Masimulizi: Beyond Pain

Masimulizi: Beyond Pain

Asantee mkuu kwa story nzuriiii mnoooo yanii japo ndefu lakini tamu haichoshi
Plz usituchinjie baharini
imalizie jaman
 
hivi jamani hii ni story ya kweli?,nimeisoma yote leo cku ya pili lakin machozi yalinitoka kwa kila sehemu huu usaliti jamani utatuua
 
Mkuu wadau wa hii story tupo wengi. Endelea kutupa nondo tafadhali
 
Ungeleta ile simulizi ya Miss Tanzania au Selena ingekuwa poa sana
 
SEHEMU YA 17
MTUNZI 😛ATRICK.CK
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
?tafadhali usilie Clara.Huu ni wakati wa
kufurahi na si wakati wa kudondosha
machozi? nikamwambia huku nikimfuta
machozi
?Wayne ninalia kutokana na furaha
niliyonayo.Nimekaa miaka mingi nikijihisi ni
mwenye furaha lakini sikuwahi hata mara
moja kuipata furaha kubwa kama niipatayo
sasa kwa kuwa nawe.Ni wewe ndiye uliyenipa
furaha hii kubwa maishani.? Akasema
Clara.na kuniangalia usoni.
?Darling twende tukaendelee na ratiba yetu ya
siku.Tuna kila sababu ya kufurahi? Tukatoka
na kuingia garini tukaelekea eneo la meserani
ambako kuna hifadhi ya nyoka.Mimi si mpenzi
kabisa wa nyoka na ni moja kati ya vitu
ninavyoviogopa sana katika hii dunia lakini
niliamua kwenda huko kwa sababu Clara
alipenda kwenda kutazama nyoka wa aina
mbali mbali wanaofugwa.Amekuwa akisikia
hifadhi hii ya nyoka na alipanga siku moja
aitembelee na sasa ameipata nafasi hiyo
hakutaka kuipoteza.
ENDELEA????????..
Meserani park moja kati ya sehemu nzuri
kutembelea iko kilometa 25 magharibi mwa
jiji la Arusha katika barabara ya kuelekea
hifadhi ya taifa ya Serengeti na bonde la
Ngorongoro.Hifadhi hii imejumuisha nyoka wa
kila aina wanaopatikana mashariki na kusini
mwa afrika.Ukiwa katika hifadhi hii ya
Meserani utapata pia kuwashuhudia mamba
wenye ukubwa wa zaidi ya meta tatu na vile
vile utafurahia safari za ngamia kuelekea
katika maboma ya wamasai na utabahatika
kujifunza utamaduni wa kimasai.
Saa kumi za jioni tulirejea jiijini
Arusha.Ilikuwa ni siku niliyofurahi
mno.Tulipanda ngamia na kwenda katika kijiji
cha wamasai ,tulikaa na kujifundisha mambo
mengi kuhusiana na utamaduni wa kimasai
pamoja na kununua badhi ya vitu walivyokuwa
wakiviuza.Kwa miaka yangu yote ya kuishi
Arusha sikuwahi hata mara moja kutembelea
vivutio mbalimbali vilivyopo hapa jijini.Nilijisi
kia furaha sana baada ya kugundua faida
ipatikanayo kutokana na utalii wa ndani.
?Clara bado naendelea kukushukuru kwa
sababu kupitia kwako nimejifunza mambo
mengi.Katika miaka yote hii niliyoishi hapa
Arusha sijawahi kutembelea hata kivutio
kimoja ha utalii.Nimehamasika sana kwa
ziara tuliyoifanya leo na kila nipatapo nafasi
nitakuwa nikifanya utalii wa ndani na
kuliongezea taifa mapato? Clara hakujibu kitu
alinitazama na kutabasamu
Clara hakutaka tena kukaa pale hotelini
.Hakutaka tena kuwa mbali nami.Akaniomba
kwa siku hizi chache ambazo atakuwepo hapa
Arusha azimalizie akiwa nyumbani
kwangu.Nilifurahi sana kwa uamuzi ule
Pale hotelini Clara hakuwa akidaiwa chochote
akapakia vitu vyake na tukaelekea nyumbani
kwangu.Furaha ikaingia tena ndani kwangu.
**********************
Siku mbili kabla ya safari ya kuelekea
Zanzibar kwa ajili ya mapumziko nilipokea
taarifa kwamba ninahitajka katika ofisi za
taasisi ya kupambana na kuzuia
rushwa.Walikuwa wakihitaji kunihoji .Tayari
Emmy alipeleka mashitaka kama alivyokuwa
ameahidi kama nisingetimiza matakwa
yake.Sikuwa tayari kutimiza matakwa ya
Emmy.Nilimweleza Clara kuhusiana na mwito
ule na akanipa moyo kwamba nisiwe na wasi
wasi hata chembe kwa sababu suala hilo liko
ndani ya uwezo wake na nihesabu kama
limekwisha.
Saa tatu za asubuhi katika siku niliyotakiwa
nifike pale ofisini ilinikuta nikiwa katika
chumba maalum kwa ajili ya mahojiano.Watu
tatu wakaingia pale wakiwa na mafaili yenya
nyaraka mbali mbali tukasalimiana na
mahojiano yakaanza.
