Video ya Balozi wa Saudi Arabia akitolea maelezo kuhusu mkataba wa bandari ya Bagamoyo

sinza pazuri

JF-Expert Member
Aug 16, 2014
3,470
9,228
Maelezo ya Balozi wa Saudi Arabia katika Televisheni ya Taifa ya Saudia ni haya; "Utiaji saini wa Mkataba wa Nia ya kufanya utafiti wa fursa za uwekezaji na ushirikiano wa kujenga na kuendeleza Bandari mpya ya Bagamoyo nchini Tanzania..


======

Kwa mujibu wa shirika la habari la Saudi Arabia (Saudi press agency) linaeleza kuwa Mnamo mwezi Februari 13, 2025 chemba ya Biashara, Viwanda, na Kilimo Tanzania (TCCIA) ilisaini Hati ya Makubaliano ya Ushirikiano (MoU) na Shirikisho la Chemba za Biashara za Saudi Arabia, pamoja na kusaini makubaliano ya ya kibiashara kati ya Saudi na makampuni ya Tanzania kupitia sekta mbalimbali za kiuchumi.

Aidha ubalozi wa Saudi Arabia kupitia ukurasa wake kwenye mtando wa X ulichapisha taarifa iliyonukuliwa kutoka televisheni ya taifa ya ufalme huo (Al-Ikhbariya) ambapo video hiyo inayomuonesha Balozi wa Ufalme huo nchini Tanzania, Yahya Okeish akieleza kuhusu utiaji saini wa mkataba wa nia ya kufanya utafiti wa fursa za uwekezaji na ushirikiano wa kujenga na kuendeleza bandari mpya ya Bagamoyo nchini Tanzania.

Februari 14, 2025 Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Mipango na Uwekezaji Prof. Kitila Mkumbo akizungumza bungeni jijini Dodoma kuhusu ujenzi wa bandari ya Bagamoyo amekanusha madai ya kusainiwa kwa makubalino kuhusu uwekezaji wa Bandari hiyo akisema Serikali haijaingia makubaliano yoyote ya uwekezaji.

"Serikali ipo katika hatua mbalimbali za kutekeleza program ya ujenzi wa eneo maalum la kiuchumi la eneo la Bagamoyo na hili ni moja ya miradi 17 ya kielelezo iliyopo katika mpango wa tatu wa maendeleo ya miaka mitano 2021/22-2025/26"

"Pamoja na mambo mengine eneo hili linahusisha ujenzi wa miradi mingi lakini moja ni ujenzi wa Bandari, Kongani za Viwanda, Kongani za TEHAMA, Ukanda huru wa biashara na kituo cha Reli. Kwahiyo sio mradi mmoja na ndio maana tunaita program"

"Utekelezaji wa program hii utatekelezwa na sekta binafsi kwakushirikiana na serikali kupitia mpango wa ubia katika sekta binafsi na sekta ya umma yaani Public–private partnership (PPP)"

"Wadau mbalimbali kutoka ndani na nje wameonyesha nia ya kuwekeza, wadau hawa wako katika hatua mbalimbali za mazungumza na taasisi husika. Serikali haijaingia makubaliano yoyote na mwekezaji yoyote kwasasa, wala hatuna mkataba na mwekezaji yoyote katika miradi ya Bagamoyo ikiwemo niliyoitaja wa Bandari"
 
Maelezo ya Balozi wa Saudi Arabia katika Televisheni ya Taifa ya Saudia ni haya; "Utiaji saini wa Mkataba wa Nia ya kufanya utafiti wa fursa za uwekezaji na ushirikiano wa kujenga na kuendeleza Bandari mpya ya Bagamoyo nchini Tanzania..
View attachment 3235962

Epuka fake news, hakuna bandari iliyouzwa.
Inaanzaga hivyo hivyo, taratibu Tu kutoka kwenye fake news Hadi kwenye ukweli....
 
