Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Taratibu maji yanaanza jitenga na mafuta


Niliyoyasema miezi kadhaa kuhusu 7hag taratibu Yanaanza kuonekana kwa mbali



Erik ten hag Mfukoni mwa Gary O' Neil |

Anasema

Mtaumia kusema hivi, lakini Chelsea wanaonekana ni timu bora uwanjani kuliko United na ni miezi miwili TU tangu Pochettino apewe timu... Wakati huo huo 10hag ni miaka miwili na United hii inayoonekana kuwa ya Hovyo kabisa.

Nimeanza kuwa na wasiwasi kuhusu juu y Talent ID ya 10 hag.. Msimu uliopita, United walikuwa na tatizo kubwa la kushindwa kuutawala mchezo, hawana kiungo ambaye ana uwezo wa kudhibiti kasi ya mchezo, ( Control the tempo)

Msimu mpya lakini tatizo bado ni lile lile, walimsajili Meson Mount, ni usajili mzuri, lakini kama mchezaji TU wakikosi (Squad player) lakini kumchezesha pamoja na Bruno na Casemiro kunaonekana hakutofanikiwa wote watatu hakuna hata mmoja mwenye uwezo wa kuutawala mchezo "
 
Mbona Thread Ya Arsenal Inakataa Kufunguka
 
Yuko mhuni anaitwa "Hujland" huyu pekee ndio atatuokoa. Al-Hadidy
 

Isije kuwa huu ni msimu wa Wolves kupiga vigogo. Tusijilaumu sana next weekend anakutana na Brighton ngoja tuone.
Ujinga mkubwa ni wa ETH, timu imeelemewa inashambuliwa kwa kasi, kiungo kimekufa halafu unamuingiza Erickson! Enzi zile tulimuingiza mhuni FRED anaenda hapo katikati kutibua tibua kila kitu bahati mbaya ndio hayupo tena.
 
Ivi nyie matakataka munaleta mazoeya na timu etu bado inatafutana yani tukimleta yule Lavia basi muneisha. #CFC💙💙💙
 

Chelsea inaonekana ni bora kwasabau inawachezaji wazuri
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…