Hakuna vita kati ya Zitto na Chadema bali ni mkakati wa mafisadi kumuondoa kwenye Agenda ya Mabilioni ya Uswis...
Watanzania wanaimani kubwa na uwezo wa Zitto kabwe katika kuisimamia serikali,ni aina ya wanasiasa ambao ni rasilimali kwa maendeleo ya nchi, hoja zake nyingi za kitaifa zimelineemesha taifa kwa ujumla bila kubagua,mfano ni haya machache.
1.Kuibua hoja ya buzwagi ,hoja ambayo ilimfanya kufuatiliwa kwa karibu na wapenda haki,mwisho wa hoja hii ni sheria ya madini ya 2010,leo walau tunanufaika na madini kuliko kabla ya sheria iliyoasisiwa na Zitto haihatungwa na kutumika.
2.Hoja ya uwajibikaji mbovu serikali na kumtaka Rais awafukuze kazi mawaziri wazembe au waziri mkuu ajiudhuru,ili hoja yake kuwa na nguvu Zitto alikusanya sahihi 72 toka vyama vyote bungeni.
3.Hoja ya kutoza kodi makampuni yanapouziana hisa,wengi hawakuwa wanalijua hili na jinsi ncgi za wenzetu zinavyolifanya, lkn baada ya kuwasilisha kitaaluma na kwa weledi,bunge lilimuunga mkono na hatimae ikatungwa sheria ambayo ndani ya mwaka mmoja tu Tanzania imepata kiasi cha Bil 400 kupitia wizara ya nishati na madini.
4.Hoja ya mabillioni ya uswis,hii ndio hoja nzitto iliyowahi kujengwa na Zitto katika maisha yake ya kisiasa,ni hoja inayowagusa wskubwa wengi ktk nchi hii,ni hoja inayowagusa watawala ,wafanya biashara na hata viongozi wenzake wa upinzani,ktk hoja hii unaweza usielewe kinachoendelea lkn ukweli ni kuwa walioficha pesa walipata homa kali baada ya hoja ya Uswis kutua bungeni,haiingii skilini eti hakuna mtanzania mwenye pesa haramu nje ya nchi,ilikuwa ni kupoteza maboya ili kutafuta jinsi ya kumuondoa Zitto kwenye agenda,wameungana na wanachadema kummaliza Kisiada ili wabaki salama na utajiri wao,hapa ndio panapokatisha tamaa kwa wale ambao tunaamini katika siada za iwajibikaji na siasa zenye maslahi kwa taifa. Mafisadi wameweza kuwanunua viongozi wa chadema ili wawasaide kuwanusuru na Zitto kabwe. hao ndio wsmefadhili mikutano ya chadema kwa kuwakodishia helkopta za kuzunguka nchi nzima kwa kutimiza malengo yao,kiukweli kwa jicho la kawaida unawrza kuona kama ni vita kati ya Zitto na chadema lkn kwa jicho la tatu. atagndua,kuna mkono wa mafisadi .
Zitto ataibuka mshindi katika hili kwa kuwa damu na jasho la watanzania vipo nyuma yake kumuunga mkono kwa kujitolea kuwa sauti ya wanyonge waliokata tamaa,Mtaalamu sigmund freud amewahi kusema kuwa mtu anapofanya makosa hudanya "Projection ego deffensive mechanism" kuwa huuficha udhaifu wake kwa kumvisha makosa yake mtumtu mwingine.hivyo ni wakati wa wanyonge kuungana na kufanya mapambano dhidi wa wakandamizaji .
Kama Mafisadi wameungana kumshambulia kiongozi wa wanyonge hatupaswi kupigwa na butwaa huku tukiwaangalia,ni lazima tuwapinge na kuwakataa,
5.Aliyoyafanya Chief mangusutsi Buthelezi dhidi ya Mandela. nayaona yakirudiwa na mbowe dhidi ya Zitto Kabwe.
yaliyofanywa na Mangope wa S.A dhidi ya Oliver Tambo nayaona yakirudiwa ma Slaa dhidi ya Zitto Kabwe.
Buthelezi na mangope walikuwa weusi waliotumiwa na wazungu kumpinga mamdela na chama chake cha ANC mangope na Buthelezi waliwaua wafuasi wa ANC na kuwaaminisha wenzao kuwa Mandela ni kibaraka wa wazungu wakati kiukweli ni wao ndio waliokuwa ---------- na wazungu kuchelewesha ukombozi.
Pamoja na hila zao,lkn hawakufanikwa ,mnamo 1994 mandela alishinda uchaguzi na kumteua Chief Buthelezi kuwa waziri wa mambo ya ndani.
Hivyo naamini hata Zitto atashinda na hao wanaotumiwa na mafisadi kumuondoa kwenye agenda wataaibika lkn atawasamehe.
Steven Bicco aliwahi kusema enzi za uhai wake kuwa;
"THE GREAT WEAPON OF OPPRESSOR IS THE MIND OF OPPRESSED" tuungane kupinga dhulma na agenda ya uswis wasiizime kwa mbinu nyepesi kama hizi"tumeshtuka"