Nilihojiwa mambo mengi sana kuhusiana na
fedha zile zilizokuwa benki.Niliwaeleza ukweli
kuhusiana na ugomvi wangu na Emmy na jinsi
gani Emmy anavyotaka kuhakakisha kwamba
ninaporomoka.Niliwaeleza vile vile kwamba si
kweli kwamba fedha zile zilitokana na ufisadi
nilioufanya wakati nikiwa mfanyakazi wa
halmashauri ya jiji la Arusha bali fedha zile
zimetokana na biashara tuliyokuwa tukiifanya
kwa ubia kati yangu mimi na Clara.Clara
akaitumia nafasi hiyo pia kulezea kwa upana
kuhusiana na biashara tunayoiendesha kwa
ubia .Aliwaonyesha vithibitisho mbalimbali
vilivyokuwa katika kompyuta yake ndogo
vilivyoonyesha kwamba nimekuwa nikipokea
mgao wa fedha toka katika kampuni ile.Kitu
kilichowaumiza kichwa ni kwamba ni wapi
basi Emmy alizitoa nyaraka zile alizokuwa
nazo? Nyaraka kuhusiana na fedha
iliyokuwepo benki nilikiri ni zangu na Emmy
alizichukua wakati nikiwa sipo nyumbani
lakini nyaraka mbalimbali ambazo alikuwa
nazo kuhusiana na ufujaji wa fedha za
halmashauri nilizikana na kuwaomba waende
wakapate taarifa sahihi kutoka halmashauri
nilikokuwa nikifanya kazi.Baada ya masaa
takribani sita ya mahojiano,tukaondoka na
kuwaacha wakiumiza vichwa vyao na
kumlaani Emmy kwa kuwasumbua pasi na
faida yoyote.Nilimshukuru sana Clara kwa
kuniokoa katika sakata lile.
?Pamoja na kulimaliza suala hili bado
nitabaki na msimamo ule ule kwamba fedha
zile ni za wananchi na itabidi tuzirudishe kwa
wananchi kwa kuzipeleka katika miradi ya
maendeleo? akanikumbusha Clara.
?Clara nalikumbuka hilo.Mara tutakaporejea
kutoka Zanzibar fedha zile zote tutazipeleka
katika miradi .Tutapanga na kuamua ni kitu
gani tunaweza tukaifanyia jamii kwa fedha
zile?
Nikamwambia Clara akatabasamu na
kunibusu.
***********************
Ni Siku ya tano sasa toka tumefika hapa
Zanzibar katika hoteli ya Zanzibar Serena
Inn.Baada ya misuko suko iliyotupata Arusha
tuliamua kuja huku mbali kwa ajili ya
mapumziko na kupanga maisha yetu.Ni mida
ya saa tisa za alasiri tukiwa katika ufukwe wa
Mangapwani unaomilikwa na hoteli hii ,simu
yangu ikaita.Niijilaumu sana kwa kutembea
na simu sehemu kama hii.Nikaitoa simu na
kuangalia mpigaji.Zilikuwa ni namba ngeni
kabisa.
?hallo ? nikaita
?hallo Wayne? Ikajibu sauti ya upande wa pili
ambayo nilihisi kama ninaifahamu.
?nani mwenzangu? Nikauliza
?Ni mimi Chris?
?Chris !! nikastuka mno.Sikuitegemea kama
Chris angeweza kunipigia simu hasa baada ya
kitendo alichonifanyia.
?Wayne najua hukutegema kama ningeweza
kukupigia simu tena.Nimelazimika kukupigia
kuongea na wewe mambo mawili makubwa?
?Chris tafadhali naomba usiniharibie siku.Kwa
sasa niko Zanzibar mapumzikoni na mpenzi
wangu mpya.Sitaki unisumbue Chris?
Nikasema kwa ukali
?Wayne tafadhali naomba unipe dakika mbili
tu za kuongea na wewe na baada ya hapo
sintakusumbua tena.? Chris akasema
?Unataka kuniambia kitu gani Cris? Nikauliza
kwa ukali
Clara aliyekuwa amebaki nyuma yangu
akanikaribia na kuniuliza
?Darling mbona unaongea kwa ukali namna
hiyo.nani huyo aliyekupigia simu ?
?Ni mume wa Emmy? nikamjibu Clara ambaye
akasogea pembeni na kunipa nafasi niongee
na Chris.
?Wayne kwanza kabisa nachukua nafasi hii
kukuomba msamaha japokuwa nafahamu
kwamba si rahisi kunisamehe kwa mambo
niliyokufanyia.Nimekuwa sina amani maishani
mwangu.jambo hili limenikondesha
mno.Japokuwa ni ngumu kwako kunisamehe
lakini naomba nikiri kwamba nilikukosea sana
na ninaomba unisamehe.?
?Chris mimi sina tatizo na wewe hata kidogo.
Nimekwisha kusamehe muda mrefu sana na
nikaendelea na maisha yangu.Nilikupa Emmy
kwa kuamini kwamba ndiye mwanamke pekee
anayekufaa maishani.Mimi kwa sasa niko na
mpenzi ambaye ndiye niliyeandikiwa na
Mungu.Ninayafurahia maisha yangu tofauti
na nilipokuwa na huyo mke wako? Nikasema
huku nikitabasamu
?nashukuru sana Wayne kama umekwisha
nisasemehe.Jambo la pili ninalotaka
kukueleza ni kwamba mimi na Emmy
tumeachana.Niligundua kwamba mtoto yule
ambaye alisema ni wa kwangu hakuwa mtoto
wangu.Kutokana na matendo yake nilipata
shauku ya kwenda kupima DNA na majibu
yakaonyesha kwamba Baraka si mwanangu
kama alivyodai.Sikuweza kuvumilia nikaamua
kumfukuza kwangu na kwa sasa amesema
kwamba anarudi kwako kwani bado ni mkeo
halali.Hivi tunavyongea tayari amerejea
nyumbani kwako anadai ni nyumbani kwake
na wewe ni mume wake halali wa
ndoa.Nimeona nikufahamishe kuhusu jambo
hilo ili ujue nini kinaendelea huku na uchukue
tahadhali.Mwanamke yule ni baradhuli na
hafai katika jamii..kwa heri wayne? Chris
akakata simu
?bastard !! nikasema kwa hasira.Nilihisi
kijasho chembamba kikinitoka
Clara aliniangalia jinsi nilivyobadilika ghafla
akahisi mambo hayakuwa sawa akanisogelea
na kunishika bega.
