MAONI: CCM wawe wanaangalia Rais gani wa kupewa uenyekiti wa chama chao

kmbwembwe

JF-Expert Member
Aug 16, 2012
10,428
7,216
Chama cha Mapinduzi hua wanajizimia taa na kuwa gizani mara kwa mara.

Utaratibu wao wa kumteua Rais akitoka chama chao kuwa mwenyekiti wa chama chao safari hii wameikosea Demokrasia kwa kumchagua Samia kuwa Mwenyekiti.

Kwa kawaida CCM wana utaratibu wa kidemokrasia kumchagua mgombea urais wa chama chao. Pia wana desturi na sio katiba ya CCM kumteua Rais wa Jamhuri ikiwa anatoka chama chao kua mwenyekiti wa chama chao kumrithi mwenyekiti aliyemaliza mihula yake ya urais wa Jamhuri.

Rais Samia hakuwahi kuwa mgombea, kuteuliwa kuwa mgombea urais wala hakuwahi kugombea urais ila ameupata urais kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano baada ya Rais aliyekuepo madarakani kufariki dunia.

Kwa maoni yangu aliyekua makamu mwenyekiti wa CCM bara ndiye alistahili kurithi uenyekiti wa CCM hadi kufanyika uchaguzi mwingine.

Kitendo cha kumpa kofia ya uenyekiti CCM mtu asiyekua na ridhaa ya wanachama naona kimekua hatari kabisa kwa msimamo wa chama kiitikadi na chama kuyumba kusimamia serikali ya chama chake.

Tangu ameingia Rais Samia tumeona mwelekeo tofauti kisiasa na kiuchumi utafikiri kumetokea mapinduzi au chama kipya kimeingia madarakani.
 
Unakumbuka namna ulivyotiki Kwenye karatasi Yako ya kupigia Kura 2020?
Kwani nilivyotiki nilikua na habari naye. Mimi nilikua nachagua magufuli. Ujue mgombea mwenza wala kikatiba hachaguliwi na chama ila mgombea mwenyewe.
 
Chama cha Mapinduzi hua wanajizimia taa na kuwa gizani mara kwa mara.

Utaratibu wao wa kumteua Rais akitoka chama chao kuwa mwenyekiti wa chama chao safari hii wameikosea Demokrasia kwa kumchagua Samia kuwa Mwenyekiti.

Kwa kawaida CCM wana utaratibu wa kidemokrasia kumchagua mgombea urais wa chama chao. Pia wana desturi na sio katiba ya CCM kumteua Rais wa Jamhuri ikiwa anatoka chama chao kua mwenyekiti wa chama chao kumrithi mwenyekiti aliyemaliza mihula yake ya urais wa Jamhuri.

Rais Samia hakuwahi kuwa mgombea, kuteuliwa kuwa mgombea urais wala hakuwahi kugombea urais ila ameupata urais kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano baada ya Rais aliyekuepo madarakani kufariki dunia.

Kwa maoni yangu aliyekua makamu mwenyekiti wa CCM bara ndiye alistahili kurithi uenyekiti wa CCM hadi kufanyika uchaguzi mwingine.

Kitendo cha kumpa kofia ya uenyekiti CCM mtu asiyekua na ridhaa ya wanachama naona kimekua hatari kabisa kwa msimamo wa chama kiitikadi na chama kuyumba kusimamia serikali ya chama chake.

Tangu ameingia Rais Samia tumeona mwelekeo tofauti kisiasa na kiuchumi utafikiri kumetokea mapinduzi au chama kipya kimeingia madarakani.
Kwani utaratib wao wa Rais awe mwenyekiti wao wa chama Marais wote waliopita ukoje? Na kwann iwe kwa Samia pekee ionekane haipasw? NB; Tangu lin CCM ikaisimamia serikali kikamilifu? Rejea mamikataba ya hovyo miaka kadhaa, je ilishindwa nn kuisimamia serikali? Hivi unazingumzia CCM ipi ya kuisimamia serikali? Refer wabunge wao wanavyopitisha miswada mpaka ya dharura meza zinapigwa vibao balaa!!!
 
Kwani nilivyotiki nilikua na habari naye. Mimi nilikua nachagua magufuli. Ujue mgombea mwenza wala kikatiba hachaguliwi na chama ila mgombea mwenyewe.
Mgombea huchagua majina mawili, chama kinayapigia kura kupata moja, ndivyo Magu alivyo Sema ktk mchakato wa kumpata sa100.
 
Kwani utaratib wao wa Rais awe mwenyekiti wao wa chama Marais wote waliopita ukoje? Na kwann iwe kwa Samia pekee ionekane haipasw? NB; Tangu lin CCM ikaisimamia serikali kikamilifu? Rejea mamikataba ya hovyo miaka kadhaa, je ilishindwa nn kuisimamia serikali? Hivi unazingumzia CCM ipi ya kuisimamia serikali? Refer wabunge wao wanavyopitisha miswada mpaka ya dharura meza zinapigwa vibao balaa!!!

