Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Inahitaji moyo sana kuangalia hili pira pelesu pelesu linalochezwa hapa

Naona timu zinazoshindana kubutua tu mpira kama gombania goli, afadhali wolves wanaweka mali chini kidogo
20230323_123828.jpg
 
Man u ni kama wanaendeleza walipoishia
Hii timu kuna kitu katikati kinakosekana kama driving force flani hamna

Coordination ya wacheza ipo low kati hapo mount - casemiro pair ni mbovu

Mbele garancho yule ni well built supersub ukimuanzisha ni mapepe ...Rashford ni preferred left wing zaidi ya ST

So far man utd atashinda ila inabid aamke kutoka usingizini
 
Mount nikama vile tumepigwa na kitu kizito kichwani

Au kitu chenye ncha kali
Mount mm namchukulia Kama mchezaji aliyemaliza mpira kwasasa anakula pension

Mount alicheza kwa kujituma kwa lampard na mwanzon kwa Tuchel ,baada ya hapo ana Mwaka na nusu ana goli 1 na assist 1 ,sijawahi muona aki progress Tena .

Sijui Kocha WENU aliona Nini kwa mount ,si Mara mia angemchukua Yuri Tielemans alikuwa free
 
Hii timu kuna kitu katikati kinakosekana kama driving force flani hamna

Coordination ya wacheza ipo low kati hapo mount - casemiro pair ni mbovu

Mbele garancho yule ni well built supersub ukimuanzisha ni mapepe ...Rashford ni preferred left wing zaidi ya ST

So far man utd atashinda ila inabid aamke kutoka usingizini
Kiungo Cha manjesta hakina Controller , ulimuona Jana Enzo vs Liverpool
 
Kucheza na Rashford yataka moyo
Rashidi ana kauPogba flani hivi mpuuzi huyu, tukiweka matumaini makubwa kwa huyu mswahili msimu huu tutafeli vibaya.
Nimeliona jini magoli Rasmus Højlund kwenye kiti linafatilia kwa makini sana hii mechi, yaani lina uchu kwelikweli pamoja na kuumwa ila unaliona kabisa linatamani liingie uwanjani.
 
Imebanwa mirija ya counter ndiyo maana united wanateseka.

Huyu Cunha kama ana bifu na United. Mara awachambue Fernandez na Kijeba sasa hv shot
 
Kiungo Cha manjesta hakina Controller , ulimuona Jana Enzo vs Liverpool
Yani huyo ni national treasure dah tokea anasajiliwa Chelsea iliniuma najua ni elite midfield sema tu mfumo wa Chelsea na performance ya msimu uliopita ulimuangusha

Enzo kweny timu kama man city ni kosa la jinani maana ana akili ya kdb nguvu za Bernardo execution decisive power ya gundo city ange run for treble once again

Turudi kwa amount.... Jamaana anachezeshwa out of position nikama vile 10hag ana experiment kitu hapo kati yule ni natural aggressive midfielder sio defensive sana
 
Back
Top Bottom