Lumbi9
JF-Expert Member
- Oct 12, 2014
- 8,564
- 11,799
BEYOND PAIN
SEHEMU YA 1
MTUNZI : PATRICK .CK
Ni saa kumi jioni nikiwa maeneo ya
Kimandolu nikielekea Usa river katika baa
iliyotulia ya Roterdam garden mahala
panapofanyika vikao vya harusi
yangu.Wanakamati ya maandalizi walichagua
mahala hapa kutokana na utulivu wake kwani
kuna bustani nzuri na hata huduma zake ni
nzuri sana.Nikiwa maeneo haya ya Kimandolu
gari ikienda taratibu kutokana na magari
mengi kukaa pembeni ya bara bara kwa muda
mrefu kwa kupisha misafara ya viongozi wa
jumuia ya Afrika mashariki waliokuwa na
kikao chao hapa Arusha.Siku zote
kunapokuwa na mikutano ya namna hii jijini
Arusha huwa kunakuwa na adha kubwa kwa
watumiaji wa bara bara hii ya Moshi - Arusha
kwa sababu ndiyo bara bara kuu waitumiayo
viongozi hawa wakitokea katika uwanja wa
ndege wa kimataifa wa Kilimanjaro
(KIA).Mara simu yangu ikaita nikaitazama na
kukuta ni Mr Cheleo mmoja kati ya
wanakamati.
?Haloo kaka? nikasema
?Haloo ,uko wapi? Sisi tumeshafika
tunakusubiri wewe tu.?
?Niko njiani kaka si unajua leo njia ilikuwa
imefungwa viongozi walikuwa
wanaondoka.Ndani ya dakika kumi nitakuwa
nimefika hapo Usa river.?
?Ok kaka tunakusubiri?
Hiki kilikuwa ni mojawapo ya kikao cha
maandalizi ya harusi yangu inayotarajiwa
kufanyika muda wa kama mwezi mmoja
ujao.Harusi ambayo kila mmoja wa rafiki
zangu alikuwa akiisubiri kwa hamu
sana.Nimekuwa mchangiaji mzuri wa harusi
za rafiki zangu na kuhakikisha zinafana safari
hii walikuwa wamepania sana kufanya
sherehe ya harusi yangu kuwa ya kihistoria.
Tulipofika maeneo ya madukani gari zikaanza
kwenda kasi na dakika tano baadae nikawasili
usa river katika baa tulivu ya
Roterdam.Nikapaki gari na kuelekea
bustanini.Nikawasalimia wanakamati na
kuwaomba radhi kwa kuchelewa kisha kikao
kikaendelea.Kilikuwa ni kikao kirefu .
Wakati kikao kikiendelea nikachukua simu na
kumtumia mpenzi wangu Emmy ujumbe
mfupi.Kwa siku tatu nilikuwa na shughuli
nyingi na sikupata hata muda wa kuonana
naye.Kwa sasa emmy anasoma digrii ya
sheria katika chuo kikuu cha Tumaini
makumira.Kila jioni huwa ana desturi ya
kupita kwangu na hata kama sipo kwa kuwa
ana ufunguo wa nyumbani kwangu huwa
ananisubiri mpaka nikirudi tunakaa wote
kisha namrudisha kwake.
?Hallow sunshine,niko kwenye kikao hapa
roterdam.Baada ya kutoka hapa nitapita
kwako.Missing you soooo much.? Huu ndio
ujumbe mfupi niliomtumia Emmy kipenzi cha
moyo wangu.
Tukaendelea na kikao.Baada ya kama robo
saa hivi tangu niutume ule ujumbe mfupi wa
maandishi kwa mpenzi wangu Emmy simu
yangu inaita kuangalia zilikuwa ni namba za
emmy.Nikainuka na kwenda mbali kidogo ili
niweze kuongea naye.
?Halloo Darling ?Nikasema kimahaba.kwani
ndivyo tulivyozoea wakati tunaongea simuni.
Nusura moyo unipasuke kwa mstuko pale
nilipoisikia sauti nzito ya kiume ikijibu.
?Mwanaharamu wewe,mpenda wake za
watu.Huna haya unamwita nani Darling?
Kumbe ndio mchezo wako huo wa kudandia
wanawake wa watu.Leo nimekupata.?
Nilibaki nimeduwaa kwa sekunde kadhaa
nisijue nini cha kusema.sikuelewa yule jamaa
alikuwa akimaanisha nini.Huku nikitabasamu
nikauliza
?Mbona sikuelewi wewe.Unasemaje? samahani
kama simu zimeingiliana?
?Simu hazijaingiliana we juha.We si ndio
Wayne? Wayne mkotela?.
?yah ndio mimi? Nikajibu huku mapigo ya
moyo yakinienda kwa kasi baada ya yule
jamaa kulitamka jina langu
? Wewe si ndio umemtumia Sarafina ujumbe
wa maandishi sasa hivi ukisema unakuja
kumuona ukitoka kwenye kikao?
?Mimi nimemtumia ujumbe Emmy na sio
sarafina?
?sasa sikiliza wewe mjinga?.?Nilihamaki
baada ya kuitwa vile lakini nikavumilia
nimsikie alichotaka kusema
?Iwe ni huyo Sara au Emmy kama unavyojua
lakini nakwambia kuwa huyu ni mke wa mtu
na mimi ndio bwana wake.?..
?Unasemaje wewe??..Nikauliza kwa hamaki
?Hebu mpe Emmy simu yake haraka.Mpuuzi
wewe? Nikasema tena kwa hasira
?Mpumbavu wewe ! hivi nikwambie mara ngapi
Hakuna Emmy hapa?Huyu anaitwa
Sarafina.Kama alikwambia anaitwa Emmy
alikudanganya.Huyu ni sarafina na mimi ndio
mumewe,mimi ndio ninayemlipia hii nyumba
anayoishi na ni mimi ndio niliyemtafutia kazi
pale AICC na baadae nikamtafutia nafasi ya
masomo pale Makumira.Mimi ndiye
ninayemlipia ada na kila kitu.Mimi ndiye
ninayemuweka mjini.Nilikuwa nje ya nchi
nilikuwa napata taarifa kuwa kuna mtu
anatembea na mke wangu nikajua ni utani.Leo
ndio nimegundua kuwa ni kweli? akasema Yule
jamaa.