Si ndio hapo sasa. Baada ya CCM kuanza kuzidiwa kwenye uga wa kisiasa kutokana na mabadiliko ya kizazi, ccm wamekuwa wanalazimisha kujichomeka moja kwa moja kwenye miradi ya serikali ili ionekane chama kinasimamia serikali. Ukweli ni kuwa serikali inaweza kufanya shughuli zake bila makada wa CCM kwenda kuuza sura kwenye miradi ya umma.
 
Nadhani si tu Kwa CCM Bali hata CD
M au ACT vinapaswa kuwa na katiba zinazowafanya Viongozi kuwajibika Kwa chama kinachowapa ridhaa ya uongozi.

Kutenganisha kofia ya Urais na Uenyekiti wa chama ni msingi wa usimamizi bora wa utekerezaji wa ilani na matakwa ya chama.Lakini pia Upo umuhimu mkubwa wa kiudhibiti Kwa maslahi ya nchi dhidi ya Serikali..Hasa inapokengeuka na kwenda kinyume na mkataba wa uongozi (Ilani,Katiba)..Chama chapaswa kuigiza Serikali yake,Kuikosoa,Kuisahihisha,Kuirekebisha,kuizibiti..

Changamoto ni aina gani ya wanachama waliomo ndani ya chama,Waliokishika chama,Wenye kupewa kipaumbele,Wenye nguvu na wenye sauti…Ikiwa ni wanachama maslahi,Wanachama wa uchaguzi (Kupiga kura),Wezi na wanyang’anyi,Mafisadi papa na Nyangumi,Wazalendo kindakindaki,Wazee wa takrima..Chawa…

Kama nilivyowahi kuandika juu ya utisho,Mamlaka,Madaraka makubwa na nguvu kubwa sana alionayo Mh Rais kikatiba hapa URT,Ama Kwa hakika kumpa Uenyekiti wa chama Kinachotawala Rais alieko madarakani ni kumpa umungu mtu (Uweza wa ajabu,Mamlaka kubwa mnoooo,Rungu Kuu mnoo,Sauti kubwa mnoo..Ni Mwenyezi Mungu pekee ndio anayeweza kumdhibiti kiongozi mwenye mamlaka ya kofia mbili..

Kwa ustawi wa Taifa na misingi bora ya maendeleo yatupasa kuweka bayana ktk katiba yetu ya kuwa ni Mwiko kabisa Kwa Rais wa nchi kuwa Mwenyekiti wa Chama cha Siasa..

Checks and Balance (Serikali inayoongozwa na Rais alietokana na Cham XXC vs Chama XXC)..Hili linapaswa kwenda sambamba na uchaguzi huru kweli kweli na wa haki kweli Kweli sio uchaguzi wa maruhani au mazingaombwe😃.
 
Si ndio hapo sasa. Baada ya CCM kuanza kuzidiwa kwenye uga wa kisiasa kutokana na mabadiliko ya kizazi, ccm wamekuwa wanalazimisha kujichomeka moja kwa moja kwenye miradi ya serikali ili ionekane chama kinasimamia serikali. Ukweli ni kuwa serikali inaweza kufanya shughuli zake bila makada wa CCM kwenda kuuza sura kwenye miradi ya umma.
Kbs
 
Chama cha Mapinduzi hua wanajizimia taa na kuwa gizani mara kwa mara.

Utaratibu wao wa kumteua Rais akitoka chama chao kuwa mwenyekiti wa chama chao safari hii wameikosea Demokrasia kwa kumchagua Samia kuwa Mwenyekiti.

Kwa kawaida CCM wana utaratibu wa kidemokrasia kumchagua mgombea urais wa chama chao. Pia wana desturi na sio katiba ya CCM kumteua Rais wa Jamhuri ikiwa anatoka chama chao kua mwenyekiti wa chama chao kumrithi mwenyekiti aliyemaliza mihula yake ya urais wa Jamhuri.

Rais Samia hakuwahi kuwa mgombea, kuteuliwa kuwa mgombea urais wala hakuwahi kugombea urais ila ameupata urais kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano baada ya Rais aliyekuepo madarakani kufariki dunia.

Kwa maoni yangu aliyekua makamu mwenyekiti wa CCM bara ndiye alistahili kurithi uenyekiti wa CCM hadi kufanyika uchaguzi mwingine.

Kitendo cha kumpa kofia ya uenyekiti CCM mtu asiyekua na ridhaa ya wanachama naona kimekua hatari kabisa kwa msimamo wa chama kiitikadi na chama kuyumba kusimamia serikali ya chama chake.

Tangu ameingia Rais Samia tumeona mwelekeo tofauti kisiasa na kiuchumi utafikiri kumetokea mapinduzi au chama kipya kimeingia madarakani.
Hama nchi bwana Mpina
 
Mgombea huchagua majina mawili, chama kinayapigia kura kupata moja, ndivyo Magu alivyo Sema ktk mchakato wa kumpata sa100.
Kuna hila ilipita. Mgombea mwenza ni chaguo la mgombea japo kwa busara anashauriana na chama chake.
 
Back
Top Bottom