Mapato ya TRA mwezi Juni yatashuka

Mapato ya TRA mwezi Juni yatashuka

Kwa kile kimbunga cha msimu cha utumbuaji sikujua kama kuna mtu anathubutu kuiba hata sindano, kumbe kuna watoto wa mjini bana kelele za milango haziwanyimi usingizi, mwezi may wamajilipa mishahara hewa bil 1.8, dah.
 
d8cae938ee866cac197d31bb95689387.jpg
 
Kwa hakika mapato yamekuwa yakishuka tofauti na ilivyokuwa mwezi Novemba mwaka jana. Cha kushangaza, matumizi nayo yameanza kuwa ya hovyo, kwa mfano kutumia mamilioni ya shilingi kuimarisha ulinzi wa Tulia Akson kama kwamba tuko Somalia, je, huu sio ubadhirifu wa fedha za wavuja jasho?
 
Never compare numbers in your life...Compare proportions....

Usilinganishe namba hata siku moja utaishia kwenye hitimisho bovu kama hili mnalotaka kulazimishia...linganisha asilimia ....kwa wana takwimu wanalielewa hili.
Mkuu hoja ni kwamba mapato yanashuka....na muda si mrefu tutarudi kwenye bilioni 900 kwa kuwa Yale majigambo ya kukusanya sana hayakutokana na uwepo wa vyanzo vipya vya kodi bali ni kukusanya madeni tu.....vyanzo vya mapato vipya vya kupa
 
Kumekuwa na maporomoko makubwa ya mapato ya TRA kutoka trilioni moja na bilioni mia nne Mwaka Jana wakati serikali ya awamu ya tano inaingia madarakani mpaka trilioni moja mwezi wa tano.Ni wazi mwezi wa sita TRA watatangaza mapato ya bilioni 900. Tunarudi kulekule kwa JK.

Ni ishara kwamba JK hakuwa mzembe bali mapato yalienda na upepo wa biashara,mwanzoni tuliaminishwa kwamba kuna wizi sijui wapi,sasa mbona na udhibiti wote ndani ya miezi sita mapato yameshuka kwa bilion 400? Zinakwenda wapi?zimepotelea wapi?

Kuna mtu Mwenye ubavu wa kuzikosoa jitihada za Kikwete kwenye kukusanya mapato na aamke nimuone.

Mwez june mbona bado jaman ndo kwanza walitangaza ya mwez may hapo majuz ambapo walivuka lengo
 
