Manchester United (Red Devils) | Special Thread

Mawazo yangu ni ya kifanyabiashara,. Mtu yoyote ambaye kauza hata genge hawezi kutokujua hili.

Sawa tupo hapa, muda utatuambia
 
Mkuu Mc cane shukrani na hongera kwa kulielezea suala hili kinagaubaga. Sasa nimeelewa vizuri hili sakata.

Pamoja na hayo nina swali moja dogo kama utakua katika wasaa mzuri wa kunijibu nitafurahi sana.

Swali langu ni kuhusu hilo deni. Nitaliuliza katika vipengele vinne kama ifuatavyo:-

1. Kwa sasa limepungua au kuongezeka kwa kiasi gani ?
Kwa maneno mengine tunadaiwa shilingi ngapi kwa sasa kwenye hiyo SONGESHA yetu sisi kama klabu ?

2. Ni nini hatma ya deni hilo katika mauzo au manunuzi ya klabu ? Je, mnunuzi mpya atauziwa deni (litahusika katika uthaminishaji wa klabu bila shaka) na kutakiwa kulihudumia ?

3. Je, deni hilo haliwezi kuwa kama kikwazo cha baadhi ya wanunuzi kuvutiwa kutaka kuinunua klabu ? Deni hilo halifukuzi wateja kweli ?

4. Je, katika mchakato huu wa kuuzwa kwa klabu, hatuwezi kupata mnunuzi mpya ambaye nayeye atakua amekopa fedha na kisha deni hilo kulihamishia klabuni kama walivyofanya hawa Glazers ?

Yangu ni hayo.

Bavaria Chief-Mkwawa na wajumbe wengine mnaweza kuweka neno pia.
 
2. Mnunuzi anaponunua na deni linajumuishwa. Ni drafting tu ya mkataba

Sent from my M2004J19C using JamiiForums mobile app
 
Mkuu deni roughly lipo vile vile sometime linapungua kidogo sometime linaongezeka kidogo.
Hili graph linaonesha deni kuanzia 2005

2006 ilikuwa ni 590M na 2022 ni 620M, ukumbuke hili deni ni la Glazzer na sio la Man U wamehamisha hili deni kwenye timu kwa ajili ya Biashara zao Binafsi.


2. Ni nini hatma ya deni hilo katika mauzo au manunuzi ya klabu ? Je, mnunuzi mpya atauziwa deni (litahusika katika uthaminishaji wa klabu bila shaka) na kutakiwa kulihudumia ?
Ndio mkuu mnunuzi mpya anauziwa deni, moja ya sababu Chelsea imeuzwa bei rahisi ni sababu Abramovich amesamehe 1.8B kama kumbukumbu zipo sahihi ambayo alikuwa anawadai Chelsea, ila kwa United ni viceversa Atakayenunua deni linamuhusu.
3. Je, deni hilo haliwezi kuwa kama kikwazo cha baadhi ya wanunuzi kuvutiwa kutaka kuinunua klabu ? Deni hilo halifukuzi wateja kweli ?
Tayari ni kikwazo kuna watu wamejitoa sababu ya Deni, halimake sense, kuna kundi la washabiki wa united wenye pesa waliwahi kujichanga hadi 1.5B na kumtest Glazzer kama miaka 12 iliopita ila alikataa, kundi hilo naona kiongozi wake tayari amekataa valuation ya sasa na wamejitoa.
Inawezekana, ila wakati Chelsea inauzwa kulikuwa na kipengele kabisa kinaitwa Anti Glazzer, kwamba mtu awe na Cash, hakuna mambo ya kuweka madeni kwenye timu, so i hope Utd pia wataweka hiko kipengele na Mmiliki aingize hela kwenye timu n sio kutoa.

Na mkuu kuongezea Glazzer wanauza sababu timu inataka investment ya maana, sio tu hilo deni, Old trafford yenyewe inahitaji karibia £1B either ibomolewe ijengwe ama ufanywe ukarAbati mkubwa, bado viwanja vya mazoezi na miundombinu mingine, kifupi Glazzer hawajaboresha chochote toka 2005 club ipo vile vile, mpaka vitimu vidogo kama Leicester vina modern infrastructure.

