BEYOND PAIN
SEHEMU YA 26
MTUNZI : PATRICK.CK
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
Mganga akamsogelea na kuanza kumpiga na usinga huku akiongea maneno ambayo Emmy hakuyafahamu.Alikuwa akimzunguka huku akipiga na usinga katika sehemu zote za mwili.Akautupa pembeni usinga na kumshika Emmy kichwani kwa mikono yake akaanza kuongea tena maneno yake ya kiganga.Akaendelea kuzishika sehemu mbali mbali za mwili Aliendelea na zoezi lile huku uume wake ukiwa umesimama wima.Akaukota tena usinga wake na kumchapa nao Emmy kichwani na ghafla Emmy akahisi mabadiliko ,akajikuta akipandwa na ashki baada ya kutomaswa na mganga.Akamkumbatia mganga kwa nguvu.Mganga alikuwa akihema kwa nguvu na hakutaka kuendelea kupoteza muda tena akaanza kufanya mapenzi na Emmy.
Baada ya kumaliza kitendo chake akachukua usinga wake na kumchapa nao Emmy kichwani na ghafla akarejewa na fahamu zake za kawaida akastuka akaona aibu na kuiokota nguo yake haraka haraka akajifunika.
" Dawa imekamilika.Mizimu imekuondolea mkosi wote na sasa uko safi.Ila kumbuka ukishaondoka hapa usiwashe simu yako na wala usiwasiliane na mtu yeyote bali nenda moja kwa moja hadi nyumbani kwa wazazi wako na hapo ndipo dawa itakapokuwa imekamilika." akasema mganga na kumuamuru Emmy amfuate.
ENDELEA???????..
Taratibu kulianza kupambazuka.Kiza kikaanza kutoweka na nuru ikaanza kuchukua nafasi.Watu wakaanza kuamka na kuanza kjiandaa kwa shughuli za siku mpya.Watu walikuwa wengi katika nyumba ya wazazi wa Emmy.Kwa muda mrefu nilikuwa nimekaa na baba mkwe yaani baba yake Emmy katika kona ya nyumba ile tukijadiliana mambo mbali mbali ya kufanya katika ule msiba.Tuliongea mambo mengi kwa kirefu na hususan suala zima la maisha ya Emmy.Kulipoanza kupambazuka tukamaliza maongezi yetu na kujumuika na waombolezaji wengine kuanza maandalizi ya msiba ule. Watu walianza kuwasili na vilio toka kwa akina mama vikaanza kusikika. Kifo cha Baraka kiliwastua watu wengi hasa kutokana na namna kilivyotokea ghafla.Wengi walijiuliza alipo Emmy wakakosa jibu. Ni mimi na Chris pekee katika hadhira ile tuliokuwa tukifahamu kilichokuwa kinaendelea lakini hatukumweleza mtu yeyote yule hadi tutakapopata uhakika.
Saa nane za mchana wakati tukiendelea na shughuli za msiba gari ya Emmy ikawasili .Minon'gono na vilio vikaanza kusikika tena.Watu wakageuza shingo zao ili kumtazama Emmy.Shughuli zilisimama kwa muda .Haraka haraka mlango wa gari ukafunguliwa na Emmy akashuka.Nilikuwa karibu na mahala aliposimamisha gari lake na niliushuhudia uso wake ukiwa na wasi wasi mwingi.Kushuka kwa Sheila kukanifanya niamini kwamba ni kweli walikuwa wamekwenda kwa mganga kama msichana yule niliyemkuta katika nyumba niliyomuachia Emmy alivyonieleza.Nilikabwa na donge kubwa kooni.Nikapandwa na hasira za ghafla.Nilitama
ni nimvae mzima mzima na kumshushia kipigo na kuanika mambo yake hadharani ili kila mtu afahamu unyama wa mwanamke huyu. Kabla sijafanya lolote ,Emmy akatembea kwa haraka kuelekea ndani lakini baada ya hatua tatu akaanguka chini.Kikaamka kizaazaa hapo msibani.
