Mapenzi yamebeba vifo

Mapenzi yamebeba vifo

pole sana mwanmke mwenzangu !mie nakuomBa ona ukimwi ni km magonjwa mengine tu ni kama pumu tu ambayo utaishi nayo milele! nimeishi na ndugu yangu hiv positive alijikubali kwanza mwenyewe !then akafuata mashart ya Dk sasa hv ukiambia anaumwa hutaamini amekuwa na afya nzuri sana sna ! na ww jikubali kwanza mamy !mkabidhi Mungu janga lako !

napia usijione huna thaman tena ya kupenda hapana wapo weeeeeeeeengi mno wenye status kama yako na wanaishi na wenza wenye status moja !naamini ww utapata mwenza atakutoa upweke ulonao ! nakuomba jitahd kutoka out na mwanao nenda beach nenda kanisani imba kwaya nk nk utaona Mungu atakavyokuondolea hizo stress !

wewe ni.................... MZURI NA WATAHAMANI SANA SANA.............


AMINAAAA!!!
 
Ngweche beautiful hii habari yako inatia mpaka simanzi kuandika, too sad!
Cha muhimu, ikiwa pamoja na michango mingine ni kuwa na positive attitude katika kila kitu kwa ajili yako na mwanao ambae anakuhitaji more than ever kama baba mwenyewe ndo hivyo tena.
Jishughulishe na vitu vinavyokupa furaha hata kama ni kidogo, pamoja na dawa, you will be strong.
 
Nimeumia jamaniii uuuuwiii nahisi kuungua moyoni sina la kusema zaidi ya "ushuhuda wako upo" utakuja ushuhudia ulimwengu,simama katika IMANI yako na MUNGU wa mbinguni azidi kukutetea..Amen!!!!

Mumu.
 
Pole sana sana
Mungu awe nawe. Nakupa ushauri kama mmoja nakuomba sana madam una mtoto huyo ndio awe faraja kwako na nakuombea Mungu akupe nguvu na subira na furaha tele kila unapomuona mwanao.

Haya maradhi sio ya kutisha sana siku hizi
Na kama utafanya shughuli zako za kila siku bila kujila roho utapambana

Naamini you are too strong mpaka umepata nguvu ya kuandika hapa.
Tupo wazee kwa vijana, kina mama pia na wengine Dada zako humu ambapo wamelia na kutoa michango yao mingi.
Jikaze please pambana kwa afya yako na kwa ajili ya mwanao.

Ntaendelea kuwaombea wote kwa ujumla.
 
Ngweche beautiful hii habari yako inatia mpaka simanzi kuandika, too sad!
Cha muhimu, ikiwa pamoja na michango mingine ni kuwa na positive attitude katika kila kitu kwa ajili yako na mwanao ambae anakuhitaji more than ever kama baba mwenyewe ndo hivyo tena.
Jishughulishe na vitu vinavyokupa furaha hata kama ni kidogo, pamoja na dawa, you will be strong.
Hayo maneno ya faraja
 
Pole sana sana
Mungu awe nawe. Nakupa ushauri kama mmoja nakuomba sana madam una mtoto huyo ndio awe faraja kwako na nakuombea Mungu akupe nguvu na subira na furaha tele kila unapomuona mwanao.

Haya maradhi sio ya kutisha sana siku hizi
Na kama utafanya shughuli zako za kila siku bila kujila roho utapambana

Naamini you too strong mpaka umepata nguvu ya kuandika hapa.
Tupo wazee kwa vijana, kina mama pia na wengine Dada zako humu ambapo wamelia na kutoa michango yao mingi.
Jikaze please pambana kwa afya yako na kwa ajili ya mwanao.

Ntaendelea kuwaombea wote kwa ujumla.


Aminaa!
 
Ndoa nyingi zinaangamia kwa kukosa nguvu mwelekeo. Wanaume wakipata pesa wanasahau familia zao.
Tujifunze kitu kutoka video hii. Ndoa bila Mungu ni ndoano

 
Im a man! Nimeumia sana, sijui niseme nini yote yameniisha, nachoweza kusema naahidi kukujumuisha katika maombi yangu ya kila siku mungu ni mwema kwa umoja wetu atasikia maombi yetu! Umejikwaa ila bado hujaanguka! Mungu anakupenda sana, hata sisi tunakupenda sana! Anza maisha mapya ishi ndani ya mungu! Samehe yote yaliyopita na sahau pia! Najua ni ngumu ila kwa atiae nguvu kila kitu kinawezekana!
 
basi niafadhali nife niende mbinguni tu sasa

Ukifa na hali uliyo nayo sasa hutaenda mbinguni maana huko wanaenda wenye amani ya moyo kupumzika. Mbingu inaanzia hapa hapa. Una hali ngumu lakini amini kuwa hilo ni jaribu na liko ndani ya uwezo wako. Maisha ni mtihani dada, mtihani wenye mchanganyiko wa maswali rahisi na magumu. Unafanya mtihani toka unazaliwa mpaka unakufa - uwe na VVU usiwe navyo mwisho wa maisha yako ni kifo. Tatizo lako unafikiri utakufa kwa UKIMWI kumbe wala. Ulikutana na swali la kuambiwa uache urembo ukaliona rahisi rahisi ukalifanya. Likaja la kuchelewa kurudi ukalifanya, likaja la kipigo. Sasa umekutana na swali gumu zaidi lakini haimaanishi kwamba ndo umeshafeli. Pambana ulimalize uende swali lingine. Huna sababu ya kuchanganyikiwa na kuendelea kulia kwa sababu huwezi kurudisha maisha nyuma na VVU havifutiki mwilini mwako. Unakuwa kama wana wa Israel safarini - nyuma majeshi ya Farao, mbele bahari. Huwezi kubaki hapo hapo ukutwe na mashambulizi ya magonjwa na msongo wa mawazo. Songa mbele bahari itakupisha utavuka. Utavuka na virusi vyako. Hivyo vidude havina dawa lakini si tishio tena. Sasa hivi tunatishiwa na kansa na homa za ini. Kwa hiyo wewe huumwi ila ukiendekeza hofu utaumwa. Hebu tafuta sababu ya kugangamala. Unataka uwaze mpaka uondoke halafu mtoto abaki na nani?

