni nini kitashindikana kuwapa Wachina wanaoanzia at scratch kuwapa mkataba wa 40! Nakumbuka TICTS walipopewa ule mkataba wa awali kabisa (kabla ya kuongeza), unaambiwa in less than 10 years wakawa wamerudisha kila kilicho chao na kuanza kula faida! Unaambiwa liliangushwa bonge la party la kusherehekea mali za wajinga!

Nimejisikia kuumia sana ulipomalizia kuhusu TICTS. Yaani Watanzania tunauzwa bila bei.

Ee Mungu, turehemu watu wako.
 
Last edited by a moderator:
hakuna mwenye nia ya kukata issue humu

Mkuu utakuwa hulitendei haki Jukwaa unapokuwa na issue halafu huileti.

Suala la ushabiki na ujinga huwezi kuliepuka popote lkn pia wenye akili na hekima watakaokuwa wanakata issue hawatakosekana.
 
Inakuwa vigumu sana kijadili hili, mkataba ni siri, nawatz tumelizika nahilo, tena huenda kuna madudu mengi kuliko tunayoyasikia. Kama China anatujengea nakuendesha bandari hii kwa miaka 40 maanake baada ya miaka hiyo kila kitu kitakuwa kimechoka, mradi huu ni sawa kabisa na mkataba wa Mlimani city na UDSM.... Wazungu wale watakabidfhi majengo na project nzima ya mlimani city kwa udsm baada ya kuvuna kwa miaka 35. Haya ni matokeo ya makubaliano ya Friends of Fastjet waliomuingiza ikulu. Leo watu apa wanashadadia friends of Mamvi kuingizwa ikulu bila kujua implication zake mbeleni zitakuwaje.
 
Nimejisikia kuumia sana ulipomalizia kuhusu TICTS. Yaani Watanzania tunauzwa bila bei.

Ee Mungu, turehemu watu wako.
Hilo la TICTS fanya kuliangalia tu hivyo hivyo... ukiupata undani wake unaweza kuugua ndio maana kila leo huwa najiuliza watu wanaomsifia Mkapa wanatumia vigezo gani manake kwenye suala la TICTS Mkapa na serikali yake walionesha taswira yao yao halisi kabisa.... kwanza, waliwapa mkataba wa miaka 15, na Mkapa alipoona anapoondoka, akawaongezea miaka mingine kumi!!!
 
Mijadala km hii wengine ndo imetufanya tujiunge JF so mkuu atheist Km kuna unalojua wee funguka hapa kila mtu anapita wenye Akili timamu na wehu cha muhimu niww kutimiza wajibu wako,,,,!
 
Last edited by a moderator:
Hapa ndio utaona watu wa Tanga na watu wanaotoka Tanga hawana influencetoka walipotaka kumpindua Nyerere

Pesa zilizopelekwa Bagamoyo zilikuwa ziende Tanga...project ilikuwa inaitwa MWAMBANI PORT PROJECT na ilikuwa ni project ya 40 billion usd.

feasibility na kila kitu kilikuwa tayari

wajanja frm BAGAMOYO wakawapiga bao hawa jamaa wa Tanga na wakapata hizo 10 billion usd toka kwa serikali ya china kupitia kitu kinachoitwa EPC na nadhani hawa jamaa walifanya DFBOOT ya mika 40

humu JF hamuwezi kupata habari zaidi kwa sababu watu hawana interest ya kumwaga data kwa kuwa mijadala ya jukwaa hili ni ya chadema na ccm na mangonda na ujunga wakusifiana. hakuna kukata issues wala nini

sioni sababu ya kupoteza muda kuelezea kitu ambacho wote mnajua hatutopata majibu kwa kuwa sirikali inasema ni siri

Aisee umeongea kweli, mijadala inayobamba humu JF ni ile ya Chadema na CCM. Hii mingine ikifika page tatu zenye hoja nzito ni bahati.
 
unapata shida ya bure. taarifa zipo kituo cha uwekezaji TIC au BRELA . ni mguu wako tu au gari lako tu kwenda huko na utapata kwa undani taarifa zote na kwa usahihi
Inasemekana ujenzi wa mradi huu utazinduliwa mwezi July.

