Maskini Tanzania!

Maskini Tanzania!

Watanzania sio wajinga kama ulivyofikiria...!! Hatuwezi kumpa fisi atawale nchi..!! Mpaka upinzani utakapokua upinzani kweli na sio timu ya wasakatumbu ndo tutawachagua upinzani...:hand:

Hamuwezi kumpa fisi atawale nchi?

Unaona sasa..huu ndo ujuha wenyewe ninaouzungumzia.

Hao CCM ni zaidi ya fisi maana wao ndo waliosababisha na watakaoendelea kusababisha hali tuliyonayo.

Kama hulioni hilo ni ama unanufaika na uwepo wao madarakani au u juha kama jiwe.
 
.............ila nafurahi kuona umepokonyoka toka kwenye mikono ya walanguzi ambao walikuwa na uchu wa kukupeleka mnadani huku wakitokwa na udenda wa tamaa ya fedha ambayo wangepiga baada ya kumpata mnunuzi toka ughaibuni! MUNGU akulinde Ooh Mama Tanzania!!!!!
Umenena vema... Nchi likuwa inauzwa.. ona Tuliaminishwa kwamaa nchi ingegeuka kuwa ya maziwa na asali ndani ya siku 100 na elimu bure kwa kukopa gesi iliyo ardhini kama walivyofanya Nigeria
 
Demokrasia tunayoifuata inaweza kufanya kazi vizuri IWAPO TU watu wahusika wako "well informed" ikiwa ni pamoja na kujua haki zao.

Kwa hali ya sasa ya Tanzania, ni bado sana. Tuombe tu hao wanaong'ang'ani kuongoza bila kuwa na sifa za uongozi, utokee muujiza mwenye madaraka awe ni mzalendo halisi.
 
Watanzania sio wajinga kama ulivyofikiria...!! Hatuwezi kumpa fisi atawale nchi..!! Mpaka upinzani utakapokua upinzani kweli na sio timu ya wasakatumbu ndo tutawachagua upinzani...:hand:

Ki demokrasia Tanzania ina tofauti gani na North Korea? Inaskitisha zaidi watanzania hatujitambui. Jiulize kuna kosa gani raia akishangilia mbunge wake kashinda? Kwa nini polisi wanawachukulia opposition parties maadaui na kuwapiga risasi za moto na mabomu? Nashangaa sana kuna watu wako hapa wanashabikia vyama wakati hamjitambui. Ukirudi kwenu unalala na kunguni huna maji huna umeme huna kazi lakini bado upo HAPA KAZI TU!! wake up people tuache ujuha.
 
Tufanye Urais upinzani ulikosea, yaani hata ubunge bado tu Watanzania wanawaamini watu waliokaa majimboni miaka 10 na zaidi???

Kuna gharama ya mabadiliko, watu wakiendelea kuwa waoga tutabaki hapa hapa...

Uchaguzi wa mwaka huu nilitegemea bunge liwe na uwiano mzuri lakini inavyoelekea tunarudi kulekule kwenye wanaosema Ndiooo waseme ndiooooo....

Watanzania wanaakili sana. hawawezi kukabidhi mifugo yao kwa fisi aliyerarua mifugo hiyo eti kwa kuwa kuna kikundi cha watu kinawaaminisha kwamba fisi huyo sasa hana tena meno na kucha kwakuwa wamenufaishwa
 
Nikiwa mtoto niliwaogopa manesi na madokta kwa hofu ya kuchomwa sindano baadaye nikawaogopa polisi na wanajeshi wenye bunduki kwa hofu ya kuuawa. Leo hii nawaogopa wanasiasa wetu kama gonjwa la ukoma. Tanzania wanasiasa viongozi wanakuwa madikteta mafashist na watu wasio na huruma kwa myonge. matendo yao leo yatapelekea watoto wangu na watoto wa watoto wangu kuwa na maisha ovyo wakati Nchi ya Tanzania imejaliwa kila mali asili ya kutupatia neema. Tujitambue!
 
Watanzania wenzangu najua kila mmoja mwenye uzalendo anamaumivu makali yanaendelea moyoni mwake kwa upande wangu sijakata tamaa najua Mungu hawezi kutuacha tukaaibika kiasi hiki ni swala la muda kabla Tanzania haijalipuka kwa shangwe pande zote za nchi kwa imani yako endelea kuomba Mungu afanye jambo kwani hawa jamaa wakiendelea kutawala hali itakuwa mbaya sana. Mpira dakika 90 lakini safari hii tutashinda dakika za nyongeza. Mungu ibariki Tanzania!

Psalms 25
 
UKAWA jipangeni tena, Lowassa hakuwa mtu potential kuwa rais wa nchi hii.
 
UKAWA jipangeni tena, Lowassa hakuwa mtu potential kuwa rais wa nchi hii.

Ni kweli lkn ameipa nguvu sana upinzani, wajipange 2020 wanaweza kuchukua wakimsimamisha mgombea mwingine, ccm Kama watashinda wana changamoto sana wanatakiwa kurekebisha mambo mengi ili wananchi waanze kuiamini. Matokeo bado lakini tusubiri
 
Ni kweli lkn ameipa nguvu sana upinzani, wajipange 2020 wanaweza kuchukua wakimsimamisha mgombea mwingine, ccm Kama watashinda wana changamoto sana wanatakiwa kurekebisha mambo mengi ili wananchi waanze kuiamini. Matokeo bado lakini tusuri

inamaana wananchi hawaiamini!!!
wameipaje ridhaa?

Atakayetudharau watanzania hana kosa.
 
inamaana wananchi hawaiamini!!!
wameipaje ridhaa?

Atakayetudharau watanzania hana kosa.

Ccm Ina madudu yake na kila mtu anayajua. Mgombea waliomsimamisha ndio jembe na mm naamini endapo atashinda atainyoosha serikali na ccm pia.
 
Msitulaumu Watanzania, tatizo UKAWA bado hamjajiandaa na hamna utayari wa kupata madaraka makubwa ya kuiongoza nchi hii.
Hii iwe nafasi ya kujipanga kimkakati, itifaki, ilani na sera na zisiwe propaganda tu kuwa mnaweza.
Vilevile kwa sasa haikuwa na maana saaaana😛😛😛 kuwaondoa CCM A na kuwaweka CCM B. Kwa kifupi zaidi ni hvy

Umenena vyema mkuu hasa la kuondoa CCM A na kuisimika CCM B.
 
labda watanzania tumeshazoea shida na kuona kuwa tuko peponi.

Lack of exposure ni shidaaaa

kweli kabisa. Kama macho hayawahi kuona tofauti na kilicho zoeleka, kumbadilisha mwenye macho ni ndoto za alinacha.
 
Back
Top Bottom