Masha adaiwa kutumia uwaziri kupita Ubunge

Zak Malang

JF-Expert Member
Dec 30, 2008
5,404
234


Hatua ya mgombea ubunge chama cha mapinduzi (CCM) Jimbo la Nyamagana, Mwanza Lawrence Kego Masha kumwekea pingamizi mgombea wa Chadema kwa madai kuwa si raia imezua utata wa kisheria wa mawaziri kuendelea na nafasi zao hata baada ya Bunge la Muungano kuvunjwa.

Mbali na suala la kutokuwa na uraia, mgombea huyo wa Chadema, Ezekieh Dibogo Weje anadaiwa pia kuwa hakuwasilisha kiapo cha kisheria kuthibitisha yale aliyojaza kwenye fomu kama inavyotakiwa pamoja na kushindwa kujaza fomu za kugombea kama inavyotakiwa.

Sababu nyingine zilizotolewa na Masha ni kuwa mgombea Wenje alidai kuwa ni mkazi wa Burola A wakati si kweli kwani hana makazi katika mtaa huo na kwamba mgombea huyo pia amesema uongo juu ya cheo chake katika Nation Group kuwa ni meneja wakati in afisa masoko pamoja na kushindwa kujaza fomu ya kugombea kama inavyotakiwa.

Masha ni Waziri wa Mambo ya Ndani na hatua yake ya ya kudai kuwa Wenje si raia na kufuatiwa na malalamiko ya Wenje kuwa Masha anamtisha maisha pamoja na kutumia maafisa uhamiaji kwenda kwao Rorya kuchunguza uraia wake imezua hisia kwamba mgombea huyo wa CCM ametumia madaraka yake kufuatilia uraia wa mpinzani wake.

Wenje alisema kwamba Alhamisi iliyopita majira ya jioni alipokea simu ya Masha akimsihi kuondoa jina lake kwenye kinyang’anyiro hicho kwa madai kuwa sera za kampuni anayofanyia kazi haziruhusu wafanyakazi wake kujiingiza katika siasa.

“Aliniuliza kama nazifahamu sera za kampuni ninayofanyia kazi kwani haziruhusu mtumishi kuingia katika siasa na hivyo kunitaka nifikirie kuondoa jina langu na kwamba angenisaidia kurudishwa kazini. Lakini mimi nilikataa na kumwambia siwezi kujitoa kugombea.

“Siku hiyo hiyo saa mbili usiku alinipigia tena simu na kunieleza kuwa atatumia rasilimali zake kuhakikisha ananiwekea pingamizi kwa kuwa mimi si raia. Na kweli maofisa sita wa Serikali (Uhamiaji) walikwenda nyumbani kwetu Rorya na kumbughudhi mama yangu mzazi kwa madai kuwa wanakusanya vielelezo juu ya uraia wangu,” alisema Wenje akieleza kwamba alimwomba Masha aache kutumia vyombo vya dola kwa masilahi yake.

Lakini Masha alikiri kumpigia simu mgombea huyo wa Chadema lakini akakana kumtishia pamoja na kutumia maofisa uhamiaji kwenda kufuatilia uraia wakekijijini kwao Rorya na akasema kuwa alimpigia kumshauri kwa nia njema, kwani siasa si ugomvi.

“Ni kweli nilizungumza naye kwa simu lakini si kwa ugomvi wala kumtisha. Milimweleza kuhusu sera za kampuni yao kutoiruhusu watumishi wake kujihusisha na siasa na kama anazifahamu.

“Pia nilimwambia kuhusu udanganyifu katika fomu zake na kwamba nilikuwa natarajia kumwekea pingamizi na nitamshinda, hivyo bora angeachia ngazi.

“Nilimshauri pia kama ndugu yangu, maana siasa si ugomvi, kuwa ukiacha kurudisha fomu nitakuombea usifukuzwe kazi kulingana na sera za chombo chako kwani kitendo cha kujiingiza katika siasa atafukuzwa kazi. Na kweli niliweka pingamizi sasa huko ni kumtishia maisha?