Binafsi mpaka sasa hivi sijaweza kupata taarifa za kutosha kuhusu mradi huu mkubwa.

Inaonekana kuna mwekezaji anaitwa CHINA MERCHANTS HOLDINGS INTERNATIONAL ambao ndiyo wadau wakubwa ktk mradi huo.

So far taarifa zote ambazo nimekutana nazo zimeniacha na maswali mengi kuliko majibu.

Kwa mfano, kuna taarifa nimekutana nayo inaelekeza kwamba China Merchants Holdings wataendesha bandari hiyo kwa muda wa miaka 40.

Pia katika mradi huohuo kuna mwekezaji mwingine anaitwa OMAN STATE GENERAL RESERVE FUND ambaye atahusika na eneo huru la kibiashara.

Naomba wenye taarifa zaidi kuhusu mradi huu watueleze. zaidi ningependa kujua nafasi ya serikali ya tanzania, na mamlaka ya bandari TPA ktk mradi huu.


cc Sangarara, salaama, Kimweri, Zitto, laiza, limetumbuka, Nguruvi3, NasDaz, Mdondoaji, Fx Trader, Zitto, Tokyo40, Kibona
 
Mkuu Kimweri heshima kwako. Wewe ni mmoja wa wanaJF ambao wana michango iliyonyoka kwelikweli. Hebu tunyoshee na hili;

Uwekezaji kama huu wa kampuni ya kichina utakao fanywa hapo bagamoyo port, share holders ni hao wachina peke yao au kuna wengine? Kama kuna wengine ni serikali ya Tanzania au kina nani hawa?

Kusema kweli shareholders watakuwa wachina peke yao.wao ndio wataamua structure ya shareholders itakuwaje. kwa ninavyowajua wale jamaa, serikali ya china itawa-back fully, kwani $10B kwa benki za serikali ya China ni pesa ndogo sana, sawa na mkopo wa TZS 1B benki za kitanzania.

Ila stakeholders watakuwa wengi.hapa ndio kuna serikali ya Tanzania, ikiwakilishwa na wizara,TPA etc etc.
 
Aisee umeongea kweli, mijadala inayobamba humu JF ni ile ya Chadema na CCM. Hii mingine ikifika page tatu zenye hoja nzito ni bahati.

CCM wanapenda iwe hivyo.kwani mijadala yenye kumvua "nguo" mfalme afadhali isiwepo. Hilo la TICTS ni timu ya mkapa na wezi wenzie walioamua kujitafutia pensheni ya lazima bila kufuata sheria.

Kuna haja kubwa ya mikataba kama hii kuidhinishwa publicly na bunge inapofikia hatua za mwisho. Sidhani kama hawa TICTS wangeweza kuongezewa miaka 10 kama hili jambo lingewekwa wazi
 
Aisee umeongea kweli, mijadala inayobamba humu JF ni ile ya Chadema na CCM. Hii mingine ikifika page tatu zenye hoja nzito ni bahati.

Mkuu,,,utakuwa hutendi haki kwa cc wengine tusio jichanganya na mambo ya ushabiki wa vyama,,,,Tatizo lakupungua mijadala ya maana humu ni km anavyofanya ndg atheist kususa inapotokea hivyo ndio mijadala yakijinga inaanzishwa yakushabikia vyama lkn Mijadala ya maana inapokuja wasio jitambua wanatulia tu,,,,,!!
 
Last edited by a moderator:
Inasemekana ujenzi wa mradi huu utazinduliwa mwezi July.

Binafsi mpaka sasa hivi sijaweza kupata taarifa za kutosha kuhusu mradi huu mkubwa.

Inaonekana kuna mwekezaji anaitwa CHINA MERCHANTS HOLDINGS INTERNATIONAL ambao ndiyo wadau wakubwa ktk mradi huo.

