Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Umeongea kwa akili kubwa sana mkuu kacnia Bruno ni tatizo kubwa kwa sasa. Nikikumbuka zile faulo mbili za hovyo alifanya kwenye uefa na zote zikazaa magoli tukaondolewa na juzi kwa Aston Villa kafamyavtena faulo wakapata goli la kwanza. Huyo mtoto wa miaka 19 anacheza dakika 80 na hasababishi faulo yoyote.
 
Nadhani kuna mpango mkubwa sana wa kupandisha vijana kutoka kwenye academy. Ukifuatilia utagundua kwa siku za karibuni wanachezeshwa sana vijana wageni. Nadhani mpango wa kuingia sokoni hautakuwepo.
 
Watu wanafumbwa macho na statistics za computer, ile hali mpira tunajionea wenyewe kuwa yule bwana yupo careless mno
 
10Hag TACTICIAN mzuri kuliko Arteta tena daaah,hizi akili nyingine sijui za wapi
 
Huyo unaemsemea wa hovyo ana takwimu nzuri za kutengeneza chance za kufunga kuliko magwiji wengi waliopita EPL ,,,,tatzo tuna forward mbovu ,,,,, chance hizo haziwi magoli,,,,

Bruno ana spirit ya timu sana, utadhani ya baba yake ,,,nadhani hii ni moja ya sifa zilizompa uongozi ,,,,


Punguza makasiriko, ile nafasi unataka acheze nani ? Panga pangua kwenye mechi muhimu lazima apangwe, hata makocha waliopita walikuwa wanampanga,,,,,

Wewe ni mtaalamu kuliko hao makocha wanaompanga???
 
Mkuu uliona mbali😃Arteta kama Jf kungekuwa na trending Basi leo angekuwa Top 1
 
Kwa issue ya Usajili Boss kasema January watu wengi wanaludi kwa hiyo sidhani hapa kama tutakuwa sana na tetesi
 
Yule kiranja wa jukwaa lao kawatoroka anasubiri papoe ili aje kuwapiga kamba mpya tena.
yote inatokanwa na tabia ya kuranda ovyo kwenye thread za team pinzani na kuandika maneno ya dhihaka na kejeli.

huku wakisahau kuna wengine wana khulka sawa na zao.

ukishafahamu mipaka yako ya ushabiki hakutokuwa na mchezo utakao kupotezea furaha kwa muda mrefu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…