Mapokezi ya CHADEMA Kigoma Yamshangaza Lema

Mapokezi ya CHADEMA Kigoma Yamshangaza Lema

sawa kamanda nakiri ni kuyumba kwa chadema kigoma.....sasa ili kutenda haki, kwa heshima na taadhima tuwekee takwimu za jimbo la hai kwa mbowe (KUB).
tuambia ni madiwani wa chama gani ni wengi na kwa nn?!

Sina , kama unayo iweke hapa...... nijuavyo jimbo lilikuwa Chini ya ccm na 2010 likatwaliwa na chadema.
 
Alikuwa TLP kwa Mrema. Ila anaijua CHADEMA kuliko aliowakuta, Thats why i hate working with Less educated People! They Tend to Know Everthing while they know nothing..Poor LEMA.

poor mwenyewe!Nne bila za LEMA unazikumbuka.linganisha na kata nane alizouza Zitto Kigoma.Lema kapoteza vingapi akipigania cdm.Zitto kavuna matrilioni kwa mgongo wa cdm.Mabomu tupigwe sie,uenyekiti apewe yeye.No
 
Hivi mwaka 2000 na mwaka 2005 Huyu ndugu Godbless J Lema. alikuwa yuko chama gani???
'''Alisema mwaka 2000 walikuwapo madiwani 11 katika jimbo la Zitto la Kigoma Kaskazini, lakini mwaka 2005 alipogombea walipungua na kubakia sita(6) na kwamba mwaka 2010 walipungua zaidi na kubakia wawili(2
Hilo si swali! Tembea na hoja hii!
 
Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema, alisema kuwa juzi walipata mapokezi makubwa mjini Kigoma na kwamba kila mtu akiwa katika chama afanye kazi ya kukijenga badala ya kukibomoa.

Alisema licha ya kuwapo na madai kuwa aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu, Zitto Kabwe, ana umaarufu mkubwa mkoani humo, jambo hilo halina ukweli.

Alidai mwaka 2010 walitegemea kupata ushindi katika Jimbo la Mpanda, lakini Zitto aliandika barua akieleza kuwa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, awe mgombea pekee.

Alisema baada ya chama kupata taaarifa na kutaka kumwajibisha Zitto, Mwenyekiti Mbowe, aliingilia kati na kusitisha uamuzi huo.

Alisema kutokana na waraka walioukamata aliodai uliokuwa na malengo ya kukisambaratisha chama, waliona hawana sababu za kuendelea na Zitto na kumvua nyadhifa zake na kwamba kitendo cha kuweka pingamizi mahakamani asijadiliwe kinamfanya awe mbunge wa Mahakama.

Alisema mwaka 2000 walikuwapo madiwani 11 katika jimbo la Zitto la Kigoma Kaskazini, lakini mwaka 2005 alipogombea walipungua na kubakia sita na kwamba mwaka 2010 walipungua zaidi na kubakia wawili, hivyo hakuna ukweli kuwa amekijenga chama katika jimbo lake.

Katika hatua nyingine na mwendelezo wa M4C OPD Umati mkubwa wa wakazi wa Manispaa ya Bukoba jana walimiminika kwa wingi katika uwanja wa Uhuru kuwasikiliza Viongozi wa Chadema waliohutubia mkutano wa hadhara.

Kabla ya mkutano huo, yalifanyika maandamano makubwa yaliyokuwa yakiongozwa na vijana waendesha pikipiki.

Source: Nipashe Jumatatu.

Tumia akili japo kidogo.
Mliweka wagombea dhaifu dhidi ya wagombea makini: kushindwa ni lazima.
Slaa alishindwa na kikwete. 2010.
mbowe alipigwa chini 2005. je. ni udhaifu wa chama au n kitu gani?
zitto hakuteua wagombea.
 
Hii nchi hiko huru na kila mtu yuko huru kwenda popote.

Sasa subiri uone zitto anatangaza kwenda arusha au mbeya uone jinsi ambavyo bavicha na chadema watakavyo anza kulia na kuahidi kufanya vurugu.

Hakika zitto ni kiboko ya chadema ndio maana wana timia muda mwingi kumjadili yeye.
Hatakiwi kupewa support wala msaada wote popote pale na wanachadema,akienda aende na bendera ya Chauma...
 
Acha uongo mtu mzima!!!!

Wana Kigoma tumeshagundua uongo na ukanda mliouweka mbele kuliko kitu chochote.

Mbona maswali yote tuliyouliza juu za ZITTO hayakujibiwa, walijiumauma kama vile wamelewa mbege?????
Kigoma ipi uliopo labda kambi ya magamba..
 
Mwenyenzi MUNGU mwenye uweza wa yote awape nguvu kila kukicha viongozi wote wa Chama waweze kuwafikia Watanzania wote na wahabarishwe unyama unaoendeshwa na chama hiki cha mafisadi ndani ya Taifa letu.
 
Jamani nyie wana M4C msiwe wepesi wa kusahau unakumbuka LEMA 2005 alichukua RUSHWA na kusaidia CCM kuchukua jiMbo leo hii mnamuina wa maana! Au na nyie mna akili kama yeye!
 
mkuu, tatizo mie sikubali kukaririshwa kama kasuku.....LAZIMA nihoji siwezi kuwa kama msukule
A%20S%2027.gif
!!

naunga mkono sana tu mabadiliko ya kisiasa 2015 BILA kuhusisha zengwe dhidi ya wenzetu wenye mawazo tofauti - vinginevyo chadema na maccm itakuwa ni wale wale, tofauti itakuwa ni majina tu!!

Hata kama ni walewale tunataka Chama Kingine Tofauti na CCM ili kuonyesha kwamba Tanzania ni yetu sote na Si ya wanafamilia wa CCM tu.
 
Jamani nyie wana M4C msiwe wepesi wa kusahau unakumbuka LEMA 2005 alichukua RUSHWA na kusaidia CCM kuchukua jiMbo leo hii mnamuina wa maana! Au na nyie mna akili kama yeye!

weka pichaaaa.acha kupiga kelele
 
Hivi mwaka 2000 na mwaka 2005 Huyu ndugu Godbless J Lema. alikuwa yuko chama gani???

Haijalishi alikuwa chama gani, ila kwa sasa ni CHADEMA, ningekuona makini ungejibu kwa hoja hili swali kuliko kupindisha mada "mwaka 2000 walikuwapo madiwani 11 katika jimbo la Zitto la Kigoma Kaskazini, lakini mwaka 2005 alipogombea walipungua na kubakia sita(6) na kwamba mwaka 2010 walipungua zaidi na kubakia wawili(2)"
 
Back
Top Bottom