Kwa anaefanya biashara zake kiuhalali Mashine za-EFD sio tatizo..
Na anaesema mfumo wa ukataji kodi wa EFD ni tatizo nadhani hajaelewa kuhusu hizo mashine, binafsi tatizo nililo liona ilikua ni mfanya biashara kuikopesha serikali pesa ya kununulia EFD machine.
Kwa sababu kiuhalisia ile gharama uliyoitumia kununua mashine unatakiwa uikate katika kodi unayotakiwa kuipeleka serikalini-TRA, kwa mfano kama umekusanya kodi(VAT) ya Million 2 kwa December 2015 katika mauzo yako na ulilipa kodi (VAT) ya laki7 katika mahitaji yako ya kibiashara, na ulinunua mashine ya EFD kwa shilingi laki5, itakapofika January 2016 badala ya kupeleka TRA-Serikalini shilingi million2 utatakiwa upeleke laki 8 (yaani kodi(VAT) uliyokusanya 2,000,000-700,000-500,000).
Pili sio kila mwenye mashine ya EFD anaweza akatoza kodi ya VAT (ni mpaka usajiliwe), kwahiyo kama hujasajiliwa utatumia mashine ya EFD kwa ajili ya kumbukumbu zako za kibiashara na pia itakusaidia usitozwe kodi zaidi ya mauzo yako...kwahiyo inampunguzia uonevu kwa sababu mauzo yako ya mwaka mzima yataonekana na sio kukadiriwa (KAMA UTATII SHERIA YA UKIUZA TOA RISITI NA UKINUNUA DAI RISITI).
:angry::angry:Tatizo tulizoea kununua vitu vya jumla toka kwa wafanyabiashara WALIOKUA WANATOA MAKONTENA BILA KULIPA KODI:angry::angry:
Ili tufike katika huo uchumi wa kati EFD-NI LAZIMA.
Tutakua ni wazalendo na wapenda mabadiliko ya kweli..kama tutaiomba serikali itupunguzie viwango vya kodi zote kama VAT, PAYE, na WHT...lakini sio kuzipinga mashine za EFD
Ushauri kwa TRA- itoe elimu zaidi juu ya hizi mashine, na usimamizi wa matumizi yake uongezwe ikiwezekana uanzie serikali za mitaa..na pia ikusanye kodi kwetu sisi tunaopangisha nyumba zetu huku sinza badala ya kuendelea kuwabana maaskari magereza, walimu n.k katika mishahara yao.