?Wayne huyo mume wa Emmy amekuambia
nini cha kukuudhi namna hiyo? Akauliza
Clara.Nilikuwa nikihema kwa nguvu kwa
hasira
?Clara ninajuta kwa nini nilimfahamu
Emmy.Nashindwa kuelewa ni mwanamke wa
aina gani yule?
?Nini kimetokea tena? Kwa nini anaendelea
kukufuata fuata wakati kila mmoja ana
maisha yake kwa sasa? Clara akauliza
?Chris amenipigia simu na kuniambia kwamba
yeye na Emmy wametengana .Amegundua
kwamba yule mtoto Baraka ambaye Emmy
alisema ni wake kumbe si wake.Jambo hilo
limemfanya amtimue Emmy na hivi
tunavyoongea amerudi nyumbani kwangu
akidai bado ni nyumbani kwake.Nashindwa
kuelewa nitamfanya nini huyu mwanamke ili
aachane na mimi.Nimechoka sasa na matukio
ya Emmy?
Clara akaniangalia kwa makini usoni na kisha
akasema
? Suala hili limekuwa gumu sana kwa
sasa.Ukiangalia kisheria Emmy bado ni mkeo
wa ndoa.Kwa mujibu wa ndoa za kikristu ni
kwamba mkisha funga ndoa kanisani hakuna
kitu kinachoweza kuwatenganisha zaidi ya
kifo.kwa maana hiyo wewe bado ni mume
halali wa ndoa wa Emmy.Kwa Emmy kurudi
katika nyumba yenu ni halali yake kwa sababu
bado ni mke wako.? Clara akasema taratibu
lakini nilijua ndani ya moyo wake alikuwa
ameumia sana.Nilijaribu kutafakari kwa kina
ni kwa nini Emmy amekuwa akinifanyia vituko
vya namna hii.Kwa nini hataki kuniona nikiwa
na furaha katika maisha yangu? Niliuma
meno kwa hasira na kusema
?Clara pamoja na yote uliyoniambia lakini ni
ukweli ulio wazi kwamba ndoa kati yangu na
Emmy ipo katika makaratasi tu.Lakini katika
uhalisia hakuna ndoa baina yetu.Hata Mungu
mwenyewe analiona hilo na hata hao viongozi
wa dini nikiwaelezea watakubaliana nami
kwamba Emmy hafai kuwa mke.Nimekwisha
mtoa Emmy moyoni mwangu na sintarudi
nyuma tena.Simtaki Emmy maishani
mwangu.Sitaki kabisa kumuona mbele ya
macho yangu.? Nikasema kwa ukali
?punguza hasira Wayne.Suala hili linatakiwa
kushughulikiwa taratibu na kwa umakini
mkubwa ili kupata suluhisho la kudumu la
mgogoro huu usiokwisha.Mimi nina wazo
moja? Clara akasema
?Wazo gani hilo Clara?
?Ninakushauri kwamba uwaite wazee wa
pande zote mbili ili muweze kukaa na
kutafuta suluhu kwa sababu kuivunja ndoa
yenu ni jambo ambalo haliwezekani.Ki
nachotakiwa kufanyika hapa ni kuitafuta
suluhu ya kudumu ili muweze kuishi kwa
amani tena.?
?Una maanisha nini Clara? Nikauliza
?Nina maana suluhisho hapa ni wewe
kurudiana na Emmy .Inavyoonekana ni
kwamba Emmy bado anakupenda na kwa
maana hiyo hata mfanye nini katu hamuwezi
kutengana?
?Tafadhali usiseme hivyo Clara?
Nikasema.Nilikuwa nimestushwa sana na
kauli ile ya Clara
?Wayne suala hili mbona liko wazi kwamba
wewe na Emmy kamwe hamuwezi
kutengana.Mnachotakiwa kukifanya kwa sasa
ni kutafuta suluhu ili muweze kuishi kwa
amani katika ndoa yenu.?
?Clara naomba tafadhali usiseme hayo
maneno.yananiumiza sana moyo
wangu.Macho yangu kwa sasa nimeyaelekeza
kwako tu.Ninachokihitaji ni kuwa nawe
maishani.?