So far taarifa zote ambazo nimekutana nazo zimeniacha na maswali mengi kuliko majibu.

Kwa mfano, kuna taarifa nimekutana nayo inaelekeza kwamba China Merchants Holdings wataendesha bandari hiyo kwa muda wa miaka 40.

Pia katika mradi huohuo kuna mwekezaji mwingine anaitwa OMAN STATE GENERAL RESERVE FUND ambaye atahusika na eneo huru la kibiashara.

Naomba wenye taarifa zaidi kuhusu mradi huu watueleze. zaidi ningependa kujua nafasi ya serikali ya tanzania, na mamlaka ya bandari TPA ktk mradi huu.


cc Sangarara, salaama, Kimweri, Zitto, laiza, limetumbuka, Nguruvi3, NasDaz, Mdondoaji, Fx Trader, Zitto, Tokyo40, Kibona

Ardhi yote ile wanaotaka
 
..inasemekana eneo linalofaa kwa masuala ya kijeshi[jeshi la majini] liko ukanda wa kusini, kule ambako Jemedari wa Kijerumani, Von Lettow alikuwa ameficha meli zake za kivita wakati wa vita kuu ya kwanza.
Paul Emil von Lettow-Vorbeck (20 March 1870 – 9 March 1964) was a general in the Imperial German Armyand the commander of its forces in the German East Africa campaign. For four years, with a force that never exceeded about 14,000 (3,000 Germans and 11,000 Africans), he held in check a much larger force of 300,000 British, Belgian, and Portuguese troops. Essentially undefeated in the field, Lettow-Vorbeck was the only German commander to successfully invade imperial British soil during the First World War. His exploits in the campaign have been described by Edwin Palmer Hoyt "as the greatest single guerrilla operation in history, and the most successful
 
napata sheeda na hii serikali#BANDARI YA MTWARA Ndio yenye kina kirefu africa mashariki#Chakushangaza haifanyi kazi zaidi ya kupaki meli za mizingo za DANGOTE CEMENT wakati huo bagamoyo ile bandar inatakiwa ichimbwe ili kupata kina sahh cha maji#Hadi hapo kimtazamo wangu serikali haina maono sahh ndio maana hii nchi imefikia pabaya#kwann isifufuriwe bandar ya mtwara ilhali inauwezo kuliko bandar ya dar#NCHI HII INAHITAJI KIONGOZI SAHH NA MWENYE MAAMUZ SAHH ATAKAYEZUIA Huu ujinga
 
CCM wanapenda iwe hivyo.kwani mijadala yenye kumvua "nguo" mfalme afadhali isiwepo. Hilo la TICTS ni timu ya mkapa na wezi wenzie walioamua kujitafutia pensheni ya lazima bila kufuata sheria.

Kuna haja kubwa ya mikataba kama hii kuidhinishwa publicly na bunge inapofikia hatua za mwisho. Sidhani kama hawa TICTS wangeweza kuongezewa miaka 10 kama hili jambo lingewekwa wazi

Nasikia Ndg. Karamagi mwenye hisa TICTS anapambana arudi bungeni kuzima mijadala ya ulaji wake huko TICTS. Sijui ile sheria ya kutenganisha siasa/uongozi na biashara iliishia wapi!

Kwa vyovyote ni vema hata mijadala ya mambo mengine yasiyo vyama/siasa nayo yapewe kipaumbele hapa JF. Kwa mfano sisi wengine hatuna taarifa nzito kama za uzi huu, hivyo wenye taarifa walete na wasio elewe waulize kueleweshawa vema, ndio mjadala unaenda. Na wa mawazo kinzani yasiyo na mahaba ya kivyama nao waje.