Emmy alipoteza fahamu.Haraka haraka akainuliwa na kupelekwa chini ya mti mti akalazwa na kuanza kupatiwa huduma.Sheila naye aliangua kilio kikubwa na kuanza kujigala gaza chini akina mama wakamfuata na kumsaidia kumsitiri ,wakamuingiza ndani.Nilikabwa na kitu rohoni kwa kitendo walichokifanya wanawake wale wawili Emmy na mwenzake Sheila.Nilitamani kama ingekuwa ni kwa amri yangu wasingekanyaga pale msibani.Nilimchukia Emmy kupita kiumbe yeyote yule hapa duniani.Nilijilaumu sana kwa kumfahamu na kufunga naye ndoa.Nilifanya kosa kubwa sana ambao sintalisahau katika maisha yangu yote.Emmy amegeuka na kuwama ni mwanamke mwenye roho ya kinyama .Nilishukuru kwa maamuzi ya kuachana naye kwa sababu angeweza hata kunitoa uhai kama ningeendelea kuishi naye.Tayari amejiingiza katika mambo ya kishirikina na mwisho wake utakuwa mbaya sana..
Nilikuwa nimesimama nikiwaza ,nikastuliwa na baba mkwe aliyenishika bega na kuniita pembeni.
? kama kusingekuwa na umati mkubwa hivi wa watu ,ningemtimua huyu mtoto hapa nyumbani.yaani mwanae anafariki dunia yeye hana habari ,amenisikitisha sana Emmy? akasema baba mkwe ambaye alionyesha kuwa na hasira nyingi.mawazo yake yalikuwa kama yangu.Sikutamani Emmy awepo pale msibani.laiti kama watu wagefahamu alichokifanya huyu mwanamke nina imani wangeweza hata kumkata vipande vipande.Kifo cha ghafla cha baraka kiliwastua na kuwaumuza watu wengi.
? Baba,nafahamu ni jinsi gani Emmy alivyowakasirisha watu wengi kwa kitendo chake hiki cha kujali starehe kuliko mwanae hadi amefariki dunia akiwa hana habari lakini naomba tuwe na uvumilivu ili tuweze kumaliza shughuli hii kwa amani. Baada ya kumzika Baraka kila mwenye neno la kusema atalisema? Nikamsihi baba mkwe.
? nakubaliana nawe wayne lakini mambo yote haya ambayo yameanza kumfika emmy ni laana zinazotokana na mambo yake anayoyafanya.Alikufanyia mambo mabaya sana na hata kufikia hatua ya kutudharau sisi wazazi wake .Huu ni mwanzo tu na bado yatamfika makubwa zaidi.Siku moja atakuja kukupigia magoti akiomba umsamehe.Atakuja akitembea kwa magoti akilia akiomba msamaha wako.Mimi kama baba yake mzazi ninakwambia wayne kama ukikubali kurudiana na mtoto huyu kamwe usikanyage ndani ya nyumba hii..? akasema baba mkwe akiwa na hasira kali.
?Baba mimi na Emmy tumekwisha fika mwisho na hatutaweza kuwa na mahusiano ya namna yoyote tena.Nina imani hatathubutu kurudi na kuomba msamaha eti turudiane tena..na kama unavyofahamu baba,kwa sasa tayari niko katika mahusiano mengine,nashukuru Mungu huyu mwanamke niliyenaye kwa sasa ananijali na kunithamini.? Nikasema.
? nashukuru kama umempata mtu ambaye ameweza kukusahaulisha mateso na machungu yote aliyokusababishia huyu shetani..Mtoto huyu sitamani hata kumuona tena..? akafoka baba mkwe.
Kuzidi kumuongelea mwanamke yule kulinifanya nizidi kuwa na hasira naye.
Ilinibidi nianzishe maongezi mengine ili tuache kuongelea masuala ya Emmy.
Emmy alizinduka na kupelekwa ndani.Alikuwa analia kwa nguvu sana.Akina mama walijaribu kumtuliza na kumtaka awe mvumilivu.Kulia kwake kulisababisha kuwepo na mingong?ono mingi pale msibani.Kila mmoja alionekana kuwa na sura yenye kukasirika kwa kilio kile cha emmy ambacho waliamini kilikuwa ni cha kinafiki.
