May Day
JF-Expert Member
- May 18, 2018
- 6,162
- 8,820
Siku chache zilizopitanilingia matatani baada ya kumtandia ngumi "mlevi" mmoja aliyekuwa anatukana hovyo matusi ya nguoni Wachezaji kwenye Luninga huku akijua fika kuwa hawamsikii bali anatusumbua tu sisi tuliopo pale kufuatilia mechi.
Utashangaa Mtu anavyomkosoa Kocha mpaka unajiuliza hivi huyu ndiye mwenye mawazo sahihi kuliko Kocha aliyepo pale? Yaani yeye ndiye Arsene Wenger au Furguson au Morinyo?
Hivi wakati huyo Kocha anaomba kazi wewe ulikuwa wapi? Si ungeomba na wewe kai upewe?.
Huyo Kocha kapeleka wasifu wake ndio maana yupo hapo, yupo kazini na analipwa kwa hiyo kazi sasa ni vipi tena nyie ndio mnataka kumuelekeza aifanye vipi kazi yake?.
Ujuzi aliojinadi nao ndio anaopaswa kuutekeleza pale ili aendelee kuwa kazini, sasa huo ushauri wenu nyie ni wa nini, kwani atakugawia mshahara wake? au siku akifukuzwa kazi atakuita ukamtetee?.
Huyo Kocha hatokaa hapo milele hivyo kama ninyi mnajua cha kufanya subirini akifukuzwa au akiondoka nanyi muombe kazi mkaweke huo utaalmu wenu, ambapo kila mkimpanga Mchezaji akikosea basi unamtoa unamuingiza mwingine, naye akikosea unamtoa na kumuingiza mwingine. Nadhani pia mtapendekeza na sheria ya substitution ibadilishwe kuwe na Wachezaji mia wanaosubiri nje, na vikombe mtazoa kwa kila shindano.
Mjinga siku zote hufikiri kila jambo ni rahisi tu, na vichwa vyenu vitupu hivyo ukipewa viatu vya Kocha wakati wa mechi anayohitaji ushinda ili ajira yake ibaki hivi ni wangapi mtaviweza?
Utamsikia Mtu analalamika kwa nini hujamuingiza huyu au yule, Watu vichwa vimeshaathiriwa na betting sasa kazi imekuwa ni kubashiri tu kila kitu...kwamba akiingia fulani atacheza vizuri, au akiingia fulan ndio atafunga magoli.
Tuache ushabiki Maandazi na tuheshimu kazi za Wengine.
Utashangaa Mtu anavyomkosoa Kocha mpaka unajiuliza hivi huyu ndiye mwenye mawazo sahihi kuliko Kocha aliyepo pale? Yaani yeye ndiye Arsene Wenger au Furguson au Morinyo?
Hivi wakati huyo Kocha anaomba kazi wewe ulikuwa wapi? Si ungeomba na wewe kai upewe?.
Huyo Kocha kapeleka wasifu wake ndio maana yupo hapo, yupo kazini na analipwa kwa hiyo kazi sasa ni vipi tena nyie ndio mnataka kumuelekeza aifanye vipi kazi yake?.
Ujuzi aliojinadi nao ndio anaopaswa kuutekeleza pale ili aendelee kuwa kazini, sasa huo ushauri wenu nyie ni wa nini, kwani atakugawia mshahara wake? au siku akifukuzwa kazi atakuita ukamtetee?.
Huyo Kocha hatokaa hapo milele hivyo kama ninyi mnajua cha kufanya subirini akifukuzwa au akiondoka nanyi muombe kazi mkaweke huo utaalmu wenu, ambapo kila mkimpanga Mchezaji akikosea basi unamtoa unamuingiza mwingine, naye akikosea unamtoa na kumuingiza mwingine. Nadhani pia mtapendekeza na sheria ya substitution ibadilishwe kuwe na Wachezaji mia wanaosubiri nje, na vikombe mtazoa kwa kila shindano.
Mjinga siku zote hufikiri kila jambo ni rahisi tu, na vichwa vyenu vitupu hivyo ukipewa viatu vya Kocha wakati wa mechi anayohitaji ushinda ili ajira yake ibaki hivi ni wangapi mtaviweza?
Utamsikia Mtu analalamika kwa nini hujamuingiza huyu au yule, Watu vichwa vimeshaathiriwa na betting sasa kazi imekuwa ni kubashiri tu kila kitu...kwamba akiingia fulani atacheza vizuri, au akiingia fulan ndio atafunga magoli.
Tuache ushabiki Maandazi na tuheshimu kazi za Wengine.