Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 360,461
- 829,854
1.Pepo la uongo
2.Pepo la uzinzi
3.Pepo la pombe na madawa
4.Pepo la wizi
5.Pepo la kisasi na malipizi
Haya ndio mapepo matano makuu tunayoyaabudu na kuyasujudia kuliko hata dini na imani zetu; ni mapepo yaliyotukamata hasa. Pepo la uongo likiwa ndio kubwa lao. Hakuna ambaye si muongo, mwizi, mlevi nk, hata ukikuta mmoja hana pepo hili basi utamkuta na pepo/mapepo mengine na wengi wetu tunayatumikia kwa utiifu mkubwa kabisa lakini bila ridhaa zetu tuko chini ya himaya zao.
Chunguza maisha waishiyo watu, mambo wafanyayo nyuma ya pazia na vile wanavyojiweka mbele ya kadamnasi utashangaa mno. Tuna watu ambao hawapitwi na Chupi wala suruali, kuna watu ambao bila kupata japo tusker baridi hawawezi kupata usingizi, tuna watu ambao wana mali nyingi tu lakini ameshazoea kuiba, yeye asipoiba anakosa amani kabisa, anaiba hata visivyoibika.
Kuna wale ambao wasipodanganya wanaugua kabisa, anadangaya familia, kazini, mtaani kwa jioni boss wake yeye anadangaya tu. Ni pepo sio yeye.
Haya yote yameleta matatizo makubwa kabisa tuliyonayo duniani kwa sasa. Visasi na malipizi vimeleta vita visivyoisha, ngono, wizi na ulevi vimeleta matatizo si haba.
Cha kushangaza ni kwamba ukiacha pombe labda na sigara wengi wetu hatuko tayari kuyasema waziwazi mapepo yetu.
2.Pepo la uzinzi
3.Pepo la pombe na madawa
4.Pepo la wizi
5.Pepo la kisasi na malipizi
Haya ndio mapepo matano makuu tunayoyaabudu na kuyasujudia kuliko hata dini na imani zetu; ni mapepo yaliyotukamata hasa. Pepo la uongo likiwa ndio kubwa lao. Hakuna ambaye si muongo, mwizi, mlevi nk, hata ukikuta mmoja hana pepo hili basi utamkuta na pepo/mapepo mengine na wengi wetu tunayatumikia kwa utiifu mkubwa kabisa lakini bila ridhaa zetu tuko chini ya himaya zao.
Chunguza maisha waishiyo watu, mambo wafanyayo nyuma ya pazia na vile wanavyojiweka mbele ya kadamnasi utashangaa mno. Tuna watu ambao hawapitwi na Chupi wala suruali, kuna watu ambao bila kupata japo tusker baridi hawawezi kupata usingizi, tuna watu ambao wana mali nyingi tu lakini ameshazoea kuiba, yeye asipoiba anakosa amani kabisa, anaiba hata visivyoibika.
Kuna wale ambao wasipodanganya wanaugua kabisa, anadangaya familia, kazini, mtaani kwa jioni boss wake yeye anadangaya tu. Ni pepo sio yeye.
Haya yote yameleta matatizo makubwa kabisa tuliyonayo duniani kwa sasa. Visasi na malipizi vimeleta vita visivyoisha, ngono, wizi na ulevi vimeleta matatizo si haba.
Cha kushangaza ni kwamba ukiacha pombe labda na sigara wengi wetu hatuko tayari kuyasema waziwazi mapepo yetu.