Ghafla kikatokea tena kizaa zaa kingine mle ndani.Emmy alipandisha mashetani na kuanza kuongea lugha ambayo hakuna aliyeielewa.Ali
kuwa akiongea maneno mengi .Alionekana kama mtu aliyerukwa na akili.Akina mama walijaribu kumshika na kumzuia kwani tayari alianza kuvua nguo na kuzitupa.Ikazuka tafrani kubwa mle chumbani.Hakutaka mtu yeyote amsogelee.Watu wakaanza kutoka mle chumbani wakikimbia wakiogopa asije akawadhuru.Watu tuliokuwa nje tulistushwa na hali ile na wakati tukijaribu kujua nini kilichokuwa kinaendelea ndani mara Emmy akatoka mbio mle ndani na kusababisha watu waanze kukimbizana hovyo ili kumkwepa .Aliangaza angaza pale nje na mara akaanza kuja mahala tulipokuwa tumesimama.Wote tulibaki tunashangaa.
? Leo utanirudishia mwanangu?..!! Nasema leo lazima umrudishe mwanangu !!..kwa nini umemuua mwanangu? Alikuwa akiyasema maneno haya kwa sauti kubwa huku akikimbia kwa kasi kuja mahala tulipokuwa tumesimama.Tulijiandaa ili tumzuie lakini ghafla akanirukia kwa nguvu zake zote na kuniangusha chini kisha akanikaba kooni.Nilimuangalia usoni ,macho yake yalionyesha kwamba hakuwa akitania kwa kile alichokusudia kukifanya.
? leo nakuua wayne..namtaka mwanangu..! nirudishie mwanangu.!! Akasema Emmy huku akinikaba kooni.Nilipandwa na hasira za ghafla,nikakusanya nguvu zote nilizokuwa nazo na kumsukuma Emmy pembeni akaanguka .Nilipotaka kuinuka akaniwahi na kutaka kuniangusha tena chini lakini safari hii niliwahi nikamshika fulana yake aliyokuwa ameivaa nikamnasa kofi zito lililompelekea mpaka chini.Aligala gala pale chini akilia.Nikamuendea tena nikamuinua na kumpiga tena kofi lingine zito akaanguka chini.
Pamoja na makofi yale mazito bado emmy aliendelea kutaka kupambana na mimi.Alikuwa anaongea maneno katika lugha ambayo sikuifahamu.Aliokota jiwe kubwa akalirusha kwa nguvu .Almanusura jiwe lile linipate.Nilipa
ndwa na hasira zisizomithilika kwa kukoswa na jiwe lile kubwa ambalo kama lingenipata ingekuwa ni habari nyingine tena.Pengine kungekuwa na msiba wa pili. Sikuwahi kumpiga Emmy hata maramoja ,huu ulikuwa ni wakati muafaka wa kumfundisha adabu.Nilimvaa na kuanza kumshushia kipigo kikali.Ndani ya dakika kadhaa Emmy hakuwa akijitambua kwa kipigo kikali nilichompa
Wakati namshushia Emmy kipigo kile kikali,baadhi ya watu walionekana kukubaliana na kukifurahia kitendo kile na baadhi ya akina mama wakishabikia nimuadhibu zaidi.Wengi wamezisikia taarifa za mwanamke huyu na mambo yote aliyonifanyia.Namshukuru Chris kwani yeye ndiye aliyenishika kwa nguvu nisiendelee kumpa Emmy kipigo zaidi.Emmy alikuwa ametakapaa damu.Akachukuliwa na akina mama wakampeleka ndani na mimi nikachukuliwa na kupelekwa nje ya nyumba.
" Wayne tafadhali naomba ujaribu kudhibiti hasira zako.Wote tuliopo hapa tumeumizwa na kifo cha Baraka na kitendo alichokifanya mama yake na kama wote tukishindwa kuzizuia hasira zetu nina imani hapatakuwa na amani eneo hili.Tujitahidi ili tumalize suala hili kwa amani halafu masuala mengine yatafuata " Chris akanishauri.Sikumjibu kitu nilikuwa bado nina hasira sana.Nilimshukuru Chris kwani bila ya yeye ningeweza kusababisha madhara makubwa kutokana na hasira nilizokuwa nazo..
