Maswali 7 ya Jaji Joseph Sinde Warioba

Maswali 7 ya Jaji Joseph Sinde Warioba

Hivi nyinyi watu kweli mnafikiri? Sheria inawaruhusu kabisa kumuita tena Warioba kwenye BMK. Kwanini basi mnaogopa kumuita Warioba ili azitolee ufafanunuzi hizo hoja zenu mnazodai. Mnataka Warioba akazitolee wapi hoja zenu? Choo.ni? get real dude. Juzi nilimsikia Hawa Ghasia akisema kwamba Judge Warioba afunge mdomo wake. Awaachie wao (wawakilishi) wa wananchi wafanye kazi yao. Hivi kweli Hawa Ghasia ni mtu wa kumwambia Warioba afunge MDOMO WAKE! Kama anagekuwa TL amesema maneno hayo tena kwa former PM of URT sasa hivi ingekuwa HULLABALOO! Lakini kwa CCM wao wana kibari cha kumtukana mtu yeyote with IMPUNITY.

Wewe ndo unajiita unafikiri?? kwani hayo maswali si aliyajenga katika kujibu hoja? aliyaulizia wapi hayo maswali? chooni? ni kwamba hana majibu ya hoja na maswali yanayoulizwa kuhusu rasimu ya tume yake. Hawa Ghasia ana haki ya kumuambia afunge mdomo wake kwa kuwa anachokifanya ni kupigia debe serikali 3 badala ya kujibu hoja za msingi. Kwa hiyo wewe umemuona Hawa Ghasia kakosea kwa kumuambia Jaji Warioba afunge mdomo wake kisa ni former PM? na sio Tundu Lissu aliyemuambia Mwl Nyerere muasisi wa taifa letu kuwa alikuwa akiishi kwa uwongo na kuwalaghai watanzania?
 
Wewe ndo unajiita unafikiri?? kwani hayo maswali si aliyajenga katika kujibu hoja? aliyaulizia wapi hayo maswali? chooni? ni kwamba hana majibu ya hoja na maswali yanayoulizwa kuhusu rasimu ya tume yake. Hawa Ghasia ana haki ya kumuambia afunge mdomo wake kwa kuwa anachokifanya ni kupigia debe serikali 3 badala ya kujibu hoja za msingi. Kwa hiyo wewe umemuona Hawa Ghasia kakosea kwa kumuambia Jaji Warioba afunge mdomo wake kisa ni former PM? na sio Tundu Lissu aliyemuambia Mwl Nyerere muasisi wa taifa letu kuwa alikuwa akiishi kwa uwongo na kuwalaghai watanzania?





Nikushangae kidogo! Kwa mtazamo wangu hapo hakuna aliye sahihi hapo! Si lisu wala si hawa ghasia wote wamekosea kwa kuwa siasa si vijembe, si matusi si upotoshaji kama hawa wawili walivyo kwisha fanya!


Mi nikuhoji kama warioba hana hoja za kujibu maswali aliyo ulizwa ina maana si mtu makini! Si mtu makini kwa kuwa hakuna alicho kifanya ndio maana hana cha kujibu!


Hii inamaana data zake juu ya taarifa zake nizakupika! Sasa ilikuwaje taasisi kubwa na inayo heshimiwa hapa nchini kuteua mtubovu kiasi hicho?

Ina maana taaasisi hiyo nibovu zaidi ya uteuzi wake kwa kutokuwa makini na uteuzi wake?

Tatizo ni misimamo ya vyama! Nakutokuwa na uvumilivu wa kisiasa kwa kumini kuwa unajua kuliko wanao jua kuea unajua! Hatufiki!
 
Warioba asipoangalia atazeeka mara mbili yeye akae kimywa dawa iweze kuingia alipotosha sana sasa moto unamwakia anajuta na mikono kichwani.

Ama kweli propaganda ni hatari sana. Mawazo yako si tofauti na ya Bi. Kilembwe wa tamthiliya ya Kivuli Kinaishi. Eti Warioba kapotosha. Naomba uthibitishe kisayansi tena kwa hoja KUNTU kama si ujuha uliopandikizwa kichwani na unga wa ndele uliolishwa na Bi. Kilembwe wa sasa
 
Warioba ninge mwelewa kama ange toa hoja za msingi zaidi ya hizo mfano! Wajumbe wengi kila wanapo simama kuchangia utawasikia wana sema takwim zilizo pelekea kupatikana kwa rasim hiyo si sahihi, wengine si za kweli, wengine hazina mashiko na nk!

