Masimulizi: Beyond Pain

Masimulizi: Beyond Pain

BEYOND PAIN
SEHEMU YA 26
MTUNZI : PATRICK.CK
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
Mganga akamsogelea na kuanza kumpiga na usinga huku akiongea maneno ambayo Emmy hakuyafahamu.Alikuwa akimzunguka huku akipiga na usinga katika sehemu zote za mwili.Akautupa pembeni usinga na kumshika Emmy kichwani kwa mikono yake akaanza kuongea tena maneno yake ya kiganga.Akaendelea kuzishika sehemu mbali mbali za mwili Aliendelea na zoezi lile huku uume wake ukiwa umesimama wima.Akaukota tena usinga wake na kumchapa nao Emmy kichwani na ghafla Emmy akahisi mabadiliko ,akajikuta akipandwa na ashki baada ya kutomaswa na mganga.Akamkumbatia mganga kwa nguvu.Mganga alikuwa akihema kwa nguvu na hakutaka kuendelea kupoteza muda tena akaanza kufanya mapenzi na Emmy.
Baada ya kumaliza kitendo chake akachukua usinga wake na kumchapa nao Emmy kichwani na ghafla akarejewa na fahamu zake za kawaida akastuka akaona aibu na kuiokota nguo yake haraka haraka akajifunika.
" Dawa imekamilika.Mizimu imekuondolea mkosi wote na sasa uko safi.Ila kumbuka ukishaondoka hapa usiwashe simu yako na wala usiwasiliane na mtu yeyote bali nenda moja kwa moja hadi nyumbani kwa wazazi wako na hapo ndipo dawa itakapokuwa imekamilika." akasema mganga na kumuamuru Emmy amfuate.
ENDELEA???????..
Taratibu kulianza kupambazuka.Kiza kikaanza kutoweka na nuru ikaanza kuchukua nafasi.Watu wakaanza kuamka na kuanza kjiandaa kwa shughuli za siku mpya.Watu walikuwa wengi katika nyumba ya wazazi wa Emmy.Kwa muda mrefu nilikuwa nimekaa na baba mkwe yaani baba yake Emmy katika kona ya nyumba ile tukijadiliana mambo mbali mbali ya kufanya katika ule msiba.Tuliongea mambo mengi kwa kirefu na hususan suala zima la maisha ya Emmy.Kulipoanza kupambazuka tukamaliza maongezi yetu na kujumuika na waombolezaji wengine kuanza maandalizi ya msiba ule. Watu walianza kuwasili na vilio toka kwa akina mama vikaanza kusikika. Kifo cha Baraka kiliwastua watu wengi hasa kutokana na namna kilivyotokea ghafla.Wengi walijiuliza alipo Emmy wakakosa jibu. Ni mimi na Chris pekee katika hadhira ile tuliokuwa tukifahamu kilichokuwa kinaendelea lakini hatukumweleza mtu yeyote yule hadi tutakapopata uhakika.
Saa nane za mchana wakati tukiendelea na shughuli za msiba gari ya Emmy ikawasili .Minon'gono na vilio vikaanza kusikika tena.Watu wakageuza shingo zao ili kumtazama Emmy.Shughuli zilisimama kwa muda .Haraka haraka mlango wa gari ukafunguliwa na Emmy akashuka.Nilikuwa karibu na mahala aliposimamisha gari lake na niliushuhudia uso wake ukiwa na wasi wasi mwingi.Kushuka kwa Sheila kukanifanya niamini kwamba ni kweli walikuwa wamekwenda kwa mganga kama msichana yule niliyemkuta katika nyumba niliyomuachia Emmy alivyonieleza.Nilikabwa na donge kubwa kooni.Nikapandwa na hasira za ghafla.Nilitama
ni nimvae mzima mzima na kumshushia kipigo na kuanika mambo yake hadharani ili kila mtu afahamu unyama wa mwanamke huyu. Kabla sijafanya lolote ,Emmy akatembea kwa haraka kuelekea ndani lakini baada ya hatua tatu akaanguka chini.Kikaamka kizaazaa hapo msibani.
Emmy alipoteza fahamu.Haraka haraka akainuliwa na kupelekwa chini ya mti mti akalazwa na kuanza kupatiwa huduma.Sheila naye aliangua kilio kikubwa na kuanza kujigala gaza chini akina mama wakamfuata na kumsaidia kumsitiri ,wakamuingiza ndani.Nilikabwa na kitu rohoni kwa kitendo walichokifanya wanawake wale wawili Emmy na mwenzake Sheila.Nilitamani kama ingekuwa ni kwa amri yangu wasingekanyaga pale msibani.Nilimchukia Emmy kupita kiumbe yeyote yule hapa duniani.Nilijilaumu sana kwa kumfahamu na kufunga naye ndoa.Nilifanya kosa kubwa sana ambao sintalisahau katika maisha yangu yote.Emmy amegeuka na kuwama ni mwanamke mwenye roho ya kinyama .Nilishukuru kwa maamuzi ya kuachana naye kwa sababu angeweza hata kunitoa uhai kama ningeendelea kuishi naye.Tayari amejiingiza katika mambo ya kishirikina na mwisho wake utakuwa mbaya sana..
Nilikuwa nimesimama nikiwaza ,nikastuliwa na baba mkwe aliyenishika bega na kuniita pembeni.
? kama kusingekuwa na umati mkubwa hivi wa watu ,ningemtimua huyu mtoto hapa nyumbani.yaani mwanae anafariki dunia yeye hana habari ,amenisikitisha sana Emmy? akasema baba mkwe ambaye alionyesha kuwa na hasira nyingi.mawazo yake yalikuwa kama yangu.Sikutamani Emmy awepo pale msibani.laiti kama watu wagefahamu alichokifanya huyu mwanamke nina imani wangeweza hata kumkata vipande vipande.Kifo cha ghafla cha baraka kiliwastua na kuwaumuza watu wengi.
? Baba,nafahamu ni jinsi gani Emmy alivyowakasirisha watu wengi kwa kitendo chake hiki cha kujali starehe kuliko mwanae hadi amefariki dunia akiwa hana habari lakini naomba tuwe na uvumilivu ili tuweze kumaliza shughuli hii kwa amani. Baada ya kumzika Baraka kila mwenye neno la kusema atalisema? Nikamsihi baba mkwe.
? nakubaliana nawe wayne lakini mambo yote haya ambayo yameanza kumfika emmy ni laana zinazotokana na mambo yake anayoyafanya.Alikufanyia mambo mabaya sana na hata kufikia hatua ya kutudharau sisi wazazi wake .Huu ni mwanzo tu na bado yatamfika makubwa zaidi.Siku moja atakuja kukupigia magoti akiomba umsamehe.Atakuja akitembea kwa magoti akilia akiomba msamaha wako.Mimi kama baba yake mzazi ninakwambia wayne kama ukikubali kurudiana na mtoto huyu kamwe usikanyage ndani ya nyumba hii..? akasema baba mkwe akiwa na hasira kali.
?Baba mimi na Emmy tumekwisha fika mwisho na hatutaweza kuwa na mahusiano ya namna yoyote tena.Nina imani hatathubutu kurudi na kuomba msamaha eti turudiane tena..na kama unavyofahamu baba,kwa sasa tayari niko katika mahusiano mengine,nashukuru Mungu huyu mwanamke niliyenaye kwa sasa ananijali na kunithamini.? Nikasema.
? nashukuru kama umempata mtu ambaye ameweza kukusahaulisha mateso na machungu yote aliyokusababishia huyu shetani..Mtoto huyu sitamani hata kumuona tena..? akafoka baba mkwe.
Kuzidi kumuongelea mwanamke yule kulinifanya nizidi kuwa na hasira naye.
Ilinibidi nianzishe maongezi mengine ili tuache kuongelea masuala ya Emmy.
Emmy alizinduka na kupelekwa ndani.Alikuwa analia kwa nguvu sana.Akina mama walijaribu kumtuliza na kumtaka awe mvumilivu.Kulia kwake kulisababisha kuwepo na mingong?ono mingi pale msibani.Kila mmoja alionekana kuwa na sura yenye kukasirika kwa kilio kile cha emmy ambacho waliamini kilikuwa ni cha kinafiki.
Ghafla kikatokea tena kizaa zaa kingine mle ndani.Emmy alipandisha mashetani na kuanza kuongea lugha ambayo hakuna aliyeielewa.Ali
kuwa akiongea maneno mengi .Alionekana kama mtu aliyerukwa na akili.Akina mama walijaribu kumshika na kumzuia kwani tayari alianza kuvua nguo na kuzitupa.Ikazuka tafrani kubwa mle chumbani.Hakutaka mtu yeyote amsogelee.Watu wakaanza kutoka mle chumbani wakikimbia wakiogopa asije akawadhuru.Watu tuliokuwa nje tulistushwa na hali ile na wakati tukijaribu kujua nini kilichokuwa kinaendelea ndani mara Emmy akatoka mbio mle ndani na kusababisha watu waanze kukimbizana hovyo ili kumkwepa .Aliangaza angaza pale nje na mara akaanza kuja mahala tulipokuwa tumesimama.Wote tulibaki tunashangaa.
? Leo utanirudishia mwanangu?..!! Nasema leo lazima umrudishe mwanangu !!..kwa nini umemuua mwanangu? Alikuwa akiyasema maneno haya kwa sauti kubwa huku akikimbia kwa kasi kuja mahala tulipokuwa tumesimama.Tulijiandaa ili tumzuie lakini ghafla akanirukia kwa nguvu zake zote na kuniangusha chini kisha akanikaba kooni.Nilimuangalia usoni ,macho yake yalionyesha kwamba hakuwa akitania kwa kile alichokusudia kukifanya.
? leo nakuua wayne..namtaka mwanangu..! nirudishie mwanangu.!! Akasema Emmy huku akinikaba kooni.Nilipandwa na hasira za ghafla,nikakusanya nguvu zote nilizokuwa nazo na kumsukuma Emmy pembeni akaanguka .Nilipotaka kuinuka akaniwahi na kutaka kuniangusha tena chini lakini safari hii niliwahi nikamshika fulana yake aliyokuwa ameivaa nikamnasa kofi zito lililompelekea mpaka chini.Aligala gala pale chini akilia.Nikamuendea tena nikamuinua na kumpiga tena kofi lingine zito akaanguka chini.
Pamoja na makofi yale mazito bado emmy aliendelea kutaka kupambana na mimi.Alikuwa anaongea maneno katika lugha ambayo sikuifahamu.Aliokota jiwe kubwa akalirusha kwa nguvu .Almanusura jiwe lile linipate.Nilipa
ndwa na hasira zisizomithilika kwa kukoswa na jiwe lile kubwa ambalo kama lingenipata ingekuwa ni habari nyingine tena.Pengine kungekuwa na msiba wa pili. Sikuwahi kumpiga Emmy hata maramoja ,huu ulikuwa ni wakati muafaka wa kumfundisha adabu.Nilimvaa na kuanza kumshushia kipigo kikali.Ndani ya dakika kadhaa Emmy hakuwa akijitambua kwa kipigo kikali nilichompa
Wakati namshushia Emmy kipigo kile kikali,baadhi ya watu walionekana kukubaliana na kukifurahia kitendo kile na baadhi ya akina mama wakishabikia nimuadhibu zaidi.Wengi wamezisikia taarifa za mwanamke huyu na mambo yote aliyonifanyia.Namshukuru Chris kwani yeye ndiye aliyenishika kwa nguvu nisiendelee kumpa Emmy kipigo zaidi.Emmy alikuwa ametakapaa damu.Akachukuliwa na akina mama wakampeleka ndani na mimi nikachukuliwa na kupelekwa nje ya nyumba.
" Wayne tafadhali naomba ujaribu kudhibiti hasira zako.Wote tuliopo hapa tumeumizwa na kifo cha Baraka na kitendo alichokifanya mama yake na kama wote tukishindwa kuzizuia hasira zetu nina imani hapatakuwa na amani eneo hili.Tujitahidi ili tumalize suala hili kwa amani halafu masuala mengine yatafuata " Chris akanishauri.Sikumjibu kitu nilikuwa bado nina hasira sana.Nilimshukuru Chris kwani bila ya yeye ningeweza kusababisha madhara makubwa kutokana na hasira nilizokuwa nazo..
Tukiwa nyuma ya nyumba ,Emmy aliingizwa garini na kukimbizwa hospitali.Alikuwa anatokwa na damu nyingi puani kutokana na kipigo nilichompatia.Sikuona uchungu wala kustuka kwa namna yoyote ile.Wakati bado mjadala unaendelea kuhusiana na kilichotokea muda mfupi uliopita simu yangu ikaita.Nikaitoa mfukoni na kutazama mpigaji alikuwa ni Clara.Nikajitenga na wenzangu na kuipokea simu
" Hallo Clara" nikasema
" Pole sana Wayne..Hajakuumiza yule mwanamke? akauliza Clara
" hapana hajaniumiza.Niliwahi kumdhibiti"
" Pole Wayne..Naomba uwe makini sana na mwanamke huyu kwani anaonekana ni kama amechanganyikiwa .halafu jitahidi usiwe na hasira naye kwani unaweza ukasababisha masuala mengine tena Vile vile si vizuri kupigana hasa katika hadhira kama hii" akasema Clara.
" Nimekuelewa Clara ,lakini halikuwa lengo langu kumpiga.Ni yeye ndiye aliyenilazimisha nikafanya vile." nikasema
" Anaonekana ameumia sana.Wamemkimbiza hospitali.Wayne nimeanza kuogopa asije akanidhuru hata mimi mara atakaporudi.Ina
onekana amepania kufanya vurugu "
" usijali Clara.hawezi kukufanyia jambo lolote lile.Nimekwisha choka naye na iwapo atajaribu kukufanyia kitu chochote kile,ninaapa nitamtoa roho .."
Shughuli ziliendelea kama kawaida hapo msibani.maandalizi ya mazishi yalikamilika.Nd
ugu wa kutoka mikoani waliendelea kuwasili.Siku iliyofuata ilipangwa tumzike Baraka.
Jioni baba mkwe akaniita pembeni kwa maongezi.
" Wayne pole sana kwa matatizo yaliyotokea mchana.Ninakupongeza ulifanya kazi nzuri sana.Ulimfundisha adabu.Nilitaka watu wakuache kwanza ili umfundishe adabu shetani yule.Nina imani kwa kipigo ulichompa tayari amekuwa na adabu" akasema baba mkwe akiwa na chupa ndogo ya konyagi mkononi.
"Nashukuru hakuweza kusababisha madhara kwa sababu alidhamiria kunidhuru" nikasema.Baba mke akaifungua ile chupa ya konyagi akanywa kidogo.
" Kwa nyakati kama hizi huwa ninapenda kutumia kinywaji hiki ili niweze kupunguza mawazo niliyonayo" akasema baba mkwe.Sikumjibu kitu.
" Wayne nimekuita hapa ili tuweze kujadili suala moja la muhimu sana.Kesho ni siku ya mazishi lakini tumekwisha fahamu baba halisi wa baraka ni nani? akauliza baba mkwe.Nilitafakari kidogo na kusema
" Suala hili ni gumu kwetu sisi na anayeweza kutoa jibu la swali hili ni emmy peke yake.yeye ndiye anayemfahamu baba halisi wa Baraka ni nani.Awali nilidhani ni mimi ,kumbe si mimi,akasema ni Chris, lakini kumbe si Chris sasa hatujui baba wa baraka ni nani..Hii ni siri yake mwenywe." nikasema
" Dah ! Sikutegemea kama Emmy angebadilika na kuwa namna hii..Sikutegemea kabisa.Litakuwa jambo la busara kama tutamzika mtoto bila kumfahamu baba yake? akauliza baba mkwe.
" iwapo kutakuwa na ulazima ,itatubidi tufanye hivyo.Sina hakika kama Emmy yuko tayari kumuweka wazi baba wa Baraka kwa sasa.Inavyoonekana hata yeye mwenyewe hamjui ni nani" nikasema
" kama ni hivyo inawezekana ikawa ni tabia yake kutembea nje ya ndoa.Inaonekana ametembea na wanaume wengi sana kiasi cha kutofahamu hata baba wa mtoto wake ni nani.Dah ! mkosi gani huu nimeupata mimi" akasema baba mkwe huku akishika kichwa chake.
" Baba lisikuumize kichwa suala hili.Mimi nitasimama kama baba wa Baraka.Amezaliwa mikononi mwangu,nimemlea na kumtunza kama mwanangu .Hata baada ya kubainika kwamba hakuwa mwanangu wa damu bado nimeendelea kumpenda na kumuhesabu kama mwanangu.Nitasimama kama baba yake." nikasema.
" Nashukuru sana wayne kwa maamuzi hayo.Suala hili lilikuwa linaniumiza kichwa sana .sikujua ingekuwaje." akasema baba mkwe.Tuliongea mambo mengi na wakati tukiongea Clara akanipigia simu akaniomba nimpeleke hotelini ili akabadili nguo pamoja na kuoga.Tuliondoka msibani tukaelekea hotelini.
" Wayne mbona uko kimya sana leo? Unamuwaza Emmy? akauliza Clara baada ya ukimya kutawala garini.
" Hapana mpenzi wangu.Siwezi hata dakika moja kumuwaza yule shetani ." nikasema
" Pole sana.Hakuwahi kukuumiza yule mwanamke?
" Niliwahi kumdhibiti.Kama nisingewahi alikuwa na dhamira ya kunidhuru." nikasema huku nikiwa makini kwenye usukani.
" Niliogopa sana pale alipoanza kuongea maneno kama mtu aliyerukwa na akili.Alikuwa ni kama mtu aliyepandisha mashetani.Alikuwa analia na kupiga kelele akidai wamrudhishe mwanae.Alikuwa anakutaja wewe kwamba umrudishie mwanae." akasema Clara.
" Haya yote ni malipo kwa mambo yote ya kikatili anayoyafanya.Inasikitisha sana Baraka amefariki bila kumfahamu baba yake ni nani.Kesho itanibidi nisimame kama baba wa baraka wakati wa mazishi kwa sababu amezaliwa mikononi mwangu na nimemlea mimi hadi hapa alipofika." nikasema
" Hilo ni jambo la msingi sana Wayne kwa sababu hata mimi nilikuwa najiuliza itakuaje kuhusu baba yake Baraka? akasema Clara.
" Mimi ndiyo baba yake anayenitambua hadi alipofariki." nikasema.
"Wayne nimeanza kuwa na wasi wasi sana hata kukaa msibani kwa sababu ninaogopa Emmy anaweza akanifanyia kitu kibaya.Anaweza akaamua hata kuniaibisha.Ninahisi anaweza kuwa na matatizo ya akili" akasema Clara.
" Usijali Clara.Hataweza kukufanyia chochote kile.Iwapo atathubutu kukugusa atakiona cha moto.Kuwa na amani kabisa mpenzi wangu."
" wayne kuna kitu nakifikira pia.Nafahamu jinsi ulivyoumia moyoni kwa kifo cha Baraka Unaonaje kama baada ya mazishi tuondoke na twende mahala tukapumzike kwanza halafu tutarejea.Hii itakusaidia hata wewe mwenyewe kupunguza machungu ya kufiwa na Baraka." akasema Clara wakati tunarejea msibani.
" Hilo ni wazo zuri sana Clara.Kwa kweli ninahitaji kuipumzisha akili yangu baada ya mambo yaliyotokea." nikasema.Sikuhitaji maongezi mengi kwa usiku huu na Clara akalitambua hilo.
Tulirejea tena msibani kwa ajili ya kulala hapo kwa siku ya pili.
" Wayne,ulifanya vizuri sana kumpa kipigo Emmy" Chris aliniambia baada ya kuniita pembeni akidai ana maongezi na mimi.Sikumjibu kitu .
" Emmy anastahili kipigo kile.Ni mwanamke mshenzi sana huyu.Ninamchukia sana Emmy alisababisha nikafanya mambo mabaya sana ambayo yananipa machungu mengi kila nikifikiria.Emmy alisababisha nikakosana nawe ...." akasema Chris lakini kabla hajaendela mbele zaidi nikawahi kumzuia
" Chris tafadhali naomba tusiyaongelee mambo hayo kwa sasa..Tumejikuta tukiongea tena kwa sababu ya msiba wa Baraka na kama isingekuwa ni msiba huu mimi na wewe tusingeongea kamwe..Naomba tufanye mambo yanayohusiana na msiba halafu baada ya hapo tutaangalia kama kuna chochote tunachoweza kuongea mimi na wewe." nikasema kisha nikaondoka na kwenda kujiunga na kundi la watu waliokuwa wanacheza karata.Chris bado alibaki amesimama mahala nilipomuacha.Ni wazi alihitaji kuongea nami.Alihitaji kuzimaliza tofauti zetu zilizojitokeza lakini sikuwa tayari kwa sasa.Alnifanyia kitendo kibaya sana na si rahisi kukisahau kwa haraka namna hii.
Nikiwa pale katika lile kundi la watu waliokuwa wakicheza karata huku wakiendeleza utani mwingi wa makabila kama ilivyo kawaida katika misiba,mara nikavutwa shati, nikageuka na kukutana na baba mkwe.Akanivuta pembeni tukaenda kukaa katika viti na kuanza kuongea.
" Wayne , nimemuona yule baradhuli Chris.Toka usiku wa jana yuko hapa..Mmekwisha elewana? Nilitamani nimtimue kabisa asionekane hapa kwangu lakini nimeogopa kufanya hivyo ili kumlindia heshima japokuwa yeye hakuijali heshima yako wakati anaanzisha mahusiano na Emmy" akasema baba mkwe akionyesha kukerwa na kitendo cha Chris kuonekana pale msibani.
" Baba mimi na Chris haujaelewana na sina hakika kama hilo linaweza kutokea.Kilicho
pelekea awepo hapa nilimpigia simu jana ili nimuulize kama anaweza akafahamu mahala tunakoweza kumpata Emmy.Nilimfahamisha kwamba Baraka amefariki ghafla ,akastuka na akaja kuungana nasi katika kumtafuta Emmy.Hata mimi sijisikii vizuri ninapokuwa karibu na mtu ambaye aliwahi kutembea na mke wangu wa ndoa.Ninajilazimisha kufanya hivyo ili tuweze kumaliza salama shughuli hizi za msiba.Katika sehemu kama hizi tofauti zote huwa zinawekwa kando.Lakini suala la kumsamehe silifikirii kwa sasa.Alinifanyia kitendo kibaya sana" nikasema huku nikitazama mahala alikokuwa amekaa Chris akiwa na baadhi ya waombolezaji Kila ninapomtazama kuna kitu kilikuwa kinanikaa rohoni na kunifanya nizidi kuwa na hasira naye.
" Nakubalina nawe Wayne,tuziweke tofauti zetu pembeni ili tumalize suala hili kwa amani japokuwa sina amani kila nikimuona hapa kwangu nadhani hata yeye amelitambua hilo na ndiyo maana anajificha sana ili asionane na mimi. Tuachane na hayo..Huyu laana Emmy alikuwa wapi muda wote tuliokuwa tunamtafuta ? Kwa kweli Emmy amenitia aibu kubwa.Kila mtu hapa mtaani anamuongelea yeye." akasema baba mkwe.Nilitamani nimweleze ukweli lakini nikaona tutaamsha mambo mengine nikaamua kuachana na suala hilo .
" Baba,Emmy unamfahamu vizuri ni mwanamke anayependa sana starehe.Nina hakika alikuwa katika starehe zake na ndiyo maana hakuwa na taarifa juu ya kilichotokea kuhusu mwanae.Inasikitisha sana" nikasema
" Wayne usinione nimekaa kimya,lakini moyoni nimeumia sana kwa matendo ya huyu mtoto.Ninajuta hata kwa nini alizaliwa na mimi." akalalamika baba mkwe.
" Baba ,unapaswa kumshukuru Mungu kwa kila jambo.yeye ndiye anayetupa watoto kwa hiyo hata Emmy kuzaliwa na wewe ilikuwa ni kwa mapenzi yake.Kitu kikubwa tunachotakiwa kukifanya ni kumuombea sana ili aweze kubadilika.Tunatakiwa kufanya maombi ya kufunga na kuomba ili kumuombea .." nikasema na kumfanya baba mkwe acheke.
" Kamwe sintathubutu kushinda na njaa kwa sababu ya laana kama Emmy. Kama ameshindwa kutusikiliza sisi wazazi wake ulimwengu ndio akaomfunza adabu.Siku zote asiyefunzwa na wazazi atafunzwa na ulimwengu." akasema baba mkwe na kunifanya na mimi kucheka.Kikapita kimya kidogo baba mkwe akauliza.
? Wayne yule msichana uliyekuwa naye ndiye mwanangu mpya uliyempata?
" Ndiyo baba..Anaitwa Clara.Anajishughulisha na ubunifu wa mitindo na kwa sasa makazi yake ni nchini Afrika ya kusini.Nimekutana naye siku kadhaa zilizopita akiwa katika harakati zake za kutoa semina kwa wanamitindo.Tumetokea kuwa marafiki na kwa muda huu mfupi tuliokuwa pamoja amenifanya niyasahau yale machungu yote niliyofanyiwa na Emmy. Utanisamehe baba kwa kuyasema haya mbele yako" nikasema.Baba mkwe akatabasamu na kusema
" Wayne huna haja ya kuogopa.Wewe ni kijana wangu na ninakupenda sana na siku zote ninakutakia mema.Nimeyashuhudia kwa macho yangu mambo aliyokufanyia mwanangu Emmy. Sikuhadithiwa na mtu yeyote.Kwa kuwa siku zote ninapenda uishi katika maisha mazuri yenye amani na furaha,ninakuunga mkono kabisa kama huyo mama uliyempata sasa hivi unaona anaweza kukufaa na siyo huyu shetani Emmy.Mimi nakuombea tu uwe na maisha mazuri yenye furaha ila nakuomba usije ukathubutu kurudiana tena na Emmy.Atakufanyi
a kitu kibaya sana.Umeona kitendo alichokifanya mchana wa leo.Kama usingekuwa hodari ukakwepa lile jiwe alilolirusha sasa hivi tungekuwa tunaongea mambo mengine tena.Kwa hiyo jitahidi sana kumuepuka ,kaa naye mbali kabisa.Muache atange na dunia na itakapomfunza atarudi kuomba msamaha na kugundua kwamba amekwisha chelewa kwani mlango umekwisha fungwa." akasema baba mkwe.Ninachompe
ndea baba mkwe siku zote amekuwa upande wangu na amekuwa akishirikiana na mimi katika kila jambo.
*************
Wakiwa katika sofa lililokuwapo mapokezi, akina mama waliompeleka Emmy kutibiwa katika zahanati ya Samaria inayomilikiwa na masista wa kanisa katoliki ,walistuliwa na muuguzi ambaye alitumwa na Emmy amuite mtu anayeitwa Sheila ana maongezi naye.Japokuwa akina mama wale walitaka sana kuingia na kumuona Emmy anaendeleaje lakini muuguzi yule alikataa kata kata kwa madai kwamba mgonjwa hakuhitaji kuonana na mtu yeyote yule kwa wakati ule zaidi ya Sheila pekee. Akiwa ameongozana na muuguzi,Sheila akaingia katika chumba alichokuwa amepumzishwa Emmy aliyekuwa amefungwa plasta kadhaa usoni kutokana na majeraha aliyoyapata kwa kipigo.
" Emmy pole sana..Unajisikiaje sasa ? akasema Sheila akikaa kitandani
" Naendelea vizuri ..Ibilisi yule Wayne alitaka kuniua,lakini nitapambana naye..Atanitambua mimi ni nani" akasema Emmy kwa sauti ya chini. Muuguzi yule akatoka nje na kuwaacha Emmy na Sheila pekee mle chumbani.Emmy ambaye alikuwa ametundikiwa chupa ya maji akamuomba Sheila amsogelee karibu zaidi.Alipomtazama katika macho yake alikuwa anatoa machozi.
" Emmy nyamaza kulia mpenzi.Jipe moyo haya ni mambo ya kawaida na yatakwisha." akasema Sheila akijaribu kumtia moyo Emmy.
" Sheila nimemuua mwanangu" akasema emmy kwa sauti ya chini.
" Unasemaje Emmy? Mbona sikuelewi? akauliza Sheila.Emmy akakohoa kidogo akarekebisha koo lake na kusema
" Sheila nimemuua mwanangu Baraka." akasema tena Emmy na kumfanya Sheila astuke,kumuangalia kwa macho ya mshangao.
" Sikuelewi unasema nini Emmy?" akauliza tena Sheila.
" Naomba unisaidie kuniinua niweze kukaa" akaomba Emmy na Sheila akamsaidia kumuinua,akakaa kitandani.
" Sheila tukiwa pale kwa mganga,aliniambia kwamba ili kunifanyia kazi yangu mizimu inahitaji sadaka.Akaniuliza kama nipo tayari kuitoa sadaka ile kwa mizimu ili inifanyie kazi yangu nikakubali na akanipa kisu nikichome katika beseni la maji .Baada ya kukichoma kisu kile katika lile beseni la maji nilisikia sauti kama ya mtu ninayemfahamu akilia na baada ya muda mfupi sauti ile ikapotea kabisa.Kumbe alikuwa ni mwanangu Baraka.Nilipokichoma kile kisu katika beseni nilikuwa namuua mwanangu bila kujua.Ouh Sheila nitafanya nini mimi? Emmy akashindwa kujizuia akaanza kulia.
" Nyamaza usilie Emmy.Usiongee kwa nguvu watu watakusikia na yatakuwa mambo mengine tena.Sasa ikawaje shoga yangu Emmy ukakubali kutoa sadaka bila kuuliza ni sadaka gani unayotakiwa kuitoa?
"Hata sielewi ilikuwaje Sheila.Nadhani nilikuwa nimepumbazwa na dawa za yule mganga.Mshenzi sana yule mganga ameniulia mwanangu na akadiriki hata kufanya mapenzi na mimi tena bila hata kutumia kinga.Ouh Mungu wangu kwa nini nilikubali kirahisi rahisi namna ile kila alichokuwa akiniambia? Halafu alifahamu kabisa kwamba tayari mwanangu amekwisha fariki ndiyo maana akaniambia kwamba nitakaporudi nisipite sehemu yoyote ile na breki ya kwanza niifunge nyumbani kwetu.Alinihakikishia kwamba Wayne lazima atarudi kwangu lakini kwa hali niliyoiona leo sina hakika kama hilo litawezekana." akasema Emmy kwa uchungu huku akilia.Sheila akamfuta machozi.
" Emmy unasema ulifanya mapenzi na yule mganga? akauliza Sheila.
" Ndiyo ! Kwani vipi?
" Mshenzi sana yule babu..Hata mimi alinilewesha dawa zake halafu akaniingilia. Kumbe alitufanyia mchezo huu wote.." akafoka Sheila na kumfanya Emmy azidi kudondosha machozi.
" Basi usilie shoga yangu.Yameshatokea na hatuna tena namna nyingine ya kufanya." akasema kwa unyonge Sheila.
" Sheila naomba ufanye kila utakavyoweza ili uweze kunitoa hapa hospitali na unipeleke kwa yule mganga usiku huu anirudishie mwanangu.Nataka amrudishe mwanangu Baraka" akasema Emmy.
" Emmy hilo ni suala lisilowezekana hata kidogo.Sahau suala la kumrudisha Baraka.Tayari ameshafariki na hawezi kurudi tena "
" Baraka hajafa Sheila.Nakuomba Sheila nipeleke kwa mganga usiku huu kabla mwanangu hajazikwa kesho.Najua anao uwezo wa kumrudisha.Na kama akishindwa kumrudisha mwanangu nitamuua" akasema Emmy.Aliongea kama mtu aliyechanganyik
iwa.Sheila akajitahidi kumtuliza lakini bado Emmy akaendelea kupiga kelele akimuomba Sheila amtoe pale hospitalina kumpeleka kwa mganga.Sheila alipoona mambo yamekuwa magumu akakimbia kwenda kuwaita wauguzi ambao walikuja haraka na kumdhibiti Emmy kisha wakamchoma sindano ya usingizi na baada ya muda akalala usngizi.
" Masikini Emmy amemuua mwanae kwa ujinga wake mwenyewe.Inaniuma sana kwa kitendo hiki alichokifanya.Anahangaika kumtafuta mchawi wakati mchawi ni yeye mwenyewe.Yeye ndiye aliyeiroga ndoa yake.Ameshindwa kumlea mume wake na badla yake kumfanyia vitimbi kila kukicha halafu leo hii anataka kumtafuta mchawi anayeiroga ndoa yake.Amenisabab
ishia hata mimi matatizo.Amenipeleka kwa yule babu mshenzi amenipumbaza kwa dawa zake na kufanya mapenzi na mimi.Sijui nitaoga na sabuni gani ili niweze kuiondoa shombo ya yule mganga mwilini mwangu.Emmy ameniingiza katika matatizo makubwa sana.Sikutegemea kabisa kama mimi Sheila ningekuja kulala na kibabu kama yule mchawi mkubwa. Najuta kuambatana na Emmy.Sitaki urafiki naye tena.Baada ya msiba huu wa mwanae kumalizika sitaki tena urafiki wala ukaribu naye.Ni msichana mbaya na anaweza akakupeleka pabaya.Itakuaje kama yule babu akawa ameniambukiza virusi vya ukimwi? Mungu nisaidie hilo lisinitokee." akawaza Sheila akiwa amesimama chini ya mti huku machozi yakimchuruzika.
TUKUTANE SEHEMU IJAYO??????.
 
BEYOND PAIN
SEHEMU YA 27
MTUNZI: PATRICK.CK
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
" Masikini Emmy amemuua mwanae kwa ujinga wake mwenyewe.Inaniuma sana kwa kitendo hiki alichokifanya.Anahangaika kumtafuta mchawi wakati mchawi ni yeye mwenyewe.Yeye ndiye aliyeiroga ndoa yake.Ameshindwa kumlea mume wake na badla yake kumfanyia vitimbi kila kukicha halafu leo hii anataka kumtafuta mchawi anayeiroga ndoa yake.Amenisabab
ishia hata mimi matatizo.Amenipeleka kwa yule babu mshenzi amenipumbaza kwa dawa zake na kufanya mapenzi na mimi.Sijui nitaoga na sabuni gani ili niweze kuiondoa shombo ya yule mganga mwilini mwangu.Emmy ameniingiza katika matatizo makubwa sana.Sikutegemea kabisa kama mimi Sheila ningekuja kulala na kibabu kama yule mchawi mkubwa. Najuta kuambatana na Emmy.Sitaki urafiki naye tena.Baada ya msiba huu wa mwanae kumalizika sitaki tena urafiki wala ukaribu naye.Ni msichana mbaya na anaweza akakupeleka pabaya.Itakuaje kama yule babu akawa ameniambukiza virusi vya ukimwi? Mungu nisaidie hilo lisinitokee." akawaza Sheila akiwa amesimama chini ya mti huku machozi yakimchuruzika.
ENDELEA????????.
Hatimaye kulipambazuka na shughuli zikaanza kwa kasi.Siku hii ilikuwa ni siku ya mazishi ya Baraka hivyo toka asubuhi kulikuwa na pilika pilika nyiingi.Kijua kilipoanza kuchomoza nilimpeleka Clara hotelini kwa lengo la kuoga na kubadili nguo.
" Emmy hakurudi jana ,inasemekana aliongezewa damu kwani alipoteza damu nyingi kwa kipigo ulichompa" akasema Clara tukiwa garini kuelekea hotelini.
" Ingekuwa vizuri kama angekufa kabisa.Sitaki hata kumuona katika macho yangu yule mwanamke" Nikasema .
? Usiseme hivyo wayne.Kama ungemuua, ungekumbana na mkono wa sheria na mimi ndiye ningeumia zaidi .Sikatai kwamba Emmy amekufanyia mambo mengi na yasiyovumilika na ninakubali kwamba anastahili adhabu,lakini next time kabla hujafanya maamuzi yoyote yale,try to think about me also.? akasema Clara.
? Nimekuelewa Clara.Wewe ni mtu mwenye thamani kubwa sana na siku zote nitakupa kipaumbele kwa kila jambo ninalolifanya? nikasema.
? Wayne tayari nimekwisha pata tiketi za ndege kama nilivyokuwa nimekueleza kwamba baada ya mazishi ya Baraka itatubidi tuondoke Arusha na kwenda kupumzika mbali katika sehemu tulivu ili tutulize akili.Mambo mengi yametokea kwa muda mfupi sana ? akasema Clara.