?Mjinga mkubwa wewe,huna haya mimi ndie
ninayemlipia Emmy ada zote za masomo na
hata nyumba anayokaa mimi ndiye
ninayelipa.Na kwa taarifa yako mpumbavu
wewe,sasa hivi tuko katika maandalizi ya
harusi yetu na kesho jumapili kanisani
wanasoma tangazo la kwanza la ndoa
yetu.Hivyo nakuomba usijaribu kwa namna
yoyote ile kuleta upumbavu wako ? Tayari
hasira ilikwisha nipanda nikatamka maneno
yale kwa hasira.
?Sikiliza we mjinga yaani pamoja na kukueleza
kote huku bado hunielewi sasa Emmy huyu
hapa hebu ongea naye?
Nikasikia akimpa mtu simu na kumlazimisha
?Hebu ongea na huyu mbwa mwenzako
mweleze ukweli mimi ni nani na mkanye
akome kuanzia leo kukufuata fuata la sivyo
nitamfanyia kitu kibaya sana ,hanijui mimi ni
nani mjinga huyu? maneno haya nikayasikia
kwa mbali.Mara nikasikia kitu ambacho
sikukitegemea kukisikia maishani
mwangu.Niliomba ardhi ipasuke niingie
ndani.Nilitamani nijimalize pale pale.sikuona
thamani tena ya kuendelea kuishi katika dunia
hii.
Niliisikia sauti ile tamu na nyororo iliyozoea
kuniburudisha kila siku na kunifanya nione
kama niko peponi,sauti ambayo niliamini ni
sauti nzuri kuliko zote duniani,sauti ya
mpenzi wangu,bibi harusi mtarajiwa
Emmy.Huku akilia kwa kwikwi akatamka
maneno ambayo yalinifanya niichukie dunia
na watu wake na hasa wanawake.
?Wayne I?m sorry mimi ni mke wa mtu,na
ninaomba usiendelee tena kumtukana mume
wangu?
Ilikuwa ni kama niko ndotoni nikazubaa kwa
sekunde kadhaa kisha nikajikaza kiume na
kuuliza tena.
?Emmy is that you????.
?Yes Wayne please leave me alone.Usinipigie
simu tena.Mimi nina bwana wangu?
Machozi yalianza kunitoka.Sikuamini kile
nilichokisikia.
?Please Emmy tell me its not true ? Nikasema
tena huku machozi yakinitoka.
?My name is not Emmy?..Akashindwa
kuendelea alikuwa akilia.Yule jamaa
akachukua tena simu
?Sasa umeamini we kijana.Tafadhali
usiendelee kumfuata fuata sarafina.Kitaka
chokupata usije kumlaumu mtu???..?Akamal
izia kwa tusi zito na kukata simu
Nikahisi miguu ikiisha nguvu nikaakaa chini.
Christopher rafiki yangu mkubwa alihisi
lazima nitakuwa na tatizo akanifuata
.Akastuka baada ya kunikuta nimekaa chini.
?Wayne.. ?Akaita nikamuangalia sikuwa na
nguvu za kujibu.
?Wayne una tatizo gani?
Akawaita wanakamati wote wakaja mbio na
kuanza kunipepea.Nikaletewa maji
nikanywa.Dakika kama tano hivi baadae
nikaweza kuongea
?Take me home? Nikamwambia Chris
?Wayne una tatizo gani.Twende hospitali?
Akasema Chris
?No ! take me home? Nikasema huku nikijaribu
kuinuka.Wakanisaidia kutembea hadi garini
kisha Chris akawasha gari na kuondoka
kunipeleka nyumbani.
Picha mbali mbali zikawa zinakuja na
kupotea.Nilihisi kama vile niko ndotoni .Chris
aliendesha kwa kasi bila kunisemesha.Tul
ipofika maeneo ya sanawari nikafungua
mdomo na kumwambia Chris.
?Nipeleke kwa Emmy? Chris alikuwa
akipafahamu anapoishi Emmy hivyo tulipofika
maeneo ya Ilboru akakata kushoto na moja
kwa moja akaelekea nyumbani kwa Emmy.
Alisimamisha gari nje ya nyumba ya
Emmy.Sikuongea kitu nikafungua mlango
nikashuka garini.Mlinzi wa kimasai wa
nyumba ya Emmy alinifahamu hivyo
aliponiona akanisalimia nikapita zangu hadi
ndani.Chris naye alikuwa akinifuata kwa
nyuma.Nilisimama mlangoni na kusikia watu
wakinong?ona kwa ndani.Nilikuwa na funguo
ya mlango nikaufungua bila kugonga na
kuingia ndani.Sebuleni nilimshuhudia Emmy
akiwa kifuani kwa baba mmoja mnene wakiwa
katika mahaba mazito.Nikaanguka na
kupoteza fahamu.
* * * *
Nilizinduka na kujikuta mahala
nisipopafahamu.Nilikuwa katika chumba
chenye harufu ya dawa.Ndani ya chumba hiki
kulikuwa na watu kadhaa.Mtu wa kwanza
kumtambua alikuwa Chris.
?Pole sana Wayne?.Akasema huku akinishika
kichwa.?Tafadhali usiinuke , endelea
kupumzika.? Muda huo huo akaja daktari
akiwa ameongozana na wauguzi
wawili,nikajua hapa nipo hospitali.daktari
akanipima kisha akasema
?Kwa sasa unaendelea vizuri.Itabidi ulale
hapa leo ili tuendelee kukuangalia zaidi?
