Master j, madam rita na salama siku za kuaibishwa na kulia zaja

Kuna watu mnachanganya mambo hapa sasa sijui ni ushabiki manesema majaji walikuwa wanampigia debe hirman kila wiki jana katoka mnasema wamechakachua matokeo wamemtoa kwa hila wakati kila siku wanampigia debe kuna watu hawapigi kura wanabaki kuwa mashabiki wa kuangalia kingine jana master j kafanya kitendo kibaya sana hivi niambie wale madada wawili misoji watakuwa wanajisikiaje yaani master j kasimama kakunja karatasi kaondoka na salama yaani inamaanisha wale madada hawkustahili kuwa pale
 
Nimepata habari kuwa mpiga gitaa ndio ameandaliwa mwaka huu kushinda maana mshindi hajawahi kutokea upande wa pili (Kama urais vile),na kumbuka wadhamini wa mwaka huu ndio kule kule,stay tuned
 
Tunawezaje kuwaamini majaji wa Epic Bongo Stars search hususani kuhusu upigaji wa kura. Kwa nini kusingekuwa na screen counts tuone vividly jinsi watu walivyopiga kura ngapi kwa nani. Nimehisi hujuma ya wazi kwa kijana Norman aliyeondolewa leo. Kuna mazingira matatu ambayo ni ya wazi ambayo hatuyapendi nayo ni:

1. Mtangazaji wa kike anapowaita na kuwatambulisha waimbaji yuko biased sana mfano anatoa sifa kibao kwa Salma Yusuf eti gitaa girl, Nshama na Wababa n.k Ukweli huyu guitar girl hana sauti (vocal) yeyote ya maana kuliko Norman. Nasema anaweza kuwa mpiga chombo na mjuzi wa muziki (nota) kama somo lakini talent ya kuimba wala kuperform jukwaani ni chini ya kiwango sana kuliko Norman na wengine wote. Anapoimba anabana sauti na anatoa sauti ya mwikwaruzo!

2. Majaji wanavyombeba Salma na Nshama pia ni bayana kwa kuonesha double stds. Wakati wa kutafuta washiriki mikoani kuna watu kibao waliingia katika mashindano toka huko Mwanza, Dodoma, hata Dar walikuwa wakali sana wa matumizi ya vyombo vya muziki na kuimba, Master J akawa anawakataa akisema kuwa waimbe tena bila vyombo maana wanatafuta mwimbaji na si mpiga vyombo. Pili, majaji wote hata Madam Rita hamkuwa mnawahitaji watu waliokuwa wanakuja na nyimbo za kiutamaduni eti kwa kuwa hiyo si miziki au style mnayoitafuta. Ni aibu sana leo tunashuhudia mkiwabeba na kuwapigia saluti akina Nshama na mwenzake yule mrefu (sikumbuki jina lake) ambaye sauti yake naye iko chini na anaimba nje ya key kila wakati anapenda kuimba nyimbo za utamaduni za Afrika kusini au za akina Helen Kijo. Je, mnataka kutuambia kuwa utamaduni wa mwafrika nje ya Tanzania ni bora kuliko ule wa wa Msukuma au Mnyamwezi, Mzigua n.k ambao uliwasilishwa kwa kiwango cha juu sana na washiriki mwazoni. Pitieni kimya kimya zile video zenu za mwanzoni huko Mwanza, Tanga muone. Majaji, mnaaibisha sana na double standards zenu halafu eti wakati wa kutoa matokeo kumfukuza Norman ili kumuandalia ‘guitar girl njia na ushindi’mnajifanya kukimbia toka jukwaani kuwa mmesikitika au kuwalaumu wapiga kura! Kila mtu anawaona kuwa mnajihuzunisha mbele ya screen kama ze comedy wanavyoweza kuamua kulia wakati hakika hawana huzuni wowote!

