Mashamba ya Mkonge Katika Manispaa ya Morogoro Usalama Umezingatiwa?

Intelligence Justice

JF-Expert Member
Oct 23, 2020
3,039
3,486
Wanabodi,

Hili bandiko la ulizo kuhusu usalama wa maisha ya wakazi wa manispaa ya Morogoro kwa kuwepo mashamba makubwa ya mkonge mali ya magereza huku idadi ya wakazi wake kuzidi kuongezeka na mahitaji ya ardhi kuwa makubwa.

Eneo kuanzia Mkambarani hadi Kingolwira kuna mashamaba makubwa kando kando ya barabara ambayo yanahatarisha usalama wa watembea kwa mguu na waendesha pikipiki kati ya Mkambarani na Kingolwira baada ya saa kumi na mbili jioni. Mashamba ya mkonge yaliyoko Kihonda mali ya magereza yaliyo kando kando ya barabara ya Moro-Dom nayo hayana manufaa sana hapo yalipo kwa kuzingatia usalama wa raia lakini pia kusababisha mahitaji ya ardhi kwa ajili ya makazi kupanda na gharama kwenda juu.

1607703102363.png


USHAURI kwa Mamlaka husika:

1. Maeneo ya mashamba haya ya mkonge yapunguzwe kwa ajili ya shughuli zingine za kiuchumi, kijamii na makazi ukizingatia treni ya mwendo kasi SGR imepitia maeneo hayo

2. Mashamba ya mkonge yahamishiwe kwingine kama Kiegea ambako jeshi la magereza watamudu vyema kuyahudumia kwa uzalishaji ulio bora kwa ajili ya viwanda;

3. Bwawa jingine kubwa lijengwe (streams water catchment) lijengwe kuhifadhi baadhi ya maji yanayotiririka kutoka katika mili Uluguru na kumwaga maji hayo ndani ya mto Ruvu au mto Ngerengere kwa matumizi ya kutosha kwa viwanda ambavyo wawekezaji wanasita kuweka miradi mikubwa kwa hofu ya kuwepo mgao wa maji maana maji ya Bwawa la Mindu huduma ya kwanza ni kwa matumizi ya binadamu

4. Kando kando ya reli ya mwendo kasi SGR wapo wawekezaji ambao wangependa kuwekeza kuchakata mazao ya chakula, biashara nk lakini ardhi ni finye sana kwa kuwa eneo kubwa ni mashamba ya mkonge mali ya jeshi la magereza kama ilivyoelezwa hapo juu

5. Pawepo na barabara ya huduma za usafiri kwa daladala kati ya Mkambarani, Kiegea hadi Mkundi mwisho hivyo kuunganisha na barabara kuu ya Moro-Dom

6. Ndani ya miaka mitano ijayo wageni wengi ikiwa pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa serikali kuu waliopangiwa vituo jijini Dodoma wangependelea kujenga hapo kwa makzi kutokana na hali hewa yake ilivyo ambayo inauoto wa asili halisi kwa kuliwaza;

7. Utalii haufanyio vizuri kuanzia kwenye mji wa Morogoro ijapokuwa kuna vivutio vingi tu lakini haieleweki tatizo ni nini
 
Naunga mkono hoja. Pia kwa kuongezea hawa magereza wana kiwanda cha kuchuna katani pale maeneo ya Kihonda Magereza ukienda Veta. Hiki kiwanda yaani ni cha kizamani utadhani ni gofu, halafu wanatumia technology ya kizamani sana na wanatiririsha maji machafu mitaani. Hiki kiwanda kiondolewe pale kwani kunachafua mitaa na kuna kipindi wananchi wa mtaa wa Kihonda Magereza walimlalamikia huyo bwana jela lakini akawajibu jeuri kwamba wananchi ndiyo wamefuata maeneo ya magereza, wakaambiwa leteni hati yenu tuone mipaka yenu inaishia wapi lakini wakashindwa kutoa. Hata mashamba yao jirani na kituo cha mwendo kasi waziri mkuu amewataka watoe maelezo kwa nini wasinyanganywe? Imagine wana karibia ekari 2000 ndani ya manispaa na mikonge yenyewe kuihudumia wameshindwa, so hili eneo serikali iligawe kwa wananchi halafu magereza wapewe maeneo mengine huko nje kabisa ya manispaa.
 
Mwisho maeneo yote bora kwa kilimo mtayageuza makazi ya binadamu na kubakiza ardhi kame isiyoweza hata kuoteshwa mkonge iwe ya kilimo.