Tukiwa nyuma ya nyumba ,Emmy aliingizwa garini na kukimbizwa hospitali.Alikuwa anatokwa na damu nyingi puani kutokana na kipigo nilichompatia.Sikuona uchungu wala kustuka kwa namna yoyote ile.Wakati bado mjadala unaendelea kuhusiana na kilichotokea muda mfupi uliopita simu yangu ikaita.Nikaitoa mfukoni na kutazama mpigaji alikuwa ni Clara.Nikajitenga na wenzangu na kuipokea simu
" Hallo Clara" nikasema
" Pole sana Wayne..Hajakuumiza yule mwanamke? akauliza Clara
" hapana hajaniumiza.Niliwahi kumdhibiti"
" Pole Wayne..Naomba uwe makini sana na mwanamke huyu kwani anaonekana ni kama amechanganyikiwa .halafu jitahidi usiwe na hasira naye kwani unaweza ukasababisha masuala mengine tena Vile vile si vizuri kupigana hasa katika hadhira kama hii" akasema Clara.
" Nimekuelewa Clara ,lakini halikuwa lengo langu kumpiga.Ni yeye ndiye aliyenilazimisha nikafanya vile." nikasema
" Anaonekana ameumia sana.Wamemkimbiza hospitali.Wayne nimeanza kuogopa asije akanidhuru hata mimi mara atakaporudi.Ina
onekana amepania kufanya vurugu "
" usijali Clara.hawezi kukufanyia jambo lolote lile.Nimekwisha choka naye na iwapo atajaribu kukufanyia kitu chochote kile,ninaapa nitamtoa roho .."
Shughuli ziliendelea kama kawaida hapo msibani.maandalizi ya mazishi yalikamilika.Nd
ugu wa kutoka mikoani waliendelea kuwasili.Siku iliyofuata ilipangwa tumzike Baraka.
Jioni baba mkwe akaniita pembeni kwa maongezi.
" Wayne pole sana kwa matatizo yaliyotokea mchana.Ninakupongeza ulifanya kazi nzuri sana.Ulimfundisha adabu.Nilitaka watu wakuache kwanza ili umfundishe adabu shetani yule.Nina imani kwa kipigo ulichompa tayari amekuwa na adabu" akasema baba mkwe akiwa na chupa ndogo ya konyagi mkononi.
"Nashukuru hakuweza kusababisha madhara kwa sababu alidhamiria kunidhuru" nikasema.Baba mke akaifungua ile chupa ya konyagi akanywa kidogo.
" Kwa nyakati kama hizi huwa ninapenda kutumia kinywaji hiki ili niweze kupunguza mawazo niliyonayo" akasema baba mkwe.Sikumjibu kitu.
" Wayne nimekuita hapa ili tuweze kujadili suala moja la muhimu sana.Kesho ni siku ya mazishi lakini tumekwisha fahamu baba halisi wa baraka ni nani? akauliza baba mkwe.Nilitafakari kidogo na kusema
" Suala hili ni gumu kwetu sisi na anayeweza kutoa jibu la swali hili ni emmy peke yake.yeye ndiye anayemfahamu baba halisi wa Baraka ni nani.Awali nilidhani ni mimi ,kumbe si mimi,akasema ni Chris, lakini kumbe si Chris sasa hatujui baba wa baraka ni nani..Hii ni siri yake mwenywe." nikasema
" Dah ! Sikutegemea kama Emmy angebadilika na kuwa namna hii..Sikutegemea kabisa.Litakuwa jambo la busara kama tutamzika mtoto bila kumfahamu baba yake? akauliza baba mkwe.
" iwapo kutakuwa na ulazima ,itatubidi tufanye hivyo.Sina hakika kama Emmy yuko tayari kumuweka wazi baba wa Baraka kwa sasa.Inavyoonekana hata yeye mwenyewe hamjui ni nani" nikasema
" kama ni hivyo inawezekana ikawa ni tabia yake kutembea nje ya ndoa.Inaonekana ametembea na wanaume wengi sana kiasi cha kutofahamu hata baba wa mtoto wake ni nani.Dah ! mkosi gani huu nimeupata mimi" akasema baba mkwe huku akishika kichwa chake.
" Baba lisikuumize kichwa suala hili.Mimi nitasimama kama baba wa Baraka.Amezaliwa mikononi mwangu,nimemlea na kumtunza kama mwanangu .Hata baada ya kubainika kwamba hakuwa mwanangu wa damu bado nimeendelea kumpenda na kumuhesabu kama mwanangu.Nitasimama kama baba yake." nikasema.
" Nashukuru sana wayne kwa maamuzi hayo.Suala hili lilikuwa linaniumiza kichwa sana .sikujua ingekuwaje." akasema baba mkwe.Tuliongea mambo mengi na wakati tukiongea Clara akanipigia simu akaniomba nimpeleke hotelini ili akabadili nguo pamoja na kuoga.Tuliondoka msibani tukaelekea hotelini.