Sikuwa na ubishi ingawa sikuhisi kuumwa
sehemu yoyote ile zaidi ya kichwa kuwa kizito
mno.Daktari akatoa maelekezo kadhaa kwa
wale wauguzi akaandika pia katika kijikadi
kisha akatoka.Pale mlangoni nilisikia
akiongea kama na kundi la watu.na dakika
hiyo hiyo watu zaidi ya ishirini wakaingia mle
chumbani.Walikuwa ni wanakamati ya
maandalizi ya harusi yangu pamoja na baadhi
ya rafiki zangu.Walinipa pole nami
nikawahakikishia kuwa niko salama
wakanitakia usiku mwema wakaondoka.pale
hospitali nikabaki na Chris
?Chris nini kilitokea mpaka nikaletwa hapa?
Chris akanitazama kisha akajibu
?Wayne ulianguka ukapoteza fahamu ,ikanibidi
nikulete hapa katika hospitali hii .Usijali kila
kitu kinakwenda vizuri.Daktari anasema kesho
asubuhi atakuruhusu?
Niliposikia kuanguka na kupoteza fahamu
,ndipo nikalikumbuka tukio zima
lililotokea.Ghafla fahamu zikanipotea tena.
Nilirejewa na fahamu baadae sikujua ni saa
ngapi.Ukiacha yule daktari mmoja
aliyekuwapo mida ile sasa walikuwapo
watatu.hali hii iliniogopesha sana.Nikaogopa
pengine hali yangu si nzuri.Daktari mmoja
mzee mwenye miwani akanisogelea na
kuniuliza
?Wayne unajisikiaje sasa hivi??
?Najisikia safi ila kichwa ni kizito sana.Nahisi
kama kizungu zungu kwa mbali?
?Ok sawa.Hali yako inaendelea vizuri,vipimo
vyote vinaonyesha uko sawa ila unachotakiwa
kwa sasa ni kujaribu kutokuwaza kitu
chochote kinachoweza kukusababishia
ukapoteza fahamu kwa mara nyingine.Jaribu
kupata mapumziko ya kutosha na jitahidi
sana kutokuwaza?..?
Nilimtazama yule daktari sikuwa na jibu la
kumpa.Nafikiri hakujua kitu gani
kilichonipata.Hakuyaelewa maumivu
yaliyokuwa moyoni mwangu.
?Ok dokta nitajitahidi?.Nilisema huku machozi
yakinilenga.
Madaktari na wauguzi wakatoka na kuniacha
chumbani mimi na Chris.hawakutaka Chris
aniache peke yangu kwa kuwa waliogopa
pengine ningeweza kujidhuru.
Niliinuka na kukaa kitandani.Chris akanisaidia
nikakaa sawa.
?Chris I hate the world?Nikasema kwa sauti
ndogo
Chris akanitazama akasema.
?Wayne jitahidi upumzike.Usiwaze lolote kwa
sasa.Everything will be ok?
?No Chris.Nothing is ok.Emmy lied to
me????????Nikasema huku machozi
yakinitoka.
?Don?t cry buddy,be strong? akasema chris
huku akinipiga piga mgongoni
? I loved her .I loved her Chris more than I love
myself.Lakini ona kitu alichonifanyia?
..Nitauweka wapi uso wangu mimi?.?.Uso
wote ulijaa machozi.Iliniuma kupita kiasi.
?Wayne lala kwanza.Tutaongea asubuhi?
Akasisitiza Chris.
?No Chris siwezi lala wakati mwanamke
niliyempenda amenisaliti?.why me????? Why
this pain????
?Ok brother let it out??let it out?.?Akasema
Chris.
?Emmy amenidanganya muda wote huu kumbe
ni mke wa mtu?.?
?what!!!!!!!!? Akahamaki Chris
?Yah! ana bwana wake.Ndiye yule tuliyemkuta
amelala naye kwenye sofa pale sebuleni
kwake.Kwa mdomo wake mwenyewe
ameniambia nisimsumbue yeye ana mume
wake ?
Chris akainuka na kuanza kuzunguka mle
chumbani huku ameshika kichwa.
?Is this true brother?Akauliza
?Yah..kwa mdomo wake amenitamkia maneno
haya?.It hurt Chris it hurt so much.?
?Mwanaharamu huyu??.?Akasema Chris kwa
hasira
?Kesho ndoa yetu inatangazwa kanisani kwa
mara ya kwanza??.nikashindwa
kuendelea.Nilishindwa kujizuia kuangusha
machozi.
?Wayne its gonna be ok.Jitahidi ulale kesho
tutayaongea mambo haya.Usiwaze sana
kilichotokea.Hii ni mitihani tu ya maisha?
Chris alijaribu kwa kila njia kunibembeleza ili
niweze kuwa katika hali yangu ya kawaida
lakini kwa hali halisi jinsi ilivyo ni ngumu
sana.
Ni Jumatano ya wiki hii tumetoka kuandikisha
ndoa kanisani na kesho tangazo la kwanza
linaanza kusomwa.tayari maandalizi yote ya
harusi yamekamilika .Nitauweka wapi uso
wangu mimi.Nitawaeleza nini watu
wanaoisubiri harusi yangu??Nitawaleleza nini
wazazi na ndugu zangu? Simlaumu
mtu.Emmy nilimchagua mwenyewe.Hakuni
chagulia mtu yeyote.Iwapo ningechaguliwa na
wazazi au mtu mwingine , ningekuwa na kila
sababu ya kuwatupia mzigo wa lawama wao
kwa uchaguzi wao usiofaa.Lakini hili lilikuwa
ni chaguo langu mwenyewe..Huu ni mzigo
wangu na inanibidi nisimame kidete
niukabili.Nilijilaza kitandani na sijui hata saa
ngapi nilipata usingizi.
Saa tano asubuhi tayari nilikuwa nyumbani
kwangu maeneo ya majengo.Nilikuwa najisikia
mzima wa afya isipokuwa kichwa kilikuwa
kikiniuma kwa mbali.Chris ndiye aliyenichukua
hospitali na kunirudisha nyumbani.
