Kwa taarifa yako Rasimu hii kwa sura ya kwanza na sita haitaji hata phd ya kuichambua inajionesha wazi mapungufu yake, Kwanza kwa takwimu za maoni hazijakidhi uwakilishi, pia muundo wenyewe na mambo ya msingi kuhusu Manufaa na hasara za kuwa na serikali tatu, kama katiba pia kuna hofu ambayo hata tume imekili juu Ya uhai wa serikali yenyewe sasa kwa nn msikubaliane na maoni ya wanaotaka serikali mbili? Ni ubishi ambao hauna maana yeyote na kutaka kuwabebesha mzigo watanzania kwa manufaa ya kisiasa, ni dhahili kbs msingi wa hoja ya serikali tatu ni hitaji la kisiasa, na tunaposema ki siasa nina maanisha kuwa kuna kundi linataka kutawala au kuwa sehemu ya utawala kwa kupitia katiba lakini cyo kwa manufaa ya wananchi ambao ndio wadau wa hiyo serikali yenyewe.. kuna hoja ya tume kuwa haya ni maoni ya wananchi , tujiulize ni mwananchi gani wa kawaida ambaye ana kero za maji, afya, elimu ,ajira ,malipo ya uzeeni , mishahara kwa watumishi kama wa elimu na kadhalika akaona Jibu la kuwa na serikali ya tatu atapata ufumbuzi?,, hii c kweli kbs, wakati wa mchakato tulimbiwa tupunguze madaraka ya Rais,halafu leo wajumbe wengine wanasema kuwa Rais wa jamhuri amepokonywa madaraka, na wakati huo huo tunaongeza serikali ingine,, jambo lingine tume inasema serikali washirika zitasimamia mambo yao ya maendeleo huku serikali.za mitaa ambazo ndizo karibu na wananchi mnaziondoa hii imekaaje? Ki uhalisia tunahitaji mjadala mpaka juu ya Huu muundo na mm naona kuna haja ya kurudi kwa wanachi juu ya hii sura ya kwanza na sita na cyo kuwaa hia wajumbe wa bunge maalumu sababu wengine wanakichukulia ki siasa zaidi.