BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,769
- 288,283
Hapana sikuwa na specific jimbo Mkuu.
Nilikuwa nadahani unamaanisha jimbo la baba yake, kule Rorya!
Nilikuwa nadahani unamaanisha jimbo la baba yake, kule Rorya!
Maria Sarungi ni binti wa Mzee Profesa Philemon Sarungi aliyewahi kuwa mkurugenzi wa kitivo cha afya cha Muhimbili na baadaye kushika nyadhifa kadhaa serikalini kabla ya kusitaafu.
Mwanamama huyu ameolewa na mwanamme mwenye asili ya Ethiopia akiwa na maskani yake Dar es Salaama ambako ana biashara zake binafsi kadhaa, mojawapo ikiwa ya kutafuta warembo wa kushiriki mshindano ya Miss World ya Donald Trump. Mmoja wa warembo waliopitia katika mikono ya Maria Sarungi ni mrembo Flaviana Matata ambaye sasa hivi anang'aa sana kwenye anga za urembo huko New York Marekani.
Ingawa sijui undani wake binafsi, najua kuwa Maria Sarungi siyo mwanasiasa, bali aliteuliwa na Rais kuingia kwenye bunge la katiba ambalo limemaliza muda wake. Mchango wake kwenye bunge hilo la katiba uko wazi.
Kwa kipindi cha zaidi ya mwezi mmoja sasa, nimekuwa nafuatlia tweets zake, na kugundua kuwa ni mwanamama mwenye msimamo thabiti ambaye hajawa corrupted na party politics za vyama. Anachukua mazuri kutoka vyama vyote na kupinga mabovu ya vyama vyote.
Ingawa hatujaruhusu kuwa na independent candidates kwenye nchi hii, mtu wa aina hiyo ndiye nilikuwa ninataka ashike uskani wa kuingoza nchi hii.
Party politics zimechangia sana kuharibu nchi yetu na tunatakiwa kuachana nazo kuanzia sasa.
Maria Sarungi si mwanasiasa bali ni mwanaharakati, ni bora abaki huko huko ndiko ataweza. Uanasisa uwe mnafiki kidogo, na huyu dada hayuko hivyo.Kuongoza nchi kwa sababu umemfuatilia tweeter!!!!????
Seriously ndio urais umekuwa hivi sasa???!!!
Asee. .,. . . . . . !!!!!
Kwa mujibu wa Katiba na sheria za nchi hii, hairuhusu mbombea asiye na chama. LAZIMA awe mwananchama wa chama cha siasa.
Surprise... Surprise... Surprise, Team Lowassa and Team Mbowe zimeungana kumshambulia mwanamama Maria Sarungi
Mama tibaijuka usingeelewa uchovu wake kama sio escrow.nilikuwa nabisha lakini mwanamke bado kidogo.Hawa viumbe utawajua wakiwa kwenye pressure ndio udhaifu wao utauona.Katiba mpya mnayoitaja inazungumza habari ya sifa za mgombea uraisi .Awe na uzoefu wa uongozi katika ngazi ya taifa.Sasa hapa mtasema alikuwa mtafuta warembo ngazi ya taifa au.Mnamkumbuka bibi Q Aquino?alisikia wanajeshi wame mutiny akajificha uvunguni.Haa unaongoza majeshi,unakabiliana na kina kenyata ,kagame,museveni.wakristo.waislamu,wauza madawa,wabunge,wana jf wana fb.hebu muulizeni Banda.Hawa wakipatiwa niniiiii ubongo unavurugwa.
huyu mdada namfahamu sana hana dharau wala kiburi nachati naye sana twita yupo tofauti na wanawake wengine ana msimamo sana kwenye hii ishu ya escrow amenihahidi wahusika wote wataghulikiwa hakuna funika kombe mwanaharamu apite document wanazo za kutosha.
huyu mdada namfahamu sana hana dharau wala kiburi nachati naye sana twita yupo tofauti na wanawake wengine ana msimamo sana kwenye hii ishu ya escrow amenihahidi wahusika wote wataghulikiwa hakuna funika kombe mwanaharamu apite document wanazo za kutosha.
Hivi kabla ya kuingia kwenye bunge la katiba aliwahi kuongelea kugombea Urais? Kama hapana ni kipi kimemvutia kwa sasa? Kama kweli ni mzalendo kwa nini hakujiuzuru kwenye bunge la katiba. Huyu anafaa kuendelea na shughuli zake za kutafuta )warembo na nyinginezo lakini sio kuongoza nchi hii hata kama imekuwa na mazuzu kiasi gani.
Wanawake wengi mwaka 2005 walimchagua JK kwa sababu kubwa kuwa ni handsome, sasa na nyie mmeshindwa kusema kuwa kawavutia kwa mambo mengine na kusema kuwa anafaa sana.
Lakini je unawajua wanawake kama vile akina Golda Meir, Margaret Thatcher, Angela Merkel, Dilma Rousseff na wengineo walioongoza nchi zao kwa msfainikio makubwa? Tofautisha kuongoza nchi na kuendesha siasa.
Angalia hali ilivyo mbaya Liberia.Angalia age ya hao kina mama ,angalia historia zao,jilize huyo merkel marekani ilichokua inamfanyia. ndugu yangu nchi sio NGO ama SACCOS umpe mdada,Ni ajabu vijana wa kisasa mnaraisisha sana mambo mnauona uraisi juujuu.Hapo unadili na Maalim Seif na wasioutaka muungano kuna issue nyingi.Mtu hupata power kutokana na alichonacho hasa knoledge na experience.Sasa kama walio wengi watakuzidi katika haya age,knowledge and experience unajikuta una authority ila huna power. Hakuna uongozi wa nchi ambao sio siasa hiyo ndio siasa hasa .it means who gets what?when and why?Hawa wadada bado damu moto nchi inaweza pata kashfa ukasikia au ukamuona ananiniliwa si mchezo.Hebu jiulize Migiro kimya.hebu jiulize watanzania wako tayari au mnafikiri ni kitchen party mnaandaa
Ndugu yangu Jokakuu,..katiba mpya si inapendekeza kila jimbo liwe na mbunge mwanaume na mwanamke??
Ninaelewa uwoga wako, lakini nadhani ni kwa sababu ya kuwa na mtazamo mfupi wa future yetu kwa vile unaingalia kwa kutumia kurunzi tunayotaka kuzima, yaani ya vyama vya siasa. Nimemtaja mama huyu kutokana na kukukubalika katika anga zote za kisiasa kwetu, yaani hajaonyesha kusapoti chama kimoja tu.