Mpaka sasa hivi hakuna mtu mwingine
aliyekuwa akijua nini kilichotokea na
kupelekea kupoteza fahamu na kulazwa
hospitali zaidi yangu na Chris.Sikutaka
kuharakisha kuliweka wazi jambo hili
gumu.Nilitaka kuacha kwanza akili yangu
itulie.Nilikaa kidogo sebuleni ,halafu
nikamwambia Chris aniache nikapumzike.
?Brother naomba nikapumzike,halafu
tutaongea jioni.Ila tafadhali naomba
usimwambie mtu yeyote nini kilichotokea..?
?Ok wayne nenda kampumzike ila tafadhali
don?t do anything stupid?Akasema Chris huku
akitoa tahadhari kwani madaktari walimuonya
asikubali kuniacha peke yangu kwa kuhofia
pengine ninaweza kujidhuru.
?C?mon Chris,I?m not a kid.Haya ni mambo ya
kawaida katika maisha.Let me have a rest
then I?ll know what to do next.?
?Ok wayne..nitapita mchana kukuangalia.Nik
uletee chakula gani mchana?
?Nothing Chris.Usiniletee chochote.I don?t feel
like eating anything.?
?Unatakiwa ule Wayne.unatakiwa uwe na
nguvu.?
Sikumjibu kitu nikamtazama na kuondoka
kuelekea chumbani kwangu.
Nilikaa kitandani,nikalifungua kabati langu na
kutoa albamu kubwa la picha.Humu kuna
picha nyingi ambazo nimepiga na emmy
tangu tulipoanza mapenzi yetu .Picha yetu ya
kwanza mimi na yeye ikanikumbusha
tulikwenda picnic Ziwa Duluti.Ni siku
tuliyofurahi sana.Siwezi kuisahau siku
hii.Nikaendelea na kuzifunua picha
nyingine.Wakati nikiendelea na kuzitazama
picha simu yangu inalia.Alikuwa ni mama
yangu.
?mama shikamoo? nikamsalimu
?Marahaba baba ,hamjambo?
?hatujambo mama,vipi mnaendeleaje?
?Huku wote wazima.Ni baba yako tu kichwa
chake kile kinamsumbua sana lakini
anaendelea vizuri?
?Mpe pole sana ?Nikajibu kwa ufupi.
?Vipi mkwe wangu hajambo?
Nikasita kujibu.
?eenh jamani hajambo mama mkwe? Mama
akauliza tena baada ya kuona sijamjibu
?Hajambo mama?Nikajibu huku nikiuma meno
kwa hasira.Mwanamke huyu amewadanganya
hadi wazazi wangu.Iliniuma sana.
?nashukuru kama ni mzima.Vipi mnaendeleaje
na maandalizi ya harusi?
?mama maandalizi ni mazuri.Tunaendelea
vizuri?
?sawa baba.Leo huku wamesoma Tangazo la
kwanza..Hivi ninavyokwambia watu
wanajiandaa isivyo kawaida,kila ndugu
anataka aje kwenye harusi yako.?
Sikuwa na cha kusema.Machozi yalikuwa
yananitoka.
?Mama nashukuru.Nitakupigia baadae
tutaongea vizuri zaidi?
?Sawa baba?
Nilikata simu na kuitupia kitandani.hasira
zikanipanda.
?Damn you Emmy?..?
Nilizungunguka zunguka mle chumbani
nikijaribu kuwaza na kuwazua bila kupata
jibu.Nikatoka na kurudi sebuleni.Nikafungua
kabati ninamoweka cd na kuchukua moja ya
cd niipendayo sana ya mmoja kati ya
wanamuziki mahiri kwenye mziki wa bongo
fleva,Hamis mwinjuma au Mwana F.A .Huu
wimbo wake niliona ni kama vile alinitungia
mimi kwa sababu ulinihusu mimi.Ubeti wa pili
ndio uliniumiza zaidi ukanifanya niurudie tena
na tena
?hata nikitaka kuoa niambie ntamuoa nani?/
watu wana watu wao wengine toka zamani/
ukiambiwa we ni boyfriend haimaanishi uko
peke yako/
wadogo usoni wanahifadhi wazee wako/
sijui ni dhiki au tamaa tu??/
watoto wanaanika njaa tu/
hawafikirii mapenzi wanachoona wao ni
mkwanja tu/?
Maneno haya yalinichoma moyo.Kijana huyu
aliimba vitu vya kweli kabisa na yote
aliyoyaimba yamenikuta mimi.
Nikarudi tena chumbani sikujua nini cha
kufanya.Nilikuwa kama nimechanganyikiwa
vile.Nikaona ni bora nijilaze kitandani na
kijiusingizi kikanipitia.
Nilistuka na mlio wa simu iliyokuwa kichwani
kwangu,alikuwa ni Chris.
? Haloo? Nikasema
?Wayne umelala??
?Ndiyo nilikuwa nimelala?
?Ok .Sasa wayne naomba uwe na moyo
mgumu na usihamaki tafadhali.Ni kwamba
Emmy amenifuata na hapa nilipo niko naye
na ni yeye ndiye alinisisitiza nikupigie simu
hii.?
?Unasemaje Chris????? ?Nikasema kwa
ukali.Sikutegemea kusikia kitu kama kile.
?Wayne niko na Emmy hapa.amenitafuta na
kuomba nafasi ya kuongea na wewe?
?Chris????..?Nilidakia,sikutaka aendelee tana
kunipa habari za yule baradhuli
?Chris tafadhali.Kama na wewe unataka
tukosane hamna shida ila tafadhali naomba
usinipe habari zozote kuhusu huyu
mwanamke.?
Nikakata simu.Mwili wote ulikuwa
unanichemka kwa hasira.Sikutaka kumsikia
tena emmy katika maisha yangu.Nilikuwa na
hasira mbaya mno kwa kitendo alichonifanyia
na kama angekuwa karibu yangu sijui hata
ningemfanya kitu gani.