CCM watakuja kufa na wasiende peponi wala kuzimu
IMG-20250214-WA0000.jpg
 
Maelezo ya Balozi wa Saudi Arabia katika Televisheni ya Taifa ya Saudia ni haya; "Utiaji saini wa Mkataba wa Nia ya kufanya utafiti wa fursa za uwekezaji na ushirikiano wa kujenga na kuendeleza Bandari mpya ya Bagamoyo nchini Tanzania..
View attachment 3235962

Epuka fake news, hakuna bandari iliyouzwa.
Akina kitila Mkumboaiding/ wanaacha Mzazibari anaiuza Tanganyika! Very sad! May be ao wameshapata uraia wa Saidia kikinuka wanatokome na familia zao! Time will tell
 
Akina kitila Mkumboaiding/ wanaacha Mzazibari anaiuza Tanganyika! Very sad! May be ao wameshapata uraia wa Saidia kikinuka wanatokome na familia zao! Time will tell
Wapi Tanzania imeuzwa?

Hii style ya uongo na kuchafua watu ndio imekuwa lifestyle ya Chadema.

Akiifanya Lissu kwa Mbowe mnajifanya mmeumia kumbe ukabila unawasumbua.
 
Nimekupa habari iloyotoka kwenye kinywa cha balozi. Wewe unarudia kuchapisha habari ya uongo kwa kuwa ndio inakupa furaha.

Kwa nini vijana wa Chadema mnampenda uzushi?
Naona mashoga m1ivamia mziki makaweza mkataka mvamie Mpira mkafurushwa Sasa mnataka kuvamia siasa
 
Deal imefanyika wapi?

Umememsikia na kumuelewa balozi?
Acheni uzushi na umbeya jengeni chama.
Dogo,
Soma hii taarifa hapa chini ambayo ni ya huko huko Saudia ikithibitisha kuwa tayari washapewa bandari ya Bagamoyo...
👇

SAUDI ARABIA ACQUIRES TANZANIA’S ’s BAGAMOYO PORT

The Tanzanian authorities granted the Saudi African Investment and Development Co. (SADC) concession and acquisition rights for Bagamoyo Port in Tanzania, Saudi Press Agency reported, citing Chairman of Federation of Saudi Chambers of Commerce Hassan Al-Huwaizi.

The approval is part of SADC's "East Gateway Project," aimed at the East African region.

The initiative will bolster Saudi Arabia’s position as a key driver of global economic development, attract greater foreign investment (particularly in Africa), and strengthen its logistical capacity to deliver Saudi exports worldwide.

At the Saudi-Tanzanian Business Forum, supported by the Saudi Chambers, the Kingdom took a strategic step to strengthen economic ties with Zanzibar and explore new investment opportunities in the region, as part of its broader initiative to expand into African markets.

The Port of Bagamoyo holds significant strategic value for Saudi Arabia, serving as East Africa's primary logistical gateway. It will facilitate trade for Tanzania and neighboring countries, becoming the central hub for exporting African raw materials and natural resources globally, and for importing goods into Africa.


Saudi Arabia acquires Tanzania’s Bagamoyo port Saudi Arabia acquires Tanzania’s Bagamoyo port

Na taarifa ya ndani ya Tanzania juu ya hilo deal ni hii hapa chini...

Saudi Arabia acquires Bagamoyo Port in Tanzania as part of the “East Gate” project | The Guardian Saudi Arabia acquires Bagamoyo Port in Tanzania as part of the “East Gate” project | The Guardian
 
Kwanza nikueleze mtu anayeweza kujadili na mimi kuhusu uwekezaji wa bandari umu ni Chige na MALCOM LUMUMBA tu. Wengine mnapiga kelele.
 
Sawa, unge POST kwenya INBOX zao mkajadili. Sio sehemu sahihi ku post public ilihali unajipambanua uko na watu wachache mnaoweza kujadili nao.

Ni hayo tu 🙏🏾.
Wewe kweli kilaza, mimi nimepost taarifa ya balozi ambayo ni sahihi. Sio ule uzushi wa bandari imeuzwa.
 
Back
Top Bottom