MAONI:. Ndoa ,,, Waislam vs Wakristo

MAONI:. Ndoa ,,, Waislam vs Wakristo

Status
Not open for further replies.
Msifungwe nira na wasioamini. Biblia inasema wazi ktk kitabu cha Mathayo. Pia Yesu alitamka hadharani mchana kweupe kuwa Nuru na giza haviwezi kukaa pamoja. Sasa iweje mkristo ukaoe muislam? Me mpk naoa na kuruka ruka kwangu kote nilikuwa sigegedi wala kutongoza demu asiye wa dini yangu.
 
kwa imani ya dini ya kiislamu, ukristo ni giza(si dini ya kweli) hivyo wakristo kwa ujumla wapo kwenye upotevu ulio mkubwa, ni nadra sana kukuta mzazi wa kiislamu kumruhusu mwanae(binti) kuplewa na mkristo kwa maana ya kutotaka kumtia gizani. Aidha hata kwa watoto wa kiume ambao wanataka kuoa mabinti wakikristo ni vigumu sana wazazi kukubaliana nao unless binti akubali kubadili dini kuingia uislamu.

And the vice versa is true
 
Muislamu wa kiume anatakiwa akae na muyahudi au mkiristo (ahlul-kitab) wakiowana kwa muda maalum tu kwa ajili ya kumuongoza mkewe katika dini ya haki. Ikiwa imeshindikana atatakiwa kumuacha ila watoto watakua chini ya baba yao katika malezi ya kiislam. Kwa sababu mwanaume ndio kiongozi wa familia.

Mbona Mzee Makamba kamuo Mkristo na kila mtu yupo na dini yake ile ile na mzee Makamba ni muumini mzuri tuu...

Muumini mzuri anamjua M'mungu peke yake. Wewe unamjuaje mtu ni muumini mzuri??!!!
 
Waislamu wanaume wameruhusika kuowa Ahlul-kitabu maana yake ni (wakristo na mayahudi) hawa ni wanawake wema miongoni mwa waliopewa kitabu“walmuhswanatu mina ladhina uutulkitaba” Mwanamke wa kiislamu haruhusiki kuolewana wakristo au mayahudi. Ni kwamba mwanamume awendiye mwenye mas-uliyah na nyumba na watoto, kwani kwa Hikma ya Allaah سبحانه وتعالى Amemfanya mume awe kiongozi wa nyumba kwa sababu itakuwa ni wepesikwake kumuongoza mkewe. Na inabidi Muislamu anapooa Ahlul-Kitaab ajitahidiawezavyo kumuongoza katika dini ya Uislamu. Lengo kubwa kwamuislamu kuowa wakristo ni kumuongoza katika njia iliyonyooka nayo nayo ni diniya kiiislamu. Mwanamke ni dhaifu na mwepesi hivo haruhusiki kuolewa na mayahusiau wakristo. Mpaka apo nadhani nimeleweka uzuri. Allah ndie anayejua zaid

Msijidanganye wakristo wa sasa si ahalul kitab.. ahalul kitab ni wale wanaoamini agano la kale.. kwani life style yao haipishani sana na waislam mfano maamrisho ya kutokula kitimoto etcl..
 
Hapo nadhani amekujibu kulingana na mafundisho ya kiislamu, kwa hiyo ukitaka na kujadili sheria ya ndoa au sijui familia ya Tanzania utachanganya mambo sana. au bidodo?

Kabisa mkuu, hawa watu hawaendi na maneno matukufu bali wanatizama nini nafsi inataka
 
Last edited by a moderator:
Hii kitu haipo hata kidogo ndugu tena haiwezekani, wengi wanaofanya hivyo kama ambavyo amesema member mmoja hapo juu, huyo muislam atakuwa hajui thamani na vigezo vya dini ya kiislam, ndo maana inatakiwa ifike time wakristo waweze kutofautisha waislam(mfano: ISSA PONDA,AMIR FAREED, ALLY MSELEM) na watu wenye majina ya kiislam( mfano: mufti SHAABAN SIMBA,alhaj MUSSA SALUM(kadhi wa mkoa dar)). Nadhani hapo nimeelweweka!

:becky:
Mkuu hiyo mifano yako Kiboko dah!! Punguza kuhukumu bwana, huenda Allah(sw) akawajaalia kheri hao unaowaona wewe si waislamu au huenda wakawa na thamani zaidi kwa Mungu kuliko wewe.
 