TUKUTANE SEHEMU IJAYO?????????..
SEHEMU YA 1
MTUNZI : PATRICK .CK
Ni saa kumi jioni nikiwa maeneo ya
Kimandolu nikielekea Usa river katika baa
iliyotulia ya Roterdam garden mahala
panapofanyika vikao vya harusi
yangu.Wanakamati ya maandalizi walichagua
mahala hapa kutokana na utulivu wake kwani
kuna bustani nzuri na hata huduma zake ni
nzuri sana.Nikiwa maeneo haya ya Kimandolu
gari ikienda taratibu kutokana na magari
mengi kukaa pembeni ya bara bara kwa muda
mrefu kwa kupisha misafara ya viongozi wa
jumuia ya Afrika mashariki waliokuwa na
kikao chao hapa Arusha.Siku zote
kunapokuwa na mikutano ya namna hii jijini
Arusha huwa kunakuwa na adha kubwa kwa
watumiaji wa bara bara hii ya Moshi - Arusha
kwa sababu ndiyo bara bara kuu waitumiayo
viongozi hawa wakitokea katika uwanja wa
ndege wa kimataifa wa Kilimanjaro
(KIA).Mara simu yangu ikaita nikaitazama na
kukuta ni Mr Cheleo mmoja kati ya
wanakamati.
?Haloo kaka? nikasema
?Haloo ,uko wapi? Sisi tumeshafika
tunakusubiri wewe tu.?
?Niko njiani kaka si unajua leo njia ilikuwa
imefungwa viongozi walikuwa
wanaondoka.Ndani ya dakika kumi nitakuwa
nimefika hapo Usa river.?
?Ok kaka tunakusubiri?
Hiki kilikuwa ni mojawapo ya kikao cha
maandalizi ya harusi yangu inayotarajiwa
kufanyika muda wa kama mwezi mmoja
ujao.Harusi ambayo kila mmoja wa rafiki
zangu alikuwa akiisubiri kwa hamu
sana.Nimekuwa mchangiaji mzuri wa harusi
za rafiki zangu na kuhakikisha zinafana safari
hii walikuwa wamepania sana kufanya
sherehe ya harusi yangu kuwa ya kihistoria.
Tulipofika maeneo ya madukani gari zikaanza
kwenda kasi na dakika tano baadae nikawasili
usa river katika baa tulivu ya
Roterdam.Nikapaki gari na kuelekea
bustanini.Nikawasalimia wanakamati na
kuwaomba radhi kwa kuchelewa kisha kikao
kikaendelea.Kilikuwa ni kikao kirefu .
Wakati kikao kikiendelea nikachukua simu na
kumtumia mpenzi wangu Emmy ujumbe
mfupi.Kwa siku tatu nilikuwa na shughuli
nyingi na sikupata hata muda wa kuonana
naye.Kwa sasa emmy anasoma digrii ya
sheria katika chuo kikuu cha Tumaini
makumira.Kila jioni huwa ana desturi ya
kupita kwangu na hata kama sipo kwa kuwa
ana ufunguo wa nyumbani kwangu huwa
ananisubiri mpaka nikirudi tunakaa wote
kisha namrudisha kwake.
?Hallow sunshine,niko kwenye kikao hapa
roterdam.Baada ya kutoka hapa nitapita
kwako.Missing you soooo much.? Huu ndio
ujumbe mfupi niliomtumia Emmy kipenzi cha
moyo wangu.
Tukaendelea na kikao.Baada ya kama robo
saa hivi tangu niutume ule ujumbe mfupi wa
maandishi kwa mpenzi wangu Emmy simu
yangu inaita kuangalia zilikuwa ni namba za
emmy.Nikainuka na kwenda mbali kidogo ili
niweze kuongea naye.
?Halloo Darling ?Nikasema kimahaba.kwani
ndivyo tulivyozoea wakati tunaongea simuni.
Nusura moyo unipasuke kwa mstuko pale
nilipoisikia sauti nzito ya kiume ikijibu.
?Mwanaharamu wewe,mpenda wake za
watu.Huna haya unamwita nani Darling?
Kumbe ndio mchezo wako huo wa kudandia
wanawake wa watu.Leo nimekupata.?
Nilibaki nimeduwaa kwa sekunde kadhaa
nisijue nini cha kusema.sikuelewa yule jamaa
alikuwa akimaanisha nini.Huku nikitabasamu
nikauliza
?Mbona sikuelewi wewe.Unasemaje? samahani
kama simu zimeingiliana?
?Simu hazijaingiliana we juha.We si ndio
Wayne? Wayne mkotela?.
?yah ndio mimi? Nikajibu huku mapigo ya
moyo yakinienda kwa kasi baada ya yule
jamaa kulitamka jina langu
? Wewe si ndio umemtumia Sarafina ujumbe
wa maandishi sasa hivi ukisema unakuja
kumuona ukitoka kwenye kikao?
?Mimi nimemtumia ujumbe Emmy na sio
sarafina?
?sasa sikiliza wewe mjinga?.?Nilihamaki
baada ya kuitwa vile lakini nikavumilia
nimsikie alichotaka kusema
?Iwe ni huyo Sara au Emmy kama unavyojua
lakini nakwambia kuwa huyu ni mke wa mtu
na mimi ndio bwana wake.?..
?Unasemaje wewe??..Nikauliza kwa hamaki
?Hebu mpe Emmy simu yake haraka.Mpuuzi
wewe? Nikasema tena kwa hasira
?Mpumbavu wewe ! hivi nikwambie mara ngapi
Hakuna Emmy hapa?Huyu anaitwa
Sarafina.Kama alikwambia anaitwa Emmy
alikudanganya.Huyu ni sarafina na mimi ndio
mumewe,mimi ndio ninayemlipia hii nyumba
anayoishi na ni mimi ndio niliyemtafutia kazi
pale AICC na baadae nikamtafutia nafasi ya
masomo pale Makumira.Mimi ndiye
ninayemlipia ada na kila kitu.Mimi ndiye
ninayemuweka mjini.Nilikuwa nje ya nchi
nilikuwa napata taarifa kuwa kuna mtu
anatembea na mke wangu nikajua ni utani.Leo
ndio nimegundua kuwa ni kweli? akasema Yule
jamaa.
