Masikini kaka huyu

Masikini kaka huyu

namna ya kulishinda ndiyo tunaomba msaada rafiki yangu kawa kama chizi ni analalamika maisha yake kaharibu

Cha kumsaidia ni kuwa amrudishe kwa wazazi wake..yaani kwa wakwe zake kama wapo then... atulie peke yake mpk hapo mtt atakapozaliwa ili ajue mstakabali wake utakuwaje!
 
Cha kumsaidia ni kuwa amrudishe kwa wazazi wake..yaani kwa wakwe zake kama wapo then... atulie peke yake mpk hapo mtt atakapozaliwa ili ajue mstakabali wake utakuwaje!
asante mkuu kwa ushauri
 
hapo wote wameshakosea kuamua kufunga ndoa bila kujua afya. sio kwamba huyo kaka hakuwahi kuwa na mwanamke kabla ya huyo, pengine hata yeye angeweza kuambukizwa. alimpenda huyo dada, akamuamini kwa tabia zake ndio maana akaamua kumuoa. kuathirika kwa huyo dada haimaanishi kua alikua na tabia mbaya ni bahati mbaya ktk mahusiano yake ya awali akaambukizwa, akaendelea na tabia yake nzuri akapata mchumba akaolewa.

kiubinadamu tu huyo kaka angekua yeye angependa ahurumiwe, asikimbiwe, atunzwe, apewe huduma zote. kwa vile imetokea kwa mwenzake basi amfanyie yaliyo mema, amtunze, bahati nzuri wamepata ujauzito wautunze vizuri wampate mtoto wao, mamlee kwa pamoja.

jitahidini kuongea na huyo wifi yenu akubali kutumia kondom maana hata yeye asingekubali pekupeku kama mumewe angekua mgonjwa. atumie dawa zake vizuri awe na afya nzuri aendelee kupendeza mpaka mungu atakapomchukua maana ukimwi sio kifo, anaweza kufa hata kwa kifo kingine na sio huo ugonjwa, wazima wanaweza kumtangulia yy akaishi miaka mingi zaidi.

yeye sio wa kwanza kuambukizwa. kaka akimuacha ni mbaya zaidi, atakua na stress, mawazo mengi atatutoka mapema. wasivunje ndoa please hilo ni jaribu lao.
 
Jaman apo amwachie nyumba tu akajipange ila amsaidie kama mkewe
 
amefanikiwa kwepa mda wote uo,sasa iv akigusa tu amenasa.maana inaonesha mwanamke anataka wapate wote.as ad apo swali n mwanamke aliupata wapi?nje ya ndoa?.jibu n ndio.so anataka washee io.akimbie haraka sana
 
Sasa hii ndo vitu huwa tunaita majaribu..jama ni dini gani kama ni muslim aaaah hiyo ndoa inavunjwa dakika sifuri tu...kama ni mkristo hapo kuna kasheshe ila naona jambo rahisi jamaa akajitafutie zake maisha mbele mana huyu bint naona kama analengo la kumuua mwenzake kwa makusudi ambapo ikifika mahakamani lazm demu afungwe...Al in All jamaa asepe tu hakuna jipya kama watoto wa kike wapo wengi hajachelewa maisha ila kama mtoto atazaliwa jamaa amkumbuke mama kwa VIJESENTE mana ni damu yake hakuna jinsi
 
ndoa za kikristo.......nashindwa hata kusema neno. Roman catholic hawakubaliani na matumizi ya condom kwa waumini wake. hata kama situation kama hii imetokea bado condom haitumiki..Ni msimamo wa kiimani zaidi...sote tutakufa na njia ya kwenda kwa baba ni kifo tu... palipo na upendo wa kweli yote yawezekana. kuna watu wanaishi na kushiriki tendo bila hata kinga ktk situation kama hii, ni wachache na ni upendo wa aina yake ,ambao kwa kizazi chetu nina mashaka nao kabisa.... Mungu atusaidie kwa kweli.
 
