Masaki flats bounce back

taffu69

JF-Expert Member
Feb 26, 2007
2,094
538
Naamini lile sakata la kuvunjwa kwa majengo ya Empire Properties Ltd (Masaki) litakuwa na impact mbaya kwa Serikali siku za usoni.

Niwakumbushe habari hizi:


Samani zavunjwa vunjwa ghorofa za Kinondoni

Sakata la maghorofa mawili ya Kinondoni bado linaendelea, ambapo sasa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni imesisitiza kuwa itamburuza kortini na kumfungulia mashtaka ya jinai mmiliki wa majengo hayo ya ghorofa nane kila moja.

Pia, Manispaa imesema itamdai fidia ya kubomoa maghorofa hayo mmiliki huyo, ambaye ni kampuni ya Empire Properties Ltd.

Halmashauri hiyo imesisitiza kuwa kampuni hiyo ilipewa kibali cha kujenga jengo moja la ghorofa mbili chenye namba 00000500 na si vinginevyo.

Imesema kibali namba 00000600 ambacho mmiliki huyo anadai kupewa na Manispaa hiyo kwa ajili ya kujenga majengo mawili yenye ghorofa nane kila moja cha Agosti mwaka 2004 ni cha kughushi na kwamba hatua za kisheria zinachukuliwa dhidi ya wote waliohusika.

Katika taarifa yake jana, Meya wa Manispaa,Bw. Salum Londa, alisema kampuni hiyo iliomba kujenga jengo moja la ghorofa mbili na ilipewa kibali cha aina hiyo.

'Baada ya kupitia michoro iliyowasilishwa na kuzingatia matumizi ya mipango miji, tuliidhinisha michoro hiyo na kutoa kibali cha kujenga ghorofa mbili kama alivyoomba, ' ilisema taarifa hiyo.

Ilisema iliomba kibali cha ujenzi katika kiwanja namba 383 kilichopo katika mitaa ya Toure na Mwaya huko Masaki, ikikusudia kujenga jengo moja lenye ghorofa mbili.

Licha ya kupewa kibali cha kujenga jengo moja la ghorofa mbili, kampuni hiyo ilijenga majengo mawili yenye ghorofa nane kila moja bila kibali chochote.

Hata ukuta unaozunguka majengo hayo ulijengwa bila kibali.

Taarifa hiyo ilisema mwezi Machi mwaka huu, Manispaa ilimpa ilani abomoe majengo hayo, ambayo aliyajenga bila kibali.

Baada ya pingamizi la mmiliki wa majengo hayo kutupwa na mahakama, Manispaa imeamua kuchukua hatua ya kubomoa majengo hayo.

Kanuni za ujenzi mijini zilizotungwa chini ya Sheria ya Miji, inazipa mamlaka za miji uwezo wa kusimamia na kudhibiti ujenzi katika eneo lake, ikiwa ni pamoja na kuhakikisha ujenzi wa jengo lolote unazingatia sheria na taratibu zilizowekwa.

'Napenda niwahakikishie wananchi kwamba hatua za ubomoaji zilizochukuliwa, zimefanywa kwa mujibu wa sheria, kanuni na taratibu za nchi.

Vile vile napenda kuwaasa wananchi kuwa wanapaswa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu zilizowekwa kuhusu ujenzi mijini ili wasije wakapata hasara pale sheria itakapochukua mkondo wake, ' alisema Meya Londa katika taarifa hiyo.

Mahakama ya Wilaya ya Kinondoni hivi karibuni iliamuru majengo hayo yaliyopo makutano ya Barabara ya Toure Drive na Mwaya, yabomolewe. Shughuli za ubomoaji majengo hayo zinaendelea.

Majengo hayo yanaweza kubomolewa wakati wowote kuanzia sasa na maandalizi yanazidi kupamba moto.

Nipashe ilishuhudia maofisa kutoka wizara mbalimbali wakiyakagua majengo hayo jana mchana.

Askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU), askari wa kawaida na mgambo wa Jiji, wameweka kambi eneo hilo.