? Ouh safi sana mpenzi wangu.Umemtuma nani ashughulikie tiketi hizo? nikauliza na kumfanya Clara acheke
? C?mon sweetie,siku hizi mambo yote yanafanyika kielektroniki..? akasema Clara huku akicheka na mimi nikacheka kidogo.
? Umepanga twende tukapumzike wapi? nikauliza
? Its just a suprise Wayne..Utaona wewe mwenyewe.Nina hakika utapapenda sana.? akasema Clara huku akitabasamu
Tulifika hotelini nikajitupa sofani wakati Clara akioga.Nikapitiwa na usingizi.Ni Clara ndiye aliyenistua toka katika usingizi mzito pale sofani..
? Baba mkwe anapiga simu? akasema Clara akiwa ameishika simu yangu mkononi.
? Hallo baba? nikasema
? Wayne uko wapi? akauliza baba mkwe
? Nimekuja huku hotelini mara moja kuoga na kubadili nguo?
? Sawa Wayne usichelewe sana kwani shughuli nzima ya hapa inakutegemea wewe.Bado tuna mambo mengi ya kushughulia asubuhi hii halafu tuelekee hospitali tukauchukue mwili na kuuleta hapa nyumbani?
? Sawa baba ninakuja si muda mrefu.?
Niliingia bafuni nikajimwagia maji,nikabadili nguo na tukaondoka kurejea msibani.Mida hiyo ilipata saa tatu za asubuhi.Tulifika msibani nikaegesha gari nikashuka na kumfungulia mlango Clara.Wakati Clara akishuka gari ya Emmy ikaingia na kuegesha karibu kabisa na lilipo gari letu.Mlango ukafunguliwa na akashuka Emmy akiwa na majeraha kadhaa usoni yaliyotokana na kipigo nilichompa jana. Akina mama wakamsaidia kushuka garini na ghafla akageuza shingo na kukutanisha macho na Clara.Akamuangalia kwa macho ya chuki.Safari hii niliapa kumfanyia kitu kibaya sana endapo angethubutu kumgusa Clara au hata kumtolea neno lolote la kumtusi.
? Usiwe na hofu Clara,hataweza kukufanyia kitu chochote.Safari hii sintamvumilia kwa kitu chochote kile.Nitampa kipigo kikali kuzidi nilichompa jana . Kuwa na amani ? nikamwambia Clara.
? wayne tafadhali mpenzi wangu nakuomba usipigane tena na huyu mwanamke. Kupigana si kitendo cha kistaarabu hata kidogo na hasa katika sehemu kama hii yenye kadamnasi ya watu.Usimpige tena Emmy tafadhali.Endapo atanikosea heshima au kunitolea lugha yoyote ile ya matusi na kashfa,leave it to me.I?ll handle it my way ? akasema Clara akiwa ameuweka mkono mmoja begani kwangu.Clara alikuwa ni mwanamke mwenye roho ya ajabu sana.pamoja na vituko vyote vya emmy lakini bado aliendelea kumuonea huruma.
? Nimekuelewa Clara.hata mimi sipendi kugombana mbele za watu,lakini jana ni yeye ndiye alinisababisha nikapoteza ustaarabu wangu na kuamua kupigana naye.Hata ungekuwa ni wewe usingeweza kuvumilia.? Nikasema
? hayo yameshapita mpenzi wangu,naomba tuyasahau na tuelekeze macho yetu katika shughuli ya leo.? Akasema Clara.
? Clara juzi usiku wakati tukiwa na Chris tunamtafuta Emmy,ulinipigia simu na kuniambia kwamba kuna maneno umesikia yanaongelewa na ungenieleza mara tutakaporudi.Kutokana na kuwa na shughuli nyingi nimeshindwa hata kukuuliza ni maneno gani yalikuwa yanaongelewa?
Clara akasita kujibu akaniangalia usoni.
? Ouh never mind Wayne..Its nothing? akasema huku akitabasamu
? Niambie Clara,ni maneno gani ambayo yalikuwa yanaongelewa? Niliisikia sauti yako wakati ule ulikuwa na wasi wasi sana?
? wayne si masuala ya msingi sana.Mimi nimekwisha yapuuzia? akajibu
? Naomba uniambie Clara na mimi niyasikie hayo yaliyokuwa yanaongelewa.? Nikasisitiza
Clara akaniangalia usoni na kusema
? Kuna maneno niliwasikia akina mama wakiyaongea .Nilikuwa nimekaa nao karibu na hawakujua kama mimi na wewe tuna mahusiano.Walikuwa wanasema?? Clara akasita kuendelea.
? walikuwa wanasemaje Clara? Nikauliza
? walikuwa wanasema eti wewe ndiye uliyemuua Baraka baada ya kupatwa na hasira kwamba si mwanao wa damu..?
Kwa sekunde kadhaa nilibaki nikimuangalia Clara ambaye naye alikuwa akinitazama.Nik
atabasamu na kumuuliza
? Do you believe them?
? Ofcourse not..Mimi nimekuwa nawe kwa muda huu wote wa matatizo ya Emmy.Ninalifahamu sakata zima jinsi lilivyo na ninakuamini huwezi ukafanya vitu kama hivyo.Ninafahamu ni jinsi gani ulivyompenda Baraka .? akasema Clara.Nikatabasamu
? Nashukuru kwa kunielewa na kuniamini? nikasema huku nikifunga mlango wa gari..Clara akaelekea ndani kuungana na akina mama wenzake.Maneno yale aliyoyasema Clara yalinipa hasira japokuwa sikutaka kuonyesha wazi wazi.Nilimpenda sana Baraka na kamwe nisingeweza kufanya kitendo kama kile kama wale akina mama walivyokuwa wakifikiri.Nash
ukuru Clara aliyapuuza maneno yale kwani ni yeye pekee niliyekuwa nikimuhofia asije akaumizwa na maneo yale yasiyokuwa na ukweli wowote.
Maandalizi ya msiba yaliendelea vizuri.watu walikuwa ni wengi sana .Baada ya kila kitu kuwekwa sawa tukaanza safari ya kuelekea hospitali kuu ya mkoa kwa ajili ya kuuchukua mwili wa Baraka na kuuleta nyumbani kwa heshima za mwisho kwa waombolezaji. Bado picha ya Baraka ilikuwa inanijia kichwani mwangu.Sikuamini kama ni kweli Baraka ambaye nilimzoea na kumpenda sana muda mchache ujao tutamfukia ardhini na sintamuaoa tena maishani.Kuna nyakati nilikuwa nadondosha machozi .Nilikuwa na uchungu mwingi sana.Kadiri tulivyokuwa tunaikaribia hospitali ya Mount Meru ndivyo hofu yangu ilivyokuwa ikizidi.
Tulikamilisha taratibu zinazotakiwa kabla ya kuchukua maiti kisha tukakabidhiwa mwili wa Baraka.Alikuwa amelala ndani ya jeneza amefumba macho kana kwamaba amelala usingizi.Alivaa suti yake nyeusi aliyokuwa anaipenda sana.Nilishindwa kujizuia kuangusha machozi.Katika maisha yangu sijawahi kuumia moyo wangu kama siku hii.Msiba usikie kwa mwenzako usiombe ukupate wewe. Watu mbali mbali walinifariji na kuniomba nijikaze japo kuwa inauma.Nikanyam
aza.Sikutaka jeneza lile lifungwe.Nilitamani niendelee kumuangalia Baraka pengine angeweza kuamka.
? Kwa heri baraka..Sikutegemea kama ungeondoka mapema namna hii. Nilikupenda na nitaendelea kukupenda hadi mwisho wa uhai wangu..? nikasema nikiwa nimeuweka mkono wangu katika paji la uso wa Baraka.Watu walinionea huruma sana.Imezoeleka kwamba wanaume ni watu majasiri na ni nadra kuangusha machozi msibani.Usemi huu uliwekwa kando kwa siku ya leo na karibu kila mtu aliyekuwapo hapa aliangusha chozi japokuwa kila mtu kwa namna yake.Ilikuwa ni simanzi kubwa.Baba mkwe akanisogelea akaninong?oneza kwamba muda unakwenda hivyo wanahitaji kuwapa nafasi watu wengine waliofika pale hospitali kutoa heshima zao za mwisho kwa mwili wa baraka.Niliuvua mkufu wangu wa dhahabu nikamvisha Baraka.Nakumbuka ni baraka ndiye aliyenichagulia mkufu huu mzuri siku moja tulipokwenda kufanya manunuzi ya mavazi.
Baada ya watu waliokuwepo pale hospitali kumaliza kutoa heshima zao za mwisho kwa miwli wa Baraka tukaanza safari ya kurejea nyumbani.Ulikuwa ni msafara mkubwa wa magari.Kifo cha Baraka kiliwaumiza wengi.Mara tulipowasili nyumbani vikaamka vilio vikubwa toka kwa akina mama.Baadhi yao walianguka na kupoteza fahamu baada ya kuliona jeneza lenye mwili wa baraka likiingia ndani. Jeneza liliwekwa katika jukwaa maalum na bila kupoteza muda shughuli ya kutoa heshima za mwisho ikaanza.Ulikuwa ni msururu mrefu wa watu ambao ulipeleka zoezi lile kuchukua muda mrefu.Saa tisa alasiri tukaelekea kanisani kwa ajili ya ibada.Pale kanisani likafanyika pia zoezi la kutoa heshima za mwisho kwa wale ambao hawakuwa wamefanya hivyo.Niliinuka na kwenda kumtazama Baraka kwa mara ya mwisho.Sikutegemea kumuona tena katika maisha yangu.
? Kwa heri mwanajeshi wangu ? hilo ndilo neno pekee nililosema kumuaga Baraka.Jeneza likafungwa na ibada ikaanza.Baada ya ibada kumalizika ukaanza msafara wa kuelekea makaburini Njiro.Hiki kilikuwa ni kipindi kigumu mno.Tulifika makaburini , ikafanyika ibada ndogo ya mazishi halafu jeneza likashushwa kaburini.Emmy alianguka na kupoteza fahamu wakati jene za linashushwa kaburini akatolewa na kupekewa pembeni kwa ajili ya msaada.Baraka akazikwa bila ya mama yake kushuhudia.Miguu yangu iliishiwa nguvu lakini nikajikaza kiume.Japokuwa bado nilikuwa na hasira naye lakini namshukuru Chris ambaye alikuwa nami kwa muda wote kunipa moyo na kunitegemeza pale nilipoishiwa kabisa na nguvu.Babu na bibi yake Baraka ndio waliokuwa wa kwanza kutupia udongo katika kaburi.baada ya hapo nikafuata mimi kama baba yake.mama yake hakuwepo alikuwa poteza fahamu hivyo wakaendelea kuweka udongo watu wengine na baada ya zoezi lile kukamilika Kaburi likaanza kufukiwa.
Ndani ya muda mfupi tayari kaburi lilikwisha fukiwa.Baraka alikuwa amezikwa tayari na nisingemuona tena maishani.Ni Mungu pekee awezaye kuyafahamu machungu niliyokuwa nayo siku ile. Kisha fukiwa likafuata zoezi la kuweka shada za maua .Yaliwekwa maua mengi sana juu ya kaburi la mtoto huyu.Nililitazama kaburi lile nikapandwa na hasira.Sikutamani tena kumuona Emmy mwanamke mwenye roho ya kikatili sana.Yeye ndiye aliyesababisha uchungu huu.Padre akalibariki kaburi na huo ndio ukawa mwisho wa safari ya Baraka hapa duniani.Watu walianza kurejea katika magari yao kwa ajili yakurejea nyumbani.sikutaka kuondoka pale makaburini.Chris na watu kadhaa walijaribu kunisihi lakini nikawaomba waniache kwa muda..Nilitaka nipate muda kidogo wa kukaa karibu na kaburi la Baraka.Chris akawaambia wale watu waliobakiname wanipe nafasi.Wakajitenga nami na kwenda kukaa mbali kidogo .Nikabaki peke yangu katika kaburi lile.Nikapiga magoti pembeni na kulia sana.Nililia kwa uchungu mkubwa.Nilimlaani Emny kwa laana zote za dunia hii.
? Kwa heri Baraka.Nitakuwa natembelea hapa kila mara kuja kulitazama kaburi lako? nikasema huku nikigeuka na taratibu nikaanza kuelekea garini.Chris akanishika mkono nakuniongoza hadi garini kisha tukaanza kurejea nyumbani.Niliegemeza kichwa kitini nikafumba macho na kwa mbali wimbo uitwao Gone to soon wa Michael Jackson ukawa unasikika mle garini .
Like A Comet
Blazing 'Cross The Evening Sky
Gone Too Soon
Like A Rainbow
Fading In The Twinkling Of An Eye
Gone Too Soon
Shiny And Sparkly
And Splendidly Bright
Here One Day
Gone One Night
Like The Loss Of Sunlight
On A Cloudy Afternoon
Gone Too Soon
Like A Castle
Built Upon A Sandy Beach
Gone Too Soon
Like A Perfect Flower
That Is Just Beyond Your Reach
Gone Too Soon
Born To Amuse, To Inspire, To Delight
Here One Day
Gone One Night
Like A Sunset
Dying With The Rising Of The Moon
Gone Too Soon
Gone Too Soon
Ni kweli Baraka alikuwa ameondoka mapema mno.Bado alikuwa na ndoto nyingi sana za maisha yake lakini zote zimeondoka naye.Alitamani sana kuwa mwandishi mahiri wa vitabu lakini hata ndoto yake hiyo nayo imetoweka.Taifa limempoteza kijana mwenye ndoto nyingi kubwa na nzuri .Yote hii imesababishwa na mwanamke mmoja tu Emmy.Kila nilipolikumbuka jina emmy nilimalizia na laana nyuma yake.Nilimlaani kwa kila laana.Nilimuombea kila baya japokuwa maandiko yanatuambia kwamba tuwapende maadui zetu na tuwaombee maisha mema na marefu..
Nyumbani kilichokuwsa kikiendelea ni kupata chakula kwa waombolezaji. Nilishindwa kabisa kula.Sikuwa na hamu ya chakula licha ya kubembelezwa sana na wenzangu.Kwa mbali kijua kilikuwa kikimalizikia .watu walikuwa wanatawanyika baada ya shughuli ndefu ya siku ya leo.Nikiwa nimekaa pembeni kabisa nikiwa na Chris na rafiki zangu wengine wawili ,akatokea Clara akiwa na sahani ya hakula.
? Wayne ,nafahamu huna hamu ya chakula ,lakini nakuomba ule japo kidogo chakula hiki .Unahitaji kupata nguvu.? Akasema huku akinikabidhi sahani ile ya chakula.Nilishindwa kumkatalia nikaipokea na kuanza kula .Alikuwa amekaa pembeni yetu na nilipomaliza kula akachukua sahani yake akaondoka.Mara baba mkwe akajitokeza.Chris na wale rafiki zangu wawili wakaondoka pale na kutucha sisi wawili..
? Wayne pole sana.Nafahamu ni jinsi gani ulivyoumia lakini haya ndiyo maisha yetu sisi wanadamu.Wote tutapitia hatua hii.Baraka yeye amekwisha maliza safari yake na kwa sisi tuliobaki hatuna budi maisha yaendelee kama kawaida japokuwa itatuchukua muda mrefu sana kusahau tukio hili.Kwa upande wangu napenda nikushukuru sana kwa msaada wako mkubwa tumeweza kufanikisha mazishi ya Baraka bila matatizo.Ninachokuomba Wayne ni kitu kimoja tu.? Baba mkwe akanyamaza kidogo akanywa konyagi kama kawaida yake kisha akaendelea
? nakuomba umsahau kabisa Emmy.Futa kabisa picha yake katika kichwa chako.Endelea na maisha yako na huyu uliyempata sasa hivi.Siku zote mimi nitaendelea kuwa msaada kwako .Endapo utarudiana na Emmy atakuua.?
? Nimekuelewa baba .Mimi na emmy tumefikia mwisho na sintathubutu kamwe kurudiana na Emmy.? Nikajibu kwa ufupi kisha tukaendelea na maongezi mengine hadi usiku mwingi.Tulilala hapo msibani siku hiyo.
****************
Kulipambazuka asubuhi na kiubaridi kikali cha Arusha.Wakati nikipiga mswaki Clara akatokea.
? Morning darling.Pole na baridi ya usiku? akasema huku akitabasamu.Pamoja na kujitanda mavazi haya ya msiba bado Clara alizidi kuonekana mrembo zaidi.Nikamtazama nikatabasamu na kusema
? Nashukuru Clara.Umeamakje?
? Mimi nimeamka salama pia.? Akajibu
? nafurahi kusikia uko salama.?
? wayne ratiba ya leo ikoje? Nini kinaendelea leo?
? Ratiba ya leo,asubuhi hii tutaenda makaburini kuwasha mishumaa katika kaburi la Baraka halafu tutarejea nyumbani na saa nne kutakuwa na kikao cha wanandugu na msiba utamalizika rasmi. Baada ya kikao hicho sisi tutawaaga na kuondoka zetu.? Nikasema .Nilimshukuru sana Clara kwa mapenzi makubwa aliyoyaonyesha kwangu kwani licha ya jina kubwa alilokuwa nalo na utajiri wake mkubwa lakini bado ameweka hayo yote kando na amekuwa nami bega kwa bega katika kipindi hiki kigumu nilichokuwa nacho.Amenidhihirishia kwamba ananipenda kwa dhati ya moyo wake.
Baada ya kuachana na Clara akaja Chris.
? wayne umeamkaje? Akanisalimu
? Nimeamka salama Chris.? Nikajibu huku nikiendelea kunawa.
? Ok wayne,niliona nikusalimie na kukuaga.Ninaondoka zangu kwani shughuli zilizobaki hapa ni za wanandugu.Tutazidi kuonana Wayne? akasemaChris huku akipiga hatua kuondoka.
? Chris ! ..? Nikaita akageuka
? Nashukuru sana kwa msaada wako jana.Bila wewe jana sijui ningefanya nini.By the way naomba tusameheane yale yote yaliyopita.Mambo mengi yametokea baina yetu lakini naomba tutafute muda tuongee na tuyamalize.Nitatafuta muda mzuri tutakaa na tutayamaliza.Thanx for everything.? Nikasema huku nikimpa mkono Chris.hakuamini kama ningeweza kuongea maneno yale.
? wayne nakushukuru sana .Sina neno la kusema lakini niko tayari muda wowote kukaa nawe,tuongee na tuyamalize haya mambo.? Akasema Chris tukaagana akaondoka.
saa mbili za asubuhi tukaelekea tena makaburini .Tukawasha mishumaa katika kaburi la Baraka pamoja na kufanya maombi.Tulirejea nyumbani na saa nne za asubuhi kama ilivyokuwa imepangwa kikaanza kikao cha wanandugu kwa ajili ya kumaliza rasmi shughuli za msiba.Kwa mshangao wa wengi Emmy hakuwepo katika kikao kile. kila mtu alikuwa anashangaa kwa sababu hata pale nyumbani hakuwepo..Tukaanza kuulizana emmy kaenda wapi lakini hakuna aliyekuwa na jibu.Baba mkwe hakutaka kuahirisha mambo ,akaamuru kikao kiendelee bila ya emmy kwani hata wakati baraka anafariki yeye hakuwepo.
Kikao kilimalizika mimi na Clara tukaaga na kuondoka zetu kwenda kupumzika hotelini
TUKUTANE SEHEMU IJAYO...............
 
Asubuhi na mapema wakati watu wameanza kuamka,Emmy alimuamsha rafiki yake Sheila na kwa haraka wakaingia katika gari na kuondoka.Hakuna aliyefahamu walikuwa wanaelekea wapi asubuhi hiyo.Emmy ambaye macho yake yalikuwa yamevimba kwa kulia alionekana kuwa na hasira nyingi.Sheila ndiye aliyekuwa akiendesha gari lile.
? Emmy una uhakika na kitu unachotaka kukifanya ? akauliza Sheila.
Emmy akainua uso wake uliokuwa na hasira akamtazama Sheila kisha akasema
? Sheila ninajua ninachokifanya endesha gari twende.? Akasema Emmy.
? Naomba usichukie Emmy lakini nimepoteza kabisa matumaini na yule mganga kama ana uwezo wa kukusaidia kumrudisha Wayne kwako .Badala yake amesababisha kifo cha mwanao na zaidi sana Wayne ameonyesha wazi kuzidi kukuchukia.Sidhani kama kurudi tena kwa mganga litakuwa suluhisho la matatizo yako.Yule mganga hana msaada.Tayari amekwisha tusababishia matatizo makubwa.? Akasema Sheila
? Sheila ,mimi ndiye mwenye matatizo.Nina imani atanisaidia na ana uwezo wa kunisaidia.Mbona alimsaidia rafiki yangu akarejewa na mumewe? Kwa nini mimi ishindikane? Iwapo atashindwa nakuapia ni lazima atamrejesha mwanangu.Ama zake ama zangu.Nataka nikiwa kwake leo hii Wayne anipigie simu na kama atashindwa ni mimi na yeye.Ametudhalilisha sana kwa kufanya nasi mapenzi na bado amemuua mwanangu .Leo ama amrejeshe mwanangu Baraka ama amrejeshe Wayne kwangu? akasema emmy akiwa na hasira
? Emmy wewe ni rafiki yangu mkubwa lakini naomba nikuweke wazi kwamba sifurahii hata kidogo kurejea tena kwa mganga kutokana na mambo aliyotufanyia na isitoshe mimi siamini kabisa katika mambo haya ya ushirikina.Iwapo atasema kwamba dawa inafanyika usiku wa leo siko tayari kulala kule tena.Nitaondoka na kukuacha peke yako.Naomba ulifahamu hilo Emmy ili tusije kulaumiana baadae.? Akasema Sheila .Emmy hakujibu kitu.
? Rafiki yangu amepotea sana. Huku alikojiingiza katika ushirikina ni sehemu hatari mno na siku zote ushirikina mwisho wake huwa mbaya .Hii ni mara yangu ya mwisho kumsindikiza kuja huku kwa mganga kumtafuta mchawi wa ndoa yake wakati mchawi ni yeye mwenyewe.Ameivuruga ndoa yake kwa ujinga wake mwenyewe na hapaswi kumlaumu mtu yeyote yule.Alipata bahati ya kumpata mume anayempenda sana lakini ameshindwa kuitumia bahati hiyo na sasa anaanza kuhaha kumtafuta mchawi.Siko tayari kuendelea na imani hizi.Hii ni mara yangu ya mwisho kushirikiana naye katika mambo haya ya kishenzi..Kile kizee kilitufanyia udhalilishaji mkubwa.Najilaumu sana kila nikikumbuka kitendo alichotufanyia.
Mpaka sasa nikikumbuka nahisi kutapika .Sijui nitaoga na sabuni gani ili niweze kuiondoa mbaya harufu ya yule babu ambayo ninaisikia kila siku.Emmy amenifanya nidhalilike namna hii...Nimeanza kumchoka Emmy.Kama akiendelea na tabia yake hii sintakuwa na njia nyingine zaidi ya kuachana naye..Sintakubali kuwa na rafiki mwenye tabia kama za Emmy? akawaza Sheila huku gari likiendelea kwenda kwa kasi.
Saa sita za mchana waliwasili nyumbani kwa mganga.Wakasimamisha gari na kushuka wakaingia ndani.Mama msaidizi wa mganga akawapokea.
? Karibuni wanangu? akasema
? Ahsante ? akasema Sheila Emmy yeye hakusema kitu alikuwa amenuna.
? kwema huko mtokako? Akauliza yule mama
? Huko kwema mama japo si kwema sana? akasema Sheila
? Huyu mganga tumemkuta? Akauliza emmy kwa ukali.Yule mama akamuangalia kisha akawaomba waingie ndani
? Naomba unipe jibu moja mganga yupo au hayupo? Akahoji Emmy huku akimtazama yule mama kwa macho makali sana.
? Mganga yuko ndani..? akasema na kuwaongoza Emmy na Sheila hadi ndani.
? karibuni hapa mketi.Mganga ana shughuli akimaliza atakuja kuwahudumia.? Akasema yule mama na kuondoka akawaacha akina Emmy mle chumbani.
? Leo ama zake ama zangu..? akasema emmy kwa sauti ndogo .Sheila hakumjibu kitu.
Baada ya masaa mawili yule mama akarejea tena akawaomba Emmy na Sheila wamfuate.Moja kwa moja wakainhgi akatika chumba cha mganga.
? karibuni wanangu.Limekuwa jambo jema mmerudi tena?.habari zsa huko mtokako? Akasema mzee Mtuguru huku akitabasamu na mkononi akiwa anaupunga usinga wake.Emmy akamuangalia kwa jicho la chuki na akiwa bado amesimama akasema
? Mzee leo sijaja hapa kufanya mzaha.Unajua ulichokifanya kwa hiyo nimekuja hapa kwa mambo mawili tu.Aidha unirudishie mwanangu au unitimizie ninavyotaka.? Akasema Emmy kwa ukali.Mganga akamtazama kisha akamwambia
?Binti naomba ukae chini..?
? Sintakaa hadi umenijibu kwamba utanirudishia mwanangu uliyemuua au utamrudisha Wayne kwangu.? Akafoka Emmy
? Binti nimekwambia kaa chini.Hii si sehemu ya kuja na kuanza kupayuka.Hii ni sehemu ya mizimu na inaweza ikakuadhibu vikali kwa kukosa adabu.Nakuamuru kwa mara ya mwisho kaa chini? akafoka mzee Mtuguru ambaye naye alikwisha aanza kukasirishwa na tabia aliyoionyesha Emmy.
? Emmy kaa chini shoga,yasije anza mambo mengine bure? akasema Sheila na Emmy akaketi mkekani.
Mganga akaongea maneno yake ya kiganga halafu akachukua usinga wake akaupunga hewani.
? Emmy umeikasirisha sana mizimu kwa utovu wa nidhamu uliouonyehsa na kwa maana hiyo unatakiwa kuiomba msamaha ama sivyo litakupata jambo baya sana .Mizimu itakuadhibu vikali.? Akafoka mzee Mtuguru .Emmy akastuka baada ya kusikia kwamba mizimu inaweza kumuadhibu.
? Mambo yako hayakwenda kama ulivyokuwa umetarajia kwa sababu bado kuna kazi moja ambayo unatakiwa uifanye wewe kwa mkono wako.kabla ya shughuli hiyo itakulazimu kwanza kuiomba msamaha mizimu .Msamaha huo huambatana na sadaka ya kuchinja mnyama.Nina mbuzi katika zizi langu hapo ambao hutumika kwa ajili ya sadaka kwa mizimu.Shughuli itaanza leo saa moja jioni hadi usiku mwingi.Hala??? kabla mzee Mtuguru hajaendelea Emmy akaingilia kati
? Mzee siwezi kulala hapa kwako usiku wa leo..Kitendo ulichotufanyia bado sijakisahau..? akafoka Emmy
? Kama hutalala hapa basi ni ishara ya kuidharau mizimu na lazima ikuadhibu ? akasema mzee Mtuguru.Emmy akabaki kimya.
? Unakubali kulala hapa ili dawa yako imalizike usiku wa leo au unarudi Arusha ?? akauliza mganga kwa ukali
? Nitabaki? akajibu Emmy baada ya kufikiri kwa muda
? Mimi naenda kuandaa mbuzi kwa ajili ya shughuli ya usiku.? Akasema mzee Mtuguru na kutoka nje.
? Shoga mimi silali hapa kwa mganga kama nilivyokwambia? akasema Sheila baada ya mganga kutoka mle chumbani
? Itakubidi ulale Sheila si umesikia mganga alivyosema? Emmy akajibu
? Mimi hayanihusu.Nimesema sintalala hapa.Kitendo alichonifanyia siwezi kukisahau hata kidogo.?
? Sheila usiondoke ukaniacha huku peke yangu? Emmy akaomba
? Hapana Emmy..siwezi kulala huku.Lazima nirejee Arusha leo hii.hayo yalikuwa ni makubalinao yetu? akasema Sheila huku akiinuka.
?Usiniache Sheila?? akasema Emmy lakini Sheila hakumjali akaenda kuchukua mkoba wake akamuomba mama msaidizi wa mganga amsaidie kumtafutia usafiri wa kumfikisha barabara kuu ambako angeweza kupanda mabasi yanayoelekea Arusha.
? Sitaki tena mambo ya kipuuzi.Sitaki kushiriki katika mambo ya ushirikina tena.hayana manufaa yoyote..? akawaza Sheila akiwa juu ya piki piki akipelekwa stendi ya mabasi kusubiri usafiri wa kuelekea Arusha.
*******************
? Clara come here close to me..? nilimwambia Clara tukiwa chumbani hotelini.Clara aliyekuwa amekaa sofani akitazama Luninga akainuka na kuja kitandani.Siku nzima ya leo tumeitumia kupumzika baada ya siku kadhaa za msiba wa Baraka.
? I?m here my love ? akasema Clara akinitazama usoni.
? Clara kwanza napenda nichukue nafasi hii kukushukuru sana kwa upendo wako wa pekee wa kusitisha shughuli zako zote na kuwa pamoja nami hasa katika kipindi kile kigumu cha msiba wa baraka.Wewe ndiye uliyekuwa mfariji wangu mkubwa katika siku hizi ngumu na bado utaendelea kuwa mfariji wangu kwani jambo hili halitakwisha leo wala kesho kichwani mwangu.Itanichukua siku nyingi kulisahau.Nina deni kubwa kwako na ambalo sijui nitalilipa vipi.Deni la upendo wako wa kweli na wa dhati..? nikamwambia Clara na kumfanya atabasamu.
? Wayne ,wewe una thamani kubwa kupita mali ,biashara na kila nilichonacho.Hivi vyote ni vitu ambavyo vinapatikana kwa juhud na kufanya kazio kwa bidii lakini mtu kama wewe si rahisi kupatikana katika ulimwenmgu wa sasa.Niko tayari kufanya lolote lile ili mradi niwe nawe kila sekunde.Nilistahili kuwa nawe msibani kwa sababu ulikuwa ni msiba wetu sote .Ulimpenda Baraka halikadhalika nilimpenda pia.? Akasema Clara.
? Pamoja na yote yaliyotokea nina kitu ninataka kukueleza.? Nikasema
? Usihofu Wayne nieleze kitu chochote kile unachohitaji kunieleza? akasema Clara.
? Clara maisha yangu ya nyuma yametawaliwa na historia inayoniumiza mno na hasa historia ya maisha yangu na Emmy.Sitaki kukumbuka maisha ya nyuma kwa sababu tayari nimeanza maisha mapya yenye furaha na amani.Pamoja na maisha haya mapya niliyoanza kuyaishai lakini bado kuna tatizo.? Nikanyamaza na kumtazama Clara ambaye alionyesha uso wa wasi wasi.
? Kuna tatizo gani Wayne ? akauliza Clara
? Kama utakumbuka tuliafikiana kwamba tutafute nyumba ya kuishi hapa Arusha kwa sababu ni sehemu unayoipenda sana.Nakubaliana na mawazo yako kwa sababu hata mimi ninaipenda Arusha.Baada ya kufikiri kwa kina nimegundua kwamba iwapo ninataka kuishi maisha yenye raha na amani itanilazimu kuhama Arusha na kwenda kuishi mbali, mahala ambako Emmy hatapata nafasi ya kuwa karibu nami.Mwanamke huyu ataendelea kutuandama kila uchao tukiendelea kukaa hapa Arusha.Wazo langu ni kwamba tutafute nyumba jijini Dar es salaam.Lile ni jiji kubwa na tutaishi kwa amani.? Clara akatabasamu na kunishika mkono wangu.
? Wayne hata mimi nilikuwa na wazo kama hilo lakini nikaogopa kukueleza kwa kujua kwamba unapenda sana kuishi Arusha.Kwa kweli nilimtazama Emmy tukiwa msibani bado ana chuki kubwa na wewe chuki ambayo sina hakika kama itakwisha.Nakubaliana na mawazo yako kwamba hatutaweza kuishi maisha ya raha na amani kama tukiwa karibu naye.Utanisamehe kwa kusema hivi lakini that woman is a monster ? akasema Clara
? nashukuru sana Clara kwa kuliona hilo na kukubali tukaishi sehemu nyingine mbali na arusha.Unapendekeza kwenda kuishi mkoa gani?
? Wayne ni mapema sana kuamua ni sehemu ipi tukaishi.Mimi ninaweza kuishi nawe sehemu yoyote ile hata kama ni shambani.? Akasema Clara na kunifanya nicheke.
? Usicheke Wayne.Ni kweli ninaweza kuishi nawe sehemu yoyote ile.Usiumize kichwa kuhusu sehemu ya kuishi mimi na wewe.Tutapanga na kuamua vizuri baada ya kumaliza mapumziko yetu.Kesho tutakapoondoka jiji la Arusha tutapunga mkono wa kwaheri kwani hatutarudi tena.Safari ya maisha yetu ya pamoja tayari imeanza.? Akasma Clara .Nikamvuta kwangu na kumbusu .
? Mbona hutaki kuniambia tunaelekea wapi kupumzika? Nikamuuliza
? Hapana Wayne sintakwambia.Just wait and see.Its a surprise? akasema huku akitabasamu.
********************
Ni saa nne za usiku sasa bado shughuli ya uganga ilikuwa ikiendelea.Emmy alikuwa amevishwa vazi jeusi na kupakwa dawa nyeupe usoni.Zoezi la kwanza la kuchinja mbuzi na kuomba msamaha kwa mizimu likakamilika kisha likafuata zoezi la pili .
Mzee Mtuguru akampa Emmy chungu akishike kisha akamuamuru amfuate.Walipita katika msitu mnene wenye kiza na milio ya kutisha.baada ya mwendo wa masaa mawili wakafika katika shamba moja la mihogo ambalo kati kati yake kulikuwa na kibanda kidogo cha udongo..Akamuamuru Emmy amfuate mle ndani.Kulikuwa na giza nene .Mganga akaongea maneno yake ya kiganga ambayo Emmy hakuyaelewa halafu akawasha kibatari na chumba ikawa na mwanga .Akachukua dawa fulani na kumpaka Emmy na ghafla Emmy akaanza kuona mambo mengi ya ajabu ajabu na ya kutisha.Mle ndani ya kile chumba aliweza kuwaona watu kadhaa wake kwa waume wakiwa wamekaa wamejikunyata.walikuwa na nywele ndefu .Walikuwa wanatisha.Emmy akaogopa na kutetemeka.Hakuwahi kuyaona mambo ya kutisha namna hii.Nje ya kibanda kile alisikia milio ya wanyama na midudu ya kutisha. Mganga akamkabidhi kisu mkononi.
? Unatakiwa ukamilishe kazi iliyobaki ili mambo yako yafanikiwe? akasema mganga lakini Emmy hakujibu chochote.Bado alikuwa anaogopa sana.Mganga akaliendea tenga moja kubwa lililokuwa pembeni ya kile chumba akaliinua na mara Emmy akaona kitu ambacho hakukiamini kama ni kweli. Aliogopa na kutetemeka mwili.Nguvu zilimuisha.Katika ile pembe ya nyumba alionekana mwanae Baraka akiwa amejikunyata.Alikuwa anatia huruma sana.
? Baraka !! ? Emmy akasema kwa mshangao..Baraka hakujibu kitu chochote aliendelea kumuangalia kwa macho ya huruma..
? Baraka kumbe bado uko hai !! ..Mganga nakuomba unirudishie mwanangu? akapiga kelele Emmy huku machozi yakimtoka.
? Baraka umekwisha mtoa sadaka kwa mizimu na hawezi tena kurudi.Unachotakiwa kufanya kwa sasa ni kumkata ulimi kwa hicho kisu nilichokupa.? Akasema mzee Mtuguru
? What !! ?siwezi kufanya upuuzi wa namna hiyo..Mwanangu yule pale ni mzima kabisa na siwezi kamwe kumkata ulimi.? Akafoka Emmy akakitupa kisu chini.Mganga akamtazama kwa hasira kisha akasema
? Muda mchache uliopita tumetoka kuiomba msamaha mizimu kwa sababu ya utovu wa nidhamu uliouonyesha kwao.Nakuonya kwa mara nyingne tena kwamba mizimu haitakuwa na uvumilivu kwa tabia yako hii.Inaweza hata kukuua kwa kuikosea heshima.Nakuomba ufanye kama unavyoelekezwa kufanya.Kwa hiyo inua kisu sasa hivi na umsogelee Baraka umkate ulimi wake haraka.?akafoka mzee Mtuguru.