3. Uchunguzi zaidi ni kuwa hawa vijana washiriki walipopelekwa katika moja ya Stars Hotel nchini eti kameraman wa BSS akawa anamtafuta yeye Norman kwa karibu kuonyesha vituko au ushamba wake mezani (unbecoming table manners) mfano kumuonyesha Norman akinyanyua bakuli lake la supu toka mezani au alipojikuna kichwani akiwa mezani. This is such a very poor way of looking for a way to discredit a talented participant. Kwa jina la wote wapenda haki duniani chukueni video ya siku kijana huyu ameimba wimbo wa Lionel Richie; nasema haijatokea katika BSS, hata Richie mwenyewe hakufikia hapo kama huyu kijana alivyoimba siku hiyo maana nilitokwa na machozi ya furaha kumuangalia. Nimesikitika sana.

Madam Rita kumbuka kuwa kufanya biashara za dhuruma ni dhabi na ni kosa la jinai. Juzi tu Lance Amstrong kavuliwa medali zake zote za ubingwa wa dunia za miaka ya nyuma yote katika kuendesha baiskeli kwa kasi kwa sababu ya udanganyifu. Hizo siku za kuaibishwa na kulia zaja kwa BSS hata kama ni baada ya miaka mitano maana tutapitia video zote polepole na kudemand kura zilivyopigwa maana record zipo kwenye servers na ndipo tutawavua ubingwa wote mnaowabeba na kukulazimisha wewe Rita urudishe fedha za ufadhili na zile ambazo zinapatikana tokana na waliopiga simu kuwapa faida makampuni ya simu ambayo mnapanga nao matokeo toka mwanzo. Kwa nini usiwe unahusisha majaji wengine wataalamu wa muziki toka Bagamoyo ili kuwa objective & transparent? why always rafiki zako akina master J na Salama ambaye hana sifa yoyote na muziki isipokuwa kuwashushua watu walivyovaa au kuwambia watafute kazi nyingine lugha za kihuni sana kwa vijana wanaotafuta kujiendeleza kimziki.

Hongera sana kwa kufuatilia kipindi hiki kwa umakini?,nakuunga mkono lakini kumbuka haya yote hayajana kenye hii BSS tu yapo tangu kilipoanza miaka hiyo iliyopita,cha msingi kwa abbu ao wanajua wanakifanya na kunufaika achana nao kam kuna mambo ya msingi endelea nayo mkuu watakupoteze muda hao.

wewe hii BSS umei take very serious aisee....

Ni kweli jamaa yuko juu kwelikweli kwenye ufuatiliaji wa hii kitu.

Kibunago ulichoandika hapo juu kina ukweli tena zaidi ya ukweli. Tatizo ni serikali yako imeshindwa kuwekeza na kusimamia vipaji vya vijana badala yake inamwachia mtu binafsi ambaye anaweza hata kunichagua mie niwe winner while mimi sina kipaji.

Hapa sasa unaanza kuchafua,ina maana wewe si serikali yako kama wewe si mtanania na unaishi nje ya nchi hii sawa endelea lakini kuwa makini,halafu pili serikali ina mambo mengi sana ya kufanya kama ambavyo umekuwa ukiilalamikia kwamba haitekelezi ahadi zake sasa unataka ianze na programu za kusimamia masuala ya vipaji vya waimbaji?,hata hao BSS wanawakilisha serikali hiyohiyo unayoilaumu kwa ababu ndio wamewapa kibali cha kufanya hivyo bada ya kuona kwamba ni sehemu ya kusaidia kuinua vipaji mkuu.

Huyu madam Rita asiye na hata mume mnampa kichwa. Huyu ni chakula ya wakubwa na kuwadi wao kama Rahma Kharoos "rais' wa kampuni la mafuta la mkuu ambaye amemgeuza nyumba ndogo. Siku ya mambo yao kuwekwa hadharani mtashangaa. Kwani Bongo kuna wafanya biashara au wasanii tu? Ipo siku mtajua uchafu wao na mtashangaa waliwezaje kuwazuga muda wote huo.