Clara akanishika mikono miwili,akanitazama
usoni na kusema taratibu
?Wayne Nakupenda sana .Toka moyoni
mwangu nakiri kwamba nakupenda zaidi ya
unavyoweza kufikiri.Nakupenda zaidi ya
ninavyojipenda mwenyewe.Sijawahi kupenda
kama nilivyotokea kukupenda.Wewe ni kila kitu
kwangu.Wewe ni mwanaume wa pekee kabisa
ambaye hujawahi kutokea maishani
mwangu.Kila nikiwa nawe najihisi kama niko
juu mawinguni.nasikia furaha ya ajabu kila
ninapokuwa nawe.Nilipokuona kwa mara ya
kwanza niliweka ahadi kwamba nitafanya kila
niwezalo kwa ajili ya kulipigania penzi
lako.Nilikuwa tayari kwenda hadi mwisho wa
dunia kwa sababu yako.Niliweka ahadi ile
kutokana na jinsi ninavyokupenda
Wayne.Kutokana na hali halisi ilivyo
ninasikitika kusema kwamba Wayne mimi na
wewe hatuwezi katu kuwa pamoja tena.Katu
hatutaweza kuwa na furaha katika maisha
yetu.Wewe ni mume halali wa Emmy.hata
kama ndoa yenu iko katika mgogoro mzito
kwa sasa lakini ukweli utabaki pale pale
kwamba wewe ni mume wa mtu.Nimekuwa
nikilifikiria sana jambo hili na limeniumiza
sana moyo.Mwanzoni nilijipa moyo
nikitegemea labda mambo haya yanaweza
yakatulia na hivyo tukapata nafasi ya
kufurahia maisha tukiwa sisi wawili bila
bughudha ya aina yoyote ile lakini kadiri siku
zinavyozidi kwenda ndivyo karaha na vituko
toka kwa mkeo vinazidi.Kusema ukweli
nimekuwa nikiumizwa sana na mambo
anayoyafanya mkeo lakini nimekuwa
nikivumilia kutokana na upendo wangu
kwako.Kwa muda huu mfupi tulioonana kila
siku limekuwa likiibuka jambo jipya toka kwa
Emmy ambaye hataki kukuona
ukipumzika.Hataki kukuona ukifurahi.Wayne
naomba nikuambie ukweli kwamba
nimevumilia na sasa nimechoka.Ninaona
itakuwa vyema kwetu sisi kuusitisha huu
uhusiano wetu ili usiendelee kuumia
zaidi.Iwapo nitaendelea kuwa nawe Emmy
hatatuacha hata kidogo.Ataendelea
kutuandama usiku na mchana.Kwa maana
hiyo ni bora kama nitajiweka pembeni na
kukuacha uendelee na Emmy?
Clara akasema kwa uchungu huku machozi
yakimtoka.Alikuwa ameumizwa mno na
mambo aliyokuwa akiyafanya Emmy.Alikilaza
kichwa chake kifuani kwangu na kukilowesha
kifua changu kwa machozi.Nilisikia uchungu
mwingi kwa machozi aliyoyamwaga malaika
wangu ,nikapandwa na zisizomithilika.Laiti
kama Emmy angekuwa karibu yangu wakati
ule ningeweza kumfanyia kitu kibaya
sana.Sikujua ni kwa nini niendelee kuteseka
kwa mambo anayonifanyia Emmy.Sijui
nimemkosea nini Emmy kiasi cha kuwa na
chuki nami ya namna hii.Niliumia sana kwa
aumuzi ule wa Clara.Baada ya kuachana na
Emmy nilitegema kwamba Clara ndiye furaha
ya maisha yangu.Nilimuona ni kama malaika
aliyeshushwa kwa ajili ya kuja kunirudishia
furaha ya maisha iliyokwisha potea.Kwa muda
huu mfupi niliokuwa na Clara nimekuwa ni
mtu mwenye furaha kubwa maishani na
nilikuwa na mipango mingi ya siku za usoni
nikiwa na Clara. Kwa upande mwingine
sikulaumu sana uamuzi huu aliouchukua Clara
kwa sababu ni kweli alikuwa amechoshwa na
karaha zinazoendelea. Toka siku ya kwanza
tuliyoanza mapenzi yetu imekuwa ni matukio
moja baada ya jingine.Clara hakuwa ametaka
kujiingiza katika mambo ya mahusiano kwa
sababu ya kuogopa mambo kama haya
yanayotokea sasa.Aliufuingua moyo wake
baada ya kuamini kwamba mimi ni
mwanaume wa pekee ambaye ninaweza
kumpa furaha ya maisha lakini kumbe alikuwa
akielekea mahala ambako alikuwa
akipakimbia miaka hii yote aliyokuwa akiishi
peke yake.Alikuwa akiyakimbia matatizo na
karaha zilizomo ndani ya mahusiano lakini
badala yake amejikuta akitumbukia katika
shimo lililojaa kila aina ya matatizo.
?Wayne nakupenda sana na sitaki kuachana
nawe lakini sintaweza kuendelea nawe kwa
sababu ya ukweli ulio wazi kwamba Emmy
anakuhitaji .Emmy ana kila sababu ya
kunifanyia vituko kwa sababu wewe ni mume
wake halali wa ndoa.Siwezi kuendelea
kupambana na Emmy kila kukicha
.Ninamuachia mume wake na kujiweka
pembeni.Nimeamua kuyarudia maisha yangu
niliyokuwa ninaishi yaani maisha ya kuwa
peke yangu.Sitegemei kama nitaingia katika
mahusiano tena kwa sababu baada ya miaka
mingi ya kuwa nje ya mahusiano nimeufungua
moyo wangu na kujaribu kupenda tena lakini
kilichotokea ni kitu kile kile nilichokuwa na
kikwepa kwa miaka mingi yaani mumivu ya
moyo.Ninaumia sana Wayne..Moyo wangu
umeumia sana na sijui kama kidonda hiki
kitaweza kupona.Nitateseka kwa maisha
yangu yote kwa sababu mtu niliyetokea
kumpenda naye akanipenda hataweza kuwa
nami.Inaniuma sana ?.? Clara alizidi
kumwaga machozi.Nikamuonea huruma
.Alikuwa amemumia moyo.Alikuwa akiteseka
kupita kiasi.Nilimlaani Emmy kwa laana zote
za dunia hii.kwa machungu na hasira
nilizokuwa nazo sikuwa tayari kumuona tena
Emmy katika maisha yangu.Nilimchukia
kupita kiasi.Nilimtazama Clara alivyokuwa
akilia na kuteseka kwa maumivu ya moyo
nikasikia uchungu sana.Huku machozi
yakinilenga nikamwambia
?Clara nafahamu ni uchungu kiasi gani ulio
nao kwa uamuzi huu mgumu uliouchukua.Naf
ahamu vile vile mateso na maumivu makali
unayoyasikia moyoni kwa mambo yote
ambayo yametokea katika kipindi hiki kifupi
tulichokuwa pamoja.Mateso na maumivu haya
hata mim ninayasikia kwa sababu sipendi
kukuona ukitoa machozi au ukiumia moyo
wako.Ninapokuona katika hali hii ninapatwa
na uchungu mwingi kwa sababu lengo langu
ni kukuona ukiwa ni mwenye furaha na
matumaini siku zote.Hata hivyo Clara uamuzi
huu umeuchukua haraka sana.Nadhani bado
nina nafasi ya kuweza kuyaweka sawa mambo
haya ili mimi na wewe tuweze kuishi kwa
amani katika maisha yetu.Naomba tafadhali
unipe nafasi nyingine ili niweze kuyamaliza
mambo haya na sisi tuweze kuishi kwa amani
bila bughudha ya aina yoyote ile.Nitafanya
lolote linalowezekana kufanyika ili mimi na
wewe tuweze kuwa pamoja.? Nikamwambia
Clara ambaye akainua kichwa na kunitazama
?Wayne nakuamini kwamba unaweza ukafanya
unavyoweza na sisi tukaishi kwa
furaha.Ndiyo ! tutaishi kwa furaha lakini
hatutakuwa na amani katika maisha
yetu.Hatutaweza kufunga ndoa kwa sababu
kisheria wewe bado ni mume wa mtu.Pamoja
na hayo Emmy hataweza kukuacha uishi kwa
furaha.Ataendelea kukuandama mpaka
mwisho wa uhai wake.Jambo la msingi
ninaloliona hapa ni sisi kuusitisha huu
uhusiano wetu ili Emmy aweze kuwa na
amani.Ninahisi vituko vyote hivi
anavyovifanya ni kwa sababu anakupenda.?