?Mjinga mkubwa wewe,huna haya mimi ndie
ninayemlipia Emmy ada zote za masomo na
hata nyumba anayokaa mimi ndiye
ninayelipa.Na kwa taarifa yako mpumbavu
wewe,sasa hivi tuko katika maandalizi ya
harusi yetu na kesho jumapili kanisani
wanasoma tangazo la kwanza la ndoa
yetu.Hivyo nakuomba usijaribu kwa namna
yoyote ile kuleta upumbavu wako ? Tayari
hasira ilikwisha nipanda nikatamka maneno
yale kwa hasira.
?Sikiliza we mjinga yaani pamoja na kukueleza
kote huku bado hunielewi sasa Emmy huyu
hapa hebu ongea naye?
Nikasikia akimpa mtu simu na kumlazimisha
?Hebu ongea na huyu mbwa mwenzako
mweleze ukweli mimi ni nani na mkanye
akome kuanzia leo kukufuata fuata la sivyo
nitamfanyia kitu kibaya sana ,hanijui mimi ni
nani mjinga huyu? maneno haya nikayasikia
kwa mbali.Mara nikasikia kitu ambacho
sikukitegemea kukisikia maishani
mwangu.Niliomba ardhi ipasuke niingie
ndani.Nilitamani nijimalize pale pale.sikuona
thamani tena ya kuendelea kuishi katika dunia
hii.
Niliisikia sauti ile tamu na nyororo iliyozoea
kuniburudisha kila siku na kunifanya nione
kama niko peponi,sauti ambayo niliamini ni
sauti nzuri kuliko zote duniani,sauti ya
mpenzi wangu,bibi harusi mtarajiwa
Emmy.Huku akilia kwa kwikwi akatamka
maneno ambayo yalinifanya niichukie dunia
na watu wake na hasa wanawake.
?Wayne I?m sorry mimi ni mke wa mtu,na
ninaomba usiendelee tena kumtukana mume
wangu?
Ilikuwa ni kama niko ndotoni nikazubaa kwa
sekunde kadhaa kisha nikajikaza kiume na
kuuliza tena.
?Emmy is that you????.
?Yes Wayne please leave me alone.Usinipigie
simu tena.Mimi nina bwana wangu?
Machozi yalianza kunitoka.Sikuamini kile
nilichokisikia.
?Please Emmy tell me its not true ? Nikasema
tena huku machozi yakinitoka.
?My name is not Emmy?..Akashindwa
kuendelea alikuwa akilia.Yule jamaa
akachukua tena simu
?Sasa umeamini we kijana.Tafadhali
usiendelee kumfuata fuata sarafina.Kitaka
chokupata usije kumlaumu mtu???..?Akamal
izia kwa tusi zito na kukata simu
Nikahisi miguu ikiisha nguvu nikaakaa chini.
Christopher rafiki yangu mkubwa alihisi
lazima nitakuwa na tatizo akanifuata
.Akastuka baada ya kunikuta nimekaa chini.
?Wayne.. ?Akaita nikamuangalia sikuwa na
nguvu za kujibu.
?Wayne una tatizo gani?
Akawaita wanakamati wote wakaja mbio na
kuanza kunipepea.Nikaletewa maji
nikanywa.Dakika kama tano hivi baadae
nikaweza kuongea
?Take me home? Nikamwambia Chris
?Wayne una tatizo gani.Twende hospitali?
Akasema Chris
?No ! take me home? Nikasema huku nikijaribu
kuinuka.Wakanisaidia kutembea hadi garini
kisha Chris akawasha gari na kuondoka
kunipeleka nyumbani.
Picha mbali mbali zikawa zinakuja na
kupotea.Nilihisi kama vile niko ndotoni .Chris
aliendesha kwa kasi bila kunisemesha.Tul
ipofika maeneo ya sanawari nikafungua
mdomo na kumwambia Chris.
?Nipeleke kwa Emmy? Chris alikuwa
akipafahamu anapoishi Emmy hivyo tulipofika
maeneo ya Ilboru akakata kushoto na moja
kwa moja akaelekea nyumbani kwa Emmy.
Alisimamisha gari nje ya nyumba ya
Emmy.Sikuongea kitu nikafungua mlango
nikashuka garini.Mlinzi wa kimasai wa
nyumba ya Emmy alinifahamu hivyo
aliponiona akanisalimia nikapita zangu hadi
ndani.Chris naye alikuwa akinifuata kwa
nyuma.Nilisimama mlangoni na kusikia watu
wakinong?ona kwa ndani.Nilikuwa na funguo
ya mlango nikaufungua bila kugonga na
kuingia ndani.Sebuleni nilimshuhudia Emmy
akiwa kifuani kwa baba mmoja mnene wakiwa
katika mahaba mazito.Nikaanguka na
kupoteza fahamu.
* * * *
Nilizinduka na kujikuta mahala
nisipopafahamu.Nilikuwa katika chumba
chenye harufu ya dawa.Ndani ya chumba hiki
kulikuwa na watu kadhaa.Mtu wa kwanza
kumtambua alikuwa Chris.
?Pole sana Wayne?.Akasema huku akinishika
kichwa.?Tafadhali usiinuke , endelea
kupumzika.? Muda huo huo akaja daktari
akiwa ameongozana na wauguzi
wawili,nikajua hapa nipo hospitali.daktari
akanipima kisha akasema
?Kwa sasa unaendelea vizuri.Itabidi ulale
hapa leo ili tuendelee kukuangalia zaidi?