" Wayne mbona uko kimya sana leo? Unamuwaza Emmy? akauliza Clara baada ya ukimya kutawala garini.
" Hapana mpenzi wangu.Siwezi hata dakika moja kumuwaza yule shetani ." nikasema
" Pole sana.Hakuwahi kukuumiza yule mwanamke?
" Niliwahi kumdhibiti.Kama nisingewahi alikuwa na dhamira ya kunidhuru." nikasema huku nikiwa makini kwenye usukani.
" Niliogopa sana pale alipoanza kuongea maneno kama mtu aliyerukwa na akili.Alikuwa ni kama mtu aliyepandisha mashetani.Alikuwa analia na kupiga kelele akidai wamrudhishe mwanae.Alikuwa anakutaja wewe kwamba umrudishie mwanae." akasema Clara.
" Haya yote ni malipo kwa mambo yote ya kikatili anayoyafanya.Inasikitisha sana Baraka amefariki bila kumfahamu baba yake ni nani.Kesho itanibidi nisimame kama baba wa baraka wakati wa mazishi kwa sababu amezaliwa mikononi mwangu na nimemlea mimi hadi hapa alipofika." nikasema
" Hilo ni jambo la msingi sana Wayne kwa sababu hata mimi nilikuwa najiuliza itakuaje kuhusu baba yake Baraka? akasema Clara.
" Mimi ndiyo baba yake anayenitambua hadi alipofariki." nikasema.
"Wayne nimeanza kuwa na wasi wasi sana hata kukaa msibani kwa sababu ninaogopa Emmy anaweza akanifanyia kitu kibaya.Anaweza akaamua hata kuniaibisha.Ninahisi anaweza kuwa na matatizo ya akili" akasema Clara.
" Usijali Clara.Hataweza kukufanyia chochote kile.Iwapo atathubutu kukugusa atakiona cha moto.Kuwa na amani kabisa mpenzi wangu."
" wayne kuna kitu nakifikira pia.Nafahamu jinsi ulivyoumia moyoni kwa kifo cha Baraka Unaonaje kama baada ya mazishi tuondoke na twende mahala tukapumzike kwanza halafu tutarejea.Hii itakusaidia hata wewe mwenyewe kupunguza machungu ya kufiwa na Baraka." akasema Clara wakati tunarejea msibani.
" Hilo ni wazo zuri sana Clara.Kwa kweli ninahitaji kuipumzisha akili yangu baada ya mambo yaliyotokea." nikasema.Sikuhitaji maongezi mengi kwa usiku huu na Clara akalitambua hilo.
Tulirejea tena msibani kwa ajili ya kulala hapo kwa siku ya pili.
" Wayne,ulifanya vizuri sana kumpa kipigo Emmy" Chris aliniambia baada ya kuniita pembeni akidai ana maongezi na mimi.Sikumjibu kitu .
" Emmy anastahili kipigo kile.Ni mwanamke mshenzi sana huyu.Ninamchukia sana Emmy alisababisha nikafanya mambo mabaya sana ambayo yananipa machungu mengi kila nikifikiria.Emmy alisababisha nikakosana nawe ...." akasema Chris lakini kabla hajaendela mbele zaidi nikawahi kumzuia
" Chris tafadhali naomba tusiyaongelee mambo hayo kwa sasa..Tumejikuta tukiongea tena kwa sababu ya msiba wa Baraka na kama isingekuwa ni msiba huu mimi na wewe tusingeongea kamwe..Naomba tufanye mambo yanayohusiana na msiba halafu baada ya hapo tutaangalia kama kuna chochote tunachoweza kuongea mimi na wewe." nikasema kisha nikaondoka na kwenda kujiunga na kundi la watu waliokuwa wanacheza karata.Chris bado alibaki amesimama mahala nilipomuacha.Ni wazi alihitaji kuongea nami.Alihitaji kuzimaliza tofauti zetu zilizojitokeza lakini sikuwa tayari kwa sasa.Alnifanyia kitendo kibaya sana na si rahisi kukisahau kwa haraka namna hii.