Aiseeeee kaka haya maneno ni mazito sana na kama ungeweza kushuka kwa data nadhani ungelipata komenti nyingi za kukupongea,lakini kwa sababu umeshindwa kumwaga,jiandae kupata za uso humu ndani.

Tanzania ina watu wa ajabu sana. Mwanaume unabandika kurasa 3 kisa bongo lala search!

Kesho njoo na nusu ukurasa kuhusu kilimo mkuu

Lakini kumbuka ni haki yake kufanya hivyo usimdharau!
 
Ukitaka jua upigani wa kura wa watz muulize Mrema 1995 na Mbowe 2005


Hata wao walikuwa washabiki wa Norman, lakini ndio hivyo hana swaga
Kwani, kura hizo haziwi audited??

Kama unadhani kumtoa Norman ilikuwa sahihi, umeshajiuliza ni kwanini majaji waliamua kukimbia jukwaa wakati Norman anatangazwa kutolewa? hukumuona hata Master J alivyosema anajua watu hawatoamini kilichokuwa kinatokea?

Ni ukweli kwamba walijua mtu wanayemtoa hakustahili kutolewa. Mtu kama Menynar wamembeba sana hadi baadae wakaona habebeki wakaamua kumtoa.
 
Kwa majuma kadhaa nimekuwa nikifuatilia kipindi hiki na ukweli ni kwamba washiriki wale wote ni washindi kwa sababu moja kuwa kila mtu ana ladha yake na mashabaiki wake. Kumkandia yule salma sioni kama ni sahihi sana kwa sababu kadhaa lakini lilokubwa sana naamini pia majaji wanaangalia na weledi wao wanapokuwa pale kambini sisi tunaangaliaga hasa siku moja ile ya Jumapili usiku. Yule mzanzibari ni lady from another planet tusimuonee gere, muziki anaujua kuupiga mpaka kuuimba.

Kimsingi nakubaliana na mtoa hoja kuhusu upigwaji wa kura, lakini yeye angependekeza tu yawepo maboresho ya kuwepo zile kampuni za mahesabu kama ernest & young, pwc ama yeyote kutupa imani kama wanavyofanya wale watu wa Tusker, ila hii ni kazi ya wadhamini sio wao.

Lakini all in all tukumbuke kuwa mshindi lazima apatikane na lazima awe mmoja. Mimi nilisikitika sana kijana wa Arusha alivyotoka lakini ni ukweli ninaoujua sikumpigia kura japo nilikuwa napenda sauti yake. Rule of the game ni kupiga kura na ni kama kamari, unapopiga wewe ujue kuna na wengine wengi zaidi wanampigia mtu flan kama wababa na wengineo. Kwa kuwa kwa kipindi hiki haiangaliwi nani anajua kuimba kuliko mwingine ni vyema kupiga kura kwa wingi iwezekanavyo kuliko kulalama. Naweza kukuthibitishia kuwa wale wote ni wakali na wanajua kuimba ila sheria ya mchezo inachukua mkondo wake.

Utakumbuka vijana kadhaa waliopita BSS wakashinda na wakapata hela waliishia kutoa single moja na wamepotea katika game kabisa wewe unawajua, na wale ambao walikuwa karibu na mshindi wako hot katika game na wanafanya vema mfano mzuri Msechu, Rogers na wengineo.

Kimsingi sioni sababu ya kuwalalamikia majaji wetu kwa sababu kiukweli sioni maslahi yoyote kwao kufanya hivyo, mimi naona kwamba wao wanalazimika kulinda institution yao kwa gharama yoyote na si kwa kuwahadaha watu, ama kutufurahisha sisi wote jambo ambalo haliwezekani 'it is very difficulty to please every one' Kumshambulia mtu kuhusiasha maisha yake binafsi na kazi zake nahisi kama ni ushamba ama utoto kidogo, mtu kuwa nyumba ndogo ya mtu sioni kama inaingiliana na mada hii, tubadilikeni jombaaa!

Na-declare kuwa sina interest yoyote na majaji ama washiriki, ila mimi ni mshabiki wa muziki na wanamuziki.
 