Emmy alikuwa analia alipomuona mwanae amejikunyata pembeni ya kona.Mganga akachukua tena dawa nyingine na kumpata kichwani.Mara Emmy akajikuta akiwa na ujasiri wa ajabu sana.Akainama akakiokota kisu na kumkaribia mwanae.Akamtazama akamshika na kumfumbua mdomo.Baraka hakuweza kuongea chochote. Emmy akaukata ulimi wa baraka kama alivyokuwa ameelekezwa kisha mzee Mtuguru akamuamuru atoke nje na yeye akaendelea na shughuli zake za uganga mle ndani .Baada ya masaa mawili akatoka na kumkuta Emmy amekaa pembeni ya nyumba ile akilia.
? usilie Emmy.Kwa hivi sasa mambo yako yote yanakwenda kuwa mazuri .? akasema mganga kisha wakaanza safari ya kurudi.
? Emmy mizimu imefurahi na ninakuhakikishia kwamba safari hii Wayne anarudi kwako.Ninachotaka kufahamu toka kwako ni kitu gani tumfanye huyu mwanamke aliyenaye? Tumuue? Akauliza mzee Mtuguru.Emmy akafikiri kidogo kisha akasema
? Ninachokitaka mimi ni kumfanya ateseke maisha yake yote.Asiweze kutembea wala kufanya kazi yoyo tile.Maisha yake yatawaliwe na mateso makali.?
Mzee mtuguru akampa Emmy pembe jeusi lililozungusiwa ushanga na kumwambia
? Sema mbele ya pembe hili unataka mizimu imfanye nini huyu mwanamke aliye na mume wako?
Emmy akaikamata pembe ile kisha akasema
? Nataka apewe ugonjwa ambao utamfanya aishi maisha ya mateso na maumivu makali hadi siku ya kufa kwake.Asiweze kufanya kazi yoyote ile tena katika maisha yake? akasema Emmy.
? Mizimu imekusikia na itafanya kama ulivyoiomba? akasema mganga.
************************
Saa tatu za asubuhi tayari tulikwisha funga mizigo yetu kwa ajili ya safari.Nilimuomba rafiki yangu Beka atupeleke uwanja wa ndege wa Kilimajnaro halafu abaki na gari langu.Saa tatu na nusu safari ya kuelekea uwanja wa ndege ikaanza.Nilikuwa na furaha isiyo kifani kwani nilitegemea kwamba sasa karaha zote za Emmy nitaziacha nyuma na mimi kuishi maisha ya furaha na amani nikiwa na malaika wangu Clara.Tuliwasili uwanja wa ndege tukaagana na Beka na sisi kuingia sehemu ya kusubiria ndege .
Hatimaye muda wetu ukafika na tukaombwa tuelekee ndegeni.Taratibu tukiwa tumeshikana mikono tukaungana na abiria wengine kuelekea mahala ilipokuwa ndege tutakayosafiri nayo.Kabla hajaikanyaga ngazi ya ndege Clara akasimama.
? Wayne naishiwa nguvu ..siwezi tena kunyanyua mguu wa??.? Hayo yalikuwa maneno ya mwisho ya Clara.Akaanguka na kabla hajafika chini nikawahi kumdaka.
TUKUTANE SEHEMU IJAYO
 
BEYOND PAIN
SEHEMU YA 29
MTUNZI : PATRICK.CK
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
Saa tatu za asubuhi tayari tulikwisha funga mizigo yetu kwa ajili ya safari.Nilimuomba rafiki yangu Beka atupeleke uwanja wa ndege wa Kilimajnaro halafu abaki na gari langu.Saa tatu na nusu safari ya kuelekea uwanja wa ndege ikaanza.Nilikuwa na furaha isiyo kifani kwani nilitegemea kwamba sasa karaha zote za Emmy nitaziacha nyuma na mimi kuishi maisha ya furaha na amani nikiwa na malaika wangu Clara.Tuliwasili uwanja wa ndege tukaagana na Beka na sisi kuingia sehemu ya kusubiria ndege .
Hatimaye muda wetu ukafika na tukaombwa tuelekee ndegeni.Taratibu tukiwa tumeshikana mikono tukaungana na abiria wengine kuelekea mahala ilipokuwa ndege tutakayosafiri nayo.Kabla hajaikanyaga ngazi ya ndege Clara akasimama.
? Wayne naishiwa nguvu ..siwezi tena kunyanyua mguu wa??.? Hayo yalikuwa maneno ya mwisho ya Clara.Akaanguka na kabla hajafika chini nikawahi kumdaka.
ENDELEA??????????.
Emmy alikuwa amesimama mbele ya kioo kikubwa akiwa amefura na hasira na sura yake ameikunja..Kwa muda wa saa moja sasa alikuwa amesimama akitazama kioo kile kikubwa mfano wa luninga ,kilichokuwa kikimuonyesha kila kilichokuwa kinaendelea kati ya Wayne na Clara.Hakuwa ameongea chochote toka alipoanza kutazama luninga ile ikiwaonyesha Wayne na Clara walivyokuwa wanajiandaa kwa safari. Wayne na Clara wakiwa uwanjani walionekana ni wenye furaha kubwa .Walikuwa wamekaa wakisubiri zamu yao ya kupanda ndegeni ifike na baadae wakashikana mikono na kuanza kuelekea ndegeni.Clara akauma meno kwa hasira
? Damn you Wayne..huwezi kunikimbia..Nit
akutafuta usiku na mchana.Na huyo mwanamitindo wako ambaye amekupagawisha na kukufanya unitaliki atakiona cha moto..? akawaza Emmy .Muda wote huu mganga alikuwa amesimama pembeni yake akiwa na usinga wake mkononi akiupunga huku na huko huku akiongea maneno yake ya kiganga.
? Emmy Wayne na Clara wanaondoka na bado haujafanya maamuzi yoyote.hii ni nafasi yako usiiache ikapita..Ukiacha wakiingia ndegeni na wakaiacha ardhi ya Arusha ,kurudi tena itakuwa vigumu mno.Kama bado unataka kuendelea na ile dhamira yako basi huu ndio wakati wake.Yeyote utakayemfunga siku ya leo hatapona hadi siku utakapokufa wewe.? Akasema mganga huku akimuonyeshea Emmy meza iliyokuwa na wanasesere wawili .Emmy hakusema kitu akageuka na kuiendea meza ile kisha akachagua mwanaserere mwenye umbo la mwanamke.Mganga akampa sindano.Emmy akasimama tena mbele ya kile kioo akawashuhudia Wayne na Clara wakikaribia kufika katika ngazi za kupandia ndege.Kwa hasira akauinua mkono wake wa kulia uliokuwa umeshika sindano ndefu na kuichoma upande wa kulia wa yule ukatoka moshi mweupe na sekunde ile ile Clara ambaye alikuwa anajiandaa kuikanyaga ngazi ya kupandia ndegeni akaanguka na hakuweza kuongea wala kuinuka tena.Emmy akatabasamu
" Leo nimekupata " akasema Emmy huku akitabasamu.
? Kazi imekwisha? akasema mganga.
? Kwa sasa huyu mwanamke kazi yake imekwisha.Nakuhakikishia Wayne lazima arudi kwako ndani ya muda mfupi. Atakufuata yeye mwenyewe.? Akajigamba mzee Mtuguru.
? Nashukuru sana Mganga. Nakuahidi zawadi nzuri mno kama Wayne atafanikiwa kuja kwangu.? Akasema Emmy huku akitabasamu
? Usiseme kama atarudi kwako.nakuhakikishia lazima arudi kwako na safari hii hataweza kuondoka tena.? Mganga akazidi kumpa moyo Emmy.
*************************
Clara..!! Clara !! ..? Niliita kwa nguvu baada ya kumdaka Clara alipotaka kuanguka lakini hakuweza kusema chochote..Nilichanganyikiwa ghafla.Mtu ambaye sekunde chache zilizopita tumekuwa tukiongea vizuri na kucheka lakini ghafla hawezi kuongea tena.Haya yalikuwa ni mambo ya ajabu sana kunitokea.Sikujua Clara amepatwa na ugonjwa gani uliomtokea ghafla namna ile.
Watu waliokuwa karibu wakanisaidia kumbeba Clara na kumuweka pembeni.Bado kichwa changu kilikuwa kizito kuamini kilichotokea.Ni
lihisi ni kama mchezo wa kuigiza lakini kadiri dakika zilivyokuwa zikisonga ndivyo nilivyojikuta nikilazimika kuamini kwamba Clara alikuwa amepatwa na ugonjwa wa ghafla ambao sikufahamu ni ugonjwa gani.Pamoja na ujasiri wangu wote niliokuwa nao nilijikuta nikitetemeka kila nilipomuona Clara na hali aliyokuwa nayo.Macho yalikuwa yamefumba,hakuweza hata kufumbua jicho.Mwili wake haukuweza hata kutikisika.Machozi ya uchungu yakanitiririka.Wanaume wawili wa makamo ambao nao walikuwa ni wasafiri wakanivuta pembeni baada ya kuiona hali nilioyokuwa nayo.
? Jipe moyo ndugu yangu..Mungu atakusaidia..? akasema mmoja wao aliyekuwa amevaa suti nyeusi..
? Tatizo hasa la mwenzio ni nini? Akauliza mwingine aliyekuwa amekaa kushoto kwangu..Nikajikaza na kusema
? Sifahamu tatizo ni nini ..imetokea ghafla tu akapatwa na ugonjwa ule..? nikajibu kwa ufupi.Tayari uongozi wa pale uwanjani ukataarifiwa kuhusiana na kilichokuwa kimetokea na kwa haraka likatolewa gari kwa ajili ya kumkimbiza Clara katika hospitali ya Rufaa ya KCMC.Kwa kasi ya aina yake wahudumu wa pale uwanjani wakampakia Clara katika gari na mimi nikaingia ndani ya gari lile kisha tukaondoka uwanjani pale kwa kasi kubwa.
Kila nilipokuwa namuangalia Clara nilishindwa kujizuia kutokwa na machozi.Sipati neno ambalo linaweza kuelezea uchungu niliokuwa nao kwa wakati ule.Rangi ya ngozi ya Clara ikaanza kubadilika na kuwa na weusi weusi..nikazidi kuogopa.Nawashukuru watu niliokuwa nao mle garini walijitahidi kwa kila namna walivyoweza kunipa moyo ingawa hata nao nyuso zao zilionyesha mstuko na uoga wa dhahiri.
? Ouh Clara..nini kimekupata malaika wangu?.. Nilisema kwa uchungu nilipomtazama Clara akiwa amelala mle ndani ya gari hajitambui.Nili
ogopa sana kwa hali aliyokuwa nayo. Gari ilikuwa inakwenda kwa mwendo mkali sana lakini niliona kama inachelewa kufika hospitali ili Clara aanze kupatiwa matibabu.
Hatimaye tukawasili katika hospitali ya rufaa ya KCMC mjini Moshi na kwa haraka wauguzi wakampokea mgonjwa na kuanza kumshughulikia mara moja. Sampuli za damu na vipimo vingine vikachukuliwa na kupelekwa maabara kwa uchunguzi.
Nilitoa malezo mafupi kwa madaktari kuhusiana na jinsi ugonjwa ule wa Clara ulivyoanza halafu wakaniomba nikasubiri nje ili waendelee na uchunguzi wao.Niliwaomba madaktari wale wafanye kila linalowezekana ili kuokoa maisha ya Clara kwani hali aliyokuwa nayo ilikuwa inaogopesha mno.Miguu haikuwa na nguvu nikatafuta sehemu nikakaa.Bado kichwa changu kilikuwa na mawazo mengi sana juu ya kilichotokea.Ilikuwa ni kama ndoto ya mchana na ilikuwa vigumu sana kuamini kilichotokea.Ni
livuta picha ya kuanzia asubuhi tulipokuwa tunajiandaa kwa safari hii ambayo Clara hakutaka kuniambia tunaelekea wapi ingawa tiketi zetu zilionyesha kwamba tulikuwa tunaelekea Dar es salaam.Nikakumbuka tulivyoliacha jiji la Arusha nikiwa na matumaini kwamba nimeyaacha nyuma matatizo yote yaliyotokea kati yangu na Emmy.Sikutarajia kurejea tena Arusha.Niliamini kwamba ninakwenda kuanza maisha mapya nikiwa na malaika wangu Clara.Nilikumbuka tulivyoagana na rafiki yangu Beka pale uwanja wa ndege naye akarejea Arusha na gari langu.Nilimuahidi kuwa nikifika huko tunakokwenda ningemtaarifu kwa simu.Nikakumbuka pia tulivyokuwa tukipiga hatua kuelekea katika ndege na mara kumbu kumbu ambayo mpaka leo nikiikumbuka huwa inaniliza ikanijia kichwani. Ilikuwa ni kama ninatazama filamu.Clara alikuwa tayari ameinua mguu wake ili akanyage ngazi za ndege lakini hakuweza kufanya hivyo kwani alianguka ghafla na hakuweza kuongea tena.machopzi yakaanza kunitiririka tena.Nikafuta machozi nikachukua simu yangu na kumtaarifu rafiki yangu Beka kilichokuwa kimetokea.Hakuamini hata kidogo na alidhani ninamtania.Nili
pomuhakikishia kwamba haukuwa utani aliamini na kunitaarifu kwamba tayari anaanza safari ya kuja Moshi kuungana nami katika wakati ule mgumu.Baada ya kuongea na Beka nikampigia simu baba mkwe na kumtaarifu kilichotokea halikadhalika naye akanitaarifu kwamba yuko njiani anakuna Moshi.Nikamtaar
ifu pia na Chris ambaye tayari tumekwisha maliza tofauti zetu . Kila mmoja niliyemtaarifu alistuka mno .hakuna aliyeamini moja kwa moja.
Nikiwa bado nimekaa pale nje nikiwasiliana na watu mbali mbali kuhusiana na kilichotokea,ni
kaitwa katika chumba cha daktari.Haraka haraka nikaingia na kuketi kitini.daktari akanitazama kisha akasema
? Wayne tumemfanyia uchunguzi mgonjwa wako na tumegundua kwamba mgonjwa wako amepatwa na ugonjwa wa kupooza??
? What ? ..Unasema ??......Nikauliza kwa mshangao nikiwa nimesimama na macho kunitoka.Nilianza kusikia joto la ghafla.Hii ilikuwa ni taarifa ya kustusha sana.
? Dakatari tafadhali naomba unielezee vizuri kwa ufasaha ili nikuelewe.Umesema Clara anaumwa nini? Nikauliza tena nikiwa bado nimesimama.
Kabla hajaendelea kunipa taarifa kuhusiana na ugonjwa wa Clara akaniomba niketi chini..
? wayne mgonjwa wako amepatwa na ugonjwa wa kupooza upande mmoja wa kulia.?
? Ouh my God !! ..? Nikasema kwa sauti kubwa mikono yangu ikiwa kichwani.Daktari akanitazama na kusema
? Tulidhani labda tatizo hili limetokana na shinikizo la damu lakini kwa Clara kila kitu kiko katika hali ya kawaida.Vipimo vyote vinaonyesha hakuna tatizo.Bado tunataka kundelea kufanya uchunguzi zaidi ili tuweze kufahamu nini chanzo cha ugonjwa huu.Hata sisi imetushangaza kidogo? akasema Daktari kisha akanyamaza akanitazama na kuendelea.
? Ugonjwa huu umekuwa ukiwapata watu wengi kwa siku za karibuni .Lakini kwa upande wa Clara hali ni tofauti kidogo hivyo itatulazimu tufanye uchunguzi wa kina tujue nini chanzo cha tatizo hili Kwa sasa kuna kipimo kimoja ambacho tunahitaji kukifanya lakini kwa bahati mbaya mashine yetu imeharibika kwa hiyo itakulazimu uende jijini arusha kwa ajili ya kipimo cha CT Scan.? Akasema daktari..
? Daktari naomba uniambie tafadhali..Clara atapona ? Ataweza kutembea tena kama zamani? Nikauliza maswali mfululizo.Daktari akanitazama na kusema
? Wayne usiwe na hofu ,mgonjwa atapona ingawa siwezi kukwambia lini anaweza akapata nafuu.Tiba kubwa ya ugonjwa huu ni mazoezi .Baada ya kujiridhisha na vipimo vyote kwamba hakuna tatizo lingine basi tutaanza kumfanyisha mazoezi mara moja ? Akasema daktari..
Pamoja na maneno yale ya kutia moyo ya daktari,niliinama na kuzama katika mawazo mengi sana.Nilijaribu kutafakari lakini nikakosa majibu . Nilihisi kama dunia inaniadhibu..
Niliongozana na daktari kwenda kumuona Clara aliyekuwa amelazwa katika chumba maalum cha peke yake.
Nilidondosha machozi nilipomshuhudia mwanamke ambaye masaa machache yaliyopita alikuwa na uzuri usioelezka lakini kwa sasa hata sura yake ilikuwa imebadilika.Alikuwa amelala kitandani hajitambui,rangi ya ngozi yake ilianza kuwa na weusi na mdomo wake ulikuwa umepinda tofauti na ulivyokuwa awali.
Beka na Chris wakawasili kila mmoja na gari lake na kila mmoja alistuka mno kwa hali aliyokuwa nayo Clara.
? Wayne nina ushauri mmoja..? akasema Chris .
? Kwa nini tusimuhamishe Clara na kumpeleka jijini Arusha.Kwa sasa kumefunguliwa hospitali moja kubwa ya kimataifa inayotibu magonjwa kama huu uliompata Clara.Kuna mabingwa wa kutibu ugonjwa huu toka nchini Marekani? akashauri Chris.Kwa pamoja tukashauriana na kuafikiana kwamba tumuhamishe Clara na kumpeleka katika hospitali hiyo mpya aliyoshauri Chris.
***************************
" Mganga nakuahidi kurudi tena nikiwa na zawadi nzuri sana ambayo hutaamini." akasema Emmy akiwa na tabasamu pana sana.
" Emmy nimekuhakikishia kwamba huyu mwaanume lazima atarudi kwako na hataondoka tena.Safari hii atakupenda kupita maelezo.Atafanya kila utakalomuamuru alifanye." akasema mganga
" Sipati neno la kukushukuru mganga..lakini utaona mwenyewe zawadi nitakayokuletea " akasema Emmy.Mganga akatoka kidogo na baada ya muda akarejea akiwa na kibuyu chenye dawa.
" Emmy ninakupa dawa hii.Hii ni dawa yenye nguvu sana na unatakiwa uipake mwilini pale tu unapokwenda kuonana na Wayne.Kwa sasa unatakiwa umtafute kwa udi na uvumba hadi umuone lakini usijaribu kumpigia simu.Unatakiwa umstukize .Wakati unakwenda kuonana naye unatakiwa ujipake dawa hii pekee na usichanganye na mafuta ya aina yoyote ile.Hilo ndilo sharti pekee la dawa hii.Ninakuhakikishia kwamba Wayne akikuona tu atastuka mno na dakika hiyo hiyo atakuomba msamaha na mtarudiana tena..." akasema mzee mtuguru na kisha wakaagana na Emmy akaanza safari ya kurejea Arusha.
" Wayne huwezi kunikimbia hata kidogo..wewe ni wangu pekee na siku zote utakuwa wangu..Hahahahaaa namuonea huruma huyo mwanamitindo wako..kwisha kazi yake.Sasa tuone hayo maringo na mikogo yake kama vitakuwepo tena.Nilimuonya asicheze na mali za watu lakini hakusikia.Hahahaaa..ukiona vimeng'aa ujue vimeng;arishwa." akawaza Emmy akiwa katika gari akirejea jijini Arusha.Alikuwa na furaha isiyo kifani nantabasamu halikukauka usoni mwake.
" Japokuwa bado nina majonzi ya kufiwa na mwanangu Baraka lakini ninafuraha kwa upande mwingine kwa sababu ninakwenda tena kurudiana na Wayne.Mimi ni mwanamke wa shoka nimempigania Wayne na mpaka sasa nimefanikiwa kumrejesha tena mikononi mwangu.Safari hii habanduki na hata hao wanga waliokuwa wananiroga ili nigombane na Wayne kwa sasa hawaniwezi tena.Kwa tiba niliyopewa mimi ni kisiki cha mpingo.Hakuna atakayeniweza kwa sasa.Nimejaa kinga kila mahala." akaendelea kuwaza Emmy.
" Kuna kitu nimekumbuka.Sheila alinidokeza kwamba James anaweza akarejea muda wowote katika wiki ijayo.Sijui itakuwaje akisikia kwamba mwanae Baraka amefariki dunia.Ah ! hilo halinihusu kwa sasa akili yangu yote ni kwa Wayne.Baada ya kumrejesha Wayne kwangu ndiyo nitaanza kushughulika na James.Nitamuweka sawa na atanielewa japokuwa itamuumiza sana kwa sababu hakuwahi kumuona mwanae kwani alipoondoka kwenda masomoni Urusi aliniacha nikiwa na mimba changa kabisa na toka wakati ule hajawahi kurejea tena.Ataumia lakini hakuna namna ya kufanya kumrejesha Baraka.Inauma sana lakini nimefanya haya yote kwa ajili ya kulipigania penzi langu.Safari hii ninataka nipate mtoto na Wayne.Nilifanya makosa makubwa sana kuzaa nje ya ndoa.Laiti kama ningezaa na Wayne haya yote yasingenikuta.Sijielewi ni kwa nini sikuwa naridhika na mume wangu hadi nikawa natoka na kwenda kubadilisha wanaume kama nguo .Wayne alinipa kila nilichokihitaji lakini bado nilitoka nje ya ndoa.Lazima nilikuwa nimerogwa.Safari hii watanikoma.." akawaza Emmy
*********************
Emmy alikuwa akiendesha gari lake kwa kasi kubwa kuwahi jijini Arusha.Uso wake haukukaukiwa na tabasamu .
" Ngoja nimpigie simu Sheila simu nimtaarifu juu ya mambo yanavyokwenda japokuwa alikimbia na kuniacha peke yangu." akawaza Emmy kisha akapunguza mwendo wa gari akachukua simu na kuzitafuta namba za simu za Sheila rafiki yake mkubwa akampigia.
" Halo Emmy, niambie shoga yangu" akasema Sheila baada ya kupokea simu ya Emmy
" Sheila mambo yanakwenda vizuri sana" akajibu Emmy huku akitabasamu
" Kivipi Emmy? akauliza Sheila ambaye sauti yake ilionekana dhahiri hakuwa akiyafurahia maongezi yale na Emmy
" Sheila yule mwanamitindo wa Wayne kwisha habari yake."
" Kwisha habari yake ! Mbona sikuelewi Emmy una maanisha nini ? akauliza Sheila
" Tayari nimekwisha mdondosha.Hatainuka tena" akajibu Emmy huku akicheka kicheko cha chini chini.Kikapita kimya cha sekunde kadhaa
" Hallo Sheila upo ." akaita Emmy baada ya kimya kile cha ghafla.
" Nipo Emmy..Nimestuka sana kwa jambo uliloniambia.Ina maana amekufa yule mwanamitindo? akauliza Sheila
" Hapana sijamuua japokuwa nilikuwa na nafasi hiyo. Nilichokifanya ni kwamba nimempa ulemavu wa kudumu na hatainuka tena katika maisha yake.Hivi ninavyokwambia amepelekwa hospitali na hataweza kuinuka wala kutembea tena.Amepooza mwili.Hili ni fundisho kwake kuvamia mabwana wa watu" akasema Emmy.Sheila akavuta pumzi ndefu
" Sheila niko njiani ninarudi.Tutaongea mengi nikisha fika.Bado kuna kazi ninataka unisaidie "
" Nikusaidie tena?.Kuna kazi unataka nikusaidie? .Sheila akauliza kwa mshangao.
" Ndiyo ..mbona umestuka?
" Lazima nistuke Emmy .Wewe ni rafiki yangu wa muda mrefu na lazima nikueleze ukweli.Kwa sasa unatakiwa utulie Emmy.Vitendo unavyoendelea kuvifanya si vya kiungwana na havitakupeleka popote. Nakwambia hivyo kama rafiki yako na mtu ninayekupenda . Nimekwisha ona mwisho wa watu waliojihusisha na masuala hayo ya ushirikina .Siku zote mwisho wao huwa si mzuri hata kidogo.Angalia shoga yangu ni hivi majuzi tu umempoteza mwanao Baraka.Hata wiki moja haijapita Clara naye anapatwa na matatizo. Mpaka lini Emmy utaendelea kuwatesa watu? Hadi lini utaendelea kumtesa Wayne? Clara unayemtesa kitandani amekukosea kitu gani? Watu wengi wanazidi kuteseka kwa sababu yako Emmy. Tafadhali hebu achana na hayo mambo ya kishirikina.Muache Wayne aendelee na maisha yake.Ulishindwa kumtunza na kwa sasa muache afurahie maisha mengine aliyoyanza.Mtegemee Mungu na kama ikimpendeza kumrudisha Wayne kwako atafanya hivyo lakini si kwa kuwategemea waganga wa kienyeji..Emm................" Kabla Sheila hajaendelea Emmy ambaye uso wake ulikwisha jikunja kwa hasira kutokana na maneno ya shoga yake akainglia kati.
" Sheila unaongea maneno gani hayo? Mbona sikuelewi ? Wewe ndiye wa kuniambia maneno kama hayo leo ..?akafoka Emmy.
" Emmy ngoja nimalizie kile ninachotaka kukwambia...." akasema Sheila.Emmy akapunguza mwendo wa gari na kuliegesha kandoni mwa bara bara.
" Emmy napenda ufahamu kwamba mimi sikukifurahia kabisa kitebdo cha kunishirikisha katika masuala yako ya kishirikina.Wazazi wangu hawakunikuza katika misingi ya kuamini mambo kama hayo.Kitendo cha kunipeleka kwa yule mganga na kusababisha akanifanyia kitendo kama alichonifanyia bado kinaniuma mno.Sijui hata nifanye nini ili niweze kuifuta taswira ya kitendo kile katika akili yangu.Nimeumia sana Emmy na kwa maana hiyo naomba ufahamu kwamba urafiki wetu kwa sasa utakuwa na mipaka.Kama unataka urafiki wetu uendelee nakushauri achana kabisa na hayo mambo ya kishirikina ambayo hayana faida yoyote kwako.Ndoa yako umeivuruga wewe mwenyewe na kwa sasa umeanza kuhangaika kumtafuta mchawi wakati mchawi ni wewe mwenyewe.Nakushaur............
............."
" Bastard.....!!!" Emmy akakata simu kwa hasira na kuitupa kitini.
" Stupid girl !!..akasema kwa hasira.
" Sheila leo anathubutu kunitamkia maneno kama haya ? Bado siamini kama hata Sheila naye amenigeuka.Mimi nimekuwa mtu wake wa karibu na nimemsaidia katika mambo yake mengi ikiwa ni pamoja na kumkopesha hata mtaji wa kufungua saluni ile anayoringia kwa sasa halafu leo hii ananitamkia maneno kama haya .!!..Hapana siwezi kukubali kudharauliwa na paka kama Sheila. Anaishi mjini kwa sababu yangu mimi na hakupaswa hata kidogo kunidharau.Kwa kuwa naye ameamua kunidharau basi nitamjumuisha katika orodha ya maadui zangu.Nitamuonyesha kazi.Nitamfundisha adabu.Nadhani bado hajanifahamu vizuri" akawaza Emmy akiwa amefura kwa hasira.
" Ninaapa Sheila lazima alikimbie jiji.Nitayafany
a maisha yake magumu sana na lazima aje anipigie magoti..." akasema kwa sauti ya hasira kisha akawasha gari lake na kuendelea na safari ....
*************************
Wazo alilolitoa Chris la kumuhamishia Clara katika hospitali kubwa ya St Patrick inayomilikiwa na wamisionari lilikubaliwa hata na madaktari wa pale hospitali ya rufaa ya KCMC. Bila kupoteza muda taratibu zikaanza kufanyika na baada ya dakika chache kila kitu kikawa tayari Clara akapakiwa katika gari la wagonjwa na safari ya kuelekea Arusha ikaanza.Clara alikuwa amelala kitandani macho ameyafumba.Nilishindwa kujizuia kudondosha machozi niliposhuhudia akipakiwa garini.Chris aljitahidi kunisihi niwe mvumilivu katika wakati ule mgumu.Hata kama ungekuwa ni wewe mpenzi msomaji sina hakika kama ungeweza kuvumilia kumuona mtu unayempenda ambaye muda mfupi uliopita ulikuwa ukiongea naye na kucheka lakini ghafla anabadilika na haongei tena.
" Chris sijui nimemkosea nini Mungu .Ninaona ni kama ninaadhibiwa kila kukicha.Wakati nikiamini kwamba kwa sasa matatizo yote ninayaacha nyuma lakini linaibuka tena tatizo lingine. Sikutegemea kama lngetokea jambo kama hili kwa wakati kama huu.Clara alikuwa mzima wa afya na hakuwa na dalili zozote za ugonjwa .Sielewi ni kwa nini mambo haya yote yananitokea mimi tu..." nikamwambia Chris nikiwa katika gari lake tukielekea jijini Arusha tukimpeleka Clara katika hospitali ya St Patrick.
" Wayne naomba usife moyo ndugu yangu.Mungu wetu ni mwema sana na siku zote amekuwa akitusamehe makosa yetu hata tunapomkosea namna gani.Hii ni mitihani tu ya maisha ambayo hatuna budi kukabiliana nayo na inaweza ikampata mtu yeyote yule.Kitu cha msingi ni kukabiliana na ugonjwa huu wa Clara hadi apone.Nina uhakika katika hospitali ile ya St Patrick watamsaidia Clara na atapona kwa sababu kuna mama wa rafiki yangu naye alipatwa na matatizo kama haya ya Clara na akapelekwa pale lakini alipona na hadi sasa hivi huwezi kuamini kama alikuwa amepooza na hakuweza kuongea kwa muda wa miezi zaidi ya sita.Nina uhakika mkubwa sana hata Clara atapona na ataendelea na maisha yake kama kawaida." akasema Chris.
" Ninafikiria labda nimuhamishie nje ya nchi.." nikasema.
" Hapana Wayne.Bado ni mapema sana kufanya maamuzi hayo ya kumpeleka Clara nje ya nchi.Ugonjwa huu unaweza ukatibika hata hapa nchini.Kama litakuwa ni suala la kumpeleka nje ya nchi basi madaktari watatushauri hivyo lakini sina hakika kama kuna ulazima wa kumpeleka nje ya nchi" akasema Chris.
Sura ya Clara haikuweza kuondoka kichwani kwangu.Bado niliendelea kumuona akiwa katika tabasamu na kicheko chake kidogo
" masikini Clara..!!.." nikasema na kutoa kitambaa nikayafuta machozi ambayo nilishindwa kuyazuia kunitoka
" Its ok Wayne..usihuzunike sana .Clara atapona tu.Tunachopaswa kwa sasa ni kumuomba Mungu ampe uponaji wa haraka" akanipa moyo Chris.
" Chris hakuna ajuaye uchungu ninaousikia moyoni mwangu kwa sasa.Ninahisi ni kama moyo wangu unakatwa vipande vipande na kisu kikali sana.Ninasikia machungu ambayo hayaelezeki kwa maneno.Clara alikuwa ni maisha yangu.Clara alikuwa ni kila kitu kwangu. Clara amenifanya niyafurahie maisha japo kwa muda huu mfupi niliokaa naye. Clara ni mwanamke wa tofauti sana.Ana moyo wa ajabu na wa kipekee kabisa.Ana upendo wa dhati na wa kweli.Upendo wake unatoka ndani kabisa ya moyo wake.Kwangu mimi Clara namchukulia ni kama malaika anayeishi..Siku
tegema hata siku moja kama angeweza kupatwa na maradhi kama haya.She doesnt deserve this Ouh Clara.why you..!!!..."
Chris akanitazama kisha akaendelea kuendesha gari.
" pamoja na yote yaliyotokea bado upendo wangu kwa Clara hauwezi kupungua.Hata kama itamchukua maisha yake yote akiwa kitandani..nitampenda Clara hadi siku ninaingia kaburini." nikasema nikiwa nimeinama chini.Kikapita kimya cha sekunde kadhaa Chris akasema
" Wayne kuna kitu nakifikiria"...Nikainua kichwa na kumtazama
" Kitu gani Chris? nikauliza
" I'm sorry to say this but I have bad feelings" akasema Chris
" What feelings? nikauliza.Chris akakaa kimya kidogo halafu akasema
" Inawezakana Emmy akawa anahusika na ugonjwa huu wa Clara" akasema Chris.Maneno yale ya Chris yakaifanya akili yangu ianze kufunguka .Muda huu wote sikuwa nimemuwaza tena Emmy.Akili yangu haikuweza kumkumbuka tena.
" Kwa nini umewaza hivyo Chris.? nikauliza
" Nimewaza hivyo kwa sababu ninamfahamu Emmy ana roho ngumu sana.Kama ameweza kumuua mwanae wa kumzaa mwenyewe hatashindwa kufanya kitu kama hiki kwa Clara.Hayo ni mawazo yangu tu Wayne na sina uhakika kama yanaweza kuwa ya kweli ama la" akasema Chris.Nilikuwa ni kama mtu niliyepigwa na bumbuwazi.Nilizama ghafla katika mawazo mengi.
" Wayne unawaza nini? akauliza Chris
" Chris umenikumbusha jambo ambalo sikuwa nimelitilia maanani kabisa.Maelezo yako yamenifanya nipate picha fulani .Usiku ule alipofariki Baraka dakika chache tu kabla ya kupokea simu ya baba mkwe akinitaarifu kwamba Baraka amefariki dunia ,Clara alikurupuka ndotoni .Alikuwa anaweweseka na jasho jingi kumtoka.Nilimuuliza amepatwa na nini akaniambia kwamba ameota ndoto ya ajabu sana na ya kutisha.Nilimuuliza ni ndoto ya namna gani aliyoota lakini hakuwa tayari kuniambia.Aliniomba tupige magoti tusali na tumtegemee Mungu.Sikuelewa alimaanisha nini kwa maneno yale.Baada ya muda mfupi baba mkwe akanipigia simu na kunitaarifu kwamba Baraka amefariki dunia.Ni usiku ule ambao Emmy alikuwa amekwenda kwa mganga Tanga.Jana asubuhi Emmy hakuonekana tena msibani.Hakuna aliyefahamu alikuwa amekwenda wapi.Nimeanza kupata picha kwamba Emmy anahusika kwa kiasi kikubwa na ugonjwa huu wa Clara.Aliapa kwamba atayafanya maisha yangu magumu na hii ndiyo kazi anayoifanya.Kwa nini amtese Clara kiasi hiki? Amemkosea nini? Kama alikuwa na kisasi na mimi alitakiwa kunitesa mimi na si Clara asiye na kosa lolote lile.Niliyemuacha ni mimi na hakupaswa kabisa kumgusa Clara. Kama ni kweli ni yeye ndiye aliyemfanya Clara hivi I swear this time ameingia katika moto.Mungu atanisamehe kwa nitakachomfanyia hayawani huyu" nikasema huku nikiuma meno kwa hasira.Chris akanitazama na kusema
" Wayne,ninamfahamu Emmy ni mwanamke mwenye roho ngumu sana na siku zote huwa hakubali kushindwa kwa maana hiyo anaweza akafanya jambo lolote lile ili kukipata kile anachokitaka. Kama lengo lake lilikuwa ni kupamaba na wewe basi nina uhakika mkubwa kwamba anaweza akawa amemfanyia Clara vile ili kulipa kisasi kwako..." akasema Chris.
" I swear this time I'm going to kill her " nikasema kwa hasira
" Wayne usiseme hivyo na wala usiweke ahadi yoyote ya kulipiza kisasi.Bado hatuna uhakika kwamba ni yeye ndiye aliyefanya hivi.Hizi ni hisia zetu tu.Kama ni yeye ndiye aliyefanya kitendo hiki basi fahamu kwamba hizi ni kazi za shetani.Shetani si lolote mbele za Mungu.Tunachotakiwa kufanya sisi ni kumtegemea Mungu na atamponya Clara.Mungu ni muweza na hashindwi na lolote. Siku zote tunaambiwa tumtegemeze yeye pekee.Tumuombee Clara apone na tumuombee pia Emmy." akasema Chris.Nilishangaa kidogo baada ya kumsikia Chris akiongea maneno yale.Toka nimemfahamu Chris sikuwahi kumsikia akiongea maneno kama haya .