Nikiwa pale katika lile kundi la watu waliokuwa wakicheza karata huku wakiendeleza utani mwingi wa makabila kama ilivyo kawaida katika misiba,mara nikavutwa shati, nikageuka na kukutana na baba mkwe.Akanivuta pembeni tukaenda kukaa katika viti na kuanza kuongea.
" Wayne , nimemuona yule baradhuli Chris.Toka usiku wa jana yuko hapa..Mmekwisha elewana? Nilitamani nimtimue kabisa asionekane hapa kwangu lakini nimeogopa kufanya hivyo ili kumlindia heshima japokuwa yeye hakuijali heshima yako wakati anaanzisha mahusiano na Emmy" akasema baba mkwe akionyesha kukerwa na kitendo cha Chris kuonekana pale msibani.
" Baba mimi na Chris haujaelewana na sina hakika kama hilo linaweza kutokea.Kilicho
pelekea awepo hapa nilimpigia simu jana ili nimuulize kama anaweza akafahamu mahala tunakoweza kumpata Emmy.Nilimfahamisha kwamba Baraka amefariki ghafla ,akastuka na akaja kuungana nasi katika kumtafuta Emmy.Hata mimi sijisikii vizuri ninapokuwa karibu na mtu ambaye aliwahi kutembea na mke wangu wa ndoa.Ninajilazimisha kufanya hivyo ili tuweze kumaliza salama shughuli hizi za msiba.Katika sehemu kama hizi tofauti zote huwa zinawekwa kando.Lakini suala la kumsamehe silifikirii kwa sasa.Alinifanyia kitendo kibaya sana" nikasema huku nikitazama mahala alikokuwa amekaa Chris akiwa na baadhi ya waombolezaji Kila ninapomtazama kuna kitu kilikuwa kinanikaa rohoni na kunifanya nizidi kuwa na hasira naye.
" Nakubalina nawe Wayne,tuziweke tofauti zetu pembeni ili tumalize suala hili kwa amani japokuwa sina amani kila nikimuona hapa kwangu nadhani hata yeye amelitambua hilo na ndiyo maana anajificha sana ili asionane na mimi. Tuachane na hayo..Huyu laana Emmy alikuwa wapi muda wote tuliokuwa tunamtafuta ? Kwa kweli Emmy amenitia aibu kubwa.Kila mtu hapa mtaani anamuongelea yeye." akasema baba mkwe.Nilitamani nimweleze ukweli lakini nikaona tutaamsha mambo mengine nikaamua kuachana na suala hilo .
" Baba,Emmy unamfahamu vizuri ni mwanamke anayependa sana starehe.Nina hakika alikuwa katika starehe zake na ndiyo maana hakuwa na taarifa juu ya kilichotokea kuhusu mwanae.Inasikitisha sana" nikasema
" Wayne usinione nimekaa kimya,lakini moyoni nimeumia sana kwa matendo ya huyu mtoto.Ninajuta hata kwa nini alizaliwa na mimi." akalalamika baba mkwe.
" Baba ,unapaswa kumshukuru Mungu kwa kila jambo.yeye ndiye anayetupa watoto kwa hiyo hata Emmy kuzaliwa na wewe ilikuwa ni kwa mapenzi yake.Kitu kikubwa tunachotakiwa kukifanya ni kumuombea sana ili aweze kubadilika.Tunatakiwa kufanya maombi ya kufunga na kuomba ili kumuombea .." nikasema na kumfanya baba mkwe acheke.
" Kamwe sintathubutu kushinda na njaa kwa sababu ya laana kama Emmy. Kama ameshindwa kutusikiliza sisi wazazi wake ulimwengu ndio akaomfunza adabu.Siku zote asiyefunzwa na wazazi atafunzwa na ulimwengu." akasema baba mkwe na kunifanya na mimi kucheka.Kikapita kimya kidogo baba mkwe akauliza.
? Wayne yule msichana uliyekuwa naye ndiye mwanangu mpya uliyempata?