Mipango ya kulinda ardhi ya kilimo iheshimiwe. Halmashauri na vijiji wa washauri wananchi kujenga maeneo mengine ya wazi ambayo ni makame kujenga makazi yao.

Mfano jiji la New York nchini Marekani wameheshimu mipaka ya maeneo ya wazi kama maeneo ya kupumzika au kuufanya mji upumue wakati wa joto. Tukijenga kila mahali basi tutalalamika mjini joto, hakuna maeneo ya kijani, hakuna maeneo bora ya kilimo n.k kwa kuendekeza kutwaa mashamba na maeneo ya wazi mijini.

Tazama eneo la wazi la Central Park jijini New York lililozungukwa na maghorofa kwa kuwa halmashauri ya mji na wakazi wa New York kubaini umuhimu wa kijani au eneo la wazi mjini



Intelligence Justice,
Tusiogope maeneo ya wazi kwa kuwaza kutakuwepo vitu kama mizuka, mahoka, wahenga wa kolelo, vibwengo au vibaka bali tuyatazame mazingira yetu kuwa ni kitu kizuri kwa afya zetu na siyo tishio.
 
Published on 31 Oct 2017
Brisbane, Australia

The City Botanic Gardens is Brisbane city's oldest park dating back to 1825. These gardens include ancient trees, rainforest glades and exotic species. It's well worth a visit.
 
Dar es Salaam, Tanzania

Bustani ya Mnazi mmoja iliyotengwa tangu enzi za mkoloni
Mnazi Mmoja garden iliyotengwa na mkoloni kupitia mipango miji ni muhimu na inatakiwa kutunzwa pia bustani hizi hutakiwa kuwepo nyingi ndani ya mji siyo moja tu.
 
14 Aug 2020
Nairobi, Kenya

My Unexpected Stroll With President Uhuru Kenyatta at Michuki Park


The newly launched John Michuki Memorial park in the capital was a beehive of activity a day after it opened its doors to the public. The park which is located between Kijabe street and Kipande road registered an impressive number of visitors who came to enjoy the promised greenspaces to escape the bustle of the city streets. This additional Park in Nairobi wants to restore Nairobi to its former glory as the city in the sun.
Source : CHAMS MEDIA TV
 
Tuyapende na kuyaboresha mazingira kwa kutoharibu mimea, miti au uoto asili.

Mpenda mazingira Reginald Mengi alionesha mfano ambao unapaswa kuigwa na halmashauri, miji, vitongoji na vijiji kutunza mazingira.

 
Magereza wameambiwa waingize hela. Wafanye hivi. Wakope benki na wajenge majumba ya kuuza hapo. Wafanyakazi wafungwa. Wachukue wafungwa wenye ujuzi nchi nzima na wajenge nyumba za bei nafuu hapo. Wanaweza toa mji wa mfano nchi nzima.
Hivi magereza huwa wanaajiri wahandisi? Kama bado ni wakati wa kuajiri wahandisi na wasanifu.
Sehemu nzuri sana hiyo lakini umekaa mkonge ambao biashara yake ni zilipendwa.
 
Mwisho maeneo yote bora kwa kilimo mtayageuza makazi ya binadamu na kubakiza ardhi kame isiyoweza hata kuoteshwa mkonge iwe ya kilimo.

Mipango ya kulinda ardhi ya kilimo iheshimiwe. Halmashauri na vijiji wa washauri wananchi kujenga maeneo mengine ya wazi ambayo ni makame kujenga makazi yao.

Mfano jiji la New York nchini Marekani wameheshimu mipaka ya maeneo ya wazi kama maeneo ya kupumzika au kuufanya mji upumue wakati wa joto. Tukijenga kila mahali basi tutalalamika mjini joto, hakuna maeneo ya kijani, hakuna maeneo bora ya kilimo n.k kwa kuendekeza kutwaa mashamba na maeneo ya wazi mijini.

Tazama eneo la wazi la Central Park jijini New York lililozungukwa na maghorofa kwa kuwa halmashauri ya mji na wakazi wa New York kubaini umuhimu wa kijani au eneo la wazi mjini

Mkuu maeneo yanayolimwa katani ni ardhi ambayo soil is poor and not fertile, wazungu waliyabaini maeneo yote fertiles wakawa wanahamisha mazao kama pamba, kahawa, chai etc pia all marginal and infertile lands yakawa ya katani kwani haihitaji rutuba nyingi.
 