Clara akasema .
Nilijaribu kuendelea kumshawishi abadili
maamuzi yake lakini ilikuwa ngumu
sana.Msimamo wake haukutetereka.Kwa mara
nyingne tena nilikuwa nimeumizwa na
Emmy.Nilisikia maumivu makali sana tofauti
na hata pale mwanzo Emmy aliponiacha na
kwenda kwa Chris.kwa sababu yake nilikuwa
nimemkosa mwanamke niliyempenda zaidi
maishani mwangu.Nilikuwa nimeikosa furaha
ya maisha yangu.
TUKUTANE SEHEMU IJAYO???????..
 
BEYOND PAIN
SEHEMU YA 18
MTUNZI😛ATRICK.CK
ILIPOISHIA SEHEMU ILIYOPITA
?Wayne nakuamini kwamba unaweza ukafanya
unavyoweza na sisi tukaishi kwa
furaha.Ndiyo ! tutaishi kwa furaha lakini
hatutakuwa na amani katika maisha
yetu.Hatutaweza kufunga ndoa kwa sababu
kisheria wewe bado ni mume wa mtu.Pamoja
na hayo Emmy hataweza kukuacha uishi kwa
furaha.Ataendelea kukuandama mpaka
mwisho wa uhai wake.Jambo la msingi
ninaloliona hapa ni sisi kuusitisha huu
uhusiano wetu ili Emmy aweze kuwa na
amani.Ninahisi vituko vyote hivi
anavyovifanya ni kwa sababu anakupenda.?
Clara akasema .
Nilijaribu kuendelea kumshawishi abadili
maamuzi yake lakini ilikuwa ngumu
sana.Msimamo wake haukutetereka.Kwa mara
nyingne tena nilikuwa nimeumizwa na
Emmy.Nilisikia maumivu makali sana tofauti
na hata pale mwanzo Emmy aliponiacha na
kwenda kwa Chris.kwa sababu yake nilikuwa
nimemkosa mwanamke niliyempenda zaidi
maishani mwangu.Nilikuwa nimeikosa furaha
ya maisha yangu.
ENDELEA??????
Hatimaye siku tuliyopanga kurejea Arusha
ikawadia.Ilikuwa ni siku ya jumamosi yenye
kijua kitamu.Kila kitu tulikwisha kiweka tayari
kwa safari .Clara alikuwa amevaa miwani
mikubwa kwa ajili ya kuyaficha macho yake
yaliyokuwa mekundu na kuvimba kutokana na
kulia.Kila alipokuwa akinitazama alishindwa
kujizuia kutoa machozi.Alikuwa amenizoea
sana na alifahamu kwamba baada ya muda
mfupi ujao hataweza kuwa nami tena.Jambo
hili lilimuumiza mno.Alitamani kuwa nami
muda wote.Hata mimi nilisikia uchungu
mwingi kila nilipomtazama malaika huyu
ambaye nilimpenda zaidi ya ninavyoweza
kuelezea..Ilikuwa ni kama nimeonjeshwa asali
kisha nikanyang?anywa.Niliumia sana.
Clara aliamua kunisindikiza hadi Arusha ili
aweze kujaribu kupata walau muda wa
kuongea na Emmy na kumweleza kwamba
yeye na mimi tumeachana na kwa hiyo awe na
amani ya moyo.Sikulipenda sana wazo hili la
Clara kutaka kukutana na Emmy kwa sababu
ninamuelewa vizuri Emmy ni mwanamke
ambaye ninaweza kusema ana roho ya kikatili
sana.Pamoja na kulipinga wazo hilo la
kuonana na Emmy bado Clara aliendelea
kusisitiza na ikanilazimu kumkubalia
atakavyo.
Saa tano juu ya alama tulipanda ndege na
kuelekea mkoani Kilimanjaro.Tukashuka katika
uwanja wa ndege wa kimataifa wa Kilimanjaro
na kisha tukakodisha taksi hadi jijini
Arusha.Nilitaka tufikie hotelini lakini Clara
alisisitiza tupite kwanza kwangu ili aniache
nyumbani kwangu na baada ya hapo yeye
angeelekea hotelini ambako angelala hadi siku
ya pili yake ambayo alipanga kuondoka
kurejea katika makazi yake afrika kusini.
