Hiyo biashara imetoka mbali sana. Hapa nilipo kuna rafiki yangu siku moja alinipa "free pass" yake anayotumia kuhudhuria katika parlour moja inaitwa "Ambassador". Utaratibu wao ni kwamba ukiingia unalipa pound 10 mlangoni halafu huko ndani unachagua unayetaka akufanyie massage kisha mnawekeana appointment ya saa ambazo utakuja. Gharama za huduma zitategemea huduma utakayochagua, maana msichana yeyote utakayechagua anayo orodha ndefu tu ya huduma wanazotoa, atakupa brochure ambayo zote hizo zimeandikwa na bei zake, lakini ngono haijaandikwa, haiko kwenye orodha. Ukiwa na free pass unaingia bure, hulipi hizo pound 10 (utalipia tu huduma utakayokubaliana na unayemchagua).
Sasa mimi nikawa curious, nikataka tu niende "niwasanifu" hao wasichana (si nina free pass bana?) halafu niondoke bila kununua huduma yoyote. Nikafika mlangoni nikabonyeza kengele, akaja mhudumu nikamwonesha pass yangu akaniruhusu kuingia. Nikaambiwa nikae kwenye kochi penye reception ambako pia kuna mashine zinauza kahawa, soda, juice na bites. Nikanunua espresso yangu, wakati nakunywa wanapita mmoja mmoja wasichana hao, wako minimally dressed kila mmoja kwa mtindo wake, wanakuja kwangu wanajitambulisha kwa majina na kutokomea. Baada ya kama 10 min, akaja yule aliyenifungulia akaniuliza umemchagua yupi? Nikamwambia kwa kweli sijachagua yeyote. Akaniambia kuna mmoja hujamwona, tulikuwa tume-reserve kwa ajili yako tulijua utakuja, hata kama hutaki huduma atakusadia tu hata kuongea na wewe, inawezekana ni upweke umekusibu ukashindwa kujua unahitaji nini, na hii huduma ya kuongea na mteja kumwondolea upweke ni ofa kwa wateja wetu, hutalipa chochote. Akaja huyo binti, na sielewi ilikuwaje hata nikajikuta nimezungumza naye zaidi ya nusu saa, ana akili kwa kweli anazungumza kila kitu kuanzia rugby hadi politics za number 10 Downing street kwa ufasaha ajabu, ana elements fulani za psychology anaongea pia, alinishangaza kwa kweli. Mwisho akanipa namba yake ya simu tukaagana. Nilishindwa kujizuia kumpigia simu.