Ni kweli siasa ndio kila kitu lakini ni vyema wakati mwengine tukienda moja kwa moja kwenye hivyo vitu badala ya kupitia siasa
 
Inakuwa vigumu sana kijadili hili, mkataba ni siri, nawatz tumelizika nahilo, tena huenda kuna madudu mengi kuliko tunayoyasikia. Kama China anatujengea nakuendesha bandari hii kwa miaka 40 maanake baada ya miaka hiyo kila kitu kitakuwa kimechoka, mradi huu ni sawa kabisa na mkataba wa Mlimani city na UDSM.... Wazungu wale watakabidfhi majengo na project nzima ya mlimani city kwa udsm baada ya kuvuna kwa miaka 35. Haya ni matokeo ya makubaliano ya Friends of Fastjet waliomuingiza ikulu. Leo watu apa wanashadadia friends of Mamvi kuingizwa ikulu bila kujua implication zake mbeleni zitakuwaje.
Kwamba kilakitu kitakuwa kimechoka, hapana coz' hata hiyo bandari ya Dar es salaam sio ya jana wala leo... watu tumezaliwa tumeikuta na hadi leo bado inapiga mzigo!

Ndugu yangu, investment kubwa kama ile usitarajie kwamba unaweza kui-refund ndani ya muda mfupi, NEVER, especially kwa kuangalia uchumi wetu! Kama alivyosema Kimweri, kwa mradi kama ule mtu akikuambia kwamba I'll operate for 10 years ni utapeli binafsi nasema hata akikuambia 20 years itakuwa ni utapeli!

In addition, usidhani kwamba kv hao Wachina wata-operate kwa miaka 40 ndio basi tena Tanzania haitapa chochote; hapana... kodi zetu zitabaki pale pale kwahiyo wakati tunasubiria full ownership ya bandari tayari ndani ya hicho kipindi tutakuwa tumevuna kodi nyingi sana tena sana, si ajabu inayokaribi na kiwango cha uwekezaji kama sio zaidi hapa nikiacha kutaja faida zingine kadhaa za kiuchumi.

Hata hivyo, ni kweli kwamba hapa tunazungumza mambo ya jumla jumla... hatujui terms zinasemaje coz' hapa tusisahau kwamba kuna tofauti kati ya ku-operate na ku-own! Ninavyofahamu ni kwamba Wachina, kupitia China Merchant wata-finance/fund mradi husika na kisha kuu-operate! Hiyo haina maana kwamba watau-own kwa 100%! Unaweza kukuta kwamba, baada ya mradi kukamilika, China Merchant wata-own % na serikali ita-own % fulani over the entire time hadi Wachina watakapo-refund pesa zao ndipo zile %age shares za China zitakapoamishiwa serikalini na kuwa fully owned na serikali/PTA! Hata hivyo, kwa kipindi chote Wachina ndio watakaokuwa na sauti ingawaje hawawezi kuwa na sauti kupitia kodi zetu! Mfano wake, angalia ownership and operation agreement ya visima vya mafuta! Kwamba, hapa investor ana-finance mradi kwa 100% from stage one na ku-operate lakini share ownership ni ya mwekezaji na serikali kupitia TPDC!

JokaKuu
 
kwanini wasiendeleze bandari ya Mtwara na kuipunguzia mzigo bandari ya Dar, bandari ya Mtwara ndiyo bandari yenye kina cha asili kwa Afrika mashariki mpaka pembe ya Afrika tofauti na bandari ya Dar ambayo kila baada ya muda inachimbwa ili kuongeza kina. Bandari ya Mtwara ni ya asili haihitaji kuchimbwa ili kuongeza kina, waiboreshe hii halafu wajenge barabara yenye urefu wa KM 654 ya kutoka Mtwara kwenda Songea kwa kiwango cha lami. Ni kitu cha kushangaza gari inatoka bandari Dar kwenda Msumbiji ila inapita Custom TRA iliyopo ndani bandari ya Mtwara au ufuta kulimwa Mtwara halafu unapelekwa bandari ya Dar kusafirishwa.
 
Kwamba kilakitu kitakuwa kimechoka, hapana coz' hata hiyo bandari ya Dar es salaam sio ya jana wala leo... watu tumezaliwa tumeikuta na hadi leo bado inapiga mzigo!

