Mashine za EFD sasa kutolewa bure na Serikali!

Mashine za EFD sasa kutolewa bure na Serikali!

Will TRA make a refund for my old machine?
Magufuli anavamia syndicate kwa pupa. Matatizo ya uchumi wetu SI mashine hizi Ni watu kama Kinana, Ritz1, Ben etc
Ubavu Hana hata WA kuwaambia tra watumie network ya ttcl....

Ukitaka kula nyama lazima uchinje na unapochinja unasababisha maumivu ndicho ambacho rais anafanya lazima mkamuliwe maji put ata mkilia kwa uchungu
 
Tatizo sio mashine,, tatizo ni kodi inakatwa mpaka kwenye mtaji badala ya faida,,,magufuli badala ya kudeal na tatizo kubwa kama hili,,,anahangaika na vi small issues visivyokuwa na tija kwa taifa

Embu fafanua, inakataje kodi hadi mtaji?
 
Ukitaka kula nyama lazima uchinje na unapochinja unasababisha maumivu ndicho ambacho rais anafanya lazima mkamuliwe maji put ata mkilia kwa uchungu
Magufuli is a toothless dog now after his meeting with CCM's cc! He can't bite no more.
Mwache atumbue vichunusi. Shit!
 
Hali ilivyo sasa mashine hii ni kidudu mtu kinanyoa kodi kwenye mauzo hatutaki....mashine hii haijui mtaji.gharama za uendeshaji.nk.yenyewe inaingia kwenye mauzo moja kwa moja ...
Efd inakata kodi kwenye mauzo, kama umeniuzia kiatu kwa laki basi 18% ni VAT, yaani 18000 ni mali ya serikali, sasa we sijui unataka ikate kwenye faida gani, wafanyakazi wamekuwa wakikatwa kodi kwenye mishahara yao, hakuna operation costs ya usafiri au chakula wakati mfanyakazi yupo kazini, inakatwa kwenye gross income, kwa hiyo na nyie tulizeni mshono tujenge nchi pamoja.
Nadhani ni muda muafaka wafanyabiashara wa kibongo kwenye price tag waweke bei yao halisi, mtu akitaka bidhaa anaongezewa 18% ya VAT, hii itaingeza ufahamu kwa wananchi wote na kila mtu atajua anachangia kodi.
 
Magufuli namfagilia sana, kila anachosema anatekeleza, hii ishu ya kugawa bure aliisema kama swali, kumbe hatimaye kamaanisha, safi sana mhe, Rais
 
Laki si tangu umeigia UKAWA umekuwa akili mingi mingi..

Tatizo si ughali wa mashine, hapana. Tatizo ni ukokotoaji wa kodi ktk mashine hizo. Kusema kila mfanyabiashara anayefikisha mauzo ya milioni kumi na nne kwa mwaka anatakiwa kulipa kodi asilimia 18, ni unyonyaji mkubwav kwa wafanyabishara.

Magufuli anatakiwa kupata maelezo sahihi kwa naibu Waziri Viwanda na biashara wa awamu iliyopita maana maelezo yote ya wadanyabiasha Wakziri huyo anayo

BACK TANGANYIKA
VAT ni 18%, we unataka ulipe ngapi? Hii hoja ni uthibitisho dhahiri wafanyabiashara wengi walikuwa hawalipi kodi inavyostahiki, kama kweli ulikuwa unalipa inavyostahiki, tofauti ni nini na sasa? Kama mimi nimekuja kununua bidhaa yoyote yenye VAT au huduma yoyote, asilimia 18 ni malipo halali ya serikali. Sielewi mnacholia lia ni nini saivi kama kweli mlikuwa mnalipa kodi halali. Wafanyakazi wanakatwa hadi karibia ya 30% kwenye gross incomes zao, nyie hadi VAT zetu mnataka kuzipigia faida.
 