“Sijamtuma ofisa yeyote kwenda kwake na hili la uraia nimelipata kutoka kwa wapambe wake. Mimi ni mwanasheria, siwezi kufanya hivyo.” alisema Masha.

Ni kutokana na maelezo hayo ya Masha, baadhi ya watu wanadai kuwa ni ngumu kutenganisha kitendo cha maofisa uhamiaji kwenda kufuatilia uraia huo wa Wenje baada ya Masha kumpigia simu kumwomba ajitoe na kwamba angemwekea pingamizi kwani si raia.

“Huyu ni Waziri wa Mambo ya Ndani mwenye dhamana ya mambo ya uraia hivyo kitendo cha yeye kuhoji uraia wa mtu na hapo hapo watu wanaenda kwake Wenje kufuatilia vielelezo vya uraia wake, moja kwa moja unaona kuwa kuna uhusiano fulani kwamba huenda ni maelekezo yake kwa idara ya uhamiaji.

“Hapa kuna conflict of interest. Pia inapaswa ujiulize ni kwa nini Masha ampigie simu kumwomba ajitoe wakati anajua atamwekea pingamizi?

“Ni kwa nini aseme angemwombea aendelee na kazi yake iwapo angejitoa. Ina maana Wenje alikuwa hajui sera za kampuni anayofanyia kazi mpaka aambiwe na Masha? Au Masha alikuwa na uchungu gani kuona Wenje atakosa kazi mpaka amwombee asifukuzwe? Masha ana uhusiano au mamlaka gani kwa mwajiri wa Wenje mpaka aseme angemwombea asifukuzwe kazi? Huyu ni msomi wa Chuo Kikuu hawezi kuamua kugombea bila kujua sera za chombo chake,” anasema mkazi mmoja wa jijini Mwanza aliye karibu na sakata hilo ambaye hakutaka jina lake litajwe.

Watu kadha waliozungumza na Raia Mwema wanasema kitendo cha mawaziri kuendelea na nafasi zao baada ya Bunge kuvunjwa kunaleta mgongano wa masilahi kwani waziri anaweza kutumia nafasi yake kujifanyia kampeni….
.


Habari zaidi katika Raia Mwema ya leo. Mwenye complete soft copy ya stori hii twamuomba atuwekee hapa.
 


Hatua ya mgombea ubunge chama cha mapinduzi (CCM) Jimbo la Nyamagana, Mwanza Lawrence Kego Masha kumwekea pingamizi mgombea wa Chadema kwa madai kuwa si raia imezua utata wa kisheria wa mawaziri kuendelea na nafasi zao hata baada ya Bunge la Muungano kuvunjwa.

Mbali na suala la kutokuwa na uraia, mgombea huyo wa Chadema, Ezekieh Dibogo Weje anadaiwa pia kuwa hakuwasilisha kiapo cha kisheria kuthibitisha yale aliyojaza kwenye fomu kama inavyotakiwa pamoja na kushindwa kujaza fomu za kugombea kama inavyotakiwa.

Sababu nyingine zilizotolewa na Masha ni kuwa mgombea Wenje alidai kuwa ni mkazi wa Burola A wakati si kweli kwani hana makazi katika mtaa huo na kwamba mgombea huyo pia amesema uongo juu ya cheo chake katika Nation Group kuwa ni meneja wakati in afisa masoko pamoja na kushindwa kujaza fomu ya kugombea kama inavyotakiwa.

Masha ni Waziri wa Mambo ya Ndani na hatua yake ya ya kudai kuwa Wenje si raia na kufuatiwa na malalamiko ya Wenje kuwa Masha anamtisha maisha pamoja na kutumia maafisa uhamiaji kwenda kwao Rorya kuchunguza uraia wake imezua hisia kwamba mgombea huyo wa CCM ametumia madaraka yake kufuatilia uraia wa mpinzani wake.

