Lucas Mwashambwa
JF-Expert Member
- Jul 28, 2022
- 15,339
- 9,766
Ndugu zangu Watanzania,
Macho na masikio ya mamilioni ya Watanzania yameelekezwa kwa Rais Samia kesho kwa kuwa mamilioni ya Watanzania wana kiu ya kuisikia sauti ya mama yao mpendwa ikiwa ndani ya uwanja wa Benjamini mkapa.
Kwa siku nyingi jumuiya ya wana michezo katika mechi nyingi imeonyesha kumuunga mkono Rais samia kutokana na kutambua mchango wake katika kuinua michezo hapa nchini.
Tumeshuhudia mara nyingi mashabiki wakiwa uwanjani wakipeperusha mabango yenye picha ya Rais Samia, ambaye ameleta hamasa kubwa sana katika michezo na kuleta ushindani mkubwa sana hasa katika eneo la ufungaji wa magoli.
Sasa kesho Rais Samia, mama wa shoka anakwenda kuingia ndani ya Uwanja wa Benjamini Mkapa kishujaa, kijemedari, kikomadoo na kibabe. Ni kishindoo kitakacho itetemesha nchi na kusimamisha shughuli zote hapa nchini na ukanda wa Afrika mashariki, macho yote yanakwenda kuelekezwa kwa Rais Samia.
Mitandao ya kijamii na vyombo vyote vya habari vinakwenda kutekwa na habari za Rais Samia. Kama unapanga kufanya shughuli yoyote ile au kutoa tamko lolote lile au kutoa malalamiko ni bora ukasubiri kwa wiki nzima, maana habari ya mjini na Bara la Afrika itakuwa ni kishindo cha Rais Samia kila eneo.
Wenye chuki na mama yetu mpendwa Samia ni bora wakajipeleka mapema hospitali maana mtetemeko wake hautawaacha salama. Nimeshuhudia mijadala mingi ikiendelea mitaani na vijiwe ni juu ya kiu na hamu ya Watanzania kumuona mama yao akiwa uwanjani.
Kwa hakika huwezi ukamshinda wala kushindana na aliyebarikiwa na Mungu, huwezi kumshusha aliyeinuliwa na mkono wa Mwenyezi Mungu, huwezi ukamchafua aliyepakwa mafuta na Mungu wala huwezi kumzuia njia aliyeongozwa na Mwenyezi Mungu. Lazima uswagwe tu, uburuzwe, maana nguvu yake ni nguvu iliyo na kibali cha Mwenyezi Mungu.
Tukae mkao wa kumsubiri mwamba na jemedari wetu, jasiri muongoza njia akiingia kwa kishindo, usipange kukosa wala kusubiri kuhadithiwa maana utajuta maishani mwako kukosa kuwa sehemu ya kuandika historia ya kuja kuwasimulia wajukuu zako juu ya siku ya kesho ambapo komandoo na mama wa shoka atakapo ingia kishujaa uwanjani.
Kazi iendelee, mama ametufikia na kuwafikia Watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya Watanzania wanyonge wasio na sauti.
Lucas Hebel, mwashambwa,
Kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.
0742-676627.
Macho na masikio ya mamilioni ya Watanzania yameelekezwa kwa Rais Samia kesho kwa kuwa mamilioni ya Watanzania wana kiu ya kuisikia sauti ya mama yao mpendwa ikiwa ndani ya uwanja wa Benjamini mkapa.
Kwa siku nyingi jumuiya ya wana michezo katika mechi nyingi imeonyesha kumuunga mkono Rais samia kutokana na kutambua mchango wake katika kuinua michezo hapa nchini.
Tumeshuhudia mara nyingi mashabiki wakiwa uwanjani wakipeperusha mabango yenye picha ya Rais Samia, ambaye ameleta hamasa kubwa sana katika michezo na kuleta ushindani mkubwa sana hasa katika eneo la ufungaji wa magoli.
Sasa kesho Rais Samia, mama wa shoka anakwenda kuingia ndani ya Uwanja wa Benjamini Mkapa kishujaa, kijemedari, kikomadoo na kibabe. Ni kishindoo kitakacho itetemesha nchi na kusimamisha shughuli zote hapa nchini na ukanda wa Afrika mashariki, macho yote yanakwenda kuelekezwa kwa Rais Samia.
Mitandao ya kijamii na vyombo vyote vya habari vinakwenda kutekwa na habari za Rais Samia. Kama unapanga kufanya shughuli yoyote ile au kutoa tamko lolote lile au kutoa malalamiko ni bora ukasubiri kwa wiki nzima, maana habari ya mjini na Bara la Afrika itakuwa ni kishindo cha Rais Samia kila eneo.
Wenye chuki na mama yetu mpendwa Samia ni bora wakajipeleka mapema hospitali maana mtetemeko wake hautawaacha salama. Nimeshuhudia mijadala mingi ikiendelea mitaani na vijiwe ni juu ya kiu na hamu ya Watanzania kumuona mama yao akiwa uwanjani.
Kwa hakika huwezi ukamshinda wala kushindana na aliyebarikiwa na Mungu, huwezi kumshusha aliyeinuliwa na mkono wa Mwenyezi Mungu, huwezi ukamchafua aliyepakwa mafuta na Mungu wala huwezi kumzuia njia aliyeongozwa na Mwenyezi Mungu. Lazima uswagwe tu, uburuzwe, maana nguvu yake ni nguvu iliyo na kibali cha Mwenyezi Mungu.
Tukae mkao wa kumsubiri mwamba na jemedari wetu, jasiri muongoza njia akiingia kwa kishindo, usipange kukosa wala kusubiri kuhadithiwa maana utajuta maishani mwako kukosa kuwa sehemu ya kuandika historia ya kuja kuwasimulia wajukuu zako juu ya siku ya kesho ambapo komandoo na mama wa shoka atakapo ingia kishujaa uwanjani.
Kazi iendelee, mama ametufikia na kuwafikia Watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya Watanzania wanyonge wasio na sauti.
Lucas Hebel, mwashambwa,
Kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.
0742-676627.