Kwa mtazamo huo kuna kiwango flani cha kitakwimu wajumbe wanadhani hicho kinge fikiwa basi maoni hayo yangekuwa valid! Sasa kwanini wanaendelea kijadili kitu ambacho hakina takwimu sahihi? Basi wavunje bunge watengeneze sample size inayo takiwa waipe tume nyingine irudi tena kwa wananchi ikusanye maoni kwa kiwango wanacho taka then wajadili upya!

Lakini pia hivi wao rasimu iliyo pendekeza serikali mbili wameitoa wapi? wanasema wanachi wanataka serikali mbili hiyo research waliifanya wapi saa ngapi na kwa nani na waka andika wapi ripoti yao kwa ajiri ya reference?

Lakini pia swali lingine la kujiuliza kama tume ya warioba iliyopewa kazi ya kukusanya maoni kisheria imefanya kazi mbovu kama wanavyo sema hawaoni ni tusi kwa aliye wateua pia? Kwamba hakuwa makini katika uteuzi wake kwa kuteua watu mizigo ambao wametumia gharama kubwa na kuleta kitu kisicho faaa?


Kwa mtazamo huu najenga picha kuwa kumbe hakukua na haja ya kuunda tume kwa kua wajumbe walio teuliwa walikuwa na maoni kabisa ya wanachi kwa nini wasinge enda tu moja kwa moja bungeni na kuyatoa huko wakatengeneza na rasimu yao waka ipitisha moja kwa moja?

Tusichezeane akili na hivi vyama vya siasa! Ifike mahala watu tuwe wakweli kama mnania ya kufanya kitu kifanyike sio kupindisha pindisha mambo mgekuwa wote mnataka umoja wakitaifa ninge waelewa kama mnataka serikali 1, mkawashawishi na wanachi lakini kwa kuwa kila chama kimeweka maslahi yake mbele ndio maana kila mtu anataka muundo wa serikali utako vutia maslahi yake!


Tanzania ya serikali moja kwanza!

Hapo kwenye red; kwanini iwe ni tusi kwa aliyewateua? acheni hoja za kubangaiza, huku ni kwa vile tu mmekosa hoja.
Kama hata baadhi ya wateule wa Mungu wanaasi (vitabu vya dini vinatuambia) je hilo ni tusi kwa Mungu? itakuwaje sembuse kwa mteule wa mwanadamu?
Mteuzi hachafuki kwa lolote eti tu kwa sababu ya uchafu wa mteule wake. Walioteuliwa wanaweza wakawa na sifa zote za uteuzi lakini wakaenda kinyume na taaluma yao kwa sababu ya matakwa ya matamanio binafsi ya nafsi zao. Kikwete kama mtu mwingine yeyote ni mwanadamu, atamteua mtu kwa taaluma na sifa zake na sio kwa usafi wa moyo wake kwa kuwa yeye Kikwete kama mwanadamu hawezi kuujua moyo wa mtu. Kilichoko moyoni kwa mtu ni siri kati yake na Mungu tu,.... otherwise mtuambie kama mnataka kumgeuza Kikwete leo kuwa Mungu.
Mteuzi kumkosoa mteule wake kwamba amekosea huo ni ujasiri na mteuzi kumkingia kifua mteule wake hata kama amekosea huo ni udhaifu,... Kikwete ni Jasiri.

Tena ni demokrasia iliyoje kwa mteuzi na mteule kupishana kauli,..... Laiti tume ya warioba ingekuja na kauli sawa na ya Kikwete, nyinyi leo hii mngegeuka na kusema tume imefanya kazi kwa shinikizo la Rais jinsi mlivyo wanafiki, kwani ni uwongo??? si tuliona hapa mara tu baada ya tume kuundwa wapo waliosema tume itafanya kazi kwa kulipa fadhila za mteuzi wao na sio kwa ajili ya wananchi? leo hii tume imepishana kauli na Rais mnasema ni aibu kwa rais.

Hiyo ndio demokrasia, karibuni kwenye nchi ya demokrasia chini ya utawala wa Kikwete
 
Hawa CCM wanacheza na akili za watanzania. Na sisi waTZ tumezidi kuwa mbumbumbu mno,tuamke sasa tujitambue..tusijekumbuka shuka kumekucha!
 
