Nilijua tu lazima Sykes atajwe
Voice of Mtwara,
Abdul Sykes alipata mkosi mkubwa wa hasad katika maisha yake.
Allah alimjaalia nema kubwa nyingi katika umri mdogo sana.
Akiwa katika King's African Rifles (KAR) Burma Infantry 6th Battalion alikuwa na cheo kikubwa kupita Waafrika wenzake, " Quarter Master Sergeant."
Abdul Sykes alikuwa na miaka 20.
Mwaka wa 1947 akiwa na miaka 24 Waingereza walimteua kuwa Secretary wa Dar es Salaam Dockworkers Union.
1950 akachaguliwa kuwa Secretary wa TAA na mwaka huu huu akafanya mkutano wa siri na President wa KAU, Jomo Kenyatta na wazalendo wengine wa Kenya: Peter Mbiu Koinange, Kungu Karumba, Bildad Kaggia, Paul Ngei na Karume Njega.
1952 Abdul Sykes akampoke Nyerere Dar es Salaam wakati huo akiwa Act. President wa TAA na Secretary.
Wakati huo ni Market Master Soko la Kariakoo.
1953 Abdul Sykes na Julius Nyerere waligombea nafasi ya Rais wa TAA Ukumbi wa Arnautoglo.
Ilikuwa tarehe 17 April 1953.
Sina haja ya kueleza zaidi ila moja.
Abdul Sykes hayupo katika historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika si kwa lolote ila hasad.
Wewe unaghadhibika jina la Abdul Sykes kutajwa kwa sifa ambayo ni haki yake.
Jiulize kwa nini Nyerere alikwenda kumzika Abdul Sykes Makaburi ya Kisutu?
Abdul Sykes sijaishia kumtaja.
Nimeandika kitabu cha maisha yake.
Kitabu hiki kimependwa sana na kimebadili si historia ya Nyerere bali hata historia ya uhuru wa Tanganyika.
Elewa kuwa kadi ya TANU ya Abdul Sykes ni kadi no. 3.
Nisimtaje Abdul Sykes nieleze nimtaje nani roho yako iridhike?
Mwalimu Nyerere alipoacha kazi ya ualimu alikwenda kuishi nyumbani kwa Abdul Sykes.
Hudhani kuwa historia hii ni ya kutukuka?
Dar es Salaam ile kulikuwa na vijana wawili tu waliokuwa wakiendesha Mercedes Benz - Abdulwahab Abbas na Abdulwahid Sykes.