Nsami,Walter na dada wa gitaa ,wananifurahisha!!
Kazi kubwa sasa ni kupiga kura !!

hii * SEARCH ni mtu mmoja tu mwenye talent halisi - Walter, ana sauti very unique, anaizidi hata ya Diamond ambayo anagezea nyimbo zake. Hata majaji wameanza kumkubali huyu kijana, ambae mwanzoni walikuwa wakimuona wa kawaida tu na wapiga kura wakifata mkumbo wakitaka kumngoa. The rest ni kawaida sana yaani.

Huyo Norman anastaili kutoka tu mbona. halafu majajji wajanja saana ukiwa unatoka wanajifanya kukukosoa unapomaliza nyimbo yako, huyu Norman walimwabia anatafunatafuna maneno ya kiswanglish, yule dada mwingine wakasema ana gubu, ananunanuna, wee waangalie judgement yao wakijua unatoka, unafiki unafi halaf eti wana walk out .


Mshindi ni huyo mwenye sauti unique , really entertainer,
 
Ukitaka jua upigani wa kura wa watz muulize Mrema 1995 na Mbowe 2005


Hata wao walikuwa washabiki wa Norman, lakini ndio hivyo hana swaga
Kwani, kura hizo haziwi audited??


Hii mifumo ya uchakachuaji kama NEC ya Makame na mwenzake Kivuitu ndio tunaipiga vita kwa nguvu zote.

Kila mshiriki ana watu wanaomuunga mkono, ndio maana hatuamini kwamba Norman alitolewa kwa haki kwakuwa tupo tuliompigia kura. Sasa kama BSS wanauhakika kwamba hatukumpigia kura za kutosha tunataka tuone kila mshiriki kapata kura ngapi.

Na kwakuwa sasa wao wenyewe hawaaminiki tena kama wanaweza wakatenda haki hapo ndipo kinahitajika chombo huru cha kusimamia suala la upigaji wa kura. Kama wanadhani kura za wananchi hazina nafasi basi wasiendelee kuwaibia watu kwa kuwataka wapige kura ilihali wameshapanga mshindi.

Tangu BSS imeanza hawajawahi kutoa mshindi mwenye kipaji kama wanavyotaka kuaminisha watu, na hapo ndipo tunadhani ni muhimu wabadilike na kuacha uhuni wanaofanyia vijana wetu.
 
Umeona eeh, I felt sorry for the girls.

Kuna watu mnachanganya mambo hapa sasa sijui ni ushabiki manesema majaji walikuwa wanampigia debe hirman kila wiki jana katoka mnasema wamechakachua matokeo wamemtoa kwa hila wakati kila siku wanampigia debe kuna watu hawapigi kura wanabaki kuwa mashabiki wa kuangalia kingine jana master j kafanya kitendo kibaya sana hivi niambie wale madada wawili misoji watakuwa wanajisikiaje yaani master j kasimama kakunja karatasi kaondoka na salama yaani inamaanisha wale madada hawkustahili kuwa pale
 
Huyu madam Rita asiye na hata mume mnampa kichwa. Huyu ni chakula ya wakubwa na kuwadi wao kama Rahma Kharoos "rais' wa kampuni la mafuta la mkuu ambaye amemgeuza nyumba ndogo. Siku ya mambo yao kuwekwa hadharani mtashangaa. Kwani Bongo kuna wafanya biashara au wasanii tu? Ipo siku mtajua uchafu wao na mtashangaa waliwezaje kuwazuga muda wote huo.

mwaga mtama hadharani acha zengwe aisee....
 
Huyu madam Rita asiye na hata mume mnampa kichwa. Huyu ni chakula ya wakubwa na kuwadi wao kama Rahma Kharoos "rais' wa kampuni la mafuta la mkuu ambaye amemgeuza nyumba ndogo. Siku ya mambo yao kuwekwa hadharani mtashangaa. Kwani Bongo kuna wafanya biashara au wasanii tu? Ipo siku mtajua uchafu wao na mtashangaa waliwezaje kuwazuga muda wote huo.
Wewe inakuhusu nini?
 