Tume ya jaji warioba upande wa mfumo wa muungano wamekosea mh mbunge, alafu si wananchi wote walopropose serikali 3,
Hiyo kitu italigawa taifa in the longrun it is obvious.
Usiwe mvivu wa kufikiri kama majumbe wa bmk, amehoji maswali 7 jaribu kuyajibu japo baadhi hatuendeshwi na hisia za mtu mmoja mmoja.
Muungano ukiwa ni wa wananchi ccm hawana cha kuogopa ila kama ni wa viongozi kweli utalindwa kwa gharama yeyote hata kwa kwa kumwaga damu kama mwaka 2001 kule Pemba
 
-Warioba amebariki Serikali ya tatu kwa kigezo cha maoni ya wananchi kwa kutumia takwimu
-Wanaompinga nao wanasema takwimu alizotumia siyo za kweli.
-Mfumo aliotumia wa "sampling" haukufuata kanuni za mfumo huo
-Hakuweka takwmu za mabaraza ya katiba
Hivyo kusema kuwa maoni ya Serikali tatu ni maoni ya wananchi siyo. Kwa maana hiyo Warioba alitakiwa kujibu hoja hizi na siyo kutuletea tena maswali.

unaongea hivyo kwa kuwa kwenye mabalaza kuna kundi kubwa la ccm?
Kwani ccm wako wangapi nchi hii?
Acheni kupotosha watu, takwimu ndo hizohizo!
 
!
!
jeshi linaweza kuasi. Wako sahihi kwani jeshi lenyewe ni la ovyo ovyo tu. Badala ya kukomaa na tafiti mbalimbali jeshi letu lipo busy na gesi mtwara
Una hakika na unachokisema?Jeshi priority ni kufanya tafiti? Huna tofauti na Lukuvi kwani huna sbb ya kuliita ni la ovyo ovyo kwa vigezo dhaifu.
Unajua kuwa kuna amiri jeshi mkuu ambae jeshi limeapa kumtii na operesheni zote lazima azi saction?Kwa akili hiyo mbovu unatuambia jeshi limeenda Mtwara kwa mapenzi yake si kwa ruhusa ya amiri jeshi? Give us a break bhanaa,tendea haki jukwaa that is too low
 
Huwa najiuliza ulinzi anaoutegemea Warioba ni wa Mungu ama ni wa hao hao anao pambana nao???

Au kuna nini kinachoendelea??? Maana dunia ya sasa kuondoana maisha ni sekunde tu.

Umewakumbuka wang'oa kucha nn? Chezea liwalo na liwe weye!
 
Muingiliano wa Mamlaka kati ya Tume na BMK Muda huu ni wa BMK Tume muda wake umekwisha Warioba hakutakiwa kujibu chochote wala Mjumbe wa Tume hawakupaswa kutoa Ufafanuzi tendo la kutoa Ufafanuzi wakati Rasimu inajadiliwa ni sawa na kuharibu Mchakato wa BMK Je wabunge hatukuwaamini kama hatukuwaamini kwanini wasingetolewa tumechelewa na lilibaki ni Kura ya Ndiyo au Hapana toka kwa Wananchi.
 
Tume ya jaji warioba upande wa mfumo wa muungano wamekosea mh mbunge, alafu si wananchi wote walopropose serikali 3,
Hiyo kitu italigawa taifa in the longrun it is obvious.

Ungeandika tu kiswahili,huku kujitutumua na lugha ya watu matokeo yake ni kuishia kupata fedheha.
 
Warioba asipoangalia atazeeka mara mbili yeye akae kimywa dawa iweze kuingia alipotosha sana sasa moto unamwakia anajuta na mikono kichwani.

Huna lolote,akae kimya kisa Hawa Ghasia anatoa uharo bungeni,hayo maswali nyie Intarahamwe yajibuni kama kweli mnajiamini,au mnasubiri mwongozo wa M/kiti wenu.
 
Mkimaliza huo u simba na yanga mtamkumbuka Warioba na tume yake. Swali? Umewahi kuiona serikali inayojipinga yenyewe? HII NI MARA YA KWANZA KWA BUNGE KUPINGA TUME YAKE TENA YA RAIS..AJABU! Kidogo nikubaliane na Mtikila kuwa hii ni laana ya Taifa kumkataa Mungu.

Wote ni waongo hapa sio rais wala wenzie interlahamwa
 
Huwezi kumjibu mtu ambaye una hakika hataelewa majibu yako. Ni sahihi kuuliza swali rahisi ili akijibu, anakuwa ameelewa hata alichouliza yeye mwenyewe.

Nawe unaamini takwimu za warioba ni mbaya na zilikusanywa vibaya? Au, zilitafsiliwa vibaya? Sema halafu tukusaidie kuwafikishia wajumbe wenzako.

We can't be cow dung like you!

