Manji sema usiposema...

Manji sema usiposema...

Inasemekana amekutwa na muhuri wa jeshi isivyo halali. Na pia vitambaa vya sare za jeshi. Mashtaka aliyofunguliwa ni uhujumu uchumi. Nadhani ana mengi ya kusema kama atabahatika kuendelea kuwepo. Je alikuwa na utaratibu wa kufanya hivyo kila mara? Vitambaa hivyo vilikuwa vikipelekwa wapi? Kazi haswa ya huo muhuri ni nini?

Maana sasa kuna shtaka la uhujumu uchumi na usalama wa taifa. Sasa kwenye usalama wa taifa sijui tatizo liko wapi, kwani hizo sare zilitakiwa kupelekwa kwa wanajeshi waasi ama kikundi chochote cha uasi?

Wafanye wafanyacho ila cha muhimu haki itendeke, msumeno wa sheria ukate kotekote. Yani hata kama kuna walioshirikiana naye na wako kwenye vyombo vya madaraka wabanwe. Unless rais aliyepo ana mpango wa kukaa madarakani maisha yake yote. Kwasababu huwezi kumkuta na makosa na kumuhukumu kama ameshirikiana na vigogo halafu ukawafumbia macho vigogo hao na hukumu ikawa ya haki.

Kwa upande mwingine pia, asiwe amebambikiwa. Lakini kama vinahusiana na ugaidi ama jitihada za uasi, basi hilo ni suala jingine kabisa.

Duh!

Kama ni kweli basi atakuwa ni bonge la zumbukuku.

Hajui kuwa sasa kuna sheriff mpya hapa mjini?
 
Mwenzie aliona mapeeema kabisa hali si hali, akauza kampuni akaachia na ngazi kwenye kilabu cha soka maarufu hapa nchini akatimua
 
Duh!

Kama ni kweli basi atakuwa ni bonge la zumbukuku.

Hajui kuwa sasa kuna sheriff mpya hapa mjini?
Nyani Ngabu umenena sawa kabisa na WaTZ tuna vichwa vilivyojaa maji hatusomi alama za nyakati.

Polisi wanatangaza kufuata sheria pasipo shurti, sisi ni sikio la kufa hatusikii dawa.

Awali tulidai na kulalamikia kwamba vyombo husika havisimamii utii wa sheria. Sasa vyombo hivyo vinatimiza wajibu wake NAMBA TUNAISOMA.

Wenzetu humu tujihadhari na maneno au lugha tunayotumia, pamoja na kuandika mambo tusiyo kuwa nayo uhakika, tutaisoma namba. Na ukifikishwa huko ni wewe peke yako, ukiacha nyuma familia yako kwenye mashaka na majonzi.
 
Jamaa anasafisha masaria ya mkwere na lowasa, ila sizani kama atayamaliza atastukia uchaguzi tu ushafika hivyo na kubakiwa na mbinu moja tu ya kupora ushindi ili aendelee kutawala.

kuna ka ukweli hapa noted.
 
Manji si Diwani wa CCM? Mbona anapeta shida kama Mbowe? Hata hivyo Manji hatokaa amsahau RC wa Dar 2017. Alijidai kuzoza naye badala ya kufagia Nyumba yake.

Mali zimekutwa kwenye Maghala ya Quality Group, kesi kafunguliwa Yusuph ambae Officially alishatangaza kuachia Ngazi Quality Group na kubaki Mshauri tu!

Hii kesi ni Nyepesi sana Kama Mahakama zingekuwa zinaendeshwa kisheria sio Ki amri
 
Nawaza hivi Mo Dew, Mengy, Abu ud, Barehhessa watakuwa wanawaza nini wanapoona haya yanayotokea kwa Josefu Minja na Frimani Mbowwe
 
Back
Top Bottom