Nimepata habari kuwa mpiga gitaa ndio ameandaliwa mwaka huu kushinda maana mshindi hajawahi kutokea upande wa pili (Kama urais vile),na kumbuka wadhamini wa mwaka huu ndio kule kule,stay tuned
Hivi Jumanne pia alikua upande wa kwanza!!!!
 
Binafsi niliangalia Shindano hilo kwa Miaka Miwili ya kwanza tu halafu nikaachana nalo baada ya kutoridhishwa na uendeshwaji wake (wakati bado ninalifuatilia Shindano hilo nilikuwa pia nawapigia Kura Washiriki niliokuwa nikiona wanafanya vizuri).

Waacheni waendelee kufurahisha nafsi zao huku wakiumbuka sokoni kwa Wasanii wanaowapa ushindi: Walimnyima ushindi KALA JEREMIAH anatoboa mtaani mpaka leo kwa Tungo zilizosimama; wakaja wakafanya tena hayo hayo kwa PETER MSECHU, naamini wanaona nini anafanya huyo Jamaa hivi sasa..NI MSHINDI GANI WA BSS ANA-SOKO TOKA SHINDANO HILO LIMEANZISHWA!!!

Waandaaji wa BSS wana Washindi wao; nasi Mtaani tuna Washindi wetu ambao BSS hawakuwaona lakini SOKO limewakubali. Sasa nani zaidi kati ya Mshindi wa SHINDANO vs Mshindi wa MTAANI/SOKONI?
 
jana wamemtoa yule mtoto mlaini Menynar sina hamu na hilo likipindi tena. wengine tulikuwa tunaangalia kwa kazi maalum. lol

423609_431492886897700_260519522_n.jpg
 
Tunawezaje kuwaamini majaji wa Epic Bongo Stars search hususani kuhusu upigaji wa kura. Kwa nini kusingekuwa na screen counts tuone vividly jinsi watu walivyopiga kura ngapi kwa nani. Nimehisi hujuma ya wazi kwa kijana Norman aliyeondolewa leo. Kuna mazingira matatu ambayo ni ya wazi ambayo hatuyapendi nayo ni:

1. Mtangazaji wa kike anapowaita na kuwatambulisha waimbaji yuko biased sana mfano anatoa sifa kibao kwa Salma Yusuf eti gitaa girl, Nshama na Wababa n.k Ukweli huyu guitar girl hana sauti (vocal) yeyote ya maana kuliko Norman. Nasema anaweza kuwa mpiga chombo na mjuzi wa muziki (nota) kama somo lakini talent ya kuimba wala kuperform jukwaani ni chini ya kiwango sana kuliko Norman na wengine wote. Anapoimba anabana sauti na anatoa sauti ya mwikwaruzo!

2. Majaji wanavyombeba Salma na Nshama pia ni bayana kwa kuonesha double stds. Wakati wa kutafuta washiriki mikoani kuna watu kibao waliingia katika mashindano toka huko Mwanza, Dodoma, hata Dar walikuwa wakali sana wa matumizi ya vyombo vya muziki na kuimba, Master J akawa anawakataa akisema kuwa waimbe tena bila vyombo maana wanatafuta mwimbaji na si mpiga vyombo. Pili, majaji wote hata Madam Rita hamkuwa mnawahitaji watu waliokuwa wanakuja na nyimbo za kiutamaduni eti kwa kuwa hiyo si miziki au style mnayoitafuta. Ni aibu sana leo tunashuhudia mkiwabeba na kuwapigia saluti akina Nshama na mwenzake yule mrefu (sikumbuki jina lake) ambaye sauti yake naye iko chini na anaimba nje ya key kila wakati anapenda kuimba nyimbo za utamaduni za Afrika kusini au za akina Helen Kijo. Je, mnataka kutuambia kuwa utamaduni wa mwafrika nje ya Tanzania ni bora kuliko ule wa wa Msukuma au Mnyamwezi, Mzigua n.k ambao uliwasilishwa kwa kiwango cha juu sana na washiriki mwazoni. Pitieni kimya kimya zile video zenu za mwanzoni huko Mwanza, Tanga muone. Majaji, mnaaibisha sana na double standards zenu halafu eti wakati wa kutoa matokeo kumfukuza Norman ili kumuandalia ‘guitar girl njia na ushindi’mnajifanya kukimbia toka jukwaani kuwa mmesikitika au kuwalaumu wapiga kura! Kila mtu anawaona kuwa mnajihuzunisha mbele ya screen kama ze comedy wanavyoweza kuamua kulia wakati hakika hawana huzuni wowote!