Wenje alisema kwamba Alhamisi iliyopita majira ya jioni alipokea simu ya Masha akimsihi kuondoa jina lake kwenye kinyang'anyiro hicho kwa madai kuwa sera za kampuni anayofanyia kazi haziruhusu wafanyakazi wake kujiingiza katika siasa.

"Aliniuliza kama nazifahamu sera za kampuni ninayofanyia kazi kwani haziruhusu mtumishi kuingia katika siasa na hivyo kunitaka nifikirie kuondoa jina langu na kwamba angenisaidia kurudishwa kazini. Lakini mimi nilikataa na kumwambia siwezi kujitoa kugombea.

"Siku hiyo hiyo saa mbili usiku alinipigia tena simu na kunieleza kuwa atatumia rasilimali zake kuhakikisha ananiwekea pingamizi kwa kuwa mimi si raia. Na kweli maofisa sita wa Serikali (Uhamiaji) walikwenda nyumbani kwetu Rorya na kumbughudhi mama yangu mzazi kwa madai kuwa wanakusanya vielelezo juu ya uraia wangu," alisema Wenje akieleza kwamba alimwomba Masha aache kutumia vyombo vya dola kwa masilahi yake.

Lakini Masha alikiri kumpigia simu mgombea huyo wa Chadema lakini akakana kumtishia pamoja na kutumia maofisa uhamiaji kwenda kufuatilia uraia wakekijijini kwao Rorya na akasema kuwa alimpigia kumshauri kwa nia njema, kwani siasa si ugomvi.

"Ni kweli nilizungumza naye kwa simu lakini si kwa ugomvi wala kumtisha. Milimweleza kuhusu sera za kampuni yao kutoiruhusu watumishi wake kujihusisha na siasa na kama anazifahamu.

"Pia nilimwambia kuhusu udanganyifu katika fomu zake na kwamba nilikuwa natarajia kumwekea pingamizi na nitamshinda, hivyo bora angeachia ngazi.

"Nilimshauri pia kama ndugu yangu, maana siasa si ugomvi, kuwa ukiacha kurudisha fomu nitakuombea usifukuzwe kazi kulingana na sera za chombo chako kwani kitendo cha kujiingiza katika siasa atafukuzwa kazi. Na kweli niliweka pingamizi sasa huko ni kumtishia maisha?

"Sijamtuma ofisa yeyote kwenda kwake na hili la uraia nimelipata kutoka kwa wapambe wake. Mimi ni mwanasheria, siwezi kufanya hivyo." alisema Masha.

Ni kutokana na maelezo hayo ya Masha, baadhi ya watu wanadai kuwa ni ngumu kutenganisha kitendo cha maofisa uhamiaji kwenda kufuatilia uraia huo wa Wenje baada ya Masha kumpigia simu kumwomba ajitoe na kwamba angemwekea pingamizi kwani si raia.

"Huyu ni Waziri wa Mambo ya Ndani mwenye dhamana ya mambo ya uraia hivyo kitendo cha yeye kuhoji uraia wa mtu na hapo hapo watu wanaenda kwake Wenje kufuatilia vielelezo vya uraia wake, moja kwa moja unaona kuwa kuna uhusiano fulani kwamba huenda ni maelekezo yake kwa idara ya uhamiaji.

"Hapa kuna conflict of interest. Pia inapaswa ujiulize ni kwa nini Masha ampigie simu kumwomba ajitoe wakati anajua atamwekea pingamizi?

"Ni kwa nini aseme angemwombea aendelee na kazi yake iwapo angejitoa. Ina maana Wenje alikuwa hajui sera za kampuni anayofanyia kazi mpaka aambiwe na Masha? Au Masha alikuwa na uchungu gani kuona Wenje atakosa kazi mpaka amwombee asifukuzwe? Masha ana uhusiano au mamlaka gani kwa mwajiri wa Wenje mpaka aseme angemwombea asifukuzwe kazi? Huyu ni msomi wa Chuo Kikuu hawezi kuamua kugombea bila kujua sera za chombo chake," anasema mkazi mmoja wa jijini Mwanza aliye karibu na sakata hilo ambaye hakutaka jina lake litajwe.

