Maswali kuhusu Bandari mpya ya Bagamoyo

Maswali kuhusu Bandari mpya ya Bagamoyo

JokaKuu

Platinum Member
Joined
Jul 31, 2006
Posts
37,868
Reaction score
71,627
Inasemekana ujenzi wa mradi huu utazinduliwa mwezi July.

Binafsi mpaka sasa hivi sijaweza kupata taarifa za kutosha kuhusu mradi huu mkubwa.

Inaonekana kuna mwekezaji anaitwa CHINA MERCHANTS HOLDINGS INTERNATIONAL ambao ndiyo wadau wakubwa ktk mradi huo.

So far taarifa zote ambazo nimekutana nazo zimeniacha na maswali mengi kuliko majibu.

Kwa mfano, kuna taarifa nimekutana nayo inaelekeza kwamba China Merchants Holdings wataendesha bandari hiyo kwa muda wa miaka 40.

Pia katika mradi huohuo kuna mwekezaji mwingine anaitwa OMAN STATE GENERAL RESERVE FUND ambaye atahusika na eneo huru la kibiashara.

Naomba wenye taarifa zaidi kuhusu mradi huu watueleze. zaidi ningependa kujua nafasi ya serikali ya tanzania, na mamlaka ya bandari TPA ktk mradi huu.


cc Sangarara, salaama, Kimweri, Zitto, laiza, limetumbuka, Nguruvi3, NasDaz, Mdondoaji, Fx Trader, Zitto, Tokyo40, Kibona
 
Taarifa niliyonayo mimi ni kwamba, mwambao wote huo inakozungumzwa kujengwa bandari hiyo unamilikiwa na Mtanzania mwenzetu na hao china nani sijui wanapanga hiyo ardhi kwake, na wameishaanza kulipia rent.

Mkataba wa pango uko complicated kidogo sababu uko governed na sharia za China.

watakuja hapa wataalamu wa PPP watakuelezea vizuri.
 
Ukisha sikia mkataba umesainiwa hapa Tanzania,jua tumesha pigwa bao kidizaini.Chezea CCM wewe?Maamuzi magumu october ni muhimu.Hiyo mikata tutakuja kufanya review
 
Huku ni kule tunakosema kuws Tanzania kutokujua ama kupuuza vipaumbele vyake. Kwa mtu mwenye akili angefuta huo mradi wa Bandari ya Bagamoyo badala yake angeimarisha/Kutanua na kuboresha kwa dhati bandari ya Dar.

Tanzania kama nchi hatuna Tatizo la uwepo wa bandari, Tatizo letu ni bandari zetu kufanya kazi chini yaw kiwango kwa makusudi ama kwa kukosa vifaa. Kwa uwekezaji unaotaka kufanyika Bagamoyo kama tungepaunua na kuboresha ile ya Dar then chenji ambayo ingebaki tungeitumia kujengea miundombinu rahisi ya usafirishaji kama reli ktk nchi zinazotuzunguka na ambazo zinatumia bandari hiyo ya dar hakika Kenya wasingetupata, na hata hawa majirani zetu wanaotukwepa kwepa kamwe wasingefanya hivyo.

Halafu mkuu kwa taarifa nilizonazo ni kwamba China itaimiliki bandari hiyo kwa miaka 50 then baada ya hapo ndo kunapercent ambazo Tanzania tutakuwa tukigawiwa....!!!!!

Ajabu na kweli.

BACK TANGANYIKA
 
JokaKuu,
Umeleta mada mahimu sana na ni matumaini yangu tutapata majibu! Binafsi, kuna wakati nilimtembelea mwana-TPA mmoja na moja ya malengo yangu ilikuwa nikamdodose kuhusu huu mradi... huyu ni mtu wa jikoni na kutokana na wadhifa wake am certain atakuwa anafahamu mengi lakini kwa bahati mbaya hatukuongea kutokana na mazingira niliyoyakuta!

