Maneno ya kejeli ya mume wangu

Maneno ya kejeli ya mume wangu

Mungu akujalie hekima katika hili!
Hivi jitu lenyewe hata halilali nyumbani hata huyo mtoto atapatikanaje?
 
Pole dada ila u mvumilivu....me nadhani chagua furaha yako....kama unahisi utaweza vumilia mikiki mikiki yake for the rest of your life tulia nae. Ila kama unaona mbele giza sepaa tuu!! alitakiwa kukutia moyo kwa kutokuwa na mtoto nasio kukunyanyasa.
 
Toka hapa...una matatizo sana ndo maana huzai

No, nadhani this is the stupidiest reply ever kwenye hii mada, ishu ya kuzaa au kutokuzaa kashaeleza huyu mwanamke sio vyema kumjibu kipumbavu hivi,wanawake mliokosa wanaume mbona mnakua na majibu mabaya hivi. sio yeye aliesababisha usiolewe dada, kua na staha na wanawake wenzako.
 
mh!!! ninavyojijua mimi! ningekuwa hata nilishasahaugi kuwa niliwahi kuolewa na huyo mtu! kha! kama kuna kitu siwezi vumilia duniani ni 'kudhalilishwa'. Yaan...dah! BWANA niepushe na jaribu kama hili, maana wanijua vyema kiumbe wako! loh
 
Duuu!!! Katika siku ya leo tazama au sikiliza mwimbo wa Christina shusho mapito kisha unipm
 
aise dadangu una limoyo,ningekuwa ni mimi ningeshajiweka pembeni muda,kama vipi muache tu kwani ye amekuwa kiroba cha unga kwamba ukimkosa utakufa njaa? aiiiih!
 
haya mambo haya! puuuuuuuuuuuuuu! Asprin hebu tuonane baadae tukazie ndoa yetu! kuna mwenye swali??

Mwenye swali ntadeal naye mimi wife. We tangulia, uwashe AC kabisa. Mi nshajinywea grants za kutosha.

Nikukute without puliiiiz...
 
hiyo kazi ni ndogo dada yangu,niPM nikupeleke kwa mganga.huyo atakuwa anakupikia,anakufuria na vyote unavyotaka niPM tafadhari

Duuh usimdanganye mwenzio kama ni wa ki dunia Mganga mzuri na mkweli ni Yesu tuu. Waliobakia wote ni matapeli tuu... Thanks...
 
Habari za asubuhi wapendwa,

Mimi ni member wa Jamii Forum kwa muda mrefu ila nimesajili ID mpya kwa sababu maalum na hayo niliyooyandika ni ya kweli na ndio hali halisi

''Unaroho mbaya ndio maana huzai'' ''Najuta kwa nini nilikuoa wapenzi wangu wa zamani ni bora kuliko wewe'' nilikuoa kwa kukuonea huruma''. Haya ndio baadhi ya maneno ya kejeli ambayo nilishawahi kuambiwa na mume wangu.

Mimi ni mwanamke mwenye umri wa miaka 36, nimeajiriwa na mume wangu ana shughuli zake binafsi. Nina miaka minnne ndani ya ndoa ila sijabahatika kupata mtoto kwa sababu nimegundulika nina (Polycystic Ovarian Disease (PCOD) na mume wangu kuwa ana low sparm count.

Mume wangu amekuwa ni mtu wa kurudi usiku mara nyingi kuanzia saa sita, siku nyingine analala huko bila hata kuniambia na hata ukimpigia simu hapokei. Asubuhi anakuja anakuambia tulikuwa tuna biashara tunafanya na simu niliacha kwenye gari. Tukawa tunagombana kwa ajili hiyo hadi tukalifikisha kwa wazazi akagombezwa aakaacha kwa uda lakini karudia tena.

Siku moja alilala tena nje bila taarifa, nikampigia simu hakupokea, ilipofika alfajiri nikapigiwa na mwanamke simu akaniambia acha kusumbua waume za watu, niko naye hapa. Kama ni mumeo mbona hayuko kwako? Kidogo nizimie ila nikapiga moyo konde. Alivyorudi nikamuuliza akasema tulikuwa naye kwenye biashara kwa hiyo alikuwa na simu zetu.