" Chris ! umeongea maneno ambayo yamenistua sana.Sikuwahi kukusikia hata mara moja ukiongea maneno kama haya uliyoyaongea leo." Chris akatabasamu kidogo kisha akasema
" Wayne sikuwa nimekuambia lakini mimi kwa sasa nimeamua kujiweka karibu zaidi na Mungu na kuachana na haya mambo ya kidunia.Nimamua kupokea wokovu.Baada ya kitendo kile kilichotokea baina yetu niliamua kupokea wokovu na kwa sasa mimi ni mtu mpya kabisa na ndiyo maana nina uhakika mkubwa kwamba Clara atapona kwa nguvu za Mungu" akasema Chris.Ni kweli Chris alikuwa amebadilika sana kuanzia tabia na maisha yake kwa ujumla.Bado niliendelea kumshangaa.
" Usisahangae Wayne.Nimeamua kuyabadili maisha yangu.Kwa sasa moyo wangu una furaha na amani.Ninayafurahia maisha yangu ya sasa.Nitamuomba baba askofu ambaye atakuwa anamfanyia maombi Clara kila siku .Kwa maombi yetu na jitihada za madaktari wetu Clara atakuwa mzima tena." akasema Chris.Maneno yale yakaanza kuniingia.Kwa wakati huu nilikuwa tayari kwa lolote lile ambalo lingeweza kumsaidia Clara aweze kupona.
Mara simu yangu ikaita alikuwa ni baba mkwe.Alitaka kufahamu hali ya mgonjwa ilivyokuwa inandelea.Yeye alikuwa katika maandalizi ya kuja Moshi nikamtaarifu kwamba tunamuhamishia Clara katika hospitali ya St Patrick jijini Arusha kwa hiyo hana haja ya kusafiri kuja Moshi.Baba mkwe akaniambia kwamba anatangulia hapo hospitali na tutamkuta pale.Nilifarijika sana kwa namna watu walivyoonyesha kuguswa na ugonjwa ule wa ghafla wa Clara.Tulikuwa nyuma ya gari la wagonjwa lililokuwa likienda kwa kasi kubwa huku likipiga king'ora kuashiria kwamba lilikuwa na mgonjwa ndani yake.
TUKUTANE SEHEMU IJAYO???????????..
 
BEYOND PAIN
SEHEMU YA 30
MTUNZI : PATRICK.CK
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
" Usisahangae Wayne.Nimeamua kuyabadili maisha yangu.Kwa sasa moyo wangu una furaha na amani.Ninayafurahia maisha yangu ya sasa.Nitamuomba baba askofu ambaye atakuwa anamfanyia maombi Clara kila siku .Kwa maombi yetu na jitihada za madaktari wetu Clara atakuwa mzima tena." akasema Chris.Maneno yale yakaanza kuniingia.Kwa wakati huu nilikuwa tayari kwa lolote lile ambalo lingeweza kumsaidia Clara aweze kupona.
Mara simu yangu ikaita alikuwa ni baba mkwe.Alitaka kufahamu hali ya mgonjwa ilivyokuwa inandelea.Yeye alikuwa katika maandalizi ya kuja Moshi nikamtaarifu kwamba tunamuhamishia Clara katika hospitali ya St Patrick jijini Arusha kwa hiyo hana haja ya kusafiri kuja Moshi.Baba mkwe akaniambia kwamba anatangulia hapo hospitali na tutamkuta pale.Nilifarijika sana kwa namna watu walivyoonyesha kuguswa na ugonjwa ule wa ghafla wa Clara.Tulikuwa nyuma ya gari la wagonjwa lililokuwa likienda kwa kasi kubwa huku likipiga king'ora kuashiria kwamba lilikuwa na mgonjwa ndani yake.
ENDELEA?????????..
Emmy aliwasili jijini Arusha .Alikuwa na hasira zisizo kifani kutokana na maneno aliyokuwa ameambiwa na rafiki yake kipenzi sheila.Moja kwa moja akaelekea nyumbani kwa wazazi wake.
" Ngoja kwanza nielekee nyumbani nikawasalimu kwa sababu nafahamu , lazima watakuwa walijiuliza maswali mengi sana kwa namna nilivyopotea ghafla.Niliondoka bila kumuaga mtu yeyote yule.Sitaki mambo yangu yajulikane kwa mtu yeyote .Nikishaweka mambo sawa pale nyumbani nielekee nyumbani kwangu nikapumzishe kichwa changu nitafakari namna nitakavyoanza mapambano upya.Kwa sasa ameongezeka adui mpya katika orodha ya maadui zangu.Sheila atanitambua.Sij
afurahishwa hata kidogo na kashfa alizonipa. Bado hajaufahamu upande wangu wa pili ukoje.Amefanya kosa moja kubwa sana katika maisha yake.Hakupaswa kunitamkia maneno ya kashfa namna ile.Ameniudhi sana na kwa hili sintamsamehe hata kidogo.Nitamuhamisha katika jiji hili." Akawaza Clara.
Alifika nyumbani kwao na kuingia ndani.Mama yake pamoja na baadhi ya ndugu jamaa na majirani ambao bado waliendelea kuomboleza msiba ule wa Baraka walikuwa wamekaa sebuleni kwa majonzi.Mara Emmy akaingia ndani na kuwafanya wote wastuke wakabaki wamemtumbulia macho kama wameona mzuka.Emmy akawasalimu kisha akapita akaenda katika chumba kingine.Wote wakabaki midomo wazi kwa tabia ile ya Emmy.Mtu ambaye amefiwa na mwanae lakini haonyeshi hali yoyote ya majonzi wala kujali .Mama yake Emmy akamfuata Emmy chumbani na kumkuta amekaa peke yake katika mkeka.Akasimama akamuangalia bila kusema chochote
" Mama mbona unaniangalia namna hiyo? akauliza Emmy.Mama yake akamsogelea na kuketi pembeni yake.
" Emmy mwanangu umepatwa na matatizo gani?
" kwa nini mama? akauliza emmy
" Kwani hujui matatizo uliyonayo mwanangu? akauliza kwa upole mama yake.
" mama mimi mbona niko sawa na wala sina tatizo lolote lile."
" Emmy mimi ni mama yako na ninakupenda sana .Sikutegemea kabisa kama ungekuja kuwa namna hii."
" Kwani nikoje mama? akauliza Emmy huku ameinama chini
" Emmy umekuwa ni mtu wa ajabu sana.Kila mtu anashindwa kukuelewa.Mwanao Baraka amefariki dunia na wewe hukujulikana uko wapi. Umeendekeza starehe na ukamsahau kabisa mwanao.Mpaka leo hii hujui na wala hujauliza nini kilimuua mwanao. Kwako wewe umechukulia hili ni jambo rahisi sana lakini kwa kweli Emmy sisi wazazi wako tumeumia mno.Umetuumiza mno Emmy.Kingine ambacho umetufanya tuumie zaidi na tushindwe kukuelewa ni kitendo cha kuondoka msibani bila kuaga siku moja tu baada ya mazishi ya mwanao.Emmy wewe ni binadamu wa namna gani? Kila mtu anakusema wewe.Hapa mtaani tumepata aibu ambayo haielezeki." akasema mama yake Emmy .Emmy hakujibu kitu alikuwa ameinama chini .
" Baba yuko wapi ? akauliza Emmy.Mama yake akamtazama na kusema
" Ina maana hujasikia kilichompata mwenzako?
" Mwenzangu nani?
" Clara.Yule mwanamke ambaye yuko na Wayne kwa sasa"...akasema mama yake Emmy na kumfanya Emmy acheke kicheko kikubwa
" Mama unanishangaza sana.Clara atakuwaje mwenzangu wakati yeye ndiye aliyemchukua mume wangu? Kwani amefanya nini huyo Clara? akauliza Emmy kana kwamba hajui kilichomtokea Clara
" Amepatwa na ugonjwa wa ghafla na amepelekwa hospitali.Inasemekana amepooza mwili ."
" Amepelekwa hospitali gani?
" Nasikia amepelekwa St Patrick Hospital."
Huku akitabasamu Emmy akasema
" Mama mimi siwezi kusema kwamba nimeumia au ninasikia uchungu wowote kwa sababu ni huyu huyu Clara ndiye aliyefanya mimi na Wayne tukatengana. Kwangu mimi nimefurahi sana kwani hii ndiyo dawa yake na akome kurukia mabwana wa watu.." akasema Emmy huku akicheka.Mama yake akamuangalia kwa macho makali
" Emmy huna haya hata kidogo ..wewe ndiye unaweza ukasimama na kuthubutu kutamka hayo maneno uliyoyatamka? Huna aibu hata kidogo.Umemfanyia Wayne mambo mabaya na ya aibu ambayo hayaelezeki .Baada ya mambo yote haya uliyomfanyia mwenzio unaweza kweli leo hii ukathubutu kusimama na kumlaumu Clara..Hayawani mkubwa wewe" akasema mama yake Emmy ambaye alianza kupandwa na hasira.
" Mama kosa langu nini hadi uniite hayawani? akauliza Emmy
" Ndiyo wewe ni sawa na hayawani.Umekuwa na roho ya kishetani hasa siku hizi.Hata mwanao amefar............." akasema mama yake kwa ukali lakini kabla hajaendelea zaidi Emmy akasimama.
" Stop it mother...Tafadhali naomba mniache mimi na maisha yangu. Msinifuate fuate .Tayari umekwisha niita mimi hayawani na ninaomba uniache na maisha yangu kama hayawani.Narudia tena mama nawaombeni mniache mimi na maisha yangu na sitaki mtu yeyote yule ayafuatilie maisha yangu.Hakuna hata mtu mmoja aliye upande wangu kwa hiyo niacheni niishi mwenyewe.Niacheni nilie mwenyewe..." akasema Emmy kwa ukali huku akiinuka na kuondoka kwa kasi mle chumbani akapanda gari lake na kuondoka zake .Mama yake akabaki chumbani akilia.
" Kuanzia sasa sitaki kabisa mtu yeyote ayafuatilie maisha yangu.Si wazazi wangu au mtu yeyote yule mwenye ruhusa na maisha yangu .Nitayaendesha maisha yangu kwa namna ninavyotaka mimi na si kwa namna wanavyotaka watu..." akasema Emmy akiwa amefura kwa hasira
" Kumbe Clara amepelekwa St Patrick hospital..hahahaaa..nitakwenda kumtembelea jioni ya leo.Kwanza ninaanza na Sheila halafu nitakwenda kumtembelea Clara jioni ..Mimi ndiyo Emmy bwana.hahahaaa.." Emmy akaongea mwenyewe huku akicheka wakati akikata kona ya kuingia nyumbani kwake.
Baada tu ya kuingia ndani mwake Emmy akajitupa sofani.
" Uuphh ! siku ilikuwa ndefu sana." akasema Emmy kisha akainuka akaelekea katika friji akachukua vipande vya barafu na chupa ya mvinyo akajimiminia katika glasi.
" Home sweet home ? akasema Emmy akiwa amekaa sofani
?This is my life now..Haya ndiyo maisha yangu mapya.Nyumba imepoa utadhani hakuna binadamu anayeishi humu.Lakini haya ni mambo ya mud amfupi tu kwa sababu muda si mrefu nina hakika Wayne atarejea na nyumba itakuwa na furaha tena. Nataka niwakate vilimi limi wale wote waliokuwa wakinicheka kwamba nimeachika. Najua wako wengi ambao walikuwa wakinicheka baada ya Wayne kuniacha.Baada ya Wayne kurudi kwangu watanikoma. Kwa kweli nilimfanyia Wayne vituko vingi sana na sikufahamu thamani yake kwa wakati ule lakini kwa sasa ndiyo ninaiona thamani yake.Japokuwa nina kila kitu .Ameniachia nyumba,gari na biashara zote lakini vyote hivi haviwezi kunipa furaha ya maisha yangu. Kwa mara ya kwanza ninaliona pengo la Wayne katika maisha yangu. Ninaapa nitatembea hadi mwisho wa dunia hadi nihakikishe Wayne anarudi katika nyumba hii.Lazima niishi naye tena.Sintaweza kumpata mwanaume mwenye moyo wa upendo na uvumilivu kama yeye." akawaza Emmy huku akipiga mafunda ya mvinyo mfululizo .
" Sina muda wa kupumzika ngoja kwanza nimuendee Sheila .Amenidharau kiasi ambacho siwezi kuvumilia.Mimi huwa sipendi kudharauriwa na hilo analifahamu fika.Alikosea sana kunitolea maneno yale ya kashfa." akawaza Emmy kisha akaingia bafuni kuoga.
" Baba na mama watakuwa wamechukia sana lakini watanisamehe kwa sasa.Niko katika kipindi kigumu mno cha kumpigania Wayne.Siwezi kukubali kupokonywa Wayne toka katika mikono yangu.Lazima nipambane kumrudisha kwangu.Ninafahamu katika mapambano haya mambo mengi yatatokea na moja wapo ni hili la kumpoteza mwanangu Baraka .Inaniuma kumtoa mwanangu sadaka kwa mizimu lakini sikuwa na namna nyingine ya kufanya .Yote haya nimeyafanya kwa ajili ya kumrudisha Wayne kwangu." akawaza Emmy akiwa bafuni amejilaza katika jakuzi.Mara akakumbuka kitu akastuka.
" Nimemuwaza Baraka nimekumbuka kuhusu baba yake.Sheila aliniambia kwamba James anaweza akarejea siku yoyote katika wiki ijayo.Sijui nitamueleza nini ili aweze kunielewa lakini hilo haliniumizi kichwa.Kitu pekee ambacho kinaniumiza kichwa kwa sasa ni kumrejesha Wayne kwangu.Hili la James ni suala dogo tu.Nitamuelewesha kwamba mwanae alifariki ghafla na atanielewa.Isitoshe hajawahi kumuona Baraka hata mara moja kwa hiyo haliwezi kuwa suala litakalomuumiza sana." akawaza Emmy kisha akatoka mle bafuni akavaa na kuondoka.
Breki ya kwanza iilkuwa katika saluni ya Sheila.Ni moja kati ya saluni kubwa na ya kisasa jijini Arusha na ambayo kila dakika huwa inajaa akina mama wanaokuja kujiremba.Emmy akashuka garini na moja kwa moja akaelekea ndani ya saluni ile.Hakuitika salamu ya mtu yeyote na moja kwa moja akamfuata Sheila aliyekuwa anamsuka nywele mteja.
" Nimekuja sasa.Naomba unieleze mbele ya macho yangu yale maneno yako uliyoniambia katika simu" akafoka Emmy bila hata salamu.Watu wote mle ndani ya Saluni wakapatwa na mshangao. Emmy na Sheila wamekuwa marafiki wakubwa kwa miaka mingi na hakuna mtu aliyetegemea kama siku moja wangefikia hatua hii.Sheila akamuacha yule mteja aliyekuwa anamsuka na kumgeukia Emmy.
" Emmy tafadhali kama unataka kuongea na mimi si wakati huu.NItafute kwa muda wako tuongee na si sasa hivi." akasema Sheila ambaye naye sura yake ilionyesha kuwa na hasira kwa ujio ule wa Emmy
" Sina muda wa kukutafuta.Nimegundua kwamba wewe ndiye mchawi wangu.Sikujua Sheila kwamba wewe ni mwanamke mbaya sana na kumbe kuachana kwangu na Wayne umefurahia sana.Hasidi mkubwa wewe" akafoka Emmy
" Mchawi ni wewe mwenyewe wala usinitake maneno.Umeshindwa kumtunza bwana kwa uzembe wako mwenyewe hadi akakuacha.Waache wenye kujua kulea wamchukue wamtunze.Nakwambai utatafuta mchawi hadi mwisho wa dunia lakini mchawi ni wewe mwenyewe.Acha kuumiza watoto wa watu ambaohawana makosa " akasema Sheila.Emmy akapandwa na hasira akataka kumvaa Sheila lakini watu waliokuwemo mle ndani wakawahi kumzuia.
" Sheila naomba unisikilize vizuri.Kuanzia sasa mimi na wewe urafiki wetu umekwisha .Nimekuweka katika kundi la maadui zangu.Nitapambana na wewe na nitakuonyesha kwamba mimi ndiye Sheila .Nakwambia ndani ya siku saba utakuwa umelihama hili jiji.Pili nataka mpaka kesho jioni uwe umenirudishia milioni saba zangu ama sivyo nitakuja kuchukua kila kitu humu saluni kwa sababu hii ndiyo inakupa kiburi na dharau .Narudia tena kesho unirejeshee pesa zangu.Ukisihindwa kuzirejesha mpaka kesho jioni utanitambua mimi ni nani" akafoka Emmy kisha akachukua mkoba wake akauvaa begani na kuanza kutoka kwa hasira.Shughuli ndani ya saluni hii zilikuwa zimesimama kwa muda watu wote wakiushuhudia ugomvi kati ya marafiki wawili wakubwa.Hakuna aliyeamini kama urafiki wa Emmy na Sheila ungefikia hatua hii.Walikuwa ni zaidi ya marafiki lakini kitendo hiki cha kurushiana maneno kilizua maswali mengi sana miongoni mwa watu walioufahamu vizuri urafiki wao.Sheila alikuwa kimya na hakutaka kuzungumza lolote licha ya baadhi ya shoga zake kutaka kufahamu sababu iliyopelekea yeye na Emmy kutoleana maneno makali namna ile hadi kutaka kupigana. Sheila hakutaka kuongea lolote kuhusiana na kilichotokea,akapanda gari lake na kuelekea nyumbani kwake.
"Ukweli niliompa Emmy umemuuma sana na sasa anataka mapambano na mimi.Mimi haniwezi bado ni msichana mdogo sana yule `kupambana na mimi.Anatakiwa ajipange vizuri kupambana na mimi. Anajivunia pesa alizonazo na uchawi anaotaka kujifunza.Mimi hanitishi kwa lolote lile na kama akihitaji kupambana na mimi nitapambana naye na atajuta kupambana na mimi.Mimi si kama hao akina Wayne ambao walikuwa wakimchekea kila alipokuwa akiwafanyia dharau." akawaza Sheila akiwa garini kuelekea nyumbani kwake.
" Najua lengo lake kwa sasa ni kutaka kuniaibisha kwa kunidai pesa alizonikopesha. N i pesa nyingi ambazo siwezi kumlipa kwa sasa.Amesema hadi kesho jioni niwe nimemlipa pesa zake na nisipofanya hivyo anaweza akaniaibisha kweli hayawani yule.Lazima nizitafute pesa hizo kwa kila jinsi leo hii ili niweze kumrejeshea Emmy kuinusuru saluni yangu .Saluni ile ndiyo pekee ninayoitegemea hapa mjini na lenbo lake ni kuifunga ili nikose kitu chochote cha kutegemea.Siwezi kukubali hilo litkee.Nitazitafuta pesa zake nimrejeshee.Lakini nani anayeweza kunipatia pesa hizo zote kwa muda huu mfupi? Sheila akazidi kuumiza kichwa.
" Mwanaharamu huyu amenipa wakati mgumu sana wa kuzitafuta pesa hizo.Lakini hakuna shaka nitazipata tu halafu nione atanitafutia wapi tena. Sikutegemea kama Emmy angefikia hatua hii aliyofika sasa hivi.Amemuua mwanae kwa ajili ya mwanaume ambaye hamtaki tena.Na siku ikitokea jamii ikajua kwamba amemuua mwanae kwa sababu ya kumrejesha Wayne kwake sijui watamfanya nini.James baba yake Baraka anarejea wiki ijayo sijui atafanya nini wapo ataufahamu ukweli kwamba Emmy alimtoa mwanae kafara kwa mizimu kwa ajili ya kurudiana na Wayne.Ninazifahamu siri nyingi za Emmy na ninaweza kuzitumia kumbomoa kabisa lakini sitaki kufanya hivyo .Kitu cha msingi ni kuachana naye kabisa na kumfuta katika orodha ya marafiki zangu.Kuna wazo nimelipata pengine linaweza kunisaidia kulitatua tatizo hili." akawaza Sheila.
" Chris anaweza akanisaidia kupata hizo pesa.Ninamfahamu Chris ni mtu pekee ambaye ananiamini na anaweza akanipatia kiasi hicho cha pesa kwa makubaliano ya kumrejeshea kidogo kidogo. Chris ni mtu mwelewa sana na isitoshe anamfahamu vizuri Emmy hivyo anaweza akanisaidia .Hata kama hatakuwa na fedha hizo anaweza akanidhamii mahala nikazipata.Ngoja nikifika nyumbani nimpigie simu" akawaza Sheila..
***********************
Clara alipokelewa katika hospitali ya St Patrick na kwa haraka akaanza kushughulikiwa.
Huduma zilizokuwa zikitolewa na madaktari na wauguzi wa hospitali hii zilitia moyo sana.Kwa muda swa masaa mawili sasa tulikuwa tumekaa katika sehemu za kupumzikia tukisubiri taarifa ya madaktari waliokuwa wakimshughulikia Clara.Hospitali pale nilikuwa na rafiki zangu Beka na Chris pamoja na baba mkwe.Hawa ndio waliokuwa watu wangu wa karibu sana katika kipindi hiki kigumu cha ugonjwa wa Clara.Nilikuwa nimeinama nikiwa na mawazo mengi sana.Sikuwa naongea chochote kile.Nilikuwa katika maumivu makali sana ya moyo.Nilikuwa nikitafakari kwa kina juu ya kilichotiokea lakini sikuweza kupata jibu la haraka haraka nini hatima ya maisha yangu na mambo yanayozidi kunikuta.Tukiwa tumeketi pale sofani katika sehemu hii ya kupumzikia Chris akapigiwa simu akainuka pale sofani na kuijtenga mbali nasi.Wakati akiongea na simu baba mkwe akanigeukia na kusema
" Wayne nakuomba usihuzunike sana kijana wangu.Hii ni mitihani ya maisha ambayo inamkuta kila mtu kwa hiyo nakuomba uwe mvumilivu na tuzidi kumuombea Clara.Mungu atamsaidia atapona.Mungu ni muweza wa yote na hashindwi na kitu chochote.Tumtegemee yeye pekee." akasema baba mkwe.
" Ahsante baba.Ninaamini Clara atapona lakini ninaumia sana kumuona akiwa katika hali ile. Kuna wakati ninawaza sijui ni kwa nini nilikutana naye.Endapo nisingekutana naye haya yote yasingemfika.Ninaona ni kama vile mimi ndiye nliyesababisha haya yote kumtokea" nikasema
" Usiseme hivyo Clara.Jambo kama hili lingeweza kumtokea mtu yeyote yule na wala usijilaumu kabisa kwa jambo kama hili kumfika Clara.Kitu cha msingi tumkazanie matibabu atapona na kurejea katika hali yake ya kawaida." akasema baba mkwe.
Chris akarejea na kujiunga nasi pale sofani.Usoni pake hakuonekana kawaida.Sikumjali nikaendelea na tafakari zangu.Saa kumi na moja za jioni tukaitwa katika ofisi ya daktari Daktari yule mzungu ambaye alikuwa akifahamu Kiswahili kidogo alitutaarifu kwamba wamemchunguza Clara na wamegundua kuna ufa katika fuvu la kichwa na tayari matibabu yake yamekwisha anza mara moja.Alitusihi tuwe wavumilivu kwa wakati huu ambao Clara ameanza kupatiwa matibabu.Alitue
leza mambo mengi kuhusiana na ugonjwa ule na kutupa moyo kwamba Clara atapona na wala hakuna haja ya kuwa na wasi wasi.
Baada ya maelezo yale ya daktari alitusihi tukapumzike kwani pale hospitali mgonjwa wetu atapata kila aina ya huduma inayotakiwa. Kabla hatujaondoka nilimuomba daktari anipeleke nikamuone Clara.Daktari akaniongoza hadi katika chumba alichokuwa amelazwa Clara .Nilimuinamia pale kitandania alipokuwa amelala amefumba macho. Sura yake nzuri ilikuwa imebadilika sana.Nilidondosha machozi kwa uchungu niliousikia.
" I'm sorry Clara kwa mambo haya kukupata.Nitaendelea kukupenda hadi mwisho wa uhai wangu" nikasema kimoyomoyo halafu nikatoka mle chumbani.
" Wayne jipe moyo ndugu yangu.Clara atapona tu.." akasema Beka baada ya kuniona jinsi nilivyobadilika baada ya kutoka katika chumba cha Clara.
" Wayne nina wazo moja." akasema Chris.
" Sikushauri urejee tena hotelini ulikokuwa unaishi.Nina nyumba kubwa na ninakuomba ukaishi pale kwangu kwa muda wote utakaohitaji.Wewe ni zaidi ya ndugu yangu nakuomba tukaishi wote nyumbani kwangu tafadhali." akasema Chris.Ulikuwa ni ushauri mzuri kwa sababu mpaka wakati huo nilikuwa sijapata nyumba ya kuishi.Nilikuwa nikiishi hotelini na Clara baada ya kumuachia Emmy nyumba yangu.Sikuwa na ubishi wowote kwa sababu tayari mimi na Chris tulikwisha zimaliza tofauti zetu.
Tuliwasili katika nyumba ya Chris maeneo ya Njiro.Chris alikuwa akishi na mdogo wake mmoja pamoja na mfanyakazi wa ndani.Nilikaribishwa ndani na kuonyeshwa chumba changu cha kulala.Nilimshukuru sana Chris kwa ukarimu wake huu mkubwa.Amekuwa ni msaada mkubwa sana kwangu kwa sasa.Baada ya kuoga niliitwa sebuleni kwa ajili ya chakula.Japokuwa sikuwa nikijisikia kula chochote niliamua kujilazimisha kula ili niweze kupata nguvu.Baada ya kula tulikaa sebuleni tukiangalia muziki wa Injili katika runinga kubwa iliyokuwamo mle sebuleni.Tukiwa bado sebuleni tukitazama muziki huku Chris akijaribu kunipa maneno ya faraja akinukuu vifungu vya biblia , mara akaingia mtumishi wa ndani.
" Kaka kuna mgeni wako" akasema yule mtumishi .
" Mkaribishe ndani" akasema Chris.
Nilishikwa na mshangao mkubwa baada ya kumuona Sheila akiingia pale mlangoni.Nilimt
olea macho makali nikimtazama kama ni yeye kweli au nimemfananisha.Alikuwa ni mwenyewe .Sheila naye alistuka mno aliponiona nikiwa pale nyumbani kwa Chris.Nadhani hakutegemea kunikuta pale kwa Chris mida kama ile.Tulibaki tunatazamana .Nilikabwa na fundo kubwa moyoni kwani huyu ndiye alikuwa mshirika mkubwa sana wa Emmy.
***********************
Saa kumi na mbili za jioni Emmy akasimamisha gari katika maegesho ya hospitali ya St Patrick.Akashuka na kuelekea moja kwa moja eneo la mapokezi.
? habari yako dada? akasema Emmy akimsalimu muuguzi aliyekuwapo mapokezi.
? Nzuri dada karibu sana ? akajibu yule muuguzi
? Samahani dada naomba kuuliza.? Akasema Emmy
? Bila samahani dada unaweza ukauliza? akajibu yule muuguzi
? Nina ndugu yangu mmoja ameletwa hapa mchana wa leo akitokea hospitali ya rufaa ya KCMC Moshi.Nimeambiwa amelazwa hapa.? Akasema Emmy
? Anaitwa nani mgonjwa wako?
? Anaitwa Clara.?
Muuguzi yule akatazama katika kompyuta yake na kulikuta jina la Clara.
? Clara ambaye amepatwa na matatizo ya kupooza mwili? Akauliza yule muuguzi.
? Ndiye huyo huyo.? Akajibu Emmy
? Amelazwa katika Private ward namba 4.? Akajibu yule muuguzi.
? Ninaweza kuruhusiwa kumuangalia .?
? Samahani dada yangu kwa muda huu huwa haturuhusu watu kuingia wodini kuwatazama wagonjwa.Mwisho wetu hapa huwa ni saa kumi na mbili za jioni? akasema yule muuguzi
? Ninaomba unisaidie dada yangu ili niweze walau kumuona ndugu yangu .Nimekuja na ndege toka Dr es salaam baada ya kupata taarifa zake.tafadhali naomba unisaidie nimuone tu japo hata kwa dakika moja.Nakuomba sana dada yangu.? Akaomba Emmy.Muuguzi yule akaingiwa na roho ya imani akaamua kumsaidia Emmy kwenda kumuona Clara.Muuguzi yule akamuomba muuguzi mwenzake amshikie kwa muda pale katika dawati lake wakati anampeleka Emmy kumuona Clara.
?Mgonjwa wako ni huyu? akasema yule muuguzi walipofika chumbani kwa Clara.
Moyo wa emmy ukapatwa na furaha ya ajabu baada ya kumuona Clara akiwa amelala pale kitandani hajitambui.
? Haya ndiyo malipo yako Clara kwa kupenda kuvamia waume za watu.Kama huu ndio mchezo wako basi safari hii uliingia sehemu mbaya sana.Na hili ni onyo kwa wengine wote ambao watajaribu kutaka kuwa na wayne.Wote nitawafanya hivi hivi.Wayne ni wangu na atabaki kuwa wangu milele.Nakusikitikia sana Clara kwa sababu utalala hapo kitandani kwa maisha yako yote yaliyobaki na utashangaa pale utakaposhudia Wayne akirudiana na mimi tena.Ona ulivyobadilika ghafla.Uzuri wako wote umepotea.Umekuwa ni kama kituko mbele za watu.Na huu ni mwanzo utateseka kwa maisha yako yote mshenzi wewe.Tena una bahati sana nilikuonea huruma ,nikaamua kukuacha hai.Wayne aliachana na mimi kwa sababu yako wewe.Wewe ndiye mchawi wa ndoa yangu lakini kwa sasa ujanja wako wote umekwisha .? akawaza Emmy wakati akimuangalia Clara aliyekuwa amelala pale kitandani.
? dada nadhani kwa leo inatosha.twende tuondoke kwani daktari akikukuta huku juu saa hizi nitakuwa katika matatizo makubwa? akasema yule muuguzi.
? nashukuru sana dada yangu kwa msaada wako? akasema Emmy kisha akaifungua pochi yake na kuchomoa bunda la noti nyekundu akampatia yule muuguzi kiasi cha shilingi elfu hamsini.
? Chukua hizi ni ahsante yangu kwa msaada wako? akasema Emmy na kumpatia yule dada pesa zile ambaye alibaki akishangaa asiamini macho yake..
? Ahsante sana ? akasema yule muuguzi huku akiufunga mlango wa chumba kile cha Clara.
? Hujaniambia jina lako unaitwa nani ? akauliza Emmy wakati wakishuka ngazi
? Ninaitwa Agnes ? akajibu yule muuguzi
? Nafurahi kukufahamu Agnes.mimi ninaitwa Emmy? akajibu Emmy
? hata mimi nafurahi kukufahamu Emmy ? akajibu Agnes.
? Agnes kama hutajali unaweza ukanipatia namba yako ya simu? Ninaweza kuwa nakupigia ili kujua maendeleo ya mgonjwa wangu. kwa sababu mimi ni mtu wa kusafiri safiri sana .?
Bila kusita Agnes akampa Emmy namba yake ya simu halafu naye akachukua ya Emmy.
? nashukuru sana kwa msaada wako Agnes.Tutazidi kuonana.Nitakuwa nikija mara nyingi tu kumjulia hali ndugu yangu? akasema Emmy
? Karibu sana dada Emmy.Mara nyingi huwa ninakuwepo zamu ya usiku.? Akajibu Agnes.
Emmy akaingia katika gari lake na kuondoka.
? Clara kwisha habari yake kwa sasa uwanja ni mpana kwangu kumrudisha Wayne.Namshukur
u sana mzee Mtuguru kwa msaada wake huu.Nitamtafutia zawadi kubwa sana yule mzee .Hizi tiba za asili zinasaidia mno lakini watu wanazidharau.Ingawa wakati mwingine zinaweza kukugharimu uhai wa mtu kama ilivyonigharimu mimi lakini zinasaidia sana.Kwa sasa ninahesabu masaa tu kabla ya Wayne hajarejea tena nyumbani kwangu.Ninachot
akiwa ni kuanza kufanya maandalizi kuanzia pale nyumbani. Itanibidi nipake nyumba rangi ,ikiwa ni pamoja na kubadilisha fenicha na kila kitu ndani ili Wayne atakaporejea tena nyumbani akute mabadiliko makubwa sana . ? akawaza Emmy huku akitabasamu usoni .
TUKUTANE SEHEMU IJAYO??
 
BEYOND PAIN
SEHEMU YA 31
MTUNZI 😛ATRICK.CK
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
Bila kusita Agnes akampa Emmy namba yake ya simu halafu naye akachukua ya Emmy.
? nashukuru sana kwa msaada wako Agnes.Tutazidi kuonana.Nitakuwa nikija mara nyingi tu kumjulia hali ndugu yangu? akasema Emmy
? Karibu sana dada Emmy.Mara nyingi huwa ninakuwepo zamu ya usiku.? Akajibu Agnes.
Emmy akaingia katika gari lake na kuondoka.
? Clara kwisha habari yake kwa sasa uwanja ni mpana kwangu kumrudisha Wayne.Namshukur
u sana mzee Mtuguru kwa msaada wake huu.Nitamtafutia zawadi kubwa sana yule mzee .Hizi tiba za asili zinasaidia mno lakini watu wanazidharau.Ingawa wakati mwingine zinaweza kukugharimu uhai wa mtu kama ilivyonigharimu mimi lakini zinasaidia sana.Kwa sasa ninahesabu masaa tu kabla ya Wayne hajarejea tena nyumbani kwangu.Ninachot
akiwa ni kuanza kufanya maandalizi kuanzia pale nyumbani. Itanibidi nipake nyumba rangi ,ikiwa ni pamoja na kubadilisha fenicha na kila kitu ndani ili Wayne atakaporejea tena nyumbani akute mabadiliko makubwa sana . ? akawaza Emmy huku akitabasamu usoni
ENDELEA???????????..
Nilipandwa na hasira kwa kumuona Sheila pale nyumbani kwa Chris.Nilisimama huku uso wangu ukiwa umejikunja kwa hasira.Midomo ilikuwa inanitetemeka.Huyu ndiye alikuwa rafiki mkubwa wa Emmy na ndiye alikwenda naye kwa mganga Mombo na kumuua Baraka.Chris aliniangalia mimi halafu akamuangalia na Sheila ambaye bado alikuwa amesimama akitetemeka alikosa neno la kusema.Midomo yake ilikuwa inamtetemeka.
?Sheila unatafuta nini huku? Emmy amekutuma uje unipeleleze? Amekutuma uje unimalize na mimi? Haya yote miliyoyafanya hayawatoshi hadi mnifuate huku? Nimewakosea nini hadi mnifanyie ukatili wa kiasi hiki? Clara amewakosea nini mpaka mumtese kiasi kile? Nikasema kwa ukali huku nikimuangalia Sheila kwa macho makali,akaogopa sana.Akiwa bado amesimama pale mlangoni ghafla kwa kasi ya ajabu nikamfuata na kumshika mkono nikamvuta kumtoa nje
? Toka ndani ya nyumba hii muuaji mkubwa wewe.Kamwambie huyo aliyekutuma kwamba siku zake zinahesabika na malipo ni hapa hapa duniani? nikasema kwa ukali.Chris akaniwahi na kunizuia
? Wayne ! tafadhali punguza hasira.? Akasema Chris
? siwezi kupunguza hasira Chris..Huyu ndiye mshirika mkubwa wa Emmy na ametumwa aje animalize.Tafadhali Chris niache nimshughulikie.Wamemuua Baraka ,na sasa wanamtesa Clara ambaye hana kosa lolote na kama haitoshi bado wananifuata hadi huku..? nikasema kwa ukali
?Wayne nakuomba ndugu yangu punguza hasira na tumsikilize Sheila amekuja kutafuta nini.? Akasema Chris huku akimshika mkono Sheila na kumuingiza ndani.Alikuwa analia.Nilitamani kumshushia kipigo kitakatifu mwanamke Yule lakini nikaheshimu ushauri wa Chris kwamba tumsikilize Sheila amekuja kutafuta nini usiku ule.
? Sheila karibu sana.Habari za huko utokako? Akasema Chris .Sheila akafuta machozi na kusema kwa sauti ndogo
? Kwema?
? Nashukuru kusikia hivyo.Karibu sana? akasema Chris
? ahsante Chris?
