Masha adaiwa kutumia uwaziri kupita Ubunge

Wera wera weraaaaaaaaaaaaaaa Presha inapanda Presha inashuka saffffffffffffffffiiiiiiiiiiiiiiiii Sana CHADEMA peleka Mahakamani kIsha Fungilia Mbali Mgombea wetu apite bila kupingwa mimi mwenyewe ndo wa Jimbo hilo naenda TZ tar 30-10-10 kwaajili ya KUra tu Wera wera weraaaaaaaaaaaa .............Watuu Piiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiipoooooooooooooooooooooooo kunani? fUNGA MASHA:becky::becky::becky::becky::becky::becky::becky::becky::becky::becky::becky::becky:
 
We real need to send away a lot of people like Masha, kuwa waziri si kwamba you can do anything bila ya kuwajibishwa, na kitu cha ajabu raisi wetu uwezo wake mdogo sana wa kufikiri kiasi kwamba anakurupuka na kumtangaza Masha ndo mbunge wa nyamagana bila hata ya kuhitaji kujiridhisha kuwa hakuna conflict of interest au uonevu? so longer ni masha basi yuko sahihi sasa kuna mategemeo kweli raisi wa aina hii ambaye hajali chochote hata kudhibiti nidhamu kwa mawaziri wake hawezi, duh! watanzania JK ana uwezo mdogo sana wa kufikiri
 
Wera wera weraaaaaaaaaaaaaaa Presha inapanda Presha inashuka saffffffffffffffffiiiiiiiiiiiiiiiii Sana CHADEMA peleka Mahakamani kIsha Fungilia Mbali Mgombea wetu apite bila kupingwa mimi mwenyewe ndo wa Jimbo hilo naenda TZ tar 30-10-10 kwaajili ya KUra tu Wera wera weraaaaaaaaaaaa .............Watuu Piiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiipoooooooooooooooooooooooo kunani? fUNGA MASHA:becky::becky::becky::becky::becky::becky::becky::becky::becky::becky::becky::becky:

Hakyanani imebidi nicheke tu manake umenikumbusha kina masanjaaaaaaa:becky::becky::becky:
 
Good; afungiliwe mbali huko; Nyamagana ni jimbo la chadema eitha kwa kushinda ktk kurfa au kupita bila kupingwa
 
Ikiwa mtu pekee anayeweza kutamka kuwa huyu ni raia ama sii raia ni waziri wa mambo ya ndani, basi uhakika Jk aliokuwa nao ndani ya NECkuweza kutamka kuwa Bashe sii raia atakuwa aliupata kwa Masha. Hivyo basi inadhihirisha wazi kwamba Tz tutakuwa na waziri wa mambo ya ndani mwongo. Na kama JK hakupata hakikisho la uraia wa Bashe kutoka kwa waziri husika, huku akiitambua itifaki, basi tutakuwa tuna rais mzushi ambacho ni kitu hatari kwa ustawi wa taifa. Cha msingi ni sisi raia kuona huu uozo wa chama tawala na kukipiga chini kwa kishindo. Pia Chadema msiacha azma yenu ya kumshitaki Masha kwa matumizi mabaya ya ofisi(kujifanya mungu mtu)
 
Safi!! Wache iwe findisho kwa viongozi wote wanaofikiri wako juu ya sheria...sorry to say, but Masha is hopeless!
 