Wachina ndio wamepewa kandarasi ya kubomoa majengo hayo na wamekiri kuwa kzi hiyo ni ngumu kuliko walivyotarajia.

Mmoja wao, ambaye hata hivyo jina lake halikupatikana mara moja, alisikika akisema kuwa watalazimika kuajiri vijana wa mtaani kwa ajili ya kurahisisha zoezi hilo.

'Hapa lazima tuwachukua vijana wa mitaani waje kutusaidia. Kazi hii ni nzito tofauti na tulivyotarajia, ' alisema

Tayari samani mbalimbali zilizokwishawekwa katika majengo hayo zimevunjwavunja na kutupwa chini ya maghorofa hayo.


SOURCE: Nipashe 05/21/2006
 
Najua wengi mmeshasahau na labda hata wengine hawajui kiliwahi kutokea. Baada ya jengo la Chang'ombe Village kuporomoka na kuua kulifuatia soul searching na kuanza kubomolewa kwa majengo mbalimbali mengine yakidaiwa yalikuwa yanajengwa kinyume cha sheria na bila ya vibali husika. Mojawapo ni jengo lililokuwa pale Masaki (kona ya Mwaya na Toure)..

Sasa habari ambazo zimeanza kutiririka siku hizi chache ni kuwa wamiliki wa jengo hilo wameshinda kesi?? na Manispaa ya Kinondoni itajikuta inawalipa fidia.
 
Mkuu, ubomoaji wa jengo lile ulinitia huzuni sana. Visingizio vilivyotumiwa na manispa vilikuwa hafifu sana, na vilidhihirisha wazi kabisa kuwa maamuzi yalifanywa kwa kukomoa na/au kudhulumiana tu.

Moja ya sababu zilizotolewa na Manispa ya Kinondoni kuhusu kubomoa jengo lile ni kwa kuwa mwenye jengo alijenga kinyume na kibali cha ujezi alichokuwa nacho (Building Permit). Hata alipothibitisha kuwa alikuwa na kibali sahihi, viongozi hao walikipinga na kumchukulia hatua afisa wa manispa aliekitoa.

Vile vile walisema amejenga majengo mawili badala ya moja, na pia urefu wa majengo yale haukuwa umehidhinishwa na mamlaka husika. Vyote hivyo vilithibitishwa na mwekezaji kuwa si sahihi.

Wakabomoa na mali nyingi ziliibiwa katika zoezi hilo. Kwa maana, walisubiri hadi jengo limekwisha kabisa, furniture zimewekwa na matangazo ya upangaji yameanza kufanywa ndipo walipoingia na kutekeleza uharibifu huo mkubwa. Ni aibu sana kwa mamlaka za nchi kuwa na maamuzi ya kiuonevu kiasi hicho.

Kwa mtazamo wangu, nilidhani manispa ya Kinondoni ingefanya yafuatayo;

1. Wangemzuia kujenga kabla hajafika katika hatua za mwisho,

2. Wangempiga fine kubwa kama kweli alikuwa amekiuka matakwa ya hati yake ya ruhusa ya kujenga (building permit). Na hata wangetaifisha kama sheria zinaruhusu,

3. Mamlaka ilitakiwa kujua kuwa kubomoa jengo lile ni hasara kubwa kwa mwekezaji na kwa Taifa. Pesa nyingi za kigeni zimetumika katika kununua samani zilizokuwa ndani ya jengo lile na kuharibiwa. Pesa nyingi zaidi zimetumika katika ujenzi.

4. Mamlaka ilitakiwa kujua kuwa, ajira nyingi ambazo zingepatikana kutokana na biashara/uwekezaji ule zilipotea na serikali ilipoteza nafasi ya kupata kodi kutokana na mapato ya uwekezaji ule.

5. Mamlaka ilitakiwa kujua kuwa, kwa kubomoa jengo lile imeharibu mazingira na uzuri wa mandhari ambapo jengo lipo.

6. Mamlaka ilitakiwa kujua kuwa, kwa kubomoa jengo lile ilishusha matumaini ya mwekezaji kuendelea kuwekeza nchini mwake, na kuwafanya wengine waliojua kuhusu utekelezaji huo kusita kuwekeza.