Mwachie huyo mumeo toka moyoni, jisamehe, shukuru una mtoto, shukuru una uhai, ndugu, kazi, na chochote unachoweza kutaja. Bado una nafasi nzuri sana na kesho yako inang'aa. Usimpe shetani nafasi ya kuiharibu. Wewe nakuona kabisa ukiishi mpaka uone mjukuu. Siyo kwamba nakupa moyo wa plastiki. Tunawajua watu walioishi na VVU toka 1986 mpaka leo na kuna walioishi na pneumonia na malaria siku 2 tu leo hawamo.

Sasa hivi wala usiwaze habari ya mwenza. Nikupe tu taarifa ambayo wewe ni shahidi: mwenza hawezi kukupa furaha na amani. Hivi hutafutwa na mtu binafsi toka ndani yake kwenye Mungu wake. Kaa utafakari maisha na Mungu wako. Ujenge uhusiano mzuri na wewe mwenyewe wa kujipenda na kujisamehe na kujiremba na kupendeza kama zamani kwa sababu uko kwenye ulimwengu wako. Umuinue Ngweche huko aliko. Ngweche akisimama vitu vitajipanga vizuri mpaka ushangae.

Ukisema hakuna mwanaume atakayekutaka kwa sababu una VVU utakaribisha mabazazi maishani mwako kwa sababu wapo wanaume watakaokutaka na hali yako hiyo sasa hivi ukiwa bado umevurugwa. Hii dunia ione hivi hivi. Sasa kwa kuwa umeshajiona duni hutajipa hata muda wa kutathmini. Utaona umeokota almasi kunduchi kumbe unaingizwa kwenye tabu mpya. Tulia mummy dhoruba ipite hii. Mwanga utauona na mbele utaendelea. Rudisha furaha ya watoto wako ambayo sasa inataka kupotea. Kama msaidizi wako wa nyumbani ameona tatizo ujue mtoto wako ameona kabla ya dada yake na ataathirika ukiendelea kubaki chini. Mbele uendelee kwa furaha mpaka siku Mungu atakapoweka nukta mwenyewe. Kama uko Dar nenda kawaone clinical psychologists kule Muhimbili msaidiane kukabiliana na hili badiliko. Watu wa dini wenye hekima na kipawa cha ushauri wapo lakini umakini unahitajika mkubwa.
 
Dear pole sana, Kuwa na imani yote yanawezekana kwa Mungu, atajibu maombi yako, omba Mungu nakuhakikishia atakujibu. Tumeona mifano kwenye jamii, kuna jirani aligundua ana HIV baada ya Mme wake kufa, na yeye alipewa masharti kama yako mama wa watu akayafuata tena yeye ilikuwa worse aliachishwa mpk kazi kwa nguvu. Mme akafa, kabaki kazi hana kazi na HIV juu na kaachiwa watoto watano. Wa kwanza alikuwa form one. Lakini siku aliyoambiwa ana HIV alirudi nyumbani akapiga goti alimuambia Mungu sikuwahi kufanya uzinzi, u know my heart please forgive me kama kuna dhambi nyingine nilitenda au wazazi wangu ni samehe. Nipe maisha marefu na nguvu ya kutunza wanangu mpk nione wajukuu zangu. Anasema baada ya kuomba alijiona na nguvu, kasomesha watoto wake wote, yuko na ma Dr Na lawyers. Mpk napoandika hii msg yupo hai kacheza harusi na wajukuu kawaona since 1990 baada ya kifo cha mumewe. So dear usikate tamaa yupo aliyejuu atakulinda muombe sana atakujibu.
 
Mungu ni mkarim,mungu ni mwenye upendo,mungu ni mwenye hekima ambae humpangia kila binadam atakavyo..muombe sana kwani anajua na anaona kila kitu,Tegemea makubwa kutoka kwake kwani hua anajib maombi yetu
 
Dah!!pole sana dada yangu/mpendwa wangu kwa khali uliyonayo jamani.

Dah!!..nimekuonea huruma bure dada yangu bhasi tu.
 
Wewe ni HIV tu unaanza kushtuka?! yaliyonikuta mimi ni zaidi ya hako kaugonjwa lakini sasa nimepona 100%!! Sijui nitumie njia gani kukueleza coz mimi ni mvivu sana wa kuandika. Me ni mdogo wako kwa umri but unatakiwa kuniiga. Mungu hana msaada kwa waoga na wepesi wa kukata tamaa. hayo tu... zaidi nifuate inbox uweze kujua ni njia gani nimetumia
 
Wanaume sisi kuna muda ni viumbe wa ajabu sana yan
 
Back
Top Bottom