Khaaa nikamwabia mdanganye mtoto ile sio mimi. Baada ya mwezi mmoja akanunua mzigo kumbe ulikuwa wa wizi akakamatwa na polisi, akaniambia mke wangu nimekamatwa kesho njoo polisi kijitonayama, hapo ilikuwa usiku. Kesho asubuhi naenda polisi kumpeleke breakfast nikaambiwa mbona mkewe kaja kuleta chai! Nikwwmbie polisi mbona mimi ndio mkewe halali? Nilidhalikika kwa kweli nikaondoka na chai yangu. Bahati nzuri nilikuwana ndugu zangu ambao ni polisi tena wana vyeo hapo kituoni, nikaweza kufuatilia hadi kesi ikaishia polisi.

Siku hiyo ya kutoka ilikuwa mida ya saa kumi na mojo, muda huo nilikuwa natoka kazini, nikawapigia maafande wakasema mume wako ameshatoka. Nikajaribu kumpigia simu yake haipatikani, kesho yake anarudi nymbani ananiambia polisi waliturudisha ndani. Nikamwabia acha uongo mie ndugu zangu walinihakikishia kama umetoka, akabisha katakata, ila mtu mwenye akili unajua ukweli.

Baada ya mwezi hivi nikwambia twende kwenye send off ya mtoto wa jirani yetu akadai amechoka, akaniambia huwa unapenda kushadadia vya watu wengine mbona mjomba wangu mke wake kajifungua hujaenda kumsalimia? ''Una roho mbaya na hutaweza kupata mtoto'' mimi huyoo nikaodoka zangu na majirani wengine. Kumbe siku hiyo walitibuana na huyo hawara wake.

Nimerudi kalala fofofo, simu yake inaita tuu. Kwa sababu yule mwanamke alishanipigia na kunitolea mbovu namba yake niliishika. Sikupokea simu kwa sababu sinaga tabia ya kupokea simu ya mume wangu.

Wazo likanijia nikaangalia messege, nikakuta huyo dada anamwabia kume una mkehukuniambia mimi na wewe basi. Kesho yake nikampigia huyo mwanamke akaniambie story yoote na ile siku aliyotoka polisi kumbe alilala kwake. Akanimbia mimi nilidanganywa na mumeo kwamba hana mke, na nilishawahi kuja hapo nyumbani pindi ukiwa umesafiri. Na kwa vile nimeujua ukweli simuhitaji tena huyo mwanaume, na roho inaniuma kutembea na mume wa mtu kitu ambacho kinaniumiza ila sikujua naomba unisamehe.

Pamoja na hayo yote anakataa katakata kuwa hana uhusiano na yule dada. Eti ''huyu dada ni girl friend wa rafiki yangu wamegombana ndio ananiforwadia hizi messege.''

Na hii sio mara ya kwanza alishawahi kuwa na mwanamke mwingine akamdanganya kuwa hajaoa hadi huyo mwanamke akaja nyumbani kuhakikisha ndio akaujua ukweli. Pindi anapokuwa na michepuko kejeli haziishi mara najuta kwa nini nilikuoa, nimekuoa kwa kukuonea huruma etc. Hizi kejeli huwa nikizikumbuka nakosa raha kabisa. Na tendo la ndoa tunaweza kufanya mara mbili kwa wiki kila akija amechoka.

Niko njia panda naona nimemchukia mume wangu ghafla, majukumu mengine ya nyumbani nafanya kawaida kama mke .

Kila mara nafikiria uamuzi wa kuachana naye lakini najiuliza is it a right decision:

Naombeni ushauri ndugu zangu wenye uzoefu na haya mambo.

Nawakilisha na mnakaribiswa kwa michango yenu

Binti,

Unapoteza muda hapo, huyo bwana hatakufaa kwa shida wala kwa raha...

Ukizingatia kwamba bado hujapata mtoto, ni fursa safi ya ku-move on na nina imani kwamba you will get kids ukitulia na kufocus kwenye matibabu, kazi na mapenzi mapya

You'd rather be alone that a person who ruins your life

Hapo sijazungumzia hatari za magonjwa na mikosi mingine
 
Jamaa anachezea shilingi chooni ukiondoka atajuta
 
Mimi leo nilikua nafikiria kama yasingekua matatizo yaliyonipata nisingejua ukuu wa Mungu. Leo hii natambua kua ukiwa kwenye matatizo ndo wakati wa kumuhitaji Mungu zaidi. Maana biala hayo matatizo huwezi jua ukuu wa Mungu katika maisha yako. Hata bila hayo matatizo huwezi kusimulia wengine ukuu wa Mungu kwa ushuhuda ambao umeuona kwa macho yako ya nyama.

