Mashine za EFD sasa kutolewa bure na Serikali!

Mashine za EFD sasa kutolewa bure na Serikali!

Sisi wajasiliali si ugomvi wetu ni mfumo uliomo ktk mashine hizo...KWAMBA HATUUTAKI MFUMO....SIO MASHINE...narudia tena ..HATUUTAKI MFUMO WA MSHINE HII KUKATA KODI KWENYE MAUZO..TUNAOMBA MASHINE IKATE KODI KWENYE FAIDA
 
Hali ilivyo sasa mashine hii ni kidudu mtu kinanyoa kodi kwenye mauzo hatutaki....mashine hii haijui mtaji.gharama za uendeshaji.nk.yenyewe inaingia kwenye mauzo moja kwa moja ...
 
Tatizo sio mashine,, tatizo ni kodi inakatwa mpaka kwenye mtaji badala ya faida,,,magufuli badala ya kudeal na tatizo kubwa kama hili,,,anahangaika na vi small issues visivyokuwa na tija kwa taifa
VAT inakatwajwe kwenye mtaji?
 
Tatizo sio mashine,, tatizo ni kodi inakatwa mpaka kwenye mtaji badala ya faida,,,magufuli badala ya kudeal na tatizo kubwa kama hili,,,anahangaika na vi small issues visivyokuwa na tija kwa taifa
Wee fisadi, kwa nini usifunge tu na kuziba matundu ya mwili wako yote?? Maana naona kila ukiandikaga ni uharo tu!
Kodo lazima ilipwe hata kwa risasi, watalipa tu, hii haikwepeki! Hata wewe kama risasi ya kichwa utakula tu, kodi haukwepi!
 
Hiyo ni hatua kubwa saaaana katika kukusanya kodi ya kutosha. Nashauri John Pombe Magufuli a.k.a Tingatinga aendelee kushikilia wizara ya fedha na mipango maana mambo yake yanaenda kasi yaani HAPA KAZI TU!

Hatua ya pili ni kupunguza VAT hadi 15%

Hatua ya tatu ni kupunguza corporate tax hadi 25%

Hatua ya nne, kili kisheria cha kudeposit 30% ya kodi unayolalamikia eti ndipo rufaa yako isikilizwe, wakati umebamkiwa kodi feki nayo itoke.

Ya tano, kupunguza PAYE hadi 9%

Akifanya hayo, walipa kodi tutakuwa wengi saaaaaana. ukikwepa kodi itakuwa aibu yako! Naamini pato la taifa litakua saana. Watanzania tujivunie kulipa kodi kwa maendeleo yetu.
 
Hamtaelewa Wewe na nani mkuu?
Hili tamko angetoa Minja angalau!!
sikiliza wewe masikini , mimi ni mfanyabiashara na mwekezaji mkubwa nina kiwanda , natengeneza na ku import , nina zaidi ya wafanyakazi 300 , sasa nafahamu namna hizi mashine zilivyoniletea shida , na ndio maana nataka tutajiwe ni nani alikuwa nyuma ya hii kitu , sasa si lazima upinge kila hoja yangu humu , utaadhirika vibaya sana !
 
Hiyo ni hatua kubwa saaaana katika kukusanya kodi ya kutosha. Nashauri John Pombe Magufuli a.k.a Tingatinga aendelee kushikilia wizara ya fedha na mipango maana mambo yake yanaenda kasi yaani HAPA KAZI TU!

Hatua ya pili ni kupunguza VAT hadi 15%

Hatua ya tatu ni kupunguza corporate tax hadi 25%

Hatua ya nne, kili kisheria cha kudeposit 30% ya kodi unayolalamikia eti ndipo rufaa yako isikilizwe, wakati umebamkiwa kodi feki nayo itoke.

Ya tano, kupunguza PAYE hadi 9%

Akifanya hayo, walipa kodi tutakuwa wengi saaaaaana. ukikwepa kodi itakuwa aibu yako! Naamini pato la taifa litakua saana. Watanzania tujivunie kulipa kodi kwa maendeleo yetu.

SIWANASEMA NI RZ1 KIJana wa madili.siunaona sasahivi tweet zake hakuna
 
Tatizo sio mashine,, tatizo ni kodi inakatwa mpaka kwenye mtaji badala ya faida,,,magufuli badala ya kudeal na tatizo kubwa kama hili,,,anahangaika na vi small issues visivyokuwa na tija kwa taifa

Laki si tangu umeigia UKAWA umekuwa akili mingi mingi..

Tatizo si ughali wa mashine, hapana. Tatizo ni ukokotoaji wa kodi ktk mashine hizo. Kusema kila mfanyabiashara anayefikisha mauzo ya milioni kumi na nne kwa mwaka anatakiwa kulipa kodi asilimia 18, ni unyonyaji mkubwav kwa wafanyabishara.