" Ndiyo baba..Anaitwa Clara.Anajishughulisha na ubunifu wa mitindo na kwa sasa makazi yake ni nchini Afrika ya kusini.Nimekutana naye siku kadhaa zilizopita akiwa katika harakati zake za kutoa semina kwa wanamitindo.Tumetokea kuwa marafiki na kwa muda huu mfupi tuliokuwa pamoja amenifanya niyasahau yale machungu yote niliyofanyiwa na Emmy. Utanisamehe baba kwa kuyasema haya mbele yako" nikasema.Baba mkwe akatabasamu na kusema
" Wayne huna haja ya kuogopa.Wewe ni kijana wangu na ninakupenda sana na siku zote ninakutakia mema.Nimeyashuhudia kwa macho yangu mambo aliyokufanyia mwanangu Emmy. Sikuhadithiwa na mtu yeyote.Kwa kuwa siku zote ninapenda uishi katika maisha mazuri yenye amani na furaha,ninakuunga mkono kabisa kama huyo mama uliyempata sasa hivi unaona anaweza kukufaa na siyo huyu shetani Emmy.Mimi nakuombea tu uwe na maisha mazuri yenye furaha ila nakuomba usije ukathubutu kurudiana tena na Emmy.Atakufanyi
a kitu kibaya sana.Umeona kitendo alichokifanya mchana wa leo.Kama usingekuwa hodari ukakwepa lile jiwe alilolirusha sasa hivi tungekuwa tunaongea mambo mengine tena.Kwa hiyo jitahidi sana kumuepuka ,kaa naye mbali kabisa.Muache atange na dunia na itakapomfunza atarudi kuomba msamaha na kugundua kwamba amekwisha chelewa kwani mlango umekwisha fungwa." akasema baba mkwe.Ninachompe
ndea baba mkwe siku zote amekuwa upande wangu na amekuwa akishirikiana na mimi katika kila jambo.
*************
Wakiwa katika sofa lililokuwapo mapokezi, akina mama waliompeleka Emmy kutibiwa katika zahanati ya Samaria inayomilikiwa na masista wa kanisa katoliki ,walistuliwa na muuguzi ambaye alitumwa na Emmy amuite mtu anayeitwa Sheila ana maongezi naye.Japokuwa akina mama wale walitaka sana kuingia na kumuona Emmy anaendeleaje lakini muuguzi yule alikataa kata kata kwa madai kwamba mgonjwa hakuhitaji kuonana na mtu yeyote yule kwa wakati ule zaidi ya Sheila pekee. Akiwa ameongozana na muuguzi,Sheila akaingia katika chumba alichokuwa amepumzishwa Emmy aliyekuwa amefungwa plasta kadhaa usoni kutokana na majeraha aliyoyapata kwa kipigo.
" Emmy pole sana..Unajisikiaje sasa ? akasema Sheila akikaa kitandani
" Naendelea vizuri ..Ibilisi yule Wayne alitaka kuniua,lakini nitapambana naye..Atanitambua mimi ni nani" akasema Emmy kwa sauti ya chini. Muuguzi yule akatoka nje na kuwaacha Emmy na Sheila pekee mle chumbani.Emmy ambaye alikuwa ametundikiwa chupa ya maji akamuomba Sheila amsogelee karibu zaidi.Alipomtazama katika macho yake alikuwa anatoa machozi.
" Emmy nyamaza kulia mpenzi.Jipe moyo haya ni mambo ya kawaida na yatakwisha." akasema Sheila akijaribu kumtia moyo Emmy.
" Sheila nimemuua mwanangu" akasema emmy kwa sauti ya chini.
" Unasemaje Emmy? Mbona sikuelewi? akauliza Sheila.Emmy akakohoa kidogo akarekebisha koo lake na kusema
" Sheila nimemuua mwanangu Baraka." akasema tena Emmy na kumfanya Sheila astuke,kumuangalia kwa macho ya mshangao.
" Sikuelewi unasema nini Emmy?" akauliza tena Sheila.
" Naomba unisaidie kuniinua niweze kukaa" akaomba Emmy na Sheila akamsaidia kumuinua,akakaa kitandani.
" Sheila tukiwa pale kwa mganga,aliniambia kwamba ili kunifanyia kazi yangu mizimu inahitaji sadaka.Akaniuliza kama nipo tayari kuitoa sadaka ile kwa mizimu ili inifanyie kazi yangu nikakubali na akanipa kisu nikichome katika beseni la maji .Baada ya kukichoma kisu kile katika lile beseni la maji nilisikia sauti kama ya mtu ninayemfahamu akilia na baada ya muda mfupi sauti ile ikapotea kabisa.Kumbe alikuwa ni mwanangu Baraka.Nilipokichoma kile kisu katika beseni nilikuwa namuua mwanangu bila kujua.Ouh Sheila nitafanya nini mimi? Emmy akashindwa kujizuia akaanza kulia.