Mungu hawezi kuja physically kwako, watu wengi wamekutana na Mungu live walipokua kwenye matatizo kama yako. Jaribu kufuatilia ya watu ambao leo hii ni mashuhuri walikutana na changamoto katika maisha yao. Mimi wakati mwingine naangalia ndoa ya cliton na kusema kunawakati matatizo ni changamoto tu katika maisha. Ukikumbuka clitton alipata kasfa kubwa ambayo ingekua kwa mwingine mkewe angekua alishoondoka na hakuna ndoa. Angalia leo hii ndoa ya clitton ni moja ya ndoa strong duniani.

Pia hua nafikiria silaha ya upendo katika maisha ni best silaha kuliko zote. Mimi nafikiria tu kama KIng Martin Luther angetumbia jino mkwa jino principle, kungekua na Rais mweusi marekani?. Jibu ni hapana kwa mawazo yangu kwani asingeshinda vita, angekufa kabla hajamaliza kazi iliacha historia yake katika dunia hii. Hivyo upendo no silaha kuu katika kila jambo na upendo unathawabu kubwa sana kama unampenda mtu anaekuchukia na kukuudhi. Ikifika kesho atajua kua yeye alikosea na ukuu wa Mungu utaonekana katika maisha yenu.

Hivyo kifupi tu, upendo ndo silaHA KUBWA na namaanisha upendo wa kweli. Na upendo wa kweli huja baada ya msamaha wa klweli kutoka moyoni. Nakushauri msamehe kwa yote alikwisha kukutendea na ambayo bado hajakutendea, muoneshe kua unampenda lakini mwambie Mungu wako anampenda zaidi kuliko wewe upendavyo. Lakini pia jua kua unamuhitaji Mungu zaidi kuliko chochote maana hata watu hawawezi kukusaidia, msaada wa kweli uko kwa Mungu tu. Na upendo wa Mungu kwetu sisi hauna kipimo na unaanzia pale msalabani alipomtoa mwanae wa pekee ili afe kwa ajili yetu. Ni nani hawezaye kukupenda kiasi hiki? ukipata majibu utajua upendo wa Mungu.

Na ukuu wa Mungu unaangaliwa kwa kukumbuka aliyokutendea kabla, kama ameweza kukuweka hapo ulipo ujue anaweka kukupeleka mbele zaidi. Mkumbuke ayubu majaribu aliyokutana nayo hakuna mtu anaweza kuyaweza katika dunia ya leo, hivyo wewe jaribu lako ni dongo sana, unamuhitaji Mungu zaidi. Kwani ayumbu pamoja na hayo yote hakumuacha Mungu alipokimbiwa na mke wake hakumuacha Mungu, alipofiwa na watotowote, hakumuacha Mungu. Hivyo ni nini kitutenge na upendo wa Mungu? hakuna!

Unamwitaji Mungu zaidi, anzia kwenye msamaha kwa kusamehe wengine wanaokutendea mabaya, halafu rudi kwa Mungu akusamehe na uanze safari mpya ya matumaini ya kwenda mbinguni. Maana hakuna binadamu atakupa suluhu katika tatizo lako, mkimbilie Mungu tu. Ukisamehe linafuata hapo ni upendo, hii ndo nguzo kuu ya mahusianao yetu na Mungu. Maana Mungu anasema huwezi kumpenda yeye usipompenda binadamu unaemuona. Baada ya kuanza maisha mapya na Mungu tegemea kupata ushuhuda mkubwa katika maisha yako kama sala na abrahamu walivyopata ushuhuda wao uzeeni sana, wakati kila elimu ya dunia inakataa. Ikiwa ngumu kusamehe anza kuomba Mungu akupe roho ya kusamehe, maana yeye ndo msaada wetu.


