makaveli10
JF-Expert Member
- Mar 27, 2013
- 37,428
- 108,436
[emoji17] [emoji17] [emoji17] [emoji17]
Ushauri wangu nenda ukapime sehemu nyengine tena, Kuna baadhi ya wakati vile vipimo huchanganya(chako akapewa mwengine na kipimo cha mwengine ukapewe wewe). Jaribu kwenda sehemu kama 3 tofauti kupima tena kama ukipata majibu sawa hapo kubali matokeo. Lakini kama ikitokea upo positive basi angalia dawa za kienyeji au za hospitali ziweze kukusaidi, kila maradhi yana dawa yake muhimu kuipata na kufata masharti yake tu. Nakutakia afya njema na maisha marefu ya furaha.
Kama ni kweli pole sana kuathirika sio mwisho wa maisha. Ushauri mcheki MziziMkavu anaweza kukuingiza katika quarantine yake akakupigisha dose ya miezi 6 utapona kabisa. Alishawahi toa shuhuda ya watu aliowaponesha kwa dawa zake za asilia. Habatt sauda na makorokoro mengine something like that. Utapona tu amini hivyoHabari zenu wana JF
Mimi sio mwenyeji katika mtandao huu lakini imenibidi niwe na akaunti, pia si mwandishi mzuri lakini mtanielewa kwa hiki nitakacholeelezea.
Niliolewa miaka 6 iliyopita na tumebahatika kupata mtoto wa kiume ambaye kwakweli alileta furaha kwenye nyumba yetu.
Wakati wa uchumba mume wangu alikua hanikatazi kujipamba yaani kusuka na kuvaa mapambo ya wanawake kama tunavyojua wasichana tunapenda kujipamba, lakini baada ya kuolewa siku moja mume wangu aliniambia yeye anapenda mtu natural hapendi kuona nasuka nywele zenye rasta wala kushonea weaving.
Nilikubaliana naye lakini kwa shingo upande kiukweli nilikua napenda kupendeza sababu nafanya kazi so wapenzi nilikata nywele zangu, hereni, bangili sijui nii vyoote niligawa hata mafuta hakuna kupaka body cream napaka nilibadili hata mafuta nikawa napaka lotion za kawaida tu za sh 2500 au 3000 kwa ujumla kila kitu changu kilibadilika. Katika mavazi mume wangu alisema nisivae suruali sababu umbo langu linaonekana sana nikivaa hivyo hata suruali niligawa nikawa navaa magauni na sketi tena magauni mapana sio iliyonishika mwili kwa ujumla hayo ndio mabadiliko baada ya kuolewa
Miaka 2 ya ndoa ilipita mume wangu Mungu akambariki akapata kazi nzuri zaidi iliyompa mshahara mzuri nilimshukuru Mungu nikamwambia tutafute kiwanja tujenge nyumba yetu walau na jujenge nyumba ya kupangisha mume wangu hakuunga mkono sana swala la nyumba ya kupangisha yeye anapenda sana magari hata sasa anapenda magari mno lakini sio ya biashara ya kutembelea tu.
Basi tulianza tulijenga nyumba yetu kabla ya kumaliza kujenga mume wangu alinunua gari harrier mimi niliumia sana sababu nilitamani tumalize kujenga ndipo angenunua gari lakini namshukuru Mungu tulimalizia kujenga na hata sasa tunaishi kwenye nyumba yetu.
Baada ya mda ambao sikumbuki vizuri ni mda gani mume wangu alianza kubadilika akawa sio wakuwahi tena nyumbani nikimwuuliza anakua mkali nikawa naogopa kumwuuliza akawa anarudi mara saa 7 mara saa 9 lakini kuna kitu kilikuja kichwani kwanini ni mkali mbona hata sina kosa nilijishusha kuliko kawaida lakini bado hakupunguza ukali ilifika mahali tendo la ndoa inapita mwezi hatugusani mimi namwogopa hadi yeye aanze.
Mawazo yalinitesa mno mno nilipungua sana hata maziwa kifuani yakwa hayatoki niliamwua kumwachisha mtoto siku hiyo hakuchelewa kurudi kwenye saa 5 alisharudi baada ya kula nimwambia nimemwachisha mtoto, sitaa kaa niisahu hii siku nilipigwa mno aliniambia nimekua Malaya nimemwachisha mtoto ili niendeleze umalaya wangu na kwanini sikuomba ruhusa ya kumwachisha mtoto. Pamoja na kipondo nilichopata niliomba msamaha sana lakini hakutaka kunisamehe alitoka akawasha gari akaondoka nilimwona baada ya siku 2 tuliendelea kuishi kama mabubu rafiki yangu akawa dada wa nyumbani, na mtoto. Siku moja nilikutana na rafiki yake akashangaa kwa mwonekano nilionao sikuweza kumwambia lolote tofauti na kumwambia napitia changamoto ila zimeisha kumbe nasema uongo mambo ndio yananoga.