Jambo la msingi kwangu, keeping other issues constant, huu mradi ni muhimu sana kinyume na watu wanavyosema ni kwanini hayo matrilioni yasitumike kupanua bandari ya Dar! Kwa anayeifahamu bandari ya Dar, pale ni kama imefika mwisho na kama tunataka kupata competitive port for the next 100 years basi hatuna budi kutafuta eneo lingine! Kwa huu upanuaji wa kawaida tu, tayari Kurasini inakaribia kuisha (kubomolewa) na sasa inaanza kutafunwa Mivinjeni kwa ajili ya maghala! Katika miaka 10 ijayo, kijiji cha kwanza ukitoka bandarini am sure kitakuwa Mtoni baada ya maeneo ya jirani yote kwisha. Kwahiyo tunahitaji eneo kubwa zaidi unless kama tunataka ku-opt kuendelea kuivunja Temeke!

That's one but concern yangu nyingine ni ule mlango wa bahari kwenye bandari ya Dar es salaam! I doubt ikiwa ule mlango una sifa za kuwa a gateway to a competitive 21st century port where we anticipate the growth of intercontinental business! Ni kama naiona mimeli mikubwa maradufu ya hii tuliyonayo hivi sasa ikija in the next 20 years, mimeli ambayo, kwa mtazamo, si tu kwamba pale bandarini hakuna pa kuya-accomodate bali pia hata ule mlango wenyewe unaweza kuwa changamoto kwa mimeli ya aina hiyo kuingia!

Kwamba hao Wachina wataendesha bandari kwa miaka 40, ktk nchi hii hakuna kinachoshindikana! Ikiwa TICTS walikuta kila kitu kipo kwenye order na bado wakapewa mkataba wa miaka 25, sioni ni nini kitashindikana kuwapa Wachina wanaoanzia at scratch kuwapa mkataba wa 40! Nakumbuka TICTS walipopewa ule mkataba wa awali kabisa (kabla ya kuongeza), unaambiwa in less than 10 years wakawa wamerudisha kila kilicho chao na kuanza kula faida! Unaambiwa liliangushwa bonge la party la kusherehekea mali za wajinga!
 
Last edited by a moderator:
kikwete ni mtu hatari sana daaaah! anatukamua hadi damu
 
Mzee, licha ya Bagamoyo kuwa strategic zone, kiutaalamu Bagamoyo haifai kujenga bandari. Tukilazimisha, tutajenga bandari moja badala ya mbili kigharama. Bagamoyo ni shallow waters yenye miamba migumu sana. Ukijenga bandari utalazimika kupasua miamba yenye gharama sawa na kujenga bandari nyingine. Kwanini tusiipanue Tanga ambayo ni deep waters na ipo kwenye strategic zone pia? Tuache dhana ya kila Rais kupendelea kwake. Itaigharimu nchi sana ki.pu.MBA.fu.
 
Hivi kwanini hio hela haijatumika kuboresha bandari ya tanga ajili ya kuteka soko la kaskazini ili kuwa port ya rwanda,uganda na hata areas the south Sudan ikiwa ina shindana na Mombasa. Pia iboreshe bandari ya mtwara kwa ajili ya kuservice zambia,drc and other aouthern countries. Dar port ibaki mainly for our own goods? Mimi sielewi kabisa bandari mpya bagamoyo inajengwa ya nini badala ya kuboresha hizo 2 ambazo strategically ziko kuzuri zaidi. Hawa wawekezaji kweli hawana hata huruma chembe na sisi hata baada ya kutambua viongozi wetu wana logical thinking capacity ya chimpanzees?
 
Hivi kwanini hio hela haijatumika kuboresha bandari ya tanga ajili ya kuteka soko la kaskazini ili kuwa port ya rwanda,uganda na hata areas the south Sudan ikiwa ina shindana na Mombasa. Pia iboreshe bandari ya mtwara kwa ajili ya kuservice zambia,drc and other aouthern countries. Dar port ibaki mainly for our own goods? Mimi sielewi kabisa bandari mpya bagamoyo inajengwa ya nini badala ya kuboresha hizo 2 ambazo strategically ziko kuzuri zaidi. Hawa wawekezaji kweli hawana hata huruma chembe na sisi hata baada ya kutambua viongozi wetu wana logical thinking capacity ya chimpanzees?

