afsa
JF-Expert Member
- Dec 6, 2012
- 1,986
- 1,592
Warioba asipoangalia atazeeka mara mbili yeye akae kimywa dawa iweze kuingia alipotosha sana sasa moto unamwakia anajuta na mikono kichwani.
we makalio/malaya unataka umuzeeshe?
Warioba asipoangalia atazeeka mara mbili yeye akae kimywa dawa iweze kuingia alipotosha sana sasa moto unamwakia anajuta na mikono kichwani.
-Warioba amebariki Serikali ya tatu kwa kigezo cha maoni ya wananchi kwa kutumia takwimu
-Wanaompinga nao wanasema takwimu alizotumia siyo za kweli.
-Mfumo aliotumia wa "sampling" haukufuata kanuni za mfumo huo
-Hakuweka takwmu za mabaraza ya katiba
Hivyo kusema kuwa maoni ya Serikali tatu ni maoni ya wananchi siyo. Kwa maana hiyo Warioba alitakiwa kujibu hoja hizi na siyo kutuletea tena maswali.
Komba naye anamtukana WARIOBA.!!!?? Hapana jamani. Its too much.
-Warioba amebariki Serikali ya tatu kwa kigezo cha maoni ya wananchi kwa kutumia takwimu
-Wanaompinga nao wanasema takwimu alizotumia siyo za kweli.
-Mfumo aliotumia wa "sampling" haukufuata kanuni za mfumo huo
-Hakuweka takwmu za mabaraza ya katiba
Hivyo kusema kuwa maoni ya Serikali tatu ni maoni ya wananchi siyo. Kwa maana hiyo Warioba alitakiwa kujibu hoja hizi na siyo kutuletea tena maswali.
Hivi nyinyi watu kweli mnafikiri? Sheria inawaruhusu kabisa kumuita tena Warioba kwenye BMK. Kwanini basi mnaogopa kumuita Warioba ili azitolee ufafanunuzi hizo hoja zenu mnazodai. Mnataka Warioba akazitolee wapi hoja zenu? Choo.ni? get real dude. Juzi nilimsikia Hawa Ghasia akisema kwamba Judge Warioba afunge mdomo wake. Awaachie wao (wawakilishi) wa wananchi wafanye kazi yao. Hivi kweli Hawa Ghasia ni mtu wa kumwambia Warioba afunge MDOMO WAKE! Kama anagekuwa TL amesema maneno hayo tena kwa former PM of URT sasa hivi ingekuwa HULLABALOO! Lakini kwa CCM wao wana kibari cha kumtukana mtu yeyote with IMPUNITY.
Mzee Warioba amewapa za usoni MaCCM, sidhani kama kuna anayeweza kujibu hayo maswali kama Dr Vitumbua ameshauri kurudi tena kwa wananchi...
kwani ni wananchi wote waliomtaka Kiwete awe raisi? 629 walioko kwenye BMK sasa ni wengi kuliko wananchi waliopendekeza serikali tatu? Fikiri tena!Tume ya jaji warioba upande wa mfumo wa muungano wamekosea mh mbunge, alafu si wananchi wote walopropose serikali 3,
Hiyo kitu italigawa taifa in the longrun it is obvious.
Umeusemea moyo wangu. Kura ingekuwa ya siri mambo yangekuwa magumu kwa chama tawala.Kinywa hutamka yaujazayo moyo! Waliobaki mjengoni ukiwaangalia kwa makini wanapotoa michango yao (kama ina hadhi ya kuitwa michango at all) utabaini hawako settled, even their vocal tones are hollow, their inner fears are vivid and you can even feel their pounding heartbeats though they pretend to be poised. The inner silent voice is haunting them, they are afraid!
Usiite watu mbumbumbu mkuu, si ustaarabu.
Sijawai fanya takwimu,
Sijafuata maelekezo ya yeyote yule, nimewaza mwenyewe nikachanganya na wanosema ukawa na walio against ukawa nimeconclude serikali 3 italeta matatizo, nitapigia kura mbili,
Ni maoni tu
Hukumsoma vizuri: Alichomaanisha ni kwamba nchi moja haiwezi kuwa na ma amiri jeshi wakuu zaidi ya mmoja. Shein pekee ndo anapigiwa mizinga 21 zenji. Kwa si JK kufanyiwa hivyo? Fikiri tena!anadai eti wanajeshi wamechoka kupiga mizinga 21 mara mbili,pointless.