" Nyamaza usilie Emmy.Usiongee kwa nguvu watu watakusikia na yatakuwa mambo mengine tena.Sasa ikawaje shoga yangu Emmy ukakubali kutoa sadaka bila kuuliza ni sadaka gani unayotakiwa kuitoa?
"Hata sielewi ilikuwaje Sheila.Nadhani nilikuwa nimepumbazwa na dawa za yule mganga.Mshenzi sana yule mganga ameniulia mwanangu na akadiriki hata kufanya mapenzi na mimi tena bila hata kutumia kinga.Ouh Mungu wangu kwa nini nilikubali kirahisi rahisi namna ile kila alichokuwa akiniambia? Halafu alifahamu kabisa kwamba tayari mwanangu amekwisha fariki ndiyo maana akaniambia kwamba nitakaporudi nisipite sehemu yoyote ile na breki ya kwanza niifunge nyumbani kwetu.Alinihakikishia kwamba Wayne lazima atarudi kwangu lakini kwa hali niliyoiona leo sina hakika kama hilo litawezekana." akasema Emmy kwa uchungu huku akilia.Sheila akamfuta machozi.
" Emmy unasema ulifanya mapenzi na yule mganga? akauliza Sheila.
" Ndiyo ! Kwani vipi?
" Mshenzi sana yule babu..Hata mimi alinilewesha dawa zake halafu akaniingilia. Kumbe alitufanyia mchezo huu wote.." akafoka Sheila na kumfanya Emmy azidi kudondosha machozi.
" Basi usilie shoga yangu.Yameshatokea na hatuna tena namna nyingine ya kufanya." akasema kwa unyonge Sheila.
" Sheila naomba ufanye kila utakavyoweza ili uweze kunitoa hapa hospitali na unipeleke kwa yule mganga usiku huu anirudishie mwanangu.Nataka amrudishe mwanangu Baraka" akasema Emmy.
" Emmy hilo ni suala lisilowezekana hata kidogo.Sahau suala la kumrudisha Baraka.Tayari ameshafariki na hawezi kurudi tena "
" Baraka hajafa Sheila.Nakuomba Sheila nipeleke kwa mganga usiku huu kabla mwanangu hajazikwa kesho.Najua anao uwezo wa kumrudisha.Na kama akishindwa kumrudisha mwanangu nitamuua" akasema Emmy.Aliongea kama mtu aliyechanganyik
iwa.Sheila akajitahidi kumtuliza lakini bado Emmy akaendelea kupiga kelele akimuomba Sheila amtoe pale hospitalina kumpeleka kwa mganga.Sheila alipoona mambo yamekuwa magumu akakimbia kwenda kuwaita wauguzi ambao walikuja haraka na kumdhibiti Emmy kisha wakamchoma sindano ya usingizi na baada ya muda akalala usngizi.
" Masikini Emmy amemuua mwanae kwa ujinga wake mwenyewe.Inaniuma sana kwa kitendo hiki alichokifanya.Anahangaika kumtafuta mchawi wakati mchawi ni yeye mwenyewe.Yeye ndiye aliyeiroga ndoa yake.Ameshindwa kumlea mume wake na badla yake kumfanyia vitimbi kila kukicha halafu leo hii anataka kumtafuta mchawi anayeiroga ndoa yake.Amenisabab
ishia hata mimi matatizo.Amenipeleka kwa yule babu mshenzi amenipumbaza kwa dawa zake na kufanya mapenzi na mimi.Sijui nitaoga na sabuni gani ili niweze kuiondoa shombo ya yule mganga mwilini mwangu.Emmy ameniingiza katika matatizo makubwa sana.Sikutegemea kabisa kama mimi Sheila ningekuja kulala na kibabu kama yule mchawi mkubwa. Najuta kuambatana na Emmy.Sitaki urafiki naye tena.Baada ya msiba huu wa mwanae kumalizika sitaki tena urafiki wala ukaribu naye.Ni msichana mbaya na anaweza akakupeleka pabaya.Itakuaje kama yule babu akawa ameniambukiza virusi vya ukimwi? Mungu nisaidie hilo lisinitokee." akawaza Sheila akiwa amesimama chini ya mti huku machozi yakimchuruzika.
TUKUTANE SEHEMU IJAYO??????.