Manji sema usiposema...

Manji sema usiposema...

Tusubiri hilo swala la manji litajulikana tu hakuna sababu ya kulaumu mtu hapo kwani hali iliyokutwa ni tata acheni wafuatilie lijulikane moja hatuwezi kujua nia ya kuwa na hivyo vitu ni nini, manji hana familia means mke na watoto still single
 
Inasemekana amekutwa na muhuri wa jeshi isivyo halali. Na pia vitambaa vya sare za jeshi. Mashtaka aliyofunguliwa ni uhujumu uchumi pamoja na kuhatarisha usalama wa taifa.

Nadhani ana mengi ya kusema kama atabahatika kuendelea kuwepo.

Je alikuwa na utaratibu wa kufanya hivyo kila mara?

Vitambaa hivyo vilikuwa vikipelekwa wapi? Kazi haswa ya huo muhuri ni nini?

Maana sasa kuna shtaka la uhujumu uchumi na usalama wa taifa. Sasa kwenye usalama wa taifa sijui tatizo liko wapi, kwani hizo sare zilitakiwa kupelekwa kwa wanajeshi waasi ama kikundi chochote cha uasi? (Mh rais ameshawahi kulihuisha na mauwaji ya kibiti pamoja na mashehe walioko lockup)

Wafanye wafanyacho ila cha muhimu haki itendeke, msumeno wa sheria ukate kotekote.

Yani hata kama kuna walioshirikiana naye na wako kwenye vyombo vya madaraka wabanwe. Unless rais aliyepo ana mpango wa kukaa madarakani maisha yake yote.

Kwasababu huwezi kumkuta na makosa na kumuhukumu kama ameshirikiana na vigogo halafu ukawafumbia macho vigogo hao na hukumu ikawa ya haki.

Kwa upande mwingine pia, asiwe amebambikiwa. Lakini kama vinahusiana na ugaidi ama jitihada za uasi, basi hilo ni suala jingine kabisa.
Wewe ulivyoandika Ni kama vile tayari umetoa hukumu..kesi iko mahakaman tusubirie maamuzi ya mahakamani,katika utawala huu lolote linawezekana maana mambo ya kubambikiziana kesi yameshika hatamu.
 
Wacha ashuhulikiwe hawa wahindi ilifika kipindi wao wanatuamulia rais Kwa ela zao mtu anatoka uzunguni alikokulia anaenda mbagala Kwa maskini anawanunua Kwa pesa zake na kujidai eti anajua matatizo Yao mimi najiuliza mbagala hawana kijana wao waliomlea anayeyaishi maisha Yao? Mpaka wanaenda kumchagua gapachori? Ama Kweli umaskini mbaya sana
Acha wivu usikua na maana,Ni wabunge wangapi wamekulia dar tena wengine wanaishi kabisa wametoka wamerudi uko vijijini na kuwa wabunge!!acha ubaguzi usokuwa na msingi!
 
Wewe una uhakika amekamatwa na sare za jeshi? Au umewasahau polisi wa kibongo kwa kubambikia kesi wanazopenda? Na ikichangiwa na bifu na bashite na mkuu wa kaya, ni bahati yake kama hajapewa kesi ya ukamanda wa Kibiti.
Mihuri inaweza kumbambikia kuna kitu kimejificha hapo hapo yafaa uchunguzi wa kina ufanyike.
 
Inasemekana aliwahi kumjibu Dereva wa sasa kwamba hawezi kuongea na mbwa anaongea na mwenye mbwa. Sasa hatujui ndio analipia kauli zake sasa ama.laa

Kwa hiyo ndio analipia kwa kujimilikisha mihuri na sare za JWTZ sio?!
 
Namba lazima tuisome woteeee....nape kaisoma, kinana kaisoma, manji njia moja na bado......tuliwabia ccm ni mbwa na ni ukoo wa panya hamtaki kisikia....

HAPA NI NISASI TUUUUU....MCHEZEA ******** WEWE

Uwe unafikiri basi hata siku moja moja tu!!!!
 
Unapomchukua nyoka angali mdogo na kumweka chumbani mwako, jua iko siku atakuwa mkubwa na bila shaka kama ni chatu jiandae kumezwa! Sisi tuendelee kuchekelea na kucheka lakini iko siku na sisi yatatukuta!
 
Wewe ulivyoandika Ni kama vile tayari umetoa hukumu..kesi iko mahakaman tusubirie maamuzi ya mahakamani,katika utawala huu lolote linawezekana maana mambo ya kubambikiziana kesi yameshika hatamu.
Hii awamu ya 5 mshauri mkuu wa Magufuli ni Daud Bashite ambaye bado ni kujana mwenye Roho ya kufurahia kukomoana ni Tabia za kukomoana zimapandikizwa ni hatari sana Nchi imekuwa ya Kesi kesi kila kona, kesi kwa Wapinzani na kesi kwa wale wenye visasi vya mambo yao binafsi huko nyuma, pia ikumbukwe kuwa Daud Bashite amekuwa akifurahia wimbi la matukio ili watanzania wawe busy huko wapate kumsahau na vyeti vyake feki, mda mwingi hutumia kutengeneza Skendo na kumpelekea Baba Jesca wanalianzisha Dude mpaka kufika 2020 kutakuwa na matukio lukuki na kesi utitiri zinazoundwa na kuratibiwa na kikundi kinachoongozwa na Bashite kwa sasa.
 