Habari za asubuhi wapendwa,

Mimi ni member wa Jamii Forum kwa muda mrefu ila nimesajili ID mpya kwa sababu maalum na hayo niliyooyandika ni ya kweli na ndio hali halisi

''Unaroho mbaya ndio maana huzai'' ''Najuta kwa nini nilikuoa wapenzi wangu wa zamani ni bora kuliko wewe'' nilikuoa kwa kukuonea huruma''. Haya ndio baadhi ya maneno ya kejeli ambayo nilishawahi kuambiwa na mume wangu.

Mimi ni mwanamke mwenye umri wa miaka 36, nimeajiriwa na mume wangu ana shughuli zake binafsi. Nina miaka minnne ndani ya ndoa ila sijabahatika kupata mtoto kwa sababu nimegundulika nina (Polycystic Ovarian Disease (PCOD) na mume wangu kuwa ana low sparm count.

Mume wangu amekuwa ni mtu wa kurudi usiku mara nyingi kuanzia saa sita, siku nyingine analala huko bila hata kuniambia na hata ukimpigia simu hapokei. Asubuhi anakuja anakuambia tulikuwa tuna biashara tunafanya na simu niliacha kwenye gari. Tukawa tunagombana kwa ajili hiyo hadi tukalifikisha kwa wazazi akagombezwa aakaacha kwa uda lakini karudia tena.

Siku moja alilala tena nje bila taarifa, nikampigia simu hakupokea, ilipofika alfajiri nikapigiwa na mwanamke simu akaniambia acha kusumbua waume za watu, niko naye hapa. Kama ni mumeo mbona hayuko kwako? Kidogo nizimie ila nikapiga moyo konde. Alivyorudi nikamuuliza akasema tulikuwa naye kwenye biashara kwa hiyo alikuwa na simu zetu.

Khaaa nikamwabia mdanganye mtoto ile sio mimi. Baada ya mwezi mmoja akanunua mzigo kumbe ulikuwa wa wizi akakamatwa na polisi, akaniambia mke wangu nimekamatwa kesho njoo polisi kijitonayama, hapo ilikuwa usiku. Kesho asubuhi naenda polisi kumpeleke breakfast nikaambiwa mbona mkewe kaja kuleta chai! Nikwwmbie polisi mbona mimi ndio mkewe halali? Nilidhalikika kwa kweli nikaondoka na chai yangu. Bahati nzuri nilikuwana ndugu zangu ambao ni polisi tena wana vyeo hapo kituoni, nikaweza kufuatilia hadi kesi ikaishia polisi.

Siku hiyo ya kutoka ilikuwa mida ya saa kumi na mojo, muda huo nilikuwa natoka kazini, nikawapigia maafande wakasema mume wako ameshatoka. Nikajaribu kumpigia simu yake haipatikani, kesho yake anarudi nymbani ananiambia polisi waliturudisha ndani. Nikamwabia acha uongo mie ndugu zangu walinihakikishia kama umetoka, akabisha katakata, ila mtu mwenye akili unajua ukweli.

Baada ya mwezi hivi nikwambia twende kwenye send off ya mtoto wa jirani yetu akadai amechoka, akaniambia huwa unapenda kushadadia vya watu wengine mbona mjomba wangu mke wake kajifungua hujaenda kumsalimia? ''Una roho mbaya na hutaweza kupata mtoto'' mimi huyoo nikaodoka zangu na majirani wengine. Kumbe siku hiyo walitibuana na huyo hawara wake.

Nimerudi kalala fofofo, simu yake inaita tuu. Kwa sababu yule mwanamke alishanipigia na kunitolea mbovu namba yake niliishika. Sikupokea simu kwa sababu sinaga tabia ya kupokea simu ya mume wangu.

Wazo likanijia nikaangalia messege, nikakuta huyo dada anamwabia kume una mkehukuniambia mimi na wewe basi. Kesho yake nikampigia huyo mwanamke akaniambie story yoote na ile siku aliyotoka polisi kumbe alilala kwake. Akanimbia mimi nilidanganywa na mumeo kwamba hana mke, na nilishawahi kuja hapo nyumbani pindi ukiwa umesafiri. Na kwa vile nimeujua ukweli simuhitaji tena huyo mwanaume, na roho inaniuma kutembea na mume wa mtu kitu ambacho kinaniumiza ila sikujua naomba unisamehe.

Pamoja na hayo yote anakataa katakata kuwa hana uhusiano na yule dada. Eti ''huyu dada ni girl friend wa rafiki yangu wamegombana ndio ananiforwadia hizi messege.''