![]()
Dar es Salaam. Aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba ameuliza maswali saba ya msingi kwa wajumbe wa Bunge la Katiba wanaopinga Rasimu ya Katiba iliyotolewa na Tume yake akitaka wawajibu wananchi ili kutuliza kiu yao.
Jaji Warioba ambaye tangu awasilishe Rasimu ya Katiba Desemba 30, mwaka jana amegeuka kuwa adui kwa watu wanaotaka muundo wa serikali mbili, aliuliza maswali hayo jana katika uzinduzi wa ripoti ya utafiti wa Taasisi ya Twaweza kuhusu mchakato wa Katiba.
Akizungumza kwa ukali, Jaji Warioba alisema: Kwanza, jibuni kwa nini mnapinga muundo wa Muungano wakati walioupendekeza ni wananchi?
Sheria inasema uwepo wa Muungano na mapendekezo katika rasimu hayasemi Muungano usiwepo. Kumbukeni kuwa wananchi walitakiwa kutoa mapendekezo ya namna ya kuboresha Muungano.
Katika swali lake la pili, Warioba alisema kwa nini Tanganyika imevaa koti la Muungano? Kwa kuwa katika ukusanyaji wa maoni wananchi walieleza kuwa Serikali ya Muungano ya sasa siyo ya Muungano, ni ya Tanganyika.
Katika swali la tatu alisema wajumbe hao wanatakiwa kujibu maelezo ya wananchi ambao waliieleza tume hiyo kuwa Katiba imevunjwa na madaraka ya rais yamechukuliwa na sasa kuna marais wawili katika nchi moja.
Tume inapewa lawama kubwa, wajibuni wananchi hii tume ilitumwa na nani kukusanya maoni ya wananchi? Waambieni ilikusanya maoni hayo kwa kutumia sheria ipi zaidi ya ile ya Mabadiliko ya Katiba? alisema Jaji Warioba katika swali lake la nne.
Katika swali lake la tano, Warioba aliwataka wajumbe hao kutoa sababu za kumtuhumu kuwa amependekeza muundo wa serikali tatu kwa sababu yeye pamoja na (Joseph Butiku) walikuwa wajumbe wa Tume ya Jaji Kisanga na Jaji Nyalali ambazo nazo zilipendekeza muundo wa serikali tatu, kitu ambacho alisema si kweli na hawakuwahi kuwa mjumbe wa tume hizo.
Pia, aliwataka wajumbe hao kujibu swali la sita, kwa nini hawataki kuzungumzia yaliyomo katika Rasimu ya Katiba na badala yake wanageuza rasimu hiyo kuwa imeandikwa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba.
Katika swali lake la saba, aliwataka wajumbe kujibu kwa nini wanaishutumu Tume ya Mabadiliko ya Katiba kuwa imeingiza maoni yake, wakati ilikusanya maoni hayo kwa mujibu wa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba?
Alisema badala ya kujadili hoja za msingi, wajumbe wa Bunge hilo wamekuwa wakitoa lugha za kejeli na matusi kwa baadhi ya watu (akiwamo na yeye), kitendo ambacho alisema si sahihi na kinaweza kuligawa taifa kwa sababu yaliyomo katika Rasimu ya Katiba yametokana na maoni ya wananchi.
Katika uzinduzi huo walikuwepo baadhi ya wajumbe wa Bunge hilo ambao ni Dk Hamisi Kigwangalla aliyemwakilisha Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana, Julius Mtatiro, Maria Sarungi na aliyekuwa mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Humphrey Polepole.
Amshukia Lukuvi
Katika maelezo yake, Jaji Warioba alieleza kushangazwa kwake na wajumbe kulitumia Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), kama mfano wa kuwashawishi Watanzania kukubaliana na matakwa yao ya kutaka kupinga mfumo wa serikali tatu.
Nchi hii imekuwa na matatizo ya rushwa na ufisadi, lakini hakuna hata siku moja mtu amesema jeshi linaweza kushika madaraka. Leo kwa sababu ya madaraka mnaingiza jeshi na mchakato wa Katiba katika makundi.