Tusubiri hilo swala la manji litajulikana tu hakuna sababu ya kulaumu mtu hapo kwani hali iliyokutwa ni tata acheni wafuatilie lijulikane moja hatuwezi kujua nia ya kuwa na hivyo vitu ni nini, manji hana familia means mke na watoto still single
Awe na mtoto asiwe na mke hiyo inakuhusu nn? Mbona unakuwa kama matambo
 
Wamegundua watanzania ni wepesi wa kusahau ya nyuma ndiyo maana kila kukicha wanaibua mapya ili watanzania wasahau vyeti vya Daud Bashite, ununuzi kivuko feki, ununuzi ndege kwa cash, ujenzi wa reli, ukarabati wa bandari, ujenzi chato international Airport ambapo mikataba yake haijapelekwa Bungeni ijadiliwe kwa Ligha ingine hilo ni jipu ambalo litakuja kutumbuliwa na Rais wa awamu ya Sita kwani wa sasa yy kaamua kusonga mbele kwa kufunika kutumia Kesi kesi kwa Wapinzani na wengineo wenye visasi nae huko nyuma:
 
Acha wivu usikua na maana,Ni wabunge wangapi wamekulia dar tena wengine wanaishi kabisa wametoka wamerudi uko vijijini na kuwa wabunge!!acha ubaguzi usokuwa na msingi!
Kama mimi mbaguzi nenda India kagombee udiwani ndio Utajua mimi na wao nani mbaguzi Alafu inaonyesha wewe ni mmoja wao ulikua unakula kupitia hao magapachori sasa unaanza kulialia baada ya bosi wako kukutana na mkono wa sheria katafute kazi nyingine ya kufanya
 
Mwanasiasa mwanachama wa CCM na Diwani wa Kata ya Mbagala Kuu Yusuph Manji inawezekana ndiye Diwani pekee wa CCM ambaye anakumbana na misukosuko mingi sana katika siku za karibuni. Lakini watu kadhaa wanadai kwamba Manji anajua nini kinaendelea dhidi yake.

Kama nadharia kwamba Manji anajua kinachoendelea dhidi yake ni ya kweli, basi ni yeye mwenyewe ndiye mwenye uwezo wa kusema ukweli ni nini hasa kinachoendelea ili ajinasue kutoka wenye mtego uliomnasa.

Yanga, Coco Beach, Quality Group of Companies,siasa ama ni nini hasa!?
Manji sema tu, wala usiogope. Haiwezekani leo asomewe mashtaka ya uhujumu uchumi, nyie waendesha mashtaka kweli hizo chaji mnazifungua baada ya kujilighisha au ni maagizo, angalieni lakini. Mungu hazihakiwi na uogo ni dhambi na hofu ni kifo. Manji sema, maana mwoga hufa, na jasiri hufa vilevile sema basi uwe jasiri na ufe!!! Kulioko kuwa mwoga na ukafa pia. Nakusihi kwa jina la Yesu Kristo akupe ujasiri na useme yote. Maana kuna kitu kinaonekana kipo nyuma yako.
 
Awe na mtoto asiwe na mke hiyo inakuhusu nn? Mbona unakuwa kama matambo
Kila awamu huwa na mbinu zake za kutawala lakini hii awamu yenyewe chaguo lao ni kesi kesi kesi mpaka 2020 inafika kutakuwa na kesi mpaka mahakamani kutajaa faili walazimike kujenga godauni zingine za mafaili.
 
Ni hivi Manji alikuwa supplier wa JWTZ wa vitambaa vya jeshi ktk kipindi kilichopita.. kama ujuavyo majeshi yetu mambo mengi hufanya wazabuni hata chakula hupika wasio wanajeshi yaan wazabuni... so Magufuli yy hataki hiyo biashara lkn kumbuka mzabuni ana mkataba wake hapo ndipo tatizo lilipo.. pia MANJI ndio SUPPLIER WA TRANSFORMA ZOTE KWA TANESCO hapo pia magufuli hataki lkn jamaa ana mikataba halali.. kwa kifupi DEREVA NI MASIKINI HIVYO HAPENDI MATAJIRI.......
hizi tenda wewe ndio uliompa mkishavimbiwa kahawa chini ya turubahi na juu ya benchi kila linalokuja tu mnasave.

Kukusaidia tu majeshi hayaagizi majora kama aliyokutwa nayo Manji bali full whole uniform na muagizaji sio yeye na haziagizwi nje huu ni mwaka wa pili.

Tanalek iliyopo nchini ndio supplier Mkuu wa transformers tanesco hizo za Manji unazijua wewe.
 
Inawezekana muhuri ulikuwa ukihusika na masuala ya "logistics" na "clearance" jule bandarini.

Si unafahamu mizigo ya jeshi huwa inapungiwa mkono tu na inapita au hufahamu hilo?

Halafu kumbuka hotuba ya kwanza ya waziri wa fedha alipozungumzia vyombo vya usalama na misamaha ya kodi kwa bidhaa zinazoingizwa nchini.

Unganisha dots hapo.
Unajua matumizi ya mihuri lakini?
Kila muhuri lazima una post signatory in accordance kama muhuri ni wa mwenyekiti wa kijiji lazima na handsign yake au fingerprints iambatane along the stamp sasa Manji ana mamlaka gani jeshini na ana sign kama nani kwenye stamp za majeshi?
 
Naumwa sana kichwa, hivi nikitumia chroquine, panadol, aspirin, cafenol, cetrizen na metacefin kwa wakati mmoja inakuwaje?
 
Kama mimi mbaguzi nenda India kagombee udiwani ndio Utajua mimi na wao nani mbaguzi Alafu inaonyesha wewe ni mmoja wao ulikua unakula kupitia hao magapachori sasa unaanza kulialia baada ya bosi wako kukutana na mkono wa sheria katafute kazi nyingine ya kufanya
Wewe ujielewi kabisa kwahiyo shida Ni gabachori kuwa Diwani ndo maana anabambkiziwa kesi..kwanza inabidi ujione mpumbavu gabachori kakukuta hapa kwenu afu bado anakuzidi hela!!
 
Back
Top Bottom