Mapato ya TRA mwezi Juni yatashuka

Mapato ya TRA mwezi Juni yatashuka

Watu hawafati mzigo tena....wadada wa hotel wanatemeshwa Kazi balaa....hoteli zimeathirika sana....hata return za mwezi wa sita TRA zitakuwa za hovyo kuliko zote

Lkn Mkuu hawa jamaa hawashindwi kujitekenya na kujichekesha. Wanaweza kupika data na kutusomea figure inayofurahisha masikio. Muda utaongea.
 
Malengo yanapangwa kabla ya mwaka mpya wa bajeti, sasa wewe unayesema yanadidimia sijui unatumia akili gani, lengo la TRA hadi la June 2017 litakuwa rasmi siku wanayopitisha bajeti, ujuaji mwingi halafu kichwani hamna kitu.
Lengo la kila mwezi ni tofauti na la mwaka wa bajeti
 
Teh teh! Lumumba wenyewe walevi na mada hii imeletwa usiku sijui kama wataleta cha maana. Rutashobya ameamka kwenye usingizi wa lubisi na nkanja akaanza kutukana, lizaboni ndo kabisa aelewi.
Me Rutashobya alinichekesha mkoa anaotoka watu wanashidwa ata mlo mmoja yeye yuko Jamii forum anapigania chama Ndugu zake wapo kwenye dimbwi la umaskini wa kupindukia
 
Nilidhani nimeona mimi tu lakini kama meli hazipo manayake hatuagizi tena aidha kwa shinikizo la ndani la kibiashara au mzunguko umekufa!! na asikuambie mtu biashara ina principle zake mfn nilisikia sukari ilikamatwa ikagawiwa taasisi za serikali bure hii manayake nini ?manayake mtaji umekufa kifo cha lazima na hapo hata ile kodi ya kubabaishia nayo imekufa vilevile lakini hilo pia nalifananisha na TCU na st joseph!! wazazi wamekamuliwa milioni kibao na mwisho TCU imewakana wanafunzi lakini pia ilitoa baraka zk kabla nani anawafidia wazazi serekali imejitoa !!lakini deci ilizaliwa na nani chini ya baraka za nani kwakua naamini km TRA wanafika kukata kodi manayake haikua siri leo bilioni kibao zimemezwa kifupi inachosha kufikria haya bora kucheza bao chini ya mnazi!!!
 
Me Rutashobya alinichekesha mkoa anaotoka watu wanashidwa ata mlo mmoja yeye yuko Jamii forum anapigania chama Ndugu zake wapo kwenye dimbwi la umaskini wa kupindukia
Jamaa wanakula viwavi tu...migonba ina mnyauko na hakuna kauli thabiti kutoka serikali ya rutasshobolwa
 
Siku hizi utabiri umezidi , toa ' analysis ' za mapato kushuka mwezi unaoutaja!!
ninekupa graph ya kuanzia serikali ya awamu ya tano ilipoingia madarakani....mapato yalikuwa juu sana...kwa sasa graph mstari wake umezama na muda si mrefu hatutauona tena
 
