Abby Uladu
JF-Expert Member
- Dec 16, 2022
- 2,241
- 4,644
Alejandro Grimaldo alikuwa mchezaji huru mwezi June mwaka huu baada ya kumalizana na SL Benfica, baadhi ya vilabu vikawa vinazubaa tu - Xabi Alonso akamuona akamchukua mwezi wa saba.
Grimaldo ni fullback ya kuogopwa sana sababu ana uwezo mzuri wa kukaba na kupanda na kupiga mipira ya adhabu, kwenye faulo ni mchawi sana.
Amecheza michezo 9, goli 3, pasi 3 za mwisho.
Jonas Hofmann ana miaka 31 amecheza muda mrefu pale Borussia Monchengladbach, kumbe release clause yake ilikuwa ni €10m tu.
Xabi Alonso akaomba pesa kipengele hicho kikavunjwa akamchukua.
Jonas Hofmann yupo kwenye ubora mkubwa sana na ni mchezaji muhimu sana kwenye kikosi cha Xabi Alonso, mpaka sasa amecheza mechi 9 na kufunga mabao 5 na kutoa pasi 3 za mwisho kwenye Bundesliga msimu huu.
Wakati mnawazungumzia akina Victor Okoh Boniface, Florian Wirtz, Exequiel Palacios, Edmond Tapsoba, Jeremie Frimpong, Granit Xhaka - msiwasahau hao sababu nao wamechangia Leverkusen kuwa kileleni mpaka sasa.
Xabi Alonso things.
Man U tumerogwa na nan?
Sent from my SM-A047F using JamiiForums mobile app
Grimaldo ni fullback ya kuogopwa sana sababu ana uwezo mzuri wa kukaba na kupanda na kupiga mipira ya adhabu, kwenye faulo ni mchawi sana.
Amecheza michezo 9, goli 3, pasi 3 za mwisho.
Jonas Hofmann ana miaka 31 amecheza muda mrefu pale Borussia Monchengladbach, kumbe release clause yake ilikuwa ni €10m tu.
Xabi Alonso akaomba pesa kipengele hicho kikavunjwa akamchukua.
Jonas Hofmann yupo kwenye ubora mkubwa sana na ni mchezaji muhimu sana kwenye kikosi cha Xabi Alonso, mpaka sasa amecheza mechi 9 na kufunga mabao 5 na kutoa pasi 3 za mwisho kwenye Bundesliga msimu huu.
Wakati mnawazungumzia akina Victor Okoh Boniface, Florian Wirtz, Exequiel Palacios, Edmond Tapsoba, Jeremie Frimpong, Granit Xhaka - msiwasahau hao sababu nao wamechangia Leverkusen kuwa kileleni mpaka sasa.
Xabi Alonso things.
Man U tumerogwa na nan?
Sent from my SM-A047F using JamiiForums mobile app