So atakayenunua inabidi awe willing kuspend zaidi ya kununua UTD awe commited kujenga na miundombinu.
 
3. Deni haliwezi kuwa kikwazo. Hawa matajiri ambao wamepanga foleni kununua klabu, wana taarifa nyingi sana kuhusu hali ya hilo deni, athari zake na namna ya kulijumuisha katika fedha watakayotoa kuinunua United. Hilo deni sio siri, lakini bado matajiri wanaitamani sana United. Ukiachana na kikosi, miundombinu n.k. asset kubwa ambayo Man United wanajivunia ni kuwa na mashabiki bilioni 1 na milioni 100 duniani. Huo ni mtaji kwa klabu.

Sent from my M2004J19C using JamiiForums mobile app
 
4. Kosa la tajiri kuipachika timu deni haliwezi kujirudia. Mfano Chelsea wakati inauzwa Boehly mnunuzi/mmiliki wa Chelsea aliwekewa kwenye mkataba kipengele kinachoitwa "Anti-Glazer Clause"

Hicho kipengele kinamzuia Boehly kujilipa faida pasipo kuzingatia ustawi wa Chelsea. Pia, kinamzuia Boehly kuhamishia madeni yake binafsi kwenye klabu

Kwa hiyo hicho kipengele kitawekwa ili kumdhibiti mmiliki mpya kuifanya klabu kubwa shamba la bibi

Sent from my M2004J19C using JamiiForums mobile app
 
Sijajua logic yako mkuu, kama unakubali hizo hela zote zimechotwa unakataa nini sasa nilichosema? Sijasema popote Glazzer wapo Against sheria.
Boss, logic yangu ilijengwa katika hili ulilolisema "Lazima kuna deal la chini ya kapeti wameingia ili Bank ifaidike..."
Nakataa kuwa kuna dili chini ya kapeti. Hizo hela hazikuchotwa kinyume na taratibu, bali ni jinsi deal lilivyoingiwa toka mwanzo.
 
Kumbe kuhusu miundombinu kuwa chakavu Ronaldo alisema ukweli
 
Boss, logic yangu ilijengwa katika hili ulilolisema "Lazima kuna deal la chini ya kapeti wameingia ili Bank ifaidike..."
Nakataa kuwa kuna dili chini ya kapeti. Hizo hela hazikuchotwa kinyume na taratibu, bali ni jinsi deal lilivyoingiwa toka mwanzo.
Mkuu chukulia mfano wa kilayman kabisa.

Wewe unataka kuinunua Mtibwa, thamani ya Mtibwa ni Bilioni 10, huna Bilioni 10 ukaenda kwa Bakhresa akukopeshe, Bakhresa akakupa Bilioni 10 ila kwa Riba ya Bilioni 1 kila mwaka, na wewe ukaamua usilipe deni la Bakhresa ukalihamisha kwenye Club, ila kila mwaka unampa Bakhresa Bilioni 1,

Baada ya miaka 15 umemlipa Bakhresa riba ya Bilioni 15, na deni lipo pale pale anakudai, na wewe mwenyewe faida uliopata hafiki hata Bilioni 10, je mtu akitumia figure of speech na kusema Mtibwa inamilikiwa na Bakhresa si sawa?

Hii figure ya Swissramble ni ya 2019 ila utapata general idea

Ukiangalia Box la kwanza kuna Interest na Debt repayments around £900m na Dividends ni £166m,

So kinachoenda bank ni kikubwa sana, compare na Faida wanayopata Glazzer, even ukijumuisha mauzo ya hisa £465M still kinachoenda Bank ni kikubwa.

Hizo ni data za 2019, mwaka huu hio figure imeshazidi £1B. Plus deni lao inakaribia £2B ambayo wanachota toka kwetu.