Geti halikuwa limefungwa.Niliamini maneno
ya Chris kweli Emmy alikuwa amerejea
nyumbani kwangu.Tukashusha mabegi yetu
na kuingia ndani.Sebuleni tulimkuta Emmy
akiwa amejaa tele akitazama luninga huku
akinywa mvinyo.Nilipomuona ghafla
nilipandwa na hasira za ajabu nikatamani
nimrukie na kumpa kipigo kikali lakini Clara
akaligundua hilo na kunisihi nisifanye jambo
lolote baya.Emmy alipotuona akasimama
akashika kiuono chake .
?Huyo Malaya wako unampeleka wapi?
Akasema Emmy kwa sauti kali
?Naomba umtoe ndani ya nyumba yangu
haraka sana?
Niliinua mkono juu kwa dhumuni la
kumtandika kibao lakini Clara akanishika
mkono
?wayne please don?t do that? akanisihi
?nani amekurudisha katika nyumba hii wewe
shetani? Nikafoka.Nilikuwa nimepandwa na
hasira kali.
?Nimerudi nyumbani kwangu.hapa ni
nyumbani kwangu na ninaweza kuingia na
kutoka muda wowote ule.Au umesahau kama
mimi ni mkeo? Emmy akasema huku akiibetua
midomo yake
Nilichukua begi langu na kulipeleka chumbani
halafu nikarudi sebuleni na kumkuta Emmy
amefura kwa hasira.
?Naomba tafadhali umtoe huyu kikaragosi
wako nje ya nyumba yangu kabla sijamfanyia
kitu kibaya? Emmy akafoka.
Kwa kasi ya aina yake nikamrukia na
kumkaba shingo yake kwa mikono yangu
miwili.Juhudi za Clara kuninasua nisimuumize
Emmy zilisaidia kwa sababu ningeweza
kufanya jambo baya kutokana na hasira
nilizokuwa nazo.
?Wayne tafadhali punguza hasira unaweza
ukamuua mwenzio.? Clara akasema huku
akihema kwa nguvu.
Nilimtazama Emmy ambaye alikuwa akihema
kwa nguvu huku akilia .
?Na iwe ni mwanzo na mwisho kumnyooshea
kidole Clara.Huyu ndiye mwanamke
ninayempenda na si wewe kunguru . Na
ukithubutu tena kumuinulia mdomo Clara
nitakukata shingo yako.? Nikamwambia Emmy
ambaye alikuwa akifuta machozi.
? Wayne mimi naomba niondoke.Hakuna
jambo lolote litakaloendelea hapa Nyote mna
hasira na hatuwezi kuongea lolote.Nitakuta
arifu nitaondoka saa ngapi siku ya kesho.kwa
heri Wayne? Clara akasema huku akilichukua
begi lake na kuanza kupiga hatua kutoka nje.
?Clara subiri kwanza? Nikamwambia na
kumfanya asimame.Nikaingia chumbani na
kutoka nikilisukuma begi langu.
?I?m going with you? Nikamwambia
Clara.Sikuwa tayari kumuona Clara akiondoka
kiurahisi rahisi namna ile. Clara akabaki
akishangaa
?Wayne !! ? Clara akasema kwa mshangao
?I?ve made up my mind Clara.I?m going with
you.Hakuna anayeweza kunitenganisha nawe.?
Nikasema huku nikilikokota begi langu.
?Wayne tumekubaliana kwamba urudi na
utafute suluhisho na mkeo.That?s for the best
of us all.Tafadhali Wayne naomba ukae na
mkeo na mtafute suluhisho la matatizo yenu ?
Clara akasema
?Clara siwezi kuwa na mke mwenye roho ya
kishetani kama huyu.This is not my wife?
Nikasema kwa hasira huku nikimshika mkono
Clara .
?Wayne humu huondoki leo. Leo utachagua
ama mimi ama huyo kahaba wako? Ikasikika
sauti ya Emmy ikisema kwa ukali.
?Twende tuondoke Clara.Usimjali huyo
mwenda wazimu? Nikamwambia Clara na
kuanza kulivuta begi lake kutoka nje.Kabla
sijaufikia mlango nikamsikia Emmy akiita kwa
ukali
?Wayne nimekwambia hutoki humu ndani leo.?
?Go to hell? nikasema bila kugeuka
?Wayne !! Emmy akasema kwa sauti kali
tayari tuliufikia mlango wa sebuleni nikageuka
na ghafla Emmy akairusha ile chupa kubwa
ya mvinyo akimlenga Clara.Kwa kasi ya ajabu
nikamsukuma Clara akaanguka pembeni na
chupa ile ikanipiga kichwani nikaanguka
chini.Likatokea giza nene.
***********************
Macho yangu yalikuwa mazito kufunguka
.Nilihisi usingizi mzito sana.Nilijitahidi
kuyafumbua macho yangu lakini bado
yalikuwa mazito.Nilijihisi kama vile niko
ndotoni.Nililifumbua jicho la kushoto lakini
sikuweza kuona vizuri.Bado nilikuwa
usingizini.Nilikuwa nikiona vitu viwili viwili na
sikuweza kutambua kitu chochote.Nikafumbua
na jicho lingine la kulia na kujaribu kuamka
katika ule usingizi mzito niliokuwa nimelala
lakini bado macho yalikuwa na
ukungu.Nikainua mkono wangu na kuyafikicha
macho na hatimaye nikaona kama niko katika
sehemu yenye mwanga mkali.Nikajaribu
kuinua kichwa lakini nikakirudisha chini kwa
haraka baada ya kuhisi maumivu makali sana
sehemu ya nyuma ya kichwa .Maumivu
niliyokuwa nikiyahisi ilikuwa ni kama
nimekatwa na kitu chenye ncha
kali.Nikausogeza mkono kichwani ili niweze
kuona sehemu niliyoumia nikakutana na
bandeji kubwa iliyokuwa imefungwa nyuma ya
kichwa changu.Hapo ndipo fahamu zilipoanza
kunirudia vizuri na kukumbuka tukio lililokuwa
limetokea mchana wa siku ile.Nilikumbuka
kwamba Emmy alinipiga na chupa ya mvinyo
kichwani iliyonipelekea kupoteza
fahamu.Nilipokumbuka jambo hili nikajikuta
nikiuma meno kwa hasira.