Jibu ni NDIO.
Takwimu za tume ya Warioba zina makosa, tena makosa makubwa ambayo yanafanya kila hitimisho lililoegemea takwimu hizo kuwa na makosa. Tena mbaya zaidi ni kwamba makosa yao si ya kibahati mbaya ya kiubinadam, isipokuwa ni ya makusudi na yaliyopangwa ili tu yaakisi utashi wao binafsi kwa kutumia mwamvuli wa utashi wa wananchi. Huku ni kuwahadaa watanzania na kuwafanya ni mbumbumbu kwa kugeuza maoni yao binafsi kuwa ni ya wananchi kama wanavyotaka kutuaminisha.
Na hata kama takwimu zao zingekuwa ni sahihi, lakini bado hitimisho lao la serikali 3 halikubaliani na takwimu zao wao wenyewe japo ni za nadharia tu na si uhalisia.
 
Warioba kama binadamu ni halali kujibu au kuwauliza maswali wajumbe hawa, lakini nahisi tofauti yake na wajumbe hawa ni kubwa sana. Uchambuzi wote unaosikika bungeni ni wa kuelekezwa kabisa. Waliowengi hawana uwezo wa kusoma document kubwa kama hii ya katiba. Siamini kabisa kwamba watu kama Nchemba, Hawa Ghasia, Sendeka, Komba, n.k. wana uwezo wa kusoma kwa makini na kuweza kukumbuka yaliyoandikwa na baadaye eti wachambue.

Hawa ni watu ambao hawana hata ufahamu wa Dunia inavyokwenda. Pale Bungeni mtu kama Sendeka kapangwa kukaa na mtu anayemsaidia kupanga ya kuzungumza, msaidizi mwenyewe naye ni hoi! Kwa ujumla hatuna wabunge na bunge lilihalibiwa na uteuzi. Aina ya wajumbe na ubora wao uko chini sana.

unachoweza kuona ni kwamba baadhi ya watu walio na uwezo mkubwa wanashindwa kuzungumza. Wengine tuliotegemea waonyeshe ufahamu mkubwa wameamua kujikomba na kujidai eti ni wasomi wazoefu, wanajua kuchambua takwimu, n.k. Lakini wako hoi na hata ukiwatafuta google hawajawahi kuhangaika na takwimu wengine kwa miaka 10 iliyopita. Mtafute Tibaijuka, mtafute yule wa UD anaitwa Francis, mtafute yule wa SU anaitwa Asei, mtafute Magembe, mtafute Msola, wote hawana kabisa zile basics za takwimu. Ni aibu kwamba hata wanaofundisha vyuo vikuu wamaekuwa ni chini ya mwanafunzi wa sekondari anayejua haki yake ya kupikiwa chakula kiive.

Ukweli mtupu!
 
Warioba amevurugwa kwa kiasi kikubwa sana anashindwa afanye lipi kwenye maisha yake alivyodanganya alijua kuwa kazi imeisha kumbe alikuwa anajaribu kina cha maji kwa miguu yote miwili.

tehe tehe tehe! kama wewe ulivyovurugwa huko nyuma!
 
Usiite watu mbumbumbu mkuu, si ustaarabu.
Sijawai fanya takwimu,
Sijafuata maelekezo ya yeyote yule, nimewaza mwenyewe nikachanganya na wanosema ukawa na walio against ukawa nimeconclude serikali 3 italeta matatizo, nitapigia kura mbili,
Ni maoni tu

kama wewe siyo pimbi, na matatizo yaliyoletwa na serikali 2 kwa miaka hamsini yataishaje na lini?
 
Warioba amezeeka,tena mbaya zaidi amezeeka ubongo! tofauti na Hayati Baba wa Taifa Julius K.Nyerere ambaye inasemekana kadri alivyokuwa anazeeka ndivyo akili yake ilivyokuwa inakuwa kali kama ''WEMBE"! Kama kweli maswali hayo yametoka kwa WARIOBA basi naomba apumzike! Ni maswali ya KITOTO kabisa! Swali lake la kwanza, katiba hiyo haijatokana na Wananchi wa Tanzania! Tunakubali ni wananchi kwa maana ya Warioba na wajumbe wake wa Tume basi! Yako wapi maoni ya Mabaraza ambayo ndiyo yalikuwa uwe msingi wa rasimu ya pili! WARIOBA JIBU HILO KWANZA!
Na wewe ni mmoja wao waliokaririshwa "yako wapi maoni ya mabaraza",umetoka ndani ya Bunge ukakimbilia na huku kuandika ugolo wako,hiyo ngojera ya maoni ya mabaraza tunaisikia sana Bungeni,usituchoshe na ngonjera zako, jibuni maswali 7 ya Mzee Warioba.
 
Back
Top Bottom