?Sema kilichokuleta na uondoke hapa haraka sana.Una bahati hapa ni nyumbani kwa Chris .Ingekuwa ni nyumbani kwangu nakuapia ningekukata shingo.Nakuchukia sana Sheila wewe na shoga yako Emmy? nikasema na kumfanya Sheila aendelee kuangusha machozi.
? Hutaki kueleza alichokutuma muuaji mwenzako? Nikasema kwa ukali huku nikisimama kumuendea pale sofani
?Sijaja hapa kwa sababu ya Emmy na wala hajanituma chochote? akajibu Sheila baada ya kuona ninamuendea.
?Nini kimekuleta hapa basi kama Emmy hajakutuma? Nikauliza
? Nimekuja kwa ajili ya maongezi na Chris na sikutegemea kama nitakukuta huku? akasema Sheila.Nikarudi mahala pangu na kukaa
?Nakusikiliza Sheila.ulikuwa na shida gani nami? akauliza Chris
? Samahani Chris tunaweza tukaongea nje?
? Hapana tuongelee hapa hapa mbele ya Wayne.Una tatizo gani?
Huku akisita Sheila akasema
?Nimekuja ninahitaji msaada wako Chris?
? Msaada gani Sheila?
?Ninahitaji unikopeshe fedha?
? Shilingi ngapi unahitaji?
? Nahitaji shilingi millioni saba?
? Millioni saba? Mimi na Chris tukastuka kwa pamoja
? Ndiyo ninahitaji unikopeshe kiasi hicho cha fedha au hata kama huna basi nitafutie hata kwa marafiki zako na nitakurejeshea ndani ya kipindi kifupi?
? Dah ! hizo ni fedha nyingi sana Sheila..una zihitaji lini na kwa tatizo gani?
? Ni kweli ni fedha nyingi lakini ninakuahidi nitazirejesha ndani ya kipindi kifupi.Ninazihitaji kabla ya kesho jioni?
? Kabla ya kesho jioni? Hilo haliwezekani Sheila.fedha hizi ni nyingi na hakuna uwezekano wa kuzipata ndani ya kipindi kifupi namna hiyo.Inahitaji muda kuzitafuta? Akasema Chris.Sheila akaonyesha uso wa kukata tamaa kwa jibu lile
?naomba unisaidie Chris.Nina shida kubwa na ya haraka? akasema
? Una tatizo gani Sheila? Nikauliza.
? kweli Sheila hebu tueleze una tatizo gani ili tufahamu pengine kunaweza kuwa na namna bora zaidi ya kukusaidia kulitatua tatizo lako? akasema Chris.Sheila akajikaza na kusema
?Nimekorofishana na Emmy na amenitaka nimlipe pesa zake alizonikopesha kwa ajili ya kufungua ile saluni.Ameahidi kunidhalilisha kama mpaka kesho jioni sintakuwa nimempatia pesa zake zote? akasema Sheila.Nilishindwa kujizuia nikacheka
? Sheila huo uongo wako kamdanganye mtu mwingine na si mimi .Chris tafadhali usimsikilize huyu mwanamke.Kuna jambo lililomleta hapa na si hilo.Huyu hawezi hata siku moja kukorofishana na Emmy.Huyu ndiye mshauri wake mkuu na mambo yote haya ambayo Emmy amekuwa akiyafanya huyu ndiye mshauri wake? nikasema
? Ni kweli Wayne nimekosana na Emmy naomba mniamini.?
? Nini kimesababisha mkakorofishana? Akauliza Chris
?Kwanza kabisa naomba nikiri kwamba ni kweli kama anavyosema wayne kwamba mimi na Emmy tulikua marafiki wakubwa na kila mara Emmy alikuwa anakuja kuniomba ushauri lakini jambo moja ambalo nyote hamlifahamu ni kwamba sikuwa namkubalia Emmy katika masuala yote aliyokuja kuniambia lakini alikuwa mbishi na nyote mnamfahamu Emmy akiamua jambo hataki mtu mwingine amshauri visivyo?
? Usitudanganye Sheila.Wewe si uliambatana na Emmy kwenda kwa mganga Mombo na mkamuua Baraka? Nikauliza.Sheila akakaa kimya
? Mbona hujibu? Kama si kweli weka wazi? nikasema
?Ni kweli Emmy aliniomba niambatane naye kwa mganga kule Mombo? akasema Sheila
? Nini lilikuwa dhumuni la kwenda kule na kitu gani kilifanyika? Nikauliza
?Emmy alidai kwamba kuna mtu aliyekuwa anamroga na ndiyo maana ukaamua kuachana naye kwa hiyo alitaka kwenda kumfahamu mtu huyo.Tulifika pale na dawa ikafanyika usiku?? Sheila akasita
? Nini kikaendelea? Nikauliza
? Ndiyo kama hayo yaliyotokea.Tulipofika hapa tukaambiwa kwamba Baraka amefariki ghafla? akasema
?Unataka kututhibitishia kwamba hamkujua toka mkiwa kwa mganga kwamba Baraka amefariki dunia?
?Mimi nilikuja kufahamu baada ya kufika huku Arusha lakini Emmy alionekana kufahamu kwa sababu yeye ndiye aliyekuwa akifanyiwa dawa usiku ule na hata wakati wa msiba aliniambia kwamba hakujua kama Baraka alikuwa anatolewa kafara kwa mizimu kama malipo ya kukurudisha mikononi mwake.? Akasema Sheila na kwa hasira nikainuka.Chris akaniwahi na kuniomba niketi
?Jana alinitaka nimsindikize tena kwa mganga lakini nikakataa akaenda mwenyewe.Wakati akirudi akanipigia simu na kunitaarifu kwamba tayari amekwisha mmaliza Clara.Nilimweleza ukweli kwamba anachokifanya si kitu kizuri na kwamba aache kuwaumiza watu wasio na makosa.Kauli ile hakuipenda ndiyo maana akaamua kuja na kutaka kunidhalilisha.Kwa hivi saa urafiki wetu umekufa.wayne ninaomba msamaha sana kwa kushirikiana na Emmy.Najua tumekukosea sana na sijui nitafanya jambo gani ili uweze kunisamehe.? Akasema Sheila huku akitoa machozi.Nikamua
ngalia kwa macho makali na kusema
? Kitu kimoja tu ambacho unaweza ukafanya kitakachonifanya nikusamehe.Nataka Clara arudishwe katika hali yake ya kawaida.Hapaswi kuteseka bila kosa.Ukiweza kulifanya hilo nitakusamehe Sheila na nitajua kwamba ni kweli unajutia ulichokifanya? nikasema na Chris akageuka na kunitazama..Sheila akainama chini
? Unaweza ukafanya hivyo? Nikamuuliza
? Wayne aliyefanya mambo haya ni mganga wa kienyeji na mimi sina nguvu zozote za kuweza kutengua uchawi huu alioufanya.Ninachoweza kufanya mimi ni kwenda kumuomba Yule mganga aweze kumponya Clara na amrudishe katika hali yake ya kawaida? akasema Sheila
?Unapakumbuka mahala anakoishi huyo mganga? Nikauliza
?Ndiyo napakumbuka?
? Kesho asubuhi mimi na wewe tunaongozana hadi kwa mganga Mombo.Nataka nikaongee naye mimi mwenyewe na kama akishindwa kufanya ninavyotaka basi ama zake ama zangu? nikasema kwa hasira
? Wayne..!! akasema Chris
?Chris niache niende kwa huyo mganga siku ya kesho.Nataka akatengue kila kitu alichomfanyia Clara.Siko tayari kumuona akiendelea kuteseka namna ile bila kosa? nikasema huku machozi yakinilenga kila pale sura ya Clara iliponijia kichwani
?Wayne sikushauri uende huko kwa mganga.Hizi ni nguvu za giza na siku zote nguvu za mwovu si lolote mbele ya nguvu za Mungu.Tumtumaini Mungu pekee na atamponya Clara.Atazivunja vunja nguvu zote za giza na Clara atakuwa mzima tena.Nimekwisha ongea na baba askofu na ameniambia kwamba kuanzia kesho atakuwa akienda kumfanyia maombi Clara mchana na jioni.Tafadhali naomba tumuachie Mungu tatizo hili? akashauri Chris
? Chris najua kwa sasa wewe umeokoka na unamuamini Mungu na hata mimi ninamuamini Mungu lakini kwa hali aliyonayo Clara inanilazimu kumfuata huyo mganga na kumtaka atengue uchawi wote aliomroga Clara.Clara hawezi kuendelea kuteseka wakati mtu aliyemroga yupo na anajulikana.Kesho asubuhi ninamfuata huko huko Mombo? nikasema halafu kikapita kimya kifupi
? Chris kwa hiyo utanisaidia kuhusu ule msaada niliokuomba? Akauliza Sheila
?Nashinda kukupa jibu Sheila kwa sababu mambo yangu kifedha hayaniendei vizuri sasa hivi.Nadhani ungenipa muda wa kama siku mbili hivi ili nikutafuitie hizo pesa? akasema Chris
? Nitakukopesha mimi hizo fedha lakini mpaka baada ya kurejea toka kwa huyo mganga huko Mombo.? Nikasema
* * * *
Saa kumi na mbili za asubuhi tayari nilikwisha mpitia Sheila na tulikuwa njiani kuelekea kwa mganga baada ya kupita kwanza hospitali kwenda kujua hali ya Clara.Bado hali yake ilikuwa vile vile na hakukuwa na unafuu wowote.Nilimuelekeza Chris kwamba afanye mawasiliano na ofisi kuu ya Clara iliyopo afrika kusini na kuwataarifu kuhusiana na ugonjwa huu wa Clara.
Safari yetu ilikuwa ya kimya kimya .Nilikuwa na mawazo mengi sana kuhusiana na mustakabali mzima wa kinachoendelea.Niliwaza ni chuki gani aliyonayo Emmy kwangu kiasi cha kunifanyia mambo ya namna hii.Nilimpatia kila kitu alichokihitaji na sikumbuki kama kuna kitu ambacho aliwahi kutaka akakikosa.Kama hakuna kitu chochote kibaya nilichomfanyia kwa nini basi anifanyie haya anayoyafanya? Ni mambo ambayo inahitaji moyo wa kipekee kuyavumilia na ninamshukuru Mungu nimeyavumilia yote lakini kwa hili la kumuumiza Clara namna ile sintakubaliana nalo hata kidogo,ni jambo ambalo limeniumiza mno? nikawaza huku tukiendelea na safari.Mawazo yale yakanipelekea nikumbuke kwamba pembeni yangu alikuwa amekaa mshirika mkubwa wa Emmy katika mambo haya yote.Nikageuza shingo na kumtazama Sheila akagundua kwamba sikumtazama kwa jicho zuri akainamisha kichwa.
Tulfika Mombo na Sheila akaniongoza hadi tulipofika nyumbani kwa mganga.
? Ni hapa? akaema Sheila
? Una hakika?
? Ndiyo ni hapa? aaksema Sheila halafu tukashuka
? Hodi wenyewe ? nikabisha hodi lakini hakukuwa na mtu yeyote aliyeniitikia.hakukuwa na dalili zozote za mtu pale nyumbani.Milango yote ilikuwa imefungwa
? Sheila mbona hakuna mtu yeyote hapa nyumbani? Nikauliza
? Hata mimi nashangaa sana lakini hapa ndipo nyumbani kwa mganga ambaye amekuwa akimfanyia Emmy mambo yote.?
? Amekwenda wapi? Nikauliza
Siwezi kujua Wayne.Pengine anaweza kuwa amekwenda shambani au katika shughuli zake
? Tutamsubiri hadi atakaporejea.Hatutaondoka leo hii kabla huyo mganga hajarejea na leo hii lazima atamrudisha Clara katika hali yake ya kawaida ama sivyo ama zake ama zangu? nikasema na kukaa juu ya jiwe.Nilikuwa na hasira sana.
Sikutaka kuondoka pale nyumbani kwa mganga hadi atakaporejea.Niliamini hatakuwa ameenda mbali sana .Wakati tukiendelea kumsubiri nilizunguka nyuma ya nyuma ile ili niiyasome mazingira lakini sikuona kitu cha maana zaidi ya vyungu vingi na vibuyu na ngozi za wanyama.Nilirudi na kukaa juu ya jiwe pembeni ya Sheila.Nikainamisha kichwa.
Tukiwa tumekaa tunaendelea kumsubiri mganga arejee simu yangu ikaita.Alikuwa ni Chris.
? Hallow Chris? nikasema baada ya kupokea simu
? Habari za huko Wayne? Umeshafika?
? Tayari nimeshafika Chris lakini huyu mganga hayupo na siwezi kuondoka hapa bila kuonana naye.Ninamsubiri hadi atakaporejea. Maendeleo vipi?
?Niko hospitali na hakuna mabadiliko yoyote lakini kuna kitu ninataka kukufahamisha?
? Kitu gani Chris?
? tayari nimewasiliana na ofisi ya Clara kule afrika ya kusini na kuwafahamisha kuhusu ugonjwa wake.Wamenitaarifu kwamba tayari wamewasiliana na wazazi wa Clara walioko jijini Dar es salaam . Muda mfupi uliopita nimepokea simu toka kwa baba yake Clara akinitaarifu kwamba watawasili hapa Arusha na ndege leo saa tisa alasiri.?
? baba yake Clara anakuja? Nikastuka kidogo
? Ndiyo Wayne.Itakuwa vizuri kama ungekuwepo wakati watakapofika.?
? sasa tutafanya nini Chris? Mimi bado naendelea kumsubiri huyu mganga? nikasema
? Wayne ninachokushauri ni kuachana na huyo mganga na uanze safari ya kurudi ili uje uonane na wazazi wa Clara na kwa pamoja tuone namna tutakavyomsaidia mgonjwa? akasema Chris.Nilikaa kimya kwa sekunde kadhaa nikitafakari kisha nikasema
?Nimekuelewa Chris.Ninaanza safari ya kurudi.?
? Ok Wayne.Utanikuta hapa hospitali?
Baada ya kumaliza kuongea na Chris nikamgeukia Sheila aliyekuwa amejiinamia juu ya jiwe.
? Sheila twende turudi Arusha.?
? Kuna nini tena? Si ulisema tukae tumsubiri mganga?
? Hapana hatuwezi kuendelea kukaa hapa.Tunatakiwa kurejea Arusha mara moja.Baba yake Clara anakuja Arusha kwa hiyo natakiwa niwepo? nikasema huku nikielekea garini.Clara naye akainuka na kuja garini tukaanza safari ya kurudi.
Kichwa changu kilikuwa na mawazo mengi sana kuhusiana na nitakachowaeleza wazazi wa Clara kwani hadi matatizo yale yanamkuta mimi ndiye nilikuwa naye.
Tukiwa tumefika moshi mjini simu ya Sheila ikaita,akapokea na kuzungumza na mtu yule aliyempigia na baada ya kumaliza kuongea akanigeukia.
? James amekuja?
? james ?!! nikashangaa
? Ndiyo James.Humfahamu?
? hapana simfahamu kabisa.Ni nani huyo James?
Sheila akakaa kimya kidogo akafikiri na kusema
?Wayne naomba nikueleze ukweli
? Ukweli gani tena Sheila?
?Huyu mtu anayeitwa James ndiye baba mzazi wa Baraka?
Nilistushwa na taarifa ile ikanilazimu kupunguza mwendo wa gari na kuliegesha pembeni .
? baba mzazi wa Baraka? Nikauliza
? Ndiyo Wayne.James ndiye baba mzazi wa Baraka?
Nikamtazama Sheila kwa muda halafu akasema
? James na Emmy walianza urafiki wao zamani sana na katika mipango yao walipanga kwamba siku moja wafunge ndoa.Emmy aliolewa na wewe bila James kujua kwa sababu ni mtu wa kusafiri safiri kwenda nje ya nchi.Hata wakati akiwa tayari ameolewa na wewe bado aliendelea kutembea na James bila ya yeye kufahau kwamba alikuwa tayari ameolewa.Ilitokea James akasema kwamba anakwenda kusoma nje ya nchi na alipoondoka alimuacha Emmy akiwa na mimba changa kabisa ambayo alikudanganya kwamba ni ya kwako.?
Jasho lilianza kunitoka kwa taarifa ile.Kumbu kumbu za nyuma zikaanza kunirudia .
?James alinipigia simu wiki mbili zilizopita na kunitaarifu kwamba anarejea nchini na hii simu aliyonipigia alikuwa ananitaarifu kwamba tayari amekwisha rejea na kwamba anahitaji kuonana nami usiku wa leo.Amefikia hotelini na hataki mtu mwingine yeyote afahamu kama amewasili? akasema Sheila.
? Huyo James anafahamu kwamba mwanae Baraka amefariki dunia?
? Hana taarifa hizo na hajui kama alimuacha Emmy akiwa na mimba changa?
? Too bad? nikasema halafu nikawasha gari na kuendelea na safari
? Emmy ni shetani.Kwa nini nilimpenda mwanamke kama yule asiyekuwa na hata chembe ya ubinadamu? Kwa mambo aliyonitendea malipo yake yatakuwa hapa hapa duniani.? Nikawaza na sikutaka kichwa changu kijishughulishe sana na Emmy kwa wakati ule akili yangu yote niliielekeza kwa Clara.Sheila alikuwa kimya akitafakari na kuna wakati nilimuona kama anatabasamu
? Unawaza nini Sheila? Nikauliza
? Wayne Its pay back time..Emmy alidhani anauwezo wa kupambana nami basi leo ndio mwisho wake.Ninakwenda kumbomoa kwa James.Nitamueleza madhambi yake yote .Safari hii amelamba galasa.Nitamueleza james kila kitu ninachokifahamu kuhusu yeye.? Akasema Sheila
? Fanya ufanyavyo Sheila lakini mimi sitaki kabisa kumsikia Emmy masikioni wangu..Mambo aliyonitenda ni makubwa na yanasikitisha.Sitaki tena kusikia chochote .Imetosha ? nikasema
Tuliendelea na safari yetu hadi tulipofika Arusha mjini,nikampeleka Sheila nyumbani kwake halafu nikaelekea hospitali.Mida hiyo ilipata saa moja za jioni na tayari giza lilikwisha ingia.Nilihisi uchovu mkubwa kwa safari ile ndefu isiyokuwa na manufaa yoyote.Pamoja na uchovu ule lakini ilikuwa ni lazima kufika hospitali kumuona Clara na kuonana na wazazi wake.
Nilimpigia simu Chris na kumfahamisha kwamba tayari nimekwisha rejea na kumuuliza kama alikuwapo hospitali,akasema kwamba alikuwa na wazazi wa Clara akiwasaidia kutafuta chumba hotelini kwa ajili kulala usiku huo .Baada ya kuongea naye nikaelekea moja kwa moja hospitali .Nilifika hospitali na kuonana na madaktari waliokuwa wanamshughulikia Clara.Bado hali yake haikuwa ya kuridhisha japokuwa madkatari walinipa moyo na kuniambia kwamba anaendelea vizuri .Sikutaka kumuona akiwa katika hali ile ya kutoweza kufanya chochote.hakuweza kula , kuongea wala kunyanyuka .Niliumia sana kwa hali ile.Nilikaa pembeni ya kitanda chake nikimuangalai huku machozi yakinitoka
? Kwa nini uteseke namna hii Clara? Umekosa nini kiasi cha kumfanya Emmy akutese kiasi hiki? Nikasema kwa sauti ndogo huku machozi yakinitoka.
**********************
Meza ilikuwa imechafuliwa na chupa za pombe na nyama za kuku.Wanawake watatu walikuwa wameizunguka meza ile wakifurahi kwa kunywa pombe na kucheza muziki.
? Kunyweni shoga zangu.Kunyweni watu wangu .Achaneni na yule shetani Sheila.Anadhani anaweza akapambana na mimi ? Nawaambia nitamuonyesha mimi ni nani.Nitamuonyesha kati yangu naye nani aliwahi kufika mjini.Sheila huyu ambaye ni mimi ndiye niliyemfanya akaonekana mtu kati ya watu lakini anakuja na kutaka kunipanda kichwani.Sintakubali hata kidogo.Na kwa nyie wote yeyote ambaye anaona kwamba hawezi kuendana na mimi ni bora akaondoka zake mapema na asisubiri hadi tukorofishane.Mimi nikikorofishana na mtu huwa nina kisasi kibaya sana.Mtaona kwa Sheila nataka nimuhamishe mji huu.tena ngoja nimkumbushe kuhusu pesa zangu.? Emmy akawaambia shoga zake wawili aliokuwa nao pale sebuleni wakinywa pombe.Akachukua simu ake na kumpigia Sheila
? Hallo we mwanamke umeshazipata pesa zangu? Akauliza Emmy kwa dharau kubwa
? Mbona unanisumbua kwa vihela vidogo kama hivi Emmy? Tayari ninayo pesa yako pita saluni kwangu kesho asubuhi uchukue vijisenti vyako? Sheila akajibu kwa dharau na kumfanya Emmy ahamaki.
? Bahati yako umezipata lakini bado nitaendelea kupambana nawe na ninakuhakikishia vita hii haitakwisha mpaka hapo utakapokuwa umeuhama huu mji? akasema Emmy kwa hasira na mara akasikia kuna simu nyingine inaingia.Akatazama ilitoka kwa nani ,simu ile ilitoka kwa Agnes yule muuguzi ambaye jana yake alimpatia kitita cha fedha kwa ajili ya kumruhusu aingie amuone Clara katika chumba alicholazwa.
? Agnes anataka nini? Ile kazi niliyomuachia tayari ameshaifanya? Akawaza Emmy halafu akaikata simu aliyokuwa amempigia Sheila akampigia Agnes
?Hallo Agnes habari yako?
? habari nzuri dada Emmy?
? Kuna habari gani hapo hospitali ? akauliza Emmy
? dada Emmy yule mtu ambaye ulisema nikufahamishe pindi akifika hapa tayari amefika na ameingia chumbani kwa Clara?
? Ouh good job Agnes.Nitakutafutia zawadi nzuri sana kwa kazi hii nzuri.Ninakuja hapo muda si mrefu? akasema Emmy na kukata simu.Uso wake ulichanua kwa tabasamu
? ladies endeleeni kula na kunywa.Kuna mahala ninataka kwenda mara moja.Nitarejea muda si mrefu? Emmy akawaambia wale mashoga zake aliokuwa nao pale sebuleni kisha akaelekea chumbani kwake.Akaoga haraka haraka na kuanza kujiandaa kwa ajili ya kutoka.Baada ya kuhakikisha kwamba amependeza vilivyo akajipaka dawa ambayo alipewa na mganga kwamba ajipake mwilini siku atakayokwenda kuonana na wayne.Ilikuwa ni dawa yenye harufu kali hivyo ikamlazimu ajipulizie na uturi mkali kupoteza harufu kali ya ile dawa.Dawa nyingine iliyokuwa katika pembe la ng?ombe akaiweka katika mkoba halafu akatoka na kuingia garini akaondoka zake.
? kama isingekuwa ni kwa ajili ya kumtaka wayne ,nisingethubutu kujipaka dawa hii yenye harufu kali na mbaya namna hii,lakini hata hivyo kwa ajili ya Wayne niko tayari kufanya kila linalowezekana .Nataka nimpate tena Wayne.Nitafanya kila ninaloweza na sintalala hadi nihakikishe Wayne amerudi kwangu tena.? Akawaza Emmy
**********************
Bado nilikuwa nimekaa pembeni ya kitanda cha Clara nikimtazama na machozi yakinitoka.Nili
kumbuka toka siku ya kwanza niliyokutana naye ,tukaanzisha urafiki na hatimaye tukawa wapenzi.Niliumia sana kwani tayari nilikuwa na ndoto nyingi na mrembo huyu aliyeingia moyoni mwangu kuliko mwanamke yeyote niliyewahi kukutana naye chini ya jua.Nilijiona ni kama mtu mwenye mkosi kutokana na namna maisha yangu yalivyokuwa yakikabiliwa na matatizo.Chuki yangu dhidi ya Emmy ikaongezeka.
? Bahati yake na yule mchawi kama ningemkuta leo sijui nini kingetokea.Ilikuwa ama zangu ama zake.? Nikawaza halafu nikamuinamia Clara na kumbusu
? Nakupenda sana Clara na nitafanya kila linalowezekana hadi upone na urejee hali yako ya kawaida? nikamwambia Clara huku machozi yakinitoka
? wewe ni mwanamke wa pekee kabisa kuwahi kutokea katika maisha yangu.Wewe ndiye maisha yangu na kila kitu changu.Ninakuahidi sintakuacha na nitafanya kila linalowezekana ili upone? nikasema na mara simu yangu ikaita.Alikuwa ni Chris.
? hallow Chris ? nikasema
? Wayne uko hapo hospitali?
?Ndiyo Chris niko hospitali? nikajibu
? Ninakuja na wazazi wa Clara.Naomba tukutane hapo chini kwa ajili ya maongezi.Wanahitaji kuongea nawe?
? sawa Chris mtanikuta pale chini nikiwasubiri? nikasema na kukata simu.Nikamuangalia tena Clara nikambusu na kutoka mle chumbani nikaanza kushuka ngazi kuelekea chini.baada ya kumaliza kushuka ngazi ghafla nikakutana na kitu kilichonistua mno na ambacho sikukitegemea kukuiona mahala pale.Nilikuwa natazamana na Emmy.Nilistuka sana nikadhani labda nilikuwa ndotoni lakini hapana ni kweli nilikuwa natazamana na Emmy ambaye ndiye mwanamke aliyefanya maisha yangu yakawa namna hii.Wote tulikuwa tumesimama tukitazamana.Kwa haraka haraka picha ya maisha yangu yote ya mateso na vitimbi toka kwa Emmy ikanijia.Nikajikuta nikipatwa na hasira za ajabu sana.
? Wayne..? akasema Emmy huku akitabasamu kwa uoga .Nadhani hata yeye aligundua kwamba nilikuwa nimekasirika kupita kiasi
?Emmy unatafuta nini huku? Nikasema kwa ukali
? wayne samahani sana....nimesikia kuhusu Clara na nikataka kuja kukupa pole kwa klichotokea..?
Kabla hajamaliza sentensi yake nikamrukia na kuanza kumshushia kipigo kikali.Nilimpiga kila mahala.Emmy akapiga kelele kubwa na watu wakaja pale kujua nini kinaendelea.Sikutaka mtu yeyote aniamue .Nilitaka niendelee kumshushia kipigo kikali mwanamke yule baradhuli.
?Nilikutafuta siku nyingi sana na leo nimekupata.Leo nitakufanya kitu kibaya sana Emmy.Nimekuachia kila kitu lakini bado unanifuata? nikasema huku nkiendelea kumshushia kipigo.Mara nikashikwa na mikono yenye nguvu .
? Stop that Wayne.Huoni kama unaweza ukaua? Alikuwa ni Chris.
? Chris niache nimmalizie huyu shetani.Amemfuata Clara mpaka hapa ,anataka ammalizie?? Nikasema kwa uchungu huku bado nikiwa nimeshikiliwa.Mwili ulikuwa unanichemka kwa hasira nilizokuwa nazo.Emmy alikuwa amelala chini akilia huku akivuja damu.Shati lake jeupe alilolivaa lililoa damu .wakati nampa kipigo mkoba wake ulifunguka na pembe iliyokuwa ndani ya mkoba ule ikaanguka.Watu wote wakaogopa kumsogelea na kumpa msaada.Lilikuwa ni tukio la kushangaza mno.Watu waliokuja kushuhudia ugomi ule walikuwa wakisemezana wao kwa wao kuhusiana na kile kilichokuwa kimetokea na hasa kuhusiana na ile pembe iliyokuwa imeanguka chini
Chris akanishika na kuniondoa mahala pale akanipeleka sehemu tulivu nikakaa halafu akamrudia Emmy aliyekuwa bado amekaa chini akilia.Emmy alikataa kata kuongea na mtu yeyote na wala hakutaka kwenda kutibiwa au kwenda kutoa taarifa polisi kama alivyokuwa ameshauriwa na baadhi ya akina mama waliokuwepo pale badala yake akainuka na huku akivuja damu akaelekea liliko gari lake akaingia na kuondoka.Pembe lake aliliacha pale pale chini lilipoanguka.Chris akafanya maombi mafupi halafu akalishika pembe lile na kwenda kulitupa mbali.
**********************
Meru view Garden ni moja ya hoteli bora kabisa na ghali jijini Arusha.Hii ni hoteli ambayo inafahamika kwa kufikia watu wenye uwezo mkubwa kifedha.Ni hoteli ambayo iko nje kidogo ya jiji na iliyo na utulivu wa kipekee.Saa mbili na nusu ilimkuta Sheila katika geti la hoteli hii tulivu akajitambulisha mapokezi kwamba alikuwa mgeni wa James .Wahudumnu wakawasiliana na James ambaye aliwaambia wampeleke Sheila katika chumba chake.Alikuwa amependeza sana usiku ule.Walifika hadi katika chumba kimoja kilichokuwa na walinzi wawili mlangoni waliokuwa wamevaa suti nyeusi ambao waliufungua mlango na kumruhusu Sheila aingie ndani
? Hallo Sheila? akasema James aliyekuwa amejilaza sofani akitazama Luninga latika chumba hiki kikubwa.Sheila alisimama akimkodolea macho James.
? James ni wewe !! akashangaa Sheila
? Ni mimi Sheila kwani umenisahau?
? hapana james siwezi kukusahau hata kidogo.Ninashangaa kwa namna ulivyobadilika.
Ama kweli duniani hakuna mtu mwembamba? akasema Sheila huku akitabasamu
James akainuka akakumbatiana na Sheila halafu akamuelekeza aketi sofani.
? karibu sana Sheila.Nimefurahi kukuona? akasema James
? nashukuru sana James.Hata mimi nimefurahi sana kukuona .Ni muda mrefu sana umepita hatujaonana .James umebadilika mno.Nini siri ya mafaniko yako.? Au ni hali ya hewa ya huko imekukubali? Akauliza Sheila.James akatabasamu na kusema
? Sheila kwanza kabisa kuna kitu ambacho unatakiwa ukifahamu.Unaponiita jina langu anza na neno Nabii.Nabii James ndilo jina langu kwa sasa?
? nabii ?!! Sheila akashangaa
? ndiyo Sheila.Kwa sasa mimi ni mtumishi wa Mungu ninaitwa Nabii James.Nimeamua kumtumikia Mungu? akasema James huku akiinua glasi yake ya kinywaji na kunywa
? maisha yana maajabu sana..James umekuwa nabii?
? ndiyo Sheila.Si jambo la ajabu kuwa nabii.Mungu amenichagua toka kundi lake la kondoo na kunipaka mafuta ili nimtumikie.Kwa hivi sasa makazi yangu ni nchini Canada na Norway.Hapa nyumbani nimekuja mara moja kuna jamo lililonileta kwa dharura? akasema James
? karibu sana nyumbani nabii James.? Akasema Sheila na kumfanya james atabasamu
? maisha yanaendaje Sheila,naona unazidi kupendeza .Wakati wengine wanabadilika na kuwa wazee kadiri miaka inavyosonga lakini kwako wewe ni tofauti unazidi kuwa binti mdogo nini siri ya urembo? Akauliza James na kumfanya Sheila acheke kicheko kikubwa
? Ninajitahdi kujitunza ndiyo maana niko hivi? akajibu Sheila.
? Maisha yanaendaje hapa Tanzania? Akauliza james
? Tunamshukuru Mungu tuko wazima na maisha yanaenda vizuri? akasema Sheila
James akainuka pale sofani
? Sheila naomba tukapate chakula .Nilijua unakuja kwa hiyo sikuwa nimepata chakula nikikusubiri? akasema James halafu wakaingia katika chumba cha pembeni kilichokuwa na meza yenye viti vinne iliyokuwa na aina nyingi za chakula mezani wakakaa na kula kisha wakarejea mahala walipokuwa wamekaa mwanzoni
? Sheila ninashukuru sana umefika kama nilivyokuomba.Nimekuita hapa kuna jambo ambalo nataka uniambie bila kunificha? akasema James
? nabii James usihofu kitu.Uliza jambo lolote lile na siwezi kukuficha wewe ni mtumishi wa bwana? akasema Sheila
? Sheila kama nilivyokwambia awali kwamba nimetua hapa Arusha kwa dharura lakini sikuwa na mpango wa kuja hivi karibuni na ndiyo maana nimekuja kimya kimya na kufkia hapa hotelini ,sitaki mtu yeyote afahamu juu ya ujio wangu.Kuna jambo lililonileta hapa.Ni kuhusu Emmy.Kwanza sijakuuliza chochote kuhusu maendeleo yake.anaendeleaje?akauliza James
? Emmy anaendelea vizuri sana? akajibu Sheila huku macho yake yakionyesha wasi wasi kidogo
? nafurahi kusikia hivyo.Sijataka afahamu kama nimekuja hapa nilitaka nisionane naye kwanza hadi nizungumze nawe kwanza kwa sababu najua wewe ni mtu wake wa karibu sana?
?Mimi na Emmy ni marafiki wakubwa.? Akajibu Sheila
? Nafurahi kusikia hivyo na kwa kulifahamu hilo ndiyo maana nimetaka kuonana nawe kwanza kabla hata sijaonana na Emmy.? Akasema James halafu akanyamaza akameza mate na kusema
? Sheila kwa sasa mimi ni mtu mkubwa sana si hapa afrika bali duniani kwa ujumla .Hapa nyumbani sifahamiki sana lakini katika nchi nyingine za Ulaya na amerika ninafahamika na kuheshimika mno kutokana na kazi zangu za kinabii.Sitaki kuelezea kwa undani sana kuhusiana na mambo haya ya kinabii lakini naomba ufahamu kwamba nimechaguliwa na kupakwa mafuta na bwana ili nimtumikie.Kwa hapa ny7mbani iko siku itafahamika kwa sababu imeandikwa kwamba nabii hakubaliki kwao lakini siku itakuja watanikubali ? akasema James halafu akamtazama Sheila na kuendelea
?Kwa muda mrefu nilikuwa namuomba bwana anisaidie niweze kupata msaidizi yaani mke na siku moja nikiwa katika maombi mazito nikaona maono .Katika maono hayo bwana alinionyesha kwamba mwanamke ambaye atakuwa mke wangu anatoka Tanzania lakini sikuonyeshwa ni yupi na anatokea sehemu gani ya Tanzania.Baada ya kukaa na kutafakari kwa muda nikagundua kwamba mwanamke pekee ambaye nilionyeshwa katika maono yale ni Emmy.Mimi na Emmy tumekuwa wapenzi wa muda mrefu sana nadhani unafahamu urafiki wetu ulikotoka.Japokuwa tulikuwa tunakorofishana mara kwa mara lakini tulisuluhisha matatizo yetu na kusonga mbele.Ninampenda Emmy toka moyoni na ndiye mwanamke ambaye nina imani bwana ameniangazia ili awe mke wangu wa ndoa.Kabla sijaonana naye nimeona nikuite kwanza wewe ambaye ndiye rafiki yake wa karibu ili uweze kunipa maelezo kuhusiana na Emmy kwa sababu ni kipindi kirefu sijaonana naye.Nataka kufahamu anaishi wapi hivi sasa,maisha yake yakoje,yuko katika mahusiano ama la.nataka kufahamu kila kitu kuhusiana na Emmy.Nina imani kwamba hutanificha kitu chochote.? Akasema James halafu akainuka na kuingia chumbani halafu akarejea na bahasha iliyofungwa vyema akampatia Sheila.
? kamata hii.Its ten thousand dollars to buy the information from you..so tell me the truth about her? akasema James.Sheila bado aliendelea kutetemeka mikono akiwa ameishika bahasha ile.Hakuamini macho yake.Ni katika kipindi kama hiki alikuwa akumiza kichwa angetoa wapi fedha za kumlipa Wayne ,fedha alizokopa ili aweze kumlipa Emmy ambaye alipanga kumdhalilisha na bila kutegemea amepata fedha ambazo alikuwa anazihitaji na zaidi.Alimtazama James kwa jicho la mshangao.