Licha ya kutomtaja mlengwa, kauli hiyo ilionekana kumlenga Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera Uratibu na Bunge), William Lukuvi ambaye Aprili 13, mwaka huu aliwataka wananchi kupinga muundo wa serikali tatu, akisema la sivyo jeshi linaweza kuchukua madaraka.
Akiwa katika Kanisa la Methodist, Jimbo la Dodoma alipokuwa mgeni rasmi akimwakilisha Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, Lukuvi alisema muundo huo ukipita, nchi itatawaliwa na jeshi kwa kuwa Serikali ya Muungano itashindwa kuwalipa mishahara wanajeshi.
Kauli kama hiyo pia iliwahi kutolewa na Rais Jakaya Kikwete wakati akizindua Bunge Maalumu la Katiba mjini Dodoma.
Msiliingize jeshi katika siasa za makundi na inakuwa mbaya zaidi kama mkienda katika makanisa na kutoa kauli za namna hii, alisema Warioba na kuongeza:
Umoja wetu, amani na utulivu kwa kiwango kikubwa mhimili wake ni viongozi wa dini. Wamekuwa wakihubiri umoja, amani na mshikamano, hivyo tusiingize siasa za makundi kwenye makanisa na misikiti.
Jaji Warioba aliwataka wajumbe wa Bunge hilo kukumbuka wajibu wao wa kuwaunganisha wananchi na kuwataka waachane na kauli za kejeli, kuudhi na matusi kwani zinaweza kuleta mgawanyiko na mpasuko nchini.
Nimekuwa mtumishi wa umma kwa muda mrefu lakini sijawahi kuona taasisi yenye uzalendo wa hali ya juu kama JWTZ, alisema Warioba.
Warioba ambaye amewahi kuwa Waziri Mkuu na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Tanzania, kuanzia mwaka 1985 hadi 1990, alisema: Katika ziara zangu mikoani nilikuwa nikikutana na wanajeshi na kunieleza matatizo yao. Licha ya wakati huo serikali za mataifa mengine zilikuwa zikipinduliwa na jeshi, hapa kwetu ilikuwa tofauti, walikuwa na uzalendo wa hali ya juu licha ya kuwa hali yetu kiuchumi ilikuwa mbaya, alisema.
Alisema wakati huo wanajeshi walikuwa wakivaa sare zilizochakaa na viatu vilivyopasuka, lakini hawakufikiria kuipindua Serikali.
Alisema hata katika vita dhidi ya Uganda, wanajeshi wa Tanzania walishinda kwa sababu ya uzalendo na siyo vifaa vya kisasa vya kivita... Inashangaza kuona watu wanatolea mfano mmoja tu wa kama wanajeshi wasipolipwa; kwa nini wasiseme mawaziri au watumishi wa serikali wasipolipwa?
Alisema kauli hiyo ni sawa na kuwaeleza wananchi kuwa jeshi ni baya na kama ikipita Katiba isiyoendana na matakwa ya walio wengi jeshi litachukua nchi.
Alisema wakati Tume ya Mabadiliko ya Katiba ikikusanya maoni ya wananchi, wanajeshi na viongozi wa vyombo vya ulinzi na usalama nchini walijikita zaidi kutoa maoni ya kuimarishwa kwa ulinzi na usalama na siyo mambo mengine.
Tatizo ambalo walitueleza ni kuchoshwa na kitendo cha kupiga mizinga 21 kwa Amri Jeshi Mkuu wakiwa Dar es Salaam na wakiwa Zanzibar. Walisema kwa nidhamu ya jeshi, Amri Jeshi Mkuu ni mmoja tu. Nadhani mngewaondolea kero hiyo na si mambo mengine, alisisitiza.
Kigwangalla
Kwa upande wake, Dk Kigwangalla alisema kama tatizo ni Muungano ni vyema suala hilo likarejeshwa upya kwa wananchi ili watoe maoni yao kwa sababu mchakato huo sasa umehamia katika muundo wa Muungano pekee.
Mchakato huu si wa kuifufua Tanganyika na kuvunja mkataba wa Muungano na siyo wa kubadili muundo wa utawala. Mambo haya yalihitaji mchakato unaojitegemea, alisema.