Sikuwa na ubishi ingawa sikuhisi kuumwa
sehemu yoyote ile zaidi ya kichwa kuwa kizito
mno.Daktari akatoa maelekezo kadhaa kwa
wale wauguzi akaandika pia katika kijikadi
kisha akatoka.Pale mlangoni nilisikia
akiongea kama na kundi la watu.na dakika
hiyo hiyo watu zaidi ya ishirini wakaingia mle
chumbani.Walikuwa ni wanakamati ya
maandalizi ya harusi yangu pamoja na baadhi
ya rafiki zangu.Walinipa pole nami
nikawahakikishia kuwa niko salama
wakanitakia usiku mwema wakaondoka.pale
hospitali nikabaki na Chris
?Chris nini kilitokea mpaka nikaletwa hapa?
Chris akanitazama kisha akajibu
?Wayne ulianguka ukapoteza fahamu ,ikanibidi
nikulete hapa katika hospitali hii .Usijali kila
kitu kinakwenda vizuri.Daktari anasema kesho
asubuhi atakuruhusu?
Niliposikia kuanguka na kupoteza fahamu
,ndipo nikalikumbuka tukio zima
lililotokea.Ghafla fahamu zikanipotea tena.
Nilirejewa na fahamu baadae sikujua ni saa
ngapi.Ukiacha yule daktari mmoja
aliyekuwapo mida ile sasa walikuwapo
watatu.hali hii iliniogopesha sana.Nikaogopa
pengine hali yangu si nzuri.Daktari mmoja
mzee mwenye miwani akanisogelea na
kuniuliza
?Wayne unajisikiaje sasa hivi??
?Najisikia safi ila kichwa ni kizito sana.Nahisi
kama kizungu zungu kwa mbali?
?Ok sawa.Hali yako inaendelea vizuri,vipimo
vyote vinaonyesha uko sawa ila unachotakiwa
kwa sasa ni kujaribu kutokuwaza kitu
chochote kinachoweza kukusababishia
ukapoteza fahamu kwa mara nyingine.Jaribu
kupata mapumziko ya kutosha na jitahidi
sana kutokuwaza?..?
Nilimtazama yule daktari sikuwa na jibu la
kumpa.Nafikiri hakujua kitu gani
kilichonipata.Hakuyaelewa maumivu
yaliyokuwa moyoni mwangu.
?Ok dokta nitajitahidi?.Nilisema huku machozi
yakinilenga.
Madaktari na wauguzi wakatoka na kuniacha
chumbani mimi na Chris.hawakutaka Chris
aniache peke yangu kwa kuwa waliogopa
pengine ningeweza kujidhuru.
Niliinuka na kukaa kitandani.Chris akanisaidia
nikakaa sawa.
?Chris I hate the world?Nikasema kwa sauti
ndogo
Chris akanitazama akasema.
?Wayne jitahidi upumzike.Usiwaze lolote kwa
sasa.Everything will be ok?
?No Chris.Nothing is ok.Emmy lied to
me????????Nikasema huku machozi
yakinitoka.
?Don?t cry buddy,be strong? akasema chris
huku akinipiga piga mgongoni
? I loved her .I loved her Chris more than I love
myself.Lakini ona kitu alichonifanyia?
..Nitauweka wapi uso wangu mimi?.?.Uso
wote ulijaa machozi.Iliniuma kupita kiasi.
?Wayne lala kwanza.Tutaongea asubuhi?
Akasisitiza Chris.
?No Chris siwezi lala wakati mwanamke
niliyempenda amenisaliti?.why me????? Why
this pain????
?Ok brother let it out??let it out?.?Akasema
Chris.
?Emmy amenidanganya muda wote huu kumbe
ni mke wa mtu?.?
?what!!!!!!!!? Akahamaki Chris
?Yah! ana bwana wake.Ndiye yule tuliyemkuta
amelala naye kwenye sofa pale sebuleni
kwake.Kwa mdomo wake mwenyewe
ameniambia nisimsumbue yeye ana mume
wake ?
Chris akainuka na kuanza kuzunguka mle
chumbani huku ameshika kichwa.
?Is this true brother?Akauliza
?Yah..kwa mdomo wake amenitamkia maneno
haya?.It hurt Chris it hurt so much.?
?Mwanaharamu huyu??.?Akasema Chris kwa
hasira
?Kesho ndoa yetu inatangazwa kanisani kwa
mara ya kwanza??.nikashindwa
kuendelea.Nilishindwa kujizuia kuangusha
machozi.
?Wayne its gonna be ok.Jitahidi ulale kesho
tutayaongea mambo haya.Usiwaze sana
kilichotokea.Hii ni mitihani tu ya maisha?
Chris alijaribu kwa kila njia kunibembeleza ili
niweze kuwa katika hali yangu ya kawaida
lakini kwa hali halisi jinsi ilivyo ni ngumu
sana.
Ni Jumatano ya wiki hii tumetoka kuandikisha
ndoa kanisani na kesho tangazo la kwanza
linaanza kusomwa.tayari maandalizi yote ya
harusi yamekamilika .Nitauweka wapi uso
wangu mimi.Nitawaeleza nini watu
wanaoisubiri harusi yangu??Nitawaleleza nini
wazazi na ndugu zangu? Simlaumu
mtu.Emmy nilimchagua mwenyewe.Hakuni
chagulia mtu yeyote.Iwapo ningechaguliwa na
wazazi au mtu mwingine , ningekuwa na kila
sababu ya kuwatupia mzigo wa lawama wao
kwa uchaguzi wao usiofaa.Lakini hili lilikuwa
ni chaguo langu mwenyewe..Huu ni mzigo
wangu na inanibidi nisimame kidete
niukabili.Nilijilaza kitandani na sijui hata saa
ngapi nilipata usingizi.
Saa tano asubuhi tayari nilikuwa nyumbani
kwangu maeneo ya majengo.Nilikuwa najisikia
mzima wa afya isipokuwa kichwa kilikuwa
kikiniuma kwa mbali.Chris ndiye aliyenichukua
hospitali na kunirudisha nyumbani.