Nimesoma maoni mengi, na naomba kuchangia bila ya nia ya kumkashifu Mtu au Dini hapa.
1. Nimesoma maoni ya ndoa baina ya mwislamu, mkristo na myahudi. Lakini, Mimi ni mwislamu na sijaoa katika Dini hizo Tatu.
2. Katika nchi Tajiri Hamna mume kuwa na Sauti au Nguvu kuliko mwamamme. Kila nchi inavyotajirika iwe ya kiislamu au kikristo , Ndio kina mama wanazidi kupata Haki sawa. Kwa hivyo, ni Vigumu kutegemea mwanamume awe na Sauti kubwa kuliko mwamamke nyumbani katika nchi Tajiri hasa Zenye demokrasia kamili.
3. Dini ni Imani yako, na Hamna binadamu anaweza kufuata masharti ya Dini hata asilimia 30 ya Sheria za Dini Yake. Dini ya kiislamu inakataza RIBA, pombe na inafuata sharia law. Kuna Mtu kakatwa mkono Tanzania baada ya kuiba? Basi Kama Tanzania haifuati waumini wao hawafuati Sheria za Quran. Pia kutumia dawa kuzuia Mimba na kondom ni marufuku kwa Sababu tunaingilia kazi ya Mungu. Katika maisha yakileo ni vigumu kuzaa bila ya kupanga, na mara nyingi wanawake wanafunga uzazi au wanatumia dawa, kinyume na sheria za dini yao.Kujiita mwislamu au mkristo peke Yake Haitoshi Kama hatuwezi Kuishi na Sheria Ngumu za Dini. Kwa Karne ya 21, kila nchi inavyotajirika, utakuta Imani za Dini zote zinapungua.

Nawakilisha.

Mkuu unachanganya mambo hapa. Mafundisho ya kiislamu ni jambo moja na kile kinachotokea duniani kwa sasa ni kitu kingine. Hapo juu bidodo ameongelea msimamo au taratibu za dini ya kiislamu sio vile wewe, nchi au watu wanavyoishi au kufanya. Na hili ni tatizo kubwa sana kwa sasa watu wanapenda kuchanganya kile wanachofanya waislamu na mafundisho ya kiislamu.

Tukija kwenye suala la nchi kuwa tajiri au la, sijui unaongelea nchi gani lakini Saudi Arabia ni nchi tajiri na sijasema hii ndiyo nchi hasa inayofuata uislamu ila ukienda Saudi kwa kiasi kikubwa utakuta wanafuata taratibu za kiislamu.

Halafu mkuu wewe ulishawahi kusema mahali kuwa hata kufunga ulishaacha kwa miaka kumi sasa na wala huna mpango wa kufunga. Sidhani kama msimamo huu unakuweza kukupa haki ya kusimama mahali na kuusemea uislamu.

Allah(sw) akuongoze umrejee na ujue thamani ya dini yako bi-idhinihi.
 
Last edited by a moderator:
Muislamu wa kiume anatakiwa akae na muyahudi au mkiristo (ahlul-kitab) wakiowana kwa muda maalum tu kwa ajili ya kumuongoza mkewe katika dini ya haki. Ikiwa imeshindikana atatakiwa kumuacha ila watoto watakua chini ya baba yao katika malezi ya kiislam. Kwa sababu mwanaume ndio kiongozi wa familia.

Hiyo kukaa nae kwa muda inaitwaje na katika uislam inaushahidi au ni maneno yako? Tusaidie
 
Katika uislam hakuna ndoa ya muislam na asiyekuwa wa dini hiyo. Kama ni lazima aolewe ni sharti akubali tena kwa hiari yake kuwa muislam ndipo ndoa ifungwe. Tusichanganye kati ya watu wenye majina ya kiislamu who knows nothing about the morals and values of the religion, and the true muslims. Kuzaa na mkristu haimaanishi kuwa ni mkeo, huyo ni mzinzi mwenzio na huyo mtoto katika dini hatambuliki.
HUU NDIO UKWELI

Umemaliza kila kitu. kilichobaki ni kika mwenye akili atajijibu kulingana na swali la ndoa zinazoonekana mitaani kuhusu pande hizi mbili
 
Ahlul kitabu sasa hv hawapo kwani ahlul kitabu hawasemi kuwa yesu ni Mungu nw kuna washirikina

Thats my point wakristo wa agano jipya si watu wakitabu waliozungumziwa kwenye quran tukufu na haturuhusiwi kuoa.. nakumbuka mdogo wangu wa kike alinitumia msg maana aliona aibu hata kunipigia simu akaniuliza "kaka hivi ikatokea mkristo kabadili dini na ataka kumuoa muislam nini maoni yako " ?