? Ouh my gosh ! siamini.yaani james amefikia hatua hii? Anaweza akanipatia fedha hizi zote kwa ajili ya kupata taarifa ya Emmy tu ? Inaonekana mambo yake ni mazuri sana..? akawaza Sheila
? Niambie Sheila .Nina hamu sana ya kutaka kufahamu.Hiki ndicho kitu pekee kilichonifanya nikuite hapa usiku huu? akasema James
? Eemmy its pay back time? akawaza Sheila halafu akakohoa kidogo na kusema
? Nabii James kwanza napenda nikushukuru sana kwa mzigo huu mkubwa.Wanasema kwamba Nabii hakubaliki kwao lakini wewe nimekukubali kwa sababu umekuja wakati nikiwa na shida ya fedha na umenipatia kiasi nilichokuwa nakihitaji hata na zaidi.Nimekukub
ali James wewe ni nabii wa kweli.? Akasema Sheila
? usihofu Sheila.Pesa si tatizo kwangu hivi sasa.Muda wowoe ukihitaji fedha niko tayari kukupatia hata mara hamsini ya hizo.Haya naomba sasa uniambie ukweli? akasema James
? Nabii James naomba nikiri kwamba maono yako yanawezekana yalimaanisha mwanamke mwingine na si Emmy?
? kwa nini unasema hivyo Sheila? Akauliza James huku akijiweka vizuri sofani
? Nabii James naomba nikiri kwako kwamba Emmy hayuko vile ambayo unamfahamu wewe.Emmy ni mtu mwenye sura zaidi ya moja.?
? Sikuelewi Sheila unamaanisha nini.Hebu niweke wazi? akasema James na kujifuta jasho lililoanza kumtoka
?nabii james,kwanza kabisa naomba ufahamu kwamba katika siku zote za urafiki wenu hakukuwa na hata chembe ya ukweli ndani ya mahusiano yenu.It was all lies.Hakukuwa na mapenzi yoyote .?
? Kwa nini unasema hivyo Sheila? I loved Emmy so much.I loved her with all my heart and she loved me too?
? Ndiyo nabii james najua ulimpenda sana Emmy na hadi sasa bado unampenda sana lakini fahamu kwamba hakukupenda hata kidogo.Alikuwa anakutumia tu.Hana hata chembe ya upendo kwako? akasema Sheila
? Ouh my gosh haya ambo ni mapya.Hebu nieleze ni kwa nini unasema hivyo Sheila? Akasema James
?James wakati ule mkiwa katika mahusiano,Emmy tayari alikuwa katika mahusiano na wanaume watatu tofauti na wewe ulikuwa wanne.Hakuna aliyemfahamu mwenzake na wote aliweza kuwatumia vile atakavyo.?
?Sheila una hakika na hicho unachoniambia? Akauliza James
? Ndiyo James nina uhakika kwa sababu mimi ndiye rafiki yake mkubwa na kila kitu chake lazima anishirikishe?
? Ok go ahead? akasema james
?Kitu ambacho hukuwa unakifahamu ni kwamba Emmy aliwahi kuolewa wakati ukiwa nje ya nchi na uliporudi kwa likizo hukujua chochote.?
? real ???,?? akauliza James huku uso wake ukianza kubadilika
? Ndiyo James.Emmy aliolewa na kijana mmoja anaitwa Wayne.?
James akavuta pumzi ndefu,alionekana kuchanganyikiwa
?Kuna mambo mengi sana ambayo nikikuelezea hapa tunaweza kukesha usiku kucha lakini kikubwa ambacho ninataka kukueleza ni kwamba,ulipoondoka kwenda Urusi kimasomo,ulimuacha Emmy akiwa na ujauzito mchanga.?
? real ???? akasema James kwa mstuko
? Ndiyo james. Emmy alibaki na ujauzito wako.Mume wake hakujua kama ujauzito ule ni wa kwako na Emmy akamdanganya kwamba mimba ile ilikuwa yake Wayne?
? what happened then? Akauliza James
?Emmy alijifungua mtoto wa kiume?
? Ouh thanx God..? akasema James huku akiinua mikono juu na kumshukuru Mungu
? Sina cha kukupa Ee Mungu wangu.? Akasema James halafu akaanza kuongea maneno Fulani ambayo Sheila hakuyaelewa ilikuwa ni lugha gani.Aliongea akiwa amefumba macho.
?Sheila hizi ni habari nzuri sana ambazo nimezipata leo hii.Umeniletea habari njema ambazo zimenifurahisha mno. Ndiyo maana kila siku nilikuwa nikiota nyumbani kumbe kuna taarifa nzuri namna hii.Ahsante sana Sheila? akasema James halafu akainuka na kutoka pale sebuleni akaingia chumbani na baada ya muda mfupi akarejea akiwa na bahasha mkononi akampatia Sheila
? kamata hii Sheila.Its ten thousand dollars again.Umenipa habari ambazo zimenifurahisha mno.Sijawahi kufurahi kama nilivyofurahi le😵uh Mungu ahsante sana ? akasema James na kurejea katika sofa.Sheila aliona kama yuko ndotoni. Ndani ya muda mfupi tayari ametengeneza zaidi ya shilingi millioni thelathini.
? So how?s my baby boy.Is he handsome? Akauliza James kwa furaha.Sheila akasita kidogo kujibu.
? I have to tell the truth? akawaza na kukohoa kidogo kisha akasema
? yes he was very handsome?
? He was ?? akauliza James kwa mshangao
? yes he was?.?akajibu.Sura ya James ikajenga wasi wasi
?James naomba niwe muwazi kwako kwa kila jambo.Miezi kadhaa iliyopita Wayne mume wa Emmy aligundua kwamba Baraka hakuwa damu yake.Jambo hili lilizua mtafaruku mkubwa sana uliopelekea ndoa yao kuvunjika na kila mmoja akaendelea na maisha yake peke yake. Baada ya kuachana na Wayne,Emmy alianzisha madai kwamba alikuwa amerogwa na ndiyo maana migogoro kati yake na Wayne haikuisha.Mwishowe aliamua kwenda kwa mganga wa kienyeji ili aweze kumfahamu mbaya wake na pia kumfanya Wayne arudi tena kwake.Mganga alimfanyia dawa na siku iliyofuata alirejea mjini lakini alikutana na taarifa mbaya.Mwanae Baraka alikuwa amefariki dunia ghafla usiku wakati akiwa kwa mganga.Naomba niwe muwazi kwako Nabii James,Emmy alimtoa kafara mwanae kwa mizimu? akasema Sheila.
Taratibu james akasimama na mara akajikuta ameishiwa nguvu na kukaa chini katika zuria.
? Sheila that?s not true..Thats a lie..mwanangu haweze kufa..Mwanangu bado mzima? akasema James.Alikuwa anaweweseka huku akiongea maneno ambayo Sheila hakuyafahamu.Macho yake yalikuwa yamelowa machozi.
?Mwanangu Baraka..ouh Emmy how could you do that? Akalia James.Alilala pale katika zuria kwa zaidi ya saa moja.Alipoinua kichwa macho yake yalikuwa yamevimba na mekundu kwa kulia
?Sheila ahsante sana kwa taarifa hizi na kuwa mkweli kwangu.Naomba kwa sasa uondoke nataka nibaki mwenyewe.I need to be alone.I want to cry alone.Kesho nakuomba uje saa nne za asubuhi unipeleke mahala alikozikwa mwanangu Baraka nikalione kaburi lake? akasema James huku machozi yakiendelea kumtoka
Sheila akatoka mle chumbani kwa James na mmoja wa walinzi akamrudisha hadi nyumbani kwake kwa kutumia gari la hoteli.Aliumia moyoni baada ya kuikumbuka historia ile hasa walipokwenda na Emmy kwa mganga na akawafanyia jambo baya lakini kwa upande mwingine alifurahi kwa sababu aliweza kumuharibia kabisa Emmy kwa James.
? James ameumia mno na niliyaona macho yake,sijui atafanya nini akionana na Emmy.Alilia sana hadi nikamuonea huruma.Sikuwa na namna nyingine na kufanya zaidi ya kumueleza ukweli James. Hii ni vita kati ya ngu na Emmy na katika vita ya kubidi utumie kila aina ya silaha uliyonayo kumbomoa adui yako.Nimetumia vyema silaha zangu.Yeye alianza na mimi nimemaliza.Alimwaga ugali na mimi nimemwaga mboga? akasema Sheila akiwa amezimwaga fedha zile alizopewa na James kitandani.Akazishika noti zile nyingi asiamini macho yake.
? Twent thousand dollars !! akashangaa..
? James amefikia hatua hii ambayo anaweza akampatia mtu fedha zote hizi bila ya kumfanyia kazi yoyote.Mhh lazima atakuwa na fedha nyingi sana.Lazima atakuwa ni bilionea.? Akawaza Sheila
Hata baada ya Sheila kuondoka bado James aliendelea kukaa katika zuria akilia.Habari za kwamba Emy alimuua mwanae kwa kumtoa kafara ilimsikitisha sana.
? Nilifurahi mno baada ya kusikia kwamba Emmy alibahatika kuzaa na mimi mtoto lakini furaha yangu yote imeyeyuka baada ya kusikia kwamba mwanangu alikufa kwa kutolewa kafara kwa mizimu.Emmy kwanini ulifanya hivyo? Kwa nini ulimuua mwanangu? Yaani umediriki kumuua mwanangu kwa ajili ya mwanaume? Uongo wote ulionidanganya haukutosha ukaamua hadi kumuua mwanangu ?.Ninaona kama dunia yote imenigeuka na kuniadhibu.Emmy I?ll never forgive you for this.Emmy sintakusamehe hata kidogo.I swear in heaven and earth I?ll never forgive you.? Akasema James kwa hasira huku mwili wake mkubwa ukitetemeka
TUKUTANE SEHEMU IJAYO???
 
BEYOND PAIN
SEHEMU YA 32
MTUNZI 😛ATRICK.CK
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
? Twent thousand dollars !! akashangaa..
? James amefikia hatua hii ambayo anaweza akampatia mtu fedha zote hizi bila ya kumfanyia kazi yoyote.Mhh lazima atakuwa na fedha nyingi sana.Lazima atakuwa ni bilionea.? Akawaza Sheila
Hata baada ya Sheila kuondoka bado James aliendelea kukaa katika zuria akilia.Habari za kwamba Emy alimuua mwanae kwa kumtoa kafara ilimsikitisha sana.
? Nilifurahi mno baada ya kusikia kwamba Emmy alibahatika kuzaa na mimi mtoto lakini furaha yangu yote imeyeyuka baada ya kusikia kwamba mwanangu alikufa kwa kutolewa kafara kwa mizimu.Emmy kwanini ulifanya hivyo? Kwa nini ulimuua mwanangu? Yaani umediriki kumuua mwanangu kwa ajili ya mwanaume? Uongo wote ulionidanganya haukutosha ukaamua hadi kumuua mwanangu ?.Ninaona kama dunia yote imenigeuka na kuniadhibu.Emmy I?ll never forgive you for this.Emmy sintakusamehe hata kidogo.I swear in heaven and earth I?ll never forgive you.? Akasema James kwa hasira huku mwili wake mkubwa ukitetemeka
ENDELEA????????
Nilikaa ile sehemu ambayo Chris aliniweka ili nitulie na baada ya hasira nilizokuwa nazo kutulia akanichukua na kunipeleka kwa wazazi wa Clara.Nilisalimiana nao nikavuta kiti na kuketi.Chris akaanzisha mazungumzo
?Wayne kama nilivyokutaarifu awali , hawa ndio wazazi wa Clara? akasema Chris
? Wazee wangu huyu ndiye Wayne ambaye alikuwa na Clara hadi dakika ambayo alipatwa na matatizo haya? baada ya Chris kufanya utambulisho ule nikasimama na kuwapa tena mikono wazazi wale
? Ninafurahi kuwafahamu wazee wangu.karibuni sana Arusha na poleni kwa matatizo? nikasema
? Hata sisi tunafurahi kukuona pia.Pole sana na matatizo Wayne? akasema baba yake Clara
? Ahsante baba.Tumekwisha poa? nikasema
? Wayne kama ulivyoelezwa na mwenzako kwamba sisi ndio wazazi wa Clara na tumetaarifiwa leo asubuhi na mtu mmoja aliyeko katika ofisi yake kule afrika kusini kwamba amepatwa na ugonjwa huu wa ghafla.Kama wazazi tulistuka sana na kujiuliza kwa nini hatukutaarifiwa mapema na watu amabo walikuwa karibu naye muda wote hadi tutaarifiwe na watu walioko nje ya nchi?.Tumejiuliza maswali mengi bila majibu na ndiyo maana tumeona hatuwezi kulala leo hii hadi tuonane nawe na utueleze kwa kina kwa nini mlifanya hivi.Je mlisubiri hadi mwanangu aage dunia ndipo mtutaarifu? Akasema mzee Yule ambaye alionekana kukabwa na donge kubwa kooni.Nilijua pale lazima kulikuwa na shughuli nzito ikanilazimu nitumie kauli ya kiungwana zaidi.
Kwanza nilikiri kosa .Ni kweli nilikosea kutokuwataarifu wazazi wa Clara mapema kuhusiana na tatizo lililompata mtoto wao.Niliwaeleza kwamba sababu kuu iliyofanya nishindwe kuwataarifu mapema ni kutokanana kuchanganyikiwa kwa ugonjwa ule wa ghafla ambao sikuutegemea.Niliwapa sababu ambazo walikubaliana nazo na wakanipa ushauri kwamba siku zote linapotokea tatizo la namna hiyo kwa mtu yeyote kuna ulazima wa kuwasiliana na ndugu wa karibu wa mgonjwa na kuwafahamisha mapema.Mzee Yule alitaka kujua mahusiano yaliyopo kati yangu na Clara.Nilimueleza kwa kifupi kwamba mimi na Clara tulikuwa tumekutana jijini Arusha tukajikuta tukipendanana na tukaanzisha mahusiano ya kimapenzi.Sikutaka kumficha kitu
? Nilishangaa kwa nini Clara aliamua kuahirisha ghafla safari yake ya kurejea afrika kusini .Kumbe tayari alikuwa katika mahusiano.? Akasema baba yake Clara.Kikapita kimya cha muda mama yake akauliza
?Yule mwanamke uliyekuwa unagombana naye ni nani? Nilistuka sana kwa swali lile.Nilisikia aibu kubwa kwa wazazi ale kukishuhudia kitendo kile cha aibu kilichotokea usiku ule
?Ni aliyewahi kuwa mke wangu? Nikasema
? Ulikuwa umeoa? Wote wakastuka
? Ndiyo niliwahi kuwa na mke lakini tuliachana ?
? Alikuja kutafuta nini hapa hospitali mida ile na kupelekea mpigane? Akauliza baba mkwe nikajikuta nikikosa jibu la kumpa.Niliogopa kumweleza ukweli wa jambo alilolifanya Emmy
?Wakati mkigombana kuna pembe iliangika toka katika moba wa Yule mwanamke.Ilikuwa ya nini pembe ile? Akauliza mama Clara
? Pembe ?? nikashangaa.Sikuwa nimeiona pembe wakati nikimshushia kipigo Emmy
? Ndiyo kulikuwa na pembe na kila mtu aliiona.? Akasema mama Clara.Nikamgeukia Chris
? Ni kweli Wayne.Katika mkoba wa Emmy kulikuwa na pembe ya mnyama lakini tayari nimekwisha iharibu na haina nguvu tena?
?Ouh my gosh ! nikashika kichwa changu kwa mshangao
? Wayne inaonyesha wazi kuna mambo yanayoendelea hapa chini kwa chini.Sifahamu lengo lenu kwa mwanangu ni nini hasa.Inaonekana ugonjwa huu wa mwanangu si ugonjwa wa kawaida .Kuna namna imefanyika hapa.Mambo niliyoyashuhudia yamenipa uoga sana ? akasema baba Clara.Nilikuwa nimeinama nikitafakari na sikujua nimjibu nini.baada ya muda baba Clara akasma
? Wayne na Chris sipendi kuchukua muda wenu mwingi kwani mnatakiwa muende kupumzika.Kwanza kabisa ninawashukuru sana kwa namna mlivyomshughulikia Clara toka alipopatwa na matatizo haya.Mmefanya kazi kubwa sana na hata madaktari wa hapa wamewasifu kwa kufanya kila jitihada ili kumtibu Clara.Nimeambiwa na madaktari kwamba kulikuwa na mpango hata wa kumpekeka nje ya nchi kwa matibabu lakini wakasema kwamba ugonjwa huu unatibika hapa hapa nchini.Ninawashukuru sana kwa kila jitihada mliyoifanya.Pamoja na hayo kuna maamuzi ambayo sisi kama wazazi tumeyachukua.kwanza kabisa kesho asubuhi tunaondoka na Clara.Tunakwenda naye jijini Dar es salaam na kuanza taratibu za kumpeleka nje ya nchi kwa matibabu ya uhakika .Sisi ni watu wenye uwezo na tunataka mwanetu atibiwe katika hospitali bora zaidi nje ya nchi.Kwa hiyo kesho tutaondoka na Clara.Tayari tumekwisha andaa kila kitu kuhusiana na safari ya kesho.Jambo la pili ambalo najua ni gumu lakini ni lazima tulifanye Wayne tunakuomba uachane kabisa na Clara. Tumegundua kwamba wewe ndiye chanzo cha mtoto wetu kupatwa na matatizo haya yaliyompata.Hatujui mmekutana wapi na ni kwa kiasi gani mnapendana lakini ninachotaka kukuhakikishia ni kwamba sisi kama wazazi hautkukubali uwe na uhusiano wa kimapenzi na mwanetu,kaa mbali kabisa na mwanangu na si kwa wakati huu tu ambao anaumwa bali katika maisha yake yote.Sitaku tena kusikia masuala ya mahusiano kati yako na Clara.Kama unataka kuwa na mahusiano na mwnangu usubiri hadi nitakapokuwa nimefariki lakini kama bado niko hai sintaruhusu kamwe uwe na mahusiano na mwanangu.Naomba usinielewe vibaya Wayne ,wewe ni kijana mzuri mwenye moyo wa upendo ,jasiri ,makini na mwenye nidhamu lakini hufai kuwa na mwanangu.Najua ni jambo ambalo hukulitegemea na ambalo linauma sana lakini kuna nyakati katika maisha ni lazima tufanye maamuzi magumu na sisi kama wazazi tumefanya maamuzi hayo kwa faida yako wewe na mwanetu.? Akasema baba yake Clara.Nilihisi kama mwili wangu unaingiwa na ubaridi na kufa ganzi .Maneno yale aliyoyasema yule mzee yalikuwa mazito sana na ambayo katu sikuyategemea kuyasikia na hasa katika wakati ule ambao nilihitaji sana faraja..
?Mzee naomba usitamke hivyo hasa kwa wakati huu ambao Clara yuko katika matatizo.Ninamp
enda Clara kwa moyo wangu wote na yeye analifahamu hilo.Clara ni kila kitu kwangu.tafadhali mzee naomba usinifanyie hivi.? Nikasema huku machozi yakinilenga.Nil
iumia sana.Mama yake Clara alionekana kunionea huruma sana lakini hakuwa na maamuzi
? Wayne tayari tumekwisha fanya maamuzi na hatuwezi kuyabadili tena.Kesho saa nne asubuhi tutamuondoa Clara na kumsafirisha.Tu
takupa nafasi ya kuonana na Clara kwa mara ya mwisho kabla ya kuondoka kwani baada ya hapo hutamuona tena katika maisha yako.Kama utakuwa tayari kuja kuagana na Clara basi ufike hospitali kabla ya saa nne za asubuhi? akasema baba Clara halafu akainuka.Mke wake alitaka kusema jambo lakini akamzuia.Wakaaga na kukodi taksi wakaondoka.
Nilibaki nimeinama kwa zaidi ya robo saa nikiwaza.Kwa mara nyingine tena nilihisi kuadhibiwa na dunia.Nilisikia maumivu makali sana ndani ya moyo wangu maumivu ambayo hayaelezeki.Ilikuwa ni zaidi ya maumivu.
? wayne its time to go home? akasema Chris kwa sauti ndogo.Nikainua uso wangu ulikuwa umejaa machozi
? Chris nimekosa nini kiasi cha kuadhibiwa na dunia kiasi hiki? Kwa nini kila mara iwe mimi tu? Nikasema kwa uchungu
? Usijali Wayne.Kila jambo hutokea kwa sababu maalum.Jitahidi kuvumilia na kumtegemea bwana Mungu naye atakushindia.Be strong Wayne? akasema Chris
?I?m hurt Chris.kwa nini Yule mzee anifanyie hivi? Why??????????????? Nikasema kwa hasira
? Calm down Wayne.Huna sababu ya kuumia sana .Kama Clara ndiye mwanamke uliyeandikiwa uwe naye basi siku moja utakuwa naye. Niamini nikwambiayo .Mapenzi yana nguvu kuliko kitu chochote kile.Mapenzi yanau wezo wa kuusambaratisha hata mlima.If you real love Clara one day you?ll be with her.believe me brother? akasema Chris.Maneno yale yalinipa moyo sana.Nikainuka pale kitini tukaelekea garini na kuondoka kurejea nyumbani kwa Chris
? Mambo yote haya yanatokea its because of Emmy..? nikasema tukiwa njiani kurejea nyumbani
? Kusema kweli Wayne Yule mwanamke ninashindwa kumuelewa hata mimi ni kitu gani hasa anachokitafuta kwako.Nilistuka sana baada ya kuiona pembe ile ikitoka katika mkoba wake.Kwa nini alikuja nayo pale hospitali? Akasema Chris
? Emmy amefikia hatua mbaya sana kwa sasa.Sintasahau mateso na maumivu yote aliyonisababishia na ninakwambia Chris siku moja lazima Emmy atalipia uovu wake.Amesababisha mateso kwa watu wengi sana.Ameniumiza kwa mengi lakini kwa hiili la Clara alivuka mipaka na ndiyo maana nilipomuona nilipandwa na hasira nikampa kipigo kikali mno.Kama usingetokea kuja kuniamua nahisi ningeweza hata kuua kwa hasira nilizokuwa nazo.?
? Pole sana Wayne. Vipi kuhusu kule Mombo mlikoenda na Sheila?
? Hatukufanikiwa kumpata yule mchawi mkubwa.Na kama tungemkuta basi ingekuwa ama zake ama zangu.Ana bahati sana ? nikasema halafu nikakumbuka jambo Fulani
? Hey Chris?unamfahamu mtu anayeitwa james?
? James ? Chris naye akashangaa
? Ndiyo James?
? Kuna akina James wengi sana hapa mjini.Unamzungumzia James yupi?
?Nikiwa garini wakati tukirejea toka Mombo , Sheila alipigiwa simu na mtu mmoja anaitwa a James na kumuomba woanane usiku wa leo.kwa mujibu wa Sheila james ndiye baba mzazi wa Baraka.Alikuwa nje ya nchi kimasomo na wakati anaondoka alimuacha Emmy akiwa na mimba yake.?
Chris akavuta pumzi ndefu kwa taarifa ile
?Wayne nakuomba ndugu yangu ,mambo yote yanayohusiana na Emmy achana nayo kwa sasa.Muweke Emmy pembeni kabisa katika maisha yako na tukabiliane na mambo ambayo yako mbele yetu kwa sasa.?
? Hilo unalosema ni jambo la kweli Chris.Baada ya mambo haya yote kutokea nadhani ni wakati sasa wa kufanya maamuzi sahihi? nikasema na kukaa kimya.bado maneno ya baba Clara yaliendelea kunitesa kila nikiyakumbuka .Niliumia mno na maneno yale ambayo yaliashiria mwisho wangu na mwanamke niliyempenda kuliko wote.
***************
Hatimaye kulipambazuka tena .Hii ni siku ambayo nitakwena kumuaga Clara na sintamuona tena kwani baba yake aliuvunja rasmi uhusiano wetu na aliweka wazi kwamba kama ninataka kuwa na mahusiano na mwanae Clara basi nisubiri hadi hapo atakapofariki.N
iliamka kama mgonjwa kwani sikuweza kupata usingizi usiku.Nilikuwa na mawazo mengi sana.Niliwaza kuhusiana na mustakabali mzima wa maisha yangu,nilikotoka ,niliko na ninakokwenda.Nilijiona ni mtu mwenye mkosi mkubwa na laana.
Saa tatu za asubuhi tuliondoka kuelekea hospitali.Tayari wazazi wa Clara walikwisha fika pale hospitalini na taratibu za kumsafirisha Clara zilikuwa zinaendelea.Tulisalimiana na mama Clara alionekana kunionea huruma sana
? Usijali mwanangu.Kama wewe na Clara mnapendana basi atakapopona mtakuwa pamoja tena.Usiache kumuombea ili aweze kupona? akasema mama yake Clara baada ya mumewe kuondoka na daktari.
? Nashukuru sana mama.Naomba nikiri kwako kwamba Clara ndiye mwanamke ninayempenda sana hapa duniani na kuumwa kwake ni pigo kubwa kwangu na katika maisha yangu.Lakini hata hivyo sina budi kuyaheshimu maamuzi ya baba na nitakaa mbali na Clara ingawa bado nitaendelea kumuombea ili aweze kupona.Pamoja na hayo mama ninaomba msaada mdogo sana toka kwako?
? Msaada gani wayne?
Nikatoa kadi yangu ya mawasiliano na kumpatia
? Hizo ni namba zangu za simu ninaomba walau mara moja moja uwe unanipigia na kunifahamisha kuhusu maendeleo ya Clara.Utakuwa umenifanyia jambo kubwa sana mama kama ukinifanyia hivyo?
? Usijali Wayne.Nitakuwa nawasiliana nawe na kukufahamisha kila kitu? akasema mama Clara huku akiiweka kadi ile katika pochi yake.
Kabla Clara hajaondolewa wodini na kupelekwa uwanja wa ndege nilipewa nafasi ya peke yangu ya kuoana naye kwa mara ya mwisho.Clara alikuwa ananitazama lakini hakuweza kusema chochote. Macho yangu yalikuwa yanatoa machozi.Niliiona michirizi ya machozi machoni pake pia.Nikainama na kumkumbatia.Nililia sana kwani ilikuwa ni mara yangu ya mwisho kuonana naye
? Clara toka ulipokuja katika maisha yangu umeweza kuyafanya yawe ni ya furaha kubwa.Ninaweza kusema kwamba nimeishi maisha yangu yote katika kipindi hiki kifupi nilichokutana nawe.Sijawahi kupata furaha na sintapata furaha tena katika maisha yangu kama niliyoipata nikiwa nawe.Siwezi kuzisahau zile nyakati nzuri za furaha tulizokuwa pamoja.Zitabaki ni kumbu kumbu pekee kwangu.Ninakupenda Clara zaidi ya ninavyoweza kueleza.Japo baba yako hataki tena mimi nawe tuendelee na uhusiano wetu lakini sintaacha kukupenda Clara.Nitakupenda katika siku zote za maisha yangu na sintakuwa na mwanamke mwingine katika maisha yangu zaidi yako.Ninakuombea upone haraka Clara? nikasema halafu nikambusu. Sina hakika kama kilio kile alikisikia lakini macho yake yalikuwa yamejaa machozi.Nikatoa kitambaa na kumfuta Mlango ukafunguliwa wakaingia madaktari na kuniomba niwapishe.Nikatoka mle chumbani huku nikifuta machozi.Kilikuwa ni kipindi kigumu mno kwangu.Sikuwahi kuumia kama nilivyoumia sasa.Chris alikuwa karibu yangu na akanipa moyo.Baada ya muda mfupi Clara akatolewa akisukumwa katika kitanda na kupakiwa katika gari la wagonjwa.Iliniuma sana.Mtu ambaye siku chache zilizopita alikuwa akitembea kwa mwendo wa madaha lakini leo hii hawezi kufanya lolote,na yote haya ni kwa sababu ya Emmy.Nilimlaani emmy kwa kila laana niliyoifahamu katika hii dunia.
Clara alipakiwa katika gari la wagonjwa na safari ya kuelekea uwanja wa ndege wa kimataifa wa Kilimanjaro ikaanza.Mimi na Chris tulipanda katika gari la Chris ,na rafiki yangu mwingine mkubwa Beka alikuwa pamoja nasi.Sikuongea chochote njiani nilikuwa na mawazo mengi sana naman maisha yangu yalivyokuwa ya matatizo.Nilimuwaza Emmy na mambo yote aliyonitendea,sikuona adhabu gani nimpatie kwa maumivu aliyonisababish
ia.Nikaamua kumuachia Mungu mambo yote yeye ndiye atakayenilipia.
Tulifika katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Kilimanjaro,.Pale nikapewa tena nafasi nyingine ya mwisho ya kuonana na Clara.Niliinama na kumbusu mdomoni.
? Nakupenda Clara na siku zote nitaendelea kukupenda.When u get better I?ll be here waiting for you? nikamwambia Clara.
? Wayne nakushukuru sana kwa msaada wako mkubwa kwa mwanangu na nitazidi kukuombea afya njema kila siku.Mungu akujalie afya na mwanamke mwingne utakayempenda kama ulivyompenda Clara.? Akasema baba yake Clara halafu tukashikana mikono tukaagana.Sikuw
eza kumtamkia chochote kwa sababu nilihisi fundo kubwa kunikaba kooni.
? Wayne usikate tamaa kijana wangu.Siku zote mtegemee Mungu naye atakusaida katika kila jambo.Endelea kumuombea mwenzako na Mungu akipenda siku moja mtaonana tena.Nitakuwa nakupigia simu mara kwa mara kila ninapopata nafasi na kukupa taarifa za maendeleo ya Clara.Ubaki salama Wayne? akasema mama yake Clara ambaye macho yake yalionyesha kulengwa na machozi.
?Wayne,.let?s go back home? akasema Chris .Sikutaka kuendelea kukaa pale uwanjani tukaingia garini na kurejea nyumbani kwa Chris.Nilikuwa kama mtu niliyechanganyikiwa akili.Sikujua nifanye nini kwa wakati huo.
?Chris kwa nini maisha yangu yamekuwa namna hii? Kwa nini yamekosa furaha ? Nimekosea nini Mungu kiasi cha kuniadhibu kiasi hiki? Nikamuuliza Chris tukiwa tumekaa sebuleni nyumbani kwake baada ya kutoka uwanja wa ndege kumsindikiza Clara
? wayne sisi sote katika hii dunia ni wakosefu na sote tunamkosea Mungu kila siku lakini pamoja na makosa yote tunayomkosea bado Mungu amezidi kutupenda na muda wote yuko tayari kutupokea pale tunapotambua makosa yetu na kutubu..Mungu hutupokea akatukumbatia na kututakasa kutufanya wapya na kutuweka katika kundi la kondoo zake safi .Bwana Mungu hajatuacha katika vilio vyetu ,katika mahangaiko yetu lakini anataka tumlilie ,tumkimbile yeye pekee katika mahangaiko yetu.Wayne ni wakati muafaka sasa wa kufanya maamuzi katika maisha yako na kuitafuta amani ya moyo?
? Chris sina hakika kama nitaipata hiyo unayoiita amani ya moyo.Nimeumizwa sana na moyo wangu umejaa hasira na visasi kwa Emmy.Moyo wangu utakuaje na amani wakati kila ninapotafuta furaha ya maisha yangu anatokea mtu mmoja na kuiharibu?.Siwezi kuwa na amani Chris?? nikasema
? Wayne amani ya moyo inapatikana pale tu unapomrudia muumba wako.Mkubali Yesu sasa kama bwana na mwokozi wa maisha yako ,mtegemeze yeye katika kila jambo na nina hakika maisha yako yatakuwa na furaha.Achana na anasa na starehe za dunia hii bali yatafute maisha ya mbinguni.Nakuha
kikishia ndugu yangu utakapompokea Yesu na kumfanya kuwa ni bwana na mwokozi wa maisha yako utakuwa na amani.Hautasumb
uliwa kamwe na historia ya maisha ya nyuma.Mungu atakubariki ,atakupa amani,atakupa mke mwema,atakupa familia,atakupa kila unachokihitaji.Tazama mimi ,nina amani ya moyo.Nimejifunza kusamehe,nimejifunza kumtolea Mungu mateso na maumivu yangu yote.Nina hakika hata wewe ukiwa ndani ya kristu utajifunza kusamehe,utawasamehe wale wote waliokutenda vibaya? akasema Chris.Nikamuangalia na kusema
? chris ungekuwa mahala pangu,ungeweza kumsamehe Emmy kwa mambo aliyonitendea?
? katika Zaburi 86:5 maandiko yanasema "Kama wewe Bwana u mwema, umekuwa tayari kusamehe, na mwingi wa fadhili kwa watu wote wakuitao".Siku zote Mungu yuko tayari kumsamehe mtu yeyote anayetubu dhambi zake .Kama Mungu yuko tayari kumsamehe mtu yeyote anatufundisha kwamba hata sisi tuwe tayari kusamehe wenzetu hata katika zile dhambi kubwa walizotutenda.Kama Emmy angetambua kosa lake na kuomba msamaha ningemsamehe.? Akasema Chris
? wayne nakushauri kama ndugu yangu,msamehe Emmy na uyaanze maisha yako mapya.yaliyopita yatabaki historia na utayafurahia mabadiliko.Utajifunza biblia,utamfahamu Mungu na utampenda.Ni wakati wa kufanya mabadiliko sasa?
?Chris maneno yako yana ukweli ndani yake.Ni kweli ninahitaji amani ya moyo,ninahitaji kuyaanza upya maisha yangu.Ninahitaji kuisahau historia yangu ya huko nyuma.Niko tayari kwa hilo na niko tayari hata kuokoka na kuishi maisha mapya lakini kabla ya kufanya hivyo kuna jambo ambalo ninataka kulifanya?
? jambo gani Wayne?
? Ninataka kwenda mapumzikoni mbali na hapa.Nataka nikatulize akili yangu kwanza kabla ya kufanya maamuzi yoyote kuhusiana na maisha yangu yajayo.Nimefikiria kwenda Zanzibar.Nimewahi kwenda Zanzibar na Clara ni sehemu nzuri na nina hakika itanisaidia sana kuifanya akili yangu irudi katika hali ya kawaida.?
?Hilo ni wazo zuri Wayne.Ni na hakika endapo utachukua mapumziko hayo yatakusaida sana katika kuifanya akili yako itulie na kuweza kufanya maamuzi yenye kufaa.Nakubaliana nawe moja kwa moja kuhusu suala hilo?
? Ahsante sana Chris kwa kulitambua suala hili.Nitakaporejea tutaongea kwa undani zaidi kuhusu masuala uliyoniambia lakini kwa sasa sina jibu la moja kwa moja kuhusiana na masuala hayo.Kufanya maamuzi makubwa kama hayo kunahitaji utulivu mkubwa wa akili.?
? Hayo unayoyasema Wayne ni ya kweli kabisa lakini nitazidi kukuombea ili maisha yako yabadilike na bwana atakwenda kufungua milango ya moyo wako na utakuwa mpya tena?
Chris aliendelea kunipa moyo na maneno ya faraja japokuwa bado kichwa changu kilikuwa kizito kwa mawazo
***********************
Saa nne na nusu za asubuhi Sheila na James wakawasili makaburini kama James alivyokuwa ameomba.Alitaka kuliona kaburi la mtoto wake Baraka.Wote walikuwa katika mavazi meusi.Sheila aliwaongozaJames na walinzi wake wawili hadi katika kaburi la Baraka.
? Hapa ndipo alipozikwa Baraka? akasema Sheila
James akalitazama kaburi lile .Machozi mengi yakamtoka.Akavua miwani na kujifuta machozi.
? Baraka mwanangu ninasikitika sikupata hata nafasi ya kukuona na kukaa nawe japo kidogo.Umeondoka katika wakati ambao ninakuhitaji sana.Nitakuenzi katika siku zote za maisha yangu.? Akasema James kwa sauti ndogo halafu akachukua shada la maua toka kwa mmoja wa walinzi wake akaliweka juu ya kaburi la mwanae.Akalibariki kaburi lile wakaondoka.
? Sheila ninakushukuru sana kwa taarifa zote.Ninakushukuru kwa kunieleza ukweli kuhusu mwanamke ambaye nilidhani nimeelekezwa kwake kumbe nilikuwa nimepotea.Emmy ni mwanamke mbaya sana.Jana usiku nilifanya maombi na nikaonyeshwa ubaya wake.Emmy ni mwanamke katili sana.Katika maombi niliuona ukatili aliomfanyia mwanangu Baraka.Ninaomba usimweleze Emmy kitu chochote kuhusiana na wewe kuonana nami.Nitamuita na kuongea naye baadae.Ninataka nimsalimie tu na siku ya kesho nitaondoka.Sina hamu ya kuendelea kukaa tena hapa Tamnzania kwa sababu kitu kilichonileta tayari nimekwisha kikosa.? Akasema James wakiwa garini .Halafu akaingiza mkono mfukoni na kutoa kitita cha noti
? Sheila hii ni ahsante yangu kwa yote uliyoniambia.Nisingeweza kufahamu chochote bila ya wewe.Nadhani pesa hizi kidogo zitakusaidia kutatua matatizo yako yote madogo madogo.Ninachoweza kuusia Sheila jitahidi usiwe kama Emmy.Jitahidi uishi maisha ya amani na upendo daima? akasema James halafu akamwambia dereva wake asimamishe gari.