Kwa mbali nikahisi kama kitu cha baridi
kikiyagusa mashavu yangu.Nikainua mkono
na kuupeleka shavuni ili niweze kuona ni kitu
gani kilichokuwa kimenitembelea nikakutana
na kitu kama mkono wa mtu.Nikayakaza
macho ili kuweza kuona vizuri zaidi nikaiona
sura ya mwanamke ambaye sikuweza
kumtambua kwa haraka alikuwa nani.Bado
macho yangu yalikuwa yakiona vitu kama
ukungu ukungu.
?Wayne unajisikiaje? Iliniambia sauti ya
mwanamke yule aliyekuwa amekaa pembeni
yangu kitandani na mara moja nikaitambua
sauti ile ilikuwa ni ya Clara.
?Ouh Cla..ra ....ki?.ki?kichw?kichwa kinauma
sana? Nikatamka kwa taabu.
?Pumzika Wayne.Endelea kupumzika.? Clara
akasema huku akiinama na kunibusu.Nilipata
faraja ya aina yake baada ya kufahamu
kwamba Clara alikuwa pembeni
yangu.Nilimpenda na kumthamini Clara kuliko
kitu chochote kile.Clara alikuwa ndiye kila kitu
kwangu kwa sasa.Ni mwanamke pekee
ambaye ameweza kunirejeshea furaha ya
maisha yangu ambayo sikuwahi kuipata
katika siku zote nilizokuwa nimeishi na
Emmy.Nilikwisha weka nadhri kwamba
nitafanya kila niwezalo ili niweze kuwa na
mwanamke huyu mwenye kila sifa nzuri.
Kwa namna mikono ile laini ya Clara
ilivyokuwa ikipita katika mashavu yangu
nilihisi kama niko sehemu moja nzuri sana
yenye upepo mzuri.Nilihisi kama vile niko
katika bustani nzuri yenye wanyama na ndege
wa kila aina.Nilihisi raha ya ajabu.
Picha ya Emmy ikanijia tena nikauma meno
kwa hasira.Maumivu niliyokuwa nayasikia
yalinizidishia hasira juu yake.Taratibu
nilianza kuwa na mawazo labda Emmy ana
matatizo ya akili kwa sababu vitendo
anavyovifanya haviendani kabisa na mtu
mwenye akili ya kawaida.Nilikubaliana na
mawazo yangu kwamba yawezekana kabisa
Emmy akawa na matatizo ya akili.Sijawahi
kumtendea kitu chochote kibaya lakini yeye
amekuwa mstari wa mbele sana katika
kupambana na mimi kila kukicha.Amekuwa
akinisababishia maumivu makali kila uchao.
?Nahitaji kumuepuka huyu mwendawazimu
Emmy kwa sababu bila hivyo anaweza
akanitoa uhai.Nahitaji sana kuwa mbali na
Emmy kwa namna yoyote ile kwa sababu
nisipofanya hivyo anaweza hata akamdhuru
Clara.Huyu mwanamke anaonekana kabisa
ana mapungufu ya akili.Sitaki kumuona tena
Emmy katika maisha yangu? Nikawaza na
kuyafumba macho yaliyokuwa mazito
nikalala.
************************
Nilifumbua macho na kwa sasa niliweza
kuona vizuri. Miale ya jua iliyokuwa ikipiga
ukutani kupitia dirishani iliniashiria kwamba
jua lilikuwa likielekea kuzama.Taratibu
nikainua kichwa changu na kisha nikakaa
kitandani.Nilikuwa katika chumba cha peke
yangu na hakukuwa na mtu yeyote mle
chumbani.Katika meza ndogo iliyokuwa
pembeni ya kitanda niliiona saa yangu ndogo
ya mkononi.Nikanyoosha mkono nikaichukua
na kutazama muda.Ilipata saa kumi na mbili
kasoro dakika kadhaa.Bado niliendelea kusikia
maumivu makali ya kichwa katika ile sehemu
niliyokuwa nimepigwa na chupa.Nikainama na
kutafakari kwa kina juu ya mwisho wangu na
Emmy.
?Kama nisipochukua hatua za haraka anaweza
akaniua huyu mwanamke.Lazima nimuepuke
haraka sana.? Nikawaza na mara mlango
ukafunguliwa akaingia daktari .
?Unajisikiaje Wayne? Akaniuliza yule daktari
?najisikia vizuri japokuwa bado nasikia
maumivu makali sana kichwani? nikamweleza
daktari
?Pole sana.Yule mwanamke hakuwa na nia
njema na wewe.Una bahati sana kwamba
jeraha halikuweza kuingia ndani sana
vinginevyo tungekuwa tunaongea mambo
mengine sasa hivi.? Daktari akanieleza huku
akinifanyia vipimo.Nilikosa neno la kumjibu
kutokana na hasira nilizokuwa nazo juu ya
Emmy .