Siku moja kuna dada yangu wa hiari alinipigia simu akiwa kama anahuzuni hivi akaniambia njoo sehemu fulani nilienda sababu dada yangu hakuwahi kuwa na huzuni ile nilipofika maeno yale niliona gari ya mume wangu imepaki nje ya hiyo hotel dada yangu aliniambia nikae kwenye gari siti ya nyuma na nitulie nilikaa pale kama masaa 2 hivi ndipo nikamwona mwanadada anatoka na mume wangu kamshika mkono yaani ni mrembo hasa kajitengeneza anang'aa kama mkristmas tree, dada yangu akaniambia usishuke acha waondoke then nitakurudisha nyumbani kweli waliondoka na sisi tuliondoka nililia mno dada akaniambia anajua tabia za mume wangu lakini alikua anaogopa kuniambia.
Hayo maombi ambayo niliomba siku hiyo sijui kama yatakuja kutokea baada ya muda mume wangu aliniambia ameoa mke wa pili hivyo hawezi kuendelea kuishi na mimi atakua anakuja kumwona mtoto niliwaeleza wazazi wangu mama yangu aliumia sana lakini ndugu zake wote walifurahi hasa mawifi zangu. nikaanza kukaa maisha ya kutokua na mume wangu nyumbani.
Baadae maumivu yakaanza kupungua ndipo tatizo jipya likazuka. Siku moja walipita watu ofisini wakiwa wanahamasisha tupime afya zetu mimi nilikua mmojawapo nilipima na ndipo majibu yangu yakaja am HIV POSITIVE ndugu zangu sina cha kuwaambia maana usiombe uambiwe una virusi vya UKIMWI nililia kwa mda wa wiki nzima sikuweza kwenda kazini dada wa kazi alikua ananipenda akawa ananshindwa ninamatatizo gani. Nilimwita mama nikaja kumweleza ukweli mama yangu alilia sana na sisi kwetu tumezaliwa wawili tu mimi ndio mkubwa. Wapendwa natamani kupona huu ugonjwa Mungu wangu anajua ukweli wangu. Bado nafanya kazi naweza kujihudumia na mtoto pia naweza kumlea.
Natamani kupona huu ugonjwa wapo wanao nipenda lakini siwezi kuwa na mahusiano. Natamani kupona sijui kwa njia gani lakini natamani hivi virusi visiwepo kwenye mwili wangu ili niweze kuwa na mtu mwingine niwe na mimi nafuraha nisaidieni wapi wanatoa huduma ya maombi mwenye matatizo kama yangu? Hakuna mwanaume atakae nipenda nikimwambia ninavirusi najua mtaona nimechanganyikwa ila natamani kupona.
Nisameheni hilo ndio linaniumiza
sio kweli wote tunahusikaWanandoa wengi wenye huu ugonjwa asilimia kubwa wanaume ndio wanaouleta ndani.
Pole sana dada. Cha kwanza kabisa ukumbuke kuwa katika tatizo hili haupo peke yako, yaani upo wewe ,huyo mme wako ,huyo mke mwenza, aliyemwambukiza mmeo na wengine wote waliowahi kuwa na uhusiano na mmeo.Kundi hill lote ni wahanga wa ugonjwa huu. Kuna mahali umesema ulimwona mmeo na mwanamke mwingine wakiwa na furaha tele,basi jitahidi kuwa na furaha hata kama ni vigumu. Jikubali kwamba hutaweza kubadili hali hii na kwamba ni mapito ambayo kwayo ilikuwa ni lazima uyapitie kuelekea ukomo was maisha yako. Pole sana dadaangu, tupo wengi kwenye mapito haya na tumejitoa na kusonga mbele kama vile hakuna lililotokea. Jikubali tu na funguka.Pole sana sana Dada. Pole sana. Naomba uje inbox tunaweza kuongea mambo mawili matatu.
Pole sana dear.... Pole sana Mwanamke mwenzangu. Pole Pole dear... Hakika inaumiza sana.
Dada hii ni hadithi ya kutunga au ni kisa cha kweli!!? Kama ni kisa cha kweli nitumie namba yako pm kuna faraja naeza kukupatia. Pole sana na usidharau