Kwanza nilijua yeye so alikuwa akitaka baraka tu za kaka.. nilimjibu kwa ufupi ran as far as u can kwa hao wanaobadili kwa ajili ya ndoa.. uislam ni total submition towards Allah..

I hv seen some cases mtu anabadili kwq ajili ya kuoa akiingia ndani ya ndoa pombe kama kawaida, kusali wala hasali, kitimoto, kila siku mwanamke kupigwa ndani ya ndoa vyo hivo ni kinyume na utaratibu wa dini..

Nashukuru alinielewa kaka yake now she's happy married kwa kijana wa kiislam
 
Mimi ni Muislamu na nashangazwa ninaposoma kuwa ninaishi katika Giza kwa kuwa nimeoa mwanamke na Dini hizo Tatu. Maisha yangu ni mazuri sana, mke wangu Ana Haki sawa. Guy udini upo kwenye nchi masikini tu. huwezi kusema inafuata Dini yako Wakati unakula RIBA, unampiga mke Wako au kumyima elimu mtoto Wako wa kike. Hao Ndio watu walio kwenye Giza Mpaka inapofika Ramadhan Ndio utamwona msikitini. Naomba Mtu ajitokeze na aseme anafata Sheria zote za Dini Yake. Kwa maoni yangu Dini na Maisha ya Kisasa , hasa ya nchi zilizoendelea, haziendi sambamba. Kama zikienda basi kila mwanamke angekuwa na watoto 20, msichana angekuwa na elimu, usingepokea riba benki, na wote tungelazimishwa Kuishi na Sheria za Dini Kama kanuni ya nchi. Mdini wa kweli ni Yule anayefuata Kila Sheria Sio Moja wala mbili. Wewe jaribu kumwambia mwanadada wa Leo arudi nyumbani saa unayotaka huko ulaya Kama hajakuacha, ujinga huu wa kusema mwanamume ndio mwenye Sauti zaidi nyumbani umepitwa na wakati,tuko Karne ya 21 sasa!

Mi nakuelewa sana mkuu, nimeishi kwenye hizo nchi pia. Ukiusoma vizuri uislamu utaelewa kwa nini pamoja na hayo unayosema lakini M'mungu anawaamrisha kumtii kwa kadri ya uwezo wao. M'mungu mwenyewe amesema katika Qur'an kuwa binadamu ni viumbe dhaifu sana na wenye mapungufu, kwa hiyo kukosea ni kitu kinachotarajiwa ila kila unapokosea ni vyema kuomba msamaha na kutubia. Kifupi ni kwamba perfectionism kwenye uislamu ni suala la mtu kukubali ubinadamu, kumtambua M'mungu na kuomba msamaha kila anapokwenda tofauti, sio kuwa malaika.

Kitu kingine kuwa muislamu ni hiari mkuu, kama unaona yale yanayosemwa katika uislamu ni mambo ya kizamani na hayawezekani, unaweza kuacha tu huo uislamu. Kwanza sina hakika sana kama unaweza kuendelea kujiita muislamu maana ushapingana na aya ya M'mungu inayosema kuwa wanaume ni viongozi wa wanawake katika Qur'an (Bahati siikumbuki hiyo sura wala namba ya aya, ila kama ni muhimu nitaitafuta nikuwekee).

Kingine unaongelea kuhusu masuala ya elimu kama vile uislamu unakataza kumsomesha mtoto wa kike. FYI kutafuta elimu ni excuse pekee inayomruhusu mtoto wa kike kwenda kinyume na amri za mume au baba yake. Yaani kama baba/mume anasema hakuna kupata elimu, mtume amemruhusu mtoto wa kike kwenda kinyume katika hili na kuelekea katika njia ya kutafuta elimu. Sasa sijui unaongelea vitu gani hapa.
 
Naomba kufahamu , ni kwanini Waislam hawako tayari dada/mabinti zao kuolewa na Wkristo wakati wao wanaoa dada zetu(WAKRISTO) ,,

Taqfadhali maoni.

NO OFFENCE PLEASE.