?Wayne unaendelea vizuri sana na hatuna
sababu ya kuendelea kukuweka hapa
hospitali.Unaweza ukarejea nyumbani kwako
lakini utaendelea kuja hapa kwa ajili ya
kusafisha na kufunga kidonda chako.Kuna
kitu kimoja ambacho ninataka kukuasa kama
mwanaume mwenzangu ni kwamba jaribu
kuwa makini sana na huyu mwanamke
aliyekusababishia jeraha hili kwa sababu
inaonekana wazi alikuwa na lengo la
kukuua.Sehemu aliyokupiga si sehemu nzuri
hata kidogo.?
?Nitajitahidi daktari .Nashukuru sana ?
nikasema .
?Nimekwisha mtaarifu rafiki yako Clara na
tayari amekwenda dirishani kulipa gharama
zote pamoja na kuchukua dawa ambazo
utakuwa ukizitumia?
?Nashukuru sana daktari ? Nikasema na kisha
daktari yule akatoka mle chumbani.Dakika
mbili baada ya daktari kuondoka mle
chumbani nilimokuwa nimelazwa mlango
ukafunguliwa akaingia Clara.Akatabasamu
baada ya kuniona nikiwa nimekaa
kitandani.Katika bega lake la kushoto alikuwa
amefungwa bandegi.
?Ouh Wayne..Unajisikiaje mpenzi wangu?
Akauliza Clara huku akikaa kitandani karibu
yangu na kunibusu
?Ninajisikia vizuri Clara ila kichwa ndiyo bado
nakisikia kinauma sana huu upande wa
nyuma? Nikasema
?Pole sana Wayne.Nashukuru sana kukuona
unaendelea vizuri .Nilikuwa na wasi wasi
mwingi kwa sababu sehemu aliyokupiga
Emmy ni sehemu mbaya sana na ambayo
inaweza kusababisha mtu akapoteza uhai
wake.? Akasema Clara
?Hata daktari amenieleza kwamba mahala
hapa Emmy aliponipiga na chupa ni pabaya
sana. Mbona bega lako limefungwa bandeji?
Nikauliza
?baada ya kukupiga na chupa kichwani
ulianguka ukapoteza fahamu na damu kuanza
kukutoka,ikanilazimu kurejea ndani kwa
dhumuni la kukusaidia na ndipo hapo
nilipokutana na Emmy akiwa na kisu mkononi
akataka kunichoma nacho nikawahi
kumdhibiti na akafanikiwa kunikata
bega.Nilikimbia nje nikaomba msaada wa
majirani ambao walifika mara moja na
kumkamata Emmy kisha kwa pamoja
tukaelekea polisi ambako aliwekwa rumande
hadi hapo utakapopona ili aweze kufikishwa
mahakamani.
Wayne nina wasi wasi mkubwa kuhusu
Emmy.Sina hakika kama atakuwa mzima wa
akili.Nina wasi wasi anaweza akawa na
matatizo ya upungufu wa akili.? Clara
akasema
?hata mimi nimekuwa nikiwaza hivyo kwa
sababu vitendo anavyovifanya Emmy
haviendani kabisa na vitendo vya binadamu
wa kawaida.Nashukuru sana kama tayari
anashikiliwa na vyombo vya dola.Mwanamke
yule hafai kabisa kukaa katika jamii
iliyostaarabika.Nitahakikisha anafungwa na
kuozea gerezani.Sintaweza kumsamehe
kamwe kwa hili alilolifanya.Pamoja na hayo
nimefikiria kwa sasa itanibidi kuishi mbali
naye.Nitajitahidi kumuepuka Emmy kwa
gharama zozote zile.Kama nikiendelea kukaa
hapa karibu naye iko siku atanitoa uhai
wangu? Nikamweleza Clara ambaye bado
alikuwa amekaa kitandani karibu yangu
akinitazama kwa huruma
?Wayne nilikwisha fanya maamuzi ya
kuachana nawe na kuondoka zangu lakini kwa
kitendo alichokifanya Emmy kimenifanya
niogope kukuacha peke yako.Nina hakika
mwanamke huyu hana nia njema nawe.Iko
siku atakufanyia jambo baya sana .Siwezi
kuondoka na kukuacha peke yao Wayne.bado
nakupenda na nitakuwa nawe siku zote.
Sikuachi tena mpenzi wangu? Clara akasema
na kunikumbatia.Siwezi kuelezea ni jinsi gani
nilivyopatwa na furaha ya ghafla kiasi
kwamba sikuhisi hata maumivu ya kichwa
tena.
?nashukuru sana Clara kwa uamuzi wako wa
kubaki nami.Hata mimi sikuwa tayari
kukupoteza kirahisi rahisi namna hii kwa
sababu ya mwanamke mwendawazimu kama
Emmy.Nakuahidi nitakuwa nawe siku zote na
sintakubali yule kichaa akuguse tena.Safari
hii nimedhamiria kumfundisha adabu.na kama
anahitaji kuufahamu ubaya wangu basi
ajaribu kunifuatilia tena.Iwapo atanifuata
fuata tena sintakuwa na huruma kwake hata
kidogo.? Nikasema na kumfanya Clara
atabasamu.
?Wayne muda unakwenda kwa kasi .Jiandae ili
tuweze kuondoka hapa hospitali kwa sababu
daktari amekwisha toa ruhusa? Clara akasema
huku taratibu akinishika mkono na
kunishusha kitandani.Akanisaidia kuvaa nguo
zangu halafu taratibu tukatoka pale hositali
na kuondoka.Sikutaka kwenda na Clara
nyumbani kwangu tena kwa kuepusha
mtafaruku mwingine.Niliichukia mno nyumba
ile licha ya kwamba ni nyumba yangu
mwenyewe.Badala yake tulikwenda kuchukua
chumba hotelini ili tupumzike kwa usiku
mmoja kabla ya kupanga nini kinaendelea.
TUKUTANE SEHEMU IJAYO?????
 
Back
Top Bottom