Nimesoma taarifa juu utolewaji wa mchine ya EFD kuanza kutolewa bure kwa wafanya biashara..ni wazo zuri na hatua nzuri ya kuipongeza TRA japo naona walichelewa kufanya hivyo toka siku nyingi..
Napenda kutoa ushauri wangu machine hizi zigawiwie kwa wafanyabiashara wote kwa kuzingatia nabusiness registration Tin no. na physical address bila ya kumbagua uwezo wake wa mtaji.
Katika technology ya leo au dunia ya leo haina maana kwa mteja au muuzaji kutembea na cash..machine hizi ziboreshwe kwa kuunganisha na mifumo ya kibenk hapa kwetu kwa maana kuwa mteja atapokuwa na card yake ya bank anaweza kutumia hiyo card yake kufanya manunuzi sehemu yoyote bila ya kuwa na cash,pesa itatoka kwenye account yake kwenda kwa mmujazi wakati huo huo TRA itakata kodi yake haka kama ni kiberiti TRA itachukua kodi yake ya kibiriti.

Kwa kutumia mfumo huu serikali itaongeza mapato yake..mfanyabiashara atakua salama na mnunuaji utakuwa salama..kwa maana hata kama ni uwizi hautakuwepo tena wakuibiana cash..hata ukipoteza mkoba wako bado pesa zako ziko salama maana hakuna atakayeweza kuchukua pesa zako.

Maelezo ya mfumo huu jinsi unavyofanya kazi ni marefu sitapenda kuwachosha maana wengine hawapendi kusoma maelezo marefu..nitaendelea wakati mwingine.

Angalizo kuanzisha mfumo kama huu inabidi tuwe na wataalam wa IT walioshiba kichwani TRA,BOT and other Commercial Banks maana unaweza kumka asubuhi ukakuta nchi yote imeibiwa pesa lakini physical cash unazo strongroom.
 
Huu sio mwandiko wa kawaida ni mwandiko wa ushauri mzuri.
Ila kwa maana hiyo itabidi sasa badala ya kutolewa na serikali basi zingetolewa na mabenki ili watu wafanye manunuzi na directly kodi ikatwe apo apo. Kwa kifupi utakuwa umediscourage use of cash hata kwenye shoppings. Hapa utapoteza paper and coin money kiaina ila economy inaweza kupaa balaa hadi nanga zikaelea angani!
Hii haishindikani, crdb , exim na NBC ni mifano ya tax collecting agents kwenye mahotel makubwa , kwenye immigration offices, kwenye sheli za mafuta na hata tourist centres. Mifano ni kule tarangire , Serengeti na manyara. Wageni wanaingi by card swarp na revenue imekua vibaya mno. Ngorongoro nasikia wakubwa waligoma mfumo huo usitumike coz ndio main gate ya stomach feeds.
Vinginevo ilo likiwezekana faida yake ni kubwa amazingly!
Na itakuwa ngumu kuiba mapato kwa wamiliki wa biashra by staff because revenue inatumbukia directly kwenye akaunti na apo apo tax estimation ishakuwa calculated. Nina uhakika huu utaratibu haukubaliki kwa kuwa wafanyakazi wote kutegemea mshahara itakuwa ni kuua watu "njaa". Watawala msiukubali watu watazimia kwa njaa.
 
Gsana shida yangu kubwa nikuongeza mapato hajalishi mashine zitolewe na commercial banks au Tra.muhumu nikuongeza kodi na kudhibiti mianya ya upoteaji kwa kodi hata ile ya kiberiti utachokwenda kununua..matumizi ya cash si muhimu kwa dunia ya leo na technology ya leo..dunia inakimbia watanzania bado tumelala sana tunashudwa kustress akili zetu hata kidogo sana.
Ni kweli matumizi ya card yatakata mirija ya pesa hata yule mgahawa kukuchukulia charge yako haitawezekana tena..
Kwa nini watu wanahofia mfumu huu kwa hapa kwetu?watanzania tunapenda shortcut sana mtu awezi kuamin kama anaweza kufanya kazi akaishi kwa pesa yake halali hili jambo nataka niliondoe akili mwetu.kila mtu afanye kazi na aishi jasho lake..ukifanya hivyo hata viongozi wetu hawataweza kutuibia maana ni wazi uhai wao utakuwa halili yetu..
 