Ndugu yangu, investment kubwa kama ile usitarajie kwamba unaweza kui-refund ndani ya muda mfupi, NEVER, especially kwa kuangalia uchumi wetu! Kama alivyosema Kimweri, kwa mradi kama ule mtu akikuambia kwamba I'll operate for 10 years ni utapeli binafsi nasema hata akikuambia 20 years itakuwa ni utapeli!

In addition, usidhani kwamba kv hao Wachina wata-operate kwa miaka 40 ndio basi tena Tanzania haitapa chochote; hapana... kodi zetu zitabaki pale pale kwahiyo wakati tunasubiria full ownership ya bandari tayari ndani ya hicho kipindi tutakuwa tumevuna kodi nyingi sana tena sana, si ajabu inayokaribi na kiwango cha uwekezaji kama sio zaidi hapa nikiacha kutaja faida zingine kadhaa za kiuchumi.

Hata hivyo, ni kweli kwamba hapa tunazungumza mambo ya jumla jumla... hatujui terms zinasemaje coz' hapa tusisahau kwamba kuna tofauti kati ya ku-operate na ku-own! Ninavyofahamu ni kwamba Wachina, kupitia China Merchant wata-finance/fund mradi husika na kisha kuu-operate! Hiyo haina maana kwamba watau-own kwa 100%! Unaweza kukuta kwamba, baada ya mradi kukamilika, China Merchant wata-own % na serikali ita-own % fulani over the entire time hadi Wachina watakapo-refund pesa zao ndipo zile %age shares za China zitakapoamishiwa serikalini na kuwa fully owned na serikali/PTA! Hata hivyo, kwa kipindi chote Wachina ndio watakaokuwa na sauti ingawaje hawawezi kuwa na sauti kupitia kodi zetu! Mfano wake, angalia ownership and operation agreement ya visima vya mafuta! Kwamba, hapa investor ana-finance mradi kwa 100% from stage one na ku-operate lakini share ownership ni ya mwekezaji na serikali kupitia TPDC!

JokaKuu

Kwa maana hiyo sisi watanzania hatuwezi kujenga hiyo bandari yaaani kumpa contract hata mchina akafanya kazi ya kujenga tu hiyo bandari?

Shida inakuwa ni nini hapo?
 
Huku ni kule tunakosema kuws Tanzania kutokujua ama kupuuza vipaumbele vyake. Kwa mtu mwenye akili angefuta huo mradi wa Bandari ya Bagamoyo badala yake angeimarisha/Kutanua na kuboresha kwa dhati bandari ya Dar.

Tanzania kama nchi hatuna Tatizo la uwepo wa bandari, Tatizo letu ni bandari zetu kufanya kazi chini yaw kiwango kwa makusudi ama kwa kukosa vifaa. Kwa uwekezaji unaotaka kufanyika Bagamoyo kama tungepaunua na kuboresha ile ya Dar then chenji ambayo ingebaki tungeitumia kujengea miundombinu rahisi ya usafirishaji kama reli ktk nchi zinazotuzunguka na ambazo zinatumia bandari hiyo ya dar hakika Kenya wasingetupata, na hata hawa majirani zetu wanaotukwepa kwepa kamwe wasingefanya hivyo.

Halafu mkuu kwa taarifa nilizonazo ni kwamba China itaimiliki bandari hiyo kwa miaka 50 then baada ya hapo ndo kunapercent ambazo Tanzania tutakuwa tukigawiwa....!!!!!

Ajabu na kweli.

BACK TANGANYIKA

Alafu aliesaini na kutoa maaumizi kipindi hicho hayupo yaani hapo hata bila kusema kufa hupangwa na mungu , tunategemea nini mtu wa miaka 55 au 60 anaingia makubaliano kama hayo. Wenzetu hata kama ana miaka 70 anafanya maamuzi yatakayoinufaisha nchi yake miaka 100 ijayo hata kama atakuwa hayupo kwa kuwa na yeye alikuta watu wameshamjengea mazingira mazuri na aliyakuta
 
Back
Top Bottom