Watu kadha waliozungumza na Raia Mwema wanasema kitendo cha mawaziri kuendelea na nafasi zao baada ya Bunge kuvunjwa kunaleta mgongano wa masilahi kwani waziri anaweza kutumia nafasi yake kujifanyia kampeni….
.


Habari zaidi katika Raia Mwema ya leo. Mwenye complete soft copy ya stori hii twamuomba atuwekee hapa.


Asante Mkuu Zak kwa kutuletea hii: lakini penye red: Hawezi kufanya hivyo kwa kuwa ni mwanasheria?? Ha Ha Ha! Siyo kampuni yake ya uanashera iliyohusika katika uanzishwaji wa kampuni feki ya Deep Green ambayo baada tu ya kuiba Tsh 13 billion za Watanzania kutoka Benki Kuu akaisimamia kuifuta? Anasema nini fisadi mkubwa huyu?
 
Na hii ni only tip katika iceberg. Mi nadhani karibu majimbo yote ambako wagombea wa jamaa hawa walipita bila kupingwa waliwahonga wale wa upinzani. Mimi nina wasiwasi sana katika jimbo la Pinda -- Mlele. Wagombea wa CUF na Chadema walijitoa dak za mwisho!!!! Haya kwenu Takukuru - kama kweli mnatumia haki!!!!!
 
Lakini nani atchunguza hili suala la Masha kwani Mgonjwa wetu kisha msifia kwa ushindi wake wa meza. Angekuwa na busara na maadili, kwanza angeagiza upelelezi wa ushindi wa mezani wa watu kama akina Masha kabla ya kuanza kuwasifia jukwaani. Lakini kuwasifia jukwaani ni onyo kwa vyombo vya sheria kwamba yeye kesha amua. It's a real f****** country!!!!
 
Tayari kuna manung'uniko mengi tu kwenye kada za polisi. Yaani mtu ambaye ofisi yake imekumbwa na kashfa nzito sana ndjio anapita bila kupingwa...?? Hata CUF na wengine hawakuwa na wagombea?
 
Tayari kuna manung'uniko mengi tu kwenye kada za polisi. Yaani mtu ambaye ofisi yake imekumbwa na kashfa nzito sana ndjio anapita bila kupingwa...?? Hata CUF na wengine hawakuwa na wagombea?

Halafu nilisikia kwa mbali eti Masha ni one of the presidential materials for 2015!!! Lakini kwa nchi kama hii na uongozi kama huu wa CCM haitakuwa ajabu sana iwapo akaukwaa.
 
Baada ya kushinda pingamizi la mgombea wao dhidi ya Lawrence Masha, CHADEMA sasa wanapanga kumburuza mahakamani Masha kwa kutumia vibaya madaraka yake, juu ya issue ya uraia.

Mwaka huu kazi, mwaga mboga ni mwage ugali.
 
Source Clouds FM

Mgombea Ubunge kwa jimbo la Nyamagana Mwanza Lawrence Masha huenda ndoto yake ya kugombea ubunge ikayeyuka baada ya CHADEMA sasa kumgeuzia kibao kwa madai yafuatayo:

  • Kutumia vibaya madaraka ya uwaziri kumwengua mshindani wake
  • Kukiuka sheria ya uchaguzi ya kutumia uwaziri au cheo cha serikalini kisiasa katika kampeni
  • Kujiona yeye ni raia zaidi kuliko wengine wakati si kweli.
  • Kufanya ufisadi wa aina yake kumwengua mgombea halali
Kaimu Katibu Katibu Mkuu wa CHADEMA John Mnyika amesema, suala hilo sasa wanapewa wanasheria wa CHADEMA ili waweze kulifanyia kazi kwa kulifikisha mbele ya vyombo vya sheria na ama msajili wa vyama ama NEC.

Tanzania kumekucha!
 
