Resilience
JF-Expert Member
- Jan 4, 2023
- 877
- 4,106
Kuna taarifa zinasambaa mitandaoni kwamba familia ya kihindi ya Ladwa inatumia hati za kusafiria za Tanzania na Uingereza. Vyombo vya habari na baadhi ya watu wameenda mbali zaidi kusambaza nyaraka hizo mitandaoni.
Idara ya Uhamiaji katika kujibu hoja hii wameeleza kwamba watajwa walikoma kuwa RAIA wa Tanzania na sasa wanaishi nchini kama RAIA wa kigeni wakiwa na vibali halali.
Nimeangalia pia pasipoti zinazosambaa mitandaoni na naomba nikubaliane na Uhamiaji kwamba pasipoti inayosambaa mitandaoni ya Tanzania inaonekana ilitolewa zamani kabla ya pasipoti ya Uingereza jambo ambalo linaashiria kwamba hawa walikuwa RAIA wa Tanzania wakaukana utanzania na kupata uraia wa Uingereza
Kwa upande mwingine naomba niombe uhamiaji watoe pia ufafanuzi, hawa RAIA wa uingereza ambao awali walikuwa RAIA wa Tanzania wanaendeleaje kumiliki mali kama Watanzania wakati katiba na sheria zinakataza?
Ardhi wanayomiliki wanatumia uraia gani? Kama wanatumia uraia wa Tanzania kumiliki ardhi ,Uhamiaji na wizara ya ardhi awaoni kama haya ni makosa?
Malalamiko yanasema wanafukuza wapangaji kwenye nyumba za NHC, ni lini wageni wamepewa mamlaka yakufukuza wapangaji katika nyumba za shirika la umma? NHC mnawezaje kumvumilia mgeni aje atawale mali za umma na kuwafundisha wananchi namna ya kuzitumia? Kiburi wanatoa wapi?
Waziri wa mambo ya nje, hawa akina Ladwa ndio tuliowatungia sheria ya kuwapa hadhi maalumu? Na je hadhi maalumu itawapa nguvu hawa wahindi kutawala?
Idara ya Uhamiaji katika kujibu hoja hii wameeleza kwamba watajwa walikoma kuwa RAIA wa Tanzania na sasa wanaishi nchini kama RAIA wa kigeni wakiwa na vibali halali.
Nimeangalia pia pasipoti zinazosambaa mitandaoni na naomba nikubaliane na Uhamiaji kwamba pasipoti inayosambaa mitandaoni ya Tanzania inaonekana ilitolewa zamani kabla ya pasipoti ya Uingereza jambo ambalo linaashiria kwamba hawa walikuwa RAIA wa Tanzania wakaukana utanzania na kupata uraia wa Uingereza
Kwa upande mwingine naomba niombe uhamiaji watoe pia ufafanuzi, hawa RAIA wa uingereza ambao awali walikuwa RAIA wa Tanzania wanaendeleaje kumiliki mali kama Watanzania wakati katiba na sheria zinakataza?
Ardhi wanayomiliki wanatumia uraia gani? Kama wanatumia uraia wa Tanzania kumiliki ardhi ,Uhamiaji na wizara ya ardhi awaoni kama haya ni makosa?
Malalamiko yanasema wanafukuza wapangaji kwenye nyumba za NHC, ni lini wageni wamepewa mamlaka yakufukuza wapangaji katika nyumba za shirika la umma? NHC mnawezaje kumvumilia mgeni aje atawale mali za umma na kuwafundisha wananchi namna ya kuzitumia? Kiburi wanatoa wapi?
Waziri wa mambo ya nje, hawa akina Ladwa ndio tuliowatungia sheria ya kuwapa hadhi maalumu? Na je hadhi maalumu itawapa nguvu hawa wahindi kutawala?