TRA YAVUKA LENGO LA MAKUSANYO YA KODI KWA MWEZI MEI 2016



MKamishna Mkuu wa TRA Bw. Alphayo Kidata akitilia mkazo jambo wakati wa kikao na waandishi wa habari kuhusu taarifa ya makusanyo ya mapato kwa mwezi Mei 2016,kilichofanyika katika Ofisi za Mamlaka ya Mapato Tanzania Mkoa wa Kilimanjaro, Kulia kwake ni Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipakodi Bw. Richard Kayombo na kushoto ni Meneja wa Mkoa wa Kilimanjaro Bw. Abdul Mapembe.
*******************
MAMLAKA ya Mapato Tanzania imefanikiwa kukusanya kiasi cha shilingi trilioni 1.032 katika mwezi Mei ambayo ni sawa na asilimia 100.7 ya lengo la kukusanya shilingi trilioni 1.025 katika mwezi huo.
Makusanyo ya kipindi cha miezi kumi na moja (Julai 2015 hadi Mei 2016) ni jumla ya shilingi trilioni 11.956 sawa na asilimia 99.2 ya lengo la shilingi trilioni 12.054 katika lengo la kipindi hicho kwa Tanzania Bara na Zanzibar.
Akizungumza na waandishi wa habari mjini Moshi leo kuhusu mwenendo wa makusanyo ya mapato, Kamishna Mkuu wa TRA Bw. Alphayo Kidata amesema TRA inaendelea na jitihada mbalimbali kuhakikisha inafikia na kuvuka lengo la makusanyo iliyopangiwa na serikali katika kipindi cha mwaka wa fedha 2015/2016 na kuendelea kukabiliana na changamoto mbalimbali zinazoikabili Mamlaka katika ukusanyaji wa mapato.
“TRA imejiwekea mikakati thabiti ya kuongeza mapato kwa kipindi cha mwezi mmoja uliobaki ili kuweza kufikia au kuvuka lengo kwa mwaka huu wa fedha, ambapo kwa sehemu kubwa tumeendelea kupambana na magendo hususani katika pwani ya bahari ya Hindi na mipaka yote, kupambana na wafanyabiashara wanaokwepa kulipa kodi na wanaokiuka kutumia mashine za kodi za keielektroniki , kuwawajibisha wafanyakazi wasio waadilifu pamoja na kuhakikisha inaboresha zaidi mifumo itakayompa urahisi mlipakodi katika zoezi zima la ulipaji kodi wa hiari, alisema Kamishna Mkuu.
Bw. Kidata ameendelea kusisitiza wananchi na wafanyabiashara kuwa wazalendo kwa nchi yao kwa kutoa na kudai risiti za EFD pindi wanaponunua au kuuza bidhaa pamoja na huduma ili kuongeza mapato ya nchi.
Katika kutekeleza agizo la Mh. Rais na kuhakikisha wafanyabiashara wanatoa ushirikiano katika matumizi ya mashine za EFD Mamlaka imeanza utekelezaji wa awamu ya kwanza ya ugawaji wa mashine za EFD kwa wafanyabiashara wadogo kwa Mkoa wa Dar es Salaam.
TRA imeanza ugawaji wa mashine za EFD kwa wafanyabiashara wapatao 5,703 wenye mauzo ghafi kati ya Shilingi milioni 14 na milioni ishirini (20) kwa mwaka, wafanyabiashara hao wanatakiwa wafike katika ofisi za Mamlaka ya Mapato za Mikoa wanayolipia kodi ya Ilala, Kinondoni na Temeke ili waweze kuhakiki usajili wao wa Namba ya Utambulisho wa Mlipakodi (TIN) na kupewa kibali cha kupewa Mashine ya EFD zoezi lililoanza Juni Mosi alisisitiza Kamishana Mkuu.
Aidha, Bw. Kidata alifafanua kuwa zoezi hili litaendelea katika Mikoa yote Tanzania kwa awamu kwa utaratibu utakaotangazwa mara kwa mara na hivyo kutoa wito kwa wafanyabiashara wenye mauzo tajwa wote nchini kutoa ushirikiano pindi inapofika zamu yao katika Mikoa yao.
Zoezi hili litasaidia kuongezaka kwa Mapato ya nchi endapo wafanyabiashara na wananchi watakuwa bega kwa bega katika kuhakikisha wanatumia mashine hizo na kutoa taarifa kwa Mamlaka kuhusu wafanyabiashara wote watakao kiuka kutumia mashine hizo za EFD.
Kwa upande wa wananchi, kamshna mkuu amewaasa kuadai risiti kila wanunuwapo bidhaa au kupata huduma na kuhakikisha usahihi wa kiwango walicholipia sambamba na risiti walizopewa
“Pamoja Tunajenga Taifa Letu"
Imetolewa na:
Idara ya Huduma na Elimu kwa Mlipakodi
Wewe zwa.zwa hapa yanazungumziwa matokeo ya June!
 
Ila propaganda zitaharibu nchi hii...wakati serikali ya awamu ya tano inaingia watu walijua kwamba nchi hii mapato mengi....ona sasa tuna rudi kwenye average yetu
 
Hali mbayaa ngoja baada ya July 1 ndio tutashuhudia uhalisia wa nchi yetu
Watu watalia njaa mno
 
Tusitarajie muujiza,hata bajeti inayojadiliwa bungeni ni kiini macho....bajeti halisi ni ya trilioni 22 kwa kuwa mapato yetu ni Yale Yale,kasi,mbwembwe na kufoka kumeishia wapiiii....mbona tunarudi nyuma hatua mia mbele hatua 80!! Matumaini yako wapi?
Ni muda hajafokafoka sijui atafoka na Lipi akija
 
Hali mbayaa ngoja baada ya July 1 ndio tutashuhudia uhalisia wa nchi yetu
Watu watalia njaa mno
Kweli....nafikiri tangu Uhuru hii ni bajeti chungu kwa walala hoi hasa watumishi...posho zao nyingi zimekatwa....hivyo hata purchasing power yao itapungua,hii
 
Kumekuwa na maporomoko makubwa ya mapato ya TRA kutoka trilioni moja na bilioni mia nne Mwaka Jana wakati serikali ya awamu ya tano inaingia madarakani mpaka trilioni moja mwezi wa tano.Ni wazi mwezi wa sita TRA watatangaza mapato ya bilioni 900. Tunarudi kulekule kwa JK.

Ni ishara kwamba JK hakuwa mzembe bali mapato yalienda na upepo wa biashara,mwanzoni tuliaminishwa kwamba kuna wizi sijui wapi,sasa mbona na udhibiti wote ndani ya miezi sita mapato yameshuka kwa bilion 400? Zinakwenda wapi?zimepotelea wapi?

Kuna mtu Mwenye ubavu wa kuzikosoa jitihada za Kikwete kwenye kukusanya mapato na aamke nimuone.
Bajeti tuliyonayo ni ya Kikwete. Ya Magufuli itaanza tarehe 1 july 2016. Ukitaka kumpima Magufuli mpime kwenye makusanyo ya July mwaka huu.
 
Back
Top Bottom