sinza pazuri
JF-Expert Member
- Aug 16, 2014
- 3,470
- 9,228
Maelezo ya Balozi wa Saudi Arabia katika Televisheni ya Taifa ya Saudia ni haya; "Utiaji saini wa Mkataba wa Nia ya kufanya utafiti wa fursa za uwekezaji na ushirikiano wa kujenga na kuendeleza Bandari mpya ya Bagamoyo nchini Tanzania..
======
Kwa mujibu wa shirika la habari la Saudi Arabia (Saudi press agency) linaeleza kuwa Mnamo mwezi Februari 13, 2025 chemba ya Biashara, Viwanda, na Kilimo Tanzania (TCCIA) ilisaini Hati ya Makubaliano ya Ushirikiano (MoU) na Shirikisho la Chemba za Biashara za Saudi Arabia, pamoja na kusaini makubaliano ya ya kibiashara kati ya Saudi na makampuni ya Tanzania kupitia sekta mbalimbali za kiuchumi.
Aidha ubalozi wa Saudi Arabia kupitia ukurasa wake kwenye mtando wa X ulichapisha taarifa iliyonukuliwa kutoka televisheni ya taifa ya ufalme huo (Al-Ikhbariya) ambapo video hiyo inayomuonesha Balozi wa Ufalme huo nchini Tanzania, Yahya Okeish akieleza kuhusu utiaji saini wa mkataba wa nia ya kufanya utafiti wa fursa za uwekezaji na ushirikiano wa kujenga na kuendeleza bandari mpya ya Bagamoyo nchini Tanzania.
Februari 14, 2025 Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Mipango na Uwekezaji Prof. Kitila Mkumbo akizungumza bungeni jijini Dodoma kuhusu ujenzi wa bandari ya Bagamoyo amekanusha madai ya kusainiwa kwa makubalino kuhusu uwekezaji wa Bandari hiyo akisema Serikali haijaingia makubaliano yoyote ya uwekezaji.
"Serikali ipo katika hatua mbalimbali za kutekeleza program ya ujenzi wa eneo maalum la kiuchumi la eneo la Bagamoyo na hili ni moja ya miradi 17 ya kielelezo iliyopo katika mpango wa tatu wa maendeleo ya miaka mitano 2021/22-2025/26"
"Pamoja na mambo mengine eneo hili linahusisha ujenzi wa miradi mingi lakini moja ni ujenzi wa Bandari, Kongani za Viwanda, Kongani za TEHAMA, Ukanda huru wa biashara na kituo cha Reli. Kwahiyo sio mradi mmoja na ndio maana tunaita program"
"Utekelezaji wa program hii utatekelezwa na sekta binafsi kwakushirikiana na serikali kupitia mpango wa ubia katika sekta binafsi na sekta ya umma yaani Public–private partnership (PPP)"
"Wadau mbalimbali kutoka ndani na nje wameonyesha nia ya kuwekeza, wadau hawa wako katika hatua mbalimbali za mazungumza na taasisi husika. Serikali haijaingia makubaliano yoyote na mwekezaji yoyote kwasasa, wala hatuna mkataba na mwekezaji yoyote katika miradi ya Bagamoyo ikiwemo niliyoitaja wa Bandari"
======
Kwa mujibu wa shirika la habari la Saudi Arabia (Saudi press agency) linaeleza kuwa Mnamo mwezi Februari 13, 2025 chemba ya Biashara, Viwanda, na Kilimo Tanzania (TCCIA) ilisaini Hati ya Makubaliano ya Ushirikiano (MoU) na Shirikisho la Chemba za Biashara za Saudi Arabia, pamoja na kusaini makubaliano ya ya kibiashara kati ya Saudi na makampuni ya Tanzania kupitia sekta mbalimbali za kiuchumi.
Aidha ubalozi wa Saudi Arabia kupitia ukurasa wake kwenye mtando wa X ulichapisha taarifa iliyonukuliwa kutoka televisheni ya taifa ya ufalme huo (Al-Ikhbariya) ambapo video hiyo inayomuonesha Balozi wa Ufalme huo nchini Tanzania, Yahya Okeish akieleza kuhusu utiaji saini wa mkataba wa nia ya kufanya utafiti wa fursa za uwekezaji na ushirikiano wa kujenga na kuendeleza bandari mpya ya Bagamoyo nchini Tanzania.
Februari 14, 2025 Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Mipango na Uwekezaji Prof. Kitila Mkumbo akizungumza bungeni jijini Dodoma kuhusu ujenzi wa bandari ya Bagamoyo amekanusha madai ya kusainiwa kwa makubalino kuhusu uwekezaji wa Bandari hiyo akisema Serikali haijaingia makubaliano yoyote ya uwekezaji.
"Serikali ipo katika hatua mbalimbali za kutekeleza program ya ujenzi wa eneo maalum la kiuchumi la eneo la Bagamoyo na hili ni moja ya miradi 17 ya kielelezo iliyopo katika mpango wa tatu wa maendeleo ya miaka mitano 2021/22-2025/26"
"Pamoja na mambo mengine eneo hili linahusisha ujenzi wa miradi mingi lakini moja ni ujenzi wa Bandari, Kongani za Viwanda, Kongani za TEHAMA, Ukanda huru wa biashara na kituo cha Reli. Kwahiyo sio mradi mmoja na ndio maana tunaita program"
"Utekelezaji wa program hii utatekelezwa na sekta binafsi kwakushirikiana na serikali kupitia mpango wa ubia katika sekta binafsi na sekta ya umma yaani Public–private partnership (PPP)"
"Wadau mbalimbali kutoka ndani na nje wameonyesha nia ya kuwekeza, wadau hawa wako katika hatua mbalimbali za mazungumza na taasisi husika. Serikali haijaingia makubaliano yoyote na mwekezaji yoyote kwasasa, wala hatuna mkataba na mwekezaji yoyote katika miradi ya Bagamoyo ikiwemo niliyoitaja wa Bandari"