Ukiwa na high logical thinking and reasoning, kwa kweli unaweza kudondoka kwa maamuz ambayo HAYANA TIJA kwa Taifa, kiuchumi hailisaidii sana Taifa. Ni purely ubinafsi, lakini kutoka moyoni haina maana kwa sasa kujenga bandari mpya kabla ya kukamilisha uboreshaji mkubwa kwanza wa zilizopo tayari! Sielewi lakini kwangu nadhani kama Taifa tuna shida kubwa katika vipaumbele!

Kwa mfano mimi binafsi ukiniuliza BRT na Flyovers nini kingeanza jibu langu lingekuwa flyovers( overpass and underpass) kwenye makutano ya barabara kubwa( Ubungo,Tazara,Morocco, Chang'ombe, VETA, Magomeni na Sealander) kwanza.

Wote leo tumesikia kuhusu azma ya kuhamisha kituo cha mabasi ya mkoani pale Ubungo kuwa itabaki palepale lakini ilivunjwa. Unatafakar unakosa majibu!
 
Hao watunga sera wana matatizo kichwani hasa kwenye kuweka sawa vipaumbele vya nchi.

Hiyo hela ya huo mradi ingetosha kupanua bandari za mtwara, dar na tanga kwa wakati mmoja na chenji itakayobaki tukawekeza kwenye reli kuunganisha.
 
Maswali ya nyongeza, kwa kuwa maelezo yako hayaja lifafanua hili, je bandari hii itakuwa chini ya TPA au Mamlaka ya Bandari China(MBC)?

Je bandari hii itakuwa mshirika wa bandari zilizoko au itakuwa mshindani?

Je kwa kuwa mizingo mingi ingiayo nchini ya wezekana inatoka China, Wachina hawata pendelea zaidi bandari yao hivyo kufifisha hizi zilizopo tayari?

Je baada ya miaka hii 40 ya uendeshaji wa Wachina Tanzania itakabidhiwa bandari yenye hali gani, miundo mbinu endelevu au magofu?

Je makuli wa Bandari hii watatoka China ua Tz? Maana kuna taarifa kuwa makuli wa China niwa gharama rahisi kuliko wa hapa.

Je....? Ok niache kwanza nitaendelea nikijibiwa haya.
 
Taarifa niliyonayo mimi ni kwamba, mwambao wote huo inakozungumzwa kujengwa bandari hiyo unamilikiwa na Mtanzania mwenzetu na hao china nani sijui wanapanga hiyo ardhi kwake, na wameishaanza kulipia rent.

Mkataba wa pango uko complicated kidogo sababu uko governed na sharia za China.

watakuja hapa wataalamu wa PPP watakuelezea vizuri.

Habari zimezagaa mitaani, kwamba huyo "Mtanzania mwenzetu" eti ni Kikwete, na eti kisa cha kumwondoa Mwakyembe katika Wizara inayohusika na Bandari, ni kwa sababu Mwakyembe alikuwa hatilii uzito umuhimu wa kuharakisha ujenzi wa Bandari ya Bagamoyo, kwa kuona ni vema kuboresha Bandari ya Dar Es Salaam, wakati JK anataka mradi wa Bandari ya Bagamoyo ushughulikiwe "fasta fasta"! Kama habari hii ni kweli, basi JK atakuwa kweli ni Profesa!!!!!
 
Hapa ndio utaona watu wa Tanga na watu wanaotoka Tanga hawana influencetoka walipotaka kumpindua Nyerere

Pesa zilizopelekwa Bagamoyo zilikuwa ziende Tanga...project ilikuwa inaitwa MWAMBANI PORT PROJECT na ilikuwa ni project ya 40 billion usd.

feasibility na kila kitu kilikuwa tayari

wajanja frm BAGAMOYO wakawapiga bao hawa jamaa wa Tanga na wakapata hizo 10 billion usd toka kwa serikali ya china kupitia kitu kinachoitwa EPC na nadhani hawa jamaa walifanya DFBOOT ya mika 40

humu JF hamuwezi kupata habari zaidi kwa sababu watu hawana interest ya kumwaga data kwa kuwa mijadala ya jukwaa hili ni ya chadema na ccm na mangonda na ujunga wakusifiana. hakuna kukata issues wala nini

sioni sababu ya kupoteza muda kuelezea kitu ambacho wote mnajua hatutopata majibu kwa kuwa sirikali inasema ni siri
 
Back
Top Bottom