Marekani kuitikisa Tanzania kwa vikwazo

Marekani kuitikisa Tanzania kwa vikwazo

Ngoja vikwazo vije tu ili tupate akili. Mie sioni kwa nini CCM baada ya kushindwa uchaguzi Zanzibar hawataki kuachia madaraka? Waache watu wa nje wajekutufundisha demokrasia kaana inaonekana ni somo gumu kwetu kulielewa.
 
Wao wanataka nn suruhu gani? Kama Mwenyekiti wa Tume ya uchaguzi Zanzibar hakumtangaza mshindi basi hapo hakukuwa na.kilichofanyika kikakiukwa hivyo lazima.uchaguzi ufanyike tena then amtangaze atakaeshinda na ndio maana tarehe 20 wanapiga kura, ndio suruhishi hili uchaguzi kurudiwa tena la sivyo waendelee kubaki na.misaada yao.
 
haya maamuzi myatoe kabla haijatokea sintofahamu ya sanctions.
Nchi imemshinda Pombe asubuhi sana.
Yaani hata miezi mitatu bado,hujafanya hata ziara moja nje, hujakutana hata na kiongozi yeyote kufahamiana, bunge lako la kwanza halijamaliza hata wiki mbili majadiliano na tayari watu wanafikiria kukuwekea vikwazo vya kiuchumi (ambayo ni adhabu maximum kwa nchi) ni gundu la aina gani hilo?
Sijapata kuona rais Afrika toka nikue aliyechaguliwa kwa kura akikumbana na dhahma kama hizi so early namna hii
 
Enyi kizazi cha nyoka, mnaopenda misaada na hisani za wafadhili yawapasa mbadilike.

Kama taifa, tusiruhusu kuvurugwa na watu kutoka nje.
Wanaotaka misaada ni hawa viongozi na hiyo misaada ni ya matumbo yao.
Ni misaada michache sana inayowafikia wananchi.

Na kinachowafanya watake misaada ni akili za hawa viongozi kuwa dormant hawataki kufanya kazi zaidi ya kuiba, kula, kucheza na ufuska.
 
nitaona ajabu nchi kama marekani kutokufuata katiba kanuni sheria za nchi husika
Endelea kushangaa kwa sababu hata Katiba ya Nchi yako yenyewe huielewi wala Sheria nazo huzielewi. Naamini Kabisa kuwa Sheria za Kimataifa ndo huzijui kabisaa! Sasa endelea hivyohivyo, namba itakapoanzwa kusomwa sitashangaa kukukosa jf kwa kukosa bundle!
 
Hao Jamaa ni Tai wanawinda mzoga... I wish Magufuli atende haki kwa Seif halafu akaze kwa kureview mikataba ya madini na Gas ...
 
nitaona ajabu nchi kama marekani kutokufuata katiba kanuni sheria za nchi husika

Wakiweka vikwazo na sisi itabidi tukakamae nao uwekezaji wao nchini kwetu .Ni heri tuwape wachina kuliko kuwapa wanaotusumbua na ujinga wa vikwazo mara sijui hamruhusu mashoga mtatukoma ujinga mtupu kila kona.Tuachane nao biashara iishie hapo.Kila mtu aende akaendeshe siasa kwake
 
I wish Magufuli atende haki kwa Seif halafu akaze kwa kureview mikataba ya madini na Gas ...

Uchaguzi wa Zanzibar si swala la muungano halimhusu Magufuli.Hao vibaraka wa wazungu wa UKAWA na wazungu wao inabidi hilo walijue
 
Pigwa economic sunction ndani ya 20 lazima unyooke.
Kina magu na team yake ya kina nkapa na msoga airline hawana cha kupoteza coz wamejihifadhia hazina yao ya kutumia hapa duniani.

Mungu amewakunia


Sanctions ni mbaya sana, pamoja na nguvu zote za Iran, Iraq, Libya nk hawa jamaa wakiamua kukupiga pini lazima kama TAIFA lipate cha moto. Na walivyo wabaya huwaambia na washirika wao. Hivyo tusiombee jambo hilo litokee nchini.
 