Ndotatizo la kuoa kwa msukumo wa nyege inaonekana wame oana kwa mihemuko ya miiri yao, lakini mwanaume nae ni ----- sababu huwezi fakamia dude kisa limeonyesha lipole kumbe limevaa ngozi ya kondoo sasa kinacho tokea kwake anavuna aricho panda ,mwambie aache usenge kumamake
 
akubali matokeo na ajitahidi kutafuta mtu rafiki wa karibu wawe wanatembelea maeneo ya kujiliwaza na kama anakunywa awe anapigapiga
 
Kijana akumbuke kiapo alichofanya kanisan kuwa atampenda ktk shida na raha,ktk shida na maradhi,

ila kama uvumilivu anaweza rudi kanisani aliyewafungusha yaweza tenguliwa ila atambue ni kwa ajili ya ugumu wa moyo wake na kutotambua maana ya agano alilo fanya
 
Ndoa za kikristo unajua tena wif hataki kusikia wala kuelewa

hapo ndo nnaposhangaa, eti ndoa za KIKRISTO....... ndoa ni watu wawili tu.....inapotokea na kudhibitika ni hatari kwa usalama wa mmojawapo.....dhahiri shahiri lazima ndoa ife.....sheria ziko wazi kabisaaa mpendwa.......na mahakamani ndo pake.......afanye maamuzi sahihi,,, kama aliweza kujitunza ajue Mungu ndie anaemlinda mpaka sasa....maamuzi magumu tu...
 
hapo ndo nnaposhangaa, eti ndoa za KIKRISTO....... ndoa ni watu wawili tu.....inapotokea na kudhibitika ni hatari kwa usalama wa mmojawapo.....dhahiri shahiri lazima ndoa ife.....sheria ziko wazi kabisaaa mpendwa.......na mahakamani ndo pake.......afanye maamuzi sahihi,,, kama aliweza kujitunza ajue Mungu ndie anaemlinda mpaka sasa....maamuzi magumu tu...

Sawa mkuu asante kwa ushaur
 
Naona kama vile hawaja yazungumza yalio mkuta kama vile mwana mke ana ona mume hajui

Nimbaya sana huyo mwanamke anaonekana kutaka kumwambukiza makusidi hata usiku inawezekana aka mchoma na kitu alichojichoma nacho

ampeleke mkewe kwa washauri nasaha apate ushauri labda anaweza badilika
 
We misschagga ni muuaji mkubwa kabisa,wewe ndo uliyemtafutia huyo kijana huyo mwanamke halafu unakuja hapa kutaka ushauri,mungu keshamnusuru hapa hakuna cha ushauri wapigane chini tu.
 
namna ya kulishinda
ndiyo tunaomba msaada rafiki yangu kawa kama chizi ni analalamika maisha
yake kaharibu

kwa afya ya kijana lazima achukuwe maamuzi sahihi atowe matumizi ns kila kitu wawajulishe wazee wa kanisa na wazazi then watengane la sivo ataambukizwa tu.
 
mbaya zaidi kuna wakati hata kumeza dawa hataki anaamini mungu atamponya .. Ushauri please
kama huyo mwanamke yupo hivyo,mwambie rafiki yako akimbie tu kuokoa maisha.ipo siku atategea kalala atajichana na wembe kisha atamchana na yeye atagusisha halafu atamwambia nipe tu na wewe unao!
 
ndoa za kikristo.......nashindwa hata kusema neno. Roman catholic hawakubaliani na matumizi ya condom kwa waumini wake. hata kama situation kama hii imetokea bado condom haitumiki..Ni msimamo wa kiimani zaidi...sote tutakufa na njia ya kwenda kwa baba ni kifo tu... palipo na upendo wa kweli yote yawezekana. kuna watu wanaishi na kushiriki tendo bila hata kinga ktk situation kama hii, ni wachache na ni upendo wa aina yake ,ambao kwa kizazi chetu nina mashaka nao kabisa.... Mungu atusaidie kwa kweli.

tendo la ndoa ni watu wawili tuu....na hufanyika sirini..... jamii imeelimika kuhusu athari za HVI... ni jukumu lako kujilinda na sio roman katoliki au dhehebu lingine lolote.
 
Back
Top Bottom