Kuna haja ya kufanya ivyo mapema ili iwe fundisho na kwa wengine.
 
Source Clouds FM

Mgombea Ubunge kwa jimbo la Nyamagana Mwanza Lawrence Masha huenda ndoto yake ya kugombea ubunge ikayeyuka baada ya CHADEMA sasa kumgeuzia kibao kwa madai yafuatayo:


  • Kutumia vibaya madaraka ya uwaziri kumwengua mshindani wake
  • Kukiuka sheria ya uchaguzi ya kutumia uwaziri au cheo cha serikalini kisiasa katika kampeni
  • Kujiona yeye ni raia zaidi kuliko wengine wakati si kweli.
  • Kufanya ufisadi wa aina yake kumwengua mgombea halali
Kaimu Katibu Katibu Mkuu wa CHADEMA John Mnyika amesema, suala hilo sasa wanapewa wanasheria wa CHADEMA ili waweze kulifanyia kazi kwa kulifikisha mbele ya vyombo vya sheria na ama msajili wa vyama ama NEC.

Tanzania kumekucha!

Kwa kweli inabidi ifike mahala hawa watawala wetu wasijione miungu sasa!! Maan hii ilikuwa mbaya na kama angechiwa this should have set the precedent: lazima akione na yeye!!!

Safi CHADEMA.
 
HTML:
Source of Information plse
hata mimi naweza kuwa source.
tumeamua kumpeleka Masha mahakamani kwa kutumia vibaya madaraka yake, na kwa ushahidi tulio nao, nahisi wakati wa Masha kuwa mwanasiasa umefika.
 
Pameshakuwa patamu sasa! Watakuwa wanajiuliza mara mbili mbili kuweka mapingamizi
 
Superman, asante kwa taarifa yako. Nilishawahi kusema huko nyuma kuwa uchaguzi wa mwaka huu sheria za Tanzania zitakuwa tested kuliko wakati wowote huko nyuma. Na hii ni dalili njema inaonesha watu wameamka na kutambua haki zao. Naomba spirit hiyo idumu kwani ina manufaa kwa demokrasi na ustawi wa nchi yetu.
Sungura
 
Apelekwe mahakamani haraka iwezekanavyo, we can't wait a minute.
Inshalah, nashukuru kwa CHADEMA kuliona hilo.
 
We dogo masha kwa kudhani wewe ni mwanasheria zaidi ya wenzio na kutumia vibaya madaraka, sasa ona.............. kama JK ana wasaidizi wa aina yako tutegemee nini?

Na kwako uliye na green kadi tutasemaje?
 
Kanza, Kwa mtazamo wangu, upo uwezekano - kwa kuwa yeye (Masha) bado ni waziri mwenye dhamana ya masuala yote ya uraia, uhamiaji na usalama wa raia - kwamba anaweza kupatikana na hatia ya matumizi mabaya ya madaraka yake, kwa kutoa taarifa (akiwa kama mtumishi wa umma) kwamba mgombea wa CHADEMA si raia, wakati anaujua ukweli. Kwenye Criminal Procedure Act (CPA), matumizi mabaya ya madaraka kwa mtumishi wa umma ni Kosa la Jinai! Amefanya UHUNI!

Pili, anaweza kushtakiwa kwa kumshtaki mtu kwa lengo la kumdhulumu, au kumsumbua, ambayo inaitwa Malicious Procecution. Ukitoa taarifa za uongo kwa chombo chochote cha dola, kwa lengo la kumkomoa au kumdhulumu mtu yeyote, basi, unatiwa hatiani, lakini inakuwa ni Kosa la Madai (Civil Suit), hivyo unaweza kudaiwa kulipa fidia kubwa ili kumfidia yule ambaye atakuwa amedhurika na mashtaka yako hayo ya uongo.

Wenje alipotezewa muda mwingi wa kufanya kampeni, kwa madai ambayo ni ya uongo, anayo haki ya kwenda mahakamani.

Ni hayo tu!

-> Mwana wa Haki
 
Back
Top Bottom