? Sheila nadhani itakuwa vyema kama ukishuka hapa na ukachukua taksi .Mimi ninaeleka moja kwa moja hotelini kwani sitaki mtu yeyote afahamu kuhusu uwepo wangu hapa Arusha.? Akasema James kisha akaagana na Sheila akashuka akakodi taksi na kurejea kwake
************************
Emmy akiwa nyumbani kwake akiuguza majeraha aliyoyapata kutokana na kipigo alichopewa na Wayne jana usiku mara simu yake ikaita.Zilikuwa ni namba ngeni kabisa katika simu yake.
? Hallo ? akaita Emmy baada ya kupokea simu
? Hallow naongea na nani? Ikasema sauti ya upande wa pili
?mimi naitwa Emmy.wewe nani mwenzangu?
? Mimi naitwa James,..habari yako emmy? Emmy akastuka
? james ?!!
? Ndiyo James.Umenisahau Emmy?
? Sijakusahau James.Habari yako?
? habari yangu nzuri sana James.habari za siku nyingi? Mbona unatumia namba za Tanzania? Uko wapi? Akauliza Emmy kwa wasi wasi
? Niko Tanzania?
? Tanzania? Umekuja lini? Mbona unakuja kimya kimya? Akauliza Emmy
? hapa ni nyumbani Emmy kwa hiyo sina haja ya kutoa taarifa kwamba ninarudi.? Akasema james
? nafurahi kusikia umerudi James.?
? Emmy uko wapi mida hii?
? Niko nyumbani kwangu,wewe uko wapi?
? Nimefikia hotelini.Ninakuomba ujiandae leo jioni nina hitaji kuonana nawe.Ni siku nyingi sijakuona mpenzi wangu nina hamu sana na wewe.Nahitaji kuupitisha usiku wa leo nikiwa nawe malkia wangu? Akasema James.uso wa Emmy ukachanua kwa tabasamu
? usijali darling nitakuja.Hata mimi nina hamu mno na wewe.Umefikia hoteli gani? Nina hamu kubwa ya kukuona mpenzi wang ni siku nyingi sana hatujaonana.?
James akamuelekeza hoteli aliyofikia na kukata simu
? Ouh jamani ! James amerudi. Kwa nini amefikia hotelini? Hoteli aliyofikia ni hoteli ya gharama kubwa sana hapa Arusha na ninafikiri atakuwa ana pesa za kutosha.Ngoja nijiandae nikamuone.Hata kama nina vidonda usoni nitamuona hivyo hivyo.James ananipenda na chochote nitakachomwambia lazima atanisikiliza.Nina hakika hana taarifa zozote kuhusiana na Baraka kwani yeye ndiye baba yake mzazi.? Akawaza emmy huku akiinukana kwenda kujitazama majeraha yake katika kioo
? siyo majeraha makubwa sana.Akiniuliza nitamwambia kwamba nilipata ajali ndogo ya gari ndiyo maana nikachubuka namna hii.Yule mshenzi alitaka kuniua jana.kama si Chris kutokea angenifanyia kitu kibaya sana.Sitaki tena madawa ya yule mganga kwani jana hazikuweza kunisaidia.Aibu niliyoipata jana ni kubwa sana kwani lile pembe la ng?ombe alilonipa nitembee nalo mkobani wakati wa kwenda kumuona Wayne lilianguka na watu wote wakaliona.Nadhani hata wayne aliliona pia.Ilikuwa ni aibu kubwa mno.Kwa nini yule mganga asababishe niaibike kiasi kile? Kila aliyekuwepo pale anatambua kwamba mimi ni mshirikina.Ninaogopa hata kutembea mtaani kwa aibu niliyoipata.Kwa sasa nitalazimika kutafuta namna nyingine ya kumpata Wayne lakini si kwa kutumia waganga wa kienyeji.Nimegundua kwamba waganga hawa ni walaghai na hawana msaada wowote.Kama dawa zao zingekuwa za kweli basi jana nisingeaibishwa na Wayne kiasi kile..Mganga yule alinihakikishia kwamba mara tu Wayne atakaponiona atastuka na kujenga tabasamu usoni mwake na atataka nirudiane naye lakini haikuwa hivyo.? Akawaza Emmy na mara picha ya tukio la jana ikamjia kichwani
? Gosh ! niliiona sura yake alikuwa amekasirika sana.Sijawahi kumuona Wayne akiwa katika hali ile. Ninafikiria kuacha kumfuatilia na kumuacha aendelee na maisha yake lakini siwezi kuishi bila ya yeye.Lazima nipambane nimrudishe wayne kwangu.? Akawaza Emmy
TUKUTANE SEHEMU IJAYO.......
 
BEYOND PAIN
SEHEMU YA 33
MTUNZI 😛ATRICK.CK
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
Kwa nini yule mganga asababishe niaibike kiasi kile? Kila aliyekuwepo pale anatambua kwamba mimi ni mshirikina.Ninaogopa hata kutembea mtaani kwa aibu niliyoipata.Kwa sasa nitalazimika kutafuta namna nyingine ya kumpata Wayne lakini si kwa kutumia waganga wa kienyeji.Nimegundua kwamba waganga hawa ni walaghai na hawana msaada wowote.Kama dawa zao zingekuwa za kweli basi jana nisingeaibishwa na Wayne kiasi kile..Mganga yule alinihakikishia kwamba mara tu Wayne atakaponiona atastuka na kujenga tabasamu usoni mwake na atataka nirudiane naye lakini haikuwa hivyo.? Akawaza Emmy na mara picha ya tukio la jana ikamjia kichwani
? Gosh ! niliiona sura yake alikuwa amekasirika sana.Sijawahi kumuona Wayne akiwa katika hali ile. Ninafikiria kuacha kumfuatilia na kumuacha aendelee na maisha yake lakini siwezi kuishi bila ya yeye.Lazima nipambane nimrudishe wayne kwangu.? Akawaza Emmy
ENDELEA????????.
Saa moja za jioni ilimkuta Emmy tayari amekwisha ifka katika hoteli hii kubwa ya kitalii.Alikuwa amependeza vilivyo.Alitaka kuonekana mrembo mbele ya james mtu ambaye alikuwa ni mpenzi wake wa siku nyingi .Taarifa zake tayari zilikuwapo mapokezi,akapok
elewa na kupelekwa hadi katika chumba cha james.Nje ya chumba kile kulikuwa na walinzi wawili waliokuwa wanalinda.Emmy akakaribishwa kwa heshima kubwa sana.Mlango wa chumba cha james ukafunguliwa akaingia ndani.Alishangazwa na uzuri wa chumba kile.Ameingia hoteli nyingi sana na hakuwahi kuoa hoteli iliyokuwa nzuri kama hii
? james !!! akasema Emmy kwa mshangao
? Emmy ? akasema James
Emmy akamkimbilia na kumkumbatia
? Ouh my love?.? Akasema Emmy
? nashukuru umerudi mpenzi wangu.Nilikuwa nakuota usiku na mchana lini utarudi.Nashuku
ru Mungu umerudi salama? akasema Emmy akiwa bado amemkubamtia james
? I?m back now my love..? akasema James na kumbusu Emmy mdomoni na ndipo alipoona vidonda usoni
?What happened?Mbona una vidonda usoni? Akauliza James
?Nilipatwa na ajali ndogo ya gari nashukuru Mungu sikuumia sana.Nilipatwa na mikwaruzo kidogo.?
? Pole sana mpenzi wangu? akasema James na kumbusu tena mdomoni kisha akamshika mkono na kumuongoza hadi sofani.
? Nimefurahi nimekuona tena Emmy.Bado unawaka kama zamani.Ninakupenda sana malaika wangu? maneno yale yakaufanya uso wa Emmy uchanue kwa tabasamu .
? Hata mimi nimefurahi mno kukuona tena mpenzi wangu.James umebadilika sana.Ilibaki kidogo nikupotee kama ni wewe kweli.Umenenepa sana James? akasema Emmy
? Emmy kabla hatujaendelea mbele na maongezi yetu kuna kitu ambacho unatakiwa ukifahamu.Kwa sasa ninafahamika kama Nabii James.Unaponiita jina langu unatakiwa kuanza na neno nabii?
? nabii James? Emmy akashangaa
? Ndiyo Emmy.Kwa hivi sasa mimi ni mpakwa mafuta wa bwana.Ninamtumikia bwana.Mbona umestuka sana kusikia mimi ni Nabii?akauliza James
? Nimestuka kwa sababu siktegemea hata siku moja kama ungeweza ukafanya kazi kama hiyo.Ninafahamu ulisomea utaalamu mwingine kabisa na si uchungaji.?
? Ndiyo emmy.Nilisomea mambo mengine kabisa lakini bwana alikuwa na kusudi na mimi na aliinita ili anitumie katika kazi zake na mimi nimeitika na kwa sasa ninamtumikia yeye pekee? akasema James
? Nimefurahi sana kwa mabadiliko haya makubwa uliyoyafanya james.?
? Ahsante sana Emmy.Ninaweza kusema kwamba bwana amenibariki na hivi sasa maisha yangu ni mazuri mno.Nina fedha za kutosha na nina uwezo wa kufanya lolote hapa duniani.Mambo yote haya ni kwa ajili yetu sisi wawili.Mimi na wewe? akasemaJames na Emmy akainuka pale alipokuwa amekaa na kwenda kumkumbatia huku akimwagia mabusu kemkem.
?Kwa sasa ninaishi Ulaya.Nina majumba katika nchi nyingi za ulaya na ninafanya kazi zangu za kinabii huko na kama mambo yatakwenda vizuri basi hata wewe utahamia Ulaya na tutaishi huko kwa amani kwa raha mustarehe? akasema James na kuzidi kumchanganya emmy
Waliongea mambo mengi na baadae wakaenda kupata chakula cha usiku halafu wakaelekea chumbani.Emmy alianza mautundu yake ili kumuhamasisha James kingono lakini kila alipojaribu hakukuwa na muitikio wowote toka kwa James .Emmy akashangazwa na hali ile
? james what happened? Nina hamu na wewe sana.Ni miaka mingi sijakuona.Nina hamu na penzi lako? akalalama Emmy kwa sauti nyembamba huku akiwa tayari mtupu kabisa.
James akamvuta kwake na kumbusu kisha akasema
? Emmy kabla ya kufanya mambo haya tuna mambo mengi ambayo nataka tuyaongee.Mimi na wewe ni wapenzi wa muda mrefu sana toka tukiwa shuleni.Ninakupenda na katika maisha yangu sijawahihata mara moja kukusaliti kwa kutembea na mwanamke mwingine yeyote..Kokote niendako nimekuwa nikijua kwamba nina mpenzi wangu ambaye ananisubiri.Sikuwa na safari ya kuja Tanzania hivi karibuni lakini nilionyeshwa katika maono kwamba nije Tanzania kuna mwanamke wa maisha yangu ambaye ni wewe Emmy.Kwa hiyo usiwe na haraka na mambo haya.Nimekuja hapa kwa sababu yako? akasema James. Halafu akambusu Emmy na kuendelea
?Emmy nina malengo makubwa na wewe.Ninataka tukaishi sote Ulaya .Nataka nikufanye malkia wa himaya yangu lakini kabla ya kufanya hivyo nataka kusikia toka kwako je unanipenda kwa moyo wako wote kama ninavyokupenda mimi?
Emmy akamuangalia James na kusema
? My love hilo sio swali la kuniuliza wakati unafahamu fika upendo wangu kwako hauna kipimo.Ninakupenda kuliko kitu chochote.Sijawa
hi kumpenda mwanaume kama ninavyokupenda James.Hata ulipopotea nimekaa mwenyewe siku zote hizi nikijua kwamba siku moja lazima utarudi tu ili tuje tuendeleze mapenzi yetu. James nakupenda sana,zaidi ya unavyofikiri? akasema Emmy
? nafurahi kusikia hivyo Emmy.Nakumbuka wakati ninaondoka nilikuhakikishia kwamba nitarudi siku moja kwa ajili yako.Ni muda mrefu umepita toka wakati huo na leo nimetimiza ahadi yangu.I?m back for you.Naomba unihakikishie Emmy kwamba kwa muda huu wote haujawahi kuwa na mahusiano na mwanaume yeyote yule.Kama umewahi kuwa katika mahusiano naomba unieleze na nitakuelewa kwani sisi ni wanadamu na wakati mwingine huwa tunashindwa kuvumilia na kuanguka.?
? James my love,sijawahi kuwa na mpenzi chini ya jua zaidi yako wewe.Ni wewe pekee ambaye ninakufamu kama mpenzi wangu na ndiyo maana siku hizi zote nimekuwa nikijitunza ili nisijiinginze katika mahusiano nikijua kwamba siku moja utarejea tu? akasema Emmy .James akatabasamu na kumbhusu.
? nashukuru kwa kunitunzia penzi langu Emmy.Ninakupenda sana.?
?hata mimni nakupenda sana James.Ninashuku
ru Mungu umerudi .Nilikuwa mpweke sana? akasema Emmy huku akimkumbata zaidi James.Kimya kifupi kikapita halafu James akasema
? Emmy wewe ni mpenzi wangu na ninaomba nikueleze ukweli kuhusu maisha yangu.Ninakueleza ukweli kwa sababau ninakupenda na kukuamini na ninakuomba nitakayokueleza hapa usimwambie mtu yeyote?
? Niamini mpenzi wangu.Siwezi kumweleza mtu yeyote yule ? akasema Emmy
James akafikiri kidogo na kusema
? Emmy kwa sasa sina tena nguvu za kiume na siwezi kufanya mapenzi tena?
Emmy aliyekuwa amemkumbatia james akastuka na kuinuka akamuangalia James kwa macho makali ya mshangao
? Sijakuelewa James unamaanisha nini unaposema kwamba huna tena nguvu za kiume?
? Sikiliza Emmy.Najua unataka tufanye mapenzi sasa hivi lakini naomba niwe wazi kwako kwamba kwa sasa siwezi kufanya hivyo.Siwezi kufanya mapenzi.Sina uwezo huo.Sina tena nguvu.Jogoo wangu hawiki tena?
?How did that happen James? Ulikuwa kidume wa shoka.Imekuaje tena? Nini kimetokea? Tafadhali naomba uniambie? akasema Emmy.James akamtazama kwa tabasamu na kusema
? Nitakwambia Emmy kwa sababu ninakuamini.?
?Tafadhali niambie James.Uliumwa? Nini kimepelekea upoteze nguvu zako?
? Ni hadithi ndefu sana lakini kwa ufupi ni kwamba nilikubali kutolewa nguvu zangu za kiume na wala sikuumwa wala kuwa na matatizo yoyote? akasema James Emmy akazidi kuchanganyikiwa
? James unazidi kunichanganya.Nani alikumaliza hizo nguvu?
? Emmy naomba ufahamu kwamba mimi si nabii wa kweli.Ninatumia nguvu za giza katika unabii wangu na ndiyo maana nimekuwa ni nabii ninayesifika kwa kuwa na nguvu za ajabu sana?
Kauli ile ya James ikamtetemesha Emmy.Jasho likaanza kumchuruzika usoni
? Ouh my gosh ! James?
? Mbona unashangaa Emmy.Hili si jambo la ajabu hata kidogo.Watu wengi siku hizi wanajifanya manabii wengine wanajiita mitume lakini wengi wao si wakweli na wanatumia nguvu za giza katika kutenda miujiza na kuwalaghai watu?
? J?ja..j.James.. imetokeaje hadi ukaingia katika mambo hayo? Akauliza Emmy huku sauti yake ikitetemeka
?Nilishawishiwa kuingia huko na rafiki yangu mmoja anayetoka nchini Nigeria na yeye pia ni nabii kama mimi.Nilipokubali nilipelekwa nchini Nigeria na huko nilipewa machaguo matatu ya kuchagua ili niweze kupata nguvu na uwezo wa kutenda miujiza.Kwangu mimi chaguo rahisi lilikuwa ni kuondoa nguvu zangu za kiume yaani kuharibu uwezo wangu wa kufanya tendo la ndoa na hivyo siwezi kabisa kupata mtoto wala mke.Baada ya hapo nimekuwa ni mtu mwenye nguvu kubwa ya kutenda miujiza mikubwa ,kutabiri mambo yakawa kweli na nimekuwa ni tajiri mkubwa.Nina pesa lukuki na sioni furaha ya maisha bila ya kuwa na mke na mtoto.Emmy kuna kitu ninataka nikuulize?
? Uliza James? akasema Emmy kwa wasi wasi.
? Siku moja nikiwa katika maombi niliona maono kwamba mimi na wewe tulibahatika kupata mtoto.Naomba unihakikishie je maono haya ni ya kweli:? Mimi na wewe tuliwahi kuwa na mtoto? Ninahitaji sana mtoto kwa sasa ambaye atakuwa mrithi wa mali zangu nyingi nilizonazo?
Emmy alistuka sana kwa kusikia maneno yale toka kwa James.Alihisi baridi kali mwilini mwake.Alikosa neno la kusema
? emmy naomba unijibu.Ni kweli kuhusu jambo hii? Akauliza james baada ya kuona Emmy amekaa kimya
? James jambo hili halina ukweli wowote.Mimi na wewe hatujawahi kuwa na mtoto kamwe.Nilitegemea ukirudi tutafute walau mtoto mmoja lakini kwa sasa haiwezekani tena? Akasema Emmy
? Nafurahi kusikia uthibitisho huo toka kwako.Inawezekana maono yangu hayakuwa ya kweli.Hata hivyo kwa kuwa tayari umeijua siri yangu kuna kitu ambacho ni lazima unywe.? Akasema James huku akiinuka.Emmy alikuwa anatetemeka kwa woga.Baada ya dakika mbili james akarejea akiwa na chupa mkononi akampatia Emmy
? Kunywa hii? akasema James.
? Emmy akaishika chupa ile yenye rangi ya kahawia akaifungua kifuniko na huku mkono wake ukitetemeka akaiweka mdomoni.Kilikuwa ni kinywaji kitamu na chenye harufu nzuri.Wakati akinywa James akamuwekea mkono kichwani na kuanza kuongea maneno ambayo Emmy hakuyafahamu.Ghafla kinywaji kile alichokuwa anakunywa Emmy kikageuka damu.Emmy akataka kutema James akamuangalia kwa jicho kali akalazimika kunywa damu ile na kuimaliza.Ghafla akaanza kuona mwili wake unabadilika na kuwa wa moto sana.
? James nimeanza kujisikia vibaya sana.Mwili umekuwa wa moto.Umenipa nini hiki? Akasema emmy kwa wasi wasi.James akachukua mafuta toka katika kichupa kidogo akampaka mikononi na lile joto alilokuwa analisikia Emmy likatoweka.
? Emmy naomba unisikilize vizuri.Tayari ninafahamu kila kitu kuhusu wewe.Ninafahamu uongo wako wote uliokuwa unanidanganya.U
linidanganya kwamba hauna mwanaume kumbe tayari ulikwisha olewa,kibaya zaidi ulinidanganya kwamba hatukuwahi kuwa na mtoto kumbe wakati ninaondoka nilikuacha ukiwa na mimba changa na ukazaa mtoto wa kiume anaitwa Baraka.Bwana aliyekuoa aligundua kwamba Baraka hakuwa mwanae ukatokea mtafaruku mkaachana,ukaenda kwa mganga na kumtoa kafara mtoto wangu wa pekee kabisa.Emmy nimeumia sana kwa mambo uliyonifanyia.Huu ni ukatili mkubwa sana ambao hauvumiliki.Ulidhani kwamba sintafahamu unyama ulioufanya kwa mtoto wangu wa pekee? Ingekuwa ni kwa kunidanganya mimi nisingekuwa na matatizo lakini kwa kumuua mtoto wangu kwa sababu zako binafsi imeniumiza mno.?
Emmy alistuka sana na mwili wake ukawa unatetemeka kwa woga
? James..? akasema Emmy lakini James akamzuia.
? Emmy sitaki uongee chochote,umenisikitisha sana na hapa nilipo moyo wangu unawaka kwa hasira .Naomba nikufahamishe kwamba leo hii ni siku yako ya kulipia uovu wako.? Akasema James huku uso wake ukianza kubadilika.Mwili wake ulionekana kama vile unaanza kujaa.
? Ouh Mungu wangu niokoe na balaa hili? akasema Emmy baada ya kuona namna James alivyoanza kubadilika na kuwa na umbo la ajabu.Mwili ulikuwa unamtetemeka kwa uoga .
? Emmy sitaki kupoteza wakati.Ni wakati wako wa kulipa sasa uovu wote ulioufanya na hasa kitendo cha kumtoa mwanangu kafara kwa sababu ya mwanaume..Nitakupa adhabu ambayo itakuwa funzo kwa wengine pia.Baraka alikuwa ni mwanangu wa pekee kabisa na kwa sasa ambapo sina tena uwezo wa kupata mtoto Baraka angekuwa ndiye mrithi wa utajiri wangu wote.Mali zote nilizonazo,utajiri wote nilionao hauna maana bila ya kuwa na mtoto au mke.Hakuna mwanamke ambaye anaweza kukubali kuishi na mwanaume ambaye hawezi kumtimizia haja zake za mwili.Kwa maana hiyo maisha yangu hapa duniani hayana thamani tena na yote hii ni kwa sababu yako Emmy kwa sababu ya tamaa zako.? Akasema James huku mwili wake ukitetemeka kwa hasira
?James naomba unisamehe..nimekosa sana na ninaomba msamaha wako..ninakupenda James na niko tayari kuishi nawe hata kama hauna nguvu za kiume.Nitavumilia yote lakini naomba usinipe adhabu yoyote James.Ni kweli nilimtoa kafara Baraka kwa mizimu nikitegemea kwamba Wayne atarudi kwangu lakini haikuwa hivyo.James niko chini ya miguu yako na niko tayari kufanya chochote unachokitaka? akalia Emmy
? machozi yako ya kinafiki hayawezi kunifanya nikageuza mawazo yangu.Lazima leo nikupe adabu kali sana.? Akasema James halafu aka chukua kichupa kidogo cha mafuta akamrushia Emmy matone na mara tu matone yale yalipomgusa Emmy mwili ukaanza kumuwasha sana.Akaanza kujikuna.Kadiri alivyokuwa anakuna ndivyo mwili ulivyozidi kumuwasha .Ghafla vikaanza kujitokeza vitu kama unga unga kila alipojikuna na taratibu ngozi ya mikono ikaanza kuwa ngumu.Mwili ukaendelea kumuwasha sana na joto likaongezeka.Wakati akijikuna James alikuwa amenyoosha mkono akiongea maneno ambayo Emmy hakuyafahamu.Emmy akaanza kuhisi joto kali mno kana kwamba alikuwa karibu na moto mkali.
?James ..james..james..!!!! ninaungua..james ninaunguaaaa..!!! akapiga kelele Emmy baada ya kuanza kuhisi alikuwa anaungua.James hakumjali akaendelea kuongea yale maneno yake aliyoyafahamu mwenyewe akiwa amefumba macho na mkono wake wa kulia akiwa ameuelekeza kwa Emmy.Ghafla Emmy akaanza kuona kizungu zungu na aliona kana kwamba kila kitu kilikuwa kinazunguka kwa kasi akaendelea kupiga kelele.Alihisi kuungua mwili mzima kwa moto mkali sana na taratibu akaanza kuhisi mabadiliko katika mwili wake.Ngozi yake ilianza kuwa ngumu.Lilikuwa ni tukio la kutisha sana.Moshi mwingi ukajaa mle chumbani na baada ya dakika kama tano hivi moshi ule ukatoweka na hapo ndipo kilitokea kitu cha ajabu mno.Emmy alikuwa ameguka nyoka lakini kichwa kilibaki kuwa cha binadamu.Lilikuwa ni joka kubwa la kutisha.James akalisogelea joka lile akalimwagia mafuta kichwani na ghafla Emmy akazinduka na kupiga ukelele mkubwa sana baada ya kujikuta katika umbo lile.
? James?.James naomba unisamehe?Nimek
ukosea sana na usinifanye hivi? akalia kwa nguvu Emmy ambaye bado mwili wake ulikuwa unatoa mvuke.
?Huo ndio mshahara wa uovu wako.Ulimkatili mwanangu na haya ndiyo malipo yake.Hii ni adhabu yako na utaishi hivyo kwa siku zote za maisha yako.Nataka dunia yote wafahamu uovu ulioufanya na ili liwe fundisho kwa wengine.Kazi iliyonileta imekamilika na hautaniona tena katika maisha yako Emmy na wala usihangaike kunitafuta kwani mimi si binadamu wa kawaida tena.I?m a half devil.Nakutakia kila la heri katika maisha yako mapya? akasema James halafu akafungua mlango na kuwaita wale walinzi wake wawili.Wakasimama kati kati ya chumba huku wameshikana mikono halafu James akawashika vichwani akaongea maneno yake aliyoyajua mwenyewe na kitu kama wingu kikatokea mle chumbani na katika wingu lile James na vijana wake wakapotea.Wingu lile lilipotoweka James na watu wake hawakuwapo wala kila kitu chao.Emmy akapiga kelele kubwa sana.
Kelele alizopiga Emmy zikawafikia wahudumu ambao walifika mara moja katika chumba kile ili kujua kama kuna tatizo lolote.Mlango haukuwa umefungwa wakaingia ndani na ndipo walipokutana na kitu cha kutisha sana.Kulikuwa na joka kubwa mno lenye kichwa cha binadamu.Muhudumu mmoja akaanguka na kuzimia kwa uoga.Mwingine akakimbia na kwenda kutoa taarifa kuhusiana na tukio lile.Kwa haraka wakataarifiwa polisi ambao walifika pale haraka sana na kuelekea chumbani.Waliingia chumbani mle wakiwa na silaha zao tayari kwa lolote linaloweza kutokea na wao kama wengine wote walistushwa mno na tukio lile la ajabu.Hakuna aliyewahi kuliona tukio kama lile la nyoka mwenye kichwa cha binadamu.Emmy alikuwa analia kwa nguvu.
Taarif za kuonekana nyoka mwenye kichwa cha binadamu zilianza kusambaa kwa kasi usiku ule na ndani ya muda mfupi watu wakaanza kufika pale hotelini hususan waandishi wa habari walotaka kufahamu ukweli wa tukio hilo.Kamanda wa polisi wa mkoa wa Arusha naye aliwasili katika hoteli ile na akathibitisha kutokea tukio lile kwa vyombo vya habari vilivyokuwapo pale hotelini.
Upelelezi wa chanzo cha tukio lile ukaanza mara moja.Wahudumu walihojiwa na wakatoa maelezo yao kwamba chumba kile kilipangwa na mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la James ambaye alijisajili hotelini hapo kama mfanya biashara wa kimataifa.Kitu cha ajabu ambacho kiliwashangaza wengi ni pale ambapo picha ya james haikuonekana katika kamera yoyote ya usalama pale hotelini.Yalikuwa ni mambo ya kushangaza sana.Kwa kupitia simu iliyokutwa katika mkoba wa Emmy wakafanikiwa kuzipata namba za baba yake wakampigia.Akiwa amelala chumbani kake akitafakari mara simu yake ikaita.Aliitazama simu ile ikiita akasita kuipokea.
?Baada ya aibu yote hii aliyotutia Emmy anadiriki kunipigia simu? Anataka nini? Akajiuliza baba yake Emmy lakini mwishowe akaamua kuipokea simu ile.
?hallo? akasema
? Hallo ndugu samahani naomba kukuuliza unamfahamu mwenye namba hii ya simu? Ikauliza sauti ya upande wa pili
? Ndiyo ninamfahamu?
? Mna mahusiano gani naye?
? Ni mwanangu? akajibu baba yake Emmy kwa wasi wasi
? Mbona unaniuliza hivyo nini kimetokea? Wewe ni nani? Akauliza baba yake Emmy
?Unaongea na afisa wa polisi hapa .Kuna tukio limetokea hapa Meru view hotel usiku huu linalomuhusisha mwanao.Tunakuomba ufike hapa mara moja?
? Afande nini kimetokea? Nini kimemtokea mwanangu? Akauliza baba yake Emmy kwa mstuko
? Sintaweza kukwambia kwa simu lakini ninakuomba ufike hapa hotelini mara moja ili u weze kushuhudia wewe mwenyewe.? Akasema afisa Yule wa polisi na kukata simu.Baba yake Emmy jasho lilikuwa linamtiririka.
? baba Emmy nini kimetokea? Akauliza mke wake ambaye naye alistushwa na mabadiliko yale ya ghafa ya mume wake
? Kuna afisa wa polisi amenipigia simu na kunitaarifu kwamba kuna tatizo limemtokea Emmy.?
? Emmy !!! mama yake naye akastuka
? Ndiyo..lakini hajasema ni tatizo gani?
? Ouh Emmy amefanya nini tena ? akajibu mama yake huku akilia
? Nyamaza usilie.Nataka nielekee huko nikaone nini kimetokea? akasema baba yake Emmy
? Tunakwenda sote?
? Hapana ,wewe utabaki hapa hapa.Vipi kama kuna tatizo kubwa?
? hapana baba Emmy.Lazima na mimi niende nikashuhudie kilichompata mwanangu. Akasema mama Emmy na wote wakainuka na kuanza kujiandaa.
*********************
Ni muda wa kwenda kulala sasa.Tayari tulikwisha fanya maombi ya usiku yaliyoongozwa na Chris.Nikiwa najiandaa kupanda kitandani mara simu yangu ikaita.Alikuwa ni baba mkwe.
?Hallo baba ? nikasema baada ya kupokea simu ile
? Wayne kuna tatizo limetokea? akasema baba mkwe
? tatizo !! ???nikastuka
?ndiyo kuna tatizo limetokea.Nimepigiwa simu na afisa wa polisi usiku huu akinitaarifu kwamba kuna tataizo limemtokea Emmy katika hoteli ya Meru view na amenitaka nifike huo mara moja?
? Umesema Meru View hotel? nikauliza
? Ndiyo?
? Huyo afisa wa polisi amesema ni tatizo gani limempata Emmy?
?Hajaniambia ni tatizo gani lakini amenitaka nifike mara moja?
?baba naomba unisubiri ninakupitia hapo nyumbani sasa hivi ili twende wote.Tafadhali usiende peke yako? nikasema na kukata simu.Nikavuta pumzi ndefu
? Emmy kafanya nini tena safari hii? Nini kimetokea katika hoteli hiyo? Nakumbuka hoteli hiyo ndiyo alifikia mtu anayeitwa james ambaye ni baba mzazi wa Baraka.Nini kimetokea hapo hotelini?Lazima kutakuwa na tukio kubwa ngoja niende nikashuhudie? nikawaza huku nikivaa nguo halafu nikatoka na kwenda kumgongea Chris nikampa taarifa zile na kwa haraka wote tukaondoka kuelekea kwa baba mkwe
? Kwa mujibu wa Sheila hoteli hiyo aliyoitamka baba mkwe ndiyo alifikia mtu anayeitwa James baba mzazi wa Baraka.Unadhani nini kinaweza kuwa kimetokea? Nikamuuliza Chris
?Sifahamu Wayne.Ngoja tukajionee wenyewe nini kimetokea? akasema Chris.Hatukuongea tena hadi tulipofika kwa baba mkwe.Tulimkuta akiwa katika hali ya wasi wasi mwingi
?Baba nini kimetokea? Nikamuuliza
? hata mimi sijui chochote wayne.Nimepigiwa simu usiku huu na afisa wa polisi akinitaka nifike hapo hotelini mara moja.Tusipoteze wakati twendeni haraka.? Akasema baba mkwe na wote tukaingia garini tukaelekea eneo la tukio
?Emmy atakuwa amefanya nini tena safari hii? Kama ni tukio linalowahusisha hadi polisi basi lazima litakuwa ni tukio kubwa ..Naomba Mungu asiwe amejeruhi mtu.? Akasema baba mkwe.hakuna aliyemjibu kila mmoja alikuwa anawaza lake.Nilianza kupata picha kwamba huyo mtu anayeitwa james lazima kuna kitu alitaka kufahamu kuhusiana na Emmy na ndiyo maana akamtaka Sheila wakaonane hotelini kabla hata hajaonana na Emmy.Sheila na Emmy walikuwa katika ugomvi mkubwa nina hakika lazima Sheila atataka kuitumia nafasi hiyo kumchafua Emmy kwa huyo bwana wake na kama atakuwa amemueleza ukweli kuhusiana na Baraka lazima kutakuwa na tukio kubwa limetokea hapo hotelini? nikawaza.
Tulifika hotelini na kukuta idadi kubwa ya askari wakilinda eneo hilo .Watu walikuwa wengi pia.Nilianza kutetemeka mwili baada ya kuuona umati ule mkubwa wa watu pamoja na askari wengi.
Baba mkwe akajitambulisha kwa askari,tukachukuliwa na kupelekwa kwa kamanda wa polisi wa mkoa ambaye alikuwapo pale hotelini,
?Lazima kutakuwa na tukio kubwa kiasi cha kuwakusanya watu wote hawa wa ngazi za juu mahala hapa.? Nikawaza baada ya kumuona pia na mkuu wa mkoa wa Arusha akiwa pembeni ya kamanda wa polisi wa mkoa.Miguu ilikuwa inanitetemeka.Tulisalimiana na mkuu wa mkoa na kamanda wa polisi wa mkoa halafu kamanda wa polia akatuvuta pembeni mimi ,baba mkwe na Chris kwa maongezi .Hakutaka mama mkwe asikie kile alichotaka kutuambia.
? Jamani kwanza nawaomba samahani kwa kwuasumbua usiku huu lakini kutokana na uzito wa tukio lililotokea imetulazimu kuwaiteni hapa .Emmy ni mwanao wa kumzaa mwenyewe?
?Ndiyo .Emmy ni mwanangu kabisa? akajibu baba mkwe
? Unaishi naye nyumba moja au yeye ana makazi yake mengine?
? Kwa sasa Emmy amekwisha olewa na ana kwake na huyu hapa ni mume wake ingawa kumetokea kutokouelewa baina yao na wakatengana? akasema baba mkwe
? Sasa baba kuna tukio limetokea usiku huu hapa hotelini.Kwa mujibu wa wahudumu wa hoteli hii walisikia kelele za mwanamke akiomba msaada na walipokimbia kwa ajili ya kwenda kumsaidia mwanao mle chumbani walikuta kitu cha ajabu sana?
? Afande naomba unieleze ukweli,mwanangu amefariki dunia? Akauliza baba mkwe
? Habana hajafariki dunia.?
? sasa nini kimemtokea? Akauliza baba mkwe huku akivunta pumzi kwa nguvu
? Ninyi ni wanaume na ninawaomba muwe na mioyo migumu lakini ukweli ni kwamba Emmy amegeuka nyoka?
Nilihisi mwili wangu wote umekufa ganzi kwa taarifa ile.Miguu haikuwa na nguvu ikanilazimu kumuegemea Chris ambaye naye alikuwa anatetemeka.Baba mkwe midomo ilikuwa inamcheza na hakuweza kuongea.Michirizi ya machozi ikaonekana machoni pake.Akaanguka chini.Haraka haraka askari wakafika na kumbeba wakamkimbiza katika gari la wagonjwa ambalo lilikuwapo pale hotelini kwa ajili ya kutoa msaada kwani ilitegemewa watu wengi wangepatwa na mstuko kwa tukio lile
? Afande naomba mnieleze ni nini hasa kilichotokea? Imewezekanaje Emmy ageuke nyoka? Nikamuuliza kamanda wa polisi wa mkoa .Kabla hajatujibu nikawaona maaskari wakiwa wamembeba mama mkwel katika machela wakimuwahisha katika gari la wagonjwa.Nadhani alikuwa amezidiwa kwani huwa ana matatizo ya shiniko la damu kwa hiyo alipomuona mume wake ameanguka ghafla naye akazidiwa..