Sasa angalia hasara nyingine ambayo serikali itapata kutokana na maamuzi mabovu.
 
LIPO JAMBO MOJA LA KUJIFUNZA BAADA YA KADHIA HIYO.

jiji limekua na tabia ya kuwavunjia wakazi wake majengo siku ya Ijumaa jioni, hii inazuia wamiliki husika kwenda mahakamani kuweka zuio la mahakama, wamefanya hivi miaka mitatu nyuma kwenye airport Night club, wakafanya hivyo kwenye ile club ya usiku pale Kamanyora Sinza JIRANI NA HOTEL 92, na wamefanya hivyo pia Kipawa.

maeneo hayo yote watu wamepata hasara nyingi, wamekua wakikwepa mfumo halali wa kisheria.
hapo mbali, najua hata yale makaburi ya pale ILALA jirani na Karume stadium yatang'olewa Ijumaa jioni kuamkia Jumamosi.

sasa wajifunze kuwa wastaarabu na kuheshimu haki za Wenzao.
 
JF is biased.. Dont believe me?

Well I hear ni la lile Jitu Patel.. still feel sorry for him? lol DDnt think so. Kilichofanyika ni kinyume na sheria.. Lakini Jitu inasemekana alimnunua hadi Magufuli akawa anamtetea in cabinet..lakini Lowassa was pissed..lol. Eti alidai yeye anaweza kujenga ata baharini na serikali haiwezi sema chochote. Lakini manispaa ilifanya uharibiufu mkubwa sana pale, waliiba ma microwave na ma A/C lorry zima and many other appliances. Ile ilikua ni majungu japokuwa majungu yenyewe yalikua kadi ya fisadi wa EPA na fisadi mwenza wa Richmond, kuuza kipande cha ikulu arusha, etc.. and the wheels on the..... go round and round..Brap!
 
Masahihisho;
Maghorofa yale mawili ya Masaki yalivunjwa hata kabla ya jengo ya Chang'ombe Village kuanguka. Amri ya kuyavunja majengo yale haikutokana na kuanguka kwa jengo la Chang'ombe Village.

Kilichopelekea kuvujwa kwa majengo yake ni mmiliki wake kukiuka masharti yaliyokuwemo kwenye hati ya ujenzi (building permit). Yeye aliomba kujenga majengo mawiliya ghorofa tatu, lakini baadaye akabadilisha kujenga majengo mawili yenye ghoroga nane!
 
Inasikitisha jinsi ile sentence ya "two wrongs wont make it right" inavyothibitishwa kwa vitendo kutokana na watu waliokosa uangalifu kwenye baadhi ya maamuzi...

Ni bora serikali ingezichukua na kuwapa senior staffs wakati saga linaendelea, sasa tumepata hasara kubwa kwani serikali itakalimika kulipia hadi furniture za lile jengo
 
Nilijua watashinda kwasababu lowassa alikuwa ametoa maigizo hayo ili amuharibu mmiliki kibiashara, kwakuwa majengo yale yako karibu na apartment za lowassa masaki..na alikuwa ametangaza competitive price..
 
najua wengi mmeshasahau na labda hata wengine hawajui kiliwahi kutokea. Baada ya jengo la chang'ombe village kuporomoka na kuua kulifuatia soul searching na kuanza kubomolewa kwa majengo mbalimbali mengine yakidaiwa yalikuwa yanajengwa kinyume cha sheria na bila ya vibali husika. Mojawapo ni jengo lililokuwa pale masaki (kona ya mwaya na toure)..