Sisi binadamu tuna hulka ya kujipendelea ktk kila hali,iwe ya kijinsia,kidini,kikabila,kirangi na kadhalika..Ndo maana utakuta kila mahali watu wanazungumzia pande fulani (UBINAFSI).Suala la kufunga ndoa ni lazima wote mke na mume wawe dini moja kwa wakati huo ndo ndoa itafungwa na kutambulika ktk dhehebu husika.Haijalishi kama ulikua mfuasi wa dini husika tokea kitambo au mpagani au umebadili dini; Hiyo ni kwa mkristo na muislam wa Tanzania japokua hapa duniani kuna dini nyingi tu ambazo TZ hazijafika,zikifika tutazijadili.

Tanzania wanawake wengi wanabadili dini na kufuata dini za waume zao (Wanawake wa kikristo kubadili kua waislam na Wanawake wa kiislam kubadili kuwa wakristo) haijalishi kama ukristo au uislam wao ni wa kweli au wa jina ila wanabadilisha dini kwa maelfu kila mwaka.Haya mambo yanatokea sehemu mbali mbali.Kimsingi mtu hafungwi na imani ya aina fulani,vitabu vya dini vinatoa mafunzo ila havilazimishi mtu,Sema sisi watu ndo tunapenda kulazimisha wenzetu tuwe watu wa dini fulani.Ukiwa mwislam lazima upende watu wote wasio waislam wawe waislam na ukiwa mkristo unapenda watu wote wasio wakristo wawe wakristo.Ukiwa mjinga mjinga wa kupokea tu vitu bila kutafakari utaona unaishi kwa shida sana hapa duniani.

Blogger
yawezekana umependa kuongelea upande mmoja au huna taarifa za kutosha kuhusu watu wanaobadili dini na kuolewa na mtu wa dini nyingine,VIZURI UENDELEE KUFANYA UCHUNGUZI ILI UJIRIDHISHE ZAIDI.
 
Mimi ni Muislamu na nashangazwa ninaposoma kuwa ninaishi katika Giza kwa kuwa nimeoa mwanamke na Dini hizo Tatu. Maisha yangu ni mazuri sana, mke wangu Ana Haki sawa. Guy udini upo kwenye nchi masikini tu. huwezi kusema inafuata Dini yako Wakati unakula RIBA, unampiga mke Wako au kumyima elimu mtoto Wako wa kike. Hao Ndio watu walio kwenye Giza Mpaka inapofika Ramadhan Ndio utamwona msikitini. Naomba Mtu ajitokeze na aseme anafata Sheria zote za Dini Yake. Kwa maoni yangu Dini na Maisha ya Kisasa , hasa ya nchi zilizoendelea, haziendi sambamba. Kama zikienda basi kila mwanamke angekuwa na watoto 20, msichana angekuwa na elimu, usingepokea riba benki, na wote tungelazimishwa Kuishi na Sheria za Dini Kama kanuni ya nchi. Mdini wa kweli ni Yule anayefuata Kila Sheria Sio Moja wala mbili. Wewe jaribu kumwambia mwanadada wa Leo arudi nyumbani saa unayotaka huko ulaya Kama hajakuacha, ujinga huu wa kusema mwanamume ndio mwenye Sauti zaidi nyumbani umepitwa na wakati,tuko Karne ya 21 sasa!

Huo ujinga unausema wewe, hakuna mahala katika Uislaam paliposema "mwanaume ndio mwenye sauti zaidi nyumbani" sijui hilo umelitoa wapi?
 
KiIslaam hakuna ndoa hapo ni zinaa tu, huyo unaezini nae ni "pangu patupu" haelewi ndee wala sikio kuhusu Uislaam.

FaizaFoxy:Nakubaliana na wewe kwa 100% kua kwa muislam hiyo si ndoa ni zinaa,Ila kwa mkristo hiyo ni ndoa halali na ina baraka na wataishi vizuri tu.Na pia mwanamke wa kikristo akibadili dini aolewe na muislam ni hivyo hivyo,wakristo watasema hiyo ni zinaa hakuna ndoa wakati huku kwenye Uislam ndoa hiyo ni halali na ina baraka tele na wataishi vizuri tu.Tumeshakua tofauti ni kawaida kusema kua ndoa ya upande mwingine ni ZINAA.Kinachotakiwa mtu binafsi uendeleze juhudi za kuelimisha watu kuhusu imani yako waijue na waifuate.
 