? Wayne ni vigumu kusimuilia kuhusu mkasa huu kwani kila kitu kinaonekana kama muujiza fulani lakini tunaendelea kufanya uchunguzi na tutabaini nini chanzo cha tukio hili.Ninalihusisha tukio hili na imani za kishirikina kwani katika hali ya kawaida haiwezekani binadamu akabadilika na kuwa nyoka.? Akasema kamanda wa polisi.Chris akaondokana kwenda kufuatili hali ya baba na mama mkwe nikabaki nimesimama na wale askari.
? Afande ninaweza kuruhusiwa kwenda kumuona Emmy huko chumbani?
? Hapana Wayne.Kwa sasa haturuhusu mtu yeyote aingie mle chumbani hadi uchunguzi utakapokamilika.Tunataka pia kuhakikisha kwamba kunakuwa na usalama wa kutosha kwani hatuna uhakika kama kiumbe kile hakiwezi kuwa na madhara kwa biandamu na ndiyo maana unaona tumewatoa hata wageni wote waliokuwa vyumbani kwa ajili ya usalama wao? Akasema kamanda wa polisi.
? Afande Emmy amekutwa na nani chumbani? nikauliza
? hakukuwa na mtu yeyote chumbani zaidi ya Emmy peke yake.Chumba hicho alichokutwa na tukio hilo kilikuwa cha mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la James na ambaye haijulikani yuko wapi hadi mida hii.Tunahisi pengine yeye ndiye aliyetenda tukio hili na kisha akakimbia.? Akasema kamanda wa polisi.Nikainama na kufikiri halafu nikasema
?Afande kuna kitu naomba nikiseme ambacho naona kinaweza kusaidia katika uchunguzi kuhusiana na tukio hili.Kuna mwanamke mmoja anaitwa Sheila nina hakika atakuwa anafahamu kitu kuhusiana na jambo hili? nikasema na kumstua kamanda wa polisi wa mkoa
? Sheila ni nani? Akauliza
? Sheila ni rafiki mkubwa wa Emmy ?
? Kwa nini unasema hivyo Wayne? Akauliza kamanda wa polisi
? Jana nilikuwa safarini na Sheila tukitokea Mombo Tanga na tukiwa njiani alipigiwa simu na mtu mmoja aitwaye james na kumtaka waonane hapa hapa hotelini usiku.Nadhani atakuwa anafahamu kitu kuhusiana na kilichotokea.Endapo atakamatwa na kuhojiwa anaweza akatusaida kujua mahala aliko huyo James? nikasema
? Wayne unamfahamu huyo mtu anayeitwa James?
? hapana afande simfahamu na sijawahi kumuona .Nimemsikia jana kwa mara ya kwanza toka kwa Sheila lakini yeye ndiye chanzo cha mimi kutenganana mke wangu kwani aliwahi kuzaa mtoto na mke wangu tukiwa ndani ya ndoa kwa hiyo naweza kusema kwamba ni watu waliokuwa wana mahusiano ya kimapenzi ? nikasema.
Kamanda wa polisi akawaita maafisa watatu wa polisi akaongea nao halafu akanifuata.
? Wayne unafahamu mahala anakoishi huyo Sheila? akauliza
? Ndiyo afande.? Nikajibu
? Basi utaongozana na hawa maafisa wa polisi na kwenda kumchukua Sheila kwa ajili ya mahojiano.?
Tuliingia katika gari la polisi na kuondoka kwa kasi kuelekea nyumbani kwa Sheila.Kwa kuwa ilikuwa ni usiku ilinilazimu nimpigie kwanza simu ili kumfahamisha kwamba ninahitaji kuonana naye.Alistuka sana kwa nini ninataka kuonana naye usiku ule.Haraka haraka akafungua mlango na kupigwa na butwaa baada ya kugundua nilikuwa nimeongozana na maaskari .
? Karibui ndani.? Akasema kwa sauti ya kutetemeka.aliogopa sana
? Wayne kuna nini? Mbona usiku huu tena ukiwa na askari? Kuna tatizo gani? Akauliza Sheila kwa wasi wasi.
?Shela kuna tatizo limetokea usiku wa leo?
? tatizo gani?
? Emmy amepatwa na matatizo ?
? matatizo?
? Ndiyo amepatwa na matatizo.?
? Matatizo gani? akauliza kwa wasi wasi
? Alikuwa amekwenda kuonana na James na hatujui kilichotokea kati yao lakini naomba ufahamu kwamba Emmy amegeuka nyoka?
Pale pale Sheila akaanguka chini na kupoteza fahamu.Damu ikaanza kumtoka mdomoni Ikatulazimu kumpakia garini na kumkimbiza hospitali.Tulipomfikisha hospitali madaktari wakasema kwamba Sheila alikwisha fariki kitambo. Nilichanganyikiwa.
Tulirejea tena hotelini nikiwa sina nguvu kabisa.mambo yale yaliyotokea yalinimaliza kabisa nguvu.Nilitafuta sehemu nikaa kwani sikuweza tena kusimama.Mambo yaliyokuwa yanatokea yalikuwa ni kama filamu.Niliwasiliana na Chris akaniambia kwamba alikuwa ameongozana na baba na mama mkwe ambao walikimbizwa hospitali kutokana na mstuko walioupata.Nilimtaarifu kuhusianana kifo cha Sheila akastuka sana
*********************
Kulipambazuka tukiwa bado pale pale hotelini.Wageni wote waliondolewa na kupelekwa katika hoteli nyingine .Asubuhi hii kulikuwa na heka heka kubwa hapa hotelini.Tayari taarifa zilikwisha samba kila kona ya dunia kwamba kuna mwanamke amebadilika na kuwa nyoka .waandishji wa habari wa vyombo mbalimbali walifika asubuhi hii ili kuweza kuipata habari hiyo.Watu wote walizuiliwa nje ya hoteli na hakuna mtu yeyote aliyeruhusiwa kuingia ndani.
Nikiwa nimekaa sofani nikiwa na rafiki yangu Beka aliyefika usiku baada ya kumpigia simu akanifuata afisa mmoja wa polisi na kuniambia kwamba kamanda wa polisi wa mkoa anahitaji kuniona.Nikaongozana na Beka na yule afisa wa polisi hadi katika mlango mmoja wa chumba kilichokuwa na idadi kubwa ya askari wamesimama nje.Nilijua hapo ndipo kwenye tukio
? wayne,kuna mambo ambayo naomba uyafahamu kuhusiana na kinachoendelea hapa..Ni kwamba kwa sasa Emmy ametulia halii tena kama jana na anaweza kuongea.Ameongea nami na amesema kwamba anahitaji kuongea nawe.Je uko tayari kuingia na kuongea naye?
? Niko tayari afande ? nikasema
? Vizuri .sasa tunataka uongee naye na ufahamu nini kilichotokea nani alifanya tukio hilo? Huyu James yuko wapi na tunawezaje kumkamata?
? sawa afande? nikajibu lakini uso wangu ukionyesha uoga
? Usiogope Wayne tutakuwa karibu na hakuna kitu chocote kitakachokutokea? akanipa moyo kamanda wa polisi nikafunguliwa mlango na kungia ndani.Hakuruhusiwa mpiga picha yeyote yule kuingia mle chumbani.Nilikuwa peke yangu na askari wawili waliokuwa na silaha.Mwili wangu ukanisisimka baada ya kuliona joka lile kubwa la kutisha likiwa na kichwa cha Emmy.Toka nimezaliwa sijawahi kuona joka la namna ile.Nilikuwa natetemeka mwili mzima kwa hofu.Niliogopa sana.Sikutaka hata kusogea karibu zaidi.
?Wayne usiogope,siwezi kukudhuru.Tafadhali sogea karibu ,kuna mambo ninayotaka kuongea nawe.? Akasema Emmy.Hakuwa amebadilika kitu kichwani.Nywele zake ndefu ,uso wake wa kung?aa,nyusi zake zilizochongwa vizuri ,kope zake za bandia kila kitu kilikuwa vile vile.Kuanzia shingoni kushuka chini alikuwa na mwili wa joka la kutisha sana
? Sogea karibu Wayne? akasema Emmy
? Nikapiga hatua kumsogela lakini kwa tahadhari kubwa sana.Wale askari wawili waliokuwa mle ndani waliziweka tayari silaha zao endapo kungetokea jambo lolote baya.Nilikuwa ninatetemeka wakati nikimsogelea karibu
? Wayne naomba usiniogope mimi ni yule yule Emmy mke wako lakini kwa sasa nina mwili wa nyoka.Wayne nimekuita hapa ili niuungame kwako na kukuomba msamaha kwa mambo yote niliyowahi kukufanyia.Nimekufanyia mambo mengi mabaya sana na ambayo hayavumiliki hata kidogo.Hukupaswa kufanyiwa mambo yale niliyokufanyia,Ulinipa kila nilichokihitaji lakini sikuridhika na kutaka kupata zaidi.Ulijitahidi kunipa kila raha ya dunia lakini sikutosheka nikataka kupata raha zaidi.Kupenda starehe na anasa vimeniponza na haya ndiyo malipo yake? akasema Emmy.Macho yangu yalikuwa yanatoa machozi
?Wayne wewe ni mwanaume wa pekee kabisa katika hii dunia.Pamoja na kukufanyia mambo mengi,vitimbi vya kila aina lakini bado uliendelea kunipenda na kunijali na hukuwahi hata siku moja kunitolea lugha ya matusi na kashfa licha ya mimi kukutukana kila mara.Naomba nikiri kwako kwamba baada ya kuamua tuachane ndipo nilipouona umuhimu wako katika maisha yangu.Nilijiona kama nimekosa kitu fulani muhimu na ndipo nilipoanza jtihada za kuyarejesha mapenzi yetu tena.Nilienda kwa mganga Tanga ambaye alinidanganya kwamba atanisaidia ili uweze kurejea kwangu.Nilikubali kumtoa kafara mwanangu Baraka kwa ajili ya kurudiana nawe.Wayne naomba unisamehe kwa kosa hili kubwa nililolifanya.Sikuishia hapo niliendelea na uovu wangu na mwishowe nikamroga Clara akaanguka na kupooza mwili.Najua nilikuumiza sana kwa mambo haya yote.Katika dakika zangu hizi za mwisho naomba unisamehe kwa yale yote niliyokukosea.Nahitaji unisamehe wayne kabla sijafa? akasema Emmy .Nilishindwa niseme nini ni machozi tu yaliyokuwa yananitoka
? wayne naomba ufahamu kwamba sikuwa mwaminifu katika ndoa yetu hata kidogo.Nilitembea na wanaume wengi nje ya ndoa na mmoja wao ni James ambaye ndiye baba mzazi wa Baraka.James ndiye aliyenifanya hivi baada ya kugundua kwamba nilikuwa nimemtoa mwanae kafara.James ana nguvu za kishetani na aliumia sana aliposikia kwamba nilifanya kitendo kile kwa mwanae wa pekee kabisa kwani kwa sasa yeye hana tena nguvu za kiume.Amefanya hvi kwa ajili ya kulipiza kisasi kwa jambo hilo.Siwezi kumlaumu kwa jambo hili alilolifanya kwani ninastahili.Nin
astahili adhabu hii kwa kosa hili na makosa yote niliyoyafanya.? Nilishindwa kujizuia nikaanza kulia kwa kwikwi
? wayne naomba usilie mpenzi wangu.Usinililie mimi.Ninastahiili adhabu hii.Nimefanya mambo mengi mabaya ,nimewakosea watu wengi na haya ndiyo malipo yake.?
? Emmy kwa nini lakini yakukute haya? Kwa nini alifanya hivi James? Nikasema kwa uchungu
? wayne usisikitike kabisa.Kama nilivyosema ninastahili adhabu hii.Nimelia usiku kucha na baada ya kutafakari nimegundua kwamba ninastahili adhabu .?
? Niambie tutampata wapi james? Nikauliza
? James hamtaweza kumpata kamwe.Yule ana nguvu za kishetani na hata mimi sifahamu ameelekea wapi kwani aliyeyuka hapa kama upepo yeye na walinzi wake na sijui wako wapi.Msisumbuke kumtafuta kwani hamtaweza kumpata na alinihakikishia hilo kwamba hakuna atakayeweza kumpata.?
? lazima tumpate james ili aweze kukurudisha katika umbo lako la ubinadamu.? Nikasema huku nikifuta machozi.Sikuwa na uoga tena wa kukaa karibu na Emmy.
? Wayne msipoteze muda huo.Yaliyotokea yamekwisha tokea na tuyaache yaende.Kupitia mimi watu wengi watajifunza kwamba atendaye kwa ubaya hulipwa kwa ubaya.Muda unakwenda sana Wayne naomba uniitie baba na mama niwaombe msamaha.Nimewakosea sana? akasema Emmy
? baba na mama wote wako hospitali baada ya kupatwa na mstuko ? nikamwambia.Akafumba macho .nahisi alisikia uchungu mkubwa
?Wayne kama sintaonana nao naomba uniombee msamaha .Waambie kwamba nimetubu makosa yangu yote niliyowakosea na ninawaomba waniombee sana? akasema Emmy
? Vile vile naomba uniombee msamaha kwa rafiki yangu Sheila .Nilkorofishana naye siku chache zilizopita nikamtolea maneno machafu.mwambie anisamehe?
? Emmy Sheila amefariki dunia jana usiku baada ya kuzipata taarifa hizi? nikamwambia Emmy ambaye alifumba tena macho
? Wayne kuna mambo mawili ambayo nataka kukuomba.Kwanza nataka uniletee padre ili niungame dhambi zangu na pili naomba ufahamu kwamba hakuna njia nyingine yoyote ya kufanya kunirejesha katika ubinadamu na siwezi kuendelea kuishi katika hali hii.Mwenye uwezo wa kunirejeshea ubinadamu ni James lakini naye ametoweka kimiujiza na si rahisi kumpata tena.kwa hiyo ninaomba baada tu ya kuungama makosa yangu kwa padre nitaomba nipigwe risasi nife.Nikisha kufa tu Clara atakuwa mzima tena.Ninaomba usimuache Clara.Yeye pekee ndiye mwanamke anayekufaa na nina hakika hata wewe unampenda pia.Fanya kila utakaloweza umuoe Clara na uanzishe familia..?
? Emmy tafadhali usiseme hivyo.Sintakubali ufe.Tutamtafuta James kila kona ya dunia na tutampata? nikasema
? Wayne naomba unisikie.hakuna atakayeweza kumpata James.Ana nguvu za kishetani na anauwezo wa kuyeyuka kama upepo kwa hiyo hataweza kukamatwa.Nenda kafanye hayo niliyokwambia Wayne.Nahitaji padre haraka sana? akasema Emmy
? Emmy hapana sintaweza kufanya hivyo hata kidogo.Siko tayari ufe..Jeshi la polisi likisaidiana na polisi wa kimataifa watamtafuta James kila kona ya dunia na atakuja kukurejesha katika ubinadamu? nikasema kwa uchungu
? Wayne hapa nilipo nina maumivu makali sana.Ninahisi kama ninaogelea kwenye tanuru la moto.Niondolee mateso haya kama unanipenda Wayne.Niitie padre niungame dhambi zangu na baada ya hapo nipigwe risasi nife niondokane na mteso haya makali.Fahamu vile vile kwamba kifo changu ndiyo uzima wa Clara.Nahitaji uwe na maisha mazuri na mwanamke unayempenda naye akakupenda kwa moyo wake wote na haya yatawezekana pale tu nitakapofariki kwani Clara atapona.? Akasema Emmy
? Nenda Wayne?nenda haraka? akasisitiza
Nilitoka ndani ya kile chumba nikilia machozi.
? Wayne nini kimetokea? Emmy amesemaje? Akaniuliza kamanda wa polisi
Niliwaleleza wale maafisa wa polisi kuhusiana na kille nilichoongea na Emmy .kamanda wa polisi mkoa aliniomba niende nikamchukue padre kama alivyotaka Emmy yeye akiambatana na maafisa wengine wa polisi na viongozi wa mkoa waliitisha kikao cha dharura kwa ajili ya kujadili suala lile lililogubikwa na utata mkubwa.
Niliongozana na askari wawili kulekea kanisani kwa ajili ya kumchukua padre.Tukiwa njiani niliwasiliana na Chris aliyekuwa hospitali akanitaarifu kwamba baba mkwe hali yake ilikuwa inaendelea vizuri ila mama mkwe bado hali yake haikuwa nzuri.Nilimweleza kila kitu nilichoongea na Emmy hata naye alipatwa na mstuko.Nilifika kanisani na kumpata padre.Nilimueleza kila kitu bila kumficha na bila kupoteza wakati tukaingia garini na kurejea hospitali.Tulipofika hotelini tulikuta kuna vurugu kubwa kati ya askari polisi na kundi la watu waliokuwa wamevunja uzio wa hoteli wakitaka kuingia ndani kumuona mwanamke aliyegeuka nyoka.Polisi walitumia mabomu ya kutoa machozi kuwatawanya.Kwa kuwa tulikuwa na gari la polisi hatukupata matatizo tukapita na kuingia ndani.Nikaingia katika chumba kile ambacho hakutakiwa kuingia mtu yeyote asiyehusika.Bado Emmy akiwa na mwili wa nyoka alikuwa amekaa pale pale.
? Wayne umerudi? Umekuja na padre? Akauliza Emmy baada ya kuniona nimeingia mle chumbani.Aliongea kwa sauti yake ile nzuri na nyororo kana kwamba hakuwa na mwili wa nyoka.Yalikuwa ni maajabu makubwa kuwahi kuyashuhudia
?Ndiyo Emmy.Nimekuja naye? nikasema na kumuita padre akaingia mle ndani
? Wayne naomba unipishe .Nataka niwe peke yangu na padre? akasema Emmy
Wale askari wawili waliokuwa na silaha walikataa kutoka kwa kuhofia labda pengine Emmy angeweza kumdhuru padre .Niliwahakaikishia kwamba Emmy hakuwa na madhara yoyote kwani bado ni binadamu halisi.Wakuu wao wakawaomba watoke mle ndani ya chumba na kuwaacha padre na yule mtu nyoka mle chumbani.hata hivyo walikuwa makini sana katika kusikiliza endapo kungetoka sauti yoyote ile
Wakati padre akiendelea kuongea faragha na Emmy mle chumbani niliomba msaada wa polisi ili nielekee hospitali kuonana na baba mkwe.Nilipanda gari la polisi tukaelekea hospitali.Tulipofika tukaonana na Chris akatupeleka moja kwa moja katika chumba alicholazwa baba mkwe.Alikuwa amekaa kitandani akionekana mwenye mawazo mengi sana
? Wayne? akasema baba mkwe baada ya kuniona
? baba unaendeleaje ? nikauliza
? Ninaendelea vizuri japokuwa hawataki kunipa ruhusa nikashughulikie tatizo la mwanangu.Kuna taarifa gani huko? Nini kinaendelea? Tukio lile limetokeaje? Akauliza baba mkwe.Ilinilazimu kumueleza kila kitu namna tukio lile lilivyotokea hadi hatua iliyopo hivi sasa.Nilimueleza pia maongezi yetu yote tuliyoongea na Emmy na mwisho nikamwambia kuhusu ombi la Emmy.Aliinama akafikiri na kusema
? wayne Emmy yuko sahihi.Hakuna namna tunayoweza kufanya ili kumrejesha katika ubinadamu.Hapo alipo anapata mateso makali sana na ili kumuepushia mateso hayo ninakubali maombi yake yatekelezwe.? Akasema baba mkwe huku akivaa shati lake
? Wayne tunakwenda wote hospitali .Nataka nikalimalize suala hili.? Akasema baba mkwe na kumuaga muuguzi aliyekuwa ameleta dawa kwamba atarejea baada ya muda mfupi.Tuliingia garini na kuondoka kurejea hotelini.Tayari padre alikwisha maliza kuongea na Emmy na alikuwa anazungumza na maafisa usalama.Baba mkwe akaingia mle chumbani kwa Emmy na tukamuacha mwenyewe ili aongee na binti yake.Baada ya kama dakika ishirini hivi baba mkwe akatoka mle chumbani.macho yake yalikuwa mekundu.
?Yuko wapi kamanda wa polisi? Akauliza baba mkwe.bahati nzuri wakati anamuulizia naye akatokea akiwa na maafisa wengine.Walimaliza mkutano wao wa dharura uliofanyika pale pale hotelini
?baba pole sana.Unaendeleaje? akasema kamanda wa polisi huku akimpa mkono baba mkwe kumsalimia
? Ninamshuku Mungu ninaendela vizuri sana.Poleni na nyie?
? ahsante sana baba tumeshapoa.?
Baba mkwe akamuomba wasogee pembeni kidogo waongee,nami pia nikajiunga nao
?Afande nimetoka kuongea na Emmy.Hali yake inasikitisha sana.Mmefikia wapi katika kumkamata mtu aliyetenda kitendo hiki? Akauliza baba mkwe
? Kwa kweli mpaka sasa bado suala hili linautata mkubwa.Bado hatujafanikiwa kumpata huyo James na haijulikani yuko wapi.Taarifa tuliyoipokea toka katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Kilimanjaro haionyeshi jina la mtu ambaye ndiye anayesemwa kuhusika na tukio hili.Kamera za ulinzi za hapa hotelini hazimuonyeshi kabisa huyo mtu kwa hiyo tumeshindwa kuipata sura yake.Mzee tukio hili limetawaliwa na nguvu za giza kwa kiasi kikubwa sana lakini tunafanya kila tuwezalo ili kumfahamu huyo James ni nani na tutampata tu? akasema kamanda wa polisi
? Kamanda ninaafikiana na mawazo ya Emmy kwamba tulimalize suala hili na tumundolee maumivu aliyonayo kwa sasa.Tufanye kama anavyotaka.Nimeongea naye na nimeyaona mateso makali aliyonayo.Huyo James inaonekana haitakuwa rahisi kumpata kutokana na mazingira yake kwani kwa mujibu wa Emmy alitoweka tu kama upepo ? akasema baba mkwe
? Mzee unamaanisha tumpige risasi mwanao?
? Ndiyo afande.Niko tayari mwanangu apigwe risasi ili aondokane na mateso haya makubwa aliyonayo.? Akasema baba mkwe
? Suala hilo ni gumu na tayari limezua mjadala mkubwa kwani sheria hazituelekezi hivyo.?
? Nalifahamu hilo lakini hakuna namna nyingine ya kuweza kumrudisha mwanangu katika ubinadamu.Hebu fanyeni maamuzi haraka haraka ili tuweze kumuondolea mwanangu maumivu makali aliyonayo.? Akasema baba mkwe.
************************
Sulala la Emmy lilizidi kuchukua sura mpya kila dakika.Eneo la kuzunguka hoteliile lilifurika watu waliotaka kumuona nyoka mtu.Hatimaye baada ya mjadala mrefu ukihusisha makundi mbali mbali ya wanaharakati wa haki za binadamu iliamriwa kwamba Emmy apigwe risasi kwani alianza tena kulia kwa mateso makali aliyokuwa anayapata.Japokuwa hata mimi niliona kwamba ni uamuzi wenye busara kwa ajili ya kumuondolea Emmy mateso aliyokuwa anayapata lakini niliumia mno.Emmy alikuwa ni mke wangu wa ndoa na japokuwa tulikuwa tumetengana na akanifanyia vitimbi vingi sana lakini nilimsamehe na niliumizwa sana na tukio lile.Hata wewe ndugu msomaji lazima ungeumia sana kwa mtu ambaye mmeishi naye kwa miaka mingi atokewe na tukio kama lile.Ilikuwa ni saa kumi na mbili za jioni maamuzi hayo yalipotolewa.Hakutakiwa mtu mwingine yeyote aingie mle chumbani kwa Emmy kwani alikuwa akipiga kelele kubwa kwamba anaumia.Saa moja za jioni askari watatu waliokuwa na bunduki zenye viwambo vya kuzuia sauti wakaingia katika chumba cha Emmy.Wengine wote tukakaa kimya kila mmoja akisali kufuatana na kitendo kinachoenda kutokea mle ndani.Sauti ya Emmy akipiga kelele za maumivu makali zilisikika.Niliumia sana.Baada ya kama dakika kumi hivi askari wale wakatoka.Tayari walimaliza kazi.Machozi yalinitoka.Tayari Emmy alikuwa amepigwa risasi.Huo ukawa mwisho wake haapa duniani.Niliumia mno.
**********************
Hatimaye siku ya siku ikafika.Ni siku ambayo safari ya mwisho ya Emmy hapa duniani ilihitimishwa.Ni siku ya mazishi ya mtu aliyewahi kuwa mke wangu wa ndoa,mwanamke niliyempenda sana licha ya vitimbi na vituko vya kila aina alivyonifanyia.Sikutegemea kama mwisho wa Emmy ungekuwa namna hii.Ulikuwa ni mwisho wa uchungu na wa masikitiko makubwa.
Tulikabidhiwa mwili na jeshi la polisi kwa ajili ya maziko ,mwili ambao ulikuwa ni kichwa tu .Ile sehemu ya chini iliyokuwa ni nyoka ilichukuliwa na kwenda kuteketezwa mbali na mji.Jeneza lenye kichwa cha Emmy halikufunguliwa hata wakati wa kutoa heshima za mwisho .
Watu walikuwa ni wengi sana makaburini.Wengi waliguswa na kifo kile cha Emmy na hasa mazingira yake .Wapo waliomuonea huruma na wapo waliokuwa wakimkejeli na kumbeza kwa vitendo vyake alivyokuwa akivifanya ili mradi kila mmoja alisema lake.Baada ya padre kufanya ibada fupi ya makaburini hatimaye jeneza lenye kichwa cha Emmy likaingizwa kaburini.Wa kwanza kutupia udongo alikuwa ni baba mkwe.Mama mkwe bado alikuwa hospitali .Wa pili kutupia udongo nilikuwa mimi.Baada yangu wakafuata ndugu jamaa na marafiki halafu zoezi la kufukia likaanza.Ulikuwa ni wakati mgumu sana kwangu .Niliumia sana kila niliposikia kishindo cha udongo ukitupiwa kaburini.
? Kwa heri Emmy.Pumzika kwa amani huko uendako.Siku zote nitakuombea ili uwe na mapumziko mema.Nina imani Mungu wetu mwenye upendo na huruma amekusameme dhambi zako zote kwani ulitubu kabla ya umauti.Siku zote nitazikumbuka na kuzienzi zile nyakati zote za furaha tulizokuwa nazo mimi wewe na Baraka .Utaendelea kuwa sehemu muhimu ya maisha yangu.Katika maisha yangu niliyoishi nawe nimejifunza mambo mengi sana,nimejifunza upendo wa kweli,uvumilivu na kumtegemea Mungu kwa kila jambo.Nitaviend
eleza vitu hivi katika siku zote za uhai wangu zilizobaki hapa duniani.Kwa heri Emmy? nilikuwa nikiwaza wakati kaburi la Emmy likifukiwa.Baada ya zoezi lile kukamilika tukaweka shada za maua halafu tukarejea nyumbani.Nawashukuru sana rafiki zangu Chris na Beka waliokuwa nami kwa kipindi hiki chote cha matatizo na kunifariji .namshukur pia mama yangu alikuja kuungana name katika wakati huu mgumu.Mwili wangu ulikuwa umechoka sana nikaomba nipatiwe sehemu nipumzike.Nilitafutiwa sehemu nzuri chini ya mti nikawekewa godoro na kujilaza hapo
Picha yote ya maisha yangu na Emmy toka tulipokutana ikanijia kichwani.Nilishindwa kujizuia kutokwa na machozi.Niliyakumbuka maongezi yangu ya mwisho na Emmy kule hotelini akiniomba msamaha.
?Huyu James ni nani ambaye alimtenda Emmy vile? Nashindwa kuelewa ni binadamu mwenye roho ya namna gani anayeweza kumgeuza mwenzake nyoka.Hata kama alimkosea hakupaswa kumtenda mwenzake namna ile.Mpaka leo kitendawili cha James ni nani hakijateguliwa.Mtu pekee ambaye alikuwa akimfahamu James viuri ni Sheila lakini naye kwa sasa ni marehemu.Hakuna tena mtumwingine atakayetusaidia kuweza kumpata .Nakumbuka Emmy alisema kwamba tusisumbuke kumtafuta James kwanio hatutaweza kumpata.Kwa mujibu wa Emmy James alitoweka ghafla yeye na walinzi wake.Ama kweli duniani humu kuna maajabu makubwa sana.? Nikawaza na Kutokana na uchovu mwingi taratibu nikajikuta nikipitiwa na usingizi.
Sikumbuki nililala kwa muda gani lakini nilistuliwa na mtu aliyekuwa akinitingisha .Alikuwa ni Chris
? hey Chris ? Nikasema kwa uchovu huku nikiyafikicha macho
? Wayne samahani kwa kukuamsha.Kuna wageni wamekuja kukupa pole?
? Ni akina nani?
? Itakuwa vizuri kama ukiinuka na kwenda kuonana nao.Ni watu wako wa muhimu? akasema Chris
Nikainuka kwa uchovu na kuongozana na Chris kuelekea waliko wageni wangu waliokuja kunipa pole.Tuliiacha nyumba ya wazazi wa Emmy na kuingia katika nyumba ya jirani.Nilimfuata Chris tukaingia sebuleni na ghafla nikakutana na kitu cha ajabu kilichonistua mno.Mwili wangu wote ukanisisimka..Nilibaki nimepigwa na butwaa kwa sekunde kadhaa nisiamini nilichokiona.
Mbele yangu alikuwa amesimama Clara akiwa na uso uliojaa machozi.Pembeni yake walikuwepo wazazi wake pamoja na baba mkwe.
? Clara !!! nikasema kwa mshangao
?Wayne ? akaita Clara halafu akapiga hatua kunfuata tukakumbatiana.Sikuamini nilihisi kama vile bado niko ndotoni.
? Ouh Wayne my love? akasema Clara na kunikumbatia kwa nguvu zaidi
? Clara is that you? Nikasema huku nikimuangalia nisiamini nilichokiona.Mtu ambaye siku mbili zilizopita alikuwa kitandani na hakuweza kufanya kitu chochote leo hii ni mzima wa afya na huwezi kuamini kama alikuwa mgonjwa hajiwezi.
? Its me Wayne..I?m ok now? akajibu Clara kisha tukakumbatiana tena.Ulikuwa ni kama muujiza kumuona Clara akiwa mzima namna ile.Niliachana na Clara na kwenda kuwasalimia wazazi wake
?Pole sana Wayne kwa kilichotokea na samahani kwa kuchelewa mazishi tulikosa usafiri wa haraka wa kutuwahisha huku Arusha? akasema Clara
? nashukuru sana kukuona tena Clara.Bado siamini kama ni wewe kweli?
? Ni mimi Wayne.? Akajibu Clara
?Imetokeaje hadi ukapona ghafla namna hii?
? Hata mimi sifahamu imetokeaje Wayne lakini nilishangaa tu nimekuwa mzima ghafla kana kwamba sikuwa ninaumwa chochote .Sielewi haya yametokeaje? akasema Clara.Mara moja nikakumbuka maneno ya Emmy alisema kwamba pindi atakapofariki tu basi Clara atapona.Ni kweli Clara amepona.Nilimshukur sana Mungu kwa kumjalia mwanamke yule ninayempenda kupona na kuwa mzima tena
? Wayne ? akaita baba yake Clara
? naam baba ? nikaitika
? Tumekuja sisi sote pamoja na Clara kukupa pole kwa matatizo yote yaliyotokea na kuungana nawe katika kipindi hiki kigumu ulichonacho.Kama ilivyo kwako hata sisi tumeumia sana na ndiyo maana tuko hapa? akasema baba Clara
? Baba nashukuru sana kwa kufika kwenu .,Nimefarikjilka sana kuwaoneni hapa mkiwa na Clara.Nimefarjika mno? nikasema
?Tulisikia kupitia vyombo vya habari kuhusiana na jambo lililotokea,tulistushwa sana lakini hatukufahamu kama aliyepatwa na tatizo lile alikuwa nimtu aliyewahi kuwa mke wako.Baada ya kupona ghafla Clara ndiye aliyetustua baada ya kuiona picha ya Emmy katika gazeti.Wayne poleni sana.Tukio lile lililotokea ni tukio kubwa na la kustusha.Clara alisisitiza kwamba lazima aje ahudhurie mazishi na kukupa pole .Wayne napenda kuchukua nafasi hii kukuomba samahani kwa maneno niliyokutamkia mimi mwenyewe wakati tulipokuja kumchukua Clara kumpeleka Dar es salaam kwa matibabu.Niliku
tamkia maneno mabaya na ambayo yalikuudhi sana.Naomba tusameheane na tufungue ukurasa mpya kati yetu.Yaliyopita yamekwisha pita, tutazame ya mbele.Clara ametueleza mengi sana na tumemuelewa.Sisi kama wazazi wake hatutakuwa na kipingamizi chochote kwake kuhusiana na hatima ya maishayake na yeye mwenyewe ndiye atakayemchagua nani anataka kuwa naye maishani mwake.Kwa kuwa kwa sasa bado tuko katika majonzi,tutaongea zaidi kesho ? akasema baba yake Clara.Pamoja na kwamba nilikuwa katika majonzi lakini nilifurahi sana moyoni kwa kauli ile ya baba Clara.
? baba nawashukuru sana kwa kufika kwenu.Kwa ufupi niI kwamba mimi sikuwa na tatizo lolote nawe.maneno yale uliyoyasema wakati ule yaliniumiza sana lakini nilikwisha yasahau yote.Yamekwisha pita.? Nikasema na kisha tukaendelea na maongezi .
Saa nne za asubuhi siku iliyofuata tuliwasindikiza wazazi wa Clara uwanja wa ndege kwa ajili ya kurejea Dar es salaam.Clara alibaki Arusha.Alitaka aendele kukaa nami na kunifariji.Baada y a kutoka uwanja wa ndege wa kimataifa wa Kilimanjaro tulielekea makaburini ambako tuliwasha mishumaa katika kaburi la Emmy
? Pumzika kwa amani Emmy.? Nikasema huku nikiweka shada la maua halafu nikampisha Clara
? Emmy najua mimi na wewe hatukuwa tukielewana.Mambo mengi yalitokea kati yetu katika kulipigania penzi la Wayne.Nilikwisha kusamehe muda mrefu sana Emmy na nitakuombea upumzike kwa amani huko uliko.Ninakushukur u kwa sababu bila wewe nisingeonana na Wayne.Pumzika kwa amani Emmy? akasema Emmy na kuweka shada la maua.Tukiwa garini nilimsimulia Clara kila kitu kilichotokea na kila alichokifanya Emmy.Clara alilia sana .
?Wayne pole saana kwa mateso yote uliyoyapata ,wewe ni mwanaume wa pekee kabisa hapa duniani.Watu kama wewe ni nadra sana kuonekana zama hizi.Niliyaona machoz I yako wakati nikiumwa nikiwa sijiwezi kitandani ,nilikuona namna ulivyoumia.Machozi yale yamenidhihirishia ni namna gani unavyonipenda..Wayne ninakupenda na ni wewe pekee nitakayekupa moyo wangu.Wazazi wangu hawakutaka kabisa nirejee Arusha lakini niliwaeleza ukweli kuhusu mimi na wewe na wakanielewa.Wayne we?re free now.Its our time to enjoy life? akasema Clara
?Ni kwelihayo unayoyasema Clara.Ni wakati wetu sasa wa kuyafurahia maisha .Lakini sintaweza kuyasahau mateso na maumivu yote niliyoyapitia katika kipindi hiki chote nilichokaa na Emmy.Ilikuwa ni zaidi ya mateso,zaidi ya maumivu.It was BEYOND PAIN? Nikasema
? Usijali wayne.I?m here now.Nitakusaidia kusahau yote yaliyotokea.Kwa pamoja tutasahau kila mateso tuliypoyapitia hapa duniani na kutengeza dunai yetu peke yetu,dunia iliyojaa furaha amani na upendo.? Akasema Clara
? I love you Clara? nikasema
? I love you too Wayne?
Wiki mbili baada ya kumalizika kwa msiba wa Emmy , mimi na Clara tukaruka kwa ndege tukaeleka katika visiwa vya Zanzibar kwa ajili ya mapumziko.Tulikuwa huru sasa na hatukuhgofia chochote kwani hakukuwa na yeyote atakaye tubughudhi.Mwanzo mpya wa maisha yangu na Clara.
TAMATI
 
Simulizi nzuri sana na inafundisha mambo mengi sana
Asante mkuu
 
Hivi kuna watu wanasoma haya maandishi yote..!


Shikamoo interest
 
Back
Top Bottom