JE! MBUNGE ANAHUDHURIA BUNGENI KWA AJILI YA POSHO YA LAKI TATU AU KUTEKELEZA MAJUKUMU MAKUU MATATU YA BUNGE?
Nimesikiliza kwa makini hotuba fupi ya ndugu Nassari iliyojaa mambo mengi ya kujadili na yenye kuacha maswali.
Binafsi namfahamu ndg. Nassari tangu tukiwa wote wanafunzi chuo kikuu cha Dar es Salaam. Hivyo nampa pole kwa yanayoendelea. Hii historia ya kujirudia kwake. Mwaka 2008 akiwa naibu spika wa bunge la wanafunzi alivuliwa unaibu spika kwa mizaha tuu ya kutokufuata kanuni za bunge na DARUSO by-laws spika akiwa ndg. Mgeta.
Ninafahamu Nassari akiwa na rafiki yake ambaye ni rafiki yangu pia Jaccob Mlikuza hawakuwa wazembe darasani, hivyo Nassari alihudhuria vyema somo la filosofia ya ujenzi wa hoja, "critical thinking and argumentation" chini ya wahadhiri mahili kama Dk. Mihanjo, Dk. Lwaitama, n.k
Nilivyo msikia akilinganisha kati ya " KUHUDHURIA BUNGENI KWA AJILI YA POSHO YA LAKI TATU AU KUBAKI AKIHUDUMIA MKEWE ANGECHAGUA NINI!" binafsi nilishtuka.
Ninajua bunge lina shughuli kuu tatu. 1. kuisimamia serikali, (oversight function) 2. Kutunga sheria (Legislative function) na 3. Uwakilishi (representative function). Katika majukumu hayo, hakuna sehemu nimeona kuwa mbunge anahudhuria bungeni kwa ajili ya kupokea posho ya laki tatu bali kutimiza majukumuhayo ya bunge. Hapa pana maswali ya kujiuliza:-
1. Je! Nassari amekuwa akihudhuria bungeni kwa ajili ya posho?
2. Je! Kauli yake hiyo inawakilisha tabia na lengo la wabunge wetu kwa ujumla wakiwa bungeni?
Hotuba ya nasari ina mengi. Badaye tutajadili ile ya kupewa Ndafu Ndugai kuitumia kama sehemu ya kuomba huruma. " argumentum ad pitium"