Alisema tume zote zilizotoa mapendekezo ya Serikali tatu zilikuwa na asilimia ndogo ya watu waliounga mkono kama ilivyo kwa Tume ya Jaji Warioba.
Source: Mwananchi
Warioba kama binadamu ni halali kujibu au kuwauliza maswali wajumbe hawa, lakini nahisi tofauti yake na wajumbe hawa ni kubwa sana. Uchambuzi wote unaosikika bungeni ni wa kuelekezwa kabisa. Waliowengi hawana uwezo wa kusoma document kubwa kama hii ya katiba. Siamini kabisa kwamba watu kama Nchemba, Hawa Ghasia, Sendeka, Komba, n.k. wana uwezo wa kusoma kwa makini na kuweza kukumbuka yaliyoandikwa na baadaye eti wachambue.
Hawa ni watu ambao hawana hata ufahamu wa Dunia inavyokwenda. Pale Bungeni mtu kama Sendeka kapangwa kukaa na mtu anayemsaidia kupanga ya kuzungumza, msaidizi mwenyewe naye ni hoi! Kwa ujumla hatuna wabunge na bunge lilihalibiwa na uteuzi. Aina ya wajumbe na ubora wao uko chini sana.
unachoweza kuona ni kwamba baadhi ya watu walio na uwezo mkubwa wanashindwa kuzungumza. Wengine tuliotegemea waonyeshe ufahamu mkubwa wameamua kujikomba na kujidai eti ni wasomi wazoefu, wanajua kuchambua takwimu, n.k. Lakini wako hoi na hata ukiwatafuta google hawajawahi kuhangaika na takwimu wengine kwa miaka 10 iliyopita. Mtafute Tibaijuka, mtafute yule wa UD anaitwa Francis, mtafute yule wa SU anaitwa Asei, mtafute Magembe, mtafute Msola, wote hawana kabisa zile basics za takwimu. Ni aibu kwamba hata wanaofundisha vyuo vikuu wamaekuwa ni chini ya mwanafunzi wa sekondari anayejua haki yake ya kupikiwa chakula kiive.
Huwa najiuliza ulinzi anaoutegemea Warioba ni wa Mungu ama ni wa hao hao anao pambana nao???
Au kuna nini kinachoendelea??? Maana dunia ya sasa kuondoana maisha ni sekunde tu.
anadai eti wanajeshi wamechoka kupiga mizinga 21 mara mbili,pointless.
Warioba asipoangalia atazeeka mara mbili yeye akae kimywa dawa iweze kuingia alipotosha sana sasa moto unamwakia anajuta na mikono kichwani.
Hivi tunaweza kuanza tena kuhoji juu ya mauti yasiyotarajiwa yaliyomkuta Dr. Sengodo Mvungi!?Yoga, ujue hizo ni tuhuma tu ambazo zinatolewa na wajumbe kutoka CCM. Kwa busara ya kawaida kabisa, kama wajumbe hao wana mashaka na TAKWIMU za Judge Warioba. Basi walitakiwa kumuita tena ndani ya BMK kuzitolea ufafanuzi takwimu zake. Kama angeshindwa kuwaondolea mashaka wajumbe, basi ndiyo wangekuwa na HAKI ya kumutuhuma kwamba AMEPIKA takwimu. Lakini CCM hawawezi kamwe kumuruhusu Warioba kurudi tena kwenye BMK kutoa ufafanuzi wa takwimu zake. Guess why?..
Ndugu yangu tatizo ni wale ambao walitaka Warioba aje na mawazo yao! ndio maana wanatumia nguvu nyingi sana badala ya kutumia Hoja, embu jiulize kitu kimoja, Muungano umedumu kwa miaka 50 sasa, maana yake tunapoujadili sasa tunatakiwa tuujadili katika mfumo ulio bora zaidi na si mfumo unaotugawa au ule ule uliopo, bali uwe mfumo unaozidi kutuunganisha, maana baada ya tarehe 26/4/1961 tumekuwa wamoja sana tumeshirikiana katika mambo mengi, Hivyo tulitakiwa tuzungumzie muundo wa serikali 1. Na si 2 au 3. Ukiona tuko palepale ujue tatizo ni kubwa na tunakoelekea ni kugawana mbao.