Marando: Nitatangaza Matokeo kabla ya Kuchakachuliwa

Marando: Nitatangaza Matokeo kabla ya Kuchakachuliwa

hakika nakuambia Marando akiwa kama mwanasheria anayejua sheria hawezi kufanya hivyo! Hizi ni siasa tu anachagiza

Mkuu inawezekana sana.Haya matokeo kila Jimbo yanabandikwa mara wanapomaliza kuya hesabu huku Mawakala wa UKAWA/Chama husika wakiwa na nakala za matokeo yenyewe na hayo ndiyo atayatangaza kadri kila jimbo linapobandika na mawakala kuwasilisha ripoti kwa Chama husika.



 
Ameshanusa harufu ya kushindwa kaona bora atafute pakuanzishia fujo.anamawazo ya kijinga unakua na chama kina washauri kama hawa sasa hili si tatizo,huwezi kutegemea mtu msomi kama marando anaongea upuuzi kama huu lakini mtu kama marando anapo jichanganya na watu kama kina mbowe tufikiri ataongea nn zaidi ya haya .kusema atatangaza matokea mapema ni upuuzinkuliko upuuzi wenyewe
 
Naona hamfikirii maneno mnayozungumza mnatumia jazba kumfagilia Lowasa hakubaliki na huyo ndio kaburi la ccm mtaona Oct name wezi wenu mbwembwe za kutia pesa za wtz mlizoiba kusudi mpigie kmpn imekula kwenu
 
Nafikiri ataka kwenda jela,Kwani yeye ni Mwenyekiti wa tume?Hapo ndipo wapinzani wanapopingana na wanamabadiliko.
 
Mwaka 1989, upepo wa mageuzi ndio unaanza kuvuma, Nyaucho Mabere Marando alikuwa ni mwana mageuzi wa kwanza kunukuliwa na gazeti akimwambia Baba wa Taifa wa Taifa kwamba kafilisika kisiasa. Hakuishia hapo akaukataa uteuzi wa Raisi Ali Hasan Mwinyi katika Tume aliyounda eti kuwauliza wananchi kama wanapenda mfumo wa vyama vingi. Akimjibu Mwinyi alisema hayuko tayari kutafuna bure hela za umma eti kuwauliza wananchi kama wangependa uhuru zaidi akidai huo ni wizi na ulaghai. Kuna watoto humu hawaijui historia ya Mabere ndio maana wanaropoka hovyo anapotoa matamshi kama hilo alilotoa.
Marando anajipa majukumu ya Tume ya Uchaguzi nakuhakikishia baada ya uchaguzi atatangaza kuwa Usalama wa Taifa wameiba kura za Ukawa.
 
hakika nakuambia Marando akiwa kama mwanasheria anayejua sheria hawezi kufanya hivyo! Hizi ni siasa tu anachagiza

Marando amekuwa mtu pekee wa kuita Press na kusema JK anahusika na wizi ndani ya ESCROW bro na hajaitwa hata polisi nalo utasema was siasa na alisema kama wanabisha wakutane mahakamani . Unakumbuka au akasema wakitaa wamkamate waungurume kwa court .
 
Alitumika kummaliza Mrema.

mkuu, tuache upotoshaji kuhusu kiini macho cha eti Lyatonga yuko upinzani.

huyu mtu hakuwahi kuwa kwenye upinzani hata siku moja. hakuwahi kuondoka CCM na hadi leo hii yupo huko.
 
Wakili Maarufu na shushu aliyebobea tangu enzi za Mwalimu JK Nyerere amesema mwaka huu atajitoa Muhanga kutangaza matokea ya Urais kabla ya matokeo hayo kuchakachuliwa. Hii ni ishara ya wazi kuwa Watanzania mwaka huu hawatakubali kuburuzwa na tume ya watawala.

Chanzo: Gazeti la Tanzania Daima

Huyu ni kichaa kabisa hajui hana mamlaka ya kutangaza matokeo? Huku ni kujifurahisha tuu na kuwafurahisha chadema...akifanya hivyo atakuwa ametenda kosa na jinai na atachukuliwa hatua.

Nchi hii imejaza vichaa sana...
 
Huyu ni kichaa kabisa hajui hana mamlaka ya kutangaza matokeo? Huku ni kujifurahisha tuu na kuwafurahisha chadema...akifanya hivyo atakuwa ametenda kosa na jinai na atachukuliwa hatua.

Nchi hii imejaza vichaa sana...


Unatia kinyaa.....
 
Miaka yote wamekuwa wakiufyata mkia sidhani kama mwaka huu wataweza...

Wapinzani na Watanzania ni waoga watupu...

Mkuu umefikiri sivyo,wamebadilika huoni Redbridge?wamepiga kelele lakini jamaa wamekaza!mwaka huu kazi ipo,na usisahau huyu jamaa anatokea kuleee!!vita ni vita muraaa hata ikiwa ya manati!
 
Hapo ni sababu ya kuwadanganya misukule inatafutwa!

CHADEMA inafahamu haiwezi kushinda uchaguzi wowote ule !

Sasa wanawaandaa misukule wao kisaikolojia!

mwenyekiti ccm amesema ccm mjiandae kisaikolojia.Kama fisadi Lowasa akipitichwa chama cha majambazi ndio mwisho wenu
 
Big Up Marando! You are a rare gem in this nation! We believe you can!!!!!!!
 
Huyu ni kichaa kabisa hajui hana mamlaka ya kutangaza matokeo? Huku ni kujifurahisha tuu na kuwafurahisha chadema...akifanya hivyo atakuwa ametenda kosa na jinai na atachukuliwa hatua.

Nchi hii imejaza vichaa sana...


Kama kutoa matangazo ya matokeo ni siri inakuwaje mawakala wa vyama wanapewa nakala za matokeo? Mwaka huu mtazisoma namba kama katika chaguzi ndogo ambako matokeo hupatikana kabla ya hiyo inayoitwa tume kutangaza.
Halafu kumbuka Wakili Marando amesema atajitoa MHANGA hivyo elewa maana ya mhanga.
 
Back
Top Bottom