Marando: Nitatangaza Matokeo kabla ya Kuchakachuliwa

Marando: Nitatangaza Matokeo kabla ya Kuchakachuliwa

MALUNGU

JF-Expert Member
Joined
Jun 2, 2011
Posts
250
Reaction score
97
Wakili Maarufu na shushu aliyebobea tangu enzi za Mwalimu JK Nyerere amesema mwaka huu atajitoa Muhanga kutangaza matokea ya Urais kabla ya matokeo hayo kuchakachuliwa. Hii ni ishara ya wazi kuwa Watanzania mwaka huu hawatakubali kuburuzwa na tume ya watawala.

Chanzo: Gazeti la Tanzania Daima
 
Miaka yote wamekuwa wakiufyata mkia sidhani kama mwaka huu wataweza...

Wapinzani na Watanzania ni waoga watupu...
 
Hongera Marando...Muhimu kwa sasa ni kuhamasisha watu wajiandikishe BVR ili zije zipatikane kura za maana ambazo tuna mandate nazo (tangible votes)...
Otherwise CCM na NEC watakuja na kura zao za mamluki ambazo kimantiki tutashindwa kuzihakiki... Rejea ualiyotokea Kenya..
 
Mungu akubariki kamanda Marando,nasi wapiganaji tupo nawe daima kuhakikisha ushindi unapatikana
 
Hapo ni sababu ya kuwadanganya misukule inatafutwa!

CHADEMA inafahamu haiwezi kushinda uchaguzi wowote ule !

Sasa wanawaandaa misukule wao kisaikolojia!
 
Wakili Maarufu na shushu aliyebobea tangu enzi za Mwalimu JK Nyerere amesema mwaka huu atajitoa Muhanga kutangaza matokea ya Urais kabla ya matokeo hayo kuchakachuliwa. Hii ni ishara ya wazi kuwa Watanzania mwaka huu hawatakubali kuburuzwa na tume ya watawala.

Chanzo: Gazeti la Tanzania Daima

hakika nakuambia Marando akiwa kama mwanasheria anayejua sheria hawezi kufanya hivyo! Hizi ni siasa tu anachagiza
 
Wakili Maarufu na shushu aliyebobea tangu enzi za Mwalimu JK Nyerere amesema mwaka huu atajitoa Muhanga kutangaza matokea ya Urais kabla ya matokeo hayo kuchakachuliwa. Hii ni ishara ya wazi kuwa Watanzania mwaka huu hawatakubali kuburuzwa na tume ya watawala.

Chanzo: Gazeti la Tanzania Daima

Sijawahi kuwa na imani na marando kuwa ni mpinzani wa kweli.
Watu kama hawa inatakiwa umakini mkubwa kuwa nao.
 
Tulisha sema cdm ni wendawazim.sasa malando hicho Alicho sema nini kama sio wendawazim
 
Lazima wa badilike kwani wanao nchi wamebadilika wanafuatilia hatua kwa hatua .ila haya Mambo ya BVR huenda ikawa advantage kwa c.c.em kwani elimu hii wengi hatuja ifahamu, wao wamesha jifunza nakuifahamu Sasa sisi bado.Hivyo ikifika muda muafaka wao ndio wataanza kutufundisha kwa jinsi watakavyo.
 
Aha.. labda ujumbe umeanza kuwafikia. I hope.
Mwaka 1989, upepo wa mageuzi ndio unaanza kuvuma, Nyaucho Mabere Marando alikuwa ni mwana mageuzi wa kwanza kunukuliwa na gazeti akimwambia Baba wa Taifa wa Taifa kwamba kafilisika kisiasa. Hakuishia hapo akaukataa uteuzi wa Raisi Ali Hasan Mwinyi katika Tume aliyounda eti kuwauliza wananchi kama wanapenda mfumo wa vyama vingi. Akimjibu Mwinyi alisema hayuko tayari kutafuna bure hela za umma eti kuwauliza wananchi kama wangependa uhuru zaidi akidai huo ni wizi na ulaghai. Kuna watoto humu hawaijui historia ya Mabere ndio maana wanaropoka hovyo anapotoa matamshi kama hilo alilotoa.
 
Utaingia katika historia ya Taifa hili na tukio hilo litakuwa documented kwa ajili ya vizazi vijavyo.
 
Sijaisoma hiyo sheria, je Tume ya Uchaguzi kabla ya kutangaza hizo takwimu itabidi zihakikiwe na Ofisi ya Takwimu ya Taifa?
 
Hapo ni sababu ya kuwadanganya misukule inatafutwa!

CHADEMA inafahamu haiwezi kushinda uchaguzi wowote ule !

Sasa wanawaandaa misukule wao kisaikolojia!
Sijui utaweka wapi uso wako labda kwenye vyoo vya ccm Wilaya ya Arusha
 
Hapo ni sababu ya kuwadanganya misukule inatafutwa!

CHADEMA inafahamu haiwezi kushinda uchaguzi wowote ule !

Sasa wanawaandaa misukule wao kisaikolojia!

yaani unajitoa akili kwamba, chadema haiwezi kushinda uchaguzi wowote hule umesahau kwamba kuna wabunge na madiwani wa chadema kwa akili yako hawa ni viongozi wa kuteuliwa?
 
Sijaisoma hiyo sheria, je Tume ya Uchaguzi kabla ya kutangaza hizo takwimu itabidi zihakikiwe na Ofisi ya Takwimu ya Taifa?

Kuna masheria mengi kweli hata waliyoyatunga hawayajui...mfano hai sheria ya kura ya maoni na alivyoongea waziri asha migiro na tume ilivyosema na mkutano wa CC ya CCM kuhusu sheria hiyo tunaachwa mdomo wazi
 
Back
Top Bottom