TRA YAVUKA LENGO LA MAKUSANYO YA KODI KWA MWEZI MEI 2016



MKamishna Mkuu wa TRA Bw. Alphayo Kidata akitilia mkazo jambo wakati wa kikao na waandishi wa habari kuhusu taarifa ya makusanyo ya mapato kwa mwezi Mei 2016,kilichofanyika katika Ofisi za Mamlaka ya Mapato Tanzania Mkoa wa Kilimanjaro, Kulia kwake ni Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipakodi Bw. Richard Kayombo na kushoto ni Meneja wa Mkoa wa Kilimanjaro Bw. Abdul Mapembe.
*******************
MAMLAKA ya Mapato Tanzania imefanikiwa kukusanya kiasi cha shilingi trilioni 1.032 katika mwezi Mei ambayo ni sawa na asilimia 100.7 ya lengo la kukusanya shilingi trilioni 1.025 katika mwezi huo.
Makusanyo ya kipindi cha miezi kumi na moja (Julai 2015 hadi Mei 2016) ni jumla ya shilingi trilioni 11.956 sawa na asilimia 99.2 ya lengo la shilingi trilioni 12.054 katika lengo la kipindi hicho kwa Tanzania Bara na Zanzibar.
Akizungumza na waandishi wa habari mjini Moshi leo kuhusu mwenendo wa makusanyo ya mapato, Kamishna Mkuu wa TRA Bw. Alphayo Kidata amesema TRA inaendelea na jitihada mbalimbali kuhakikisha inafikia na kuvuka lengo la makusanyo iliyopangiwa na serikali katika kipindi cha mwaka wa fedha 2015/2016 na kuendelea kukabiliana na changamoto mbalimbali zinazoikabili Mamlaka katika ukusanyaji wa mapato.
“TRA imejiwekea mikakati thabiti ya kuongeza mapato kwa kipindi cha mwezi mmoja uliobaki ili kuweza kufikia au kuvuka lengo kwa mwaka huu wa fedha, ambapo kwa sehemu kubwa tumeendelea kupambana na magendo hususani katika pwani ya bahari ya Hindi na mipaka yote, kupambana na wafanyabiashara wanaokwepa kulipa kodi na wanaokiuka kutumia mashine za kodi za keielektroniki , kuwawajibisha wafanyakazi wasio waadilifu pamoja na kuhakikisha inaboresha zaidi mifumo itakayompa urahisi mlipakodi katika zoezi zima la ulipaji kodi wa hiari, alisema Kamishna Mkuu.
Bw. Kidata ameendelea kusisitiza wananchi na wafanyabiashara kuwa wazalendo kwa nchi yao kwa kutoa na kudai risiti za EFD pindi wanaponunua au kuuza bidhaa pamoja na huduma ili kuongeza mapato ya nchi.
Katika kutekeleza agizo la Mh. Rais na kuhakikisha wafanyabiashara wanatoa ushirikiano katika matumizi ya mashine za EFD Mamlaka imeanza utekelezaji wa awamu ya kwanza ya ugawaji wa mashine za EFD kwa wafanyabiashara wadogo kwa Mkoa wa Dar es Salaam.
TRA imeanza ugawaji wa mashine za EFD kwa wafanyabiashara wapatao 5,703 wenye mauzo ghafi kati ya Shilingi milioni 14 na milioni ishirini (20) kwa mwaka, wafanyabiashara hao wanatakiwa wafike katika ofisi za Mamlaka ya Mapato za Mikoa wanayolipia kodi ya Ilala, Kinondoni na Temeke ili waweze kuhakiki usajili wao wa Namba ya Utambulisho wa Mlipakodi (TIN) na kupewa kibali cha kupewa Mashine ya EFD zoezi lililoanza Juni Mosi alisisitiza Kamishana Mkuu.
Aidha, Bw. Kidata alifafanua kuwa zoezi hili litaendelea katika Mikoa yote Tanzania kwa awamu kwa utaratibu utakaotangazwa mara kwa mara na hivyo kutoa wito kwa wafanyabiashara wenye mauzo tajwa wote nchini kutoa ushirikiano pindi inapofika zamu yao katika Mikoa yao.
Zoezi hili litasaidia kuongezaka kwa Mapato ya nchi endapo wafanyabiashara na wananchi watakuwa bega kwa bega katika kuhakikisha wanatumia mashine hizo na kutoa taarifa kwa Mamlaka kuhusu wafanyabiashara wote watakao kiuka kutumia mashine hizo za EFD.
Kwa upande wa wananchi, kamshna mkuu amewaasa kuadai risiti kila wanunuwapo bidhaa au kupata huduma na kuhakikisha usahihi wa kiwango walicholipia sambamba na risiti walizopewa
“Pamoja Tunajenga Taifa Letu"
Imetolewa na:
Idara ya Huduma na Elimu kwa Mlipakodi
Hii mada ya kuombea serikali ishindwe kukusanya mapato huwa lazima iletwe hapa jukwaani kila mwezi na kila mwezi lazima waumbuliwe....kama unavyomuumbua huyu barvicha.
 
Tuanze kusubiria mapato ya July....kwenda mbele! Baada bajeti hewa!!
 
Kabla ya matumizi kinachotangulia ni bajeti nyie vijana wa chadema mnafuata wanachosema viongozi tu hata kama ni uzushi
 
Hii mada ya kuombea serikali ishindwe kukusanya mapato huwa lazima iletwe hapa jukwaani kila mwezi na kila mwezi lazima waumbuliwe....kama unavyomuumbua huyu barvicha.
Hoja ni kwamba...kila mwezi mapato yanashuka tangy serikali ya awamu ya tano iingie madarakani,walianza na trilionj moja na bilioni mia nne ,leo wanakusanya trilioni moja,maana take kuna upungufu wa bilioni 400 ndani ya miezi sits katika makusanyo.....
 
Hii mada ya kuombea serikali ishindwe kukusanya mapato huwa lazima iletwe hapa jukwaani kila mwezi na kila mwezi lazima waumbuliwe....kama unavyomuumbua huyu barvicha.
Mapato yalianza trilioni moja na bilioni 400 wakati serikali inaingia madarakani,Leo mwezi wa tano yametangazwa kuwa ni trilioni moja ....ukusanyaji una upungufu wa bilioni 400
 
Hoja ni kwamba...kila mwezi mapato yanashuka tangy serikali ya awamu ya tano iingie madarakani,walianza na trilionj moja na bilioni mia nne ,leo wanakusanya trilioni moja,maana take kuna upungufu wa bilioni 400 ndani ya miezi sits katika makusanyo.....

Wew ni mchawi nini ,kawange sasa kutwa nzima unashinda huku ,kupiga ramla nani atafariki
 
Mkuu, hizo ni hisia zako tu ila ukweli unabaki kwamba TRA wanakusanya mapato kwa kuvuka malengo yao
Ukichukua Property tax ya Halmashauri uksipeleka TRA unajifumba tu na kuwazuga watanzania. Hujaongeza kitu
 
Hoja ni kwamba...kila mwezi mapato yanashuka tangy serikali ya awamu ya tano iingie madarakani,walianza na trilionj moja na bilioni mia nne ,leo wanakusanya trilioni moja,maana take kuna upungufu wa bilioni 400 ndani ya miezi sits katika makusanyo.....
Never compare numbers in your life...Compare proportions....

Usilinganishe namba hata siku moja utaishia kwenye hitimisho bovu kama hili mnalotaka kulazimishia...linganisha asilimia ....kwa wana takwimu wanalielewa hili.
 
Back
Top Bottom