Wakiweka vikwazo na sisi itabidi tukakamae nao uwekezaji wao nchini kwetu .Ni heri tuwape wachina kuliko kuwapa wanaotusumbua na ujinga wa vikwazo mara sijui hamruhusu mashoga mtatukoma ujinga mtupu kila kona.Tuachane nao biashara iishie hapo.Kila mtu aende akaendeshe siasa kwake
Ndio utakapo jua ujinga wa viongozi wenu wa ccm. Vikwazo vya nchi na mikataba ya kibiashara ni vitu viwili tofauti. Wakati mnakubali kuweka mikataba ya miaka 100 na kuambiwa msifanye siri mkajiona wajanja.
Sasa msaada ng'oo na mikataba haifi! Ina mnavyotuumiza nunda nyie
 
Sio Iran tu mkuu... Russia yenyewe hali mbaya baada ya kuwekewa vikwazo... watu ni ma'mbumbumbu' sana kubeza hili

Usilinganishe Tanzania na Iran na Russia.Wale uchumi wao wote unategemea mafuta na gesi wanazouza nchi za magharibi.Wakisusa tu kununua uchumi hoi na maisha hoi maana maisha yao yote hutegemea wapate pesa wanunue hadi chakula nje ya nchi.Tanzania tuna nini cha kuuza nchi za magharibi? Kila siku bidhaa zetu twazila wenyewe.Wanatupa visingizio kibao mara ziko viwango vya chini.Sisi wenyewe twala wala hatufi.

Ndio maana hata wakiweka vikwazo vinalenga kwenye luxury goods kama hiyo misaada ya umeme ambao ni kwa ajili ya wale ambao maisha bora kwa kila mtanzania yalishawafikia.
 
Sanctions ni mbaya sana, pamoja na nguvu zote za Iran, Iraq, Libya nk hawa jamaa wakiamua kukupiga pini lazima kama TAIFA lipate cha moto. Na walivyo wabaya huwaambia na washirika wao. Hivyo tusiombee jambo hilo litokee nchini.
Hawa jamaa wanakupa muda tu na wanakuwa wameshakusoma uchumi wako.
Kama sisi Tz ndiyo zero kabisa hatuna tunachozalisha.
Leo wakisema wasituletee mitumba tu, kuna watu watabaki uchi.
Tukiminywa kidogo tu, chali
 
Ndio utakapo jua ujinga wa viongozi wenu wa ccm. Vikwazo vya nchi na mikataba ya kibiashara ni vitu viwili tofauti. Wakati mnakubali kuweka mikataba ya miaka 100 na kuambiwa msifanye siri mkajiona wajanja.
Sasa msaada ng'oo na mikataba haifi! Ina mnavyotuumiza nunda nyie

Mikataba inaweza kufilia mbali asikudanganye mtu.Uchukulie umenunua nyumba kijijini una hati zote.Halafu ukaanza kutukana wanakijiji kuwa uongozi wao haufai halafu kila siku wanakijiji wanakujia na mapanga na marungu kwamba funga virago uondoke.Utaondoka tu

Na ndivyo sultani wa Zanzibar alivyoondoka alikuwa na mikataba yote ya kisheria ya kutawala Zanzibar siku ya siku wakamwibukia alitimka mbio mikataba hata uulize iko wapi hajui.Alivyotembezewa kipigo na mikataba yake

Mkataba ukisaini wa kibiashara unasimamiwa na mahusiano mema.Si kwamba maadamu unao unafikiri waweza tu lindwa na mkataba tu lazima uchunge usijiingize kwenye mambo yanayoweza athiri biashara zako.
 
Hawa jamaa wanakupa muda tu na wanakuwa wameshakusoma uchumi wako.
Kama sisi Tz ndiyo zero kabisa hatuna tunachozalisha.
Leo wakisema wasituletee mitumba tu, kuna watu watabaki uchi.
Tukiminywa kidogo tu, chali
Hiyo mitumba wanagawa bure?
Wewe ndi zero mbeba box!
 
Back
Top Bottom