Tatizo ni Glazers. January baada ya Ronaldo kuondoka EtH alimtaka Gakpo akaambiwa anaweza kusajili kwa mkopo tu, akamtaka Joao Felix ikashindikana kwasababu ya ada ya mkopo, Glazers wakagoma kutoa pesa ikabidi amchukue Weghorst. Msimu huu akataka RCB mpya ikaonekana kama atamsajili Min-Jae, Kim akaenda Bayern, akamtaka Pavard Glazers wakasema hakuna pesa mpaka auze wachezaji, Maguire akagoma kuondoka ikabidi EtH amsajili Evans.
Sasa hivi anamtaka El Ghazi kwasababu hana option nyingine na msimu bado mrefu sana na dirisha la usajili limefungwa.
Hawa wachezaji wengi wa mkopo na free agents hawana viwango vya kucheza United ila uongozi wa timu unamfelisha kocha maana hana namna.