na Sitta Tumma, Mwanza


WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni mgombea ubunge wa Jimbo la Nyamagana, jijini Mwanza, Lawrence Kego Masha, na msafara wake jana alionja joto la jiwe, baada ya wananchi kumtamkia hadharani jina la mpinzani wake, Ezekiel Wenje (CHADEMA), huku wakimuonyesha vidole viwili, ishara iliyopo kwenye bendera ya CHADEMA.
Masha alikumbana na hali hiyo ya upinzani muda mfupi baada ya kumaliza kuhutubia mkutano wake wa uzinduzi wa kampeni jana katika viwanja vya Shule ya Msingi Mirongo jijini hapa, ambapo wakati akitoka mkutanoni hapo baadhi ya wananchi walianza kumtajia jina la Wenje.
Wenje ndiye mpinzani wa Masha katika kinyang'anyiro cha kusaka ubunge wa jimbo hilo katika Uchaguzi Mkuu uliopangwa kufanyika Oktoba 31 mwaka huu, na kwamba hali hiyo ya jana imeonyesha waziri huyo anakabiliwa na upinzani mkali.
Wakati Masha na msafara wake wakipita kandokando ya barabara eneo hilo la Mirongo, wananchi hao walisikika wakisema: “Wenje CHADEMA, Wenje CHADEMA, Wenje CHADEMA, huku wakimuonyesha Masha vidole viwili juu na picha za Wenje na zile za mgombea urais wa CHADEMA, Dk. Willibrod Peter Slaa.
Hata hivyo Masha ambaye alikuwa amekaa kwenye kiti cha mbele kushoto katika gari alilokuwa amepanda, naye alishuhudia hali hiyo, lakini hakubabaika, alikuwa akiwapungia mkono wananchi hao waliokuwa wakimtaja mpinzani wake.
Kutokana na kitendo hicho, walinzi wa CCM maarufu kwa jina la 'Green Guard' walilizunguka gari hilo la Masha huku wakiwa wameshikana mikono, kuashiria kuzuia mtu mwingine kulisogelea gari hilo alilokuwa amepanda mgombea huyo wa CCM wa Jimbo hilo la Nyamagana.
Awali, Masha wakati akiwahutubia wananchi katika uzinduzi wa kampeni Zake, alikiri kumuwekea pingamizi ya uraia mgombea wa CHADEMA, Wenje, na kusema pingamizi hilo aliliweka kama mgombea ubunge na si kwa nafasi ya uwaziri alionao.
Katika mkutano wake huo wa kampeni, Masha alisema hana tabia ya kumuonea mtu wala hana tabia ya kutumia vibaya madaraka, na aliitumia fursa hiyo kulishambulia gazeti moja linalotoka kwa wiki la Kanda ya Ziwa, kwa kuandika habari kuwa Wenje ameitikisa CCM.




Mimi nadhani masha , siku aliposikia wenje karejeshwa alishindwa hata, kula, na usiku hakupata hata usingizi.
 
nimeona kwenye taarifa ya habari TBC, mkutano wake umejaza wasanii wa muziki wa kila aina, bilashaka wahudhuriaji walienda kuburudika kwa nyimbo za wasanii mbalimbali ambao kwao ingebidi watoe viingilio kuingia ila neema imewajia kupitia mkuu MASHA kwa wkt huu. hawajaenda kusikiliza sera za Masha ndo maana baada ya mkutano walimtaja WENJE na DR. SLAA.
 
nimeona kwenye taarifa ya habari tbc, mkutano wake umejaza wasanii wa muziki wa kila aina, bilashaka wahudhuriaji walienda kuburudika kwa nyimbo za wasanii mbalimbali ambao kwao ingebidi watoe viingilio kuingia ila neema imewajia kupitia mkuu masha kwa wkt huu. Hawajaenda kusikiliza sera za masha ndo maana baada ya mkutano walimtaja wenje na dr. Slaa.

ndio maana kuna mtu humu alisema mikutano ya ccm ni concert!!! Au sawa na disko vumbi, uswazi tunaita kigodoro!!
 
Vijana wa kileo wanasema CCM wanaforce king,
Niko makambako apa naona kila kona zapigwa nyimbo za CCM na sioni dalili za mkutano for the last 4 days.
Si bugdha kwa raia jamani mna miaka 50 madarakani mbona mwatumia nguvu nyingi kumchinja kuku wako mwenyewe.
Tafakari,chukua hatua
 
Ndiye muhusika mkuu wa ile issue ya deep Green na kampuni yake ya IMMMA ADVOCATES !
 