Last edited by a moderator:
wanajamvi,

kilio cha muda mrefu cha wafanyabiashara nchini waliokuwa wanalalamikia serikali kwamba mashine za efd's zinauzwa ghali, kwa sasa tatizo hilo limetauliwa kwani zitatolewa bure na serikali.

Kaimu kamishna mkuu wa mamlaka ya mapato tanzania (tra), dk. Philip mpango, ametoa kauli hiyo leo jijini dar es salaam na kwamba mashine hizo za efd hazitauzwa, wafanyabiashara nchini watapewa vifaa hivyo bure.

Nadhani sasa serikali imeamua kujielekeza kuondoa vikwazo vyote vilivyokuwa vinalalamikiwa ili kufanikisha zoezi la kukusanya mapato.
nahisi huu ulikuwa pia ulikuwa mlango wa wizi. Huwezi kumuuzia mteja zana inayokusaidia kwa malengo yako. Ni kama cocacola company wauze fridges au chupa kwa agent wao hii inaingia akilini kweli? Huu nao ulikuwa wizi uliofanywa na serikali ya kikwete ikiwa ni pamoja kampuni za maxmalipo, halotel, skagit, pwani hauliers.
 
Tatizo sio mashine,, tatizo ni kodi inakatwa mpaka kwenye mtaji badala ya faida,,,magufuli badala ya kudeal na tatizo kubwa kama hili,,,anahangaika na vi small issues visivyokuwa na tija kwa taifa

So which is which.. what should be takled first?
At least kiongozi ungekua constructive kuwa hatua ipi ianze katika lipi.
 
serekali iziagize yenyewe toka china isifanye mambo ya tender Kwani mashine moja haizidi $45-60,ili kuepuka wapiga deal,lakini kwa kuwa wizara ipo chini ya rais kwa sasa mambo yatanyooka tu!
 
Hizi mashne za EFD hazina tofauti na kile kitu kilichokuwa kinachoitwa speed governors, ambazo kipindi cha utawala wa yule jamaa aliyewaita wapinzani wote kuwa ni wapumbavu na malofa, utawala wa wakati ule uliwalazimisha wamiliki wa mabasi yote nchini wazinunue speed governors hizo walizokuwa wanaziagiza wao, kwa bei waliyokuwa wameipanga wao.
Mradi huo wa speed governors ulikufa kimya kimya baada ya kuonekana haujaleta nafuu yoyote ya kupunguza ajali za barabarani.
Ilipokuja awamu ya JK nayo ikaona 'ichonge' dili hiyo ya mashine za EFD.
Tatizo kubwa lililokabili Taifa hili kwa miongo miwili sasa ni watawala wetu wa awamu za 3 na 4 kuigeuza Ikulu kuwa ni pango la kupigia dili!
 
Naiomba pia serikali iwaamuru wafanyabiashara ambao endapo mashine zao zitaharibika wazinunue wenyewe ili kuweza kukabiliana na wale watakao kuwa na nia ya kuzihujumu hizo mashine
 
Kwa hiyo aliyekuwa anapiga hilo dili kashavuna vya kutosha, duh wabongo vichwa kweli!
 
Tatizo sio mashine,, tatizo ni kodi inakatwa mpaka kwenye mtaji badala ya faida,,,magufuli badala ya kudeal na tatizo kubwa kama hili,,,anahangaika na vi small issues visivyokuwa na tija kwa taifa
Wewe ni mkwepa kodi.kila shilingi unayoingiza lazima ulipe kodi,kama hutaki katafute nchi ambayo hawalipi kodi
 
wafanyabiashara wa bongo shule ndogo.kenya iliziondoa haraka wafanyabiashaza wakenya wanashule kubwa walicheza na IT serikali ikaziondoa fasta
 
Back
Top Bottom