Na hii sio mara ya kwanza alishawahi kuwa na mwanamke mwingine akamdanganya kuwa hajaoa hadi huyo mwanamke akaja nyumbani kuhakikisha ndio akaujua ukweli. Pindi anapokuwa na michepuko kejeli haziishi mara najuta kwa nini nilikuoa, nimekuoa kwa kukuonea huruma etc. Hizi kejeli huwa nikizikumbuka nakosa raha kabisa. Na tendo la ndoa tunaweza kufanya mara mbili kwa wiki kila akija amechoka.

Niko njia panda naona nimemchukia mume wangu ghafla, majukumu mengine ya nyumbani nafanya kawaida kama mke .

Kila mara nafikiria uamuzi wa kuachana naye lakini najiuliza is it a right decision:

Naombeni ushauri ndugu zangu wenye uzoefu na haya mambo.

Nawakilisha na mnakaribiswa kwa michango yenu
 
Pole sana , chukua likizo ya ndoa.

Hata akichukua likizo ya ndoa bado furaha ya maisha yake hayapo, kwani hata huyo mume Mwengine akipata jee kuna uhakika gani ya kupata mtoto? Wanaume ambao hawajapata watoto sio rahisi kuivumilia ndoa bila ya mtoto, ni ngumu sana sana.
Suala langu kwako, jee mulichukua hatua gani kukabiliana na matatizo yenu ya kupata mtoto?

Mumeo ana stress za kutopata mtoto hivyo cha kufanya wewe kwanza kukaa na mumeo ongea nae vizuri mpe matumaini.

Jengine nendeni kwa wataalamu wa masuala ya kupata mtoto, kuna njia za kitaalamu za kupata mtoto. In sha Allah mutapata mtoto.

Kwa mungu hakuna kubwa, kuna mtu ambae namjua, alikaa muda mwingi bila ya kupata mtoto, walifika India kwa ajili hio lakini haikufua dafu, itapita kama miaka 2 hivi Allah akawajalia mtoto, hivi sasa wana watoto wawili chap chap baada ya kusafa muda mrefu.

Nikuulize suali Jengine? Jee mumeo nae ana miaka mingapi umri wake?
Nayo pia inachangia kuchelewa kupata mtoto kutoka kwa mwanamme ambae umri wake mkubwa na kuchelewa kuzaa mapema, hilo nimefanya uchunguzi, tatizo sio wewe hata mumeo tatizo.

Kama kidume kweli mbona hao wanawake zake njee hakuna alie zaa nae kama kweli yeye hana tatizo?

Hivyo nakuomba kaa na mumeo, jadilini kwa kina suala hili, ndoa inahitaji uvumilivu mkubwa.

Jengine zaidi kuwa makini na hili jonjwa la siku hizi,asije kukupatia, kama unaona ni hatari kwako usidai talaka, nenda nyumbani kwa wazazi wako pumzika mpaka pale atakapo kuwa tayari mumeo kukuhitaji na kubadilisha tabia yake. Tena hayo kwa makubaliano baina yako na yeye na wazee kama ma judge.

Shukran
Nakutakia ndoa njema
 
kwani nyie wanawake huwa nasikia mara tunakutana kimapenzi na mume wangu mara mbil tu kwa wiki!!!. ivi kiuharisia huwa mnataka kufanya mapenzi na waume zenu mara ngapi kwa wiki?. wanaume wengi hawapendi kufanya mapenzi kila siku, na ata akifanya ni miezi miwili anabadilika ratiba.
 
Tafuta Kidumu aiseeee,au nawe akitoka nawe toka jino kwa jino,aone uchungu wa kugongewa
 
kwani nyie wanawake huwa nasikia mara tunakutana kimapenzi na mume wangu mara mbil tu kwa wiki!!!. ivi kiuharisia huwa mnataka kufanya mapenzi na waume zenu mara ngapi kwa wiki?. wanaume wengi hawapendi kufanya mapenzi kila siku, na ata akifanya ni miezi miwili anabadilika ratiba.

Labda wewe mlo mmoja, sisi wanaume wengine tuna gonga kila siku anytime hata mchana, hata sebule, jikoni unakopata. Hivi umekaa na kuandika upuuzi huu?
 
Back
Top Bottom