Mjasiria, Salaam Aleikum, Ahsante kwa maoni yako. Nimekuelewa. Swali langu ni hili: Kwa nini wewe ni Mwislamu zaidi yangu kwa kuwa unafunga na mimi sifungi? Dini ni sharia si ndio? Sasa kama wewe hufuati masharti ya dini yako, kwa nini uwaambie wengine kwamba wamepotea na warudi kwenye mwanga wakati wewe mwenyewe huwezi kufuata masharti ya dini yako. Kama nilivyosema mwanzo, hamna binadamu anayeweza kufata masharti YOTE ya dini yake. kwa hivyo kama wewe unafunga na mimi sifungi , lakini wewe hufuati sharia law Tanzania na unampeleka mkeo apewe dawa ya kuzuia mimba au kufunga kizazi basi kwa nini wewe uwe Muislamu bora zaidi wakati umeshavunja sharia ya Uislamu ya kutoingilia mambo ya Mungu? Umenipata? Katika maisha ya leo, narudia, hasa maisha ya karni hii, ni vigumu kujiita Mdini wakati huwezi kufuata sharia za dini. Hata Saudi Arabia yenyewe, watoto wa kiume wengi wanabatiliwa kwa kuwa wasichana wanafungiwa na hawana ruhusa kukutana na wanaume ambao sio ndugu zao na hamna ruhusa kutembea na mwanamme na mwanamke kama sio ndugu yako au jamaa yako. Hi ni sharia ya Kiislamu, je wewe unaishi namna hivi? Je, unapokea riba katika benki? Unatoa sadaka kamili kama inavyosema dini kila mwaka? Humtongozi mwanamke kazini au kuongea nae? Je, unakubali kukatwa mkono ukikamatwa na wizi? Kabla ya kunitenga na kuniambia mimi sio mwislamu kamili kwa kuwa sifungi, wewe pia jiangalia nafsi yako na toa jibu kamili kama wewe pia unafuata sharia ZOTE za dini yako, sio kuchambua chambua tu. Narudia, dini na maisha ya kisasa hayalingani, kama yangelingana basi tusiongetumia vidonge vya kuzuia mimba au wote tungeishi katika sharia za dini zetu ya karne ya 15. Sijui wewe, lakini mimi sitaki kuishi chini ya sharia za dini kama kanuni ya nchi kwa sababu zimepitwa na wakati wake ndio maana kuna binadamu wachache mno wanaoweza kusimama na kusema wanafuata aamri yoye ya dini zao.
 
Msifungwe nira na wasioamini. Biblia inasema wazi ktk kitabu cha Mathayo. Pia Yesu alitamka hadharani mchana kweupe kuwa Nuru na giza haviwezi kukaa pamoja. Sasa iweje mkristo ukaoe muislam? Me mpk naoa na kuruka ruka kwangu kote nilikuwa sigegedi wala kutongoza demu asiye wa dini yangu.

Bangu-silo sijiui wewe ni dini gani ila ninavyojua mimi ni kwamba dini nyingi zinasisitiza kufundisha na kueneza imani yao ktk hali ya nidhamu;shawishi watu waamini mafunzo ya imani yako.Suala la kutoa elimu ya imani yako lisiwe la kuchagua/kubagua watu wa aina fulani,fundisha mtu yoyote ambaye sio wa dini yako ili wajue na ikiwezekana wajiunge.Una haki ya kuwa na mwanamke yeyote ilimradi kama mmependana na kukubaliana kufuata masharti ya dini husika (kwa suala la ndoa) ila suala la kugegeda bila ndoa hiyo ni ZINAA haikubaliki katika mafunzo ya dini yoyote,ni DHAMBI.
 
Waislamu wanaume wameruhusika kuowa Ahlul-kitabu maana yake ni (wakristo na mayahudi) hawa ni wanawake wema miongoni mwa waliopewa kitabu“walmuhswanatu mina ladhina uutulkitaba” Mwanamke wa kiislamu haruhusiki kuolewana wakristo au mayahudi. Ni kwamba mwanamume awendiye mwenye mas-uliyah na nyumba na watoto, kwani kwa Hikma ya Allaah سبحانه وتعالى Amemfanya mume awe kiongozi wa nyumba kwa sababu itakuwa ni wepesikwake kumuongoza mkewe. Na inabidi Muislamu anapooa Ahlul-Kitaab ajitahidiawezavyo kumuongoza katika dini ya Uislamu. Lengo kubwa kwamuislamu kuowa wakristo ni kumuongoza katika njia iliyonyooka nayo nayo ni diniya kiiislamu. Mwanamke ni dhaifu na mwepesi hivo haruhusiki kuolewa na mayahusiau wakristo. Mpaka apo nadhani nimeleweka uzuri. Allah ndie anayejua zaid

Kwa kweli umemalizia maelezo yako kwa hekima sana....Allah ndie anayejua zaidi.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom