Kipi kigezo cha kuoa au kuolewa?

Kipi kigezo cha kuoa au kuolewa?

Richer

JF-Expert Member
Joined
Jun 9, 2025
Posts
2,114
Reaction score
3,479
Habari wakuu,

So, nimekumbuka hili jambo nikaone nishare kupata na kuelea mitazamo tafauti.
Wikendi hii nilipata fursa ya kwenda maeneo fulani na pia nilibahatik kushuhudia harusi ya jamaa yetu mmoja wa kitambo sana.

Nilipata nafasi kushuhudia wakifunga pingu za maisha kanisani na baada ya hapo tulifika location ya wao kufanya photo shoot kama kumbukumbuku ya siku yao mpya.

Ajabu location tuliyoenda nilishuhudia karibu harusi saba zilikuja hapo kwa ajili ya photo shoot, wakati nikishangaa mpiga picha akanambia yaani unashangaa ni harusi saba, kuna siku hadi kumi tano zinafika kwa siku maana ni location pendwa.

Nilishangaa sana maan mimi kila nikikaa na majamaa zangu wa kazini yaani stori zteu mwelekeo ni kama hakuna mwenye matarajio ya kuoa au kuolewa hivi karibuni, yaani ni kama mitano tena

Sasa nimebaki nikijiuliza au ni mimi ndo nina mtazamo wa kihafidhina kuhusu kuoa au kuolewa?
 
Ukiwa umebalehe we oa tu mkuu maana sasa utakuwa na uwezo wa kupachika mimba (kwa mwanaume).

Mwanamke ukishabalehe unaweza kuolewa kwa maana sasa unaweza kupachikwa mimba, vijana wa siku hizi wanasema kibendi.
 
Ukiwa umebalehe we oa tu mkuu maana sasa utakuwa na uwezo wa kupachika mimba (kwa mwanaume).

Mwanamke ukishabalehe unaweza kuolewa kwa maana sasa unaweza kupachikwa mimba, vijana wa siku hizi wanasema kibendi.
daaah 😂 😂 😂
 
Kigezo cha kuoa au kuolewa ni ukomavu wa akili, ukiwa na akili iliyokomaa basi ni kigezo tosha cha kuoa au kuolewa
 
Kama una sababu za msingi za kukataa ndoa ikatae, kama huna jitaftie wa kumvalisha kichuma cha duara
 
Back
Top Bottom