Wanabodi,

Hili bandiko la ulizo kuhusu usalama wa maisha ya wakazi wa manispaa ya Morogoro kwa kuwepo mashamba makubwa ya mkonge mali ya magereza huku idadi ya wakazi wake kuzidi kuongezeka na mahitaji ya ardhi kuwa makubwa.

Eneo kuanzia Mkambarani hadi Kingolwira kuna mashamaba makubwa kando kando ya barabara ambayo yanahatarisha usalama wa watembea kwa mguu na waendesha pikipiki kati ya Mkambarani na Kingolwira baada ya saa kumi na mbili jioni. Mashamba ya mkonge yaliyoko Kihonda mali ya magereza yaliyo kando kando ya barabara ya Moro-Dom nayo hayana manufaa sana hapo yalipo kwa kuzingatia usalama wa raia lakini pia kusababisha mahitaji ya ardhi kwa ajili ya makazi kupanda na gharama kwenda juu.

View attachment 1647449

USHAURI kwa Mamlaka husika:

1. Maeneo ya mashamba haya ya mkonge yapunguzwe kwa ajili ya shughuli zingine za kiuchumi, kijamii na makazi ukizingatia treni ya mwendo kasi SGR imepitia maeneo hayo

2. Mashamba ya mkonge yahamishiwe kwingine kama Kiegea ambako jeshi la magereza watamudu vyema kuyahudumia kwa uzalishaji ulio bora kwa ajili ya viwanda;

3. Bwawa jingine kubwa lijengwe (streams water catchment) lijengwe kuhifadhi baadhi ya maji yanayotiririka kutoka katika mili Uluguru na kumwaga maji hayo ndani ya mto Ruvu au mto Ngerengere kwa matumizi ya kutosha kwa viwanda ambavyo wawekezaji wanasita kuweka miradi mikubwa kwa hofu ya kuwepo mgao wa maji maana maji ya Bwawa la Mindu huduma ya kwanza ni kwa matumizi ya binadamu

4. Kando kando ya reli ya mwendo kasi SGR wapo wawekezaji ambao wangependa kuwekeza kuchakata mazao ya chakula, biashara nk lakini ardhi ni finye sana kwa kuwa eneo kubwa ni mashamba ya mkonge mali ya jeshi la magereza kama ilivyoelezwa hapo juu

5. Pawepo na barabara ya huduma za usafiri kwa daladala kati ya Mkambarani, Kiegea hadi Mkundi mwisho hivyo kuunganisha na barabara kuu ya Moro-Dom

6. Ndani ya miaka mitano ijayo wageni wengi ikiwa pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa serikali kuu waliopangiwa vituo jijini Dodoma wangependelea kujenga hapo kwa makzi kutokana na hali hewa yake ilivyo ambayo inauoto wa asili halisi kwa kuliwaza;

7. Utalii haufanyio vizuri kuanzia kwenye mji wa Morogoro ijapokuwa kuna vivutio vingi tu lakini haieleweki tatizo ni nini
Pia unatakiwa kujengwa Uwanja wa Ndege (Airport) mkubwa katika Mji wa Morogoro. Nashauri eneo la Hifadhi la Misitu liliopo eneo la Mkundi na Makunganya mpakani na eneo la Wilaya ya Mvomero litwaliwe ili litumike kwa ajili ya Ujenzi wa Uwanja wa Ndege Mkubwa, ule uwanja uliopo eneo la Kihonda ni mdogo sana, hauna uwezo wa kuruhusu ndege kubwa kutua.
Viongozi wa Serikali waliopo ndani ya Mkoa wa Morogoro, hususani ndani ya Manispaa ya Morogoro na wale wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege wachukue wazo hili na kulifanyia kazi haraka. Wakichelewa kuchukua gatua haraka upo uwezekano mkubwa kwa ardhi hiyo ya Misitu ikavamiwa na Wananchi na hatimaye kukosekana kabisa kwa ardhi kubwa itakayofaa kujengwa uwanja wa ndege mkubwa ndani ya Manispaa ya Morogoro. Ardhi na eneo nililopendekeza linaonekana kuwa linafaa sana kwa ujenzi wa uwanja wa ndege kwani Lina landform nzuri sana, liko flat sana. Ujenzi wa uwanja huo utasaidia kwa kiasi kikubwa sana kukuza Uchumi wa Mji wa Morogoro na wilaya zote za jirani kama vile Wilaya ya Mvomero, Morogoro Vijijini, Kilosa, Gairo, n.k.
 
Back
Top Bottom