Sasa habari ambazo zimeanza kutiririka siku hizi chache ni kuwa wamiliki wa jengo hilo wameshinda kesi?? Na manispaa ya kinondoni itajikuta inawalipa fidia. More info to come.. (i'm going to sleep!)
yule jamaa alionyesha vibali vyote then kinondoni wakasema siyo vyakwao na wakaendelea na kubomoa. Sasa kama ameshinda wale waliokataa vibali wako wapi? Inatakiwa wawajibishwe kwa kuleta hasara na pia kutosimamia kazi yao vizuri.
 
yule jamaa alionyesha vibali vyote then kinondoni wakasema siyo vyakwao na wakaendelea na kubomoa. Sasa kama ameshinda wale waliokataa vibali wako wapi? Inatakiwa wawajibishwe kwa kuleta hasara na pia kutosimamia kazi yao vizuri.
Kama ni kuwajibishwa ujue ni kunyang'anywa madaraka au kuhamishwa kituo cha kazi basi. Hatimae kodi za walalahoi ndizo zilipie fidia hiyo badala ya kupewa huduma muhimu za kijamii. Ndio maana naiota sana China na sheria zake.
 
Jaribu kukumbuka kauli ya Lowassa ya kumtimua kazi yule Msanifu wa majengo wa wilaya ya Temeke na hivyo tu ulikuwa ni sifa za Nguvu mpya na Ari mpya ambayo leo ni kitendawili tu na misamiati
 
kila jambo nnchi hii linalofanywa na sekta ya UMMA lina mapungufu, swali Je kufanya kazi serikalini kunapunguza uwezo wa kufikiri ama serikali inawaajili wafanyakazi vimeo, walioiba mitihani ? nini tafsiri ya failures hizi ndani ya serikali yetu.?
 
Kama ni kuwajibishwa ujue ni kunyang'anywa madaraka au kuhamishwa kituo cha kazi basi. Hatimae kodi za walalahoi ndizo zilipie fidia hiyo badala ya kupewa huduma muhimu za kijamii. Ndio maana naiota sana China na sheria zake.


Hapo umenena mkuu, nami nakuunga mkono. Ingawa china kila kitu feki lakini si SHERIA, SILAHA na SUMU - UKIVIDHARAU HIVYO UTAONDOKA.

..............................................
Amani yetu inatumiwa vibaya
 
Nilijua watashinda kwasababu lowassa alikuwa ametoa maigizo hayo ili amuharibu mmiliki kibiashara, kwakuwa majengo yale yako karibu na apartment za lowassa masaki..na alikuwa ametangaza competitive price..

Nyuma ya majengo yale kuna ofisi za ubalozi wa Afrika Kusini, ambazo ziko katika nyumba ya Lowassa.

Kuna baadhi walikuwa wakisema kuwa, sababu za kuyabomoa majengo yale ni kwakuwa yalikuwa yanazuia upepo mwanana uliokuwa ukifika kwenye nyumba hizo za Waziri Mkuu wa zamani. Na hiyo ndio ikawa hasira ya kiongozi huyo iliyosababisha kuamuru kuvunjwa kwa majengo yale.
 
Mwanakijiji nawe umezidi sana kuwafuatilia waislamu. Unataka Lowasa abadili dini awe mkristo ndiyo umpe pumzi?
 
Kichekesho kikubwa ni kwamba jirani yake tu limejengwa jengo jingine kubwa na refu kuliko hilo lililodaiwa kuwa refu na kujengwa kinyume cha sheria ya ujenzi ktk eneo hilo!
 
Hapa nachapa bia bardiiii na aliyekuwa victim wa lowasa jengo la changombe. Kashinda na bia zinashuka tu kama kawa.
Mwenye jengo la masaki ilikuwa wazi lazima ashinde. Mtuhumiwa pekee aliykuwa a.ebaki naye ambaye alikuwa ni mwajiri wa manispaa ameshashatangulia mbele ya haki RIP dadangu mpendwa.
 
Kichekesho kikubwa ni kwamba jirani yake tu limejengwa jengo jingine kubwa na refu kuliko hilo lililodaiwa kuwa refu na kujengwa kinyume cha sheria ya ujenzi ktk eneo hilo!

Wako wapi wanaotetea haki za kutopitishwa umeme? Maamuzi mabovu na yenye ubabaishaji ni jambo linalowa-affect watz sio kikundi cha watu, wakwapi tuwaone wamepiga kambi nje ya mlango wa meya wakitaka maamuzi yenye akili?

Offf point lakini. Najua kuna watu watshambulia humu.
 
Back
Top Bottom