Mpaka sasa hivi hakuna mtu mwingine
aliyekuwa akijua nini kilichotokea na
kupelekea kupoteza fahamu na kulazwa
hospitali zaidi yangu na Chris.Sikutaka
kuharakisha kuliweka wazi jambo hili
gumu.Nilitaka kuacha kwanza akili yangu
itulie.Nilikaa kidogo sebuleni ,halafu
nikamwambia Chris aniache nikapumzike.
?Brother naomba nikapumzike,halafu
tutaongea jioni.Ila tafadhali naomba
usimwambie mtu yeyote nini kilichotokea..?
?Ok wayne nenda kampumzike ila tafadhali
don?t do anything stupid?Akasema Chris huku
akitoa tahadhari kwani madaktari walimuonya
asikubali kuniacha peke yangu kwa kuhofia
pengine ninaweza kujidhuru.
?C?mon Chris,I?m not a kid.Haya ni mambo ya
kawaida katika maisha.Let me have a rest
then I?ll know what to do next.?
?Ok wayne..nitapita mchana kukuangalia.Nik
uletee chakula gani mchana?
?Nothing Chris.Usiniletee chochote.I don?t feel
like eating anything.?
?Unatakiwa ule Wayne.unatakiwa uwe na
nguvu.?
Sikumjibu kitu nikamtazama na kuondoka
kuelekea chumbani kwangu.
Nilikaa kitandani,nikalifungua kabati langu na
kutoa albamu kubwa la picha.Humu kuna
picha nyingi ambazo nimepiga na emmy
tangu tulipoanza mapenzi yetu .Picha yetu ya
kwanza mimi na yeye ikanikumbusha
tulikwenda picnic Ziwa Duluti.Ni siku
tuliyofurahi sana.Siwezi kuisahau siku
hii.Nikaendelea na kuzifunua picha
nyingine.Wakati nikiendelea na kuzitazama
picha simu yangu inalia.Alikuwa ni mama
yangu.
?mama shikamoo? nikamsalimu
?Marahaba baba ,hamjambo?
?hatujambo mama,vipi mnaendeleaje?
?Huku wote wazima.Ni baba yako tu kichwa
chake kile kinamsumbua sana lakini
anaendelea vizuri?
?Mpe pole sana ?Nikajibu kwa ufupi.
?Vipi mkwe wangu hajambo?
Nikasita kujibu.
?eenh jamani hajambo mama mkwe? Mama
akauliza tena baada ya kuona sijamjibu
?Hajambo mama?Nikajibu huku nikiuma meno
kwa hasira.Mwanamke huyu amewadanganya
hadi wazazi wangu.Iliniuma sana.
?nashukuru kama ni mzima.Vipi mnaendeleaje
na maandalizi ya harusi?
?mama maandalizi ni mazuri.Tunaendelea
vizuri?
?sawa baba.Leo huku wamesoma Tangazo la
kwanza..Hivi ninavyokwambia watu
wanajiandaa isivyo kawaida,kila ndugu
anataka aje kwenye harusi yako.?
Sikuwa na cha kusema.Machozi yalikuwa
yananitoka.
?Mama nashukuru.Nitakupigia baadae
tutaongea vizuri zaidi?
?Sawa baba?
Nilikata simu na kuitupia kitandani.hasira
zikanipanda.
?Damn you Emmy?..?
Nilizungunguka zunguka mle chumbani
nikijaribu kuwaza na kuwazua bila kupata
jibu.Nikatoka na kurudi sebuleni.Nikafungua
kabati ninamoweka cd na kuchukua moja ya
cd niipendayo sana ya mmoja kati ya
wanamuziki mahiri kwenye mziki wa bongo
fleva,Hamis mwinjuma au Mwana F.A .Huu
wimbo wake niliona ni kama vile alinitungia
mimi kwa sababu ulinihusu mimi.Ubeti wa pili
ndio uliniumiza zaidi ukanifanya niurudie tena
na tena
?hata nikitaka kuoa niambie ntamuoa nani?/
watu wana watu wao wengine toka zamani/
ukiambiwa we ni boyfriend haimaanishi uko
peke yako/
wadogo usoni wanahifadhi wazee wako/
sijui ni dhiki au tamaa tu??/
watoto wanaanika njaa tu/
hawafikirii mapenzi wanachoona wao ni
mkwanja tu/?
Maneno haya yalinichoma moyo.Kijana huyu
aliimba vitu vya kweli kabisa na yote
aliyoyaimba yamenikuta mimi.
Nikarudi tena chumbani sikujua nini cha
kufanya.Nilikuwa kama nimechanganyikiwa
vile.Nikaona ni bora nijilaze kitandani na
kijiusingizi kikanipitia.
Nilistuka na mlio wa simu iliyokuwa kichwani
kwangu,alikuwa ni Chris.
? Haloo? Nikasema
?Wayne umelala??
?Ndiyo nilikuwa nimelala?
?Ok .Sasa wayne naomba uwe na moyo
mgumu na usihamaki tafadhali.Ni kwamba
Emmy amenifuata na hapa nilipo niko naye
na ni yeye ndiye alinisisitiza nikupigie simu
hii.?
?Unasemaje Chris????? ?Nikasema kwa
ukali.Sikutegemea kusikia kitu kama kile.
?Wayne niko na Emmy hapa.amenitafuta na
kuomba nafasi ya kuongea na wewe?
?Chris????..?Nilidakia,sikutaka aendelee tana
kunipa habari za yule baradhuli
?Chris tafadhali.Kama na wewe unataka
tukosane hamna shida ila tafadhali naomba
usinipe habari zozote kuhusu huyu
mwanamke.?
Nikakata simu.Mwili wote ulikuwa
unanichemka kwa hasira.Sikutaka kumsikia
tena emmy katika maisha yangu.Nilikuwa na
hasira mbaya mno kwa kitendo alichonifanyia
na kama angekuwa karibu yangu sijui hata
ningemfanya kitu gani.
TUKUTANE SEHEMU IJAYO?????????..