Huyu mjamaa navyomchukia nashindwa kuelezea!! Akiangushwa na Wenje ninaweza kutoka nje bila nguo!! I reall would!!!
 
Mgombea ubunge katika jimbo la Nyamagana kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Lawrence Masha juzi alikimbizwa katika hospitali ya rufaa Bugando jijini hapa kwa ajili ya uchunguzi wa afya yake, baada ya kuishiwa nguvu wakati akijiandaa kwenda kwenye kampeni.
Katika tukio lingine, mgombea ubunge katika jimbo hilo kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) juzi hiyo alifikishwa katika kituo cha Polisi jijini hapa akidaiwa kufanya kampeni, nje ya ratiba.
Habari zilizolifikia NIPASHE JUMAPILI zinadai kwamba Masha ambaye ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi alikumbwa na mkasa huo majira ya mchana, wakati akijiandaa kuelekea katika kata ya Buhongwa kwa ajili ya mkutano wa kampeni.
Kwa mujibu wa chanzo chetu cha habari, hali hiyo ilisababisha Masha achelewe kufika Buhongwa.
“ Yeye mwenyewe alifika mkutanoni majira ya saa 11 jioni na kuanza kutuhutubia majira ya saa 11:30 na kutuambia kwamba alichelewa kufika kwa sababu alikuwa amekwenda kuchunguzwa afya yake katika hospitali ya rufaa Bugando,” kilidai chanzo chetu cha habari.
Kwa mujibu wa habari, Masha aliwaambia wananchi waliokuwa wamehudhuria kwenye mkutano huo kwamba aliishiwa nguvu wakati akijiandaa kuelekea Buhongwa.
“ Sisi tulikuwa tumetangaziwa kuwa mkutano huo ulikuwa umepangwa kuanza majira ya saa 8 mchana” kilifafanua chanzo cha habari.
Hata hivyo, Masha hakuweza kuzungumzia suala hilo kwa madai kuwa alikuwa kwenye kikao cha chama (CCM).
“ Niko kwenye kikao cha chama; tafadhali,” alisema Masha wakati alipopigiwa simu na gazeti hili, jana majira ya saa 5 asubuhi .
Jitihada za kumpata Meneja Kampeni wa CCM katika jimbo la Nyamagana, Sikitu Sanziyote hazikuzaa matunda baada ya simu yake ya mkononi kuita bila kupokelewa.
Kuhusu kukamatwa kwa Wenje, inadaiwa kuwa alishikiliwa kwa muda akidaiwa kufanya kampeni, nje ya ratiba.
Inadaiwa kuwa Wenje alikamatwa na askari polisi majira ya jioni, wakati akiwa eneo la Kamanga jijini hapa.
Kwa mujibu wa habari, Wenye alikuwa katika matembezi ya kawaida huku akisalimiana na wanachama pamoja na wapenzi wa Chadema.
Inadaiwa pia kwamba Wenje alitembea mwenyewe kutoka eneo la kivuko cha Kamanga hadi makao makuu ya Polisi wilaya ya Nyamagana baada ya kukataa kupanda kwenye gari la Polisi.
Habari zaidi zinadai kuwa askari polisi walitaarifiwa na baadhi ya wana-CCM kwamba Wenje alikuwa kwenye kampeni; huku akitumia vipaza sauti.
Katibu wa Chadema mkoani hapa, Wilson Mushumbusi amethibitisha kuwepo kwa hali hiyo.
“ Ni kweli Wenje alikamatwa kwa muda akisingiziwa kuwa alikuwa akifanya kampeni, madai ambayo hayana ukweli wowote. Lakini baadaye ameachiwa”, alisema Mushumbusi alipoulizwa na gazeti hili kwa njia ya simu juzi jioni.
Alisema njama hizo zinapangwa na baadhi ya wana-CCM ili kumdhoofisha Wenje.
Hakuweza kuzungumzia suala hilo kwa undani kwa madai kuwa litafikishwa ngazi ya juu ya Chadema ili liweze kufanyiwa maamuzi.
 
Back
Top Bottom