3. Uchunguzi zaidi ni kuwa hawa vijana washiriki walipopelekwa katika moja ya Stars Hotel nchini eti kameraman wa BSS akawa anamtafuta yeye Norman kwa karibu kuonyesha vituko au ushamba wake mezani (unbecoming table manners) mfano kumuonyesha Norman akinyanyua bakuli lake la supu toka mezani au alipojikuna kichwani akiwa mezani. This is such a very poor way of looking for a way to discredit a talented participant. Kwa jina la wote wapenda haki duniani chukueni video ya siku kijana huyu ameimba wimbo wa Lionel Richie; nasema haijatokea katika BSS, hata Richie mwenyewe hakufikia hapo kama huyu kijana alivyoimba siku hiyo maana nilitokwa na machozi ya furaha kumuangalia. Nimesikitika sana.

Madam Rita kumbuka kuwa kufanya biashara za dhuruma ni dhabi na ni kosa la jinai. Juzi tu Lance Amstrong kavuliwa medali zake zote za ubingwa wa dunia za miaka ya nyuma yote katika kuendesha baiskeli kwa kasi kwa sababu ya udanganyifu. Hizo siku za kuaibishwa na kulia zaja kwa BSS hata kama ni baada ya miaka mitano maana tutapitia video zote polepole na kudemand kura zilivyopigwa maana record zipo kwenye servers na ndipo tutawavua ubingwa wote mnaowabeba na kukulazimisha wewe Rita urudishe fedha za ufadhili na zile ambazo zinapatikana tokana na waliopiga simu kuwapa faida makampuni ya simu ambayo mnapanga nao matokeo toka mwanzo. Kwa nini usiwe unahusisha majaji wengine wataalamu wa muziki toka Bagamoyo ili kuwa objective & transparent? why always rafiki zako akina master J na Salama ambaye hana sifa yoyote na muziki isipokuwa kuwashushua watu walivyovaa au kuwambia watafute kazi nyingine lugha za kihuni sana kwa vijana wanaotafuta kujiendeleza kimziki.
Huyo norman sawa alikuwa anaimba ila hakuwa mkali kihivyo, mi sio shabiki wake na huyo salma unayempondea mi ndo napenda awe mshindi..kwahiyo unapolalamika usimlaumu salma laumu majaji
 
Mi naona walikokanyaga tusker wakabandua wao ndio wnakanyaka, sijui hawana ubunifu.
 
Hii Ya kumtoa Norman Sikuipenda kabisa jamaa ni very talented anakipawa hasa
sijui ni kigezo gani walitumia labda ni kule kwenda kuimba nyimbo asiyoiweza ya Bruno mars
ila jamaa ni realy musician atakuja kuwa mwimbaji mzuri don't give up bro
huyu nshama hafai kabisa toeni haraka kwanza anaweza kuimba katika keys za juu tu
hana jipya pia yule dogo white tupilia mbali hafai
 
Dag hii kitu watu wanaichukulia serious sana,,, kaka kama mpenzi wa idols cheki X Factor etc bongo magumashi tu...

SIJAWAHI FIKIRIA KAMA KUNA WATU THEY TAKE THIS SHIT SERIOUS HADI KULETA HOJA JAMVINI YA PAGE NZIMA...
 
Back
Top Bottom