Ukumbuke Utd haikuwa na deni kwa miaka takriban 100, inajiendesha yenyewe bila tabu.
 
Kumbe kuhusu miundombinu kuwa chakavu Ronaldo alisema ukweli
Mambo aliyoongea Ronaldo kuhusu Glazzer ni sawa, na sio kwamba hayajulikani mashabiki wa UTD wanayaongelea miaka na miaka. Old trafford kukinyesha mvua inavuja sio siri na kuna video kibao. Na sio kuvuja vitone maji yanatiririka kabisa kwamba unaoga.


 
Nadhani unajua valuation ya makampuni inavyofanywa.

Hilo deni ni inclusive ya valuation.
 
Nadhani unajua valuation ya makampuni inavyofanywa.

Hilo deni ni inclusive ya valuation.
Ndio maana haimake sense kwa wanunuzi. Sijakataa kama deni ni inclusive na ukisoma vizuri nimegusia hicho kipengele.

Habari nyingi za wanunuzi wa UTD ni fake news tu, kama vile kunavyokua na tetesi za usajili zisizo na kichwa wala miguu wakati wa usajili.
 
Unaweza ku verify ufake wa hizi news?

Manake tunazipata kutoka kwenye credible sources.
 
Unaweza ku verify ufake wa hizi news?

Manake tunazipata kutoka kwenye credible sources.
Macrumors website maarufu ya Apple imekataa kwamba Apple anainunua United

Source ya hii habari kwamba Apple yupo interested kununua UTD ni Daily star, gazeti lenye hadhi kama ya Uwazi na kiu.

Pia Ortega mwenyewe amejitokeza kwamba hayupo Interested kuinunua UTD.
 
Kuhusu Apple niliileta mimi kutoka Sky Sport. Hiyo daily star umeileta wewe.

Macrumours sio official channel ya apple kutoa taarifa, ni kijarida kinafuatilia rumours tu zinazohusu apple & its products. As of now hakuna sehemu apple wamekubali au kukataa.


So hoja yako bado haina mashiko.

Kuhusu Zara hakuna sehemu credible waliyokanusha.

Vipi kuhusu Saudia? Nazo ni taarifa feki?



 
1. Ukisoma tu hicho kichwa cha habari cha sky kuhusu Apple hakimaanishi Apple wana interest na Utd bali Sky wanadiscuss report, same ukiskiza Video hakuna hata sehemu moja Muandishi amesema kwamba wao Sky wamereport hii issue bali anadai ni report from somewhere else, kama una credible source sky wameclaim hii weka hapa, as far as i know ni daily star ndio waliosema.

2. Ortega mwenyewe amekanusha na hana sababu yoyote ya kudanganya, so again tusikilize Gazeti la udaku Daily star ama Ortega mwenyewe?

3. Nimesoma Hio interview ya Saudi, waziri wa michezo wa Saudia amesema kama kuna kampuni ya Saudia inataka kununua UTD ama Liver wapo tayari kuisaidia hakuna sehemu hata moja aliposema wanataka kuinunua UTD, ni just twist ya maneno.

Hii interview ilifanyika na BBC

Prince Abdulaziz bin Turki Al Faisal said there was a lot of "interest and appetite" in United and Liverpool.

He told BBC Sport: "From the private sector, I can't speak on their behalf, but there is a lot of interest and appetite and there's a lot of passion about football.

"It's the most-watched league in Saudi and the region and you have a lot of fans of the Premier League.

"We will definitely support it if any [Saudi] private sector comes in, because we know that's going to reflect positively on sports within the kingdom.

"But if there's an investor willing to do so and the numbers add up, why not

Source hapa

Saudi Tayari wanamiliki Newcastle sheria hairuhusu mmiliki mmoja kuwa na Timu mbili competition moja, refer issue ya RB leipzig na Salszburg.
 
Manchester Evening News (MEN) moja kati ya credible source kuhusu habari za United na Sky Sports wameripoti kuhusu Ortega na Apple ku explore possibility ya kununua klabu ya United

Sent from my M2004J19C using JamiiForums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…