Magufuli anatakiwa kupata maelezo sahihi kwa naibu Waziri Viwanda na biashara wa awamu iliyopita maana maelezo yote ya wadanyabiasha Wakziri huyo anayo

BACK TANGANYIKA
 
Tatizo sio mashine,, tatizo ni kodi inakatwa mpaka kwenye mtaji badala ya faida,,,magufuli badala ya kudeal na tatizo kubwa kama hili,,,anahangaika na vi small issues visivyokuwa na tija kwa taifa

Mtaji unakatwa vipi wakati mwisho wa siku kodi yenyewe analipa mlaji. Mfanyabiashara ananunua bidhaa, anaweka gharama za kusafirisha, anaweka gharama za ushuru na kodi anaweka faida yake halafu ndio anamuuzia mlaji.
 
sikiliza wewe masikini , mimi ni mfanyabiashara na mwekezaji mkubwa nina kiwanda , natengeneza na ku import , nina zaidi ya wafanyakazi 300 , sasa nafahamu namna hizi mashine zilivyoniletea shida , na ndio maana nataka tutajiwe ni nani alikuwa nyuma ya hii kitu , sasa si lazima upinge kila hoja yangu humu , utaadhirika vibaya sana !
Ndio maana ulikuwa unampigia upatu yule jamaa, #HapaHakunaKukwepaKodi tu!
 
Sisi wajasiliali si ugomvi wetu ni mfumo uliomo ktk mashine hizo...KWAMBA HATUUTAKI MFUMO....SIO MASHINE...narudia tena ..HATUUTAKI MFUMO WA MSHINE HII KUKATA KODI KWENYE MAUZO..TUNAOMBA MASHINE IKATE KODI KWENYE FAIDA

Mkuu hizo ni kodi mbili tofauti, na kwa kisheria ya sasa, lazima zilipwe. Ninacho kubaliana na wadau ni kwamba hizi sheria zinataka marekebisho makubwa tu kwa faida ya pande zote mbili kwa kutizama hali ya uchumi ya sasa kwa nchi yetu.

1. Kodi ya mtumiaji (VAT). Mutaniwia radhi kwa vile sina uhakika ni kiasi gani ya mauzo kwa mwaka ukifikisha unatakiwa ukusanye kodi hii katika mauzo. Lakini, lets say, ni 50,000,000 approx US$23,000 kwa mwaka ni sawa na 4,166,000 (US$1920) kwa mwezi ikiwa ni sawa na 140,000 (US$64) kwa siku. Ukiitizama hii hesabu ni masihara kwa serikali yetu kuweka sheria kama hii. Hata muuza machungwa na madafu na wanaotembeza soda na chinga wote wanafikisha mauzo haya kwa siku. Jee na wao wapewe mashine za EFD? Kwa hali ya sasa ingetakiwa angalau mauzo ya mwaka 360,000,000 yaani ikiwa sawa na 1,000,000 kwa siku ndio ulazimishwe kukusanya VAT.

2. Jee wateja wa nje ya nchi, Rwanda, Zambia, Msumbiji nk wataipataje VAT yao kwa vile hawatakiwi walipie? TRA watakaa na marundo ya hela mipakani kuwalipa marehesho yao au wafanyabiashara watatakiwa wasiwatoze VAT hawa. Sifikirii kama TRA wako tayari kuwalipa hawa mipakani na sifikirii kama wafanya biashara watakuwa waaminifu katika mauzo yao kwa kutumia mwanya huu kutowatoza kodi watumizi wa ndani kwa kutumia details za foreigners katika risiti. Hapo ndio mwanzo wa kuibiana.

3. Jee faida ya mfanya biashara itachukuwa vigezo gani kwa vile huduma nyingi tu nchi hii hazitolewi risiti kama vile uchukuzi wa local, kwenye vi carry na mgongoni pamoja na trolleys. Hizi zote ni gharama ambazo mashine haziwezi kuzitambua.

4. Msongamano wa mfumo katika kutoa ripoti ya marejesho. Kwa sasa tunaona namna gani mitandao inavyosumbua ofisini kwa TRA. Inaweza kusumbua kwa siku mbili nzima. Na hizi mashine haziwezi kukuruhusu kuitumia kufanya mauzo siku ya pili mpaka utume ripoti ya mauzo ya siku ya nyuma. Jaalia unatuma hongera za mwaka mpya saa sita usiku on New year eve. Nini kinatokezea? Sms haiendi kwa msingamano. Jaalia machine 1,000,000 moja zinatumika ndani ya mkoa wa Dar maduka yanapifungwa (saa 11 -12) kila siku. Nafikiria hiyo server ya TRA itaungua.

5. Kufanya marudisho mwisho wa mwaka itakuwa msongamano mkubwa ofisi za TRA. Kwa vile mfumo mzima ni automated, itachukuwa muda mrefu kwa kila mteja kumaliza huduma ya marejesho kutokana na miundo mbinu isyoaminika. Na sababu nyengine nyingi tu itakuwa usumbufu kuzitaja zote hapa.

Kwa sasa rates zetu za kodi ni kubwa mno, in theory atleast, na tunashindwa kukusanya hata 25% ya kodi. Tungezipunguza nusu yake tujakusanya 75% tu ya kodi basi tungekusanya kodi nyingi kuliko tunavyokusanya sasa.

Kwa muono wangu, kwa nini tutumie mifumo iliyokuwa hatujaibuni sisi wenyewe na kuwapa faida Wachina na Wazungu kwa kununua vifaa vyao na kulipia huduma za matengenezo kwao. Tutumie mfumo wetu wenyewe, na kwa sasa ni makadirio, manually, tuajiri vijana wengi tu wawe wanapita kuhakikisha kila mfanya biashara analipa kodi aliyokadiriwa kila mwezi. Ukimpa kijana mmoja maduka 200 ahakikishe mfanya biashara amelipa bank lets say 200,000 kila mwezi. Atakuwa kakusanya 40,000,000 na yeye mshahara wake ni 1,500,000. Itakuwa TRA imekosa nini? Vijana wanamaliza masomo hawana kazi, tunawatajirisha Wachina kwa kununua mashine zao mbovu kutiana hasara tu, kwa nini? Halafu eti Wachina wameendelea! Wasiendelee na sisi tunajizarau wenyewe. Kwetu tuseme hatuna mafundi wanaoweza kushona sare za jeshi, polisi etc?. Kama rates kubwa za kodi ndio maendeleo, basi Dubai ingekuwa mkiani kimaendeleo. Kama EFD machines ndio maendeleo, basi India na China wangekuwa tiro kimaendeleo. Tubadilike.
 
Ila elimu itolewa kwa wanunuzi maana wao ndio walipa hiyo Vat, yaani mnunuzi aambiwe kabisa kuwa ukinunua kitu laki moja basi ongezea vat asilimia kumi na nane alipe kama laki na ishirini elfu hivi.
 
Tatizo sio mashine,, tatizo ni kodi inakatwa mpaka kwenye mtaji badala ya faida,,,magufuli badala ya kudeal na tatizo kubwa kama hili,,,anahangaika na vi small issues visivyokuwa na tija kwa taifa
Real great thinker, very true wanakata capital (grass earnings) badala ya profit.
 
Walionunua walikuwa wanarudishiwa kwa kukatana na TRA kwenye kodi stahiki mpaka kufidia kiasi walichokitumia kununua hiyo machine!

Acha Ngonjera lini walikata. Nimenunua 1.5m na hakuna hata siku TRA wamekata
 
Mtaji unakatwa vipi wakati mwisho wa siku kodi yenyewe analipa mlaji. Mfanyabiashara ananunua bidhaa, anaweka gharama za kusafirisha, anaweka gharama za ushuru na kodi anaweka faida yake halafu ndio anamuuzia mlaji.

Sawa. Hebu tuambiane je elimu hiyo imetolewa kwa mnunuzi au muuzaji, maana bila mnunuzi kupewa hiyo elimu itaonekana muuzaji anamuibia mnunuzi. Pili je hiyo vat inakatwa mara ngapi mpaka imfikie mlaji wa mwisho. Kwa mfano kule kiwandani imelipwa vat wakati wa duka la jumla ananunua, halafu anamuuzia wa duka reja reja na vat inalipwa, nk. Mwisho wa siku unakuta bidhaa moja mpaka inamfikia mlaji wa mwisho imelipiwa vat kama mara tatu au zaidi, je hii ni sahihi!!?
 
sikiliza wewe masikini , mimi ni mfanyabiashara na mwekezaji mkubwa nina kiwanda , natengeneza na ku import , nina zaidi ya wafanyakazi 300 , sasa nafahamu namna hizi mashine zilivyoniletea shida , na ndio maana nataka tutajiwe ni nani alikuwa nyuma ya hii kitu , sasa si lazima upinge kila hoja yangu humu , utaadhirika vibaya sana !


Umeambiwa zitatolewa bure.
Unasema lazima uambiwe ni biashara ya nani ili muelewane,itasaidia nini?
Haya ukishaambiwa kuwa ni ya somebody,roho yako itaridhika?

Na usipoambiwa ,utafanya nini?

Utajiri wako na umaskini wangu sidhani kama vinahusiana hata kidogo
 
Tatizo sio mashine,, tatizo ni kodi inakatwa mpaka kwenye mtaji badala ya faida,,,magufuli badala ya kudeal na tatizo kubwa kama hili,,,anahangaika na vi small issues visivyokuwa na tija kwa taifa

Acha kulalamika inakatajwe kwenye mtaji? au huelewi maana ya vat, vat registered ni wakala wa kukukusanya kodi zile 18% zote unakusanya kwanini usiwakilishe serekalini tuache biashara za ujanja ujanja.
 
Back
Top Bottom